Machapisho

DKT. MADELE AVUTIWA NA JUHUDI ZA SEKTA BINAFSI UTEKELEZAJI DIRA 2025-2050

Picha
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Fabian Madele amevutiwa na jitihada zinazoendelea kuchukuliwa na sekta binafsi kwenye kutafsiri kwa vitendo Dira ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050. Hayo yamejiri wakati wa ziara yake ya kutembelea Kiwanda cha kusindika maziwa cha Kilimanjaro na Shamba la Mwekezaji binafsi la kuzalisha malisho na maziwa la NURU mkoani Arusha Julai 18,2026 ambapo amewapongeza wadau hao kwa kuwa na maono yanayounga mkono juhudi za Serikali za kuendeleza sekta ya Mifugo. Akiwa kwenye kiwanda cha Kilimanjaro Dkt. Madele amesema kuwa kiwanda hicho mbali na kuwa fursa ya kuwahamasisha wafugaji kuzalisha maziwa kwa wingi kimetekeleza kwa vitendo sehemu ya vipengele vilivyopo kwenye mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwakusanya wafugaji kwenye vikundi na kujenga vituo vya kukusanyia maziwa. “Sisi kama Serikali kupitia mradi huo tumeanza  kuongeza nguvu kwenye matumizi ya teknolojia ya uhimilishaji ili kuhakikisha wafu...

DKT. BASHIRU AMALIZA MGOGORO WA WAFUGAJI WEST KILIMANJARO

Picha
◼️Awataka “Laigwanan” kusimamia maadili kwenye jamii yao Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amemaliza mgogoro wa wafugaji waliopo kwenye ranchi ya Mifugo ya West Kilimanjaro iliyopo Siha mkoani Kilimanjaro ambapo amewataka viongozi wa kimila wa kaya za kimasai maarufu kama “Laigwanan” kuendelea kuhimiza elimu ya maadili kwa kwenye jamii zao ili kukomesha vitendo vya kihalifu kwenye maeneo yao. Balozi Dkt. Bashiru amefanikiwa kumaliza mgogoro huo uliokuwa ukihusisha mwekezaji na wafugaji wanaozunguka ranchi hiyo mara baada ya kufika hapo na kufanya kikao na pande zote zinazokinzana Julai 17,2026 ambapo amewasisitiza wafugaji hao kuwa mfugaji mkubwa na mdogo wote wapo sawa mbele ya sheria. “Mimi siwezi kuwa Waziri nayetembea kwenye mashamba ya wawekezaji wakubwa wenye ng’ombe nzuri wanaotoa maziwa huku wafugaji wadogo ambao ndo wengi wakiwa wamechoka pamoja na ng’ombe wao na hapo Uwaziri wangu utakosa mashiko” amesisitiza Balozi Dkt. Bashiru. Kwa upande wake ...

DKT. KILEMILE AONGOZA KIKAO CHA KUIMARISHA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA ZA KIDIJITI KATIKA HUDUMA ZA AFYA YA WANYAMA

Picha
Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania, Dkt. Amani Kilemile, ameongoza kikao cha kujadili namna bora ya kuboresha ukusanyaji wa taarifa za huduma za afya ya Wanyama nchini kwa kutumia teknolojia za kidijiti kikao hicho kimefanyika Julai 15, 2026, katika Ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, jijini Dodoma. Akiongoza majadiliano hayo, Dkt. Kilemile alisisitiza umuhimu wa matumizi ya mfumo wa kidijiti utakao endana na mifumo ya serikali kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi na kwa wakati.  Katika kikao hicho washiriki walijadili fursa na changamoto zilizopo katika matumizi ya mfumo uliopo sasa ili  kubaini maeneo yanayohitaji maboresho katika kuandaa uandaaji wa mfumo mpya wa kidijitali.  Majadiliano yalijikita katika uboreshaji wa mifumo ya taarifa za afya ya wanyama, usimamizi wa taarifa za wataalamu wa mifugo, utoaji wa huduma kwa njia za kidijiti pamoja na kuimarisha uratibu na ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali zinazohusika na sekta ya afya ya wanya...

