Machapisho

MHE. KAMANI AWEKA BAYANA UBORA NA USALAMA WA SAMAKI WA KUFUGWA

Picha
◾Ahamasisha vijana kuchangamkia fursa za Mikopo Serikalini. ◾Awataka vijana kujifunza ujuzi kutoka kwa wawekezaji. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amesema Samaki wanaofugwa kwa njia ya vizimba na mabwawa hawana changamoto yeyote na ni salama na bora kwa matumizi ya chakula. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 13, 2026, Wilayani Sengerema jijini Mwanza, wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani hapo alipomtembelea muwekezaji wa Sekta ya Uvuvi Kampuni ya Ukuzaji Viumbemaji ya Tanzania Zhongzhi Aquaculture Company Limited. Aidha, Mhe. Kamani amesisitiza kuwa chakula kinachotumika kulishia Samaki ufanyiwa uhakiki wa mara kwa mara ili kuzingatia ubora unaohitajika na Wizara. "Samaki hawa wanapimwa kisayansi katika Maabara ya Taifa ya Uvuvi, na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI)  wanafanya utafiti wa ubora wa Vifaranga vya Samaki na kufuatilia ubora wa mazingira ya samaki wanapofugwa" amesema Mhe. Kamani  Aidha, Mhe. Kamani amewataka vijana...

SHAMBA LA MIFUGO SAO HILL KUEKEWA MIFUMO YA UMWAGILIAJI

Picha
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, amesema mpango wa kujenga miundombinu ya maji kwa ajili ya umwagiliaji katika Shamba la Kuzalisha Mifugo la Sao Hill, lililopo Mafinga, mkoani Iringa, unatakiwa kuharakishwa na kuwaagiza wataalamu kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, iliyo chini ya Wizara yake, kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kufanya tathmini kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Hatua hiyo imekuja wakati Mhe. Chongolo, akiwa na mwenyeji wake, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, walipotembelea na kukagua vyanzo vya maji katika Shamba la Mifugo la Serikali la Sao Hill leo, Septemba 12, 2026, ambapo Mawaziri hao wamekubaliana kushirikiana kwa lengo la kuleta mapinduzi katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi. Lengo la kuweka miundombinu ya maji katika shamba hilo ni kuhakikisha wafugaji wanapata malisho ya uhakika na kufanya ufugaji wenye tija, hatua ambayo itasaidia kupunguza tabia ya kuvamia mashamba ya kilimo cha maza...

MHE. KAMANI AITAKA TADB KUENDELEA KUTOA MIKOPO NA KUFANYA UFUATILIAJI WA KINA KWA WANUFAIKA WA MRADI WA BBT

Picha
◾ Aitaka TADB kuanzisha Mfumo wa Taarifa za Wanufaika. ◾ Aitaka TADB kuendelea kutoa mikopo kwa vijana. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, ameitaka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kuendelea kutoa mikopo kwa vijana wanaonufaika wa Mradi wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) Mifugo na Uvuvi, huku ikifanya ufuatiliaji wa kina na tathmini ya miradi inayotekelezwa ili kuhakikisha mikopo hiyo inaleta tija na matokeo yaliyokusudiwa. Mhe. Kamani ametoa agizo hilo leo, Septemba 12, 2026, jijini Mwanza, alipofanya ziara maalum ya kikazi katika Ofisi ya TADB Kanda ya Ziwa, ziara ambayo ni sehemu ya siku tatu za ufuatiliaji wa utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa. Katika ziara hiyo, Mhe. Kamani ameitaka TADB kuhakikisha inapatikana takwimu sahihi kuhusu idadi ya vijana wanaonufaika na Mradi wa BBT pamoja na thamani ya miradi yao, hatua ambayo itasaidia Serikali kupima mafanikio ya programu hiyo na ...

MHE. KAMANI AITAKA TAFIRI KUFANYA TAFITI KUHUSU ATHARI ZA EL NINO KATIKA UZALISHAJI SEKTA YA UVUVI

Picha
◾ Aitaka FETA kujenga vyumba vya ubaridi kuhifadhia samaki. ◾ Awapongeza vijana BBT na kutaka waenndelee kutumia fursa vizuri. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kuendelea kufanya tafiti kuhusu athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño katika uzalishaji sekta ya uvuvi, ili kuwezesha serikali na wadau kuchukua hatua stahiki kukabiliana na changamoto hizo. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 12, 2026, jijini Mwanza, wakati wa ziara maalum ya kikazi ya siku tatu yenye lengo la kufuatilia utekelezaji wa maelekezo yaliyotolewa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, kwa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Nyegezi, pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Mwanza, ziara ambayo pia inalenga kuzungumza na vijana wanaoshiriki katika mpango wa Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) – Uvuvi. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Kamani amesema TAFIRI ina...

WIZARA ZA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI ZAANZA NA MAMBO MANNE YA MASHIRIKIANO

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo imeanza kutekeleza mkakati wa kuimarisha ushirikiano baina ya sekta hizo kwa lengo la kutatua changamoto zinazochangia migogoro kati ya wakulima na wafugaji na kuongeza tija katika uzalishaji. Hatua hiyo imekuja baada ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, na Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo, kufanya ziara leo, Septemba 11, 2026, katika Skimu ya Umwagiliaji ya Bonde la Mkombozi na Mradi wa Visima kwa ajili ya wafugaji katika eneo  la Mboliboli, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa. Akizungumza na wakulima na wafugaji baada ya kukagua miradi hiyo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ametaja mambo manne ya msingi yatakayozingatiwa katika ushirikiano kati ya Wizara hizo.  Mambo hayo ni kujenga mahusiano mema ya wazalishaji wa Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ili kukomesha uhasama na ugomvi baina ya wafugaji na wakulima, eneo la p...

WIZARA YALENGA KUBORESHA KOSAFU ZA SAMAKI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeandaa kikao kazi cha wataalam kujadili maandalizi ya kuanzisha Programu ya Taifa ya Uboreshaji wa Kosafu za Samaki (National Fish Breeding Programme), kwa lengo la kuongeza tija, ubora wa mbegu za samaki na kuhakikisha uendelevu wa sekta ya ukuzaji viumbe maji nchini. Kikao hicho kimefanyika leo tarehe 11 Septemba, 2026, jijini Dodoma, kinawaleta pamoja wataalam kutoka Wizara na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kujadili mikakati, fursa na hatua muhimu za kuanzisha programu hiyo. Akiongoza kikao hicho, Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji, Dkt. Nazael Madalla, amesema kuwa kuanzishwa kwa programu hiyo ni hatua muhimu katika kuimarisha upatikanaji wa kosafu bora za samaki, kuongeza uzalishaji na tija kwa wafugaji, pamoja na kuchochea maendeleo endelevu ya sekta ya ukuzaji viumbe maji nchini.

SERIKALI KUIMARISHA UTEKELEZAJI MPANGO WA KAMPENI ZA CHANJO NA UTAMBUZI WAMIFUGO

Picha
Naibu Katibu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele, ameshiriki kikao cha wataalamu wa Idara ya mifugo na Vituo vya Kanda (ZVCs) Septemba 11, 2026, kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi za wizara hiyo, Mtumba jijini Dodoma. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kujadili na kuimarisha utekelezaji wa mpango wa kampeni za chanjo na utambuzi wa mifugo, ambapo pamoja na mambo mengine, wataalamu hao wamejadili tathmini ya kampeni za chanjo na utambuzi wa mifugo kwa mwaka 2025/2026, mpango wa kampeni hizo kwa mwaka 2026/2027, pamoja na maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa Duniani 2026.