Machapisho

FETA YAENDESHA MAFUNZO YA UTUNZAJI NA MATENGENEZO YA BOTI NA INJINI ZA UVUVI KATIKA MKOA WA TANGA

Picha
Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) imeendesha mafunzo ya Utunzaji na Matengenezo ya Boti na Injini kwa Maafisa Uvuvi, Wahifadhi wa Maeneo Tengefu na wavuvi  wanufaika wa mkopo wenye masharti nafuu wa boti za kisasa za uvuvi zilizotolewa na Serikali. Mafunzo hayo yamehusisha washiriki 22 ambao ni Maafisa Uvuvi wa Wilaya wanne (4) na wavuvi 15 kutoka Wilaya za Mkinga, Tanga Jiji, Pangani na Muheza, Afisa Uvuvi mmoja (1) kutoka Kituo cha FRP - Tanga na Wahifadhi wawili (2) wa Hifadhi ya Bahari - Tanga. Mafunzo hayo ya siku 4 yalianza tarehe18 hadi 21 Agosti 2026 katika ukumbi wa Costal Zone mkoani Tanga. Akiongea wakati wa kufunga mafunzo hayo kwa niaba ya Mtendaji Mkuu FETA, Naibu Mkuu wa FETA Bi. Merisia Mparazo amewaasa wahitimu wa mafunzo kutumia ujuzi walioupata kuboresha shughuli zao za uvuvi na kusambaza elimu kwa wavuvi wengine ambao hawakubahatika kupata mafunzo haya. Aidha amesema mafunzo haya yatapunguza gharama za uendeshaji na kuimarisha usalama wa vyombo kwa kuon...

DKT. KIMIREI AFUNGA MAFUNZO YA PILI YA TEKNOLOJIA YA SATELAITI KATIKA SEKTA YA BAHARI NA UVUVI

Picha
Na Herry Kilele – TAFIRI, Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Ismael Kimirei, amefunga Mafunzo ya Pili ya Matumizi ya Teknolojia ya Satelaiti katika Sekta ya Bahari na Uvuvi, yaliyolenga kuimarisha uwezo wa wataalamu katika matumizi ya teknolojia hiyo kwa ajili ya utafiti, ufuatiliaji na usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari na uvuvi. Mafunzo hayo ya siku tatu yamefanyika kuanzia Agosti 19 hadi 21, 2026, katika Hoteli ya Southern Sun, Dar es Salaam, kwa ushirikiano kati ya TAFIRI na Taasisi ya Korea ya Sayansi na Teknolojia ya Bahari (KIOST). Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo, Dkt. Kimirei amesema rasilimali za bahari na uvuvi zina mchango mkubwa katika uchumi, usalama wa chakula na lishe, ajira, maisha ya wananchi pamoja na maendeleo ya Uchumi wa Buluu nchini. Amesema, Tanzania imeanza utekelezaji wa Dira2050 ambayo inatambua utafiti na matumizi ya sayansi na teknolojia kama nguzo muhimu katika kufikia malengo ya Dira2050...

KAMATI YA BUNGE YAPOKEA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI WA NARCO, TMB NA TDB

Picha
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Deodatus Mwanyika, leo Agosti 21, 2026 imepokea taarifa za utekelezaji wa majukumu kutoka Bodi ya Nyama Tanzania (TMB), Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) katika kikao kilichofanyika Bungeni Jijini Dodoma. Katika taarifa yake, Bodi ya Nyama Tanzania (TMB) imeeleza kuwa biashara ya nyama nje ya nchi imeendelea kuimarika, ambapo Tanzania imeingiza Dola za Marekani milioni 61.5 kutokana na mauzo ya nyama katika nchi 11. Kiasi hicho ni ongezeko la asilimia 8.4, ikilinganishwa na mwaka uliotangulia huku, Nyama ya mbuzi imeongoza kwa kuchangia asilimia 67 ya jumla ya nyama yote iliyouzwa nje ya nchi. Kwa mwaka 2025/2026, jumla ya tani 14,213.66 za nyama zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 61.5 ziliuzwa nje ya nchi, ikilinganishwa na tani 13,112.44 zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 53.9 mwaka 2024/2025. Kwa upande wa tasnia ya maziwa, taarifa ime...

