TALIRI YAPONGEZWA KWA KUWEKEZA KWENYE UZALISHAJI WA MALISHO YA MIFUGO
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa juhudi zake za kuwekeza katika uzalishaji wa malisho na mbegu bora za malisho ya mifugo, hatua aliyosema ni muhimu katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa malisho nchini. Dkt. Madele ametoa pongezi hizo leo Mei 22, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kituo cha West Kilimanjaro kwa lengo la kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo. Akizungumza katika ziara hiyo, Dkt. Madele amesema sekta ya mifugo inaendelea kukabiliwa na changamoto ya upungufu wa malisho kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, hivyo uwekezaji unaofanywa na TALIRI ni hatua muhimu ya kuimarisha ufugaji wenye tija na kuongeza uzalishaji. Aidha, Dkt. Madele amewataka wataalamu wa TALIRI kuendelea kutoa elimu kwa wafugaji kuhusu mbinu bora za ufugaji wa kisasa i...