Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2023

PROF. SHEMDOE CHUONI NDC

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe  akiwasili na kupokelewa na Maafisa wa Chuo Cha Taifa Cha Ulinzi – Tanzania (NDC) kwa ajili ya kutoa Mhadhara kuhusu" Livestock and Fisheries Sector's Development in Tanzania"kwa Washiriki wa Kozi ya Kumi na Mbili jana tarehe  12 Disemba 2023. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe akisaini kitabu cha Wageni mara tu baada ya kuwasili katika Ukumbi wa Chuo cha Taifa cha Ulinzi (NDC) Jana  tarehe 12 Disemba2023 jijini Dar es salaam .  

WADAU WAHIMIZWA KUFUGA SAMAKI KUKUZA SEKTA YA UVUVI NCHINI

Picha
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe amewahimiza wadau wa sekta ya uvuvi kujikita katika ufugaji wa viumbe maji ili kusaidia kukuza mchango wa sekta ya uvuvi katika Pato la Taifa kutoka asilimia 1.7 walau kufika mpaka asilimia 5 ifikapo mwaka 2025. Prof. Shemdoe alitoa rai hiyo wakati akifungua kikao kazi cha wadau wa Ukuzaji   Viumbe maji kilichofanyika jijini Dodoma Oktoba 31, 2023. Alisema kuwa hivi sasa wanaandaa kanuni zitakazosaidia kuwa na usimamizi madhubuti wa tasnia ya uvuvi kwa lengo la kuimarisha ukuzaji wa viumbe maji ili kuchangia vyema katika Pato la Taifa. "Tunaandaa kanuni kwa ajili ya ufugaji viumbe maji , kwenye ufugaji wa samaki na mavuvi ya samaki ili kuona   namna tutaweza ndani ya miaka hii miwili   kuchangia   asilimia 5 kwenye pato la taifa," alisema Prof. Shemdoe Aliongeza kuwa kanuni hizo zitakwenda kuboresha namna tasnia ya ukuzaji viumbe maji inasimamiwa na kuwezesha kile kinachozalishwa kiweze kufika kwe...

WATAALAMU WATAKIWA KUKUSANYA TAKWIMU SAHIHI ZA KITAFITI

Picha
Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, maliasili na Mifugo Mhe. Shamata Saame amewataka wataalamwa Sekta ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha wanachukua   takwimu sahihi wakati wa kukusanyataarifa za kitafiti    ili ziweze kuisaidia Serikali katika kupanga mipango yake. Waziri   Shaame ameyasema hayo wakati akifunga Kongamano la 46 la Uzalishaji na Uendelezaji wa Mifugo na Mkutano   Mkuu wa 47 wa Mwaka wa Chama cha Wataalamu wa Uzalishaji na Uendelezaji wa Mifugo na Uvuvi (TSAP) lililofanyika kwenye Ukumbi wa Olasit Garden, Arusha   Oktoba 27, 2023. "Takwimu sahihi kuhusu taarifa za mifugo na uvuvi zitasaidia kutunga sera,   kunyoosha maono, fikra na miongozo ya ilani ya chama cha mapinduzi kuweza kufikia   malengo ya kuwainua wananchi   kupata mafanikio kwa haraka," alisema Aliongeza kwa kusema kuwa Serikali inawategemea sana wataam na hivyo watumie vizuri teknolojia walizonazo ili zikaboreshe tasnia nzima ya ufugaji ili kupata maendeleo. “Wizara ...

WADAU WAKUTANA KUWEKA MIKAKATI KUENDELEZA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Wataalam na wadau wa   sekta ya Mifugo Nchini, wamekutana jijini  Arusha kwa lengo la kujadili namna ya kuongeza uzalishaji katika sekta hizo ambayo italeta tija  kwa wananchi. Hayo yamesemwa na   Mwenyekiti wa chama cha wataalamu wazalishaji mifugo na Uvuvi ,Dkt. Jonas  Kizima katika ziara ya kutembelea mbuga ya  Tarangire, ikiwa ni sehemu ya kongamano la siku tatu la kisayansi liloanza Oktoba  26 jijini  Arusha Alisema kuwa  lengo kubwa ni  kupitia machapisho ya kisayansi yaliyoletwa na wadau  ili angalau waweze kutoa matokeo ya tafiti, na kutatua changamoto  katika sekta ya Mifugo na Uvuvi "Katika hizi siku tatu, tumetenga siku moja ya kuja kutembelea mbuga za wanyama nchini, na mwaka huu tumechagua  Tarangire   ili kupata muda wa kufurahi na kujifunza zaidi, Pia tunaunga juhudi za Rais katika kuongeza watalii nchini kupitia Royal  tour na kuongeza pato kupitia utali,"alisema Dkt. Kizima Na...

