Machapisho

BI. MEENA AKUTANA NA WATAALAM WA MRADI WA TASFAM KUJADILI MAENDELEO YA MRADI

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena amekutana na wataalam wa Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi wa Baharini na Ufugaji wa Viumbe Maji (TASFAM) kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa ya maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo Kikao hicho kimefanyika leo, Septemba 9, 2026, katika ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, jijini Dodoma, ambapo wataalam wamewasilisha hatua mbalimbali zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo, unaolenga kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za uvuvi wa baharini na kuendeleza sekta ya ufugaji wa viumbe maji nchini.

DKT. BASHIRU AZINDUA PROGRAMU YA KOPA NG’OMBE, LIPA MAZIWA, ATOA ANGALIZO BIMA ZA MIFUGO

Picha
KYERWA, KAGERA  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amezindua Programu ya iMbeju Kilimo – Kopa Ng’ombe, Lipa Maziwa katika Wilaya ya Kyerwa, Mkoani Kagera, akipongeza CRDB Bank Foundation kwa ubunifu unaolenga kuwawezesha wafugaji wadogo kupata rasilimali za uzalishaji, maarifa, huduma za kifedha, bima na masoko. Akizungumza leo Septemba 08, 2026, katika uzinduzi huo, Balozi Dkt. Bashiru amesema programu hiyo ni mfano wa uchumi jumuishi unaomuwezesha mfugaji kutumia ng’ombe kama rasilimali ya kuzalisha maziwa, maziwa kuzalisha kipato na kipato kujenga uwekezaji huku akitaka usimamizi mzuri wa mifumo ya uwezeshaji wa wafugaji ikiwemo Bima ya mifugo. Mhe. Waziri amesema mafanikio ya programu hiyo yatapimwa kwa ongezeko la uzalishaji wa maziwa na kipato cha wafugaji na kutoa angalizo kwa taasisi za benki ikiwemo CRDB Foundation kuhusu usimamizi mzuri wa bima za mifugo ili kuwasaidia wafugaji kuzalisha na kuyafikia malengo ya mradi huo. Kwa upande wake, Mk...

DKT. BASHIRU APOKEA WASILISHO LA TAARIFA YA MRADI WA C-SDTP

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally leo Septemba 05, 2026 amepokea wasilisho la  taarifa ya kamati ya ushauri wa manunuzi ya ng'ombe kwa ajili ya Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP), ambapo baada ya kupokea taarifa hiyo alitoa mapendekezo, maoni na maagizo yake kwa kamati hiyo ili kutekeleza hatua hiyo muhimu inayolenga kuboresha na kuimarisha sekta ya mifugo hususan tasnia ya maziwa nchini. Katika kikao hicho kilichofanyika Hoteli Gerwill jijini Dodoma kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina na Wataalam wengine wa Wizara walioshiriki kikao hicho kwa ajili ya kupokea maelekezo ili kufanyia kazi na kuanza utekelezaji wa mradi huo.

MSIMU WA NYANGUMI 2026 WAFUNGULIWA

Picha
◼️RC MTWARA ASISITIZA UHIFADHI MAENEO TENGEFU Mkuu wa Mkoa Wa Mtwara Mhe. Kanali Donald Msengi amefungua msimu wa nyangumi kwa mwaka 2026 kwenye tukio lililofanyika Septemba 05,2026 kwenye ghuba ya Mnazi iliyopo eneo la Msimbati mkoani humo. Akizungumza katika tukio hilo Kanali Msengi amesema kuwa tukio hilo mbali na kuwavutia wengi kwa kushuhudia mnyama huyo mkubwa kuliko wote ulimwenguni linatumika kutoa elimu ya uhifadhi wa Maeneo Tengefu ili kuendeleza kulinda rasilimali za bahari. “Tunafungua msimu wa Nyangumi 2026 ambao utaendelea hadi mwishoni mwa mwezi Novemba ambapo hii inafungua ukurasa mpya wa wajibu wetu wa kulinda bahari, nyangumi na kutengeneza fursa endelevu za utalii kwa wananchi wetu hapa Mtwara na Tanzania kwa ujumla” Amesema Kanali Msengi. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Hifadhi za bahari na Maeneo Tengefu Dkt. Bonaventure Baya amesema kuwa ghuba hiyo ni miongoni mwa hifadhi tatu na maeneo Tengefu 15 ambapo amebainisha kuwa uhifadhi wa bahari unajumuisha ulinzi...

