Machapisho

MAJOSHO 754 YAJENGWA KUOGESHEA MIFUGO NCHINI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema itaendelea kuratibu ujenzi, ukarabati na uendelezaji wa miundombinu muhimu ya mifugo nchini, ikiwemo majosho katika Wilaya ya Bunda, kwa lengo la kuimarisha huduma za mifugo na kudhibiti magonjwa yanayoathiri mifugo kadri ya upatikanaji wa fedha. Kauli hiyo imetolewa leo June 2,2026 bungeni na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt Bashiru Ally Kakurwa wakati akijibu swali la Mbunge wa Bunda, Boniphace Getere,(CCM)  aliyehoji ni lini Serikali itajenga majosho katika maeneo ya wafugaji ya Mahanga, Tingirime, Nyabuvumbu, Nyabuzume, Kaloreli na Tirig’ati. Akijibu Balozi Dkt. Bashiru alisema Serikali inatambua umuhimu wa majosho katika kudhibiti magonjwa yanayoenezwa na kupe na mbung’o, na kwamba tangu mwaka wa fedha 2021/2022 imeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa majosho ambapo hadi sasa jumla ya majosho 754 yamejengwa nchini kote. Alisema  kuwa katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilitumia shilingi milio...

MAZIWA NI UCHUMI, TUCHANGAMKIE FURSA - RC JAMES

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Kheri James amewataka Watanzania kuchangamkia fursa za kiuchumi zitokanazo na maziwa. Mhe. James amebainisha hayo Juni 01,2026 kwenye kongamano la wadau wa tasnia hiyo wakati akifunga Maadhimisho ya 29 ya wiki ya maziwa yaliyokuwa yakifanyika mkoani Iringa. “Siku hii ina umuhimu sana kwa sababu kwanza huongeza uelewa kuhusu faida za maziwa kwa watoto, vijana, wazazi na wazee, pili huhamasisha matumizi ya lishe bora kwa jamii, tatu huunga mkono wafugaji na sekta ya mifugo kwa kuongeza matumizi ya maziwa na bidhaa zake na kukuza uchumi kupitia uzalishaji, usindikaji, na ajira zinazotokana na sekta ya maziwa nchini” Amesema Mhe. James. Aidha Mhe. James amewataka wananchi kutoishia kusherehekea pekee bali watumie siku hiyo kujenga utamaduni wa kunywa maziwa yaliyosindikwa angalau kwa wastani wa glasi moja kwa siku kwa ustawi wa afya zao na maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla. Kwa upande wake Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini Prof. George Msalya amesema kuwa m...

JAMII YATAKIWA KUONGEZA JUHUDI MAPAMBANO DHIDI YA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI.

Picha
Wananchi wametakiwa kuongeza juhudi katika kupambana na athari zinazotokana na mabadiliko ya hali ya nchi yanayoikumba nchi na dunia kwa ujumla. Wito huo umetolewa  leo Juni 1, 2026 na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Kwagilwa Reuben (MB) wakati akifungua maadhimisho ya wiki ya mazingira katika Viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma. Mhe. Kwagilwa amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha mazingira yanatunzwa ili kuwezesha nchi kutimiza mipango ya Dira 2050 kwani athari za mabadiliko ya tabia ya nchi yana athari hasi kwenye uchumi wananchi na dunia. “Mazingira ni Uchumi pia mazingira ni afya, tunatakiwa kuyatunza  mazingira yetu ili malengo yetu ya Dira ya Taifa 2050 yanatimia.  Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi tutaendelea kutekeleza wajibu wetu  katika kulinda mazingira.” Amesisitiza Mhe.Kwagilwa. Kwa upande wake mratibu wa maonesho hayo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI), Bw. M...

TANZANIA KUWA NA MKAKATI MAALUM WA MAWASILIANO WAKATI WA MLIPUKO WA MAGONJWA YA MIFUGO

Picha
Na. Chiku Makwai – ARUSHA Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH), kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, limeanza mchakato wa kuandaa Rasimu ya Mkakati wa Kitaifa wa Mawasiliano Wakati wa Dharura kwa Huduma za Mifugo Tanzania, hatua inayolenga kuimarisha uwezo wa nchi katika kuzuia, kudhibiti na kukabiliana na milipuko ya magonjwa ya mifugo. Warsha ya kuandaa rasimu hiyo imefunguliwa leo, Juni 1, 2026, katika Ukumbi wa Masailand Hall jijini Arusha na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo, Dkt. Benezeth Lutege, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Agness K. Meena. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha hiyo, Dkt. Lutege amesema mawasiliano yenye ufanisi ni nyenzo muhimu katika kudhibiti na kukabili milipuko ya magonjwa ya mifugo kwa kuwa huwezesha utoaji wa taarifa sahihi kwa wakati kwa wadau wote wanaohusika. Amesema Serikali inaendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari na mwitikio wa haraka ili kuhakikisha magonjwa ya mifugo yanagunduliwa na kudhibitiwa mapem...

