Machapisho

NARCO YAZINDUA "BULLDOZER " KUIMARISHA SEKTA YA MIFUGO

Picha
 Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imezindua "bulldozer" lenye thamani ya Shilingi milioni 450 katika Ranchi ya NARCO Ruvu, hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa Ranchi hiyo, na kuongeza upatikanaji wa malisho, maji pamoja na kukuza uzalishaji wa mifugo nchini. Akizungumza Leo Julai 20, 2026 wakati wa hafla ya uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa NARCO, Balozi Dkt. Aziz Ponary Mlima, amesema ununuzi wa "bulldozer" hilo ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya DIRA ya Taifa ya 2050, huku akibainisha kuwa litasaidia kukabiliana na changamoto za malisho na maji ambazo zinawakabili wafugaji nchini. "Bulldozer hili litatumika kuchimba visima vya maji, kuondoa vichaka vinavyozuia ukuaji wa malisho na kutengeneza mipaka ya Ranchi ili kudhibiti uvamizi, na Ranchi hii ya NARCO Ruvu ndiyo ya kwanza kunufaika na matumizi ya mashine hii ambayo pia itasaidia kuboresha mazingira ya uwekezaji ndani ya ranchi za taifa." Amesema Dkt. Mlima Balozi Dkt. Mlima...

WAZIRI KAKURWA ATOA MWELEKEO WA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAFANYABIASHARA WA MIFUGO

Picha
  Awahimiza kuimarisha umoja wao  Aahidi kuziwasilisha hoja kwa wizara na taasisi husika Daudi Nyingo – DAR ES SALAAM Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema kuwa, Serikali itaendelea kusikiliza na kushughulikia changamoto zinazowakabili wafanyabiashara wa mifugo nchini, huku akiahidi kuziwasilisha hoja zinazohusu wizara na taasisi mbalimbali ili zipatiwe ufumbuzi. Waziri Kakurwa alitoa kauli hiyo Julai 19, 2026, wakati wa kikao na wafanyabiashara wa mifugo na mazao yake kilichofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) Temeke, Dar es Salaam. Katika kikao hicho, Umoja wa Wafanyabiashara wa Mifugo na Mazao Yake Temeke (UWAMIMATE) uliwasilisha changamoto 15 zinazoathiri biashara ya mifugo na mazao yake. Akizungumza baada ya kupokea hoja hizo, Waziri alisema changamoto zilizowasilishwa hazihusu wafanyabiashara wa Temeke pekee, bali zinaakisi hali halisi ya wafanyabiashara wa mifugo katika maeneo mengi nchini. “Nimep...

DKT. MADELE AVUTIWA NA JUHUDI ZA SEKTA BINAFSI UTEKELEZAJI DIRA 2025-2050

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amevutiwa na jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na sekta binafsi kwenye kutafsiri kwa vitendo Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050. Hayo yamejiri wakati wa ziara yake ya kutembelea Kiwanda cha kusindika maziwa cha Kilimanjaro na Shamba la Mwekezaji binafsi la kuzalisha malisho na maziwa la NURU mkoani Arusha Julai 18,2026 ambapo amewapongeza wadau hao kwa kuwa na maono yanayounga mkono juhudi za Serikali za kuendeleza sekta ya Mifugo. Akiwa kwenye kiwanda cha Kilimanjaro Dkt. Madele amesema kuwa kiwanda hicho mbali na kuwa fursa ya kuwahamasisha wafugaji kuzalisha maziwa kwa wingi kimetekeleza kwa vitendo sehemu ya vipengele vilivyopo kwenye mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwakusanya wafugaji kwenye vikundi na kujenga vituo vya kukusanyia maziwa. “Sisi kama Serikali kupitia mradi huo tumeanza  kuongeza nguvu kwenye matumizi ya teknolojia ya uhimilishaji ili kuhakikisha wafu...

