Machapisho

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI ARIDHISHWA NA UKAMILIKAJI WA GATI LA TAFICO

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena, leo Februari 15, amepokea mradi wa  ukarabati wa gati la kuegeshea meli (floating jetty) wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), uliopo Makao Makuu ya Shirika Ras Mkwavi, Kigamboni jijini Dar es Salaam. Akipokea mradi huo, Katibu Mkuu ameridhishwa na kukamilika kwa ukarabati wa gati hilo ambalo limekamilika kwa zaidi ya 98%, huku kazi zilizobaki zinatarajiwa kukamilika tarehe 18 Februari 2026. Ukarabati wa gati hili ni maandalizi ya upokeaji wa meli ya Uvuvi wa bahari kuu ambayo itaendeshwa kwa ubia kati ya sekta binafsi na Serikali .  Akipokea taarifa ya maandalizi ya mapokezi ya meli ambayo ilihusisha ukarabati wa gati na upatikanaji wa mbia , Bi. Meena amepongeza  kwa hatua iliyofikiwa ya kumpata mbia wa uendeshaji wa meli. Aidha, amewahimiza watumishi wa Shirika hilo kufanya kazi kwa bidii, weledi na ubunifu ili kuliinua shirika na kulifanya kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya sekta ya uvuvi nchini. TAFICO inatar...

CHUO CHA KIMATAIFA CHA UVUVI KUJENGWA BAGAMOYO

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatarajia kujenga chuo kipya Uvuvi chenye hadhi ya kimataifa kitakachokuwa chini ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi nchini  (FETA) kampasi ya Mbegani Bagamoyo mkoani Pwani. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt.Bashiru Ally kakurwa alipotembelea kampasi hiyo Februari 12, 2026 ambapo ameeleza kuwa chuo hicho kitakuwa cha kisasa zaidi kwenye eneo la utoaji wa mafunzo ya uvuvi, miundombinu ya kufundishia, mifumo ya kiteknolojia, vifaa vya kufundishia na uwezo wa wakufunzi. "Nafurahi kusikia mmeunda kamati ya mazungumzo baina ya Chuo kwa niaba ya Wizara na Mamlaka ya bandari na kamati hiyo isiwe na picha ya chuo kilichojengwa wakati Mwalimu Nyerere anahangaika kujenga Taifa bali kiwe na hadhi inayofanana na kumbukizi ya baba wa Taifa" Amesema Balozi Dkt Bashiru. Mbali na ujenzi wa chuo hicho, Balozi Dkt. Bashiru amesema Serikali inatarajia kununua meli mpya ya uvuvi kwaajili ya shughuli za mafunzo. Naye Nai...

MAPINDUZI SEKTA YA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUKUZA UCHUMI WA KATI WA JUU

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi iko tayari kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Mageuzi ya Shoroba za Kilimo, Mifugo na Uvuvi (AMP 2050) utakaosaidia kuchochea ukuaji wa uchumi wa kati wa juu kwa taifa. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa uhamasishaji wa ukuzaji na uendelezaji wa shoroba za kilimo uliofanyika Februari 12, 2026 mkoani Singida, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamwile, amesema lengo kuu la mkutano huo ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu mpango huo kwa wataalam wa mikoa na halmashauri, hususan kuhusu dhana ya shoroba za kilimo. “Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msisitizo mkubwa katika mageuzi ya sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi kama injini ya kukuza uchumi wa taifa, kuongeza ajira na kuinua maisha ya Watanzania kwa ujumla,” amesema Mhe. Senyamwile. Aidha, ameongeza kuwa mpango huo unalenga kupunguza gharama za uzalishaji na usafirishaji ili kuongeza thamani ya maz...

DKT. BASHIRU AWATAKA WAUZA NYAMA NJE YA NCHI KUUNGANA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewataka wauzaji wa nyama nje ya nchi kuunda umoja imara utakaowawezesha kufanya biashara kwa tija na kuhimili ushindani wa kimataifa. Akizungumza Februari 11, 2026 katika kikao na wadau hao kilichofanyika Hoteli ya Gerwill, Dodoma, Dkt. Bashiru alisema umoja huo utarahisisha mawasiliano na Serikali na kusaidia kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo. Pia amesisitiza umuhimu wa kuendesha biashara kwa uendelevu ili kuhakikisha upatikanaji wa malighafi za kutosha viwandani. “Katika uchumi wa kisasa wenye ushindani mkali, hasa katika masoko mnayolenga, mnashindana na nchi ambazo zimewekeza kwa muda mrefu. Hakuna njia ya mkato. Nawashauri kikao hiki kiwe chimbuko la wazo la kuunda umoja imara wa wauza nyama nje ya nchi, ambao utarahisisha mawasiliano kati yenu na Serikali,” amesema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele, kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo ...

BI. MEENA AWATAKA WATUMISHI KUWA NA USHIRIKIANO MADHUBUTI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena amewataka watumishi wa Wizara hiyo kuwa na ushirikiano madhubuti na kufanya kazi kwa pamoja ili kuimarisha utendaji kazi na kufikia malengo ya Sekta kwa ufanisi zaidi. Bi. Meena ametoa wito huo leo Februari 11, 2026 kwenye ofisi ya Makao Makuu ya Wizara iliyopo Mji wa Kiserikali Mtumba Dodoma, wakati wa hafla ya kuwakaribisha Manaibu Makatibu Wakuu wapya wa wizara hiyo. “Nitumie nafasi hii kuwasihi watumishi wote kuendelea kutoa ushirikiano kwa viongozi ili kufanikisha malengo tuliojiwekea,” amesema Bi. Meena. Katika hafla hiyo, Bi. Meena amemshukuru aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo kwa mchango wake katika kuendeleza sekta na kuwapongeza viongozi wapya kwa kuaminiwa kushika nyadhifa hizo muhimu katika wizara. Aidha aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Edwini Mhede amesema katika kipindi chake alichokuwa hapa Wizarani amejifunza mambo mengi kuhusu sekta za mif...

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKAGUA GATI LA KUEGESHEA MELI TAFICO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh amekagua utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa gati la kuegeshea meli (floating jetty), unaotekelezwa na Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), katika Makao Makuu ya Shirika yaliyopo Ras Mkwavi–Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Katika ziara hiyo iliyofanyika Februari 10, 2026, Prof. Sheikh alimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena, ambapo amekagua maendeleo ya mradi huo muhimu unaotarajiwa kuongeza ufanisi wa shughuli za uvuvi na huduma za meli za uvuvi chini ya TAFICO, pamoja na maandalizi ya ujio wa meli ya kwanza ya uvuvi ya Shirika. Akiwa katika eneo la mradi, alimuelekeza mkandarasi wa mradi, kampuni ya Songoro Marine, kuhakikisha kazi zote zilizobakia zinakamilika na mradi huo ukabidhiwe ifikapo tarehe 15 ya mwezi Februari 2026. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Prof. Sheikh alisema kuwa kukamilika kwa gati ambao ni miundombinu muhimu katika uendeshaji wa meli ambayo itaingia nchin...

SERIKALI KUONGEZA UZALISHAJI WA MBEGU BORA ZA NG'OMBE

Picha
Na. Fausta Njelekela Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha sekta ya mifugo nchini, kwa lengo la kuboresha mbari za mifugo, kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora za ng’ombe, hatua itakayoongeza ubora wa nyama na wingi wa maziwa bora. Hayo yameelezwa leo Februari 10, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa wakati akizungumza na watendaji wa wizara hiyo katika kikao cha uwasilishaji wa maendeleo ya Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC). Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa amesema serikali inaendelea kuimarisha uzalishaji wa malisho bora kwa njia za kisayansi, ikiwemo kuanzisha na kusimamia mashamba ya malisho ya kisasa pamoja na kuhimiza ushiriki wa sekta binafsi katika kufanya tafiti, uzalishaji wa malisho na mbegu bora za mifugo. "Tunataka kuwa na maabara ya rufaa ya mifugo kitaifa ambayo ina vifaa, nyenzo na mitambo ya kubaini na kudhibiti magonjwa ya mifugo," amesema Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa Aidha, Mhe. Ba...