Machapisho

MRADI WA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIANCHI BAHARINI KUTEKELEZWA NCHINI

Picha
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar zinatarajia kutekeleza wa mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa upande wa uvuvi wa bahari utakaofanyika kwa mwaka mmoja na nusu hadi Januari 2028. Akizungumza wakati wa kuzindua mradi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh mbali na kuahidi ushirikiano kwenye utekelezaji wa mradi huo amewataka wavuvi watakaoshiriki kwenye utekelezaji huo kuainisha yale wanayohitaji yaguswe na mradi huo. “Kumekuwa na athari kubwa sana katika sekta ya Uvuvi kuanza kuharibika kwa matumbawe na hata joto la maji na ardhini limekuwa kubwa mpaka upatikanaji wa samaki umepungua hivyo tunaamini mradi huu utakuja kushughulikia na eneo muhimu sana kwa wavuvi” Amesema Prof. Sheikh. Kwa upande wake mwakilishi wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi ambaye pia ni Afisa Mdhamini wa Wizara hiyo Bw. Salim Ahmed Hamza amesema kuwa mradi huo una manufaa makubwa kwa wavuvi waliopo visiwani Zanz...

SERIKALI KUENDELEZA MPANGO WA KUTOKOMEZA MAGONJWA YA MIFUGO

Picha
Serikali imesema itaendelea kuratibu ujenzi, ukarabati na uendelezaji wa miundombinu muhimu ya mifugo nchini, ikiwemo majosho katika Jimbo la Newala Mjini, ili kudhibiti magonjwa yanayoenezwa na kupe na mbung’o. Kauli hiyo imetolewa Bungeni jijini Dodoma leo Agosti 26, 2026 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Kamani wakati akijibu swali la Mhe. Rashid Mohamed Mtima, Mbunge wa Newala Mjini, aliyetaka kujua ni lini Serikali itajenga josho la kuogeshea mifugo katika jimbo hilo. Mhe. Kamani amesema Serikali inatambua umuhimu wa majosho katika kudhibiti magonjwa ya mifugo na kwamba imekuwa ikitekeleza mpango wa ujenzi wa majosho nchini tangu mwaka wa fedha 2021/2022. "Serikali imeendelea kujenga na kukarabati miundombonu ya kuongeshea mifugo ambapo hadi sasa jumla ya majosho 754 yamejengwa nchini kote, kwa gharama ya takribani shilingi bilioni 15.19." alisema Mhe. Kamani. Amesema kwa sasa Serikali imejielekeza katika kutekeleza na kukamilisha miradi ya kimkakati, i...

CHUO CHA MAFUNZO YA MIFUGO KUJENGWA SAMUNGE NGORONGORO

Picha
 Na. Stanley Brayton, WMUV Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Taasisi ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) pamoja na kikundi rika cha jamii ya wafugaji wa kata ya Samunge (Erumasidai) wamekuja na Mkakati mpya wa kujenga Chuo cha Mafunzo ya Mifugo katika Wilaya ya Ngorongoro, mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha elimu na huduma za kitaalam kwa wafugaji katika eneo hilo. Chuo hicho kinatarajiwa kuwa kituo muhimu cha mafunzo kwa wafugaji, vijana na wadau wa sekta ya mifugo, kwa kuwapatia ujuzi wa kisasa kuhusu ufugaji bora, afya ya mifugo, lishe, uzalishaji pamoja na namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili wafugaji. Akizungumza Agosti 24, 2026 Wilayani Ngorongoro jijini Arusha wakati wa ziara yake ya kutembelea wafugaji wa eneo la Ngorongoro, Mtendaji Mkuu wa LITA, Dkt. Pius Lazaro Mwambene, amesema mpango huo unalenga kusogeza elimu ya mifugo karibu na wafugaji na kuhakikisha wanapata maarifa yatakayowawezesha kuongeza tija n...

TDB YAKARIBISHA VIONGOZI WA CHAMA CHA MIFUGO TANZANIA (TSAP), YAIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA TASNIA YA MAZIWA

Picha
Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) imewakaribisha viongozi wa Chama cha Wataalam wa Mifugo Tanzania (TSAP) katika ofisi za Bodi, hatua inayolenga kuimarisha ushirikiano na kubadilishana uzoefu katika kuendeleza Tasnia ya Maziwa nchini. Mkutano huo uliwakutanisha Viongozi hao chini ya  Mwenyekiti wa TSAP, Dkt. Zabron Nziku, pamoja na Msajili wa TDB, Prof. George Msalya, ambapo walijadili masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya Tasnia ya Maziwa na Sekta ya Mifugo kwa ujumla. Akizungumza katika mkutano huo Septemba 24, 2026, Dkt. Zabron Nziku alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya TSAP na TDB, hususani katika maeneo ya kitaalam, utafiti, ubunifu na kubadilishana maarifa yatakayosaidia kuongeza tija na ushindani katika Tasnia ya Maziwa nchini. Kwa upande wake, Prof. George Msalya alieleza kuwa TDB ipo tayari kuendelea kushirikiana na TSAP pamoja na wadau wengine wa Sekta ya Mifugo katika kutafuta na kutekeleza mikakati itakayochochea ukuaji endelevu wa Tasnia ya ...

