RIDHIWANI AVUTIWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA BANDA LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI
Na. Chiku Makwai- Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ameonesha kuvutiwa na huduma na elimu mbalimbali zinazotolewa katika banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi alipotembelea banda hilo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akiwa katika banda hilo, Waziri huyo alipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa Wizara na taasisi zake kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi, ikiwemo ushauri wa kitaalamu katika sekta za mifugo na uvuvi, fursa za uwekezaji, pamoja na mikakati inayotekelezwa na Serikali katika kuendeleza sekta hizo kwa manufaa ya wananchi na uchumi wa Taifa. Waziri Ridhiwani alieleza kuridhishwa na namna wataalamu wanavyotoa huduma kwa wananchi kwa ukaribu na ufanisi, huku akisisitiza umuhimu wa taasisi za umma kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuwafikia wananchi moja kwa moja na kusikiliza changamoto zao ili kuboresha ut...