Machapisho

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA CHUO CHA MINNESOTA KUWAJENGEA UWEZO WATAALAM WA MIFUGO

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Minnesota cha Nchini Marekani, imeendelea kujadiliana na kuimarisha mahusiano yenye lengo la kuwajengea uwezo wataalam wa sekta ya mifugo kupitia mradi wa CAHFS ProgRESSVet ili kuhakikisha wataalam hao wanatoa huduma za afya ya wanyama zinazokidhi viwango vya kimataifa. Hatua hiyo inafuatia ujio wa wataalam kutoka Kituo cha Afya ya Wanyama na Usalama wa Chakula cha Minnesota kwa ajili ya kujadili mashirikiano mapya ya mafunzo katika eneo la usalama wa chakula, Majadiliano yaliyo fanyika leo, Februari 25, 2026, katika Makao Makuu ya Wizara yaliyopo Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma. Ujumbe huo uliongozwa na Naibu Mkurugenzi wa CAHFS, Dkt. Maria Perez, na kupokelewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena, ambaye alisisitiza dhamira ya serikali katika kuendeleza ushirikiano huo. “Serikali itaendelea kushirikiana na Chuo Kikuu cha Minnesota kuhakikisha wataalam wetu wa mifugo wanapata mafunzo ...

VCT YAWATAKA WATOA HUDUMA ZA AFYA YA WANYAMA KUJISAJILI

Picha
Baraza la Veterinari Tanzania (VCT) limewataka wamiliki wa Vituo vya kutoa Huduma za Wanyama pamoja na Wataalam wake kujisajili katika Baraza ili waweze kutambulika na Baraza hilo. Akizungumza kwa niaba ya Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania (VCT), wakati wa Ukaguzi wa Vituo mbalimbali vya kutolea Huduma za Afya ya Wanyama pamoja na Wataalam wake, leo Februari 24, 2026 Mkoani Dar es Salaam, Mkaguzi wa Baraza hilo, Dkt. George Mtinda, amesema takwa la kusajili Wataalam na Vituo vya Huduma za Afya ya Wanyama ni takwa la kisheria ambalo linamtaka Mtaalam au mtoa Huduma hizo kujisajili ili kutambulika na Baraza. "hii ni moja ya utekelezaji wa Sheria ya Veterinari SURA 319, ambayo inawataka Wataalam na Vituo vya kutolea Huduma hizo kujisajili ili kujua kama wamekidhi vigezo katika kutoa huduma.” amesema Dkt. Mtinda Aidha, Dkt. Mtinda amebainisha kuwa ni vyema kuhakikisha watoa Huduma wote wa Afya za Wanyama wanasajili Vituo vyao pamoja na kutumia Wataalam wenye sifa na waliojasili...

GHARAMA ZA UZALISHAJI NA USAFIRISHAJI MAZAO YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUPUNGUA

Picha
Serikali imelenga kupunguza gharama za uzalishaji na usafirishaji wa mazao katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi ili kuongeza thamani na kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi ili kuongeza kipato cha wakulima, wafugaji na wavuvi. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano Uendelezaji na ukuzaji wa shoroba za Kilimo, Mifugo, na Uvuvi uliofanyika February 20, 2026, mkoani Mtwara, Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Rajab amesema mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ina fursa kubwa za kimkakati katika utekelezaji wa shoroba za kilimo, Mifugo na Uvuvi kutokana na rasilimali Ardhi na Bahari pamoja na maziwa katika mikoa hiyo. “Mikoa hii ina fursa kubwa za kimkakati katika utekelezaji wa Shoroba za kilimo kutokana na rasilimali zilizopo, mazao ya kipaumbele ambayo ni korosho, ufuta, mbaazi pamoja na  choroko yanayozalishwa zaidi katika Mikoa ya Lindi na Mtwara vilevile mazao ya mahindi, maharage, kahawa, soya na tumbaku yanazalishwa zaidi katika Mkoa wa Ruvuma” amesema Mhe. Rajab. Aidha Mhe. Raja...

