Machapisho

DKT. BASHIRU AHIMIZA KAMPENI YA TUTUNZANE KUTATUA MIGOGORO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewahimiza wafugaji na wakulima kote nchini kuzingatia Kampeni ya Tutunzane inayotekelezwa Wilayani Mvomero inayolenga kuimarisha mahusiano baina yao ili kuepukana na migogoro na uhasama unaotokana na matumizi ya ardhi kati ya Wafugaji na watumiaji wengine wa Ardhi.  Balozi Dkt. Bashiru ametoa wito huo  leo Machi 06, 2026 wakati  akizungumza na Uongozi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma ambako amefika kutekeleza maelekezo ya Waziri Mkuu yaliyomtaka kufika katika Wilaya hiyo kwa ajili ya kuimarisha uhusiano baina ya wakulima na wafugaji, hivyo amewahimiza kuiga na  kuzingatia kampeni ya tutunzane . “Mhe. Rais mara nyingi amekuwa akisema hafurahishwi na migogo kati ya wakulima na wafugaji hivyo niwasihi viongozi wenzangu na wakulima na wafugaji tujifunze kupitia kampeni ya tutunzane ya Mvomero ili kuondokana na uhasama huu ambao unaturudisha nyuma.” Alisema Dkt. Bashiru. Pia, amesema ...

VITUO 31 VYASITISHWA KUTOA HUDUMA ZA AFYA YA WANYAMA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Baraza la Veterinari Tanzania (VCT) limesitisha Huduma za Vituo 31 vya Huduma za Afya ya Wanyama Mkoani Dar es Salaam, hii ni kutokana na Vituo hivyo kutokuwa na uhalali na kutokidhi vigezo vya kutoa Huduma hizo, ikiwemo kutokuwa na Usajili pamoja na kutozingatia Sheria ya Veterinari SURA 319 ya mwaka 2003. Akizungumza kwa niaba ya Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania (VCT), wakati wa Ukaguzi wa Vituo mbalimbali vya kutolea Huduma za Afya ya Wanyama pamoja na Wataalam wake, leo Machi 6, 2026 Mkoani Dar es Salaam, Mkaguzi wa Baraza hilo, Dkt. Winston Billy, amesema mpaka sasa wamekagua jumla ya vituo 261 vya Huduma hizo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam na kukuta changamoto kwenye Vituo 31 ambavyo havijakidhi vigezo na kuamua kusitisha Huduma za Vituo hivyo. "tumesitisha Huduma kwenye Vituo hivi kutokana na wamiliki kutofuata Sheria za Veterinari na tumewaelekeza wamiliki na Wataalam wa Huduma za Afya ya Wanyama kufuata Sheria, Kanuni na...

DKT. LUGENDO AITAKA FETA KUZALISHA KWA WINGI NA KUBORESHA BIDHAA ZA MWANI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Mwenyekiti wa Bodi ya Tatu ya Ushauri ya Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), Dkt. Blandina Lugendo ameitaka FETA kuboresha na kuzalisha zaidi bidhaa za mwani kwa ubora mkubwa na kwa wingi ili kuleta tija katika Sekta ya Uvuvi. Akizungumza leo Machi 6, 2026 jijini Dodoma katika Kikao cha Kwanza cha Bodi, Dkt. Lugendo amesema soko la mazao ya mwani linapanda kwa kasi sana kwa sababu ni lishe na ni tiba kwa mwanadamu, hivyo ni jumuku la FETA kuhakikisha kuwa wanazalisha bidhaa bora za mwani ili watu waweze kuzipata kwa urahisi.  "tunatakiwa kuboresha kwa wingi bidhaa hizi za mwani na tufanye uzalishaji wa kibiashara na wenye tija ambao utaleta manufaa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla." amesema Dkt. Lugendo Aidha, Dkt. Lugendo amewataka FETA kuandaa Mpango Mkakati wa Kibiashara wa bidhaa zinazozalishwa na FETA ili kuongeza mapato katika Wakala hiyo.  Vilevile, Dkt. Lugendo ameitaka FETA kutafuta mbinu bora za kulinda viwango vya ubora wa bidhaa z...

