Nav bar

Jumamosi, 28 Juni 2025

BI. MEENA AHIMIZA USHIRIKIANO KATIKA KUTEKELEZA MAJUKUMU SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Na. Stanley Brayton  

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena amewataka Watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa na Ushirikiano katika utekelezaji majukumu Wizarani hapo.

Bi. Meena amesema hayo Juni 28, 2025 wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Nyaraka za Ofisi baina yake na Mtangulizi wake Prof. Riziki Shemdoe katika hafla fupi iliyofanyika Makao Makuu ya wizara hiyo yaliyopo Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma.

Aidha Bi. Meena amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kumuamini na kumteua katika nafasi hiyo ambapo ameahid kutekeleza maelekezo yote aliyopewa wakati akiapishwa.

Kwa upande wake aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, amewashukuru Watumishi wote wa Wizara hiyo, kwa ushirikiano alioupata na kazi kubwa waliyoifanya katika kipindi chake. 

Vilevile, Prof. Shemdoe amewasihi Watumishi wote kuishi kama familia, kuombeana mema na kuheshimiana ikiwa ni pamoja na kumpa ushirikiano Katibu Mkuu wa sasa kama walivyompatia yeye.

Akitoa Shukrani kwa niaba ya Watumishi wote, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede amemshukuru aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Riziki Shemdoe kwa Utumishi wake uliotukuka pamoja na Uongozi ulioutumikia katika kipindi chote huku pia akimpongeza Katibu Mkuu wa sasa Bi. Agness Meena kwa imani kubwa aliyopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (kulia), akikabidhiwa Nyaraka za Utendaji Kazi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Riziki Shemdoe (kushoto), mara baada ya kuwasili kwa ajili ya makabidhiano ya Ofisi, makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara - Mtumba, Juni 28, 2025 Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (wa tatu kushoto), akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwin Mhede (wa kwanza kulia), mara baada ya kuwasili kwa ajili ya makabidhiano ya Ofisi, makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara - Mtumba, Juni 28, 2025 Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (kulia), akimkabidhi Tuzo ya Heshima, aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (kushoto), mara baada ya kuwasili kwa ajili ya makabidhiano ya Ofisi, makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara - Mtumba, Juni 28, 2025 Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (kushoto), akimkabidhi Tuzo ya Heshima, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, mara baada ya kuwasili kwa ajili ya makabidhiano ya Ofisi, makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara - Mtumba, Juni 28, 2025 Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena (katikati mstari wa mbele), akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Wakurugenzi, Wakuu wa Taasisi na Idara ya Wizara hiyo, mara baada ya makabidhiano ya Ofisi, makabidhiano hayo yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara - Mtumba, Juni 28, 2025 Dodoma.





Ijumaa, 27 Juni 2025

TAKRIBAN WATANZANIA MILIONI 6 WANAJIHUSISHA NA SHUGHULI ZA UVUVI - RAIS DKT SAMIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kutokana na uwekezaji katika sekta ya Uvuvi mazao ya uvuvi yameongezeka kutoka tani 4077.18 zenye thamani ya shilingi bilioni 2.77  mwaka 2020/2021 hadi kufikia tani  543598.9  zenye thamani ya shilingi bilioni 3.04 mwaka 2025.

Mhe. Dkt. Samia amesema hayo wakati akihutubia na kuhitimisha shughuli za Bunge la Jamhuri za Bunge Muungano wa Tanzania hafla iliyofanyika Bungeni Jijini Dodoma leo Juni 27, mwaka 2025.

Aidha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan serikali amesema takriban watanzania milioni 6 wanajihusisha na shughuli za uvuvi .

Pia, amesema kuwa kukamilika kwa bandari ya uvuvi ya Kilwa Masoko kunatarajiwa kuzalisha  ajira  takriban elfu 30,000 ambapo hadi sasa ujenzi wa bandari hiyo unaogharimu shilingi bilioni  279.5 umefikia asilimia 81.9.



MASOKO YA NYAMA NJE YA NCHI YAFUNGUKA MIAKA 4 YA RAIS SAMIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema jitihada za serikali ya awamu ya sita za kufungua masoko nje ya nchi zimeongeza mauzo ya nyama kwa upande wa sekta ya Mifugo kutoka Dola za marekani milioni 4.2 mwaka 2020/2021 hadi kufikia Dola za Marekani milioni 61. 4 Mwaka 2025.

