BIMA YA KIDIGITALI YA MIFUGO YAZINDULIWA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amezindua Bima ya Kidigital ambayo imewezeshwa kwa ushirikiano baina ya Kampuni ya Bima ya CRDB pamoja na Kampuni ya ACRE Africa ambayo itatumia teknolojia ya kisasa kulinda mali za wafugaji nchini. Akizungumza leo Juni 29, 2026, katika Uzinduzi wa Bima ya Kidigitali ya Mifugo ijulikanayo kama Smart Mifugo, katika Hoteli ya Serena iliyopo Jijini Dar es Salaam, Bi. Meena amesema katika kukabiliana na changamoto za wafugaji, Kampuni ya Bima ya CRDB pamoja na Kampuni ya ACRE Africa, zimeleta suluhisho la ubunifu ambalo linatumia teknolojia ya kisasa kulinda mali za wafugaji wetu kupitia Smart Mifugo, na wafugaji kwa sasa wanaweza kupata bima kwa urahisi zaidi kwa njia ya kidijitali, salama na yenye uwazi. "Nimejulishwa kuwa kutakuwa na mfumo wa DigiBima App unaorahisisha usajili, malipo ya bima, na uwasilishaji wa madai, ambayo ni hatua muhimu katika kupeleka huduma karibu zaidi na wananchi, hususan wafugaji walioko vi...