PROF. SHEIKH AAGIZA UFUATILIAJI WA UBORA WA VIFARANGA VYA SAMAKI
Na Chiku Makwai, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, ameielekeza Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kuimarisha ufuatiliaji wa ubora na idadi ya vifaranga vya samaki vinavyozalishwa na kusambazwa kwa wanufaika kwenye shamba la Katabe, mkoani Kigoma. Ametoa maelekezo hayo leo Aprili 15, 2026, wakati wa ziara yake ya kutembelea na kusikiliza changamoto za wanufaika wa mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika eneo hilo. Prof. Sheikh amesema Serikali ina mpango wa kufanya utafiti wa kitaalamu ili kupata vifaranga bora vya samaki nchini kote kwa kutumia teknolojia ya kisasa, hatua itakayochangia samaki kukua kwa haraka na kuzaliana kwa wingi zaidi kulingana na mabadiliko ya mazingira. “Ubora wa vifaranga ni msingi muhimu wa kuongeza uzalishaji katika ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba, kukuza kipato cha wafugaji, pamoja na kuhakikisha mafanikio ya miradi ya maendeleo katika sekta ya uvuvi” amesema Prof. Sheikh Kwa upa...