Machapisho

PROF. SHEIKH AAGIZA UFUATILIAJI WA UBORA WA VIFARANGA VYA SAMAKI

Picha
Na Chiku Makwai, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, ameielekeza Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kuimarisha ufuatiliaji wa ubora na idadi ya vifaranga vya samaki vinavyozalishwa na kusambazwa kwa wanufaika kwenye shamba la Katabe, mkoani Kigoma. Ametoa maelekezo hayo leo Aprili 15, 2026, wakati wa ziara yake ya kutembelea na kusikiliza changamoto za wanufaika wa mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika eneo hilo. Prof. Sheikh amesema Serikali ina mpango wa kufanya utafiti wa kitaalamu ili kupata vifaranga bora vya samaki nchini kote kwa kutumia teknolojia ya kisasa, hatua itakayochangia samaki kukua kwa haraka na kuzaliana kwa wingi zaidi kulingana na mabadiliko ya mazingira. “Ubora wa vifaranga ni msingi muhimu wa kuongeza uzalishaji  katika ufugaji wa samaki kwa  njia ya vizimba, kukuza kipato cha wafugaji, pamoja na kuhakikisha mafanikio ya miradi ya maendeleo katika sekta ya uvuvi” amesema Prof. Sheikh  Kwa upa...

BI. MEENA AHIMIZA USHIRIKIANO KUINUA SEKTA YA MIFUGO

Picha
 Na, Fausta Njelekela  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena amekutana na Watendaji wakuu wa Taasisi na Wataalam wa Sekta ya Mifugo kwa lengo la kujadili kwa pamoja jinsi ya kuongeza ushirikiano baina ya viongozi na Wataalamu wa Sekta hiyo ili kubaini na kutatua changamoto zinazowakabili wataalam hao katika utendaji kazi ili kuleta tija katika Sekta hiyo. Akizungumza wakati wa Kikao hicho cha majadiliano na Wataalamu wa Sekta hiyo, yaliofanyika leo Aprili 15, 2026 Katika Ukumbi wa Ofisi ya Wizara Jijini Dodoma, Bi. Meena amesema Ushirikiano Katika Sekta ya Mifugo utaleta mbinu bora za kutatua changamoto zinazoikumba Sekta ya mifugo Kwa kutumia wataalamu walioko kwenye maeneo ya wafugaji. "Ushirikiano baina ya viongozi na Wataalamu wa Sekta ya Mifugo utasaidia kutambua changamoto zilizopo na kuzitatua, Ili kuongeza thamani ya mazao ya mifugo." amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena, ameweka msisitizo kwa Watendaji hao kujikita katika kuongeza ushirikiano ili kuta...

MIFUMO YA TAARIFA ZA UVUVI NA UFUATILIAJI NA TATHIMINI KUIMARISHWA

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi ya kaa Kikao kazi ili kuimarisha mipango ya mifumo ya taarifa za uvuvi, ufuatiliaji na tathmini kupitia Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Bahari Tanzania (TASFAM), kikao kinachofanyika Mjini Morogoro, na kinaendelea leo ili kubaini mapungufu na kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha mifumo ya taarifa na takwimu. Kikao hicho kimefunguliwa rasmi jana (14.04.2026) na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena, ambaye amebainisha juhudi mbalimbali zinazotekelezwa chini ya idara na taasisi zitasaidia kuepusha urudiaji wa kazi, kuongeza ufanisi na kuhakikisha matumizi bora ya rasilimali fedha, watu na muda. 

PROF. SHEIKH AELEKEZA UZALISHAJI WA VIFARANGA KUANZIA 200,000 KILA MWEZI KUFIKIA JUNI 2026

Picha
Na. Chiku Makwai, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, amezitaka taasisi za Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) kuimarisha ushirikiano ili kufikia uzalishaji wa vifaranga vya samaki kuanzia 200,000 hadi 300,000 kwa mwezi ifikapo Juni 2026. Maelekezo hayo aliyatoa Aprili 14, 2026, wakati wa kikao kazi kilichowakutanisha watumishi wa Wizara pamoja na taasisi hizo, kilichofanyika katika ofisi za TAFIRI mkoani Kigoma. Prof. Sheikh alisisitiza kuwa lengo la uzalishaji huo ni kurahisisha upatikanaji wa vifaranga bora kwa vijana wanaonufaika na mikopo ya vizimba, pamoja na wananchi wengine wanaojihusisha na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika Ziwa Tanganyika.