Mhe. Dkt. Samia amesema hayo wakati akihutubia na Kuhitimisha shughuli za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hafla inayofanyika Bungeni Jijini Dodoma leo Juni 27, mwaka 2025.

Aidha Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan serikali itabeba nusu ya gharama ya chanjo ya ng’ombe,Mbuzi na Kondoo huku gharama zote za chanjo ya Kuku zitabebwa na serikali.

Pia Rais Mhe. Dkt. Samia ametoa rai kwa wabunge kuhimiza wananchi kuwa na matumizi bora ya ardhi baina ya wafugaji na wakulima kwa kufanya ufugaji wa kisasa.



Alhamisi, 26 Juni 2025

SEKTA YA UVUVI YATAJWA KUWA NA MAENEO MAHSUSI YA KIMKAKATI, KUPITIA TEKNOLOJIA

Na. Edward Kondela

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman amesema Sekta ya Uvuvi inayo maeneo mahsusi ya kimkakati ili kukuza sekta hiyo kupitia teknolojia.

Akizungumza jijini Dar es Salaam (25.06.2025) wakati akizindua ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi, ametaja maeneo hayo kuwa ni ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani.

“Ripoti itasaidia mahitaji mahsusi ya kufahamu teknolojia ya namna gani inahitajika na kipindi gani ili wakulima wa mwani kuwa na uhakika wa mbegu zinazotumika, mahitaji ya soko na ufugaji wa mazao ya samaki kuwa na tija kwa wananchi.” amesema Mhe. Othman

Amefafanua kuwa kwa muda mrefu dunia imekuwa ikikabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi hivyo umuhimu wa tekonolojia ni dhahiri katika kufanya tathmini halisi ili kwenda na wakati.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede akimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema ripoti hiyo imeangalia maeneo makubwa ikiwemo Sekta ya Uchumi wa Buluu ambayo ina samaki na mwani, huduma za usafirishaji na madini majini ambayo ni muhimu katika uzalishaji.

Dkt. Mhede ameongeza kuwa ripoti hiyo imebaini bado kunahitajika msukumo zaidi wa ushirikiano kati ya watunga sera na wachambuzi wa sera pamoja na sekta binafsi ambao ndiyo watumiaji wa sera hizo ili majibu ya teknolojia yazingatie uhalisia wa kitafiti.

Aidha, amesema kasi ya tekonolojia na tija lazima iendane sawa na ukuaji wa jamii ili mahitaji ya huduma mbalimbali hususan katika Sekta ya Uvuvi yasiwe na mapungufu.

Nao baadhi ya washiriki wa uzinduzi wa ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia katika Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi, wamepata fursa ya kutoa maoni ambapo wamesema ripoti hiyo ni muhimu katika kukuza Sekta ya Uvuvi hususan katika Uchumi wa Buluu.

Wamesema ni muhimu ripoti hiyo ikatumika vyema katika kufikia malengo na kuifanya Tanzania kufaidika na uchumi unaotegemea Bahari ya Hindi.

Umoja wa Mataifa una kitengo mahsusi ambacho kinafanya uchambuzi katika mataifa mbalimbali duniani juu ya uhalisia wa sekta za kiuchumi na mahitaji ya teknolojia ambapo Tanzania ni moja ya mataifa hayo.

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman (wa pili kushoto) akizindua ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi na Kilimo. Hafla hiyo fupi imefanyika jijini Dar es Salaam. (25.06.2025)

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman akizungumza wakati akizindua ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi, ambapo amesema Sekta ya Uvuvi inayo maeneo mahsusi ya kimkakati ili kukuza sekta hiyo kupitia teknolojia. Hafla hiyo fupi imefanyika jijini Dar es Salaam (25.06.2025)

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede akibainisha umuhimu wa ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi yakiwemo ya Sekta ya Uchumi wa Buluu ambayo ina samaki na mwani, huduma za usafirishaji na madini majini ambayo ni muhimu katika uzalishaji. Amebainisha hayo katika hafla fupi ya uzinduzi wa ripoti hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam. (25.06.2025)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) Dkt. Emmanuel Sweke akitoa baadhi ya maelezo kuhusu umuhimu wa ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam. (25.06.2025)

