Machapisho

BIMA YA KIDIGITALI YA MIFUGO YAZINDULIWA

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amezindua Bima ya Kidigital ambayo imewezeshwa kwa ushirikiano baina ya Kampuni ya Bima ya CRDB pamoja na Kampuni ya ACRE Africa ambayo itatumia teknolojia ya kisasa kulinda mali za wafugaji nchini. Akizungumza leo Juni 29, 2026, katika Uzinduzi wa Bima ya Kidigitali ya Mifugo ijulikanayo kama Smart Mifugo, katika Hoteli ya Serena iliyopo Jijini Dar es Salaam, Bi. Meena amesema katika kukabiliana na changamoto za wafugaji, Kampuni ya Bima ya CRDB pamoja na Kampuni ya ACRE Africa, zimeleta suluhisho la ubunifu ambalo linatumia teknolojia ya kisasa kulinda mali za wafugaji wetu kupitia Smart Mifugo, na wafugaji kwa sasa wanaweza kupata bima kwa urahisi zaidi kwa njia ya kidijitali, salama na yenye uwazi. "Nimejulishwa kuwa kutakuwa na mfumo wa DigiBima App unaorahisisha usajili, malipo ya bima, na uwasilishaji wa madai, ambayo ni hatua muhimu katika kupeleka huduma karibu zaidi na wananchi, hususan wafugaji walioko vi...

BI. MEENA AMTAKA MKANDARASI KUKAMILISHA SOKO LA SAMAKI KIPUMBWI KWA WAKATI

Picha
◾Mradi wafikia asilimia 60 za utekelezaji. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya World Class Engineering Contractors Limited kuongeza kasi ya ujenzi wa Soko la Samaki la Kipumbwi, lililopo Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, ili mradi huo ukamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa Wavuvi na wadau wa Sekta. Akizungumza leo Juni 27, 2026, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Masoko ya Samaki Mkoani Tanga, Bi. Meena amesema Soko la Samaki la Kipumbwi ni miundombinu muhimu kwa maendeleo ya Sekta ya Uvuvi, kwani litawawezesha wavuvi na wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi kuongeza thamani ya bidhaa zao, kukuza biashara na kuinua vipato vyao, hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla. Amesema pamoja na umuhimu wa mradi huo, utekelezaji wake umefikia asilimia 60 pekee, huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Juni 30, 2026. "Fedha zote za mradi zipo tayari, hivyo ni wajibu wa mkanda...

DKT. LUTEGE: MAFUNZO YA MADAKTARI WA MIFUGO YATAIMARISHA FURSA ZA MASOKO YA NJE

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wa mifugo nchini kwa kuwapatia mafunzo yanayolenga kukidhi viwango vya kimataifa katika sekta ya mifugo, hatua itakayochangia kuongeza fursa za masoko ya mifugo na mazao yake ndani na nje ya nchi. Akizungumza katika hafla ya kuhitimu mafunzo kwa Madaktari wa Mifugo iliyofanyika leo Juni 25, 2026 katika Ukumbi wa Royal Hotel jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo nchini, Dkt. Benezeth Lutege, amesema mafunzo hayo yamekuja kufuatia tathmini iliyofanywa na Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH) ili kubaini kama wataalamu wa mifugo nchini wanaendana na viwango vya kimataifa vinavyohitajika katika biashara ya mifugo na mazao ya mifugo. "Kupitia ushirikiano kati ya Shirika la Afya ya Wanyama Duniani na Chuo Kikuu cha Minesota, Tanzania imepata fursa ya kushiriki katika mafunzo hayo ambapo wataalamu tisa (9)wamehitimu, huku wataalamu wengine 26 wakitarajiwa kuanza mafunzo kwa njia ya mtandao." Amesema Dkt. ...

DKT. BASHIRU APIGA MARUFUKU KUKAMATWA KWA MALI ZISIZOHUSIKA NA UVUVI HARAMU

Picha
◼️Aelekeza kufutwa “ubalozi” wa Uvuvi haramu ziwa Tanganyika Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amepiga marufuku wataalam kukamata mali zisizohusika wakati wa utekelezaji operesheni za udhibiti wa uvuvi usiofuata sheria kwenye maeneo yote nchini. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo Juni 25,2026 Bungeni jijini Dodoma wakati wa kikao baina yake na wabunge wa mikoa ya Kigoma na Katavi ambacho kililenga kujadili zana za uvuvi wa ziwa Tanganyika. “Nimeshamwelekeza Mkurugenzi wa Sheria Wizarani kwangu zifuatwe taratibu zote za kisheria ili vyombo na mali zote zilizokamatwa zirejeshwe kwa wahusika na kuanzia sasa wanaotekeleza operesheni hizo wakamate nyavu na wavuvi wanaojihusisha na Uvuvi huo usiofaa” Amesisitiza Balozi Dkt. Bashiru. Aidha Balozi Dkt. Bashiru pia amewaelekeza wataalam kutowadhalilisha wavuvi hao wakati wa utekelezaji wa operesheni hizo ambapo amesisitiza kumchukulia hatua mtaalam yoyote atakayethibika kufanya hivyo. Katika hatua nyingine Baloz...

