Machapisho

DKT. MWIGULU AHIMIZA UFUGAJI WA KISASA KUONGEZA UZALISHAJI NA TIJA

Picha
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amewahimiza wataalam na wadau sekta ya mifugo nchini kuendelea kutoa  mafunzo ya ufugaji bora na wa kisasa  kwa wananchi wote ili kuwa na tija katika uzalishaji katika sekta ya mifugo. Mhe. Dkt. Nchemba amesema hayo mara baada ya kukagua shughuli za ufugaji  katika Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Mashariki leo Agosti 04, 2026 ambapo kwa kanda hiyo maonesho hayo yanafanyika Mkoani Morogoro. Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Nchemba alivutiwa na ng'ombe aliyefugwa na Magereza ya mkoani Morogoro ambaye anauwezo wa  kuzalisha Lita 30 za maziwa kwa siku na kuielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na taasisi hiyo kuendelea kutoa elimu ya uzalishaji wenye tija kwa wananchi kupitia mafunzo na ugani. Aidha, Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Nchemba alisema ili kukabiliana na changamoto za uhaba wa maeneo kwa ajili ya ufugaji ni muhimu wadau wa sekta ya mifugo kujifunza mbinu za ufugaji wa kisasa wenye tija n...

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AIPONGEZA FETA KWA KUSIMAMIA VIZURI MRADI WA BBT UVUVI

Picha
Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Ng'wasi Kamani ameipongeza Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kwa kusimamia vizuri mradi wa BBT Uvuvi ambapo kwa hivi sasa vijana waliopatiwa mikopo isiyo na riba wanaendelea na ufugaji samaki kwenye vizimba katika Ziwa Victoria. Mhe.Kamani ametoa pongezi hizo alipotembelea banda la FETA kwenye maonesho ya nanenane kitaifa yanayoendelea katika viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma na kutaka kupatiwa maendeleo ya mradi wa vijana wa BBT Uvuvi.  Akitoa maelezo kwa Mhe. Kamani, Mtendaji Mkuu wa FETA Dkt. Semvua Mzighani amesema hadi sasa FETA imeshapeleka vifaranga kwa asilimia 82 kwa vijana 168 wa Mikoa ya Mwanza, Kagera na Mara, vijana wanaendelea vizuri na mradi ambapo wale waliopo Mwanza wanatarajia kuanza kuvuna samaki mwezi Oktoba mwaka huu. "Hivi sasa samaki waliopo kwenye shamba la Nyegezi, Mwanza wamefikisha uzito wa wastani wa gramu 300 na wanatarajiwa kuanza kuvunwa mwezi Oktoba" alisema Dk...

DKT. NCHIMBI AHIMIZA UBORA WA MIFUGO NA MASOKO

Picha
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuendelea kuwasisitiza wafugaji kuboresha Mifugo yao ili kupanua wigo wa soko la mazao ya Mifugo ndani na nje ya nchi. Balozi Dkt. Nchimbi ameyasema hayo Agosti 03,2026 wakati wa ziara yake kwenye mnada wa Mifugo uliopo kwenye viwanja vya maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma. “Kwa mara ya kwanza nimejua kuwa na Mifugo nayo imefurahi hivyo nawashukuru kwa kazi kubwa mliyofanya na kwenye maeneo haya ya mifugo changamoto kubwa ni ubora wa Mifugo yenyewe na masoko kwa hiyo nadhani mnapojielekeza kwenye maeneo hayo mawili mnasaidia sana taifa letu”, Amesema Balozi Dkt. Nchimbi. Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani amesema kuwa moja ya vitu ambavyo Wizara yake imejielekeza kwa sasa ni upatikanaji wa mbegu bora za Mifugo ambazo anaamini zitakuwa na tija kwa mfugaji ambapo zitawafanya kuwa na mi...

VIJANA 85 RUVUMA WAPATIWA MAFUNZO YA UWEKEZAJI NA UFUGAJI WA KISASA

Picha
 Vijana  kutoka halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Ruvuma wamepatiwa mafunzo ya uwekezaji na ufugaji wa kisasa kupitia Programu ya Uwezeshaji Vijana Kiuchumi, inayoratibiwa na Serikali kupitia  Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Agosti 3, 2026. Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Songea, Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Afisa Uvuvi wa Mkoa, Bw. Basil Amuli, amewataka vijana kutumia kikamilifu mafunzo na mikopo watakayopata kwa kuanzisha na kuendesha miradi yenye tija itakayowawezesha kujiongezea kipato na kujiajiri. "Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kupitia programu mbalimbali za uwezeshaji kiuchumi, hivyo ni wajibu wa wanufaika kuhakikisha wanatumia fursa hizo kwa malengo yaliyokusudiwa ili kupata matokeo chanya na kuwa mfano kwa vijana wengine." amesema Bw. Amuli Aidha, amewahimiza washiriki kutekeleza kwa vitendo maarifa watakayoyapata wakati wa mafunzo hayo ili kuongeza uzalishaji, kuboresha mai...

