DKT. MWIGULU ATAKA KILIMO CHA MALISHO KUWA MWAROBAINI WA MIGOGORO YA WAFUGAJI
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amewataka wafugaji kulima malisho ya mifugo ili kupunguza changamoto ya migogoro ya ardhi na ukosefu wa malisho ya mifugo. Mhe. Dkt. Mwigulu ametoa kauli hiyo leo Juni 19, 2026 Wilayani Chalinze Mkoani Pwani wakati akifungua Maonesho na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo na kueleza kuwa changamoto ya uhaba wa malisho imekuwa kikwazo kwa wafugaji nchini, hivyo amewahimiza wafugaji na wadau wote wa sekta ya mifugo kutumia maonesho hayo kujifunza juu ya kilimo cha malisho, uboreshaji wa mbegu za mifugo ili kuleta tija na kuchangia pato la taifa. “Nitumie fursa hii kuwahimiza wadau wote wa mifugo nchini kutumia fursa ya maonesho haya kujifunza kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa za ufugaji na kilimo cha malisho ya mifugo ili kuongeza uzalishaji, kuuza na kununua mifugo bora kwenye minada inayoambatana na maonesho haya." amesema Mhe. Dkt. Mwigulu Aidha, Mhe. Dkt. Mwigulu...