Machapisho

RIDHIWANI AVUTIWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA BANDA LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Na. Chiku Makwai- Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ameonesha kuvutiwa na huduma na elimu mbalimbali zinazotolewa katika banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi alipotembelea banda hilo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akiwa katika banda hilo, Waziri huyo alipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa Wizara na taasisi zake kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi, ikiwemo ushauri wa kitaalamu katika sekta za mifugo na uvuvi, fursa za uwekezaji, pamoja na mikakati inayotekelezwa na Serikali katika kuendeleza sekta hizo kwa manufaa ya wananchi na uchumi wa Taifa. Waziri Ridhiwani alieleza kuridhishwa na namna wataalamu wanavyotoa huduma kwa wananchi kwa ukaribu na ufanisi, huku akisisitiza umuhimu wa taasisi za umma kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuwafikia wananchi moja kwa moja na kusikiliza changamoto zao ili kuboresha ut...

DKT. MHINA AHIMIZA USHIRIKI WA SEKTA BINAFSI KATIKA KUIMARISHA MATUMIZI YA CHANJO ZA MIFUGO

Picha
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina, amesema kuwa matumizi sahihi ya chanjo ni moja ya nyenzo muhimu katika kudhibiti magonjwa ya mifugo, kuongeza uzalishaji na kuimarisha ushindani wa sekta ya mifugo nchini.  Dkt. Mhina ameyasema hayo leo Juni 16, 2026 jijini Arusha wakati akifungua Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Mifugo kuhusu Chanjo na Uchanjaji wa Mifugo ulioandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, GALVmed, FAO Tanzania na TAHO. Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Mhina amesema sekta ya mifugo ina mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania kupitia usalama wa chakula na lishe, ajira, kipato cha kaya pamoja na mauzo ya bidhaa za mifugo ndani na nje ya nchi.  Hata hivyo, amesema maendeleo ya sekta hiyo bado yanakabiliwa na changamoto za magonjwa mbalimbali ya mifugo yakiwemo Sotoka ya Mbuzi na Kondoo (PPR), Ugonjwa wa Midomo na Miguu (FMD), Brucellosis na...

SERIKALI KUANDAA MWONGOZO WA ULINZI NA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UVUVI NCHINI

Picha
 Na. Stanley Brayton, WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza kuandaa Mwongozo wa Utendaji Kazi kwa ajili ya Shughuli za Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi nchini ikiwa na lengo la kuandaa Mwongozo ambao utawezesha utekelezaji wa majukumu ya Usimamizi wa Rasilimali hizo kufanyika kwa ufanisi zaidi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali inayotumika katika Sekta ya Uvuvi. Akizungumza leo Juni 11, 2026 Mkoani Morogoro, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uvuvi Nchini, katika Kikao kazi cha Kuandaa Mwongozo huo, Mkurugenzi Msaidizi wa Uvuvi Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Christian Nzowa amesema kuwa Wizara imekutana na wadau mbalimbali kutoka Halmashauri zenye Maeneo ya Uvuvi wa mwambao wa Ziwa Victoria, Tanganyika, Nyasa, Maji Madogo na Bahari ya Hindi, pamoja na Maafisa Wandamizi Wastaafu wa Uvuvi na Maafisa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ili kupitia Mwongozo wa kiutendaji ujulikanao kama Standard Operating Procedure SOPs, na ambao utat...

SERIKALI NA BROOKE EAST AFRICA KUIMARISHA USTAWI NA ULINZI WA PUNDA NCHINI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuimarisha mikakati na hatua mbalimbali zinazolenga kuboresha ustawi wa punda nchini, ikiwemo upatikanaji wa lishe bora, maji, huduma za afya, ulinzi pamoja na matumizia salama ya wanyama hao. Akizungumza leo Juni 9, 2026 jijini Dodoma wakati wa kikao na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Brooke East Africa, Dkt. Raphael Kinoti, pamoja na watendaji wa shirika hilo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha ustawi na usalama wa mifugo akiwemo punda unaendelea kuimarika kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa vya ustawi wa wanyama. Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kufanya maboresho ya sera, sheria na kanuni zinazosimamia sekta ya mifugo ili kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo na kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo. “Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha mfumo wa sera na sheria zinazolinda mifugo ili kuendan...

