Machapisho

MHE. KAMANI AWAONESHA FURSA WAWEKEZAJI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amewataka wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa zilizopo katika Sekta za Mifugo na Uvuvi, akiahidi ushirikiano wa Serikali katika kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanaendelea kuwa rafiki na wezeshi. Mhe. Kamani ametoa kauli hiyo leo, Septemba 17, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara maalum ya kikazi ya kutembelea wawekezaji wanaofanya shughuli katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Katika ziara hiyo, Naibu Waziri ametembelea Kampuni ya Alphakrust Limited pamoja na Kampuni ya Farmbase, ambapo amepata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanyika katika sekta hizo. Amesema Serikali imedhamiria kushirikiana kwa karibu na Sekta binafsi katika kukuza Sekta za Mifugo na Uvuvi, akieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Kamani amesema Serikali inaendelea kuweka mifumo inayorahisisha ushirikiano kati ya...

DKT. MADELE AHIMIZA MABADILIKO MRADI WA MAGEUZI YA TASNIA YA MAZIWA

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amewataka watekelezaji wa mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi kuhakikisha hatua ya pili ya utekelezaji wa mradi huo inawagusa wafugaji moja kwa moja. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kikao kazi cha wadau wanaotekeleza mradi huo Dkt. Madele amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo kwa mwaka uliopita ulijikita zaidi kwenye maandalizi ya miongozo hivyo ana imani hatua iliyobaki kwa sasa ni kwenda uwandani kwa wafugaji. “Lengo letu hapa ni kuweka alama ya mabadiliko ya Tasnia ya Maziwa kwa kiwango tulichowdka kwenye malengo na kutengeneza mifumo ambayo inahimili mabadiliko ya tabianchi kwa sababu huyu mfugaji tunayemuongelea hayupo hapa Dodoma mjini bali yupo huko Rungwe, Kilolo na kwingineko” Amesema Dkt. Madele. Aidha Dkt. Madele amewataka wataalam hao kupunguza vikao na kuelekeza nguvu uwandani ili kutambua wahusika wa mradi, wanachofanya na wanachopaswa kusaidiwa. Kwa upande wake mratibu w...

TANZANIA YASHIRIKI JUKWAA LA DUNIA LA MAEDELEO YA BAHARI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewasili katika Jiji la Qingdao nchini China kuhudhuria Jukwaa la Kidunia la Maendeleo ya Bahari (Global Ocean Development Forum) linafanyika kuanzia leo Septemba 16 hadi 18, 2026, ambapo ataiwakilisha Tanzania Katika jukwaa hilo kujadili fursa za Bahari Kuu. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru anashiriki Jukwaa hilo baada ya kupata mwaliko kutoka Kituo cha Taifa cha Utafiti wa Bahari Kuu (National Deep - Sea Center), cha Jamhuri ya Watu wa China  lengo ni kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na ubadilishanaji wa Maarifa katika sekta ya Bahari na Uchumi wa Buluu. Vile vile, Jukwaa hilo linawakutanisha wawakilishi kutoka Umoja wa Mataifa, Mamlaka ya Masuala ya Bahari za Nchi za Pwani, Viongozi wa Mashirika ya Kimataifa  yanayohusiana na masuala ya bahari , wataalam mashuhuri, wasomi, wajasiriamali na wadau wa sekta ya bahari. Baada ya kuwasili katika Jiji la Qingdao ametembelea na kujionea shughuli zinazofanywa na Taasisi y...

DKT. SAMIA KINARA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA MAGONJWA YA MIFUGO – MHE. KAMANI

Picha
Tanzania imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Sotoka ya Mbuzi na Kondoo (Peste des Petits Ruminants – PPR), ikiwa ni pamoja na kuandaa Mpango Mkakati wa Kudhibiti na Kutokomeza ugonjwa huo hadi mwaka 2030. Hatua hiyo pia imehusisha kuimarisha ushirikiano wa kikanda na nchi jirani, kwa lengo la kudhibiti na hatimaye kutokomeza PPR, ambao huathiri mifugo na maisha ya wafugaji. Akizungumza wakati wa kuhitimisha Mkutano wa Kikanda wa PPR uliofanyika leo, Septemba 16, 2026, katika ukumbi wa Mikutano wa White Sands Resort jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, amesema Tanzania imeendelea kuweka nguvu katika mapambano dhidi ya magonjwa ya mifugo. Mhe. Kamani alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano huo, akimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa. Katika hotuba yake, Mhe. Kamani ameushukuru Umoja wa Afrika (AU) kwa kumtambua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kama ki...

TANZANIA KUONGEZA NGUVU KUTOKOMEZA SOTOKA YA MBUZI NA KONDOO

Picha
Tanzania imeendelea kuongeza nguvu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Sotoka ya Mbuzi na Kondoo (Peste des Petits Ruminants - PPR) kwa kutengeneza Mpango Mkakati wa hadi mwaka 2030, na kuimarisha ushirikiano wa kikanda na nchi jirani katika kudhibiti na hatimaye kutokomeza ugonjwa huo unaoathiri mifugo na maisha ya wafugaji, hatua itakayoiweka Tanzania katika mstari wa mbele barani Afrika katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo unaodhuru mifugo. Akizungumza wakati wa kuhitimisha Mkutano wa Kikanda wa PPR uliofanyika leo Septemba 16, 2026 Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa Mikutano wa White Sands Resort, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, amesema Mpango huo ni wa kimkakati na ushirikiano wa nchi hizo ni hatua muhimu katika kukabiliana na magonjwa ya mifugo yanayovuka mipaka ya nchi. Mhe. Kamani, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano huo akimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Tanzania imekuwa ikikabiliwa...

DKT. MADELE AFUNGUA MAFUNZO YA ENEO LA KAZI KWA WATUMISHI

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele Septemba 16,2026 amefungua mafunzo kwenye eneo la kazi kwa watumishi wa Wizara hiyo waliopo makao makuu jijini Dodoma ambayo yametolewa na Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi (WCF), Wakala wa usalama na afya mahala pa kazi na Mfuko wa hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma.