Machapisho

UVUVI HARAMU KUTAFUTIWA MWAROBAINI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani amewataka watendaji wa Wizara kuja na mwarobaini ambapo utakuwa ni tiba katika kudhibiti uvuvi haramu, na amewataka watendaji hao kuangalia mifumo yao kama inafanya kazi vizuri na kuboresha pale ambapo panahitaji kuboreshwa ili uvuvi haramu ufike kikomo. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 14, 2026, jijini Mwanza, wakati wa kupokea wasilisho la andiko dhana la kudhibiti Uvuvi haramu, andiko ambao litasaidia katika kutokomeza tatizo hilo sugu, andiko ambalo limeandaliwa na Mkufunzi wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP) Mwanza, Bw. Jackson Bulili pamoja na Mtaalam wa mambo ya Teknolojia kutoka Kampuni ya Affordable Computes and Technology for Tanzania (ACTT) Mwanza, Bw. Amos Zacharia. "Uandishi wa andiko hili linaonesha fika kuwa Wizara inaungwa mkono na wananchi katika kutokomeza Uvuvi haramu" amesema Mhe. Kamani  Aidha, Mhe. Kamani amesema hii inaonesha Wizara itapata namna nyingine ya kupambana na...

WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI MKOANI KIGOMA WAMETAKIWA KWENDA KUZALISHA SAMAKI

Picha
Rai hiyo imetolewa 14 Septemba, 2026 na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma Bw. Hassan Rugwa Wakati akifunga mafunzo ya wiki nne kwa washiriki 57 wa mafunzo ya ufugaji samaki yaliyoendeshwa  Mkoani Kigoma na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Kigoma kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Ubegiji Enabel kupitia mradi wa wezesha binti. Bw. Rugwa amesema mafunzo waliopata washiriki hawa yawe chachu kwa wao kwenda kufanya shughui za uzalishaji, ufugaji na uchakataji wa samaki kwani Taifa linawategemea waweze kuongeza tija katika sekta ya ufugaji samaki. Naye Mtendaji Mkuu wa FETA Dkt. Semvua Mzighani ambao ndio walioendesha mafunzo hayo amesema kuwa mafunzo haya ni kipaumbele cha Taifa kwa hivi sasa kwani serikali inaweka mkazo katika ukuzaji wa viumbe maji na ufugaji wa samaki. Kwa upande wake Meneja wa FETA kampasi ya Kigoma Bw August Shirima amesema Mafunzo haya yalianza tarehe 17 Agosti mpaka tarehe 11 September 2026 ambapo washiriki kutoka Halmashauri ya kigoma vij...

MHE. KAMANI AKUTANA NA MENEJA TADB KANDA YA ZIWA KUJADILI UWEZESHAJI WA MIKOPO KWA VIJANA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo Septemba 14, 2026 Jijini Mwanza, amekutana na Meneja wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) Kanda ya Ziwa, Bw. Ally Janja, katika Ofisi za Benki hiyo na kujadiliana kuhusu Utoaji wa mikopo kwa vijana, mikopo ambayo inatolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kuwezesha vijana kufanya shughuli za uzalishaji katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi.

MHE. KAMANI AWAITA WAWEKEZAJI KUWEKEZA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
◾Ataka wawekezaji kuzingatia ustawi wa wafanyakazi wao.  ◾Ataka wataalam kutatua changamoto za uhaba wa chakula cha samaki na mifugo. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani amewataka wawekezaji nchini kuendelea kuwekeza katika sekta ya mifugo na uvuvi, huku wakizingatia ustawi na usalama wa wafanyakazi wao pamoja na kuhakikisha wanazalisha kwa tija. Mhe. Kamani ameyasema hayo leo, Septemba 14, 2026, wilayani Magu mkoani Mwanza, wakati wa ziara maalum ya kikazi ya kuwatembelea wawekezaji katika tasnia yaukuzaji viumbemaji, ikiwemo Tangreen Farming Company na M/S ROFI Farming Company Limited, kwa lengo la kujionea shughuli za uzalishaji zinazofanyika katika sekta hiyo. Amesema uwekezaji katika sekta ya mifugo na uvuvi una umuhimu mkubwa katika kuongeza uzalishaji wa chakula, kutoa ajira na kukuza uchumi, hivyo wawekezaji wanapaswa kuhakikisha wafanyakazi wanapata mazingira salama na stahiki za msingi katika maeneo yao ya kazi. Aidha, Mhe. Kamani amewataka wananchi...