Baadhi ya washiriki wa hafla fupi ya uzinduzi wa ripoti ya kitaalamu katika kutambua mahitaji ya teknolojia kwenye Sekta ya Uvuvi upande wa Bahari ya Hindi, iliyofanyika jijini Dar es Salaam. (25.06.2025)


Jumatatu, 23 Juni 2025

MILIONI 268 ZATUMIKA UKARABATI MNADA WA KINTINKU MANYONI

Na. Hamis Hussein

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekamilisha kwa asilimia 100 ujenzi wa uzio wenye mzunguko wa mita za mraba 500 katika Mnada wa Kinyinku wilayani Manyoni wenye thamani ya shilingi milioni 268, fedha zilizotengwa katika bajeti ya mwaka 2022/ 2023 ikiwa ni sehemu ya ukarabati wa miundombinu kwa ajili ya mazingira wezeshi ya biashara ya mifugo na mazao yake nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti leo Juni 23, Mwaka 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Manyoni Mashariki Mhe. Dkt. Pius Chaya, lililohoji ni  lini  serikali itakamilisha ujenzi wa uzio wa mnada wa Kintinku uliopo Halmashauri  ya Wilaya ya Manyoni mkoani Singida.

Aidha Mhe. Mnyeti ameongeza kuwa  serikali itaendelea kuboresha mindombinu muhimu kurahisisha biashara hiyo katika maeneo mbalimbali nchini.



Jumanne, 17 Juni 2025

WAZALISHAJI WA CHANJO ZA MIFUGO KUUNGANA AFRIKA

Na Daudi Nyingo

◼️ Waandaa Mwongozo wa Kudhibiti Chanjo

Wasajili wa Chanjo na Wakurugenzi wanaosimamia uzalishaji wa chanjo za mifugo kutoka nchi 25 za ukanda wa Afrika wamekutana nchini Tanzania kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo. Mkutano huu umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam.

Akifunga mkutano huo tarehe 17 Juni 2025, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, alisema kuwa mkutano huo umekuja kwa wakati muafaka kwani siku ya jana, tarehe 16 Juni 2025, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alizindua rasmi kampeni ya chanjo za mifugo kitaifa, na ameidhinisha fedha kwa ajili ya kuchanja ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku, sambamba na kuwawekea utambuzi.

“Kikao hiki kina lengo la kuandaa mwongozo ambao utatumika na wazalishaji wa chanjo katika nchi hizo 25, hasa katika kupambana na sotoka ya mbuzi na kondoo. Pia wanakusudia kuanzisha mtandao wa mawasiliano baina yao kwa lengo la kuendelea kupata chanjo bora kwa mifugo ya Afrika.”

“Kitu kitakachotengenezwa Tanzania hakitapishana na kile kinachotoka Kenya, Zambia au nchi nyingine yoyote barani Afrika. Ndiyo maana wote wamekusanyika hapa kuridhia mfumo wa pamoja. Chanjo itakayouzwa Tanzania itauzwa sehemu yoyote Afrika bila vikwazo.” Alisema Prof. Shemdoe

Mkurugenzi wa AU-PANVAC, Dkt. Bodjo S. Charles, alisema kuwa mkutano huu unalenga kuweka viwango vya pamoja na mwongozo utakaosaidia kufanya ukaguzi na kuthibitisha ubora wa uzalishaji wa chanjo, jambo ambalo litahakikisha kuwa vifaa vyote vya uzalishaji vinazalisha chanjo bora. Baada ya hapo, kutakuwa na mtandao wa wadhibiti wa sekta hii ambao watakuwa wakibadilishana taarifa kati yao.

Naye Meneja wa Taasisi ya Chanjo Tanzania (TVI), Dkt. Charles Ngassa, alisema kuwa mkutano huu umewakutanisha mamlaka zinazohusika na usajili wa chanjo pamoja na wakurugenzi wanaozalisha vya chanjo barani Afrika, kwa lengo la kupata mwongozo wa usajili wa chanjo ya sotoka ya mbuzi na kondoo.

