FETA YAENDESHA MAFUNZO YA UTUNZAJI NA MATENGENEZO YA BOTI NA INJINI ZA UVUVI KATIKA MKOA WA TANGA
Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) imeendesha mafunzo ya Utunzaji na Matengenezo ya Boti na Injini kwa Maafisa Uvuvi, Wahifadhi wa Maeneo Tengefu na wavuvi wanufaika wa mkopo wenye masharti nafuu wa boti za kisasa za uvuvi zilizotolewa na Serikali. Mafunzo hayo yamehusisha washiriki 22 ambao ni Maafisa Uvuvi wa Wilaya wanne (4) na wavuvi 15 kutoka Wilaya za Mkinga, Tanga Jiji, Pangani na Muheza, Afisa Uvuvi mmoja (1) kutoka Kituo cha FRP - Tanga na Wahifadhi wawili (2) wa Hifadhi ya Bahari - Tanga. Mafunzo hayo ya siku 4 yalianza tarehe18 hadi 21 Agosti 2026 katika ukumbi wa Costal Zone mkoani Tanga. Akiongea wakati wa kufunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mtendaji Mkuu FETA, Naibu Mkuu wa FETA Bi. Merisia Mparazo amewaasa wahitimu wa mafunzo kutumia ujuzi walioupata kuboresha shughuli zao za uvuvi na kusambaza elimu kwa wavuvi wengine ambao hawakubahatika kupata mafunzo haya. Aidha amesema mafunzo haya yatapunguza gharama za uendeshaji na kuimarisha usalama wa vyombo kwa kuon...