SERIKALI YAPOKEA MTAMBO WA KISASA KUIMARISHA SEKTA YA UVUVI KIGOMA

Picha
Na. Chiku Makwai, WMUV ◾ Zaidi ya Tani 15 za barafu kuzalishwa kwa siku. ◾ Dagaa zaidi ya Kilo 300 kukaushwa kwa siku. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepokea mtambo wa kisasa wa kuzalisha barafu na kukaushia dagaa, pamoja na majokofu yanayotumia nishati ya jua, kutoka mradi wa FISH4ACP ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha sekta ya uvuvi mkoani Kigoma. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya mtambo huo iliyofanyika Aprili 14, 2026 katika mwalo wa Katonga mkoani Kigoma, Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhe. Hassan Rungwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amesema kuwa mtambo huo utawasaidia wavuvi kuongeza ufanisi katika shughuli zao na kukuza uzalishaji utakao wawezesha kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na nje ya nchi. “Hatua hii itaongeza ubora wa mazao ya uvuvi, kuimarisha ushindani wa bidhaa zetu katika masoko ya ndani na nje ya nchi, pamoja na kuinua kipato cha wananchi wa Mkoa wa Kigoma,” amesema Mhe. Rungwa. Aidha, Mhe. Rungwa amewataka wavuvi pamoja na mamlaka zinazo...

TALIRI YAKABIDHIWA JENGO LA MIKUTANO LA WADAU WA MIFUGO

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) imekabidhiwa Rasmi Jengo la Mikutano la wadau wa Mifugo, Jengo ambalo litatumika kuhaulisha teknolojia zitokanazo na Utafiti kwa wadau mbalimbali wa Sekta hiyo wakiwemo Maafisa Mifugo, Wafugaji, Watafiti wa Mifugo na wadau wengine katika kufanya shughuli za Maendeleo ya Mifugo. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Aprili 13, 2026 Jijini Tanga wakati wa kukabidhiwa Jengo hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi (DRTE), Ndg. Samwel Mdachi amesema Jengo hilo limejengwa kwa Ufadhili wa Mradi wa Maziwa Faida ambao unatekelezwa na TALIRI pamoja Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA). "Huu Mradi ni Ufadhili kutoka nchi ya Ireland kupitia Taasisi za Utafiti na Mafunzo TEAGASC., ambao umewalenga wafugaji wa ng'ombe wa Maziwa wa Kanda ya Mashariki ikiwemo wafugaji wa Mkoa wa Tanga, Morogoro, Dar es Salaam, Pwani na mikoa mingine...

MABALOZI WATEULE WAHIMIZWA KUZINADI FURSA ZA MIFUGO NA UVUVI KIMATAIFA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekutana na Mabalozi Wateule wa Tanzania kwa lengo la kuwafahamisha fursa zilizopo katika sekta za mifugo na uvuvi ili kwenda kuzinadi kwenye Nchi walizopangiwa kuiwakilisha Tanzania  ikiwa ni sehemu ya kuimarisha diplomasia ya uchumi kimataifa. Mhe. Dkt. Bashiru amekutana na Mabalozi hao katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dodoma leo Aprili 13, 2026 na kuwaeleza kuwa sekta za mifugo na uvuvi zinahitaji kupanua wigo wa masoko ya kimataifa yatakayochochea uzalishaji na ukuaji wa uchumi wa wananchi. “Kama ambavyo mtakavyokuwa  makini na sekta zingine za kiuchumi kama maliasili na utalii, pia sekta za mifugo na uvuvi ni eneo muhimu, nchi yetu bado tuna nafasi ya kujikomboa kiuchumi kutokana na Kilimo, Mifugo na Uvuvi, kwa hiyo uwakilishi wenu unakuwa na mchango mkubwa katika diplomasia ya uchumi” alisema Mhe. Dkt. Bashiru. Aidha, Mhe. Dkt. Bashiru ameongeza kuwa Wizara bado inahitaji mashirikian...