BI. MEENA ATAKA UTAFITI KUWA CHACHU YA MAENDELEO YA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena, amesema kuwa utafiti una nafasi kubwa katika kuleta mageuzi na maendeleo endelevu ya sekta za mifugo, uvuvi na ukuzaji viumbe maji nchini, hivyo ni muhimu kuhakikisha agenda za utafiti zinaendana na mahitaji ya sasa na ya baadaye ya Taifa. Bi. Meena amesema hayo leo Juni 9, 2026, wakati akifungua Warsha ya Wadau ya Kupitia Ajenda za Taifa za Utafiti wa Mifugo pamoja na Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji za mwaka 2026–2030 iliyofanyika katika Ukumbi wa Brand Hotel jijini Dodoma. Amesema uwepo wa wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali, sekta binafsi, vyuo vikuu, taasisi za utafiti, mashirika ya maendeleo, mamlaka za serikali za mitaa na wadau wengine wa sekta hizo unaonesha dhamira ya pamoja ya kutambua mchango wa utafiti katika kukuza uchumi wa Taifa. "Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuimarisha shughuli za utafiti kwa kuanzisha taasisi maalumu za utafiti ambazo ni Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania ...

PROF. SHEIKH AAGIZA MABWAWA YA KITUO CHA UKUZAJI VIUMBEMAJI KINGOLWIRA KUFANYIWA MAJARIBIO YA MWISHO IFIKAPO JUNI 30

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Agnes Meena, ameagiza kufanyika kwa majaribio ya mwisho ya mradi wa mabwawa kumi (10) ya kufugia samaki unaotekelezwa katika Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira mkoani Morogoro ifikapo Juni 30, 2026 ili kuhakikisha miundombinu hiyo inaanza kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa ya kuongeza uzalishaji wa vifaranga bora vya samaki nchini. Prof. Sheikh ametoa maelekezo hayo leo Juni 8, 2026, alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), ikiwemo ukarabati wa kituo cha kutotolesha vifaranga na jengo la mitambo ya umeme pamoja na uchimbaji wa visima na usakinishaji wa pampu za maji. Amesema Serikali ina matarajio makubwa ya kukifanya Kituo cha Kingolwira kuwa kituo kikuu cha kitaifa cha ukuzaji viumbemaji na shamba darasa kwa ajili ya mafunzo, uzalishaji wa vifaranga bora na uhamasishaji wa tek...

DKT. BASHIRU AVUTIWA NA UWEKEZAJI SEKTA YA MIFUGO LEMOTI - MONDULI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amevutiwa na Mfugaji na Mwekezaji wa mfano Bw. Isaya Ole Mpekure anayemiliki ng'ombe zaidi ya 2,000 mitambo na ghala la kuhifadhia chakula cha mifugo ambapo shamba hilo limekuwa kitovu cha jamii ya wafugaji wa eneo hilo kuboresha mifugo yao na kufuga kwa tija. Amesema serikali itaendelea na mikakati ya kuendeleza sekta ya mifugo ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma za chanjo na utambuzi wa mifugo ili kudhibiti magonjwa,usimamizi na uendelezaji wa ardhi ya malisho na uimarishaji wa mbegu za mifugo na miundombinu ya ufugaji ili kuongeza uzalishaji na kuwakwamua wafugaji nchini. Kauli hiyo ya Waziri Balozi Dkt. Bashiru Juni 7, 2026 akiwa kwenye ziara yake wilayani Monduli Mkoani Arusha ziara  iliyolenga kukagua utekelezaji wa shughuli za mifugo, uwekezaji wa sekta ya mifugo wa Bw. Isaya Ole Mkupure na kushiriki sherehe za kimila za jamii ya wamasai katika kijiji cha Lemote. Katika hatua nyingine Balozi Dkt. Bashiru alisis...