MIFUGO NA UVUVI YATINGA NUSU FAINALI KIBABE!

Picha
◾ Kukutana na Katiba na Sheria Oktoba 10  Timu ya soka ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetinga hatua ya nusu fainali ya Michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Iringa baada ya kuifumua timu ya bunge kwa magoli 2-1 kwenye mchezo uliochezwa leo Oktoba 08, 2023 uwanja wa Samora mkoani humo. Katika mchezo huo uliokuwa wa kasi kwa pande zote mbili timu ya Wizara ya Mifugo iliweka kimiani magoli yake kupitia kwa mlinzi wa pembeni Ignatus Mwasa aliyefunga kwa shuti kali la  mpira wa adhabu dakika ya 06 ya mchezo kabla ya timu ya bunge kusawazisha kupitia kwa mshambuliaji wao Mnubi Kajobi dakika ya 37 na kufanya timu hizo kwenda mapumziko wakiwa wametoshana nguvu. Timu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilianza kipindi cha pili kwa kasi kubwa huku ikielekeza mashambulizi ya nguvu upande wa Bunge hali iliyoilazimu timu yote kurudi nyuma kwa ajili ya kuzuia mashambulizi hayo. Mashambulizi hayo makali ya timu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi yalizaa matunda katika dakika ya 71 baada ya kupata goli l...

MIFUGO NA UVUVI NAFASI YA 3 BAISKELI WANAUME

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia mshiriki wake Siraji Mohammed imefanikiwa kushika nafasi ya 3 kwenye mashindano ya mbio za baiskeli umbali wa Km.40 yaliyofanyika leo Oktoba 08, 2023 kwenye michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Iringa. Siraji ambaye alionesha upinzani wa hali ya juu na kuwa miongoni mwa washiriki 3 wa kwanza walioanza mzunguko wa pili kukamilisha umbali huo huku akitetea nafasi ya 3 aliyoibeba kwenye mashindano ya mwaka jana yaliyofanyika mkoani Tanga. Wizara ya Mifugo na Uvuvi itakuwa kibaruani tena leo mchana kwenye hatua ya robo fainali ambapo timu yake ya mpira ya miguu itapepetana na timu ya Bunge huku upande wa mchezo wa kamba wanaume watachuana vikali na timu ya Ikulu.

ULEGA AZITAKA LITA, NARCO KUANDAA VIJANA KUWA WAFANYABIASHARA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amezitaka Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) na Bodi ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) kuwa na mkakati wa pamoja wa kuwaandaa vijana kuwa wafanyabiashara katika sekta ya mifugo kupitia programu kielelezo ya BBT Mifugo. Waziri Ulega ametoa maelekezo hayo wakati akizindua Bodi ya Nne ya Ushauri ya Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) na Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) katika tukio lililofanyika jijini Dar es Salaam leo Oktoba 7, 2023. "Huu ndio uwe mtazamano wetu, kijana anapofundishwa na kumaliza Mafunzo yake pale LITA nyie NARCO muweke utaratibu wa kutenga maeneo kwa ajili ya kuwapa vijana hao ili wajifunze kwa vitendo ufugaji wa kisasa, hatutaki kufundisha watu ili waende kuangaika bali waingie katika biashara ya mifugo na mazao yake," alisema Waziri Ulega  Aidha, aliwataka  LITA kuhakikisha wanakuwa na mkakati wa kuwaunganisha vijana hao na taasisi ...

