Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2026

JAMII YATAKIWA KUONGEZA JUHUDI MAPAMBANO DHIDI YA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI.

Picha
Wananchi wametakiwa kuongeza juhudi katika kupambana na athari zinazotokana na mabadiliko ya hali ya nchi yanayoikumba nchi na dunia kwa ujumla. Wito huo umetolewa  leo Juni 1, 2026 na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Kwagilwa Reuben (MB) wakati akifungua maadhimisho ya wiki ya mazingira katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma. Mhe. Kwagilwa amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha mazingira yanatunzwa ili kuwezesha nchi kutimiza mipango ya Dira 2050 kwani athari za mabadiliko ya tabia ya nchi yana athari hasi kwenye uchumi wananchi na dunia. “Mazingira ni Uchumi pia mazingira ni afya, tunatakiwa kuyatunza  mazingira yetu ili malengo yetu ya Dira ya Taifa 2050 yanatimia.  Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi tutaendelea kutekeleza wajibu wetu  katika kulinda mazingira.” Amesisitiza Mhe.Kwagilwa. Kwa upande wake mratibu wa maonesho hayo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Bw. M...

TANZANIA KUWA NA MKAKATI MAALUM WA MAWASILIANO WAKATI WA MLIPUKO WA MAGONJWA YA MIFUGO

Picha
Na. Chiku Makwai – ARUSHA Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo. Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika. Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapem...

MRADI WA BBT KUTENGENEZA AJIRA 6000 KWA WANAWAKE NA VIJANA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kilimo cha Malisho, ambao unatekelezwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, umepanga kuwawezesha wanawake na vijana 6000 ndani ya muda wake wa utekelezaji wa Miaka Mitano wa Mradi huo, ambao ukiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake na vijana katika ujasiliamali wa Biashara ya Mifugo. Akizungumza leo Juni 1, 2026 Mkoani Morogoro, katika Warsha ya Upitiaji, Uhakiki wa Uwasilishaji wa Ripoti ya awali ya Jinsia na Ujumuishaji wa Kijamii katika Programu hiyo ya BBT, Meneja Mradi wa BBT Upande wa Jinsia na Ujumuishaji wa Kijamii, Bi. Neema Urassa amesema Mradi huo una lengo la kuwawezesha Wanawake na Vijana kupitia shughuli za unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo kibiashara pamoja na Kilimo cha Malisho ya Mifugo. "Mradi huu unawalenga zaidi Wanawake na vijana, ambao kupitia Mradi huu watapata kujifunza vitu mbalimbali kwa vitendo katika mnyororo mzima wa thamani wa...

DKT. BASHIRU AZINDUA MAADHIMISHO YA KITAIFA WIKI YA MAZIWA 2026

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa leo Mei 31,2026 amezindua Maadhimisho ya 29 ya kitaifa ya wiki ya Maziwa ambayo mwaka huu yanafanyika kwenye viwanja vya Mwembetogwa mkoani Iringa. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Balozi Dkt. Bashiru amesema kuwa Maadhimisho hayo yamekuwa na lengo la kuhamasisha uwekezaji, urasimishaji wa tasnia ya maziwa,matumizi ya maziwa bora na salama ili kulinda afya ya mlaji, kukuza biashara rasmi ya maziwa na kuhakikisha tasnia hiyo inaongeza mchango wake kwenye maendeleo ya kaya za wafugaji na uchumi wa Taifa kwa ujumla. “Sisi kama wizara kwa dhati kabisa kupitia mradi wetu wa mageuzi ya tasnia ya maziwa na mabadililo ya tabia nchi tutahakikisha mfugaji anajikwamua kiuchumi kwa sababu mradi huu umekusudiwa kununua na kufuga ng’ombe bora wa maziwa, kufanya ujenzi wa miundombinu itakayowezesha ufugaji bora, kuongeza uzalishaji na kuboresha mnyororo wa thamani wa maziwa, ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kukusanyia maziwa, kupa...