MRADI WA MALISHO J-CRISD WAANZA KUTEKELEZWA CHAMWINO

Picha
Mradi wa Uoteshaji wa Malisho ya Mifugo aina ya Juncao na Ustahimilivu wa Tabianchi (J-CRISD) unaofadhiliwa na IDN Norway umeanza kutekelezwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na IDN Africa pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, ambapo wafugaji wanapatiwa mafunzo ya kulima malisho kwa njia ya mashamba darasa. Uzinduzi wa utekelezaji wa mradi huo umefanyika Februari 19, 2026 katika shamba la mfugaji Mayunga Mashishanga lililopo Kata ya Mpayungwa, Katika uzinduzi huo, Afisa Usimamizi wa Nyanda za Malisho Bw. Boniphace Shija, alimwakilisha Mkurugenzi wa Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo na kutoa wito kwa wafugaji kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa mradi huo. “Zao hili tunalolipanda linalenga kusaidia upatikanaji wa malisho ya kutosha, pamoja na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, nitumie fursa hii kulishukuru Shirika la IDN Africa kwa kuwezesha utekelezaji wa shughuli hii, hivyo wafugaji mtoe ushirikiano,” alisema Bw. Shija. Aidha, Meneja...

“UWAZIRI” WANGU HAUNA MAANA KAMA HAUBADILI MAISHA YA WAFUGAJI-DKT. BASHIRU

Picha
◼️Aagiza Tanga Fresh ifanyiwe ukaguzi wa kiuchunguzi  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema kuwa kiapo alichokula wakati akiteuliwa kushika wadhifa huo kinamtaka kusimamia maslahi ya wafugaji ikiwa ni pamoja na kuwaondoa kwenye ufukara na kudhibiti matapeli wanaodhulumu wafugaji. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo wakati wa kikao chake kilicholenga kutathmini hali ya utendaji na kutafuta suluhu ya kukinusuru kiwanda cha kusindika maziwa cha Tanga Fresh kilichofanyika Februari 18,2026 jijini Tanga. “Uwaziri wangu hauna maana kama maziwa ya wafugaji yanamwagwa, Uwaziri wangu hauna maana kama wafugaji ni mafukara, Uwaziri wangu hauna maana kama matapeli wanadhulumu wafugaji” Amesema Balozi Dkt. Bashiru. Balozi Dkt. Bashiru amebainisha kuwa kiapo chake kinamlazimisha kusimamia sekta ya Mifugo ili iendeshwe kwa tija, kibiashara, kwa ufanisi na kwa maslahi ya wafugaji na Taifa. Akielezea maazimio yaliyotokana na kikao hicho, Balozi Dkt. Bashiru pamoja na m...

TASFAM YATAJWA KUAKISI DIRA YA TAIFA

Picha
Na. Edward Kondela Imeelezwa kuwa Mradi wa Utekelezaji wa Rasilimali za Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji (TASFAM), lazima uakisi matarajio ya dira ya maendeleo ya taifa katika kukuza sekta ya uvuvi nchini. Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh, amebainisha hayo leo (19.02.2026) jijini Dar es Salaam, wakati wa kikao kazi cha watumishi wanaohudumu katika mradi huo na watendaji wakuu wa taasisi za sekta ya uvuvi, ambapo amesisitiza mradi huo lazima utoe matokeo makubwa kwa wadau wa sekta ya uvuvi hususan vijana na wanawake. Prof. Sheikh ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo katika sekta ya uvuvi, amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa akitoa maelekezo kadhaa kuhusu sekta ya uvuvi katika matukio mbalimbali hivyo lazima maelekezo yake yatekelezwe kufikia malengo ya kukuza sekta hiyo. Ameongeza kuwa mradi wa TASFAM ni mkubwa katika sekta ya uvuvi, ambao unaweza kubadilisha maisha ya watanzania hususan wavuvi wadogo w...

WAFUGAJI CHAMWINO WAPEWA MAFUNZO KULIMA MALISHO

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Maendeleo, Norway katika Ukanda wa Africa (IDN- AFRICA) kupitia Mradi wa Uoteshaji wa Malisho ya Mifugo na Ustahimilivu wa Tabianchi  (J- CRISD) imeanza kutoa mafunzo kwa wafugaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino kuzalisha malisho aina ya Juncao ili kukabiliana na uhaba wa malisho na kuwa na ufugaji wenye tija Mafunzo hayo ambayo yameanza leo Februari 18, 2026  yameshirikisha wafugaji na wataalamu wa mifugo kutoka kata za Mpwayungu, Itiso, Mvumi, Makang’wa na Chilonwa ambapo lengo ni kutoa mafunzo kwa vitendo moja kwa moja kwenye maeneo ya wafugaji. Akifungua mafunzo hayo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chamwino Bi. Zaina Msangi amesema ujio wa mradi huo wa kuhamasisha wafugaji kulima malisho utasaidia kuondoa migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi. “Kwa upande wetu Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino hatukuwa na elimu hii ya malisho, kwahiyo mradi huu utasaidia kufikisha elim...