Machapisho

MHE. KAMANI AWATAKA TVLA KUSIMAMIA UBORA WA VYAKULA VYA MIFUGO

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, ameitaka Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) kuimarisha usimamizi wa ubora wa vyakula vya mifugo vinavyozalishwa na kampuni mbalimbali nchini, ili kuhakikisha vinakidhi viwango na vigezo vinavyotakiwa. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 18, 2026, jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara katika Shamba la Kuku la Harvest Point Limited, linalojishughulisha na uzalishaji wa kuku wa mayai, chakula cha kuku pamoja na kutoa huduma za ugani kwa wafugaji. Amesema TVLA inapaswa kuhakikisha viwanda vinavyozalisha vyakula vya mifugo vinakaguliwa na kusimamiwa ipasavyo, sambamba na kutoa elimu na ushauri kwa wataalamu wa viwanda hivyo, ili kuhakikisha chakula kinachozalishwa kinakuwa na ubora unaokidhi mahitaji ya mifugo. “Ni muhimu TVLA kuhakikisha mnakagua viwanda hivi na kuwapatia wataalamu wake elimu ya kutosha, ili chakula kinachozalishwa kiwe bora na kiweze kumsaidia mfugaji kuongeza uzalishaji,” amesema Mhe. Kama...

PROF. SHEIKH ASISITIZA NIDHAMU,KUJITUMA SHIMIWI 2026

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amewataka watumishi watakaoiwakilisha Wizara hiyo kwenye michuano ya SHIMIWI mwaka huu kuhakikisha wanadumisha nidhamu na wanajituma kwenye michezo yote watakayoshiriki kwenye michuano hiyo. Prof. Sheikh amesema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wachezaji hao iliyofanyika leo Septemba 18,2026 kwenye ofisi za Wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma ambapo amewataka wachezaji hao kuhakikisha wanarejea na vikombe vingi zaidi ya walivyotwaa mwaka jana mkoani mwanza. “Najua mnalipwa posho lakini juhudi zenu za kujitoa ndio kubwa zaidi kuliko posho mlizolipwa na kwa hilo niwapongeze sana kwani sio kila mtu anaweza kujitoa kiasi hicho” Amesema Prof. Sheikh. Aidha Prof. Sheikh amewataka wachezaji hao kudumisha furaha na amani wakati wote wa michuano hiyo huku akisisitiza umoja kwa wachezaji wote mbali na kila mtu kushiriki mchezo aliofanyia mazoezi. Kwa upande wake katibu wa Michezo Wizarani hapo Bw. Salamala Masoud ames...

DKT. BASHIRU ASHIRIKI UZINDUZI WA MPANGO WA KIMATAIFA WA USTAWI WA UMMA BAHARINI

Picha
Septemba 17, 2026 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameshuhudia uzinduzi wa Mpango wa Kimataifa wa Ustawi wa Umma wa Baharini katika Muongo wa Bahari (Global Initiative for the Ocean Decade Marine Public Welfare Action). Mpango huo unajikita katika uwezeshaji wa kisayansi, uhifadhi wa mazingira, ushiriki wa umma, na uchumi wa bluu ili kutoa matokeo katika usimamizi wa bahari kwa jamii za pwani duniani na kwa vizazi vijavyo. Mpango huo umezinduliwa wakati wa ufunguzi rasmi wa Jukwaa la Dunia la Maendeleo ya Bahari linaloendelea katika Jiji la Qingdao nchini China. Pia Mhe. Balozi Dkt. Bashiru alihutubia Jukwaa la Kimataifa la Maendeleo ya Bahari, ambapo aliwaeleza washiriki kuhusu Dira 2050  pamoja na fursa zilizopo katika Sekta ya Uvuvi.  Amesema Dira2050 ambayo imeanza kutekelezwa Julai Mosi 2026, imeweka msisitizo katika uchumi wa buluu na Uvuvi kama sekta muhimu za ukuaji wa uchumi  kuelea Tanzania ya uchumi wa Kati wa Juu wa Dola trilioni...