BANDARI ALIYOAHIDI MHE. DKT. SAMIA SASA IPO TAYARI – MHE. TELACK

Picha
Na Kilwa, Lindi Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, amesema Bandari ya Uvuvi ya Kilwa Masoko, ambayo iliahidiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ipo tayari kuanza kutoa huduma baada ya kufikia hatua za mwisho za ukamilishaji wake. Akizungumza leo Juni 25, 2026, wilayani Kilwa mkoani Lindi wakati wa zoezi la kihistoria la majaribio ya mitambo na miundombinu mbalimbali ya bandari hiyo, Mhe. Telack amesema kiwango cha ukamilishaji wa mradi huo kimefikia asilimia 99.99, huku hatua iliyobaki ikiwa ni kuwasha na kuthibitisha utendaji wa mitambo mbalimbali. Amesema miongoni mwa majaribio yaliyofanyika leo ni pamoja na kuwasha mitambo  ya kuzalisha barafu, ambayo inauwezo wa kuzalisha barafu tani 100 kwa siku mitambo hiyo inauwezo wa kugandisha barafu kwa nyuzi joto 3 sentigredi. “Hii ni ishara kuwa Bandari yetu sasa iko tayari kuanza kazi, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameandika historia kwa kujenga Bandari ya kwanza ya kisasa ya uvuv...

TATHMINI YA AWALI TANGA FRESH YAWASILISHWA KWA WABUNGE WA TANGA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewawasilishia wabunge wa mkoa wa Tanga taarifa ya tathmini ya awali ya kiwanda cha kusindika maziwa cha Tanga Fresh iliyofanywa na timu iliyoongozwa na Ofisi ya Mrajisi wa vyama vya ushirika nchini. Akizungumza wakati wa kikao cha kuwasilisha tathamini hiyo kilichofanyika leo Juni 24,2026 Bungeni jijini Dodoma, Balozi Dkt. Bashiru amesema kuwa taarifa hiyo ni ya awali na haiwezi kutumika kufanya maamuzi yoyote kwa sasa mpaka taarifa ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali itakapokamilika pia. “Rai yangu ni kukamilika kwa haraka kwa uchunguzi huo na ni lazima uchunguzi huo ufike mpaka kwenye mzizi wake ili suluhu ya kudumu iweze kupatikana na rai yangu naomba tuendelee kuimarisha ushirika kwa sababu wafugaji wetu ni wadogo hivyo wanahitaji kuwa na mifumo ambayo kidogo kinachopatikana kitakuwa na usawa”  Amesema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Kwa upande wa wabunge hao mbali na kumpongeza Balozi Dkt. Bashiru kwa ji...

WAZIRI KAKURWA AMEKUTANA NA CHAMA CHA UMOJA WA WAFUGAJI SAMAKI TANZANIA, ATOA WITO WA UMOJA NA USHIRIKIANO

Picha
Na Chiku Makwai – Dodoma Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Kakurwa, amekutana na kufanya mazungumzo na Chama cha Umoja wa Wafugaji Samaki Tanzania kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati bora ya ushirikiano kati ya chama hicho na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kuendeleza sekta ya ufugaji samaki nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika leo Juni 23, 2026 katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi Kambarage jijini Dodoma, ambapo pande zote mbili zimejadili fursa, changamoto na mikakati ya kuimarisha uzalishaji wa samaki pamoja na kuongeza mchango wa sekta hiyo katika uchumi wa taifa. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhe. Kakurwa amekipongeza chama hicho kwa juhudi zake za kuwaunganisha wafugaji samaki nchini na kuwataka wanachama wake kuendeleza umoja, nidhamu, hekima na ushirikiano ili kuhakikisha chama kinaendeshwa kwa weledi na kuleta matokeo chanya kwa wanachama na sekta kwa ujumla. Amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kushirikiana na wa...