Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2026

HISTORIA YAANDIKWA! RAIS SAMIA AZINDUA MELI YA UVUVI BAHARI KUU

Picha
◼️Ni ya kwanza tangu nchi ilipopata uhuru mwaka 1961 ◼️Ina uwezo wa kubeba hadi tani 48 kwa wakati mmoja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua meli ya kwanza ya Uvuvi wa bahari kuu ambayo itaiwezesha nchi kuvua samaki waliopo kwenye  ukanda wa maalum wa uchumi wa bahari (EEZ) ambao awali haukuweza kufikiwa kutokana na kukosekana kwa meli ya aina hiyo. Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Makao makuu ya Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam ambapo Mhe. Rais Samia amesema kuwa hatua hiyo inalenga kukuza fursa za ajira, kuongeza mapato ya Serikali na kuboresha lishe. “Niipongeze Serikali ya Japan kwa kushirikiana nasi katika kutengeneza meli hii na kupitia wao kwa kushirikiana na UNDP tutapata boti mbili za kasi ambazo zitasimamia doria ya uvuvi wa bahari kuu” Ameongeza Mhe. Rais Samia. Aidha Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha sekta ya Uvuvi kupitia ujenzi wa bandari...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA EQUITY BENKI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amekutana na Watendaji Wakuu wa Benki ya Equity, na kufanya nao mazungumzo ambayo yalilenga kuboresha na kukuza Sekta za Mifugo na Uvuvi kwa kuwawezesha Wafugaji na Wavuvi kupata mikopo kwa urahisi zaidi. Akizungumza leo Aprili 23, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao cha kuimarisha mashirikiano hayo ili kukuza Sekta hizo, kikao kilichofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara hiyo zilizopo Kambarage Towel, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru, amesema Wizara kwa sasa inaendelea kukutana na wadau mbalimbali wa Sekta za Mifugo na Uvuvi ili kuweza kuwaelezea malengo ya Serikali katika kukuza Sekta zote mbili na kuona namna za kukuza Sekta hizo. "hii yote imelenga katika kusikiliza changamoto zao mbalimbali pamoja na maoni yao, katika kuimarisha Sekta hii na ndio mana leo tumekutana na Uongozi wa Benki ya Equity ili kuangalia namna gani wafugaji na wavuvi wanaweza pata mikopo ili waweze kutanua wigo wa shughuli zao za biashara" amesema...

WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UONGOZI NA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA PWANI WATAKIWA KUSIMAMIA RASILIMALI ZA BAHARI KWA UWAZI NA USAWA

Picha
Na. Maria Mtambalike Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mafunzo,Tafiti na Huduma za Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw Samwel Mdachi wakati akifunga mafunzo ya uongozi na usimamizi wa rasilimali za pwani kwa washiriki 12 waliopata mafunzo kwa siku 14 kuanzia tarehe 8 April mpaka  tar 21 April 2026 katika chuo cha Uvuvi FETA.  Bw Mdachi amesema kuwa mafunzo haya hayatakuwa na maana kama washiriki hawatafanya kazi zao kwa ubora na kwa vitendo zaidi huku akiwataka watumie mbinu walizojifunza kutatua migogoro kwa amani. Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt Semvua Mzighani ambao wameendesha mafunzo hayo kwa kushirikiana na Shirika la IUCA kupitia mradi wa  Re sea amesema FETA itaendelea kushirikiana na  wadau mbalimbali katika utoaji wa elimu katika jamii. Naye Mwakilishi kutoka IUCN ambae ni meneja wa program ya uhifadhi wa bahari Bw Joseph Orila amesema kuwa lengo la mradi wao ni kutoa mafunzo kwa washiriki/wakufunzi ambao wa...