Machapisho

BILION 7 KUKWAMUA VIJANA KIUCHUMI KUPITIA UFUGAJI SAMAKI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi ,imetenga shilingi bilioni 7 katika mwaka wa fedha 2025/2026 Kwa lengo la kuwezesha vijana kupata mitaji kupitia mikopo yenye masharti nafuu, fedha zitakazo wanufaisha vijana 308 waliopatiwa mafunzo ya ufugaji wa samaki. Hayo yamesemwa   Februari 3, 2026, Bungeni Jijini Dodoma na Naibu  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani  wakati akijibu swali la mbunge wa Bukoba Vijijini Mhe. Dkt. Jasson Samson Rwekiza aliyetaka kufahamu kuhusu mikopo ya vizimba vya samaki ili kukuza uchumi ambapo  amesema katika awamu ya kwanza Serikali ilitoa mikopo ya vizimba 44 yenye thamani ya shilingi milioni 986.80 katika Mkoa wa Kagera ambapo wanufaika 101 walinufaika na mpango huo. Aidha, Mhe. Kamani amesema, Serikali imeanza utekelezaji wa ahadi ya Mhe. Rais ya kutenga shilingi bilioni 200 kwa ajili ya mikopo ya vizimba ndani ya siku 100, hatua itakayoongeza fursa kwa vijana katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Bukoba na Musoma. "Serikali imetoa...

BBT IWEKEZE KATIKA KUZALISHA MALISHO YA MIFUGO – DKT. BASHIRU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amezitaka taasisi zinazotekeleza Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) kutumia maeneo yao kuzalisha malisho ya mifugo ili kuimarisha ufugaji wa kibiashara. Ametoa kauli hiyo leo Januari 31, 2026 alipokagua Kituo cha BBT cha unenepeshaji wa mbuzi na kondoo Kongwa mkoani Dodoma, akizitaka Kampuni za Ranchi ya Taifa (NARCO), Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) na Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) kuweka kipaumbele katika uzalishaji wa malisho kibiashara, kutokana na kwamba taasisi hizo zina ardhi, utaalam na uzoefu wa kutosha kufanikisha azma hiyo. “Vituo vyetu vyote vyenye ardhi kubwa kama hizi TALIRI, NARCO, LITA kwa sababu tunautaalam na uzoefu  mkubwa nguvu zote zipelekwe kwenye uzalishaji wa malisho, mimi ningefurahi kuona  kuwa hii ni BBT ya malisho” alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.  Aidha, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amehimiza wafugaji kupewa elimu ya uzalishaji wa malisho na kuagiza utekel...

FETA YATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI WA VIFARANGA VYA SAMAKI

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede ameitaka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kuongeza uzalishaji wa vifaranga vya samaki ili viweze kukidhi hitajio kubwa lililopo hapa nchini. Dkt. Mhede ametoa kauli hiyo jana,  29 Januari 2026 alipotembelea FETA Kampasi Kuu ya Mbegani kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na FETA pamoja na miundombinu ya kujifunzia na kufundishia. "Niwapongeze kwa utotoleshaji huu wa vifaranga na ufugaji samaki kwa ujumla ila niwasihi muongeze zaidi kasi ya uzalishaji vifaranga ili viende maeneo yenye uhitaji na nyie kujipatia kipato" amesema Dkt. Mhede. Aidha, ameishauri FETA kuwekeza katika ufugaji samaki (hasa kwenye vizimba) katika maeneo mbalimbali ikiwepo Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa lengo la kutoa mafunzo zaidi kama mashamba darasa na pia uzalishaji wa biashara ili kuongeza mapato. Awali Mtendaji Mkuu wa FETA, Dkt. Semvua Mzighani amesema kuwa kwasasa FETA inaendelea kutoa mafunzo ya muda...

