Machapisho

PROF. SHEIKH AWATAKA IUCN KUZINGATIA VIPAUMBELE VYA WIZARA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amelitaka Shirika la Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira (IUCN) kuzingatia vipaumbele vya Wizara katika utekelezaji wa Mradi wa Pamoja Tuhifadhi Bahari Yetu ili kuleta tija katika Sekta ya Uvuvi. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa Kikao cha kupitia Mradi wa Pamoja Tuheshimu Bahari Yetu unaoratibiwa na ICUN na kutekelezwa na Wizara za Kisekta na Taasisi zisizo za kiserikali, leo Machi 2, 2026 Mkoani Morogoro, Prof. Sheikh amewataka IUCN kuzingatia vipaumbele vya Wizara katika utekelezaji wa Mradi huo. "ni vyema ICUN kufuata Miongozo na Taratibu za Wizara katika kutekeleza Mradi kwa kuchangia katika Mkakati wa Mageuzi wa Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbemaji kwa mwaka 2026/2050, na programu zenu zilenge kwenye kufanya Mageuzi katika Sekta ya Uvuvi.” amesema Prof. Sheikh Vilevile, Prof. Sheikh amesema kwa sasa Wizara inataka kufanya Mageuzi kat...

KINGOLWIRA INAFAA KUWA KITUO KIKUBWA CHA UKUZAJI VIUMBEMAJI NCHINI - PROF. SHEIKH

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amesema  Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kinafaa kuwa Kituo kikubwa na cha Kitaifa cha Ukuzaji Viumbemaji nchini kwani kina Miundombinu nyinyi ambaazo zinajengwa na za kisasa. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, alipotembelea Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kwa ajili ya kukagua Miundombinu na Uzalishaji, leo Machi 2, 2026 Mkoani Morogoro, Prof. Sheikh amesema Kituo kinazalisha vifaranga 600,000 kwa mwaka ikiwa kuna Vizimba 6 tu. "kwa hiyo ni vyema kuharakisha kujenga Miundombinu nyingine haraka hili kuweza kuzalisha vifaranga vya Samaki zaidi ili wananchi wape kufuga.” amesema Prof. Sheikh Aidha, Prof. Sheikh amesema Mradi huo wa Ukuzaji Viumbemaji wa Kingolwira unaendelea kuboreshwa zaidi kwa kutengeneza Vizimba vingine na Miundombinu nyingine ambazo zitakuwa zinazalisha vifaranga kwa wingi. Vilevile, Prof. Sheikh amewataka Wata...

DKT. BASHIRU AZINDUA VITUO VYA KUKUSANYIA MAZIWA VYENYE THAMANI YA BIL. 1.157

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Bashiru Ally Kakurwa, amezindua vituo vya ukusanyaji wa maziwa vilivyojengwa kupitia mradi wa TI3P, uliogharamiwa na Serikali kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa kushirikiana na Heifer International. Uzinduzi huo umefanyika Machi 2, 2026 mkoani Kagera, ukihusisha kituo cha kukusanyia maziwa cha Maruku kilichopo Manispaa ya Bukoba, Kituo cha Nshamba kilichopo Wilaya ya Muleba pamoja na kukabidhi mitamba 110 ya ngo’mbe wa maziwa kwa wanawake na vijana wilayani Karagwe. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Bashiru amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, anasisitiza kuwa wazalishaji wadogo, wakiwemo wafugaji na wavuvi, wanawezeshwa ili kuongeza uzalishaji wenye tija. “Mhe. Rais alivyoniteua aliniambia, sekta hizi unazokwenda kuziongoza zinawahusu wanaovuja jasho ambao ni wazalishaji wadogo; lazima utafute mbinu za kuwaunganisha ili waongeze uzalishaji. Naipongeza benki ya TADB kwa kuja na mradi hu...

