FURSA MBALIMBALI ZA UKUZAJI JONGOO BAHARI ZABAINISHWA
Na. Stanley Brayton, WMUV Afisa Uvuvi Mwandamizi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Fatuma Rajabu Juma amebainisha fursa mbalimbali za ukuzaji wa jongoo bahari, ambapo amewashauri wakulima wa jongoo bahari kukuza zao hilo la Uvuvi kwa wingi ili kujiongezea kipato, kwani masoko ya Jongoo Bahari yapo kuanzia ndani na nje ya nchi. Akizungumza leo Machi 27, 2026 Jijini Tanga wakati wa zoezi la kuwajengea uwezo wakulima wa mwani na jongoo bahari, elimu inayotolewa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Mradi wa Utekelezaji wa Rasilimali za Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji (TASFAM), Bi. Fatuma amesema jongoo bahari ni fursa adhimu na zao lenye tija kubwa kiuchumi na lina faida kubwa kwa walaji na wafanyabiashara kutokana na uhitaji wake mkubwa, ambapo kilo moja ya jongoo bahari huuzwa kati ya shilingi 75,000 hadi 150,000. “Katika nchi mbalimbali, jongoo bahari hutumika kuboresha afya na kusaidia kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza,” amesema Bi. Fatuma. Aidha, Bi. Fatuma amesema Rais wa Jamhuri ya ...