Machapisho

KAMANI AELEZA MKAKATI WA SERIKALI KUONGEZA MAENEO YA WAFUGAJI NNCHINI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Damas Kamani amesema Serikali inaendelea kutenga, kupima na kumilikisha kwa wafugaji maeneo ya shughuli za ufugaji kutoka hekta Milioni 3.46 hadi hekta Milioni 6 pamoja na kuyaboresha maeneo hayo kwa kuyapatia huduma muhimu zikiwamo maji, majosho, malisho na huduma za ugani. Hatua hiyo ya kutenga maeneo ya shughuli za ufugaji ni utekelezaji wa maelekezo ya Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Novemba 14, 2025 pamoja na Maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2025. Mhe. Kamani amesema hayo leo Aprili 21, 2026 vacati akijibu Swali la Mbunge wa Kalambo Mkoani Rukwa Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni aliyehoji kuwa serikali ina mango gani wa kuongeza ardhi ya kilimo kwa wananchi wa kata ya Mkoe na Mbuluma kutoka katika eneo la NARCO. “Mheshimiwa Spika, Ranchi ya Kalambo ni moja kati ya ranchi 15 zinazomilikiwa na Kam...

SHILINGI BIL. 9.5 ZATENGWA KUTOA MIKOPO YA BOTI ZA KISASA ZA UVUVI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi Katika bajeti ya mwaka 2025/2026, imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 9.5 kwa ajili ya kutoa mikopo ya boti za kisasa za uvuvi 100, boti saidizi 76, na vifaa vyake kwa masharti nafuu kwa wavuvi na wakuzaji viumbemaji. Hayo, yameelezwa leo Aprili 20, 2026 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Kamani wakati wa Kipindi cha Maswali na Majibu  Bungeni Jijini Dodoma, alipokuwa ajibu swali la Mbunge wa Nyasa Mhe. John John Nchimbi lililohoji  ni lini Serikali itatoa mikopo nafuu ya Boti za Uvuvi za Fiber kwa Wavuvi wa Wilaya ya Nyasa? “Mikopo hiyo itatolewa kwa wananchi wa mwambao wa Bahari ya Hindi, Maziwa Makuu na madogo, mabwawa na mito ambapo takribani wananchi 2,100 watanufaika moja kwa moja ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi, ajira na kipato” alisema Mhe. Kamani. Aliongeza kuwa Mikopo hiyo inalenga kutoa vifaa na pembejeo muhimu za ufugaji samaki kwa vizimba, zana za uvuvi, ufugaji wa kuku, ufugaji wa nguruwe, ufugaji...

RAIS SAMIA ATAZINDUA MELI YA UVUVI WA BAHARI KUU APRILI 25, 2026 - DKT BASHIRU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani anatarajiwa kuzindua Meli ya Kwanza ya Uvuvi wa Bahari Kuu, ambapo uzinduzi wake utafanyika Makao Makuu ya  Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) Kigamboni Jijini Dar es Salaam. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo Aprili 17, 2026, wakati wa ziara ya  Kamati ya Uchumi na Uwekezaji ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kutembelea na kukagua ujenzi wa bahari ya uvuvi Kilwa Masoko Mkoani Lind na kuieleza kamati hiyo kuwa  bandari ya uvuvi Kilwa masoko iliyogharimu shilingi bilioni 280 baada ya kukamilika itafanyiwa majaribio kabla ya kukabidhiwa kwa serikali. “ Mradi huu kwa sawa  tuko asilimia 97, asilimia tatu zilizobaki ni kwa sababu kuna mitambo mingine imeagizwa ili ifungwe halafu tufanye majaribio kabla ya kukabidhiwa, wakati wowote ndani ya mwezi wa nne na watano mkandarasi anaweza kutukabidhi” alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. ...