DKT. BASHIRU AFANYA MAZUNGUMZO NA FAO KUENDELEZA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amekutana na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Nchini Tanzania Dkt. Nyabenyi Tipo  na kufanya mazungumzo yanayolenga kuendeleza ushirikiano  katika kukuza na kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi nchini. Kikao hicho kimefanyika leo Januari 29, 2026 katika ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi  zilizopo Kambarage Tower Jijini Dodoma ambapo Mwakilishi Mkazi wa FAO nchini Tanzania Dkt. Tipo ametumia nafasi hiyo, pia kujitambulisha na kumpongeza Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kukurwa kwa kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi. Akizungumza Katika kikao hicho Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema serikali ya awamu ya sita imetoa kipaumbele kwenye bajeti kwa sekta za uzalishaji ikiwemo kilimo, mifugo na uvuvi, hivyo juhudi zinazofanywa na FAO katika  sekta za  uzalishaji ni  ishara ya kuimarisha uchumi wa wananchi, na kum...

SERIKALI YAELEZA MKAKATI WA WA KUENDELEZA MINADA YA MIFUGO

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, imeeleza mkakati wa Serikali wa kuendeleza Mnada wa Mifugo wa Magena uliopo mpakani, kwa lengo la kukuza biashara ya mifugo na kurahisisha usafirishaji wa mifugo kwenda katika nchi jirani.  Hayo yamesemwa Leo Januari 29,2026 Bungeni Dodoma na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Kamani, wakati akijibu la swali la mbunge wa Tarime Mjini Mhe. Esther Matiko,aliyetaka kujua  mkakati wa Serikali wa kuendeleza mnada wa Mifugo wa Magema, amesema Mnada wa Magena. “Katika jitihada za kuendeleza mnada huo, serikali imeendelea kuboresha miundombinu muhimu ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022, kiasi cha shilingi milioni 175.65 kilitengwa na kutumika kujenga mazizi, kipakilio, birika la maji pamoja na vyoo, na miundombinu hiyo imekamilika.”Mhe. Kamani. Aidha, amesema kuwa pamoja na uwepo wa miundombinu hiyo, Mnada wa Magena bado haufanyi vizuri kutokana na changamoto mbalimbali zikiwemo utoroshaji wa mifugo kwenda nchi jirani unaofanywa na baad...

KAMANI ATAJA MIKAKATI YA SERIKALI KUONGEZA MAENEO YA MALISHO

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza kutekeleza mkakati wa miaka mitano wa kuongeza maeneo kwa ajili ya shughuli za ufugaji kwa kutenga hekta milioni 2.51, ikiwa ni sehemu ya kuongeza maeneo yaliyopimwa na kutengwa kwa shughuli za ufugaji kutoka hekta milioni 3.49 hadi hekta milioni sita kama ilivyoahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi  (CCM) ya mwaka 2025- 2030 na hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa kufungua Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwezi Novemba 14, 2025. Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani  leo Januari 28, 2026 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu Swali la Mbunge wa Ngorongoro Mhe. Yannick Ikae Ndoyinyo lililohoji serikali inampango gani wa kuongeza maeneo ya malisho kutoka hekta milioni Tatu hadi hekta milioni sita kama Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inavyosema?. “Mhe. Spika Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na wiz...

DTK. BASHIRU AITAKA TADB KUONGEZA WIGO WA MIKOPO SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa( Mb.) amekutana na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TABD) na kufanya mazungumzo  na yanayolenga kuendeleza ushirikiano kati ya wizara na benki hiyo  na kuitaka kuendeleza miradi ya sekta za mifugo na uvuvi. Mazungumzo hayo yamefanyika leo 27 Januari 2026 katika ofisi ndogo ya wizara hiyo iliyopo Kambarage Tower Jijini Dodoma, ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TADB alifika kujitambulisha kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi na kuimarisha ushirikiano kati ya Wizara hiyo na Benki ya TADB katika kuendeleza sekta za Mifugo na Uvuvi. Katika Mazungumzo hayo Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameipongeza Benki ya TADB kwa jinsi inavyoshirikiana na wizara na kuiagiza  kupanua wigo wa kuwasaidia wafugaji wadogo kupata mikopo nafuu ili waweze  kuendeleza miradi yao, pamoja na kuongeza ushiriki wa Taasisi za kifedha kupitia TADB katika kutoa mikopo kwenye Sekta ya Mifugo na Uvuvi. Kwa upande wa Mkur...