Machapisho

DKT. BASHIRU AKUTANA NA GATSBY AFRICA KUJADILI MKAKATI WA UZALISHAJI WA CHAKULA CHA SAMAKI NA KUKU

Picha
Serikali imeendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa maendeleo katika kuongeza tija ya sekta za mifugo na uvuvi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kukuza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuongeza mchango wa sekta hizo katika uchumi wa Taifa. Katika hatua hiyo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, leo Julai 24, 2026 amekutana na timu ya wataalam kutoka Taasisi ya Gatsby Africa katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, na kujadiliana kuhusu uwekezaji katika ukuzaji wa viumbemaji na kuongeza upatikanaji wa chakula cha samaki na kuku. Mazungumzo hayo yalijikita katika namna Serikali na Gatsby Africa zinavyoweza kushirikiana kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi kupitia uwekezaji katika uzalishaji wa malighafi za chakula cha mifugo, matumizi ya teknolojia za kisasa na kuimarisha mnyororo wa thamani wa uzalishaji. Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Bashiru alisema Serikali inaendelea kuweka mazingira weze...

VIFARANGA VYA SAMAKI MILIONI 1.5 VYAPANDIKIZWA ZIWA RWAKAJUNJU - KARAGWE

Picha
◼️Bashungwa atoa pikipiki kwa Afisa Uvuvi wa Kata kuimarisha usimamizi. Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa ameishukuru Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwawezesha wananchi wa Wilaya ya Karagwe kuanza kunufaika na uchumi wa buluu kupitia zoezi la upandikizaji wa vifaranga milioni 1.5 vya samaki aina ya sato katika Ziwa Rwakajunju lililopo wilayani Karagwe. Bashungwa ametoa shukrani hizo leo, tarehe 23 Julai 2026, katika hafla ya uzinduzi wa zoezi la upandikizaji wa vifaranga vya samaki katika Ziwa Rwakajunju, iliyofanyika Kijiji cha Kafunjo, Kata ya Kamagambo, Wilaya ya Karagwe. “Hili jambo halijawahi kutokea tangu nchi ipate uhuru, Tunamshukuru Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa upendo wake. Jambo hili linaenda kuleta mageuzi makubwa na kuongeza kipato cha wananchi wetu,” amesema Bashungwa Bashungwa ameeleza kuwa zoezi la upandikizaji wa vifaranga linaenda kuleta mageuzi makubwa kwa wananchi na ameiomba Serikali kuongeza vifaranga vya samaki kufiki...

DKT. MADELE ATETA NA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO NAMANGA

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amekutana na wafanyabiashara wa Mifugo waliopo eneo la Namanga mkoani Arusha kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya. Dkt. Madele amekutana na wafanyabiashara hao Julai 20,2026 ambapo aliwapa fursa ya kuzungumza kero zinazowakabili na maoni waliyonayo katika kuboresha biashara ya Mifugo kwenye mnada huo ambapo waliiomba Wizara yake kutengeneza mazingira na sera wezeshi ili waweze kuuza mifugo yao kwenye mnada huo badala ya kwenda kuiuza nchini Kenya. “Huu mnada ungeboreshwa na Sera nzuri ikatengenezwa, badala ya sisi kusafirisha mbuzi wetu kwenda Kenya, Wakenya wavutiwe kuja kuchukua mbuzi huku kwetu kwa makubaliano ambayo Serikali yetu na ya kwako watakubaliana ambapo itatusaidia kuokoa hasara ya usafirishaji na tutalipa mapato ya Serikali yetu” Amesema mmoja wa wafanyabiashara hao. Akijibu hoja hizo Dkt. Madele amesema kuwa atakaa na watalaam wake na kuzitafutia ufumbuzi huku akiahidi kukutana tena na wafanyabiashara h...