“Chanjo hiyo ni muhimu sana kwa kutokomeza ugonjwa huo duniani ifikapo mwaka 2030. Kama bara, tunahitaji kuwa na mwongozo mmoja ili kupata chanjo bora kwa mifugo wetu.” Alisema DKt. Mayenga

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi wa AU-PANVAC, Dkt. Bodjo S. Charles kwenye mkutano wa Wasajili wanaousika na chanjo za mifugo pamoja na wakurugenzi wanaozalisha vya chanjo za mifugo barani Afrika kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo tarehe 17 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam ambapo Mkutano huo umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe akifungua akifungua mkutano wa Wasajili wanaousika na chanjo za mifugo pamoja na wakurugenzi wanaozalisha vya chanjo za mifugo barani Afrika kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo tarehe 17 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam ambapo Mkutano huo umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (katikati) akiwa kwenye picha ya Pamoja na Wasajili wanaousika na chanjo za mifugo pamoja na wakurugenzi wanaozalisha vya chanjo za mifugo barani Afrika kwenye mkutano wa kujadili namna ya kuwa na mfumo wa pamoja wa kutokomeza ugonjwa wa sotoka ya mbuzi na kondoo tarehe 17 Juni 2025 katika Ukumbi wa King Jada Hotel uliopo jijini Dar es Salaam ambapo Mkutano huo umeanza tarehe 16 hadi 20 Juni 2025.






Jumatatu, 16 Juni 2025

RAIS SAMIA ATOA RUZUKU YA BIL. 216 CHANJO ZA MIFUGO 2025/2029

Na. Omary Mtamike

◼️Chanjo ya kuku sasa kutolewa bure

◼️akabidhi pikipiki 700 kwa Maafisa ugani

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa ruzuku ya Shilingi Bil. 216 kwenye kampeni ya kuchanja mifugo na utambuzi kwa kipindi cha miaka 5 kuanzia mwaka huu.

Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya chanjo hizo na Utambuzi wa Mifugo iliyofanyika kwenye Viwanja vya Nyakabindi mkoani simiyu Mhe. Dkt. Samia amewataka Wakuu wa Mikoa yote nchini kusimamia matumizi ya  vifaa hivyo na kuhakikisha vinatumika kwa maslahi ya wafugaji kama ilivyokusudiwa.

Aidha Mhe. Dkt. Samia amebainisha kuwa hivi sasa Serikali imeanza kuona matunda ya mabadiliko ya ufugaji wa kisasa yaliyofanyika ambapo ameongeza kuwa Serikali itaendelea kuboresha sekta hiyo ili tija iendelee kuonekana.

"Serikali imedhamiria kutokomeza magonjwa ya Mifugo na ndio maana leo tunazindua mpango huu wa chanjo 2025/2029 na hapa kwa dhati kabisa nataka niwapongeze kabisa wafugaji wote Tanzania kwa sababu mmekubali kuchangia nusu na sisi Serikali tutoe nusu kwenye chanjo ya Ng'ombe, Mbuzi na Kondoo" Ameongeza Mhe. Dkt. Samia

Aidha Mhe. Dkt. Samia amebainisha kuwa baada ya kutoa ruzuku kwenye sekta ya kilimo, Serikali imeanza kutoa ruzuku kwenye sekta ya Mifugo kwa upande wa chanjo za Mifugo.

Mhe. Dkt. Samia amesema kuwa Serikali imeweka mazingira wezeshi kwa sekta ya umma na sekta binafsi ambazo zimetengeneza chanjo zitakazotumika kwenye kampeni hiyo na amefarijika na mipango yao ya kuhakikisha Tanzania inajitegemea kwa upande wa chanjo za mifugo nchini.

"Tulipokuwa tukiagiza wakati mwingine tunakuwa na mashaka kuhusu usalama wa chanjo tunazotumia lakini sasa kwa kuwa zimetengenezwa hapa hapa na wazawa inatuongezea imani ya chanjo zilizopo hivyo niipongeze Wizara kwa uamuzi huo wa kutumia wazalishaji wa ndani kwenye upande huu.

Akizungumzia kuhusu hereni za kielektroniki Mhe. Dkt. Samia amesema kuwa kwa muda mrefu Serikali imekuaa ikikisia kuhusu kanzidata ya Mifugo iliyopo nchini hivyo hereni hizo zitakuwa ni nyenzo ya upatikanaji wa kanzidata hizo.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mhe. Rais, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji mbali na kumshukuru Mhe. Dkt. samia kwa kutoa ruzuku hiyo amesema kuwa tayari Wizara yake imeshanunua vifaa vya kutekelezea zoezi hilo kwa awamu ya kwanza ambavyo ni pamoja na vifaa vya kutolea chanjo, pikipiki 700 na vishkwambi 4500 vitakavyotolewa kwa Maafisa mifugo kwenye Halmashauri zote nchini.

