SERIKALI KUTOA PIKIPIKI 200 KUIMARISHA HUDUMA ZA UGANI
Na. Stanley Brayton Wizara ya Mifugo na Uvuvi imezamiria kuimarisha huduma za Ugani kwa kununua pikipiki 200 ambazo zitasaidia kuongeza ufanisi katika utendaji kazi wa maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi katika kutekeleza majukumu ya kuwahudumia wananchi ili kuongeza uzalishaji katika sekta hizo. Akizungumza Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Pwani, Ndg. Shangwe Twamala, wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo rejea kwa maafisa hao kutoka Kanda ya Kati Mashariki leo Machi 11, 2026, mkoani Pwani, Ndg. Twamala amesema pikipiki hizo 200 zitasambazwa kwa maafisa ugani wote nchini. "Wote tunashuhudia utekelezaji huo na hatua za Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwa miongoni mwenu wapo wataalam wa ugani ambao wameshapatiwa vifaa pamoja na mafunzo mbalimbali yakiwemo haya mafunzo ya leo ambayo nimepata nafasi ya kuyafungua kwa Kanda ya Kati Mashariki.” Amesema Ndg. Twamala Aidha, Ndg. Twamala amebainisha kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza majukumu mb...