DKT. BASHIRU AKAGUA NA KUZINDUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MARA
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekagua na kuzindua miradi ya mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara na kueleza kuwa serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika kutenga fedha kwa wakati katika ujenzi na uboreshaji miundombinu ya barabara, umeme na maji ili miradi hiyo ikamalishwe kwa wakati. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo Agosti 11, 2026 wakati wa ziara yake maalum ya siku nne inayolenga kutembelea, kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara. Katika ziara hiyo Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezindua Daraja la Majengo mapya - Pambazuko lenye thaman ya zaidi ya shilingi milioni 287 ambalo litaunganisha Kata za Bweri na Rwamlimi ndani ya Manispaa ya Musoma. Pia, alitembelea na kukagua ujenzi wa Soko la Nyayo, Kituo cha Mabasi na Barabara za mitaa ndani ya Manispaa ya Musoma, kuweka jiwe la Msingi la Madarasa matano, matundu ya vyoo na Ofisi katika shule ya Msingi Jitirola na kuka...