SERIKALI YADHAMIRIA KUWAINUA VIJANA WA BBT-LIFE KWA KUWATAFUTIA MASOKO YA MIFUGO

Picha
SERIKALI kupitia  Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema kuwa inaendelea na majadiliano  na Wadau wa sekta ya Mifugo nchini  ili kuona namna bora ya kushirikiana na vijana waliopo kwenye Programu ya  BBT  -LIFE katika kunenepesha Mifugo na kuisafirisha kwenye masoko ya nje ya nchi. Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, (Mifugo) Dkt. Daniel Mushi wakati wa  kikao kati ya menejimenti ya sekta mifugo na wadau kuhusu kuwaunga mkono vijana waliopo kwenye programu ya BBT- LIFE , jijini Dodoma, tarehe 06.10.2023. Dkt.Mushi amebainisha kuwa wamekutana na Kampuni za ELIA FOOD na TANCHOICE  Limited za uchakataji nyama  kwa ajili ya  kutengeneza muunganiko wa BBT -LIFE na Soko kubwa la nje ya nchi la uuzaji wa mazao ya Mifugo ili kukabiliana na changamoto ya masoko ya mifugo kwa vijana wa BBT-LIFE. "Tumefikiria kuwa tukiwapata  wanunuzi wakubwa wa Mifugo programu yetu ya BBT - LIFE itakuwa imefanikiwa katika kuwawezesha vijan...

MIFUGO NA UVUVI YATAKATA MBELE YA MAMBO YA NDANI NA KUTINGA ROBO FAINALI

Picha
Timu ya soka kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetinga hatua ya robo fainali ya michuno ya SHIMIWI 2023 inayoendelea mkoani Iringa baada ya kuishindilia timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani goli 1-0 leo Oktoba 06, 2023 kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Samora. Goli hilo limefungwa na mshambuliaji hatari wa timu hiyo Joseph Buhigwe dakika ya 35 ya mchezo baada ya vuta nikuvute iliyotokea kwenye lango la timu ya timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani kabla ya mpira kufika kwa Buhigwe aliyeachia shuti kali lililozama wavuni moja kwa moja. Timu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilionekana kuutawala mchezo huo wakati wote na kama si uimara wa mabeki na golikipa wa timu ya Wizara ya  Mambo ya Ndani huenda wangefungwa magoli mengi zaidi. Baada ya ushindi huo Wizara ya Mifugo na Uvuvi sasa imeingiza timu 2 kwenye hatua ya robo fainali baada ya kutanguliwa na timu ya kamba wanaume waliofuzu hatua hiyo mapema leo asubuhi.
Picha
 MIKOPO NA MAFUNZO YATAJWA KUWA NA TIJA KWA WALENGWA    Na. Edward Kondela   Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza, umesema mikopo itakayotolewa na serikali kwa kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kwa wanawake wanaojihusisha na uvuvi itakuwa na tija kwa kuwa imezingatia utoaji wa mafunzo ya namna ya kutumia mikopo hiyo. Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Bw. Binuru Shekideli amebainisha hayo (05.10.2023) wakati alipotembelewa ofisini kwake na wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na wakufunzi wa vikundi vya kuweka na kukopa ili kumuarifu juu ya mradi wa kusimamia na kuendeleza uvuvi mdogo nchini ambao unatekelezwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na FAO kwa vikundi vya FARAJA na TEGA ZIFE vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema. Bw. Shekideli amesema mikopo hiyo ni dhahiri itavifanya vikundi hivyo hususan vya wanawake wanaojihusha na masuala ya uvuvi kuwa na tija kwa kuwa licha ya kupatiw...

KAMBA WANAUME YATINGA ROBO FAINALI KIBABE!