DKT. BASHIRU AKOSHWA UWEKEZAJI SEKTA YA MAZIWA IRINGA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na kamati  ya kudumu ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo  wamekoshwa na kiwango cha uwekezaji uliofanywa kwenye sekta ya Maziwa mkoani Iringa. Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea na kukagua shughuli za ufugaji na uzalishaji maziwa kwenye kiwanda cha ASAS, Balozi Dkt. Bashiru amewataka wafugaji kuheshimu misingi ya sayansi na taaluma ili wawe na ufugaji wenye ufanisi na wa kibiashara. “Tumeona wataalam ambao amewaajiri ASAS wanaelewa kazi yao na katika hili nchi imefundisha sana wataalam hivyo ni lazima tuheshimu utaalam wao lakini pia tuwape nafasi na nyenzo za kuonesha utaalam wao” Amesisitiza Balozi Dkt. Bashiru. Aidha Balozi Dkt. Bashiru amempongeza mwekezaji huyo kwa kuweka miundombinu bora ya uvunaji wa maji ya mvua na matumizi bora ya ardhi kwa upande wa uzalishaji wa malisho ya mifugo ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ambayo yamekuwa yakitolewa na Serikali kwa wafugaji ili kuwa na uhak...

BI. MEENA AWAASA WAFUGAJI KUJIFUNZA TEKNOLOJIA MBALIMBALI ZA UFUGAJI WA KISASA

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amewaasa Wafugaji kujifunza teknolojia mbalimbali za ufugaji wa kisasa ili kufuga kisasa na kwa tija zaidi. Akizungumza leo Mei 30, 2026 Mkoani Shinyanga, katika Maonesho ya Mifugo ya Kanda ya Ziwa yajulikanayo kama Lake Zone Livestock expo 2026 nyenye Kauli mbiu ya Tufuge Kibiashara ambayo yameandaliwa na Kampuni ya FARMFLEX Group, Bi. Meena amesema Maonesho hayo ni fursa kwa wafugaji katika kujifunza na kupata elimu kuhusu teknolojia mbalimbali za ufugaji ili kuepukana na ufugaji wa kizamani na kujikita katika ufugaji wa kisasa wenye tija na wa kibiashara.  "Sisi tunaamini mifugo ni biashara, mifugo ni migodi na mifugo ni utajiri, na ndio mana tunawataka wafugaji wetu wajifunze kufuga kisasa ili kuongeza tija, ili kuhakikisha Sekta ya Mifugo inaongeza ajira, kipato cha wafugaji na mchango wake katika uchumi wa nchi." amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena ameweka wazi jinsi Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na ...

MIPANGO MAHSUSI IKIWEMO YA TASFAM YATAJWA KUONGEZA THAMANI YA PWEZA

Picha
Na. Edward Kondela Wadau wa uvuvi waja na mipango mahsusi ya kuongeza thamani ya samaki aina ya pweza ukiwemo wa kuboresha miundombinu ya masoko na maeneo ya kushushia samaki hao, kupitia Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Bahari Tanzania (TASFAM). Akizungumza (28.05.2026) jijini Dar es Salaam, wakati wa kufungua kikao cha siku mbili cha wadau hao kutoka katika halmashauri za Ukanda wa Pwani zinazovua pweza, Mkurugenzi Msaidizi wa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Christian Nzowa amesema changamoto kubwa kwa sasa ni upotevu wa mazao hayo baada ya kuvuliwa hususan nyakati za mvua na mavuvi yanapokuwa mengi. Akimwakilisha Katibu Mkuu wa wizara hiyo Bi. Agnes Meena, Bw. Nzowa amesema kwa sasa miundombinu  ya barafu na kuhifadhia pweza bado haijakaa vizuri, hivyo kupitia mradi wa TASFAM ambao umejikita kuboresha sekta ya uvuvi katika Ukanda wa Pwani, baadhi ya miundombinu hiyo itaboreshwa hivyo kuongeza thamani ya samaki hao ambapo kwa siku z...