Mhe. Dkt. Kijaji ameongeza kuwa katika kampeni hiyo wanaratajia kuchanja magonjwa 5 ambayo ni Homa ya mapafu kwa upande wa Ng'ombe, Sotoka kwa upande wa Mbuzi na Kondoo, Kideri/mdondo, Ndui na mafua ya kuku kwa upande wa kuku wa kienyeji.

"Aidha zoezi hili linatarajiwa kuzalisha ajira za muda mfupi 3540 ambazo zitahusisha wataalam wa afya ya Mifugo waliopo nje ya mfumo rasmi wa ajira.

Chanjo hizo zilizozalishwa na viwanda vilivyopo hapa nchini zitatolewa kwa kufuata mwongozo wa uliotolewa na Wizara hiyo ambapo ng'ombe atachanjwa kwa shilingi 500 badala ya 1000 iliyokuwa awali, mbuzi na kondoo watachanjwa kwa shilingi 300 badala ya 600 ya awali huku chanjo ya kukabiliana na magonjwa ya kuku ikitolewa bure.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua rasmi kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya nanenane  Nyakabindi wilayani Bariadi mkoa Simiyu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua Mifugo mara Baada ya kuzindua rasmi kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya nanenane Nyakabindi wilayani Bariadi mkoa Simiyu.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikabidhi kishkambi kwa Afisa Ugani Lusia Nyangoma ambacho kitatumika wakati wa kampeni ya chanjo na Utambuzi kwenye hafla ya uzinduzi wa kampeni hiyo leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya nanenane Nyakabindi wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimpa maelekezo Afisa Ugani Absolom Ndyamkama kabla ya kumkabidhi funguo ya Pikipiki kwa lengo la kufanya ufuatiliaji wa zoezi la chanjo wakati wa uzinduzi wa  kampeni ya kitaifa ya  chanjo na utambuzi wa mifugo leo Juni 16, 2025 katika viwanja vya nanenane Nyakabindi,  Bariadi mkoani Simiyu.










BALOZI DKT. NCHIMBI AHIMIZA KAMPENI YA TUTUNZANE ITUMIKE NCHI NZIMA

 Na Chiku Makwai- WMUV SIMIYU

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewahimiza wafugaji na wakulima kote nchini kuitumia kampeni ya Tutunzane ambayo imelenga kuimarisha maelewano na ustawi kati ya wakulima na wafugaji na kuondokana na migogoro ya matumizi ya ardhi.

Balozi Dkt. Nchimbi amesema hayo leo Juni 15, mwaka 2025 katika eneo la Nyakabindi Wilaya ya Bariadi Mkoa wa Simiyu wakati akifungua Kongamano la wafugaji kwa mwaka 2025 ambapo amehimiza kampeni hiyo itumike nchi nzima kuimarisha umoja wa jamii ya wafugaji na wakulima.

" Kampeni hii ya tutunzane iliyoanzishwa na Mkuu wa  Wilaya ya Mvomero imeonyesha thamani ya wafugaji na wakulima kwa kuimarisha maelewano baina yao kwani sisi sote ni taifa moja, hivyo kampeni hii ya tutunzane itumike nchi nzima ili wafugaji wote wanufaike" alisema Balozi Dkt. Nchimbi.

Aidha Balozi Dkt. Nchimbi ameogeza kwa kusema kuwa Chama cha Mapinduzi kinadhamira ya kuinua ufugaji kwakutambua sekta ya mifungo ni sekta muhimu katika ukuwaji wa uchumi na kuzalisha ajira kwa vijana hivyo kitaenedelea kutoa kipaubele lengo ikiwa ni kuimarisha na kuwezesha upatikanaji wa ufugaji wa kisasa.

Katika hatua nyingine Balozi Dkt. Nchimbi ameipongeza serikali kwa kuiongezea fedha kweye bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kufikia bilioni 476.6 mwaka huu wa fedha 2025/2026 jambo litaisaidia wizara kutekeleza miradi ya sekta za mifugo na uvuvi.