Picha
◾ Wanawake watolewa na Mahakama  Timu ya kamba ya wanaume ya  Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Iringa mara baada ya kufanikiwa kupata ushindi wa mivuto yote miwili kwenye mchezo wao dhidi ya Wizara ya Afya uliochezwa leo Oktoba 06, 2023 kwenye uwanja wa Mkwawa. Dalili ya ushindi katika mchezo huo ilianza kuonekana mapema ambapo Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliuanza kwa kasi na kuthibitisha namna ilivyojipanga kubeba pointi kwenye mivuto yote. Wakati huo huo timu ya kamba ya wanawake kutoka Wizarani hapo leo imeaga rasmi mashindano hayo baada ya kupoteza mchezo wao dhidi ya timu ngumu ya Mahakama kwenye mivuto yote miwili. Wawakilishi wengine wa Wizara hiyo timu ya Mpira wa Miguu wanatarajia kutupa karata yao dhidi ya timu ya Wizara ya Mambo ya Ndani leo Oktoba 06, 2023 mchana kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa.

KAHAMA FRESH WAUNGA MKONO BBT MIFUGO

Picha
Kampuni ya Kahama Fresh inayomiliki Kiwanda cha kusindika maziwa na Shamba la mifugo imeunga mkono Programu ya BBT kwa kutoa ng'ombe wa maziwa (mitamba) watano (5) kwa kikundi cha vijana 17 ili kuwawezesha kujishughulisha na uzalishaji wa maziwa na  kujiongezea kipato. Tukio hilo limefanyika katika shamba la mifugo la kampuni hiyo lililopo wilayani Karagwe, Mkoani Kagera leo Oktoba 5, 2023. Akizungumza wakati wa kukabidhi ng'ombe hao kwa vijana, Waziri Ulega alimpongeza Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Bw. Josam Ntangeki kwa kuunga mkono Programu ya BBT kwa vitendo. "Nampongeza Ndugu Josam kwa kuunga mkono Programu hii ya BBT kwa kuwakopesha ng'ombe wa maziwa vijana wetu kupitia mpango wa Kopa Ng'ombe Lipa Maziwa ili kuwawezesha vijana wetu kuzalisha maziwa kwa wingi na kuyapeleka katika viwanda vya uchakataji wa maziwa kikiwemocha Kahama Fresh", alisema Mhe. Ulega Aliongeza kwa kusema kuwa programu hiyo ya BBT haiwezi kuendeshwa na Serikali peke yake bila ya wadau...

MIFUGO NA UVUVI YATINGA FAINALI RIADHA MITA 100

Picha
◾ Yafikia rekodi yake ya mwaka jana kupitia kwa mwanariadha yule yule.  Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia kwa mwanariadha wake William Valentino imefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya riadha umbali wa mita 100 baada ya kukamilisha hatua ya nusu fainali akiwa mshindi wa 2. Kwa hatua hiyo William anaifikia rekodi aliyoiweka kwenye michuano ya SHIMIWI msimu uliopita ambapo pia alifanikiwa kutinga hatua ya fainali. Mpaka sasa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefanikiwa kushika nafasi ya 3 kwenye riadha upande wa mita 3000, imeingia fainali upande wa mita 100 na nusu fainali upande wa mita 200. Michuano ya SHIMIWI itaendelea tena kesho Oktoba 06, 2023  kwa hatua ya 16 bora ambapo kwa upande wa mpira wa miguu timu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi itamenyana na timu ya Mashitaka kwenye uwanja wa Samora majira ya saa 8 kamili mchana, timu ya kamba wanawake itachuana na timu ya Mahakama saa 12:30 asubuhi kwenye uwanja wa Mkwawa huku timu ya kamba wanaume ikitoana jasho na timu ya Wizara ya Afya...

SALEMA AIPA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI NAFASI YA 3 TUFE

Picha
◾ Kufutiwa kwa matokeo yake ya ushindi kwazua utata na kushangaza wengi.  Mchezaji Theodata Salema kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi amefanikiwa kuipa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ushindi wa nafasi ya 3 kwenye mchezo wa kurusha tufe uliofanyika leo Oktoba 05, 2023 uwanja wa Samora mkoani Iringa. Mchezaji huo alirusha mitupo yote mitatu na kupata ushindi wa mita 10. 05 kwenye mtupo wa kwanza na 7.45 kwenye mtupo wa pili huku mtupo wake wa 3 ukifutwa baada ya kurusha tufe nje ya mstari. Hata hivyo katika hali iliyowashangaza wengi waliokuwa wakishuhudia mashindano hayo matokeo ya mtupo wa mita 10.5  yaliyopaswa kumpa ushindi kwenye mitupo yote mitatu ambayo yalikubaliwa hapo awali na waamuzi wote yalifutwa baadae ambapo ilibainika kuwa  alilalamikiwa na mmoja wa viongozi wa timu zilizokuwa zikishiriki wakidai hakuweka mkono wake mahala sahihi wakati akirusha tufe jambo lililolalamikiwa na wengi kuwa ameonewa. Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo upande wa wanawake ni Tume y...

