SERIKALI YAPOKEA MTAMBO WA KISASA KUIMARISHA SEKTA YA UVUVI KIGOMA
Na. Chiku Makwai, WMUV ◾ Zaidi ya Tani 15 za barafu kuzalishwa kwa siku. ◾ Dagaa zaidi ya Kilo 300 kukaushwa kwa siku. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepokea mtambo wa kisasa wa kuzalisha barafu na kukaushia dagaa, pamoja na majokofu yanayotumia nishati ya jua, kutoka mradi wa FISH4ACP ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha sekta ya uvuvi mkoani Kigoma. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya mtambo huo iliyofanyika Aprili 14, 2026 katika mwalo wa Katonga mkoani Kigoma, Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhe. Hassan Rungwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amesema kuwa mtambo huo utawasaidia wavuvi kuongeza ufanisi katika shughuli zao na kukuza uzalishaji utakao wawezesha kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na nje ya nchi. “Hatua hii itaongeza ubora wa mazao ya uvuvi, kuimarisha ushindani wa bidhaa zetu katika masoko ya ndani na nje ya nchi, pamoja na kuinua kipato cha wananchi wa Mkoa wa Kigoma,” amesema Mhe. Rungwa. Aidha, Mhe. Rungwa amewataka wavuvi pamoja na mamlaka zinazo...