Machapisho

HISTORIA YAANDIKWA! RAIS SAMIA AZINDUA MELI YA UVUVI BAHARI KUU

Picha
◼️Ni ya kwanza tangu nchi ilipopata uhuru mwaka 1961 ◼️Ina uwezo wa kubeba hadi tani 48 kwa wakati mmoja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua meli ya kwanza ya Uvuvi wa bahari kuu ambayo itaiwezesha nchi kuvua samaki waliopo kwenye  ukanda wa maalum wa uchumi wa bahari (EEZ) ambao awali haukuweza kufikiwa kutokana na kukosekana kwa meli ya aina hiyo. Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika Aprili 25,2026 kwenye ufukwe wa Makao makuu ya Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) Kigamboni mkoani Dar-es-salaam ambapo Mhe. Rais Samia amesema kuwa hatua hiyo inalenga kukuza fursa za ajira, kuongeza mapato ya Serikali na kuboresha lishe. “Niipongeze Serikali ya Japan kwa kushirikiana nasi katika kutengeneza meli hii na kupitia wao kwa kushirikiana na UNDP tutapata boti mbili za kasi ambazo zitasimamia doria ya uvuvi wa bahari kuu” Ameongeza Mhe. Rais Samia. Aidha Rais Samia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuboresha sekta ya Uvuvi kupitia ujenzi wa bandari...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA EQUITY BENKI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amekutana na Watendaji Wakuu wa Benki ya Equity, na kufanya nao mazungumzo ambayo yalilenga kuboresha na kukuza Sekta za Mifugo na Uvuvi kwa kuwawezesha Wafugaji na Wavuvi kupata mikopo kwa urahisi zaidi. Akizungumza leo Aprili 23, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao cha kuimarisha mashirikiano hayo ili kukuza Sekta hizo, kikao kilichofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara hiyo zilizopo Kambarage Towel, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru, amesema Wizara kwa sasa inaendelea kukutana na wadau mbalimbali wa Sekta za Mifugo na Uvuvi ili kuweza kuwaelezea malengo ya Serikali katika kukuza Sekta zote mbili na kuona namna za kukuza Sekta hizo. "hii yote imelenga katika kusikiliza changamoto zao mbalimbali pamoja na maoni yao, katika kuimarisha Sekta hii na ndio mana leo tumekutana na Uongozi wa Benki ya Equity ili kuangalia namna gani wafugaji na wavuvi wanaweza pata mikopo ili waweze kutanua wigo wa shughuli zao za biashara" amesema...

WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UONGOZI NA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA PWANI WATAKIWA KUSIMAMIA RASILIMALI ZA BAHARI KWA UWAZI NA USAWA

Picha
Na. Maria Mtambalike Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Mafunzo,Tafiti na Huduma za Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw Samwel Mdachi wakati akifunga mafunzo ya uongozi na usimamizi wa rasilimali za pwani kwa washiriki 12 waliopata mafunzo kwa siku 14 kuanzia tarehe 8 April mpaka  tar 21 April 2026 katika chuo cha Uvuvi FETA.  Bw Mdachi amesema kuwa mafunzo haya hayatakuwa na maana kama washiriki hawatafanya kazi zao kwa ubora na kwa vitendo zaidi huku akiwataka watumie mbinu walizojifunza kutatua migogoro kwa amani. Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt Semvua Mzighani ambao wameendesha mafunzo hayo kwa kushirikiana na Shirika la IUCA kupitia mradi wa  Re sea amesema FETA itaendelea kushirikiana na  wadau mbalimbali katika utoaji wa elimu katika jamii. Naye Mwakilishi kutoka IUCN ambae ni meneja wa program ya uhifadhi wa bahari Bw Joseph Orila amesema kuwa lengo la mradi wao ni kutoa mafunzo kwa washiriki/wakufunzi ambao wa...

KAMANI AELEZA MKAKATI WA SERIKALI KUONGEZA MAENEO YA WAFUGAJI NNCHINI

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Damas Kamani amesema Serikali inaendelea kutenga, kupima na kumilikisha kwa wafugaji maeneo ya shughuli za ufugaji kutoka hekta Milioni 3.46 hadi hekta Milioni 6 pamoja na kuyaboresha maeneo hayo kwa kuyapatia huduma muhimu zikiwamo maji, majosho, malisho na huduma za ugani. Hatua hiyo ya kutenga maeneo ya shughuli za ufugaji ni utekelezaji wa maelekezo ya Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wakati wa Kufungua Rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dodoma, Novemba 14, 2025 pamoja na Maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2025. Mhe. Kamani amesema hayo leo Aprili 21, 2026 vacati akijibu Swali la Mbunge wa Kalambo Mkoani Rukwa Mhe. Edifonsi Joackim Kanoni aliyehoji kuwa serikali ina mango gani wa kuongeza ardhi ya kilimo kwa wananchi wa kata ya Mkoe na Mbuluma kutoka katika eneo la NARCO. “Mheshimiwa Spika, Ranchi ya Kalambo ni moja kati ya ranchi 15 zinazomilikiwa na Kam...

