Machapisho

SERIKALI YAPOKEA MTAMBO WA KISASA KUIMARISHA SEKTA YA UVUVI KIGOMA

Picha
Na. Chiku Makwai, WMUV ◾ Zaidi ya Tani 15 za barafu kuzalishwa kwa siku. ◾ Dagaa zaidi ya Kilo 300 kukaushwa kwa siku. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepokea mtambo wa kisasa wa kuzalisha barafu na kukaushia dagaa, pamoja na majokofu yanayotumia nishati ya jua, kutoka mradi wa FISH4ACP ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha sekta ya uvuvi mkoani Kigoma. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano ya mtambo huo iliyofanyika Aprili 14, 2026 katika mwalo wa Katonga mkoani Kigoma, Katibu Tawala wa Mkoa huo, Mhe. Hassan Rungwa, ambaye alikuwa mgeni rasmi, amesema kuwa mtambo huo utawasaidia wavuvi kuongeza ufanisi katika shughuli zao na kukuza uzalishaji utakao wawezesha kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na nje ya nchi. “Hatua hii itaongeza ubora wa mazao ya uvuvi, kuimarisha ushindani wa bidhaa zetu katika masoko ya ndani na nje ya nchi, pamoja na kuinua kipato cha wananchi wa Mkoa wa Kigoma,” amesema Mhe. Rungwa. Aidha, Mhe. Rungwa amewataka wavuvi pamoja na mamlaka zinazo...

TALIRI YAKABIDHIWA JENGO LA MIKUTANO LA WADAU WA MIFUGO

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) imekabidhiwa Rasmi Jengo la Mikutano la wadau wa Mifugo, Jengo ambalo litatumika kuhaulisha teknolojia zitokanazo na Utafiti kwa wadau mbalimbali wa Sekta hiyo wakiwemo Maafisa Mifugo, Wafugaji, Watafiti wa Mifugo na wadau wengine katika kufanya shughuli za Maendeleo ya Mifugo. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Aprili 13, 2026 Jijini Tanga wakati wa kukabidhiwa Jengo hilo, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi (DRTE), Ndg. Samwel Mdachi amesema Jengo hilo limejengwa kwa Ufadhili wa Mradi wa Maziwa Faida ambao unatekelezwa na TALIRI pamoja Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA). "Huu Mradi ni Ufadhili kutoka nchi ya Ireland kupitia Taasisi za Utafiti na Mafunzo TEAGASC., ambao umewalenga wafugaji wa ng'ombe wa Maziwa wa Kanda ya Mashariki ikiwemo wafugaji wa Mkoa wa Tanga, Morogoro, Dar es Salaam, Pwani na mikoa mingine...

MABALOZI WATEULE WAHIMIZWA KUZINADI FURSA ZA MIFUGO NA UVUVI KIMATAIFA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekutana na Mabalozi Wateule wa Tanzania kwa lengo la kuwafahamisha fursa zilizopo katika sekta za mifugo na uvuvi ili kwenda kuzinadi kwenye Nchi walizopangiwa kuiwakilisha Tanzania  ikiwa ni sehemu ya kuimarisha diplomasia ya uchumi kimataifa. Mhe. Dkt. Bashiru amekutana na Mabalozi hao katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dodoma leo Aprili 13, 2026 na kuwaeleza kuwa sekta za mifugo na uvuvi zinahitaji kupanua wigo wa masoko ya kimataifa yatakayochochea uzalishaji na ukuaji wa uchumi wa wananchi. “Kama ambavyo mtakavyokuwa  makini na sekta zingine za kiuchumi kama maliasili na utalii, pia sekta za mifugo na uvuvi ni eneo muhimu, nchi yetu bado tuna nafasi ya kujikomboa kiuchumi kutokana na Kilimo, Mifugo na Uvuvi, kwa hiyo uwakilishi wenu unakuwa na mchango mkubwa katika diplomasia ya uchumi” alisema Mhe. Dkt. Bashiru. Aidha, Mhe. Dkt. Bashiru ameongeza kuwa Wizara bado inahitaji mashirikian...

