Machapisho

TASFAM YATOA MAFUNZO KUONGEZA THAMANI ZAO LA MWANI MKOANI LINDI

Picha
Na. Martha Mbena. Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kupitia Mradi Kuendeleza na Kusimamia Uvuvi wa Baharini na Ukuzaji viumbe maji kwa njia endelevu nchini Tanzania (TASFAM) Umeanza kutoa mafunzo ya kilimo cha Mwani,  Ufugaji Jongoo Bahari, uanzishwaji wa Vikundi pamoja na Kanuni za Ukuzaji viumbe maji kwa wanufaika wa mradi huo ndani ya Manispaa ya Lindi, Mkoani Lindi. Akizungumza wakati wa kutoa mafunzo hayo yaliyofanyika Machi 26,2026 Mkoani humo Afisa Uvuvi Mkuu Bi. Happy Kapinga amesema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo wakulima wa zao la mwani pamoja wafugaji wa jongoo Bahari. "Leo tumekuja hapa  Mkoani Lindi, Kata ya Mchinga kwa ajili ya kutekeleza malengo ya mradi wa TASFAM  ambapo  takribani wakulima 600 tunatarajia wapate uelewa katika Ukuzaji Viumbe maji kwa mkoa wa Lindi", Amesema Bi. Kapinga. Aidha, Kapinga  ameongeza kuwa mradi huo unatarajiwa kutekelezwa ndani ya miaka mitano, hivyo utasaidia katika ukuaji wa uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na...

WAVUVI TANGA WAPEWA ELIMU YA UZALISHAJI ZAO LA MWANI NA JONGOO BAHARI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2025/2026 imeanza utekelezaji wa Mradi wa Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji (TASFAM) kwa kuwajengea uwezo katika mnyororo wa thamani wakulima wa mwani na wakuzaji Jongoo Bahari, Mradi ambao unatekelezwa kwa miaka mitano (2025 hadi 2030), wenye lengo kuimarisha Usimamizi wa Rasilimali za Baharini na kuboresha maisha ya jamii za pwani Tanzania Bara na Zanzibar. Akizungumza leo Machi 26, 2026 Jijini Tanga kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa zoezi la kuwajengea uwezo Wakulima wa Mwani na Jongoo Bahari Jijini hapo, Afisa Uvuvi Mkuu wa Wizara hiyo, Ndg. Silas William, amesema Mafunzo hayo ni fursa adhimu kwa Wakulima wa Mwani na Jongoo Bahari kwani wanapata kujifunza kuhusu Mnyororo mzima wa thamani wa Mazao hayo ambayo yenye tija kwa soko la sasa. "Wizara kwa sasa imekuja na Mpango madhubuti wa kuwaelimisha Wakulima ili waweze kufanya shughuli zao za uzalishaji kwa vikundi na u...

DKT. BASHIRU AKUTANA NA MAAFISA WAFAWIDHI KUJADILIANA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekutana na Maafisa Wafawidhi wa Vituo vya Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi kwa lengo la kujadili kwa pamoja  jinsi kusimamia rasilimali hizo na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazowakabili wataalam katika utendaji kazi wao. Katika Majadiliano  hayo na Maafisa Wafawidhi yaliofanyika leo Machi 25, 2026 Jijini Dodoma Mhe. Balozi Dkt. Bashiru aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena, Naibu Katibu Mkuu(Uvuvi) Prof. Mohamed Sheikh, Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Nchini, Dkt. Baraka Sekadende na Wataalam wengine wa Wizara. Pamoja mambo mengine yaliyojadiliwa kwenye Kikao hicho, msisitizo mkuu ulijikita katika kutafuta mbinu bora za kuimarisha usimamizi wa rasilimali za uvuvi hususan kudhibiti utoroshwaji wa samaki na dagaa katika maeneo ya mipakani, uimarishaji wa uvuvi endelevu pamoja na kukabiliana na uvuvi usiofuata sheria, lakini kuangalia mianya inavyosababisha upotevu wa map...

