MHE. KAMANI AWEKA BAYANA UBORA NA USALAMA WA SAMAKI WA KUFUGWA
◾Ahamasisha vijana kuchangamkia fursa za Mikopo Serikalini. ◾Awataka vijana kujifunza ujuzi kutoka kwa wawekezaji. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amesema Samaki wanaofugwa kwa njia ya vizimba na mabwawa hawana changamoto yeyote na ni salama na bora kwa matumizi ya chakula. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 13, 2026, Wilayani Sengerema jijini Mwanza, wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani hapo alipomtembelea muwekezaji wa Sekta ya Uvuvi Kampuni ya Ukuzaji Viumbemaji ya Tanzania Zhongzhi Aquaculture Company Limited. Aidha, Mhe. Kamani amesisitiza kuwa chakula kinachotumika kulishia Samaki ufanyiwa uhakiki wa mara kwa mara ili kuzingatia ubora unaohitajika na Wizara. "Samaki hawa wanapimwa kisayansi katika Maabara ya Taifa ya Uvuvi, na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) wanafanya utafiti wa ubora wa Vifaranga vya Samaki na kufuatilia ubora wa mazingira ya samaki wanapofugwa" amesema Mhe. Kamani Aidha, Mhe. Kamani amewataka vijana...