WAFUGAJI NG'OMBE WA MAZIWA WAPEWA ELIMU YA NADHARIA NA VITENDO KUONGEZA UZALISHAJI NCHINI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Taasisi ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) zilizopo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi zimeendelea kutoa Mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wafugaji wa ng’ombe wa Maziwa ili kukuza Tasnia ya Maziwa kwa kuongeza uzalishaji wa maziwa nchini. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Aprili 13, 2026 Jijini Tanga katika Ufunguzi wa Semina ya Wafugaji wa ng'ombe Bora wa Maziwa kupitia Mradi wa Maziwa Faida, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi (DRTE), Ndg. Samwel Mdachi amesema lengo la mafunzo hayo ni kuongeza uzalishaji wa maziwa nchini na kuweza kuwafikia wafugaji 3,000 ndani ya miaka Mitano (5) ya utekelezaji wa Mradi huo, ambapo hadi sasa wafugaji 1,888 wamefikiwa. "Uboreshaji wa uzalishaji wa ng’ombe wa maziwa mlionao utasaidia kuongeza kiwango cha uzalishaji wa maziwa bora na hivyo kuongeza kipato katika kaya zenu, na...

SERIKALI NA TDCU KUZITATUA CHANGAMOTO ZA KIWANDA CHA MAZIWA TANGA

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Taasisi ya Bodi ya Maziwa, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Chama cha Ushirika wa Wazalishaji Maziwa Mkoa wa Tanga (TDCU) inaendelea na utatuzi wa changamoto za Kiwanda cha Kusindika Maziwa cha Tanga (Tanga Fresh) ambacho kina uwezo wa kusindika maziwa lita 120,000 kwa siku.  Hayo yameelezwa leo Aprili 13, 2026 Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Kamani wakati akijibu swali la Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM) Mhe. Timotheo Paul Mnzava wakati wa Kipindi cha Maswali na Majibu cha Bunge la Kumi na Tatu (13), Mkutano wa Tatu (3), Kikao cha Saba (7). Swali hilo lilihoji juu ya mkakati wa serikali wa kuwasaidia wafugaji wa Korogwe Vijijini na Mkoa wa Tanga kwa ujumla kupata soko na bei ya uhakika ya maziwa, ambapo Naibu Waziri Mhe. Kamani amesema kuwa Wizara kwa kushirikiana na wadau wa maziwa zikiwemo taasisi za fedha imeshaanza kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ili kiwanda hicho kiendelee na uzalishaji. “Mheshimiwa Mwenyek...

TASFAM YAIWEZEASHA MAABARA YA TAIFA YA UVUVI NCHINI (DSM), KUISAKA ITHIBATI YA KIMATAIFA

Picha
Na. Edward Kondela Maabara ya Taifa ya Uvuvi nchini (NFQCLAB), Kituo cha Dar es Salaam, kupitia Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Bahari Tanzania (TASFAM), yafanya kikao maalum kupata miongozo 24 ya kuwezesha maabara hiyo kuwa na mfumo wa kimataifa ili kupata ithibati ya ISO/IEC 17025.  Kikao hicho kinafanyika Mjini Morogoro, ambapo baadhi ya wataalamu wanakutana kwa wiki moja kuanzia Tarehe 8 hadi 15 Aprilii 2026 kwa ajili ya kuandaa mfumo huo ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kupata ithibati na kuifanya kuaminika kimataifa kwa kuthitibitisha ubora wa mazao ya uvuvi na kukubalika katika masoko ya kimataifa.  ISO/IEC 17025 ni Kiwango cha Kimataifa kinachotumika kwa maabara za upimaji (testing) na upimaji sahihi/ugezi (calibration) ili kuthibitisha kuwa maabara zinafanya uchunguzi na kutoa majibu sahihi yanayokubalika kimataifa, hivyo kuongeza imani kwa wadau na kurahisisha biashara ya kimataifa.

SERIKALI KUIMARISHA TASNIA YA KUKU NCHINI

Picha
Na. Stanley Brayton Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepania kuimarisha Tasnia ya kuku kwa kushirikiana na wadau wa Tasnia hiyo katika kuleta mabadiliko yenye tija ili kuongeza uzalishaji nchini ambao utasaidia kuinua vipato vya wananchi na Taifa kiujumla. Akizungumza leo Aprili 11, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao cha Mkakati na Viongozi pamoja na wadau wa Mnyororo wa thamani wa kuku nchini, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Uzalishaji kuku ni miongoni mwa Sekta zinazotakiwa kupewa kipaumbele kwani ndio inagusa maisha ya kila mwananchi, na ndipo chakula chenye usalama kinapopatikana, na ni vyema kufanya mabadiliko katika Sekta hiyo ili iwe rasmi na kufuga kisasa kwa kuendana na Teknolojia mpya ya ufugaji kuku. "Ili kunyanyua Uchumi wetu ni lazima kutanua wigo wa Sekta ya Mifugo katika Tasnia ya kuku kwa kutumia teknolojia mbalimbali, mana tunaweza zalisha kwa wingi mazao ya kuku na kwa ubora zaidi na kuuza nchi za nje na kupata fe...