BI. MEENA AWATAKA WATUMISHI KUWA NA USHIRIKIANO MADHUBUTI
Na. Stanley Brayton, WMUV Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena amewataka watumishi wa Wizara hiyo kuwa na ushirikiano madhubuti na kufanya kazi kwa pamoja ili kuimarisha utendaji kazi na kufikia malengo ya Sekta kwa ufanisi zaidi. Bi. Meena ametoa wito huo leo Februari 11, 2026 kwenye ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mji wa Kiserikali Mtumba Dodoma, wakati wa hafla ya kuwakaribisha Manaibu Makatibu Wakuu wapya wa wizara hiyo. “Nitumie nafasi hii kuwasihi watumishi wote kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi ili kufanikisha malengo tuliojiwekea,” amesema Bi. Meena. Katika hafla hiyo, Bi. Meena amemshukuru aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo kwa mchango wake katika kuendeleza sekta na kuwapongeza viongozi wapya kwa kuaminiwa kushika nyadhifa hizo muhimu katika wizara. Aidha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwini Mhede amesema katika kipindi chake alichokuwa hapa Wizarani amejifunza mambo mengi kuhusu sekta za mif...