DKT. BASHIRU AZINDUA BODI YA TAFIRI, ATAKA TAFITI ZA UVUVI ZENYE SULUHISHO

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally, ameitaka Bodi Mpya ya Wakurugenzi ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kuhakikisha tafiti zinazofanywa na Taasisi hiyo zilenge kutatua changamoto halisi zinazoikabili Sekta ya Uvuvi, hususani katika ukuzaji wa viumbe maji na kusisitiza kipaumbele kinapaswa kuwa tafiti za uzalishaji wa mbegu bora na chakula bora cha samaki ili kuongeza uzalishaji.  Akizungumza leo Septemba 05, 2026 katika Hoteli ya Gerwill Jijini Dodoma wakati wa kuzindua Bodi hiyo, Balozi Dkt. Bashiru ameitaka TAFIRI kuanzisha na kusimamia kwa uthabiti programu ya kuboresha mbari za samaki (breeding program), pamoja na kufanya tafiti na uhaulishaji wa teknolojia zinazotumika katika ufugaji wa samaki kwa vizimba katika maji baridi na baharini. “Bodi hii iisimamie TAFIRI kufanya tafiti zenye suluhisho katika Sekta ya Uvuvi,  kusimamia sheria na utawala bora, ili Taasisi iweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na kutoa mchango mkubwa katika maend...

NYANGUMI-FURSA MPYA UCHUMI WA BULUU

Picha
Kila ifikapo kati ya mwezi Julai hadi Novemba Tanzania hufanya tamasha la Nyangumi ambalo msingi wake mkuu ulitokana na tabia ya mnyama huyo kuhamia ukanda wa Hifadhi za bahari na Maeneo Tengefu wa MnaziBay uliopo Msimbati mkoani Mtwara ambao kwa kipindi hicho huwa na asili ya joto. Katika kipindi hicho Nyangumi ambaye mbali na kuwa na sifa ya kuwa mnyama mkubwa kuliko wote ulimwenguni, anakadiriwa kutembea umbali wa takribani kilomita 8,000 katika kipindi chote cha Mwaka huweka makazi yake katika ukanda huo kwa malengo makuu ambayo ni kutafuta chakula na mazingira salama ya kuzaa na kulea watoto wake. Uwepo wa tukio hilo sio tu unathibitisha utajiri wa maliasili zinazopatikana nchini bali ni alama ya kudumu inayowakumbusha wananchi wa Mtwara na wengine wote wanaofanya shughuli zao za uvuvi kwenye bahari ya hindi kuendelea kutunza mazingira na kuhifadhi mazalia ya asili ya maeneo hayo ili kuvutia viumbe maji wengi zaidi kufika na kuweka makazi yao nchini katika siku za usoni. Kwa mujib...

TAMASHA LA NYANGUMI LAFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI MTWARA

Picha
Tamasha la Nyangumi linalofanyika mkoani kuanzia Septemba 02-05 mkoani Mtwara limeanza kufungua fursa za kiuchumi ambapo wadau mbalimbali wa sekta binafsi wameonesha nia ya kuchangamkia fursa hizo. Hayo yamebainika Septemba 04,2026  wakati wa kongamano lililofanyika kando ya tamasha hilo ambalo limekutanisha wadau hao kutoka mashirika yasiyo na kiserikali, Taasisi za kifedha,Vyombo vya habari na wawekezaji binafsi ambapo wameainisha fursa kadhaa zinazoambatana na uwepo wa Tamasha la nyangumi ikiwa ni pamoja na ajira kwa vijana wenye vyombo vya usafiri hususan mitumbwi inayopelekea watalii kushuhudia tukio hilo na nyumba za kulala wageni hao.