Machapisho

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI ATEMBELEA MAMLAKA YA KUSIMAMIA UVUVI WA BAHARI KUU

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng'wasi Damas Kamani leo ametembelea Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA) kwa lengo la kujionea utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo pamoja na kuzungumza na viongozi na watumishi kuhusu maendeleo ya sekta ya uvuvi wa bahari kuu. Katika ziara hiyo, Mhe. Kamani alipokea taarifa kuhusu shughuli zinazotekelezwa na mamlaka, ikiwemo usimamizi wa rasilimali za uvuvi wa bahari kuu, utoaji wa leseni, ufuatiliaji wa shughuli za uvuvi, na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali za bahari. Akizungumza na viongozi na watumishi wa mamlaka hiyo, Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa kuendelea kusimamia rasilimali za bahari kwa weledi, uwazi na ufanisi ili kuongeza mchango wa sekta ya uvuvi katika ukuaji wa uchumi wa taifa, kuongeza ajira na kuimarisha usalama wa chakula. Aidha, aliwahimiza watumishi kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta hiyo katika kupambana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa pamo...

DKT. NCHEMBA KUZINDUA MAONESHO YA NANE NANE 2026 AGOSTI MOSI

Picha
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo  ametembelea na kukagua maandalizi kuelekea Maonesho ya Kimataifa ya Nane Nane kwa Mwaka 2026, na kueleza kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba. Mhe. Chongolo ameeleza kuwa uzinduzi huo utafanyika kesho Agosti Mosi 2026 katika Viwanja vya Maonesho ya Kimataifa vya Dkt. John Malecela jijini Dodoma. Aidha, katika ziara yake ya ukaguzi wa Maandalizi hayo, Mhe. Chongolo ameeleza kufurahishwa  jinsi Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ilivyojipanga kwa kutoa huduma ya nyama choma na akaeleza kuwa kutakuwa na shughuli mbalimbali za maonesho katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi ambapo ameeleza kuwa  Paredi la Mifugo linaloratibiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi llitafanyika Agosti 5, Mwaka huu. Vilevile, alieleza kuwa baada ya uzinduzi wa maonesho hayo, serikali, wadau, taasisi wataendelea kutoa huduma mbali kwa wananchi wakati na baada maonesho ...

SERIKALI YAHIMIZA MATUMIZI BORA YA MIKOPO KWA WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI

Picha
Jumla ya vijana 69 kutoka Mkoa wa Lindi katika wilaya za Kilwa, Mtama na Ruangwa wanaonufaika na Programu ya Uwezeshaji wa Vijana Kiuchumi katika Sekta ya Mifugo na Uvuvi wamepatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kusimamia miradi yao kibiashara na kuhakikisha mikopo waliyopewa inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Mafunzo hayo yamefanyika Julai 30, 2026, katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, yakiratibiwa na wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, pamoja na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). Kupitia mafunzo hayo, wanufaika wamepatiwa maarifa kuhusu kanuni bora za ufugaji wa kuku, kondoo, nguruwe na mbuzi, sambamba na elimu ya ujasiriamali, usimamizi wa biashara, stadi za maisha na mbinu za kuongeza tija na mafanikio katika miradi yao. Akifungua mafunzo hayo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Ndg. Mwinjuma Mkungu amewataka wanufaika kutumia fursa hiyo kwa ufanisi ili kujijengea msingi imara wa kiuchumi. Amesisitiza umuhimu wa vijan...

WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI WAPATIWA MAFUNZO DODOMA

Picha
Na. Martha Mbena. Wanufaika wa Uwezeshaji wa Programu ya Vijana kiuchumi katika Sekta za Mifugo na Uvuvi wapatao 45 kwa mkoa wa Dodoma wamepatiwa mafunzo kwa lengo la kusimamia miradi yao kwa ufanisi, kutumia mikopo kwa malengo yaliyokusudiwa na kuongeza ajira pamoja na uzalishaji katika sekta hizo. Mafunzo hayo yametolewa Julai 30.2026 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na timu ya wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo  wanufaika hao wamepata ujuzi wa namna bora ya ufugaji wa Nguruwe, Ufugaji wa kuku, Ufugaji wa Kondoo, utengenezaji wa Malisho ya Mifugo na mambo Muhimu ya kuzingatia kabla ya kuanza uwekezaji.  Daktari wa Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Pius Bunga. Ambaye pia ni muwezeshaji wa mafunzo hayo, Amewapongeza wanufaika wa mikopo hiyo na kuwasisitiza kuzingatia malengo ya kuanzishwa kwa programu za ufugaji na kuweka nidhamu ya katika usimamizi wa fedha watakazokopeshwa ili kuweza kujiongezea kipato na kukuza uchumi wa Nchi. “Hii...

