Machapisho

MAAFISA UGANI WAHIMIZWA KUBADILISHANA UZOEFU ILI KUBORESHA HUDUMA KWA WANANCHI

Picha
Wataalamu wa ugani wa sekta za mifugo na uvuvi kutoka Kanda ya Ziwa wameanza mafunzo rejea katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita leo Machi 9, 2026, yaliyoandaliwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa wafugaji na wavuvi. Akifungua mafunzo hayo, mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe Lois Bura amewahimiza maafisa ugani kubadilishana uzoefu na kutumia ujuzi wao wa kitaalamu ili kuboresha huduma wanazozitoa kwa wananchi, hususan wafugaji na wavuvi  wanaotegemea ushauri wao katika shughuli za uzalishaji. "Maafisa ugani ni kiungo muhimu katika kufikisha sera, sheria na teknolojia bora za ufugaji na uvuvi ili kuongeza tija katika uzalishaji na kuendelea kuimarisha usalama wa chakula na kipato kwa wananchi." amesema Mhe. Bura Aidha, Mhe. Bura amesema kuwa huduma za ugani zina mchango mkubwa katika kuleta mageuzi  kwa kusaidia kupeleka mbinu na teknolojia mpya kwa wafugaji pamoja na kukabiliana na changamoto mbalim...

MAAFISA UGANI MIFUGO NA UVUVI TATUENI CHANGAMOTO ZA WAFUGAJI NA WAVUVI KITAALUMA - BI. MAYEMBA

Picha
Na. Stanley Brayton  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Makambako, ambaye ni Mkuu wa Idara ya usafi na uthibiti wa taka ngumu, Bi. Appia Mayemba amewataka Maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi kutatua changamoto mbalimbali kitaaluma ambazo zinawakumba wafugaji na wavuvi ili kuongeza tija katika Sekta hizo za Uzalishaji. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Makambako wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Mafunzo Rejea kwa Nyanda za Juu Kusini kwa Maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi Nchini, leo Machi 9, 2026, Wilayani Makambako Mkoani Njombe, Bi. Mayemba amesema Maafisa Ugani wanapopata Mafunzo hayo mbalimbali ya Ugani na baada ya kutoka kwenye Mafunzo ni vyema kwenda kuwahudumia wafugaji na wavuvi ili kuweza kuzitatua changamoto zao kwa umakini na utulivu. "Kama kuna jambo lolote ni vyema kushirikisha uongozi wa juu ikiwemo Wakurugenzi wa Idara mbalimbali ili kutatua changamoto za wafugaji na wavuvi kwa lengo la kupunguza masononeko kwa Serikali pa...

TASFAM YAHAKIKI MAENEO YA MIUNDOMBINU

Picha
Wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kupitia Mradi wa Uendelezaji wa Rasilimali za Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji (TASFAM), wanafanya ziara ya kikazi katika mikoa mitano ya utekelezaji wa mradi huo ili kuhakiki umiliki na kupata mahitaji ya maeneo patakapojengwa miundombinu mbalimbali ya kukuza sekta ya uvuvi. Mikoa hiyo ni Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara, ambapo katika Mkoa wa Mtwara wataalamu hao wamefanya ziara kuanzia Tarehe 5 hadi 8 Mwezi Machi 2026, katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kuhakiki eneo patakapojengwa mwalo wa kupokelea samaki katika Mtaa wa Miseti kata ya Chuno pamoja na Halmashauri ya Mtwara Vijijini, Mtaa wa Naumbu Kusini, Kata ya Naumbu patakapojengwa ghala la kuhifadhia mwani. Aidha, wakiwa katika Halmashauri ya Mtwara Vijjini wametembelea Kituo cha Hifadhi ya Bahari ya Ghuba ya Mnazi na Maingilio ya Mto Ruvuma ambacho kipo chini ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) katika Kijiji cha Ruvula Kata ya Msimbati, ambapo patajengwa...

WAFUGAJI NA WAKULIMA WAASWA KUTOCHUKUA SHERIA MKONONI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OWM- TAMISEMI) zimetoa pole kwa wahanga wa migogoro ya wakulima na wafugaji Wilayani Tunduru mkoni Ruvuma iliyosabahisha vifo vya watu nane  na wengine kadhaa kujeruhiwa tukio lililotokea mwishoni mwa mwezi septemba 2025. Akizungumza na Wananchi wa Tarafa ya Nalasi Wilayani Tunduru Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewaasa wafugaji na wakulima nchini kuacha kujichukulia sheria mkononi hasa pale inapotokea changamoto ya kuingilia matumizi ya ardhi. “Nimekuja hapa na Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI kwanza kuwapa pole wote walifariki kutokana na migogoro huo uliotokea mwenyezi Mungu Awarehemu , lakini niwaase ndugu zangu wafugaji na wakulima mjishichukulie sheria mkononi , toeni taarifa mapema kwa mamlaka za kisheria” alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, Dkt. Bashiru amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Ardhi na Ofisi ya Waziri Mkuu Ta...

