Machapisho

UCHUMI WA BULUU NI FURSA - MHE. KAMANI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani amesema kuwa mbali na Uchumi wa buluu kuhakikisha usalama wa chakula na lishe pia ni eneo lenye fursa kubwa za ajira, uwekezaji, biashara, utalii na burudani. Mhe. Kamani amesema hayo aliposhiriki Kongamano kubwa la uchumi wa buluu lililofanyika Agosti 12,2026 eneo la Kizimkazi lililopo Kusini Unguja visiwani Zanzibar. Hata hivyo Mhe. Kamani amebainisha kuwa uwezo wa kunufaika na fursa hizo unategemea kwa kiasi kikubwa matumizi endelevu ya bahari na rasilimali zake ikiwa ni pamoja na maziwa, mito, mabwawa na vyanzo vingine vya maji. “Kauli mbiu yetu ya Hifadhi Bahari, Changamkia fursa za uchumi wa Buluu ni wito wa kuchukua hatua za kuimarisha usimamizi endelevu wa rasilimali za bahari, kukabiliana na uvuvi haramu na uharibifu wa mazingira pamoja na kuongeza ushiriki wa jamii katika uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali hizo” Ameongeza Mhe. Kamani. Aidha Mhe. Kamano ameelezea umuhimu wa kutumia teknolojia, utafiti na ubunifu kati...

TANZANIA MWENYEJI MKUTANO WA 10 WA WATAALAM WA MIFUGO AFRIKA 2029

Picha
Nchi ya Tanzania imechaguliwa  kuwa mwenyeji wa Mkutano wa 10 wa Wataalam wa Mifugo Barani Afrika unaotarajiwa kufanyika mwaka 2029.  Uamuzi huo umefikiwa Agosti 12,2026  wakati wa Mkutano wa 9 wa Wanachama wa Jumiya ya Wataalam wa Mifugo Barani Afrika (AASAP) unaoendelea mjini Wusa, Abuja, Nigeria Kuanzia Agosti 9 hadi 13 2026 ambapo wataalam hao wamekubaliana na kufikia uamuzi huo baada ya kuvutiwa na jitihada za Tanzania kwenye upande wa maendeleo ya Sekta ya Mifugo.  Awali kabla ya uamuzi huo Mwakilishi wa Tanzania katika Mkutano huo, Dkt. Titus Lyatuu ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Wataalam wa Mifugo Tanzania (TSAP) alieleza utayari wa Tanzania katika maandalizi na uendeshaji wa Mkutano huo huku akibainisha fursa nyingi mbalimbali za tafiti na maendeleo zilizopo nchini. Dkt. Lyatuu alieleza pia vivutio vilivyoko nchini Tanzania kwa upande wa sekta ya Utalii, tamaduni za watu wa Tanzania, hali ya amani na usalama iliyopo nchini na mifumo ya ufuga...

SERIKALI KUONGEZA UWEKEZAJI KATIKA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuwekeza katika uboreshaji wa miundombinu ya elimu na mafunzo ya ufundi ustadi ili kuendelea kujenga  taifa la kujitegemea kupitia elimu ya amali. Amesema hayo Wakati wa ziara yake mkoani Mara leo Agosti 12, 2026 baada Kukagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Amali na Ufundi Musuguri iliyopo Wilayani Butiama inayogharimu shilingi bilioni 1.6.  " Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika uboreshaji wa  miundombinu ya elimu na mafunzo ya amali ili kutengeneza taifa linaloweza kujitegemea kupitia vijana kama alivyoasisi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, hivyo ujenzi wa shule za amali kama hii ya Musuguri utatusaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira nchini" alisema Dkt. Bashiru. Akizungumz...

DKT. BASHIRU AKAGUA NA KUZINDUA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI MARA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekagua na kuzindua miradi ya mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara na kueleza kuwa serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika kutenga fedha kwa wakati katika ujenzi na uboreshaji miundombinu ya barabara, umeme na maji ili miradi hiyo ikamalishwe kwa wakati. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo Agosti 11, 2026  wakati wa ziara yake maalum  ya siku nne inayolenga kutembelea, kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali mkoani Mara. Katika ziara hiyo Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezindua Daraja la Majengo mapya - Pambazuko lenye thaman ya zaidi ya shilingi milioni 287 ambalo litaunganisha Kata za Bweri na Rwamlimi ndani ya Manispaa ya Musoma. Pia, alitembelea na kukagua ujenzi wa Soko la Nyayo, Kituo cha Mabasi na Barabara za mitaa ndani ya Manispaa ya Musoma, kuweka jiwe la Msingi la Madarasa matano, matundu ya vyoo na Ofisi katika shule ya Msingi Jitirola na kuka...

DKT. BASHIRU: SERIKALI ITASHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUTATUA CHANGAMOTO ZA TASNIA YA KUKU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi  Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema kuna haja ya serikali kushirikiana na sekta binafsi katika kusimamia ubora wa uzalishaji wa vifaranga vya kuku, chanjo pamoja na chakula cha kuku ili tasnia hiyo iweze kuendelea kukua na kuchangia uchumi na usalama wa chakula. Mhe.Balozi Dkt. Bashiru ameeleza hayo Agosti 10, 2026  baada kufika katika shamba la uzalishaji wa kuku la Homeland Farm lililopo Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza ambapo amesema ushirikiano wa serikali na sekta binafsi utajikita zaidi katika udhibiti wa mifumo ya kulinda ubora wa tasnia ya kuku hususan uzalishaji wa vifaranga vyenye ubora, chakula cha kuku na chanjo. "Yale ambayo sekta binafsi inauwezo nayo tushirikiane nayo, yale ambayo serikali tunapaswa kufanya mfano ya udhibiti, mfano haiwezekani mtu yuko sokoni anauza vifaranga viko chini ya ubora" alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, alisema kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo zimepanga kuwa...

MIFUGO NA UVUVI KINARA WIZARA ZA KISEKTA NANENANE 2026

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa pili mfululizo imefanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwa upande wa Wizara za kisekta kwenye Maonesho ya kitaifa na kimataifa ya NaneNane kwa mwaka 2026. Wizara imepata ushindi huo kutokana na kuongoza kwenye vipengele mbalimbali ikiwemo ubunifu wa teknolojia rafiki kwa matumizi ya wadau wote wa sekta za Mifugo na Uvuvi. Aidha miongoni mwa matukio bunifu yaliyoipa Wizara hiyo ushindi huo ni teknolojia ya malisho ya Mifugo aina ya Juncao, kilimo mseto cha Mpunga na samaki, Paredi ya Mifugo iliyokuwa na rekodi ya Ng’ombe mwenye uzito wa kilo 922, Mnada wa Mifugo ambao kwa mwaka huu ulishuhudia ng’ombe wawili wakiuzwa kwa shilingi Mil.22 na Kijiji cha Protini ambacho kilikuwa kivutio cha wengi kutokana na upatikanaji wa mazao yote ya protini itokanayo na samaki na wanyama. Mbali na Ushindi huo wa Wizara, Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo zimefanikiwa kufanya vizuri kwenye Maonesho hayo ambapo Wakala ya Mafunzo ya Uvuvi (FETA) ilishika nafasi ya pil...

KAMANI ASHIRIKI UZINDUZI WA “OKOA MVUVI ZANZIBAR”

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani ameshiriki uzinduzi wa programu ya “Okoa Mvuvi” zanzibar uliofanyika kwenye kiwanja cha Magarawa visiwani Zanzibar Agosti 10,2026. Programu hiyo imezinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdullah.