Machapisho

SERIKALI KUTOA PIKIPIKI 200 KUIMARISHA HUDUMA ZA UGANI

Picha
Na. Stanley Brayton Wizara ya Mifugo na Uvuvi imezamiria kuimarisha huduma za Ugani kwa kununua pikipiki 200 ambazo zitasaidia kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi katika kutekeleza majukumu ya kuwahudumia wananchi ili kuongeza uzalishaji katika sekta hizo. Akizungumza Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Pwani, Ndg. Shangwe Twamala, wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo rejea kwa maafisa hao kutoka Kanda ya Kati Mashariki leo Machi 11, 2026, mkoani Pwani, Ndg. Twamala amesema pikipiki hizo 200 zitasambazwa kwa maafisa ugani wote nchini. "Wote tunashuhudia utekelezaji huo na hatua za Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwa miongoni mwenu wapo wataalam wa ugani ambao wameshapatiwa vifaa pamoja na mafunzo mbalimbali yakiwemo haya mafunzo ya leo ambayo nimepata nafasi ya kuyafungua kwa Kanda ya Kati Mashariki.” Amesema Ndg. Twamala Aidha, Ndg. Twamala amebainisha kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza majukumu mb...

BODI YA MAZIWA YAWAJENGEA UWEZO WATAALAMU WA MIFUGO NA LISHE

Picha
 Bodi ya Maziwa nchini imefanya kikao na wadau wa tasnia ya maziwa nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo madaktari wa mifugo, maafisa lishe kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe pamoja na wataalamu kutoka Bodi ya Maziwa Tanzania. Akizungumza Machi 11,2026 wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Msajili wa Bodi hiyo Prof. George Msalya, amesema lengo la Serikali ni kuendelea kuimarisha sekta ya maziwa ili iweze kuchangia zaidi katika kuboresha lishe ya wananchi, kuongeza ajira pamoja na kukuza uchumi wa nchi. Amesema kupitia mafunzo hayo, wataalamu hao wanawezeshwa kupata ujuzi na maarifa yatakayowasaidia kufanya kazi kwa ufanisi zaidi katika maeneo yao, ikiwa ni pamoja na kuongeza tija katika uzalishaji wa maziwa na kuwasaidia wafugaji kupata elimu sahihi ya ufugaji bora. Aidha, Prof. Msalya amesema mafunzo hayo pia yanatoa fursa kwa wataalamu hao kujifunza kuhusu hali ya sasa ya taasisi ya maziwa nchini, mafanikio yaliyopatikana kupitia Bodi ya Maziwa Tanzania pamoja na kujadili chan...

KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA TAFICO, CHANJO YA MIFUGO

Picha
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kutekeleza miradi ya maendeleo inayolenga kuongeza uzalishaji na mchango katika pato la taifa. Mwenyeketi wa Kamati hiyo Mhe. Deoudatus Mwanyika ametoa pongezi hizo leo Machi 10, 2026 Bungeni Dodoma kwa niaba ya wajumbe baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) na Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa mifugo ilizinduliwa Juni 2025. “Kama kamati tunaipongeza wizara kwa kuelimisha wafugaji na jamii kwa ujumla kuhusu chanjo, zoezi hili lilikuwa na mvutano sana kutokana na ukosefu wa elimu lakini sisi kamati tulisema ni lazima chanjo ifanyike. lakini pia, tunapongeza kwa miradi ya meli za TAFICO kwa ajili ya uvuvi wa Bahari Kuu, kamati hii imelipigania sana suala hili” alisema Mhe. Mwanyika. Awali akitoa taarifa ya miradi inayotekelezwa na TAFICO Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo CPA Shaibu Matessa amesema jumla ya...

SERIKALI YAONGEZA NGUVU KWA MAAFISA UGANI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuimarisha uwezo wa maafisa ugani wa sekta ya mifugo kwa kuwapatia mafunzo rejea yanayolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wafugaji na kuongeza uzalishaji wa mifugo nchini. Mafunzo hayo yaliyodumu kwa siku mbili  Kwa upande wa maafisa ugani wa Mifugo yamehitimishwa leo Machi 10, 2026 Katika ukumbi wa IFM  Wilayani Chato mkoani Geita kwa kuwahusisha maafisa ugani kutoka Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi. Akizungumza wakati wa hitimisho la mafunzo hayo, Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Afisa Mifugo Mkuu, Bi. Mary Yongolo amewashukuru maafisa ugani kwa nidhamu waliyoionesha katika kipindi chote cha mafunzo hayo. "Hakikisheni maarifa mliyoyapata yawe chachu ya kuboresha utendaji kazi wenu pindi mrejeapo vituoni ili kuleta tija katika sekta ya mifugo." Amesema Bi. Yongolo Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Dkt. Sostenes Nkombe, amewapongeza washiriki ...