DKT. BASHIRU AZIKARIBISHA KAMPUNI KUTOKA ITALIA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa leo Juni 14, 2026 amekutana na ujumbe wa kampuni mbili kutoka nchini Italia ambayo ni ITARE na MULMIX katika Ofisi ndogo za Wizara zilizopo Kambarage Tower jijini Dodoma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuangalia maeneo ya  uwekezaji katika sekta za mifugo na uvuvi. Kampuni ya ITARE kutoka nchini Italia inajihusisha na ushauri wa kifedha yenye mchanganyiko wa kipekee wa utalaamu na uzoefu katika fedha za miradi na biashara pamoja na uendelezaji wa biashara katika masoko yanayoibukia, ikiwa na mkazo maalum katika Ukanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na Kampuni ya MULMIX imejikita katika usanifu, uzalishaji na usimikaji wa vihenge na mitambo ya kuhifadhia nafaka katika sekta ya kilimo. Baada ya ujumbe wa kampuni hizo kujitambulisha na kuonyesha utayari wa kuwekeza nchini Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezihakikishia kampuni hizo kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na sekta binafsi katika kuwekeza na kufanya bi...

DKT. BASHIRU AIAGIZA BODI MPYA YA TAFICO KUIGEUZA TAASISI HIYO KUWA INJINI YA UCHUMI SEKTA YA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameitaka Bodi mpya ya pili ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) kuhakikisha uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika sekta ya uvuvi unatafsiriwa kuwa uzalishaji wa kibiashara, mapato na mchango mkubwa zaidi katika uchumi wa Taifa. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa bodi hiyo iliyofanyika leo Julai 13, 2026, katika Ofisi za Makao Makuu ya TAFICO, Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam, Waziri Dkt. Bashiru alisema Bodi hiyo inaanza kazi katika kipindi muhimu ambacho Serikali  imeweka msisitizo mkubwa katika kukuza uchumi wa buluu kupitia uwekezaji wa kimkakati kwenye sekta ya uvuvi ikiwa ni utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050. "Mnaanza kazi wakati ambao msingi wa uwekezaji umeanza kujengwa. Hivyo jukumu lenu ni kuhakikisha uwekezaji huo unazaa matokeo chanya ya kibiashara na ya maendeleo kwa Taifa," alisema Dkt. Bashiru. Katika maelekezo yake, Waziri aliitaka Bodi kusimamia kwa karibu ukamilishaji w...

TANZANIA YAPATA HESHIMA KUWA MWENYEJI KUANDAA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA UKUZAJI VIUMBEMAJI

Picha
Na. Stanley Brayton ◾Dkt. Bashiru azindua Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Uvuvi Tanzani (TAFICO) na Kitabu cha Mapishi ya Samaki. Tanzania imepata heshima ya kuwa mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Ukuzaji Viumbemaji Duniani (WA26T) na Kongamano la Ukuzaji Viumbemaji Afrika (AFRAQ26), baada ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jumuiya ya Wakuzaji Viumbemaji Duniani (WAS) kusaini hati ya makubaliano ya maandalizi ya kongamano hilo litakalofanyika nchini Jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), kuanzia Desemba 1 hadi 4, 2026. Makubaliano hayo yamesainiwa leo Julai 13, 2026 Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, kwa niaba ya Serikali, huku WAS ikiwakilishwa na Mwenyekiti wa Tawi la Afrika (AFRAQ), Prof. Julius Manyala. Akizungumza baada ya utiaji saini huo, Mheshimiwa Balozi Dkt. Bashiru alisema uteuzi wa Tanzania kuwa mwenyeji wa kongamano hilo ni matokeo y...

PROF. SHEIKH AKAGUA MRADI WA BBT UVUVI MWANZA

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Ali Sheikh Julai 11, 2026 amekagua maendeleo ya mradi wa kuwezesha vijana kiuchumi kupitia Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT UVUVI) eneo la Nyegezi jijini Mwanza ambao ni sehemu ya shilingi bilioni 7 za mkopo zilizotolewa na serikali kwa vijana. Akikagua mradi huo kwa niaba ya Katibu Mkuu Prof. Sheikh ameridhishwa na hatua iliyofikiwa na kueleza kuwa serikali inaendelea kuboresha sera, sheria na kanuni za uvuvi ili kuongeza uzalishaji wa samaki nchini na kuwahimiza vijana hao kupanua wigo katika kufanya ubunifu wa kuongeza thamani ya mazao hayo. Katika hatua nyingine Prof. Sheikh amewatembelea wawekezaji wanaozalisha vifaranga vya samaki jijini Mwanza ambapo aliiagiza Idara ya Ukuzaji Viumbe maji kwa kushirikiana na  Maabara ya Taifa ya Uvuvi na Taasisi  ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania  kufanya utafiti wa vinasaba vya samaki ili kubaini ubora wa samaki wanaozalishwa na wawekezaji hao. Naye Msimamizi ...