Machapisho

KAMANI AITAJA MIKAKATI KUKABILIANA NA UPUNGUFU WA SAMAKI ZIWA TANGANYIKA

Picha
DODOMA: Serikali imesema wingi wa samaki katika Ziwa Tanganyika umepungua kwa asilimia 62, kutoka tani 304,500 mwaka 1998 hadi kufikia takribani tani 116,000 mwaka 2026.  Hayo yamesemwa leo Septemba Mosi 2026 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani wakati akijibu swali la Mbunge wa Kalambo, Mhe. Edifonsi Joakim Kanoni, aliyetaka kujua lini Serikali itafanya utafiti wa kubaini wingi wa samaki katika ziwa hilo. Mhe. Kamani amesema Serikali kupitia Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) hufanya tafiti za kubaini wingi na mtawanyiko wa samaki wa tabaka la juu (pelagic species) kwa kushirikiana na nchi za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Zambia huku kwa upande wa Tanzania, tafiti hizo zilifanyika mwaka 1998, 2022 na 2024, huku utafiti wa mwaka 2025 na 2026 ukifanyika kwa ushirikiano wa nchi hizo. "Matokeo yanaonesha mwenendo wa kupungua kwa rasilimali za samaki, hususan dagaa na migebuka, hali inayolazimu kuimaris...

TANZANIA, QATAR KUONGEZA USHIRIKIANO WA UWEKEZAJI KATIKA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Daudi Nyingo, DAR ES SALAAM  Serikali ya Tanzania imesema iko tayari kushirikiana na wawekezaji kutoka Qatar katika kuendeleza fursa za uwekezaji katika sekta za mifugo na uvuvi, ikiwemo kuongeza uzalishaji na usindikaji wa nyama, kupanua masoko ya bidhaa za mifugo katika nchi za Mashariki ya Kati, kuendeleza sekta ya kuku na kuwekeza katika miundombinu ya uvuvi. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, wakati wa mazungumzo yake na Naibu Waziri Mkuu wa zamani wa Qatar, Mhe. Dkt. Khalid bin Mohammad Al Attiyah, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Thirty-Five Investment Holding, katika ziara yake ya kikazi nchini Tanzania. Kikao hicho kilichofanyika Agosti 31, 2026 katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar es Salaam kilihudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara, Bi. Agnes Kisaka Meena; Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh, pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Wizara.  Akizungum...

KAMANI AKUTANA NA WATAALAM KUJADILI MAENDELEO YA SEKTA YA MIFUGO

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amekutana na wataalamu kutoka Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT), Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko (DPMD) na Idara ya Huduma za Mifugo (DVS), kwa lengo la kupokea na kujadili taarifa pamoja na majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na idara hizo. Vikao vyote vilivyomkutanisha Naibu Waziri Mhe. Kamani  pamoja na wataalam kutoka vitengo na idara hizo vilifanyika  leo Agosti 31, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Kambarage Tower, jijini Dodoma kwa nyakati tofauti. Katika kikao na wataalamu wa ICT, Mhe. Kamani alipokea taarifa na kushuhudia maonesho ya mfumo (demonstration) utakaotumika katika zoezi la utoaji wa mikopo kwa ajili ya kuwawezesha vijana kiuchumi, ambapo baada ya kupitia mfumo huo, alitoa mapendekezo na maelekezo mbalimbali kwa ajili ya kuuboresha kabla ya kuanza kutumika. Katika hatua nyingine, kikao na wataalamu wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Mhe. Kamani alijadiliana...

TANZANIA YAANZA KUJADILI USTAWI WA VIUMBEMAJI

Picha
Nchi ya Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya ufadhili wa Shirika lisilo la Serikali linalohamasisha kampeni ya “AFYA MOJA” (OHD) imeanza mkutano wa siku 2 unaojadili ustawi wa samaki wanaofugwa na  viumbe maji kwa ujumla unaofanyika Agosti 31 hadi Septemba 1, 2026 jijini Dar-es-salaam. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mkutano huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena amesema kuwa mbali na lengo la kutoa uelewa na kuongeza ufahamu kuhusu ustawi wa samaki na wanyama wa majini mkutano huo pia unalenga kubadilishana maarifa na uzoefu kuhusu afya ya samaki,usalama wa viumbe maji na uzalishaji unaowajibika. “Tanzania pamoja na Afrika kwa ujumla suala la ukuzaji viumbe maji limeshika kasi na watu wengi wamekuwa wakiwekeza kwenye tasnia hiyo hivyo mkutano huu unaangazia fursa na changamoto zinazoikabili tasnia ya ukuzaji viumbe maji ili kuhakikisha kwamba ufugaji wa viumbe maji unafanyika kwa uadilifu na kwa kuzingatia ustawi” Amesema Bi. Meena. Aidha Bi...

