DKT. MADELE: LISHE DUNI YA PROTINI NI CHANZO KIKUU CHA UDUMAVU
Na. Stanley Brayton, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Magawa Madele, amesema ulaji mdogo wa vyakula vyenye protini ni miongoni mwa sababu kuu zinazochangia tatizo la udumavu, hususan kwa watoto, na kuwataka wananchi kuongeza matumizi ya bidhaa zitokanazo na mifugo na uvuvi ili kuboresha afya na ustawi wa jamii. Dkt. Madele aliyasema hayo leo Agosti 7, 2026, katika Viwanja vya Ngongo mkoani Lindi wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini, alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika shughuli za kuhamasisha ulaji wa bidhaa za mifugo na uvuvi. Alisema bidhaa zinazotokana na mifugo, samaki na viumbe wengine wa majini zina mchango mkubwa katika kuboresha lishe, ukuaji wa watoto, kuongeza ufanisi wa kazi na kujenga taifa lenye nguvu kazi yenye afya na tija. "Taifa lenye wananchi wenye afya bora lina uwezo mkubwa wa kuzalisha, kubuni na kupunguza gharama za matibabu zinazotokana na magonjwa yanayozuilika...