Machapisho

DKT. MADELE: LISHE DUNI YA PROTINI NI CHANZO KIKUU CHA UDUMAVU

Picha
 Na. Stanley Brayton, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Magawa Madele, amesema ulaji mdogo wa vyakula vyenye protini ni miongoni mwa sababu kuu zinazochangia tatizo la udumavu, hususan kwa watoto, na kuwataka wananchi kuongeza matumizi ya bidhaa zitokanazo na mifugo na uvuvi ili kuboresha afya na ustawi wa jamii. Dkt. Madele aliyasema hayo leo Agosti 7, 2026, katika Viwanja vya Ngongo mkoani Lindi wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Kusini, alipokuwa akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika shughuli za kuhamasisha ulaji wa bidhaa za mifugo na uvuvi. Alisema bidhaa zinazotokana na mifugo, samaki na viumbe wengine wa majini zina mchango mkubwa katika kuboresha lishe, ukuaji wa watoto, kuongeza ufanisi wa kazi na kujenga taifa lenye nguvu kazi yenye afya na tija. "Taifa lenye wananchi wenye afya bora lina uwezo mkubwa wa kuzalisha, kubuni na kupunguza gharama za matibabu zinazotokana na magonjwa yanayozuilika...

CAG AVUTIWA NA MIKAKATI YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUIMARISHA UVUVI WA BAHARI KUU

Picha
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Bw. Charles Kichere ametembelea Banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Kitaifa ya nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma ambapo alipata fursa ya kujionea mafanikio na mikakati mbalimbali ya Serikali katika kuendeleza sekta ya uvuvi hususan uvuvi wa bahari kuu, ziara hiyo imefanyika leo tarehe 07 Agosti 2026. Akiwa katika banda hilo CAG alipokea maelezo kutoka kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) Dkt. Mathew Silas kuhusu mikakati ya Wizara ya kuongeza tija na mchango wa sekta ya uvuvi katika uchumi wa taifa Dkt. Silas alieleza kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha sekta ya uvuvi inachangia kufikia lengo la asilimia 10 katika uchumi kupitia uwekezaji, usimamizi endelevu wa rasilimali za uvuvi wa bahari kuu na uimarishaji wa miundombinu ya sekta hiyo.

DKT. BASHIRU: CHUO CHA KAOLE KITOVU CHA ELIMU YA KILIMO NA MIFUGO

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amekitaja Chuo cha Kilimo na Mafunzo ya Mifugo Kaole kilichopo Bagamoyo Mkoani Pwani kuwa ni mfano wa mafanikio ya mageuzi kutoka kuwa eneo la harakati za ukombozi wa Afrika hadi kuwa kitovu cha kuzalisha wataalamu wa kilimo na mifugo wanaochangia maendeleo ya uchumi wa Taifa. Akizungumza katika Mahafali ya Kumi ya Chuo hicho iliyofanyika leo Agosti 6, 2026, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru  alisema kabla ya kuwa taasisi ya elimu, eneo la Kaole lilitumika kama kambi ya mafunzo ya wapigania uhuru wa Msumbiji kupitia Chama cha FRELIMO  ambapo baada ya nchi hiyo kupata uhuru mwaka 1975, eneo hilo lilikabidhiwa kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye kusimamiwa na Jumuiya ya Wazazi Tanzania kwa lengo la kuendeleza elimu na mafunzo ya ufundi stadi. "Kaole imebadilika kutoka kuwa kitovu cha mapambano ya ukombozi wa kisiasa na sasa ni kitovu cha mapambano ya maendeleo ya kiuchumi kupitia elimu inayolenga kuo...

NAIBU WAZIRI CHANDE APONGEZA TEKNOLOJIA YA UFUGAJI SAMAKI YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Hamad Hassan Chande ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa ubunifu na matumizi ya teknolojia ya kisasa katika ufugaji wa samaki baada ya kutembelea mabwawa ya kufugia samaki yaliyopo katika banda la Wizara kwenye Viwanja vya Maonesho ya Kitaifa na Kimataifa vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma Agosti 6, 2026. Akizungumza baada ya kutembelea mabwawa hayo Mhe. Chande alisema teknolojia inayotumika katika ufugaji wa samaki inaonesha dhamira ya Serikali ya kuimarisha sekta ya uvuvi kupitia matumizi ya mbinu za kisasa zinazoongeza uzalishaji kuboresha usalama wa chakula na kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla. Aidha Naibu Waziri huyo aliwataka wananchi hususan vijana kutumia fursa zilizopo katika sekta ya ufugaji wa samaki kwa kujifunza teknolojia hizo na kuwekeza katika shughuli za uzalishaji wa samaki hatua ambayo itasaidia kuongeza ajira, kipato na upatikanaji wa lishe bora. Sambamba na hilo Mhe. Chande alitembelea...