UFUGAJI SATO BAHARI (CHOTARA) NA KAA NI FURSA MUHIMU KATIKA MASOKO YA MAZAO YA UVUVI - PROF. SHEIKH

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amesema teknolojia mpya ya Ukuzaji kaa na Samaki aina ya Sato (Chotara) ni fursa muhimu katika kufungua Masoko ya nje na kukuza Sekta ya Uvuvi. Akizungumza Prof. Sheikh, alipotembelea shamba la Ukuzaji Viumbemaji la Tanga Fish Aqua, leo Februari 28, 2026 Mkoani Tanga, amesema uvumbuzi wa teknolojia mpya ya Ukuzaji Kaa na Sato ambae anafugika kwenye maji Bahari kwa njia ya Vizimba, ambazo hutumia maboksi ya plasti katika kukuza Viumbemaji hao, imeleta tija kwenye tasnia ya Uvuvi kwa kuongeza Uzalishaji wa zao hilo la Uvuvi nchini. "Kaa na Sato waweza kukua kwenye maji Bahari, na ni fursa adhim kwa wananchi, kwani inafungua Masoko ndani na nje ya nchi ambapo upelekea kuinua Uchumi wa mtu binafsi na wa Taifa kiujumla.” amesema Prof. Sheikh Aidha, Prof. Sheikh amebainisha kuwa kilo moja ya kaa ni shilingi 25,000 hadi 30,000 kiasi ambacho kinaweza mpatia mtu utajiri, na Ufugaji huo una...

DKT. BASHIRU ASHANGAZWA NA WABUNGE WANAOTETEA UVUVI HARAMU NCHINI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakukrwa amesema kwa sasa serikali haita chukua hatua za kufunga Ziwa Victoria na badala yake itawafungia wavuvi na wale wote watakaobainika kujihusisha na uvuvi haramu. Dkt. Bashiru amesema hayo Februari 28, 2026 baada ya kushuhudia nyavu haramu zilizokamatwa na timu ya elimu kwa vitendo kuhusu uvuvi haramu kwa vitendo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kituo cha Rubambagwe Wilayani Chato Mkoa wa Geita. Aidha, Balozi Dkt. Bashiru ameshangazwa na baadhi ya wabunge na madiwani kuwa mstari wa mbele kutetea uvuvi haramu ambapo amesema kitendo hicho  sio  cha kiungwana.

DKT. BASHIRU: NATAKA MTAMBO WA KUKAUSHIA DAGAA SOKO LA CHATO BEACH

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally amemtaka Mkandarasi anayesimamia ujenzi wa miundombinu ya Soko la Kimataifa Samaki la Chato Beach mkoani Geita kukamilisha ufungaji wa mtambo wa kukaushia dagaa pamoja na kumalizia kazi zingine zilizobaki kabla ya mwezi Machi Mwaka huu. Dkt. Bashiru ametoa maagizo hayo leo Februari 28, 2026 baada ya kukagua mwenendo wa ujenzi wa miundombinu ya soko hilo ambapo ameonesha kutoridhishwa na kasi ya kazi zinazofanywa licha ya changamoto  za mkandarasi  pia ameagiza kufanyika tathmini mpya ya gharama za mtambo huo ili upatikane kwa haraka katika soko hilo “Nataka kazi kwa kasi, maelekezo niliyopewa na mamlaka iliyioniteua , sasa  nataka Jumatatu barua iwe imejibiwa mpaka jumatano(mkandarasi) awe ameipata na mimi nipate ‘copy’, mimi nataka mtambo hapa, kama mtambo huu ni wa kukausha dagaa lazima uwepo ndio tuzindue soko hili ” alisema Dkt. Bashiru. Akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja zilizoibuliwa na mjadala huo mbele ya Wazi...

MAENDELEO YA UJENZI WA SOKO LA SAMAKI KIPUMBWI HAYARIDHISHI - PROF. SHEIKH

Picha
Na. Stanley Brayton  ◾Wizara yagoma kuzungumzia kuongeza Mkataba. ◾Awashauri wataalam wa Halmashauri kufuatililia kwa karibu Maendeleo ya Mradi. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya World Class Engineering Contractors Limited kumaliza Ujenzi wa Mradi wa soko la Samaki Kipumbwi haraka iwezekanavyo ili kuweza kuwapa nafasi wavuvi wanaotegemea Soko ilo katika kukuza vipato vyao kwa kufanya biashara, Mradi ambao unatekelezwa chini ya Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) na kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kilimo (IFAD). Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, katika ziara yake ya kikazi Mkoani Tanga na kukagua Maendeleo ya Miradi wa Soko la Samaki la Kipumbwi lililopo Wilayani Pangani, leo Februari 27, 2026, Prof. Sheikh amesema soko la Samaki la Kipumbwi ni tegemo kubwa sana kwa wavuvi na ni soko ambalo litasaidia kukuza Uchumi wa wananchi na wa Taifa kiujumla. "ni vy...