MHE. KAMANI AWAONESHA FURSA WAWEKEZAJI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amewataka wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kutumia fursa zilizopo katika Sekta za Mifugo na Uvuvi, akiahidi ushirikiano wa Serikali katika kuhakikisha mazingira ya uwekezaji yanaendelea kuwa rafiki na wezeshi. Mhe. Kamani ametoa kauli hiyo leo, Septemba 17, 2026, jijini Dar es Salaam, wakati wa ziara maalum ya kikazi ya kutembelea wawekezaji wanaofanya shughuli katika Sekta za Mifugo na Uvuvi. Katika ziara hiyo, Naibu Waziri ametembelea Kampuni ya Alphakrust Limited pamoja na Kampuni ya Farmbase, ambapo amepata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali za uzalishaji zinazofanyika katika sekta hizo. Amesema Serikali imedhamiria kushirikiana kwa karibu na Sekta binafsi katika kukuza Sekta za Mifugo na Uvuvi, akieleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Kamani amesema Serikali inaendelea kuweka mifumo inayorahisisha ushirikiano kati ya...

DKT. MADELE AHIMIZA MABADILIKO MRADI WA MAGEUZI YA TASNIA YA MAZIWA

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amewataka watekelezaji wa mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi kuhakikisha hatua ya pili ya utekelezaji wa mradi huo inawagusa wafugaji moja kwa moja. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kikao kazi cha wadau wanaotekeleza mradi huo Dkt. Madele amesema kuwa utekelezaji wa mradi huo kwa mwaka uliopita ulijikita zaidi kwenye maandalizi ya miongozo hivyo ana imani hatua iliyobaki kwa sasa ni kwenda uwandani kwa wafugaji. “Lengo letu hapa ni kuweka alama ya mabadiliko ya Tasnia ya Maziwa kwa kiwango tulichowdka kwenye malengo na kutengeneza mifumo ambayo inahimili mabadiliko ya tabianchi kwa sababu huyu mfugaji tunayemuongelea hayupo hapa Dodoma mjini bali yupo huko Rungwe, Kilolo na kwingineko” Amesema Dkt. Madele. Aidha Dkt. Madele amewataka wataalam hao kupunguza vikao na kuelekeza nguvu uwandani ili kutambua wahusika wa mradi, wanachofanya na wanachopaswa kusaidiwa. Kwa upande wake mratibu w...

TANZANIA YASHIRIKI JUKWAA LA DUNIA LA MAEDELEO YA BAHARI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewasili katika Jiji la Qingdao nchini China kuhudhuria Jukwaa la Kidunia la Maendeleo ya Bahari (Global Ocean Development Forum) linafanyika kuanzia leo Septemba 16 hadi 18, 2026, ambapo ataiwakilisha Tanzania Katika jukwaa hilo kujadili fursa za Bahari Kuu. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru anashiriki Jukwaa hilo baada ya kupata mwaliko kutoka Kituo cha Taifa cha Utafiti wa Bahari Kuu (National Deep - Sea Center), cha Jamhuri ya Watu wa China  lengo ni kuimarisha ushirikiano wa kimataifa na ubadilishanaji wa Maarifa katika sekta ya Bahari na Uchumi wa Buluu. Vile vile, Jukwaa hilo linawakutanisha wawakilishi kutoka Umoja wa Mataifa, Mamlaka ya Masuala ya Bahari za Nchi za Pwani, Viongozi wa Mashirika ya Kimataifa  yanayohusiana na masuala ya bahari , wataalam mashuhuri, wasomi, wajasiriamali na wadau wa sekta ya bahari. Baada ya kuwasili katika Jiji la Qingdao ametembelea na kujionea shughuli zinazofanywa na Taasisi y...

DKT. SAMIA KINARA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA MAGONJWA YA MIFUGO – MHE. KAMANI

Picha
Tanzania imeendelea kuimarisha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Sotoka ya Mbuzi na Kondoo (Peste des Petits Ruminants – PPR), ikiwa ni pamoja na kuandaa Mpango Mkakati wa Kudhibiti na Kutokomeza ugonjwa huo hadi mwaka 2030. Hatua hiyo pia imehusisha kuimarisha ushirikiano wa kikanda na nchi jirani, kwa lengo la kudhibiti na hatimaye kutokomeza PPR, ambao huathiri mifugo na maisha ya wafugaji. Akizungumza wakati wa kuhitimisha Mkutano wa Kikanda wa PPR uliofanyika leo, Septemba 16, 2026, katika ukumbi wa Mikutano wa White Sands Resort jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani, amesema Tanzania imeendelea kuweka nguvu katika mapambano dhidi ya magonjwa ya mifugo. Mhe. Kamani alikuwa Mgeni Rasmi katika mkutano huo, akimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa. Katika hotuba yake, Mhe. Kamani ameushukuru Umoja wa Afrika (AU) kwa kumtambua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kama ki...