MRADI WA BBT KUTENGENEZA AJIRA 6000 KWA WANAWAKE NA VIJANA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) ya Unenepeshaji wa Mbuzi na Kilimo cha Malisho, ambao unatekelezwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, umepanga kuwawezesha wanawake na vijana 6000 ndani ya muda wake wa utekelezaji wa Miaka Mitano wa Mradi huo, ambao ukiwa na lengo la kuongeza ushiriki wa wanawake na vijana katika ujasiliamali wa Biashara ya Mifugo. Akizungumza leo Juni 1, 2026 Mkoani Morogoro, katika Warsha ya Upitiaji, Uhakiki wa Uwasilishaji wa Ripoti ya awali ya Jinsia na Ujumuishaji wa Kijamii katika Programu hiyo ya BBT, Meneja Mradi wa BBT Upande wa Jinsia na Ujumuishaji wa Kijamii, Bi. Neema Urassa amesema Mradi huo una lengo la kuwawezesha Wanawake na Vijana kupitia shughuli za unenepeshaji wa Mbuzi na Kondoo kibiashara pamoja na Kilimo cha Malisho ya Mifugo. "Mradi huu unawalenga zaidi Wanawake na vijana, ambao kupitia Mradi huu watapata kujifunza vitu mbalimbali kwa vitendo katika mnyororo mzima wa thamani wa...

DKT. BASHIRU AZINDUA MAADHIMISHO YA KITAIFA WIKI YA MAZIWA 2026

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa leo Mei 31,2026 amezindua Maadhimisho ya 29 ya kitaifa ya wiki ya Maziwa ambayo mwaka huu yanafanyika kwenye viwanja vya Mwembetogwa mkoani Iringa. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Balozi Dkt. Bashiru amesema kuwa Maadhimisho hayo yamekuwa na lengo la kuhamasisha uwekezaji, urasimishaji wa tasnia ya maziwa,matumizi ya maziwa bora na salama ili kulinda afya ya mlaji, kukuza biashara rasmi ya maziwa na kuhakikisha tasnia hiyo inaongeza mchango wake kwenye maendeleo ya kaya za wafugaji na uchumi wa Taifa kwa ujumla. “Sisi kama wizara kwa dhati kabisa kupitia mradi wetu wa mageuzi ya tasnia ya maziwa na mabadililo ya tabia nchi tutahakikisha mfugaji anajikwamua kiuchumi kwa sababu mradi huu umekusudiwa kununua na kufuga ng’ombe bora wa maziwa, kufanya ujenzi wa miundombinu itakayowezesha ufugaji bora, kuongeza uzalishaji na kuboresha mnyororo wa thamani wa maziwa, ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya kukusanyia maziwa, kupa...

DKT. BASHIRU AKOSHWA UWEKEZAJI SEKTA YA MAZIWA IRINGA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na kamati  ya kudumu ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo  wamekoshwa na kiwango cha uwekezaji uliofanywa kwenye sekta ya Maziwa mkoani Iringa. Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara ya kutembelea na kukagua shughuli za ufugaji na uzalishaji maziwa kwenye kiwanda cha ASAS, Balozi Dkt. Bashiru amewataka wafugaji kuheshimu misingi ya sayansi na taaluma ili wawe na ufugaji wenye ufanisi na wa kibiashara. “Tumeona wataalam ambao amewaajiri ASAS wanaelewa kazi yao na katika hili nchi imefundisha sana wataalam hivyo ni lazima tuheshimu utaalam wao lakini pia tuwape nafasi na nyenzo za kuonesha utaalam wao” Amesisitiza Balozi Dkt. Bashiru. Aidha Balozi Dkt. Bashiru amempongeza mwekezaji huyo kwa kuweka miundombinu bora ya uvunaji wa maji ya mvua na matumizi bora ya ardhi kwa upande wa uzalishaji wa malisho ya mifugo ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ambayo yamekuwa yakitolewa na Serikali kwa wafugaji ili kuwa na uhak...