GHARAMA ZA UZALISHAJI NA USAFIRISHAJI MAZAO YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUPUNGUA
Serikali imelenga kupunguza gharama za uzalishaji na usafirishaji wa mazao katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi ili kuongeza thamani na kuvutia uwekezaji wa sekta binafsi ili kuongeza kipato cha wakulima, wafugaji na wavuvi. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano Uendelezaji na ukuzaji wa shoroba za Kilimo, Mifugo, na Uvuvi uliofanyika February 20, 2026, mkoani Mtwara, Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Rajab amesema mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ina fursa kubwa za kimkakati katika utekelezaji wa shoroba za kilimo, Mifugo na Uvuvi kutokana na rasilimali Ardhi na Bahari pamoja na maziwa katika mikoa hiyo. “Mikoa hii ina fursa kubwa za kimkakati katika utekelezaji wa Shoroba za kilimo kutokana na rasilimali zilizopo, mazao ya kipaumbele ambayo ni korosho, ufuta, mbaazi pamoja na choroko yanayozalishwa zaidi katika Mikoa ya Lindi na Mtwara vilevile mazao ya mahindi, maharage, kahawa, soya na tumbaku yanazalishwa zaidi katika Mkoa wa Ruvuma” amesema Mhe. Rajab. Aidha Mhe. Raja...