MKANDARASI WA GHALA LA UBARIDI TAFICO ATAKIWA KUKAMILISHA KAZI KWA WAKATI

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena, ameiagiza kampuni ya Kabirirti Engineering Limited inayotekeleza mradi wa ukarabati wa ghala la ubaridi (Cold Storage) la Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa. Prof. Sheikh ametoa agizo hilo leo Machi 9, 2026 wakati alipotembelea Makao Makuu ya TAFICO yaliyopo Ras Mkwavi-Kigamboni jijini Dar es Salaam, kwa lengo la kukagua miundombinu ya uhifadhi wa samaki na mazao ya uvuvi. Amesema kukamilika kwa mradi huo kwa wakati ni muhimu katika kuimarisha shughuli za uvuvi na kuongeza uwezo wa kuhifadhi mazao ya baharini, jambo litakalosaidia kuongeza thamani ya bidhaa za uvuvi pamoja na kuchochea uchumi wa sekta hiyo. Kwa upande wake, mkandarasi wa mradi huo kutoka Kabirirti Engineering Limited ameeleza kuwa kazi ya ukarabati inaendelea vizuri na kwamba watahakikish...

MAAFISA UGANI WAHIMIZWA KUBADILISHANA UZOEFU ILI KUBORESHA HUDUMA KWA WANANCHI

Picha
Wataalamu wa ugani wa sekta za mifugo na uvuvi kutoka Kanda ya Ziwa wameanza mafunzo rejea katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita leo Machi 9, 2026, yaliyoandaliwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa wafugaji na wavuvi. Akifungua mafunzo hayo, mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe Lois Bura amewahimiza maafisa ugani kubadilishana uzoefu na kutumia ujuzi wao wa kitaalamu ili kuboresha huduma wanazozitoa kwa wananchi, hususan wafugaji na wavuvi  wanaotegemea ushauri wao katika shughuli za uzalishaji. "Maafisa ugani ni kiungo muhimu katika kufikisha sera, sheria na teknolojia bora za ufugaji na uvuvi ili kuongeza tija katika uzalishaji na kuendelea kuimarisha usalama wa chakula na kipato kwa wananchi." amesema Mhe. Bura Aidha, Mhe. Bura amesema kuwa huduma za ugani zina mchango mkubwa katika kuleta mageuzi  kwa kusaidia kupeleka mbinu na teknolojia mpya kwa wafugaji pamoja na kukabiliana na changamoto mbalim...

MAAFISA UGANI MIFUGO NA UVUVI TATUENI CHANGAMOTO ZA WAFUGAJI NA WAVUVI KITAALUMA - BI. MAYEMBA

Picha
Na. Stanley Brayton  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Makambako, ambaye ni Mkuu wa Idara ya usafi na uthibiti wa taka ngumu, Bi. Appia Mayemba amewataka Maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi kutatua changamoto mbalimbali kitaaluma ambazo zinawakumba wafugaji na wavuvi ili kuongeza tija katika Sekta hizo za Uzalishaji. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Makambako wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Mafunzo Rejea kwa Nyanda za Juu Kusini kwa Maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi Nchini, leo Machi 9, 2026, Wilayani Makambako Mkoani Njombe, Bi. Mayemba amesema Maafisa Ugani wanapopata Mafunzo hayo mbalimbali ya Ugani na baada ya kutoka kwenye Mafunzo ni vyema kwenda kuwahudumia wafugaji na wavuvi ili kuweza kuzitatua changamoto zao kwa umakini na utulivu. "Kama kuna jambo lolote ni vyema kushirikisha uongozi wa juu ikiwemo Wakurugenzi wa Idara mbalimbali ili kutatua changamoto za wafugaji na wavuvi kwa lengo la kupunguza masononeko kwa Serikali pa...