Machapisho

DKT. BASHIRU AKAGUA NA KUZINDUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MARA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekagua na kuzindua miradi ya mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara na kueleza kuwa serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika kutenga fedha kwa wakati katika ujenzi na uboreshaji miundombinu ya barabara, umeme na maji ili miradi hiyo ikamalishwe kwa wakati. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo Agosti 11, 2026  wakati wa ziara yake maalum  ya siku nne inayolenga kutembelea, kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara. Katika ziara hiyo Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezindua Daraja la Majengo mapya - Pambazuko lenye thaman ya zaidi ya shilingi milioni 287 ambalo litaunganisha Kata za Bweri na Rwamlimi ndani ya Manispaa ya Musoma. Pia, alitembelea na kukagua ujenzi wa Soko la Nyayo, Kituo cha Mabasi na Barabara za mitaa ndani ya Manispaa ya Musoma, kuweka jiwe la Msingi la Madarasa matano, matundu ya vyoo na Ofisi katika shule ya Msingi Jitirola na kuka...

DKT. BASHIRU: SERIKALI ITASHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUTATUA CHANGAMOTO ZA TASNIA YA KUKU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi  Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema kuna haja ya serikali kushirikiana na sekta binafsi katika kusimamia ubora wa uzalishaji wa vifaranga vya kuku, chanjo pamoja na chakula cha kuku ili tasnia hiyo iweze kuendelea kukua na kuchangia uchumi na usalama wa chakula. Mhe.Balozi Dkt. Bashiru ameeleza hayo Agosti 10, 2026  baada kufika katika shamba la uzalishaji wa kuku la Homeland Farm lililopo Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza ambapo amesema ushirikiano wa serikali na sekta binafsi utajikita zaidi katika udhibiti wa mifumo ya kulinda ubora wa tasnia ya kuku hususan uzalishaji wa vifaranga vyenye ubora, chakula cha kuku na chanjo. "Yale ambayo sekta binafsi inauwezo nayo tushirikiane nayo, yale ambayo serikali tunapaswa kufanya mfano ya udhibiti, mfano haiwezekani mtu yuko sokoni anauza vifaranga viko chini ya ubora" alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, alisema kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo zimepanga kuwa...

MIFUGO NA UVUVI KINARA WIZARA ZA KISEKTA NANENANE 2026

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa pili mfululizo imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwa upande wa Wizara za kisekta kwenye Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane kwa mwaka 2026. Wizara imepata ushindi huo kutokana na kuongoza kwenye vipengele mbalimbali ikiwemo ubunifu wa teknolojia rafiki kwa matumizi ya wadau wote wa sekta za Mifugo na Uvuvi. Aidha miongoni mwa matukio bunifu yaliyoipa Wizara hiyo ushindi huo ni teknolojia ya malisho ya Mifugo aina ya Juncao, kilimo mseto cha Mpunga na samaki, Paredi ya Mifugo iliyokuwa na rekodi ya Ng’ombe mwenye uzito wa kilo 922, Mnada wa Mifugo ambao kwa mwaka huu ulishuhudia ng’ombe wawili wakiuzwa kwa shilingi Mil.22 na Kijiji cha Protini ambacho kilikuwa kivutio cha wengi kutokana na upatikanaji wa mazao yote ya protini itokanayo na samaki na wanyama. Mbali na Ushindi huo wa Wizara, Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo zimefanikiwa kufanya vizuri kwenye Maonesho hayo ambapo Wakala ya Mafunzo ya Uvuvi (FETA) ilishika nafasi ya pil...

KAMANI ASHIRIKI UZINDUZI WA “OKOA MVUVI ZANZIBAR”

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani ameshiriki uzinduzi wa programu ya “Okoa Mvuvi” zanzibar uliofanyika kwenye kiwanja cha Magarawa visiwani Zanzibar Agosti 10,2026. Programu hiyo imezinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdullah.

SERIKALI YAWAHIMIZA WAWEKEZAJI KUTUMIA SAYANSI, TAFITI NA UBORA WA VIFARANGA KATIKA UFUGAJI SAMAKI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuwahamasisha wawekezaji katika sekta ya uvuvi kuzingatia matumizi sahihi ya Sayansi na Tafiti za uvuvi katika kusimamia ubora na uzalishaji wa vifaranga vya samaki ili kuwa na tija katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.. Kauli ya Serikali imetolewa Agosti 10, 2026 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa wakati wa ziara yake mkoani Mwanza kwenye Shamba la Ufugaji Samaki kwa Njia ya Vizimba  la Big Best Company Limited lililopo Ilemela mkoani humo. Alieleza kuwa serikali kupitia wizara anayoisimamia inaendelea kuwahamasisha wawekezaji wakubwa katika sekta ya uvuvi kuchangamkia fursa ya kuwekeza katika viwanda vya chakula cha samaki huku  na akasisitiza juu ya matumizi ya Sayansi, tafiti pamoja na vifaranga vyenye ubora katika ufugaji wa samaki. "Wawekezaji wakubwa wa sekta ya uvuvi changamkieni fursa ya kuwekeza kwenye viwanda vya kuzalisha vyakula vya samaki, sekta hii ya ukuzaji viumbe ma...

KATIBU MKUU MEENA AFUNGUA KIKAO CHA KUJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI KUPITIA SGR

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena, amefungua kikao cha kujadili fursa za uwekezaji wa kiuchumi kupitia Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR), kikao kilichofanyika Agosti 10, 2026, Mtumba jijini Dodoma. Kikao hicho kililenga kujadili na kubainisha fursa mbalimbali za kiuchumi zinazoweza kunufaisha sekta ya mifugo na uvuvi pamoja na kilimo kupitia uwepo na maendeleo ya miundombinu ya SGR, sambamba na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa maendeleo katika kukuza uwekezaji nchini. Kikao hicho kilishirikisha wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na taasisi zake, wataalam kutoka Wizara ya Kilimo, pamoja na wawakilishi kutoka Benki ya Dunia, ambao walishiriki katika kubadilishana uzoefu na kutoa mapendekezo kuhusu namna bora ya kutumia fursa zinazotokana na mradi huo kwa ajili ya kukuza shughuli za kiuchumi.

RAIS SAMIA AAGIZA TAMISEMI, WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUSIMAMIA NAESA

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameziagiza Wizara za Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, Taasisi za umma na sekta binafsi kushirikiana na Wakala ya Taifa ya huduma za ugani (NAESA) ili iweze kufanya kazi na kufikia malengo ya kuanzishwa kwake. Rais Samia ameyasema hayo Agosti 08,2026 wakati  akifunga Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane yaliyofanyika kitaifa Mkoani Dodoma na kwenye kanda nyingine mbalimbali nchini. “Mtakumbuka pia kwamba nilipotembelea maonesho haya mwaka jana nilisisitiza kuimarishwa kwa huduma za ugani nchini ili ziwafikie wakulima wengi na kwa ufanisi zaidi hivyo nafurahi kwamba sasa tumefikia hatua ya kuanzisha kwa wakala wa huduma za ugani za kilimo kwa ufupi NAESA ulioanza kazi mwezi julai mwaka huu na tayari leo nimezindua na kukabidhi magari 48 kwa awamu ya kwanza yakayaoenda kutumiwa kutekeleza majukumu ya wakala hiyo” Amesema Mhe. Rais Samia. Aidha Mhe. Rais Samia ameonesha kuvutiwa na kaul...