DKT. BASHIRU AZINDUA MWONGOZO WA KITAIFA KUSIMAMIA RASILIMALI ZA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amezindua Mwongozo wa Kitaifa wa Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi Nchini (BMUs) ili kulinda rasilimali hizo ambazo ni muhimu katika kukuza uchumi na kuimarisha usalama wa chakula. Mhe. Dkt. Bashiru amezindua mwongozo huo leo Machi 25, 2026 wakati akifunga Mkutano wa Siku Mbili wa Ngazi ya Juu Kuhusu Mustakabali wa Uendelevu na Usimamizi Shirikishi wa Rasilimali za Uvuvi na Uchumi wa Buluu aliofanyika Jijini Dodoma, na kutoa rai kwa Wataalam, Viongozi na Wadau wa Sekta ya Uvuvi nchini kutafuta mbinu shirikishi katika kukabiliana na uvuvi usiofuata sheria. “Nimefanya ziara Kanda ya Ziwa nimeona kuna watu wanafanya ubunifu wa uhalifu kwa kubadilisha nyavu halali kufanya uvuvi usiofuata sheria, utaratibu wa namna ile  huwezi kudhibiti kwa Polisi, utakuwa na Polisi wangapi ?, njia pekee ya kufanikiwa ni kuwa na mbinu shirikishi na kuelimishana bila kuchoka, kwa hiyo huu mwongozo usiishie kwenye makaratasi” alisem...

KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUIMARISHA USALAMA WA CHAKULA NCHINI

Picha
Baraza la Kumshauri Rais Masuala ya Kilimo na Chakula limekutana na Wizara ya Kilimo pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa lengo la kujadiliana namna ya kuongeza uzalishaji katika sekta hizo ili kuimarisha  usalama wa chakula nchini. Mwenyekiti wa Baraza hilo na Waziri Mkuu Mstaafu  Mhe. Mizengo Pinda  ameongoza kikao hicho leo Machi 24, 2026 katika Ukumbi wa Kilimo Four Jijini Dodoma ambapo amesema kuwa  baraza hilo limekuwa likiimarisha ushirikiano wa wadau na sekta binafsi katika kuongeza uzalishaji na kuzihimiza Wizara za Kilimo, Mifugo na Uvuvi kufanya kazi kwa umoja ili kuyafikia malengo ya kuongeza uzalishaji ifikapo Mwaka 2030. “Malengo haya yanatupeleka 2030 leo hii 2026 unaona kabisa muda sio rafiki kwa hiyo nguvu kubwa sana inahitajika lakini tukiwa wamoja hatutashindwa kuyafikia” amesema Mhe. Pinda. Akisoma taarifa ya Mpango wa Kuongeza Uzalishaji wa Chakula Nchini Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt. Florence Turuka amesema dhamira ya serikali katika se...

UHIMILISHAJI WA MIFUGO KUONGEZA UZALISHAJI WA MAZIWA NCHINI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) unaolenga kuongeza uzalishaji wa maziwa na nyama kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya uhimilishaji.  Kauli hiyo imetolewa leo Machi 23, 2026 na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Stephen Michael, wakati akifungua  mafunzo ya uhimilishaji kwa wataalamu wa mifugo yaliyofanyika  katika Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) mkoani Arusha. kuongeza tija na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. “Mafunzo haya ni sehemu muhimu ya kuhakikisha wataalamu wanapata ujuzi wa kisasa utakaowawezesha kuwahudumia wafugaji kwa ufanisi zaidi ili kuongeza tija na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi,” amesema  Bw. Michael. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) Dkt. Dafay Bura amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea wataalam wa mifug...

SERIKALI KUANZISHA PROGRAMU YA MAFUNZO YA TEKNOLOJIA YA UZALISHAJI KUKU NCHINI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, imeanza mchakato wa kuanzisha programu ya mafunzo ya teknolojia ya kuku ili kukidhi mahitaji ya wadau wa sekta hiyo, mchakato ambao umeanza na maandalizi ya mtaala pekee ambapo warsha ya wadau imefanyika ili kupitia na kuboresha Rasimu ya Mtaala wa Teknolojia ya Uzalishaji wa kuku ngazi ya Astashahada na Stashahada yenye lengo la kuanzisha programu hiyo ili kupata wataalamu mahiri watakaochangia kuleta mabadiliko makubwa katika Tasnia. Akizungumza leo Machi 23, 2026 Jijini Dar es Salaam katika Warsha hiyo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amesema Mafunzo ya ufugaji kuku yamekuwa yakitolewa kwa sehemu ndogo sana ndio maana sasa Serikali imeona ni vyema kuanzisha Mtaala mahususi wa kuzalisha wataalam wabobevu kwenye tasnia hiyo kutokana na uhitaji wa wadau wa sekta binafsi na ukuaji wa sekta yenyewe nchini. "Wizara kupitia Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) kwa kushirikiana na wadau wa s...