MAENDELEO YA UJENZI WA SOKO LA SAMAKI KIPUMBWI HAYARIDHISHI - PROF. SHEIKH
Na. Stanley Brayton ◾Wizara yagoma kuzungumzia kuongeza Mkataba. ◾Awashauri wataalam wa Halmashauri kufuatililia kwa karibu Maendeleo ya Mradi. Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya World Class Engineering Contractors Limited kumaliza Ujenzi wa Mradi wa soko la Samaki Kipumbwi haraka iwezekanavyo ili kuweza kuwapa nafasi wavuvi wanaotegemea Soko ilo katika kukuza vipato vyao kwa kufanya biashara, Mradi ambao unatekelezwa chini ya Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) na kufadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Kilimo (IFAD). Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, katika ziara yake ya kikazi Mkoani Tanga na kukagua Maendeleo ya Miradi wa Soko la Samaki la Kipumbwi lililopo Wilayani Pangani, leo Februari 27, 2026, Prof. Sheikh amesema soko la Samaki la Kipumbwi ni tegemo kubwa sana kwa wavuvi na ni soko ambalo litasaidia kukuza Uchumi wa wananchi na wa Taifa kiujumla. "ni vy...