RIDHIWANI AONGOZA PAREDI YA MIFUGO 2026

Picha
◼️Ng’ombe mwenye kilo 922 kutoka Kondoa Mji avunja rekodi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete ameongoza paredi ya Mifugo iliyofanyika Agosti 05,2026 kwenye Viwanja vya kitaifa na kimataifa vya Maonesho ya NaneNane vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma. Akizungumza mara baada ya kufanyika kwa Paredi hiyo Mhe. Kikwete amesema kuwa tukio hilo linadhihirisha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuimarisha sekta ya Mifugo na kuifanya kuwa moja ya nguzo muhimu za maendeleo ya kiuchumi nchini. “Mifugo ni sehemu ya utamaduni, urithi na maisha yetu kwa sehemu kubwa hivyo tukio hili linaonesha fursa kwa wafugaji kuonesha mbinu na teknolojia za kisasa za utunzaji wa Mifugo” Ameongeza Mhe. Kikwete. Aidha Mhe. Kikwete amebainisha kuwa tukio hilo linatoa fursa kwa wafugaji kujifunza kutoka kwenye ufugaji wa kujikimu na kwenda kwenye ufugaji wa kisasa unaozingatia uzalishaji wenye ubora, ubora wa bidhaa zake, ushindani wa soko n...

MHE. RIDHIWANI AZINDUA KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA CHA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
 Na. Stanley Brayton Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete (Mb), amezindua Kituo cha Huduma kwa Wateja cha Wizara ya Mifugo na Uvuvi, hatua inayolenga kuimarisha mawasiliano kati ya Wizara na wadau wa sekta za mifugo na uvuvi, pamoja na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. Uzinduzi huo umefanyika leo Agosti 5, 2026, katika banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela, jijini Dodoma. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Ridhiwani amesema kuanzishwa kwa kituo hicho ni utekelezaji wa azma ya serikali ya kuboresha huduma kwa wananchi kwa kutumia mifumo ya kisasa ya mawasiliano, ambayo itawawezesha wafugaji, wavuvi na wadau wengine kupata taarifa sahihi na huduma kwa wakati. Amesema kituo hicho kitasaidia kupokea maoni, maswali, ushauri na malalamiko ya wadau, pamoja na kuhakikisha changamoto zinazowasilishwa zinashugh...

MHE. MACHA AWATAKA VIJANA KUTUMIA MIKOPO KWA USAHIHI ILI KUJENGA UCHUMI IMARA

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anamringa Macha, leo Agosti 5, 2026, amefungua mafunzo ya Programu ya Uwezeshaji Vijana Kiuchumi na kuwataka vijana walionufaika na mikopo ya Serikali kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa ili iwe chachu ya kujikwamua kiuchumi na kuchochea maendeleo ya Taifa. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhe. Macha amesema kuwa mafanikio ya vijana katika miradi ya mifugo na uvuvi yanategemea utayari wao wa kujifunza, kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia ushauri wa wataalamu. Amesema vijana wanapaswa kujifunza kutoka kwa wataalamu wa mifugo pamoja na wafugaji wenye uzoefu wa ufugaji wa kisasa ili wapate maarifa na mbinu bora zitakazowawezesha kuongeza uzalishaji na kuendesha miradi yao kwa ufanisi. "Ninawasihi mtumie mikopo hii kwa malengo yaliyokusudiwa na mjifunze kutoka kwa wataalamu wa mifugo pamoja na wafugaji wenye uzoefu ili muweze kuendesha miradi yenu kwa ufanisi. Msiwe na haraka ya kutafuta mafanikio, kwani yanahitaji uvumilivu, nidhamu na usi...