DKT. ASHATU- WAFUGAJI KUUPOKEA UFUGAJI WA KISASA

 Na Chiku Makwai - WMUV SIMIYU

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema kuwa wafugaji wameonyesha nia kuupokea ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija kwenye sekta ya mifugo nchini.

Mhe. Dkt. Kijaji amesema hayo leo (Juni 15, 2025) wakati wa  Kongamano la Wafugaji Tanzania lililofanyika katika Viwanja vya Nanenane Nyakabindi vilivyopo Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.

“Tupo tayari kubadilika na kuanza kufuga kisasa kwa kutumia njia za kisasa ili kufikia mageuzi makubwa ya serikali kwenye Sekta ya Mifugo nchini” amesema Mhe. Dkt. Kijaji

Aidha, amesema wizara imefanya mikutano na wafugaji wote nchini kwa kukutana na wawakilishi wao ili kujadili changamoto za sekta hiyo na kuzigeuza kuwa fursa ili kuiboresha Sekta ya Mifugo.

Pia, amesema kwa kutambua mchango mkubwa unaotokaana na sekta hiyo serikali itaendelea kushirikiana na wadau wake wote waliopo katika mnyororo mzima wa Sekta ya Mifugo ili kuipa thamani sekta hiyo. 

Ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa wa Simiyu kujumuika katika Uzinduzi wa Kaampeni ya Chanjo Kitaifa na Utambuzi wa Mifugo utakaofanyika kesho (Juni 16, 2025) katika Viwanja vya Nanenane Nyakabindi mkoani hapo ambapo Mgeni Rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.



WAFUGAJI WAASWA KUFUGA KISASA ILI KUONGEZA TIJA

 Na. Stanley Brayton, WMUV 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amewataka wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kufuga kisasa ili kuongeza tija katika Mifugo.

Akizungumza katika Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo yalioshirikisha nchi tatu ikiwemo Tanzania, Kenya na Namibia, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani, Mhe. Mnyeti, amesema Serikali awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sasa inaendelea na mchakato wa kuhamasisha wafugaji kuachana na Ufugaji wa kizamani na kuingia kwenye Ufugaji wa kisasa wenye tija.

“ni matumaini yangu kuwa wafugaji mtachangamkia fursa hii kwa kutafuta na kununua mbegu bora za mifugo zitakazowaletea tija zaidi kwenye ufugaji wenu kuliko kuendelea na Ufugaji wa kizamani usio na tija.” ameseama Mhe. Mnyeti 

Aidha, Mhe. Mnyeti amesema maonesho haya ya mifugo yana lengo la kuhamasisha matumizi ya mbegu bora za mifugo ili kumwezesha mfugaji kuzalisha mazao mengi ya mifugo na kupata faida zaidi, pamoja na kuiwezesha Sekta ya Mifugo kuchangia kikamilifu katika ukuaji wa uchumi wa Taifa, pamoja na kuwawezesha wafugaji kuleta mabadiriko katika Ufugaji wao wa kisasa.

Vilevile, Mhe. Mnyeti amesema swala la Malisho ya Mifugo imekuwa changamoto na wafugaji wengi wanatembea na rundo kubwa la mifugo kwa ajili ya kutafuta malisho, lakini Ufugaji wa kisasa utasaidia kuwa na Mifugo michache yenye tija ambayo italeta faida kubwa kutokana na uzito na ubora wa mifugo kuliko kuwa na Mifugo mingi yenye uzito mdogo ambayo haina faida yeyote wala tija.

Pia, Mhe. Mnyeti amewataka wafugaji kutafuta mbegu Bora za Malisho na kuzipanda kwa wingi kwa ajili ya Mifugo yao ili Mifugo iweze kupata chakula Cha kutosha kitakachowafanya kuwa Bora zaidi, na amesisitiza wafugaji kuendelea kujitokeza kwenye Benki na Serikali ili waweze kupata mikopo ambayo itawasaidia kukua katika swala la Ufugaji wa Kibiashara.

Halikadhalika, Mhe. Mnyeti amebainisha kuwa Serikali inaendelea kutatua changamoto zinazowakabili Wafugaji na wadau wa Sekta ya Mifugo, ikiwa ni pamoja na kufanya jitihada zake za kuhakikisha wafugaji wanafikiwa na kupata huduma za ushauri wa kitaalam kwa wakati ambapo imeendelea kuajiri maafisa ugani pamoja na kusambaza vitendea kazi kwa maafisa wote, kwani Lengo la Serikali ni kuwa na Afisa ugani katika ngazi ya Kijiji ili kuwawezesha wafugaji kufikiwa na huduma kwa wakati.

