DKT. MADELE AVUTIWA NA JUHUDI ZA SEKTA BINAFSI UTEKELEZAJI DIRA 2025-2050
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amevutiwa na jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na sekta binafsi kwenye kutafsiri kwa vitendo Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050. Hayo yamejiri wakati wa ziara yake ya kutembelea Kiwanda cha kusindika maziwa cha Kilimanjaro na Shamba la Mwekezaji binafsi la kuzalisha malisho na maziwa la NURU mkoani Arusha Julai 18,2026 ambapo amewapongeza wadau hao kwa kuwa na maono yanayounga mkono juhudi za Serikali za kuendeleza sekta ya Mifugo. Akiwa kwenye kiwanda cha Kilimanjaro Dkt. Madele amesema kuwa kiwanda hicho mbali na kuwa fursa ya kuwahamasisha wafugaji kuzalisha maziwa kwa wingi kimetekeleza kwa vitendo sehemu ya vipengele vilivyopo kwenye mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwakusanya wafugaji kwenye vikundi na kujenga vituo vya kukusanyia maziwa. “Sisi kama Serikali kupitia mradi huo tumeanza kuongeza nguvu kwenye matumizi ya teknolojia ya uhimilishaji ili kuhakikisha wafu...