TANZANIA YAPATA HESHIMA KUWA MWENYEJI KUANDAA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA UKUZAJI VIUMBEMAJI
Na. Stanley Brayton ◾Dkt. Bashiru azindua Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Uvuvi Tanzani (TAFICO) na Kitabu cha Mapishi ya Samaki. Tanzania imepata heshima ya kuwa mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Ukuzaji Viumbemaji Duniani (WA26T) na Kongamano la Ukuzaji Viumbemaji Afrika (AFRAQ26), baada ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jumuiya ya Wakuzaji Viumbemaji Duniani (WAS) kusaini hati ya makubaliano ya maandalizi ya kongamano hilo litakalofanyika nchini Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), kuanzia Desemba 1 hadi 4, 2026. Makubaliano hayo yamesainiwa leo Julai 13, 2026 Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, kwa niaba ya Serikali, huku WAS ikiwakilishwa na Mwenyekiti wa Tawi la Afrika (AFRAQ), Prof. Julius Manyala. Akizungumza baada ya utiaji saini huo, Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru alisema uteuzi wa Tanzania kuwa mwenyeji wa kongamano hilo ni matokeo y...