DKT. BASHIRU AHIMIZA KUDHIBITI UVAMIZI MASHAMBA YA MIFUGO
◾Awataka Watendaji wa Wizara kuendelea kufanya kazi Kisayansi Na. Stanley Brayton, WMUV Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewahimiza Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo kudhibiti uvamizi wa mashamba ya Mifugo na maeneo ya Uzalishaji wa Mifugo na Uvuvi ili maeneo hayo yaweze kutimiza malengo yaliyokusudiwa ya kuwa maeneo ya kuzalisha mazao ya Mifugo na Uvuvi. Akizungumza leo Mei 9, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo, Dkt. Bashiru amesema kuwa mashamba ya Mifugo yamekuwa na changamoto kubwa kiasi cha maeneo hayo kumegwa na kufanyiwa matumizi mengine bila kufuata utaratibu wa kisheria. "siridhishwi na uvamizi wa mashamba ya Mifugo, na umegaji wa maeneo hayo ambayo yalikuwa yamepangwa kwa ajili ya shughuli za Uzalishaji Mifugo" amesema Dkt. Bashiru Aidha, Dkt. Bashiru amewataka Watendaji Wakuu wa Wizara kuhakikisha Sekta za Mifugo na Uvuvi zinaendeshwa Kisayansi ili kuweza kuboresha Sekta hizo ambazo ni miongoni ...