SHILINGI BIL. 9.5 ZATENGWA KUTOA MIKOPO YA BOTI ZA KISASA ZA UVUVI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi Katika bajeti ya mwaka 2025/2026, imetenga kiasi cha shilingi Bilioni 9.5 kwa ajili ya kutoa mikopo ya boti za kisasa za uvuvi 100, boti saidizi 76, na vifaa vyake kwa masharti nafuu kwa wavuvi na wakuzaji viumbemaji. Hayo, yameelezwa leo Aprili 20, 2026 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Kamani wakati wa Kipindi cha Maswali na Majibu  Bungeni Jijini Dodoma, alipokuwa ajibu swali la Mbunge wa Nyasa Mhe. John John Nchimbi lililohoji  ni lini Serikali itatoa mikopo nafuu ya Boti za Uvuvi za Fiber kwa Wavuvi wa Wilaya ya Nyasa? “Mikopo hiyo itatolewa kwa wananchi wa mwambao wa Bahari ya Hindi, Maziwa Makuu na madogo, mabwawa na mito ambapo takribani wananchi 2,100 watanufaika moja kwa moja ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi, ajira na kipato” alisema Mhe. Kamani. Aliongeza kuwa Mikopo hiyo inalenga kutoa vifaa na pembejeo muhimu za ufugaji samaki kwa vizimba, zana za uvuvi, ufugaji wa kuku, ufugaji wa nguruwe, ufugaji...

RAIS SAMIA ATAZINDUA MELI YA UVUVI WA BAHARI KUU APRILI 25, 2026 - DKT BASHIRU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassani anatarajiwa kuzindua Meli ya Kwanza ya Uvuvi wa Bahari Kuu, ambapo uzinduzi wake utafanyika Makao Makuu ya  Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) Kigamboni Jijini Dar es Salaam. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo Aprili 17, 2026, wakati wa ziara ya  Kamati ya Uchumi na Uwekezaji ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar kutembelea na kukagua ujenzi wa bahari ya uvuvi Kilwa Masoko Mkoani Lind na kuieleza kamati hiyo kuwa  bandari ya uvuvi Kilwa masoko iliyogharimu shilingi bilioni 280 baada ya kukamilika itafanyiwa majaribio kabla ya kukabidhiwa kwa serikali. “ Mradi huu kwa sawa  tuko asilimia 97, asilimia tatu zilizobaki ni kwa sababu kuna mitambo mingine imeagizwa ili ifungwe halafu tufanye majaribio kabla ya kukabidhiwa, wakati wowote ndani ya mwezi wa nne na watano mkandarasi anaweza kutukabidhi” alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. ...

PROF. SHEIKH AAGIZA UFUATILIAJI WA UBORA WA VIFARANGA VYA SAMAKI

Picha
Na Chiku Makwai, WMUV Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, ameielekeza Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kuimarisha ufuatiliaji wa ubora na idadi ya vifaranga vya samaki vinavyozalishwa na kusambazwa kwa wanufaika kwenye shamba la Katabe, mkoani Kigoma. Ametoa maelekezo hayo leo Aprili 15, 2026, wakati wa ziara yake ya kutembelea na kusikiliza changamoto za wanufaika wa mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba katika eneo hilo. Prof. Sheikh amesema Serikali ina mpango wa kufanya utafiti wa kitaalamu ili kupata vifaranga bora vya samaki nchini kote kwa kutumia teknolojia ya kisasa, hatua itakayochangia samaki kukua kwa haraka na kuzaliana kwa wingi zaidi kulingana na mabadiliko ya mazingira. “Ubora wa vifaranga ni msingi muhimu wa kuongeza uzalishaji  katika ufugaji wa samaki kwa  njia ya vizimba, kukuza kipato cha wafugaji, pamoja na kuhakikisha mafanikio ya miradi ya maendeleo katika sekta ya uvuvi” amesema Prof. Sheikh  Kwa upa...