KAMANI AELEZA MKAKATI WA SERIKALI KUONGEZA MAENEO YA WAFUGAJI NNCHINI
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Damas Kamani amesema Serikali inaendelea kutenga, kupima na kumilikisha kwa wafugaji maeneo ya shughuli za ufugaji kutoka hekta Milioni 3.46 hadi hekta Milioni 6 pamoja na kuyaboresha maeneo hayo kwa kuyapatia huduma muhimu zikiwamo maji, majosho, malisho na huduma za ugani. Hatua hiyo ya kutenga maeneo ya shughuli za ufugaji ni utekelezaji wa maelekezo ya Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Novemba 14, 2025 pamoja na Maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2025. Mhe. Kamani amesema hayo leo Aprili 21, 2026 vacati akijibu Swali la Mbunge wa Kalambo Mkoani Rukwa Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni aliyehoji kuwa serikali ina mango gani wa kuongeza ardhi ya kilimo kwa wananchi wa kata ya Mkoe na Mbuluma kutoka katika eneo la NARCO. “Mheshimiwa Spika, Ranchi ya Kalambo ni moja kati ya ranchi 15 zinazomilikiwa na Kam...