DKT. NCHEMBA AZINDUA MKAKATI WA MIAKA 10 UFUGAJI WA KUKU NCHINI
◼️KUKU WA SINGIDA, DODOMA SASA KUTAMBULIKA KAMA KUKU WA KANDA YA KATI. ◼️ATAKA TEKNOLOJIA YA UFUGAJI WA SAMAKI KWENYE MABWAWA KUWAFIKIA WANANCHI Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amezindua mkakati wa miaka 10 wa ufugaji wa kuku ambao umelenga kubadilisha tasnia ya kuku nchini na kuifanya kuwa shindani, jumuishi na endelevu ili kuchangia usalama wa chakula, lishe, ajira, kipato, ukuaji wa uchumi na biashara. Dkt. Nchemba amezindua mkakati huo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane iliyofanyika Agosti 1,2026 kwenye viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma. “Kuku ni moja ya zao tambulisho kwa mikoa ya kanda ya kati na kaya mbalimbali, na kuzinduliwa kwa Mkakati huu kwa Serikali ni jambo la faraja ambalo litaenda kuleta mageuzi katika Sekta hiyo ndogo ya kuku na kuongeza uzalishaji wenye tija.”amesema Mhe. Dkt. Nchemba. Aidha Dkt. Nchemba ameielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha utekelez...