DKT. BASHIRU AKUTANA NA GATSBY AFRICA KUJADILI MKAKATI WA UZALISHAJI WA CHAKULA CHA SAMAKI NA KUKU
Serikali imeendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa maendeleo katika kuongeza tija ya sekta za mifugo na uvuvi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kukuza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuongeza mchango wa sekta hizo katika uchumi wa Taifa. Katika hatua hiyo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, leo Julai 24, 2026 amekutana na timu ya wataalam kutoka Taasisi ya Gatsby Africa katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, na kujadiliana kuhusu uwekezaji katika ukuzaji wa viumbemaji na kuongeza upatikanaji wa chakula cha samaki na kuku. Mazungumzo hayo yalijikita katika namna Serikali na Gatsby Africa zinavyoweza kushirikiana kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi kupitia uwekezaji katika uzalishaji wa malighafi za chakula cha mifugo, matumizi ya teknolojia za kisasa na kuimarisha mnyororo wa thamani wa uzalishaji. Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Bashiru alisema Serikali inaendelea kuweka mazingira weze...