DKT. MADELE ATUMA UJUMBE WIKI YA MAZIWA 2026.

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amewataka wananchi wa mkoa wa Iringa na maeneo jirani kujitokeza kwenye maadhimisho ya kitaifa ya wiki ya maziwa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwembetogwa mkoani Iringa. Dkt. Madele ametoa ujumbe huo Mei 29,2026 muda mfupi baada ya kukagua shughuli zinazofanywa na wadau mbalimbali wa sekta ya Mifugo waliojitokeza kwenye maonesho hayo ambapo amesisitiza kuwa lengo la Serikali ni kuhamasisha unywaji wa maziwa ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo. “Mradi tuliouona mbele yetu hapa ni mkubwa na umelenga kufanya mapinduzi kwenye tasnia ya maziwa ambapo lengo lake kubwa ni kuhakikisha tunaleta ng’ombe bora wa maziwa na wafugaji wetu watapata fursa ya kufahamu teknolojia za uzalishaji wa mbegu bora” Ameongeza Dkt. Madele. Dkt. Madele amesema kuwa maziwa ni fursa kubwa ya kiuchumi huku ikinufaisha wadau na makampuni mbalimbali yanayofanya kazi kupitia tasnia hiyo. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Fab...

DKT. MDETELE AELEZEA MPANGO MKAKATI WA SERIKALI KUTOKOMEZA MAGONJWA YA MIFUGO KIKAO CHA ADB

Picha
◾Aelezea uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya Tanzania katika Huduma za Mifugo ikiwemo Udhibiti wa Magonjwa na Utambuzi wa Mifugo. Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Msaidizi sehemu ya Magonjwa ya Mlipuko na magonjwa yasiyo na Mipaka (E&TADs), Dkt. Daniel Mdetele ameelezea Mpango Mkakati wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutokomeza Magonjwa ya Mifugo ili kuongeza uzalishaji wa Mifugo yenye ubora zaidi ikianzia kwa Mifugo yenyewe hadi Mazao yake. Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB), uliofanyika leo Mei 28, 2026 nchini Jamuhuri ya Congo (Congo Brazzaville), Dkt. Mdetele ameelezea jinsi uwekezaji huo mkubwa ulivyofanywa na Serikali ya Tanzania katika Huduma za Mifugo kupitia Mpango wa Kitaifa wa Miaka Mitano wa Udhibiti wa Magonjwa na Utambuzi wa Mifugo wenye thamani ya Dola za kimarekani milioni 85. “Mwaka 2025/2026, jumla ya Dola Milioni 24 zimeshatolewa kugharamia Chanj...

SERIKALI YAONGEZA HAMASA YA UNYWAJI WA MAZIWA, WATOTO WAPEWA KIPAUMBELE

Picha
Serikali kupitia Bodi ya Maziwa Tanzania imeendelea kuhamasisha matumizi ya maziwa nchini kwa kutoa elimu kwa wananchi, wanafunzi na wadau wa sekta kuhusu umuhimu wa maziwa katika kuboresha afya na lishe. Akizungumza wakati wa ugawaji wa paketi 2,110 za maziwa ya mililita 500 kwa wanafunzi wa shule sita za msingi mkoani Iringa, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya 29 ya Maziwa Kitaifa yanayoendelea kuanzia Mei 25 hadi Juni 1, 2026, Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini Prof. George Msalya, alisema serikali imejipanga kuhakikisha Watanzania, hususan watoto, wanapata virutubisho muhimu vinavyopatikana katika maziwa kwa ajili ya ukuaji bora wa mwili na akili. Prof. Msalya alisema watoto wamepewa kipaumbele katika mkakati wa kuongeza matumizi ya maziwa nchini kutokana na mahitaji yao makubwa ya virutubisho vinavyopatikana kwenye maziwa. Aidha Prof. Msalya ameeleza kuwa serikali imeanza kutekeleza mpango wa kupeleka maziwa shuleni mara kwa mara ili kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kutumia ...