NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKAGUA GATI LA KUEGESHEA MELI TAFICO
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh amekagua utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa gati la kuegeshea meli (floating jetty), unaotekelezwa na Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), katika Makao Makuu ya Shirika yaliyopo Ras Mkwavi–Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Katika ziara hiyo iliyofanyika Februari 10, 2026, Prof. Sheikh alimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena, ambapo amekagua maendeleo ya mradi huo muhimu unaotarajiwa kuongeza ufanisi wa shughuli za uvuvi na huduma za meli za uvuvi chini ya TAFICO, pamoja na maandalizi ya ujio wa meli ya kwanza ya uvuvi ya Shirika. Akiwa katika eneo la mradi, alimuelekeza mkandarasi wa mradi, kampuni ya Songoro Marine, kuhakikisha kazi zote zilizobakia zinakamilika na mradi huo ukabidhiwe ifikapo tarehe 15 ya mwezi Februari 2026. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Prof. Sheikh alisema kuwa kukamilika kwa gati ambao ni miundombinu muhimu katika uendeshaji wa meli ambayo itaingia nchin...