BODI YA TAFICO YARIDHISHWA KUKAMILIKA KWA BANDARI YA UVUVI KILWA MASOKO

Picha
Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), imefanya ziara ya ukaguzi katika  mradi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko, kwa lengo la kujionea hatua ya utekelezaji wa mradi, kukagua miundombinu na maandalizi yaliyofanyika kuelekea kuanza kwa matumizi ya bandari hiyo, pamoja na kutathmini fursa zitakazotokana na uwekezaji huo katika shughuli za uvuvi na uchumi wa buluu. Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 20 Agosti 2026, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Prof. Yunus D. Mgaya, ambapo Bodi hiyo imepata fursa ya kukagua maeneo mbalimbali ya bandari na kupata maelezo kuhusu hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya kuanza kwa shughuli zake. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Prof. Mgaya, amesema ameridhishwa na maendeleo ya mradi huo, akieleza kuwa kukamilika na kuanza kufanya kazi kwa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko kutakuwa hatua muhimu katika kuimarisha sekta ya uvuvi nchini. "Bandari hii ina nafasi kubwa katika kuongeza ufanisi wa shughuli za uvuvi, kuongeza thamani ya mazao ...

TAFIRI YASHIRIKI MAFUNZO YA PILI YA TEKNOLOJIA YA SATELAITI KATIKA SEKTA YA BAHARI NA UVUVI

Picha
Na Herry Kilele – TAFIRI, Dar es Salaam. Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) imeshiriki  kufanya mafunzo ya Pili ya Matumizi ya Teknolojia ya Satelaiti katika Sekta ya Bahari na Uvuvi yanayofanyika katika Hoteli ya Southern Sun, Dar es Salaam, kwa ushirikiano na Taasisi ya Korea ya Sayansi na Teknolojia ya Bahari (KIOST). Mafunzo hayo yanalenga kuimarisha uwezo wa wataalamu katika matumizi ya teknolojia ya satelaiti kwa ajili ya utafiti, ufuatiliaji na usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari na uvuvi. Akizungumza Agosti 19, 2026, wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Uendelezaji Tafiti na Uratibu wa TAFIRI, Dkt. Mary Kishe, amesema rasilimali za bahari na uvuvi zina mchango mkubwa kwenye uchumi wa Tanzania, usalama wa chakula na lishe, ajira, maisha ya wananchi pamoja na maendeleo ya uchumi wa buluu. Amesema rasilimali za bahari na uvuvi zinaendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali zinazohusisha mabadiliko ya mazingira, tabianchi, mabadiliko ya hali ya b...

WAZIRI DKT. BASHIRU AZINDUA BENKI YA USHIRIKA TAWI LA KAGERA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amezindua Benki ya Ushirika (COOP BANK) tawi la Mkoa wa Kagera  na kufanya benki hiyo kufikisha matawi saba nchi nzima tangu kuanzishwa kwake, matawi mengine ni pamoja na Mtwara, Tandahimba, Dodoma, Dar es Salaam, Moshi na Tabora. Uzinduzi wa benki hiyo umefanyika leo Agosti 18, 2026, katika Manispaa ya Bukoba, lilikiwa ni tawi la kwanza kufunguliwa kwa Kanda ya Ziwa na kubainisha kuwa uchumi wa sasa unahitaji jitihada za pamoja kupitia ushirika  kwa kwamba benki hiyo itaufufua ushirika kupitia sekta za kilimo, mifugo na uvuvi. Katika hatua nyingine ametoa rai kwa vyama vya ushirika kujikita zaidi katika sekta za uzalishaji hususan kuongeza thamani ya bidhaa na mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi, maliasili, madini ili kuwa na tija ya kujikwamua kiuchumi, pamoja na kuondokan na umaskini huku akiwataka vijana na wanawake kuanzisha na kujiunga  na vyama vya ushirika katika sekta za mifugo na uvuvi. "Katika dunia ya sasa ...

SERIKALI KUIMARISHA MIFUMO YA TAARIFA ZA MIKOPO KWA VIJANA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaimarisha mifumo ya taarifa na takwimu kuhusu mikopo na uwezeshaji wa vijana kiuchumi ili kuongeza usimamizi wa miradi hiyo na kuhakikisha inakuwa na tija iliyokusudiwa. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo, Agosti 17, 2026, mara baada ya kuwasili mkoani Kagera akitokea jijini Mwanza, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua miradi na shughuli zinazotekelezwa na serikali, ikiwemo sekta ya mifugo na uvuvi. Akiwa Kagera, amekutana na Kaimu Mkuu wa Mkoa huo, ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Mhe. Erasto Sima, na kufanya naye mazungumzo yanayolenga kuendeleza sekta za uvuvi na mifugo. Katika mazungumzo hayo, amesema mfumo mzuri wa taarifa na takwimu za utoaji wa mikopo kwa vijana utasaidia kuwa na usimamizi mzuri wa miradi ya uwezeshaji, lakini pia utaondoa upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya watu wenye nia ovu, hivyo akatoa rai kwa viongozi wa mikoa, wilaya...