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AHIMIZA MATUMIZI BORA YA ARDHI KUMALIZA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI RUFIJI

Picha
Na. Daudi Nyingo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Serikali imejipanga kupata suluhisho la kudumu la migogoro kati ya wakulima na wafugaji kwa kuimarisha mipango ya matumizi bora ya ardhi na kuhamasisha ufugaji wa kisasa, ili sekta hizo ziendelee kuchangia usalama wa chakula na ukuaji wa uchumi wa Taifa. Mhe. Dkt. Kakurwa alitoa kauli hiyo Julai 20, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi katika Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani, ambapo alitembelea wafugaji na wakulima wa Kijiji cha Chumbi, kukagua maendeleo ya mpango wa Ranchi Ndogo, Vitalu vya Kilimo vya Kijiji cha Nyamwage na baadaye kufanya mkutano wa hadhara katika Tarafa ya Ikwiriri kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili. “Wakulima na wafugaji ni nguzo muhimu za maendeleo ya Taifa kwani ndiyo wanaohakikisha upatikanaji wa chakula na malighafi za mifugo, hivyo migogoro baina yao inapaswa kutatuliwa kwa njia ya mazungumzo na usimamizi mzuri wa ardhi.”  "Bila wakulima na waf...

NARCO YAZINDUA "BULLDOZER " KUIMARISHA SEKTA YA MIFUGO

Picha
Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imezindua "bulldozer" lenye thamani ya Shilingi milioni 450 katika Ranchi ya NARCO Ruvu, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa Ranchi hiyo, na kuongeza upatikanaji wa malisho, maji pamoja na kukuza uzalishaji wa mifugo nchini. Akizungumza Leo Julai 20, 2026 wakati wa hafla ya uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NARCO, Balozi Dkt. Aziz Ponary Mlima, amesema ununuzi wa "bulldozer" hilo ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya DIRA ya Taifa ya 2050, huku akibainisha kuwa litasaidia kukabiliana na changamoto za malisho na maji ambazo zinawakabili wafugaji nchini. "Bulldozer hili litatumika kuchimba visima vya maji, kuondoa vichaka vinavyozuia ukuaji wa malisho na kutengeneza mipaka ya Ranchi ili kudhibiti uvamizi, na Ranchi hii ya NARCO Ruvu ndiyo ya kwanza kunufaika na matumizi ya mashine hii ambayo pia itasaidia kuboresha mazingira ya uwekezaji ndani ya ranchi za taifa." Amesema Dkt. Mlima Balozi Dkt. Mlima ...

WAZIRI KAKURWA ATOA MWELEKEO WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO

Picha
  Awahimiza kuimarisha umoja wao  Aahidi kuziwasilisha hoja kwa wizara na taasisi husika Daudi Nyingo – DAR ES SALAAM Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema kuwa, Serikali itaendelea kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa mifugo nchini, huku akiahidi kuziwasilisha hoja zinazohusu wizara na taasisi mbalimbali ili zipatiwe ufumbuzi. Waziri Kakurwa alitoa kauli hiyo Julai 19, 2026, wakati wa kikao na wafanyabiashara wa mifugo na mazao yake kilichofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Temeke, Dar es Salaam. Katika kikao hicho, Umoja wa Wafanyabiashara wa Mifugo na Mazao Yake Temeke (UWAMIMATE) uliwasilisha changamoto 15 zinazoathiri biashara ya mifugo na mazao yake. Akizungumza baada ya kupokea hoja hizo, Waziri alisema changamoto zilizowasilishwa hazihusu wafanyabiashara wa Temeke pekee, bali zinaakisi hali halisi ya wafanyabiashara wa mifugo katika maeneo mengi nchini. “Nimep...

DKT. MADELE AVUTIWA NA JUHUDI ZA SEKTA BINAFSI UTEKELEZAJI DIRA 2025-2050

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amevutiwa na jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na sekta binafsi kwenye kutafsiri kwa vitendo Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050. Hayo yamejiri wakati wa ziara yake ya kutembelea Kiwanda cha kusindika maziwa cha Kilimanjaro na Shamba la Mwekezaji binafsi la kuzalisha malisho na maziwa la NURU mkoani Arusha Julai 18,2026 ambapo amewapongeza wadau hao kwa kuwa na maono yanayounga mkono juhudi za Serikali za kuendeleza sekta ya Mifugo. Akiwa kwenye kiwanda cha Kilimanjaro Dkt. Madele amesema kuwa kiwanda hicho mbali na kuwa fursa ya kuwahamasisha wafugaji kuzalisha maziwa kwa wingi kimetekeleza kwa vitendo sehemu ya vipengele vilivyopo kwenye mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwakusanya wafugaji kwenye vikundi na kujenga vituo vya kukusanyia maziwa. “Sisi kama Serikali kupitia mradi huo tumeanza  kuongeza nguvu kwenye matumizi ya teknolojia ya uhimilishaji ili kuhakikisha wafu...