HISTORIA YAANDIKWA! RAIS SAMIA AZINDUA MELI YA UVUVI BAHARI KUU
◼️Ni ya kwanza tangu nchi ilipopata uhuru mwaka 1961 ◼️Ina uwezo wa kubeba hadi tani 48 kwa wakati mmoja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua meli ya kwanza ya Uvuvi wa bahari kuu ambayo itaiwezesha nchi kuvua samaki waliopo kwenye ukanda wa maalum wa uchumi wa bahari (EEZ) ambao awali haukuweza kufikiwa kutokana na kukosekana kwa meli ya aina hiyo. Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Makao makuu ya Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam ambapo Mhe. Rais Samia amesema kuwa hatua hiyo inalenga kukuza fursa za ajira, kuongeza mapato ya Serikali na kuboresha lishe. “Niipongeze Serikali ya Japan kwa kushirikiana nasi katika kutengeneza meli hii na kupitia wao kwa kushirikiana na UNDP tutapata boti mbili za kasi ambazo zitasimamia doria ya uvuvi wa bahari kuu” Ameongeza Mhe. Rais Samia. Aidha Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha sekta ya Uvuvi kupitia ujenzi wa bandari...