Machapisho

WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MIRADI YAO

Picha
Na, Fausta Njelekela  Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Bw. Salum Khalfan Mterera, leo Agosti 3, 2026, amefungua mafunzo kwa wanufaika wa Programu ya Uwezeshaji Vijana kupitia Miradi ya Kiuchumi katika Sekta za Mifugo na Uvuvi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Bunda, mkoani Mara. Akifungua mafunzo hayo, Bw. Mterera amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwapatia mikopo yenye riba nafuu ili kuwajengea uwezo wa kuanzisha na kuendeleza miradi ya uzalishaji, uongezaji thamani wa mazao ya mifugo na uvuvi pamoja na huduma katika minyororo ya thamani ya sekta hizo, na amesema hatua hiyo inalenga kuongeza ajira, kipato cha wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa. "Mkoa wa Mara umenufaika na jumla ya miradi 272 yenye thamani ya shilingi bilioni 1.77, ikijumuisha ufugaji wa kuku, mbuzi, kondoo, nguruwe pamoja na miradi ya zana za uvuvi." Aidha, amewataka wanufaika kusimamia kwa weledi miradi hiyo, kuzingatia matumizi...

TUMEFANIKIWA UPANDE WA MALISHO YA MIFUGO, UFUGAJI SAMAKI-BALOZI KHAMIS

Picha
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Musa Omar amesema kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa kwenye eneo la uzalishaji wa malisho ya mifugo na ufugaji wa samaki ukilinganisha na hali ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita. Balozi Omar amebainisha hayo Agosti 02,2026 wakati wa ziara yake kwenye Taasisi za Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI), Taasisi ya Mafunzo ya Mifugo (LITA),mashamba ya malisho ya Mifugo na mabwawa ya kufugia samaki yaliyopo eneo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijiji Dodoma. “Kwenye malisho kuna mafanikio makubwa kwa sababu tumekuja na mbegu mpya mfano haya majani ya juncao ambayo asili yake ni China na tumeambiwa hapa unaweza kuzalisha mpaka tani 60 katika ekari moja tu na hii inaweza kuwa ni suluhu kubwa ya changamoto ya wakulima na wafugaji” Amesema Mhe. Balozi Omar. Akizungumzia upande wa ufugaji wa samaki Mhe. Balozi Omar amesema kuwa eneo hilo limeonekana kuwa na tija...

DKT. NCHEMBA AZINDUA MKAKATI WA MIAKA 10 UFUGAJI WA KUKU NCHINI

Picha
◼️KUKU WA SINGIDA, DODOMA SASA KUTAMBULIKA KAMA KUKU WA KANDA YA KATI. ◼️ATAKA TEKNOLOJIA YA UFUGAJI WA SAMAKI KWENYE MABWAWA KUWAFIKIA WANANCHI Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amezindua mkakati wa miaka 10 wa ufugaji wa kuku ambao umelenga kubadilisha tasnia ya kuku nchini na kuifanya kuwa shindani, jumuishi na endelevu ili kuchangia usalama wa chakula, lishe, ajira, kipato, ukuaji wa uchumi na biashara. Dkt. Nchemba amezindua mkakati huo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane iliyofanyika Agosti 1,2026 kwenye viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma. “Kuku ni moja ya zao tambulisho kwa mikoa ya kanda ya kati na kaya mbalimbali, na kuzinduliwa kwa Mkakati huu kwa Serikali ni jambo la faraja ambalo litaenda kuleta mageuzi katika Sekta hiyo ndogo ya kuku na kuongeza uzalishaji wenye tija.”amesema Mhe. Dkt. Nchemba. Aidha Dkt. Nchemba ameielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha utekelez...