𝐖𝐀𝐓𝐄𝐊𝐄𝐋𝐄𝐙𝐀𝐉𝐈 𝐌𝐑𝐀𝐃𝐈 𝐖𝐀 𝐂-𝐒𝐃𝐓𝐏 𝐖𝐀𝐏𝐄𝐖𝐀 𝐌𝐀𝐅𝐔𝐍𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐌𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐔𝐉𝐈𝐅𝐔𝐍𝐙𝐀 𝐍𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐔𝐊𝐔𝐀 𝐇𝐀𝐓𝐔𝐀 𝐙𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐈𝐍𝐒𝐈𝐀 (𝐆𝐀𝐋𝐒)⁣

Picha
Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) umetoa mafunzo ya Mfumo wa Kujifunza na Kuchukua Hatua za Kijinsia (Gender Action Learning System – GALS) kwa watekelezaji wa mradi katika ngazi ya jamii.⁣ Mafunzo hayo yaliyoanza leo, tarehe 31 Agosti 2026 jijini Dodoma, kwa uratibu wa C-SDTP kupitia ufadhili wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), yanawakutanisha maafisa kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Vituo vya mafunzo vya LITA na SUZA, pamoja na Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka wilaya na shehia zinazotekeleza mradi wa C-SDTP Tanzania Bara na Zanzibar.⁣ Kupitia mafunzo haya, washiriki wanajengewa uwezo na ujuzi wa kutumia mbinu za GALS ili kwenda kutoa mafunzo katika ngazi ya jamii, kwa lengo la kuwezesha wanawake, wanaume na vijana kushiriki kikamilifu katika kuweka malengo ya kaya, kupanga kwa pamoja, kufanya maamuzi na kutumia rasilimali na fursa za kiuchumi kwa usawa.⁣ Hatua hii inalenga kuimarisha ushirikiano ndani ya kaya, kuongeza ushirik...

SERIKALI YAANZA KUPITIA KANUNI ZA UVUVI ZA MWAKA 2009

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza mchakato wa kupitia Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009, hatua inayolenga kuendana na mabadiliko ya kisera, kiuchumi, kimazingira na kiteknolojia yaliyotokea katika Sekta ya Uvuvi. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo Agosti 31, 2026 wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Sylvia Francis Sigula,  aliyetaka kujua lini Serikali itapitia Kanuni za Uvuvi ili kupunguza kero zinazotokana na tozo nyingi kwa wavuvi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi alisema mapitio hayo yamefanyika na kufanyiwa marekebisho mwaka 2026. Mhe. Kamani amesema katika mapitio hayo, Serikali imepita upya tozo na ada mbalimbali kwa lengo la kupunguza kero na gharama kwa wavuvi na wadau wengine wa sekta hiyo, huku ikihakikisha kuwa wajibu wa Wizara wa kusimamia, kuhifadhi na kuendeleza rasilimali za uvuvi hauathiriki. Aidha, Serikali imeandaa na kuziunganisha Kanuni zote zinazohusu ada na tozo na kuunda Kanu...

WAZIRI DKT. BASHIRU AFANYA MAZUNGUMZO NA BODI YA NARCO

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa leo Agosti 29, mwaka 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na  Bodi ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kujadili utekelezaji wa majukumu ya kampuni hiyo pamoja na kupata maoni, ushauri na mapendekezo ya bodi kuhusu namna ya kuzitatua changamoto  zinazoikabili NARCO ili iweze kujiendesha kwa faida na tija katika uzalishaji na uwekezaji kwenye sekta ya mifugo ikiwemo usimamiaji wa Vitalu na mashamba ya mifugo ya serikali. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, uliopo Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, ambapo Wajumbe wa Bodi ya NARCO, viongozi wa wizara akiwemo Katibu Mkuu Bi. Agnes Meena, Naibu Katibu Mkuu Anayesimamia Sekta ya Mifugo Dkt. Fabian Madele, Naibu Katibu Mkuu Anayesimamia Sekta ya Uvuvi Prof. Mohamed Sheikh na Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Dkt. Charles Mhina, walishiriki kikao hicho.