PROF. SHEIKH AAGIZA UFUATILIAJI WA UBORA WA VIFARANGA VYA SAMAKI

Picha
Na Chiku Makwai, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, ameielekeza Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kuimarisha ufuatiliaji wa ubora na idadi ya vifaranga vya samaki vinavyozalishwa na kusambazwa kwa wanufaika kwenye shamba la Katabe, mkoani Kigoma. Ametoa maelekezo hayo leo Aprili 15, 2026, wakati wa ziara yake ya kutembelea na kusikiliza changamoto za wanufaika wa mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika eneo hilo. Prof. Sheikh amesema Serikali ina mpango wa kufanya utafiti wa kitaalamu ili kupata vifaranga bora vya samaki nchini kote kwa kutumia teknolojia ya kisasa, hatua itakayochangia samaki kukua kwa haraka na kuzaliana kwa wingi zaidi kulingana na mabadiliko ya mazingira. “Ubora wa vifaranga ni msingi muhimu wa kuongeza uzalishaji  katika ufugaji wa samaki kwa  njia ya vizimba, kukuza kipato cha wafugaji, pamoja na kuhakikisha mafanikio ya miradi ya maendeleo katika sekta ya uvuvi” amesema Prof. Sheikh  Kwa upa...

BI. MEENA AHIMIZA USHIRIKIANO KUINUA SEKTA YA MIFUGO

Picha
 Na, Fausta Njelekela  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena amekutana na Watendaji wakuu wa Taasisi na Wataalam wa Sekta ya Mifugo kwa lengo la kujadili kwa pamoja jinsi ya kuongeza ushirikiano baina ya viongozi na Wataalamu wa Sekta hiyo ili kubaini na kutatua changamoto zinazowakabili wataalam hao katika utendaji kazi ili kuleta tija katika Sekta hiyo. Akizungumza wakati wa Kikao hicho cha majadiliano na Wataalamu wa Sekta hiyo, yaliofanyika leo Aprili 15, 2026 Katika Ukumbi wa Ofisi ya Wizara Jijini Dodoma, Bi. Meena amesema Ushirikiano Katika Sekta ya Mifugo utaleta mbinu bora za kutatua changamoto zinazoikumba Sekta ya mifugo Kwa kutumia wataalamu walioko kwenye maeneo ya wafugaji. "Ushirikiano baina ya viongozi na Wataalamu wa Sekta ya Mifugo utasaidia kutambua changamoto zilizopo na kuzitatua, Ili kuongeza thamani ya mazao ya mifugo." amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena, ameweka msisitizo kwa Watendaji hao kujikita katika kuongeza ushirikiano ili kuta...

MIFUMO YA TAARIFA ZA UVUVI NA UFUATILIAJI NA TATHIMINI KUIMARISHWA

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya kaa Kikao kazi ili kuimarisha mipango ya mifumo ya taarifa za uvuvi, ufuatiliaji na tathmini kupitia Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Bahari Tanzania (TASFAM), kikao kinachofanyika Mjini Morogoro, na kinaendelea leo ili kubaini mapungufu na kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha mifumo ya taarifa na takwimu. Kikao hicho kimefunguliwa rasmi jana (14.04.2026) na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena, ambaye amebainisha juhudi mbalimbali zinazotekelezwa chini ya idara na taasisi zitasaidia kuepusha urudiaji wa kazi, kuongeza ufanisi na kuhakikisha matumizi bora ya rasilimali fedha, watu na muda. 

PROF. SHEIKH AELEKEZA UZALISHAJI WA VIFARANGA KUANZIA 200,000 KILA MWEZI KUFIKIA JUNI 2026

Picha
Na. Chiku Makwai, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, amezitaka taasisi za Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kuimarisha ushirikiano ili kufikia uzalishaji wa vifaranga vya samaki kuanzia 200,000 hadi 300,000 kwa mwezi ifikapo Juni 2026. Maelekezo hayo aliyatoa Aprili 14, 2026, wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watumishi wa Wizara pamoja na taasisi hizo, kilichofanyika katika ofisi za TAFIRI mkoani Kigoma. Prof. Sheikh alisisitiza kuwa lengo la uzalishaji huo ni kurahisisha upatikanaji wa vifaranga bora kwa vijana wanaonufaika na mikopo ya vizimba, pamoja na wananchi wengine wanaojihusisha na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika Ziwa Tanganyika.