NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATEMBELEA MAMLAKA YA KUSIMAMIA UVUVI WA BAHARI KUU
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo ametembelea Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) kwa lengo la kujionea utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo pamoja na kuzungumza na viongozi na watumishi kuhusu maendeleo ya sekta ya uvuvi wa bahari kuu. Katika ziara hiyo, Mhe. Kamani alipokea taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na mamlaka, ikiwemo usimamizi wa rasilimali za uvuvi wa bahari kuu, utoaji wa leseni, ufuatiliaji wa shughuli za uvuvi, na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali za bahari. Akizungumza na viongozi na watumishi wa mamlaka hiyo, Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa kuendelea kusimamia rasilimali za bahari kwa weledi, uwazi na ufanisi ili kuongeza mchango wa sekta ya uvuvi katika ukuaji wa uchumi wa taifa, kuongeza ajira na kuimarisha usalama wa chakula. Aidha, aliwahimiza watumishi kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta hiyo katika kupambana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa pamo...