WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MIRADI YAO
Na, Fausta Njelekela Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Bw. Salum Khalfan Mterera, leo Agosti 3, 2026, amefungua mafunzo kwa wanufaika wa Programu ya Uwezeshaji Vijana kupitia Miradi ya Kiuchumi katika Sekta za Mifugo na Uvuvi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Bunda, mkoani Mara. Akifungua mafunzo hayo, Bw. Mterera amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwapatia mikopo yenye riba nafuu ili kuwajengea uwezo wa kuanzisha na kuendeleza miradi ya uzalishaji, uongezaji thamani wa mazao ya mifugo na uvuvi pamoja na huduma katika minyororo ya thamani ya sekta hizo, na amesema hatua hiyo inalenga kuongeza ajira, kipato cha wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa. "Mkoa wa Mara umenufaika na jumla ya miradi 272 yenye thamani ya shilingi bilioni 1.77, ikijumuisha ufugaji wa kuku, mbuzi, kondoo, nguruwe pamoja na miradi ya zana za uvuvi." Aidha, amewataka wanufaika kusimamia kwa weledi miradi hiyo, kuzingatia matumizi...