SHILINGI BIL. 30.7 KUWANUFAISHA VIJANA PROGRAMU YA BBT
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Kamani amesema serikali inaendelea kutekeleza Programu ya Jenga Kesho Iliyobora (Building Better Tomorrow - BBT) ambapo katika mwaka wa fedha 2025/2026 wizara hiyo imepokea shilingi bilioni 30.7 (Sekta ya uvuvi shilingi bilioni 25.9 na sekta ya mifugo shilingi bilioni 4.75) kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi wadogo pamoja na vijana katika maeneo mbalimbali hapa nchini. Mhe. Kamani amesema hayo leo Aprili 10, 2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Vitimaalum, Mhe. Maryam Azan Mwinyi, kwenye Kipindi cha Maswali na Majibu cha Bunge la 13, Mkutano wa Tatu, Kikao cha Sita. Swali la Mbunge huyo lilihoji hatua inayochukuliwa na serikali kuwawezesha Wananchi hususani Vijana na Wavuvi wadogo kushiriki kikamilifu katika uchumi wa Bluu. “ Mheshimiwa Spika, Kupitia programu ya BBT, vijana 308 wamepatiwa mikopo isiyo na riba na yenye masharti nafuu kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya ufugaji wa samaki kwenye vizimba, ufug...