DKT. MWIGULU AHIMIZA UFUGAJI WA KISASA KUONGEZA UZALISHAJI NA TIJA
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amewahimiza wataalam na wadau sekta ya mifugo nchini kuendelea kutoa mafunzo ya ufugaji bora na wa kisasa kwa wananchi wote ili kuwa na tija katika uzalishaji katika sekta ya mifugo. Mhe. Dkt. Nchemba amesema hayo mara baada ya kukagua shughuli za ufugaji katika Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki leo Agosti 04, 2026 ambapo kwa kanda hiyo maonesho hayo yanafanyika Mkoani Morogoro. Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Nchemba alivutiwa na ng'ombe aliyefugwa na Magereza ya mkoani Morogoro ambaye anauwezo wa kuzalisha Lita 30 za maziwa kwa siku na kuielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na taasisi hiyo kuendelea kutoa elimu ya uzalishaji wenye tija kwa wananchi kupitia mafunzo na ugani. Aidha, Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Nchemba alisema ili kukabiliana na changamoto za uhaba wa maeneo kwa ajili ya ufugaji ni muhimu wadau wa sekta ya mifugo kujifunza mbinu za ufugaji wa kisasa wenye tija n...