SERIKALI YAKABIDHI BILIONI 7 KWA VIJANA 308 MRADI WA BBT UVUVI

Picha
 Serikali kupitia Waziri Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekabidhi hundi ya shilingi Bil. 7 kuwezesha mitaji kwa vijana waliohitimu mafunzo ya program ya Jenga Kesho iliyo Bora kwa upande wa sekta ya Uvuvi (BBT-UVUVI) ambapo zitatumika kwenye shughuli za ukuzaji viumbe maji. Akizungumza kabla ya kukabidhi hundi hiyo Mgeni rasmi wa hafla hiyo ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Mhe. Joel Nanauka amesema kuwa fedha hizo zinatolewa kama mikopo yenye mashart nafuu kwa vijana kwa ajili ya kuwezesha mitaji, vifaa, pembejeo muhimu za ukuzaji  viumbe maji pamoja na posho ya kujikimu kwa washiriki. "Program hii haitaishia tuu hapa , itaenda ukanda wa pwani na mtwara kwani mradi wenyewe una sura ya ukuzaji wa uchumi wa buluu ” Amesema Mhe. Nanauka Aidha amewakumbusha vijana wanufaika kuwa hii ni mikopo, wana wajibu wa kufanya marejesho kwa uaminifu ili fedha zinazopatikana ziweze kuwasaidia vijana wengine ambao wana uhitaji. Naye Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe...

DKT. BASHIRU AHIMIZA KAMPENI YA TUTUNZANE KUTATUA MIGOGORO YA WAFUGAJI NA WAKULIMA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amewahimiza wafugaji na wakulima kote nchini kuzingatia Kampeni ya Tutunzane inayotekelezwa Wilayani Mvomero inayolenga kuimarisha mahusiano baina yao ili kuepukana na migogoro na uhasama unaotokana na matumizi ya ardhi kati ya Wafugaji na watumiaji wengine wa Ardhi.  Balozi Dkt. Bashiru ametoa wito huo  leo Machi 06, 2026 wakati  akizungumza na Uongozi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma ambako amefika kutekeleza maelekezo ya Waziri Mkuu yaliyomtaka kufika katika Wilaya hiyo kwa ajili ya kuimarisha uhusiano baina ya wakulima na wafugaji, hivyo amewahimiza kuiga na  kuzingatia kampeni ya tutunzane . “Mhe. Rais mara nyingi amekuwa akisema hafurahishwi na migogo kati ya wakulima na wafugaji hivyo niwasihi viongozi wenzangu na wakulima na wafugaji tujifunze kupitia kampeni ya tutunzane ya Mvomero ili kuondokana na uhasama huu ambao unaturudisha nyuma.” Alisema Dkt. Bashiru. Pia, amesema ...

VITUO 31 VYASITISHWA KUTOA HUDUMA ZA AFYA YA WANYAMA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Baraza la Veterinari Tanzania (VCT) limesitisha Huduma za Vituo 31 vya Huduma za Afya ya Wanyama Mkoani Dar es Salaam, hii ni kutokana na Vituo hivyo kutokuwa na uhalali na kutokidhi vigezo vya kutoa Huduma hizo, ikiwemo kutokuwa na Usajili pamoja na kutozingatia Sheria ya Veterinari SURA 319 ya mwaka 2003. Akizungumza kwa niaba ya Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania (VCT), wakati wa Ukaguzi wa Vituo mbalimbali vya kutolea Huduma za Afya ya Wanyama pamoja na Wataalam wake, leo Machi 6, 2026 Mkoani Dar es Salaam, Mkaguzi wa Baraza hilo, Dkt. Winston Billy, amesema mpaka sasa wamekagua jumla ya vituo 261 vya Huduma hizo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Dar es Salaam na kukuta changamoto kwenye Vituo 31 ambavyo havijakidhi vigezo na kuamua kusitisha Huduma za Vituo hivyo. "tumesitisha Huduma kwenye Vituo hivi kutokana na wamiliki kutofuata Sheria za Veterinari na tumewaelekeza wamiliki na Wataalam wa Huduma za Afya ya Wanyama kufuata Sheria, Kanuni na...