Machapisho

TALIRI YAPONGEZWA KWA KUWEKEZA KWENYE UZALISHAJI WA MALISHO YA MIFUGO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa juhudi zake za kuwekeza katika uzalishaji wa malisho na mbegu bora za malisho ya mifugo, hatua aliyosema ni muhimu katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa malisho nchini. Dkt. Madele ametoa pongezi hizo leo Mei 22, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kituo cha West Kilimanjaro kwa lengo la kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo. Akizungumza katika ziara hiyo, Dkt. Madele amesema sekta ya mifugo inaendelea kukabiliwa na changamoto ya upungufu wa malisho kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, hivyo uwekezaji unaofanywa na TALIRI ni hatua muhimu ya kuimarisha ufugaji wenye tija na kuongeza uzalishaji. Aidha, Dkt. Madele amewataka wataalamu wa TALIRI kuendelea kutoa elimu kwa wafugaji kuhusu mbinu bora za ufugaji wa kisasa i...

BWAWA LA LITA MILIONI 1.2 LAJENGWA TALIRI KUIMARISHA UZALISHAJI WA MALISHO YA MIFUGO

Picha
Katika jitihada za kuimarisha uzalishaji wa malisho ya mifugo na kuongeza uwezo wa wafugaji kukabiliana na athari za ukame, Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kanda ya Kaskazini imefanikiwa kujenga bwawa lenye uwezo wa kuhifadhi lita milioni 1.2 za maji kwa ajili ya shughuli za umwagiliaji katika eneo la shamba darasa la uzalishaji wa malisho ya mifugo. Mradi huo unatekelezwa kupitia programu ya kuwajengea uwezo wafugaji na kuimarisha mifumo ya ufugaji kwa familia za kifugaji sambamba na kuchangia uendelevu wa usalama wa chakula nchini. Bwawa hilo lina uwezo wa kuhakikisha upatikanaji wa maji ya uhakika kwa shughuli za umwagiliaji katika shamba darasa lenye ukubwa wa ekari moja kwa kipindi cha hadi miezi mitatu bila kujazwa tena. Hatua inatarajiwa kuongeza ufanisi wa uzalishaji wa malisho hata katika vipindi vya ukame vinavyosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi. Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta y...

DKT. BASHIRU ATAKA MKAKATI WA TASNIA YA KUKU UZINDULIWE NANE NANE 2026

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameiagiza Ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo pamoja na Watendaji wake kuhakikisha inakamilisha uandaaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Kuendeleza Tasnia ya Kuku nchini na kuuzindua mkakati huo wakati wa Maonesho ya Nane Nane ya Mwaka huu 2026. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo wakati  akifungua rasmi Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Wadau kuhusu Kilimo cha Mikataba, Uwezeshaji wa Fedha kwa Wakulima na Maendeleo ya Vyama vya Wakulima uliofanyika jijini Dodoma leo Mei 22, 2026 ambapo ameeleza kuwa kukamilishwa na kuzinduliwa kwa mkakati huo kutasaidia kuirasimisha tasnia ya kuku ambayo ina mchango mkubwa kwa uchumi na usalama. "Tatizo Kubwa tulilonalo pamoja na sekta hii kuwa kubwa, ni sekta  ambayo haijarasimishwa wala kupewa hadhi inayostahili, ndio maana ndani ya wizara tunaandaa Mkakati wa Kitaifa wa Maendeleo ya sekta ya Kuku, Napenda kuelekeza Ofisi ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wataalam wenzake nahitaji...