WANUFAIKA WA PROGRAMU YA UWEZESHAJI VIJANA KIUCHUMI SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI WATAKIWA KUSIMAMIA VYEMA MIRADI YAO

Picha
Na, Fausta Njelekela  Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda Bw. Salum Khalfan Mterera, leo Agosti 3, 2026, amefungua mafunzo kwa wanufaika wa Programu ya Uwezeshaji Vijana kupitia Miradi ya Kiuchumi katika Sekta za Mifugo na Uvuvi yaliyofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Bunda, mkoani Mara. Akifungua mafunzo hayo, Bw. Mterera amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwapatia mikopo yenye riba nafuu ili kuwajengea uwezo wa kuanzisha na kuendeleza miradi ya uzalishaji, uongezaji thamani wa mazao ya mifugo na uvuvi pamoja na huduma katika minyororo ya thamani ya sekta hizo, na amesema hatua hiyo inalenga kuongeza ajira, kipato cha wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa. "Mkoa wa Mara umenufaika na jumla ya miradi 272 yenye thamani ya shilingi bilioni 1.77, ikijumuisha ufugaji wa kuku, mbuzi, kondoo, nguruwe pamoja na miradi ya zana za uvuvi." Aidha, amewataka wanufaika kusimamia kwa weledi miradi hiyo, kuzingatia matumizi...

TUMEFANIKIWA UPANDE WA MALISHO YA MIFUGO, UFUGAJI SAMAKI-BALOZI KHAMIS

Picha
Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Musa Omar amesema kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa kwenye eneo la uzalishaji wa malisho ya mifugo na ufugaji wa samaki ukilinganisha na hali ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita. Balozi Omar amebainisha hayo Agosti 02,2026 wakati wa ziara yake kwenye Taasisi za Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI), Taasisi ya Mafunzo ya Mifugo (LITA),mashamba ya malisho ya Mifugo na mabwawa ya kufugia samaki yaliyopo eneo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijiji Dodoma. “Kwenye malisho kuna mafanikio makubwa kwa sababu tumekuja na mbegu mpya mfano haya majani ya juncao ambayo asili yake ni China na tumeambiwa hapa unaweza kuzalisha mpaka tani 60 katika ekari moja tu na hii inaweza kuwa ni suluhu kubwa ya changamoto ya wakulima na wafugaji” Amesema Mhe. Balozi Omar. Akizungumzia upande wa ufugaji wa samaki Mhe. Balozi Omar amesema kuwa eneo hilo limeonekana kuwa na tija...

DKT. NCHEMBA AZINDUA MKAKATI WA MIAKA 10 UFUGAJI WA KUKU NCHINI

Picha
◼️KUKU WA SINGIDA, DODOMA SASA KUTAMBULIKA KAMA KUKU WA KANDA YA KATI. ◼️ATAKA TEKNOLOJIA YA UFUGAJI WA SAMAKI KWENYE MABWAWA KUWAFIKIA WANANCHI Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amezindua mkakati wa miaka 10 wa ufugaji wa kuku ambao umelenga kubadilisha tasnia ya kuku nchini na kuifanya kuwa shindani, jumuishi na endelevu ili kuchangia usalama wa chakula, lishe, ajira, kipato, ukuaji wa uchumi na biashara. Dkt. Nchemba amezindua mkakati huo wakati wa hafla ya uzinduzi wa Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane iliyofanyika Agosti 1,2026 kwenye viwanja vya Dkt. John Samwel Malecela jijini Dodoma. “Kuku ni moja ya zao tambulisho kwa mikoa ya kanda ya kati na kaya mbalimbali, na kuzinduliwa kwa Mkakati huu kwa Serikali ni jambo la faraja ambalo litaenda kuleta mageuzi katika Sekta hiyo ndogo ya kuku na kuongeza uzalishaji wenye tija.”amesema Mhe. Dkt. Nchemba. Aidha Dkt. Nchemba ameielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhakikisha utekelez...