DKT. BASHIRU AITAKA LITA KUENDANA NA MABADILIKO YA SEKTA YA MIFUGO

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameitaka Wakala ya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) kuendelea kuboresha mafunzo na kutoa wataalamu wenye uwezo wa kukabiliana na mahitaji na mabadiliko yanayoendelea katika sekta ya mifugo nchini. Waziri Dkt. Bashiru ameyasema hayo leo Septemba 14, 2026 alipotembelea Kampasi ya LITA Temeke, Dar es Salaam, ambapo amesisitiza umuhimu wa taasisi hiyo kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta ya mifugo, hususan kupitia mafunzo, tafiti, mawazo na ushauri wa kitaalamu, akiitaka LITA kutoa mawazo na mapendekezo yatakayosaidia katika maboresho ya sera za mifugo ili ziendane na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050. Amesema sekta ya mifugo kwa sasa ina umuhimu wa kipekee kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu, kukua kwa mahitaji ya protini, kufunguka kwa masoko pamoja na mabadiliko ya ufugaji kuelekea mifumo ya kisasa, hivyo LITA inapaswa kuendana na mabadiliko hayo kwa kutoa huduma na mafunzo yenye ubora. Wazi...

FETA YAZINDUA MAFUNZO YA MUDA MFUPI JUU YA UONGOZI WA JAMII KATIKA UHIFADHI WA RASILIMALI ZA BAHARI NA PWANI

Picha
Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Mbegani leo 14 Septemba, 2026 imezindua mafunzo ya muda mfupi ya uongozi wa jamii katika uhifadhi wa rasilimali za Bahari na Pwani, yanayolenga kuwajengea uwezo viongozi wa jamii 20 kutoka Tanga na Pemba. Mafunzo hayo yalioanza tarehe 14 hadi 27 Septemba 2026, yanafadhiliwa na shirika la IUCN Tanzania ambapo yatahusisha maeneo muhimu yakiwemo uongozi, utawala bora, usimamizi wa fedha, mawasiliano na ushirikiano wa wadau, sera na sheria, utatuzi wa migogoro, utetezi wa maslahi ya jamii na uibuaji wa shughuli mbadala za kuongeza kipato. Akizungumza wakati wa uzinduzi, Capt. Nicas Mbandi aliyemwakilisha Naibu Mkuu wa FETA, amesisitiza umuhimu wa kuwa na viongozi wenye maarifa na ujuzi wa kusimamia rasilimali za Bahari kwa kuunganisha uhifadhi na maendeleo ya jamii. Aidha amesema mafunzo haya yanachangia utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kwa kuwekeza katika watu wenye ujuzi na uwezo wa kuongoza, pamoja na kukuza uchumi wa b...

MHE. KAMANI AKUTANA NA MKUU WA MKOA WA MWANZA KUJADILI MAENDELEO SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo Septemba 14, 2026 amewasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. CP. Salum Rashid Hamduni. Mazungumzo ambayo yalijikita katika kuboresha Sekta za Mifugo na Uvuvi ili kuongeza tija katika shughuli za uzalishaji wa sekta hizo, hususan suala ya uwezeshaji wa mikopo kwa vijana kwenye sekta hizo pamoja na uwekezaji na udhibiti wa shughuli za uvuvi haramu.