DKT. BASHIRU AAGIZA KUFANYIKA TATHMINI MIUNDOMBINU YA KUFUGIA SAMAKI - NANE NANE

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amemwagiza Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kufanya tathmini ya miundombinu ya kufugia samaki kutoka kwa Mwekezaji Hawa Fish Farm ili eneo hilo litumike kwa ajili ya Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT Uvuvi). Balozi Dkt. Bashiru ametoa agizo hilo leo Mei 21, 2026 wakati alipotembelea na kukagua Mabwawa ya Kufugia Samaki ya  Mwekezaji Hawa Fish Farm yaliyopo Viwanja vya Nane Nane vya John Malecela jijini Dodoma, ambapo mwekezaji huyo amesema anaondoka na kwenda kuwekeza sehemu nyingine. "Hatuwezi kuendesha shughuli za kiserikali zinazohusu watu bila kuwa karibu nao na kurahisisha mawasiliano, Nataka maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Viumbe maji kwa nini tumechelewa kumpa majibu mwekezaji huyu kutokana na mapendekezo yake?, Pia ifanyike tathmini ya miundombinu  hii kama inafaa kwa shughuli gani? amesema Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, Balozi Dkt. Bashiru ameongeza kwa kuitaka idara hiyo kuja na wazo mbadala la...

DKT. MADELE AAGIZA UJENZI WA SOKO LA SAMAKI KIPUMBWI, PANGANI KUKAMILIKA KWA VIWANGO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele, amemtaka mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Ujenzi wa Soko la Samaki Kipumbwi kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa huku ukizingatia viwango vya ubora vinavyokidhi mahitaji ya soko la kisasa. Dkt. Madele ametoa maelekezo hayo leo Mei 21, 2026 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo unaotekelezwa katika eneo la Kipumbwi, Wilaya ya Pangani mkoani Tanga. Mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo Juni 30, 2026. Amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika miundombinu ya kisasa ya sekta ya uvuvi kwa lengo la kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi, kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza ajira pamoja na kuinua uchumi wa wananchi wanaotegemea shughuli za uvuvi na biashara ya samaki. Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji, mradi huo umefikia asilimia 52 ya utekelezaji ukiwa na gharama ya jumla ya shilingi bilioni 1.34 hadi kukamilika kwake ukihusisha uj...

DKT. MADELE ASISITIZA TAASISI ZA MIFUGO KUWAPA WAFUGAJI SULUHISHO LA KISASA NA LENYE TIJA

Picha
“Tunayo kazi kubwa ya kuhakikisha wafugaji wanapata majawabu ya changamoto zinazowakabili katika sekta ya mifugo. Matarajio yao makubwa ni kuona wanapata mbari bora za mifugo, mbegu bora za malisho pamoja na huduma bora za afya ya mifugo.” Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele, wakati wa kikao chake na watumishi wa taasisi zilizo chini ya wizara hiyo kilichofanyika leo Mei 20, 2026 katika ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) jijini Tanga. Taasisi zilizoshiriki katika kikao hicho ni pamoja na TALIRI, Wakala wa Mafunzo ya Mifugo (LITA) pamoja na Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA). Katika hotuba yake, Dkt. Madele amesema sekta ya mifugo ina nafasi kubwa katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa, hivyo ni muhimu kwa taasisi zote za wizara kufanya kazi kwa weledi, ubunifu na mshikamano ili kuhakikisha wafugaji wanapata teknolojia sahihi za ufugaji kwa wakati. Amesema upati...

TALIRI YATAKIWA KUFANYA TAFITI ZENYE TIJA KWA MAENDELEO YA SEKTA YA MIFUGO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele ameielekeza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kuongeza nguvu katika kufanya tafiti zinazolenga kutatua changamoto halisi za wafugaji ili kuchochea maendeleo ya sekta ya mifugo na kuongeza tija nchini. Dkt. Madele ametoa maelekezo hayo leo Mei 20, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi katika Kituo cha TALIRI Kanda ya Mashariki, ikiwa ni sehemu ya ukaguzi wa utekelezaji wa majukumu ya taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Katika ziara hiyo, Dkt. Madele amesema tafiti zinazofanywa na TALIRI zinapaswa kuendana na mahitaji ya sasa ya wafugaji pamoja na mabadiliko ya sekta ya mifugo, huku akisisitiza umuhimu wa kutumia tafiti hizo kama nyenzo ya kuongeza uzalishaji, kuboresha afya za mifugo na kuinua uchumi wa wafugaji. Aidha, ameiagiza taasisi hiyo kuongeza kasi ya usambazaji wa teknolojia bora za mifugo zilizoibuliwa na watafiti wake, ikiwemo uendelezaji wa mbari bora...