BI. MEENA AKUTANA NA WATAALAM WA MRADI WA TASFAM KUJADILI MAENDELEO YA MRADI
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena amekutana na wataalam wa Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi wa Baharini na Ufugaji wa Viumbe Maji (TASFAM) kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo Kikao hicho kimefanyika leo, Septemba 9, 2026, katika ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, jijini Dodoma, ambapo wataalam wamewasilisha hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo, unaolenga kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za uvuvi wa baharini na kuendeleza sekta ya ufugaji wa viumbe maji nchini.