DKT. BASHIRU AMALIZA MGOGORO WA WAFUGAJI WEST KILIMANJARO

Picha
◼️Awataka “Laigwanan” kusimamia maadili kwenye jamii yao Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amemaliza mgogoro wa wafugaji waliopo kwenye ranchi ya Mifugo ya West Kilimanjaro iliyopo Siha mkoani Kilimanjaro ambapo amewataka viongozi wa kimila wa kaya za kimasai maarufu kama “Laigwanan” kuendelea kuhimiza elimu ya maadili kwa kwenye jamii zao ili kukomesha vitendo vya kihalifu kwenye maeneo yao. Balozi Dkt. Bashiru amefanikiwa kumaliza mgogoro huo uliokuwa ukihusisha mwekezaji na wafugaji wanaozunguka ranchi hiyo mara baada ya kufika hapo na kufanya kikao na pande zote zinazokinzana Julai 17,2026 ambapo amewasisitiza wafugaji hao kuwa mfugaji mkubwa na mdogo wote wapo sawa mbele ya sheria. “Mimi siwezi kuwa Waziri nayetembea kwenye mashamba ya wawekezaji wakubwa wenye ng’ombe nzuri wanaotoa maziwa huku wafugaji wadogo ambao ndo wengi wakiwa wamechoka pamoja na ng’ombe wao na hapo Uwaziri wangu utakosa mashiko” amesisitiza Balozi Dkt. Bashiru. Kwa upande wake ...

DKT. KILEMILE AONGOZA KIKAO CHA KUIMARISHA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA ZA KIDIJITI KATIKA HUDUMA ZA AFYA YA WANYAMA

Picha
Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania, Dkt. Amani Kilemile, ameongoza kikao cha kujadili namna bora ya kuboresha ukusanyaji wa taarifa za huduma za afya ya Wanyama nchini kwa kutumia teknolojia za kidijiti kikao hicho kimefanyika Julai 15, 2026, katika Ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, jijini Dodoma. Akiongoza majadiliano hayo, Dkt. Kilemile alisisitiza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa kidijiti utakao endana na mifumo ya serikali kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi na kwa wakati.  Katika kikao hicho washiriki walijadili fursa na changamoto zilizopo katika matumizi ya mfumo uliopo sasa ili  kubaini maeneo yanayohitaji maboresho katika kuandaa uandaaji wa mfumo mpya wa kidijitali.  Majadiliano yalijikita katika uboreshaji wa mifumo ya taarifa za afya ya wanyama, usimamizi wa taarifa za wataalamu wa mifugo, utoaji wa huduma kwa njia za kidijiti pamoja na kuimarisha uratibu na ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali zinazohusika na sekta ya afya ya wanya...

DKT. BASHIRU AZIKARIBISHA KAMPUNI KUTOKA ITALIA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa leo Juni 14, 2026 amekutana na ujumbe wa kampuni mbili kutoka nchini Italia ambayo ni ITARE na MULMIX katika Ofisi ndogo za Wizara zilizopo Kambarage Tower jijini Dodoma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuangalia maeneo ya  uwekezaji katika sekta za mifugo na uvuvi. Kampuni ya ITARE kutoka nchini Italia inajihusisha na ushauri wa kifedha yenye mchanganyiko wa kipekee wa utalaamu na uzoefu katika fedha za miradi na biashara pamoja na uendelezaji wa biashara katika masoko yanayoibukia, ikiwa na mkazo maalum katika Ukanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na Kampuni ya MULMIX imejikita katika usanifu, uzalishaji na usimikaji wa vihenge na mitambo ya kuhifadhia nafaka katika sekta ya kilimo. Baada ya ujumbe wa kampuni hizo kujitambulisha na kuonyesha utayari wa kuwekeza nchini Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezihakikishia kampuni hizo kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na sekta binafsi katika kuwekeza na kufanya bi...

DKT. BASHIRU AIAGIZA BODI MPYA YA TAFICO KUIGEUZA TAASISI HIYO KUWA INJINI YA UCHUMI SEKTA YA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameitaka Bodi mpya ya pili ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) kuhakikisha uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika sekta ya uvuvi unatafsiriwa kuwa uzalishaji wa kibiashara, mapato na mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa bodi hiyo iliyofanyika leo Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam, Waziri Dkt. Bashiru alisema Bodi hiyo inaanza kazi katika kipindi muhimu ambacho Serikali  imeweka msisitizo mkubwa katika kukuza uchumi wa buluu kupitia uwekezaji wa kimkakati kwenye sekta ya uvuvi ikiwa ni utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050. "Mnaanza kazi wakati ambao msingi wa uwekezaji umeanza kujengwa. Hivyo jukumu lenu ni kuhakikisha uwekezaji huo unazaa matokeo chanya ya kibiashara na ya maendeleo kwa Taifa," alisema Dkt. Bashiru. Katika maelekezo yake, Waziri aliitaka Bodi kusimamia kwa karibu ukamilishaji w...