MIFUGO NA UVUVI RIADHA WASHIKA NAFASI YA 3 RIADHA MITA 3000.

Picha
◾ Yatinga nusu fainali mita 100 na 200.  Mkimbiaji Deonatus Magendelo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi amefanikiwa kushika nafasi ya 3 kwenye mashindano ya riadha umbali wa mita 3000 mbio zilizofanyika kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa leo Oktoba 05, 2025. Magendelo amefanikiwa kushika nafasi hiyo mara baada ya kuwapiku wanariadha wenzake 54 waliokuwa nyuma yake ambao kwa muda mrefu walionekana kuwa na ushindani wakati wote wa mbio hizo. Kwa upande wa wanawake umbali huo huo mkimbiaji Beatrice Ilomo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi licha ya kushindwa kushika nafasi za juu amefanikiwa kumaliza mbio hizo jambo ambalo limewashinda baadhi ya wanariadha wenzake. Katika hatua nyingine Mwanariadha Fihiri Mbawala amefanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali ya mbio za mita 200 mara baada ya kufanikiwa kushika nafasi ya 2 kwenye kundi lake. Kwa upande wa mbio za mita 100 wakimbiaji William Valentino na Nuru Musa nao wamefanikiwa kutinga hatua ya  nusu fainali ya mbio hizo ambapo Willia...

KAMPENI YA TUTUNZANE MVOMERO DAWA YA MIGOGORO YA ARDHI

Picha
Kampeni ya upandaji wa Malisho ya mifugo, uchimbaji wa visima na malambo katika mashamba binafsi ya wafugaji, hamasa ya kilimo biashara na rafiki kwa mazingira imelenga kutatua migogoro ya ardhi wilayani Mvomero.   Kampeni hii inayokwenda na kauli mbiu, “Mfugaji Mtunze Mkulima, Mkulima Mtunze Mfugaji ili Kulinda Mazingira Yetu” inalenga kuwaelimisha kwanza kuanza kumiliki ardhi kwa ajili ya kupanda malisho ya mifugo yao na kuanza kufuga mifugo inayoendana nae neo la ardhi wanalomiliki ili kuondokana na migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara kutokana na wafugaji kuhamahama.   Akizungumza wakati wa kuhitimisha jukwaa la maandalizi ya kampeni hiyo ijulikanayo kama Tutunzane Mvomero, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amesema kuwa utekelezaji wa kampeni hiyo unakwenda kutatua tatizo la migogoro ya ardhi iliyopo kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi hasa wakulima.   Naibu Waziri Mnyeti amesema kumekuwa na migogoro mi...

VIONGOZI WATEMBELEA KAMBI YA TIMU YA WIZARA IRINGA

Picha
◾ Meneja SAO-HILL atoa motisha ya Maji na Maziwa kwa wachezaji  Wakurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu  kwa upande wa sekta za Mifugo na Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina na  Bw. Emmanuel Kayuni wametembelea kambi ya timu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi inayoshiriki michuano ya SHIMIWI iliyopo kwenye viunga vya chuo kikuu cha Mkwawa mkoani Iringa leo Oktoba 04, 2023 ambapo mbali na kutoa pongezi kwa timu hiyo kufanya vizuri kwenye michezo mbalimbali wamewasilisha salamu kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Riziki Shemdoe. Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu kwa upande wa sekta ya Uvuvi Bw. Emmanuel Kayuni amevitaka vikosi vyote vya Wizara hiyo kuhakikisha vinashinda kwenye michezo yake yote iliyosalia na kupunguza matokeo ya sare ambayo timu ya mpira wa miguu imeyapata kwenye baadhi ya mechi zake. “Lakini jambo la pili naomba tusiendekeze sana haya mambo ya kupewa ushindi wa mezani, tunataka kucheza na y...