MHE. KAMANI AITAKA FETA KUONGEZA UZALISHAJI WA VIFARANGA VYA SAMAKI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, ameitaka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kuongeza uzalishaji wa vifaranga vya samaki kutoka kiwango cha sasa na kufikia kati ya milioni 5 hadi 10 kwa mwezi, ili kuchochea ukuaji wa Sekta ya uvuvi na kuongeza tija kwa wananchi. Akizungumza leo Machi 5, 2026 jijini Dodoma katika hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Tatu ya Ushauri ya FETA, Mhe. Kamani amesema kuwa ongezeko la uzalishaji wa vifaranga litasaidia kuimarisha shughuli za ukuzaji viumbemaji na kuongeza mchango wa Sekta ya uvuvi katika Pato la Taifa. "Bodi mpya inapaswa kusimamia kwa karibu Mpango Mkakati wa Wakala, na kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora za samaki, pamoja na kushirikiana na Taasisi nyingine zikiwemo Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), katika kuanzisha Mpango wa Kitaifa wa kuboresha mbegu za mazao ya viumbe  maji" amesema Mhe. Kamani. Aidha, Mhe. Kamani amewataka wajumbe wa Bodi hiyo kuimarisha mafunzo...

MAFUNZO REJEA YA MAAFISA UGANI YAZINDULIWA NCHINI

Picha
Na. Fausta Njelekela ◾Wizara kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa kununua pikipiki 200. Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaanza kutoa Mafunzo rejea kwa Maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi ambapo mafunzo hayo yenye lengo la kuwafundisha maafisa Ugani masuala mbalimbali ikiwemo kuzingatia ufugaji na uvuvi endelevu, usimamizi endelevu wa rasilimali za mifugo na uvuvi pamoja na sheria na kanuni mbalimbali zinazosimamia sekta za mifugo na uvuvi. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa hafla hiyo iliyofanyika Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma Machi 3, 2026, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele amesema mafunzo hayo ni moja ya hatua na mikakati iliyowekwa na wizara ya kuhakikisha inaimarisha huduma za ugani kwa kutoa mafunzo rejea kwa maafisa ugani ili kujenga uelewa wa pamoja katika masuala mbalimbali ya kitaalamu yanayolenga kuongeza tija katika uzalishaji ili kufikia malengo ya kitaifa na kimataifa yanayolenga kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza kipato kw...

PROF. SHEIKH AWATAKA IUCN KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amelitaka Shirika la Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira (IUCN) kuzingatia vipaumbele vya Wizara katika utekelezaji wa Mradi wa Pamoja Tuhifadhi Bahari Yetu ili kuleta tija katika Sekta ya Uvuvi. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa Kikao cha kupitia Mradi wa Pamoja Tuheshimu Bahari Yetu unaoratibiwa na ICUN na kutekelezwa na Wizara za Kisekta na Taasisi zisizo za kiserikali, leo Machi 2, 2026 Mkoani Morogoro, Prof. Sheikh amewataka IUCN kuzingatia vipaumbele vya Wizara katika utekelezaji wa Mradi huo. "ni vyema ICUN kufuata Miongozo na Taratibu za Wizara katika kutekeleza Mradi kwa kuchangia katika Mkakati wa Mageuzi wa Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbemaji kwa mwaka 2026/2050, na programu zenu zilenge kwenye kufanya Mageuzi katika Sekta ya Uvuvi.” amesema Prof. Sheikh Vilevile, Prof. Sheikh amesema kwa sasa Wizara inataka kufanya Mageuzi kat...

KINGOLWIRA INAFAA KUWA KITUO KIKUBWA CHA UKUZAJI VIUMBEMAJI NCHINI - PROF. SHEIKH

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amesema  Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kinafaa kuwa Kituo kikubwa na cha Kitaifa cha Ukuzaji Viumbemaji nchini kwani kina Miundombinu nyinyi ambaazo zinajengwa na za kisasa. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, alipotembelea Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kwa ajili ya kukagua Miundombinu na Uzalishaji, leo Machi 2, 2026 Mkoani Morogoro, Prof. Sheikh amesema Kituo kinazalisha vifaranga 600,000 kwa mwaka ikiwa kuna Vizimba 6 tu. "kwa hiyo ni vyema kuharakisha kujenga Miundombinu nyingine haraka hili kuweza kuzalisha vifaranga vya Samaki zaidi ili wananchi wape kufuga.” amesema Prof. Sheikh Aidha, Prof. Sheikh amesema Mradi huo wa Ukuzaji Viumbemaji wa Kingolwira unaendelea kuboreshwa zaidi kwa kutengeneza Vizimba vingine na Miundombinu nyingine ambazo zitakuwa zinazalisha vifaranga kwa wingi. Vilevile, Prof. Sheikh amewataka Wata...