MHE. KAMANI AWATAKA TVLA KUSIMAMIA UBORA WA VYAKULA VYA MIFUGO
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, ameitaka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kuimarisha usimamizi wa ubora wa vyakula vya mifugo vinavyozalishwa na kampuni mbalimbali nchini, ili kuhakikisha vinakidhi viwango na vigezo vinavyotakiwa. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 18, 2026, jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara katika Shamba la Kuku la Harvest Point Limited, linalojishughulisha na uzalishaji wa kuku wa mayai, chakula cha kuku pamoja na kutoa huduma za ugani kwa wafugaji. Amesema TVLA inapaswa kuhakikisha viwanda vinavyozalisha vyakula vya mifugo vinakaguliwa na kusimamiwa ipasavyo, sambamba na kutoa elimu na ushauri kwa wataalamu wa viwanda hivyo, ili kuhakikisha chakula kinachozalishwa kinakuwa na ubora unaokidhi mahitaji ya mifugo. “Ni muhimu TVLA kuhakikisha mnakagua viwanda hivi na kuwapatia wataalamu wake elimu ya kutosha, ili chakula kinachozalishwa kiwe bora na kiweze kumsaidia mfugaji kuongeza uzalishaji,” amesema Mhe. Kama...