Mhe. Mnyeti amekishukuru Chama cha Wafugaji Ng’ombe Kibiashara, Ranchi ya Mbogo pamoja na wadau wengine kwa kuandaa na kufanikisha maonesho hayo ambayo yameambatana na mnada wa mbegu bora za mifugo zenye tija zaidi kwenye uzalishaji wa Mifugo Bora mana wameungana na Serikali katika kuhamasisha Ufugaji wa kisasa.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (aliyenyoosha mikono juu), akionyesha ishara ya Uzinduzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo baada ya kukata utepe, wakati wa Ufunguzi wa Maonesho hayo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti, akihutubia wadau wa Sekta ya Mifugo, wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (wa pili kushoto), akisalimiana  na Kamishna Mkuu wa Namibia nchini Tanzania, Mhe. Lebbius Tobias (wa nne kulia), mara baada ya kuwasili kwenye Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani, wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (wa kwanza kulia), akisalimiana  na Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Ndg. Isaac Njenga (wa kwanza kushoto), mara baada ya kuwasili kwenye Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani.

Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Uzalishaji na Masoko Sehemu ya Uzalishaji Mifugo, Dkt. Yeremia Sanka (wa pili kulia), akimuelezea Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (wa nne kulia), juu ya shughuli zinazofanyika katika Sekta ya Mifugo, wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Ranchi ya Mbogo, Ndg. Naweed Mulla.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (anaekunywa Juisi), akionja bidhaa ya Ranchi ya Mbogo (Juisi) inayotokana na mchanganyiko wa Maziwa na Matunda, wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani, wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (katikati), akitazama mbegu Bora za Mifugo, wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani, wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (wa tatu kushoto), akikabidhi Cheti cha Usajili kwa Wafugaji wanaofuga ng'ombe za mbegu nchini, wakati wa Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (waliokaa katikati), akiwa kwenye picha ya Pamoja na Maafisa wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, mara baada ya Ufunguzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Ufugaji Kibiashara na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo, Juni 14, 2025, Chalinze - Pwani.


DKT. KIJAJI AKAGUA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA KAMPENI YA CHANJO ZA MIFUGO NA UTAMBUZI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametembelea na kufanya ukaguzi wa maandalizi ya Uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya mifugo na utambuzi leo, Juni 13, mwaka 2025 katika Viwanja vya nane nane eneo la Nyakabindi wilayani Bariadi Mkoa wa  Simiyu.

Mhe. Dkt. Ashatu ameambatana na  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Riziki Shemdoe, Naibu Katibu Mkuu (Mifugo) Bw. Abdul Mhinte na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa wizara hiyo  Dkt. Benezeth Lutege.

Katika Ukaguzi huo Waziri Dkt. Kijaji amekagua eneo la uzinduzi wa kampeni ya chanjo, sehemu ya itakayotumika kuwakabidhi vitendea kazi wataalam watakaotekeleza zoezi la Chanjo Kitaifa. Pia ametembelea eneo ambalo litafanyika Kongamano la Wafugaji siku ya Jumapili ya Juni 15, 2025 kabla ya Uzinduzi wa Kampeni ya Chanjo na Utambuzi Kitaifa Juni 16, mwaka 2025 mkoani Simiyu.






Ijumaa, 13 Juni 2025

MAFUNZO YA MATUMIZI YA MFUMO KIDIJITALI WA UTAMBUZI WA MIFUGO YATOLEWA

Na Chiku Makwai-WMUV SIMIYU

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Abdul Mhinte amefungua mafunzo ya matumizi ya mfumo kidijitali  wa utambuzi wa mifugo kwa Waratibu wa Chanjo na Maafisa Tehama kanda ya ziwa.

Akizungumza na wataalam hao leo Juni 12, 2025 Mkoani Simiyu Bw. Mhinte amesema kuwa lengo la kuwapatia mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa kuhusu matumizi ya mfumo huo wa kidijitali.

Aidha Mhinte amewasisitiza kuwa ni wajibu wa kila mtaalam kutunza vifaa hivyo ili viweze kuwasaidia katika shuguli hiyo mpaka itakapo kamilika.