DKT. NCHIMBI AHIMIZA UBORA WA MIFUGO NA MASOKO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuendelea kuwasisitiza wafugaji kuboresha Mifugo yao ili kupanua wigo wa soko la mazao ya Mifugo ndani na nje ya nchi. Balozi Dkt. Nchimbi ameyasema hayo Agosti 03,2026 wakati wa ziara yake kwenye mnada wa Mifugo uliopo kwenye viwanja vya maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma. “Kwa mara ya kwanza nimejua kuwa na Mifugo nayo imefurahi hivyo nawashukuru kwa kazi kubwa mliyofanya na kwenye maeneo haya ya mifugo changamoto kubwa ni ubora wa Mifugo yenyewe na masoko kwa hiyo nadhani mnapojielekeza kwenye maeneo hayo mawili mnasaidia sana taifa letu”, Amesema Balozi Dkt. Nchimbi. Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani amesema kuwa moja ya vitu ambavyo Wizara yake imejielekeza kwa sasa ni upatikanaji wa mbegu bora za Mifugo ambazo anaamini zitakuwa na tija kwa mfugaji ambapo zitawafanya kuwa na mi...