WADAU WAHIMIZWA KUWEKEZA KWENYE SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI WILAYANI PANGANI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amewasihi wadau kuwekeza kupitia Sekta za Mifugo na Uvuvi wilayani pangani ili kuongeza uzalishaji na tija.   Naibu Waziri Mnyeti ameyasema hay oleo (03.10.2023) wakati wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji la Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga ambapo aliwaeleza washiriki kuwa zipo fursa nyingi kupitia sekta za mifugo na uvuvi.   Wadau wamehimizwa kutumia fursa zilizopo katika ufugaji wa mifugo na samaki kwa kuhakikisha wanaongeza uzalishaji na uongezaji wa thamani wa mazao ya mifugo na uvuvi ili kuongeza ajira, kipato na mchango wa sekta hizo kwenye pato la taifa.   “Niwaombe wadau kuja kuwekeza hapa pangani kupitia sekta hizi za mifugo na uvuvi kwa kuwa fursa zipo kuanzia kwenye kuongeza uzalishaji na uongezaji wa thamani wa mazao ya mifugo na uvuvi, hivyo kupitia kongamano hili ni vema tukazitumia fursa hizi kwa ajili ya kuleta maendeleo yetu, ya wanapangani na taifa kwa ujumla,’ alisema   Naibu Wa...

RAIS SAMIA AMEDHAMIRIA KUWAINUA WAVUVI TANZANIA - ULEGA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuwainua wavuvi kwa kuwawezesha vifaa vya kisasa vya uvuvi ikiwemo maboti na vizimba ili waweze kuboresha maisha yao. Waziri Ulega ameyasema hayo wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa vizimba na boti leo Oktoba 3, 2023 jijini Mwanza. "Mradi huu wa ugawaji wa maboti na vizimba kwa wavuvi bila riba ni wa kwanza, haujawahi kufanywa na yeyote, Rais Dkt. Samia ndio wa kwanza kuutekeleza, ametoa jumla ya shilingi bilioni 25 kwa ajili ya kuwezesha wavuvi kupata vifaa vya kisasa ili kuboresha maisha yao", amesema Ulega Ameongeza kwa kusema kuwa Rais Dkt. Samia anafanya uwezeshaji wa wananchi kiuchumi kwa vitendo na hivi karibuni atagawa kwa wavuvi wa Kanda ya ziwa boti takriban 55 na vizimba 615.

PETE MIFUGO NA UVUVI YAIADHIBU RAS SINGIDA

Picha
Timu ya Mpira wa pete kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendeleza wimbi lake la ushindi kwenye michuano ya SHIMIWI baada ya kufanikiwa kuifunga timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida kwa jumla ya magoli 25-11 mchezo uliochezwa leo Oktoba 03, 2023 kwenye uwanja wa RUCU B mkoani Iringa. Kwa ushindi huo timu hiyo imezidi kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kutinga hatua ya 16 bora ambapo sasa italazimika kusubiri kukamilika kwa michezo mingine hatua ya makundi ili kubaini timu zilizofuzu hatua hiyo.

MPIRA WA MIGUU WATINGA 16 BORA SHIMIWI 2023

Picha
◾ Ni baada ya kutoa suluhu dhidi ya MSD  Timu ya soka kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora ya Michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Iringa baada ya kutoka suluhu na timu ya MSD kwenye mchezo uliopigwa Uwanja wa mkwawa 2 leo Oktoba 03, 2023. Mchezo huo uliokuwa na upinzani mkali kutokana na kila timu kuhitaji pointi 3 muhimu ili iweze kufuzu hatua hiyo ulishuhudia timu zote zikitengeneza nafasi na kushindwa kuzitumia jambo lililoufanya kuwa mgumu zaidi hasa kwa upande wa MSD ambao kwa namna yoyote walihitaji kushinda mchezo wa leo. Upinzani mkali uliokuwepo baina ya timu hizo mbili ulishuhudia mlinzi wa kati Abdallah Bajwala kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kiungo Omary Kibaranga kutoka MSD wakitolewa nje kwa kadi nyekundu ambapo Bajwala alioneshwa kadi hiyo baada ya kuunawa mpira huku akiwa mchezaji wa mwisho kwenye lango lao na Kibaranga aliadhibiwa mara baada ya kumsukuma mwamuzi baada ya kutoridhika uamuzi wake. Kwa matokeo hayo Wizara ya Mif...