PROF. SHEIKH AONGOZA KIKAO CHA UZINDUZI WA UTAFITI WA KUANDAA MRADI WA UCHUMI WA BULUU

Picha
Naibu Katibu Mkuu, Prof. Mohamed Sheikh, leo Julai 28, 2026, ameongoza kikao cha uzinduzi wa utafiti wa awali utakaoweka msingi wa kuandaliwa kwa andiko la Mradi wa Uchumi wa Buluu unaojulikana kama "Leading an Ecological and Inclusive Ocean-Based Economic Growth in the United Republic of Tanzania". Lengo la kikao hicho lilikuwa kujadili utekelezaji wa utafiti huo, kubainisha majukumu ya wadau mbalimbali na kukusanya maoni na mapendekezo yatakayosaidia kufanikisha uandaaji wa andiko la mradi. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Prof. Sheikh alisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa taasisi zote zinazoshiriki katika kuhakikisha utafiti huo unafanyika kwa ufanisi na unazalisha matokeo yatakayochangia maendeleo ya uchumi wa buluu nchini kwa kuzingatia matumizi endelevu ya rasilimali za bahari na mazingira yake. Kikao hicho kilihudhuriwa na wawakilishi kutoka Shirika la Maendeleo la Ufaransa (Agence Française de Développement – AFD), wataalamu washauri kutoka BRLi, pamoja na wawakilis...

DKT. BASHIRU APIGA MARUFUKU UUZAJI HOLELA WA NYAMA, MACHINJIO BUBU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameiagiza Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) kuzifunga mara moja bucha zinazouza kiholela nyama na mazao yake bila kuzingatia sheria na kueleza kwamba hali hiyo inaweza kuathiri afya ya walaji. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru  amesema hayo leo Julai 27, 2026 baada kuelezwa kuwepo kwa changamoto hiyo kutoka kwa wachinjaji wa mifugo katika machijio ya Vingunguti yaliyopo Halmashauri ya Jijini Dar es Salaam. Amesema kumekuwa na uholela wa uchinjaji wa mifugo hususan mbuzi na Kondoo hali inayorudisha nyuma jitihada za serikali ambayo imewekeza Shilingi Bilioni 19.5 kwa ajili ya machinjio ya kisasa. Aidha, amewaagiza viongozi wa Halmashauri hiyo kukamilisha haraka mchakato wa kupata wawekezaji kwa ajili ya kuendesha machinjio hayo kwa kukidhi taritibu na vigenzo vinavyokubaliwa na serikali kuhusu uendeshaji vinginevyo machinjio hayo itafungwa. Bodi ya Nyama Kamateni wote wanaouza nyama kiholela ni hatari kiafya kuuza nyama na mazao yak...

DKT. BASHIRU AKUTANA NA GATSBY AFRICA KUJADILI MKAKATI WA UZALISHAJI WA CHAKULA CHA SAMAKI NA KUKU

Picha
Serikali imeendelea kuimarisha ushirikiano na wadau wa maendeleo katika kuongeza tija ya sekta za mifugo na uvuvi, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kukuza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuongeza mchango wa sekta hizo katika uchumi wa Taifa. Katika hatua hiyo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, leo Julai 24, 2026 amekutana na timu ya wataalam kutoka Taasisi ya Gatsby Africa katika Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma, na kujadiliana kuhusu uwekezaji katika ukuzaji wa viumbemaji na kuongeza upatikanaji wa chakula cha samaki na kuku. Mazungumzo hayo yalijikita katika namna Serikali na Gatsby Africa zinavyoweza kushirikiana kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi kupitia uwekezaji katika uzalishaji wa malighafi za chakula cha mifugo, matumizi ya teknolojia za kisasa na kuimarisha mnyororo wa thamani wa uzalishaji. Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Bashiru alisema Serikali inaendelea kuweka mazingira weze...