TASFAM YATOA MAFUNZO KUONGEZA THAMANI ZAO LA MWANI MKOANI LINDI
Na. Martha Mbena. Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kupitia Mradi Kuendeleza na Kusimamia Uvuvi wa Baharini na Ukuzaji viumbe maji kwa njia endelevu nchini Tanzania (TASFAM) Umeanza kutoa mafunzo ya kilimo cha Mwani, Ufugaji Jongoo Bahari, uanzishwaji wa Vikundi pamoja na Kanuni za Ukuzaji viumbe maji kwa wanufaika wa mradi huo ndani ya Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi. Akizungumza wakati wa kutoa mafunzo hayo yaliyofanyika Machi 26,2026 Mkoani humo Afisa Uvuvi Mkuu Bi. Happy Kapinga amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wakulima wa zao la mwani pamoja wafugaji wa jongoo Bahari. "Leo tumekuja hapa Mkoani Lindi, Kata ya Mchinga kwa ajili ya kutekeleza malengo ya mradi wa TASFAM ambapo takribani wakulima 600 tunatarajia wapate uelewa katika Ukuzaji Viumbe maji kwa mkoa wa Lindi", Amesema Bi. Kapinga. Aidha, Kapinga ameongeza kuwa mradi huo unatarajiwa kutekelezwa ndani ya miaka mitano, hivyo utasaidia katika ukuaji wa uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na...