KAMBA WANAWAKE WAFUZU 16 BORA

Picha
Ni baada ya kuwagaragaza RAS Kilimanjaro  Timu ya kamba upande wa wanawake kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora ya michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani Iringa baada ya kushinda mvuto 1-0 dhidi ya timu ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro leo Oktoba 03, 2023 mchezo uliofanyika kwenye uwanja wa Mkwawa. Timu hiyo iliibuka na ushindi huo kwenye raundi ya pili ya mchezo huo ambapo raundi ya kwanza iliisha kwa timu hizo kutoshana nguvu. Timu hiyo inakuwa ya pili kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kufuzu hatua hiyo ikitanguliwa na ile ya Kamba wanaume ambayo ilifuzu mara baada ya mechi zake tatu za awali.

WAZIRI ULEGA ATAJA FAIDA LUKUKI ZILIZOPATIKANA KUTOKANA NA MKUTANO WA AGRF 2023

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kufuatia Jukwaa la Mkutano wa Mifumo ya Chakula Barani Afrika (AGRF), Sekta ya Mifugo na Uvuvi hapa nchini zimenufaika kwa kupata fursa mbalimbali za kibiashara, uwekezaji, mitaji na masoko. Waziri Ulega alibainisha hayo leo Oktoba 2, 2023 wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari kuwaelezea  mafanikio yaliyopatikana kutokana uwepo wa Mkutano wa Mifumo ya Chakula Barani Afrika (AGRF) uliofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 5 hadi 8, 2023. Alisema kupitia mkutano huo  Tanzania  ilipata fursa ya kuonesha programu bunifu ya BBT ambayo ni programu ya kielelezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na kupelekea kupata ahadi ya kuungwa mkono kwa Kiasi cha Dola za Marekani milioni 500 zilitolewa na wahisani kwa ajili ya kufadhili programu hiyo. Vilevile, alisema, Benki ya CRDB imetoa ahadi ya kiasi cha Dola Milioni 50 kama mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kusaidia Vijana waliopo katika sekta za Mifugo na Uvuvi k...

KAMPENI YA TUTUNZANE MVOMERO DAWA YA MIGOGORO YA ARDHI

 
Picha
  Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) Dkt. Pius Mwambene (katikati) akiongea na wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya ufugaji bora wa ng'ombe wa maziwa, chini ya mradi wa maziwa faida, yaliofanyika LITA kampasi ya Buhuri Mkoani Tanga, Septemba 29,2023

WADAU WAKUTANA KUTATHIMINI MRADI WA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA BAHARI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Kamati tendaji ya mradi wa ushirikiano kati ya Nairobi Convention na Southwest Indian Ocean Commission imekutana jijini Tanga kwa ajili ya kufanya tathmini ya mradi huo unaolenga usimamizi wa mazingira ya bahari na nchi kavu pamoja na usimamizi wa rasilimali za uvuvi Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI ), Dkt. Ismael Kimirei Oktoba 04,2023 ambapo amesema kuwa mradi huo unaotekelezwa katika Wilaya ya Mkinga na Pemba unalenga kutoa majibu ya mahitaji katika uchumi wa buluu Tumeanzia eneo la Mkinga kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano kati ya Tanzania, Msumbiji na Madagascar na tunategemea kwamba utapanuka kwenda nchi nyingine na ukiangalia upande wa kaskazini mwa bahari ya Hindi kuna nchi ya Kenya ambayo tunatarajia iwe mdau katika mradi huu" amesema Bi. Oliver Naye Mratibu wa Mradi unaoshughulikia maendeleo ya usimamizi wa rasilimali za bahari kutoka Shirika la Chakula na kilimo ...