DKT. BASHIRU AFUNGUA KONGAMANO LA NNE LA KIMATAIFA LA UVUVI NA UKUZAJI VIUMBE MAJI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. BashirAlly Kakurwa, leo Agosti 24, 2026 amefungua Kongamano la Nne la Uvuvi na Ukuzaji Viumbemaji (4tFAR4ViBE) linalowakutanisha Wanasayansi, watafiti na wadau wa uvuvi na wakuzaji viumbe maji na wataalam wa vyuo vikuu kutoka katika Nchi 17 ikiwemo mwenyeji Tanzania kujadili kuhusu maendeleo endelevu ya sekta ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji na kuweka wazi kiwa sekta ya uvuvi zinahitaji sayansi na tafiti ili kuwanufaisha wavuvi. Kongamano hilo linalofanyika kwa siku tatu katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere International Convetion Center (JNICC) Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amewasisitiza wataalam hao kutumia kongamano hilo kujadili kwa kina jinsi ya kutumia sayansi na tafiti kwa ajili ya uvuvi endelevu na ukuzaji viumbe maji. "Shughuli za uvuvi ni sayansi, ni jambo linalohitaji utaalam wa wanasayansi na shughuli nyeti katika usalama wa chakula katika dunia yetu, ndio maanda leo nimekuja kuzindua Kongamano lao la Siku tat...

FETA YAENDESHA MAFUNZO YA UTUNZAJI NA MATENGENEZO YA BOTI NA INJINI ZA UVUVI KATIKA MKOA WA TANGA

Picha
Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) imeendesha mafunzo ya Utunzaji na Matengenezo ya Boti na Injini kwa Maafisa Uvuvi, Wahifadhi wa Maeneo Tengefu na wavuvi  wanufaika wa mkopo wenye masharti nafuu wa boti za kisasa za uvuvi zilizotolewa na Serikali. Mafunzo hayo yamehusisha washiriki 22 ambao ni Maafisa Uvuvi wa Wilaya wanne (4) na wavuvi 15 kutoka Wilaya za Mkinga, Tanga Jiji, Pangani na Muheza, Afisa Uvuvi mmoja (1) kutoka Kituo cha FRP - Tanga na Wahifadhi wawili (2) wa Hifadhi ya Bahari - Tanga. Mafunzo hayo ya siku 4 yalianza tarehe18 hadi 21 Agosti 2026 katika ukumbi wa Costal Zone mkoani Tanga. Akiongea wakati wa kufunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mtendaji Mkuu FETA, Naibu Mkuu wa FETA Bi. Merisia Mparazo amewaasa wahitimu wa mafunzo kutumia ujuzi walioupata kuboresha shughuli zao za uvuvi na kusambaza elimu kwa wavuvi wengine ambao hawakubahatika kupata mafunzo haya. Aidha amesema mafunzo haya yatapunguza gharama za uendeshaji na kuimarisha usalama wa vyombo kwa kuon...

DKT. KIMIREI AFUNGA MAFUNZO YA PILI YA TEKNOLOJIA YA SATELAITI KATIKA SEKTA YA BAHARI NA UVUVI

Picha
Na Herry Kilele – TAFIRI, Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Ismael Kimirei, amefunga Mafunzo ya Pili ya Matumizi ya Teknolojia ya Satelaiti katika Sekta ya Bahari na Uvuvi, yaliyolenga kuimarisha uwezo wa wataalamu katika matumizi ya teknolojia hiyo kwa ajili ya utafiti, ufuatiliaji na usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari na uvuvi. Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika kuanzia Agosti 19 hadi 21, 2026, katika Hoteli ya Southern Sun, Dar es Salaam, kwa ushirikiano kati ya TAFIRI na Taasisi ya Korea ya Sayansi na Teknolojia ya Bahari (KIOST). Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Kimirei amesema rasilimali za bahari na uvuvi zina mchango mkubwa katika uchumi, usalama wa chakula na lishe, ajira, maisha ya wananchi pamoja na maendeleo ya Uchumi wa Buluu nchini. Amesema, Tanzania imeanza utekelezaji wa Dira2050 ambayo inatambua utafiti na matumizi ya sayansi na teknolojia kama nguzo muhimu katika kufikia malengo ya Dira2050...