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATEMBELEA MAMLAKA YA KUSIMAMIA UVUVI WA BAHARI KUU

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo ametembelea Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) kwa lengo la kujionea utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo pamoja na kuzungumza na viongozi na watumishi kuhusu maendeleo ya sekta ya uvuvi wa bahari kuu. Katika ziara hiyo, Mhe. Kamani alipokea taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na mamlaka, ikiwemo usimamizi wa rasilimali za uvuvi wa bahari kuu, utoaji wa leseni, ufuatiliaji wa shughuli za uvuvi, na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali za bahari. Akizungumza na viongozi na watumishi wa mamlaka hiyo, Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa kuendelea kusimamia rasilimali za bahari kwa weledi, uwazi na ufanisi ili kuongeza mchango wa sekta ya uvuvi katika ukuaji wa uchumi wa taifa, kuongeza ajira na kuimarisha usalama wa chakula. Aidha, aliwahimiza watumishi kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta hiyo katika kupambana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa pamo...

DKT. NCHEMBA KUZINDUA MAONESHO YA NANE NANE 2026 AGOSTI MOSI

Picha
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo  ametembelea na kukagua maandalizi kuelekea Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane kwa Mwaka 2026, na kueleza kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba. Mhe. Chongolo ameeleza kuwa uzinduzi huo utafanyika kesho Agosti Mosi 2026 katika Viwanja vya Maonesho ya Kimataifa vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma. Aidha, katika ziara yake ya ukaguzi wa Maandalizi hayo, Mhe. Chongolo ameeleza kufurahishwa  jinsi Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ilivyojipanga kwa kutoa huduma ya nyama choma na akaeleza kuwa kutakuwa na shughuli mbalimbali za maonesho katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi ambapo ameeleza kuwa  Paredi la Mifugo linaloratibiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi llitafanyika Agosti 5, Mwaka huu. Vilevile, alieleza kuwa baada ya uzinduzi wa maonesho hayo, serikali, wadau, taasisi wataendelea kutoa huduma mbali kwa wananchi wakati na baada maonesho ...

SERIKALI YAHIMIZA MATUMIZI BORA YA MIKOPO KWA WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI

Picha
Jumla ya vijana 69 kutoka Mkoa wa Lindi katika wilaya za Kilwa, Mtama na Ruangwa wanaonufaika na Programu ya Uwezeshaji wa Vijana Kiuchumi katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kusimamia miradi yao kibiashara na kuhakikisha mikopo waliyopewa inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Mafunzo hayo yamefanyika Julai 30, 2026, katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, yakiratibiwa na wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, pamoja na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Kupitia mafunzo hayo, wanufaika wamepatiwa maarifa kuhusu kanuni bora za ufugaji wa kuku, kondoo, nguruwe na mbuzi, sambamba na elimu ya ujasiriamali, usimamizi wa biashara, stadi za maisha na mbinu za kuongeza tija na mafanikio katika miradi yao. Akifungua mafunzo hayo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Ndg. Mwinjuma Mkungu amewataka wanufaika kutumia fursa hiyo kwa ufanisi ili kujijengea msingi imara wa kiuchumi. Amesisitiza umuhimu wa vijan...

WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI WAPATIWA MAFUNZO DODOMA

Picha
Na. Martha Mbena. Wanufaika wa Uwezeshaji wa Programu ya Vijana kiuchumi katika Sekta za Mifugo na Uvuvi wapatao 45 kwa mkoa wa Dodoma wamepatiwa mafunzo kwa lengo la kusimamia miradi yao kwa ufanisi, kutumia mikopo kwa malengo yaliyokusudiwa na kuongeza ajira pamoja na uzalishaji katika sekta hizo. Mafunzo hayo yametolewa Julai 30.2026 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na timu ya wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo  wanufaika hao wamepata ujuzi wa namna bora ya ufugaji wa Nguruwe, Ufugaji wa kuku, Ufugaji wa Kondoo, utengenezaji wa Malisho ya Mifugo na mambo Muhimu ya kuzingatia kabla ya kuanza uwekezaji.  Daktari wa Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Pius Bunga. Ambaye pia ni muwezeshaji wa mafunzo hayo, Amewapongeza wanufaika wa mikopo hiyo na kuwasisitiza kuzingatia malengo ya kuanzishwa kwa programu za ufugaji na kuweka nidhamu ya katika usimamizi wa fedha watakazokopeshwa ili kuweza kujiongezea kipato na kukuza uchumi wa Nchi. “Hii...