Machapisho

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKAGUA GATI LA KUEGESHEA MELI TAFICO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Prof. Mohammed Sheikh amekagua utekelezaji wa mradi wa ukarabati wa gati la kuegeshea meli (floating jetty), unaotekelezwa na Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), katika Makao Makuu ya Shirika yaliyopo Ras Mkwavi–Kigamboni, jijini Dar es Salaam. Katika ziara hiyo iliyofanyika Februari 10, 2026, Prof. Sheikh alimuwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agness Meena, ambapo amekagua maendeleo ya mradi huo muhimu unaotarajiwa kuongeza ufanisi wa shughuli za uvuvi na huduma za meli za uvuvi chini ya TAFICO, pamoja na maandalizi ya ujio wa meli ya kwanza ya uvuvi ya Shirika. Akiwa katika eneo la mradi, alimuelekeza mkandarasi wa mradi, kampuni ya Songoro Marine, kuhakikisha kazi zote zilizobakia zinakamilika na mradi huo ukabidhiwe ifikapo tarehe 15 ya mwezi Februari 2026. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Prof. Sheikh alisema kuwa kukamilika kwa gati ambao ni miundombinu muhimu katika uendeshaji wa meli ambayo itaingia nchin...

SERIKALI KUONGEZA UZALISHAJI WA MBEGU BORA ZA NG'OMBE

Picha
Na. Fausta Njelekela Serikali imeendelea kuchukua hatua madhubuti za kuimarisha sekta ya mifugo nchini, kwa lengo la kuboresha mbari za mifugo, kuongeza uzalishaji na upatikanaji wa mbegu bora za ng’ombe, hatua itakayoongeza ubora wa nyama na wingi wa maziwa bora. Hayo yameelezwa leo Februari 10, 2026 jijini Dodoma na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa wakati akizungumza na watendaji wa wizara hiyo katika kikao cha uwasilishaji wa maendeleo ya Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC). Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa amesema serikali inaendelea kuimarisha uzalishaji wa malisho bora kwa njia za kisayansi, ikiwemo kuanzisha na kusimamia mashamba ya malisho ya kisasa pamoja na kuhimiza ushiriki wa sekta binafsi katika kufanya tafiti, uzalishaji wa malisho na mbegu bora za mifugo. "Tunataka kuwa na maabara ya rufaa ya mifugo kitaifa ambayo ina vifaa, nyenzo na mitambo ya kubaini na kudhibiti magonjwa ya mifugo," amesema Mhe. Balozi Dkt. Kakurwa Aidha, Mhe. Ba...

RAIS SAMIA: SEKTA ZA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI ZISIMAMIWE KISANYANSI

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan,  amewataka Viongozi na Wataalam wa sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kusimamia sekta hizo kwa misingi ya kisayansi na kisasa ili ziwe chachu ya kuongeza uzalishaji utakaoimarisha usalama wa chakula, kutoa ajira kwa vijana na kuchangia mapato na ukuaji wa uchumi wa Taifa. Mhe. Dkt. Samia  ameyasema hayo leo Februari 9, 2026 Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati wa hafla ya uapisho wa viongozi wateuli wa nafasi mbalimbali, ambapo kwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi walioapishwa ni Naibu Katibu Mkuu anayesimamia sekta ya Uvuvi, Prof. Mohamed Ali Sheikh pamoja na Dkt. Fabian Magawa  Madele, Naibu Katibu Mkuu anayesimamia sekta ya mifugo. Akizungumza katika hafla hiyo, kwa wateule hao pamoja na wengine Mhe. Dkt. Samia amebainisha kuwa sekta za mifugo na uvuvi ni miongoni mwa sekta zenye mavuno ya haraka, hivyo zinapaswa kupewa kipaumbele cha pekee katika mipango ya maendeleo ya taifa.  "Soko la kimataifa linahitaj...

TPHPA KUIMARISHA MAHUSIANO NA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) waazimia kuimarisha mahusiano ya kiutendaji kazi katika utumiaji wa teknolojia inayoweza kutambua vinasaba vya virus, bakiteria, fangasi, na vimelea wengine wa magonjwa ya wanyama na mimea (NANOPODS) na matumizi ya ndege nyuki ya ufuatiliaji wa magonjwa. Akizungumza, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Nchini, Dkt. Benezeth Lutege leo Februari 06, 2026 mara baada ya kutembelea Makao Makuu ya Ofisi ya TPHPA iliyopo Mkoani Arusha, amesema wamejadiliana juu ya matumizi ya teknolojia ya kisasa ya ufuatiliaji wa magonjwa ya mifugo na mimea, inayotumika katika mashamba ya parachichi, na kutumika katika ufuatiliaji wa magonjwa ya mifugo. Aidha, Dkt. Lutege amebainisha wazi kuwa mazungumzo hayo yalikuwa na lengo la kujifunza namna taasisi hiyo ilivyofanikiwa katika kufungua Masoko 408 ya kimataifa ya mazao ya kilimo ndani ya miaka 2. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph Ndunguru ameonesha nia ya ...

NARCO YATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI MAZAO YA MIFUGO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede ameisisitza  Kampuni ya Ranchi za Taifa  Nchini (NARCO) kutekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maelekezo ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally, ya kuleta ufanisi wa Kampuni hiyo na kuzalisha mazao yenye ubora katika sekta ya mifugo hapa nchini. Dkt. Mhede ametoa rai hiyo leo Februari 05, 2026 Makao Makuu ya NARCO mjini Dodoma wakati wa kikao kazi cha utekelezaji wa maelekezo ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi kuhusu utekelezaji wa maagizo ya Rais ya kuongeza ufanisi wa Kampuni hiyo katika  kufanya mageuzi ya sekta ya mifugo.  “Kampuni hii inatakiwa iongoze kwa kuzalisha mazao ya mifugo yenye ubora, niwasihi tujitoe kwa nguvu zote katika kutekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  pamoja na maelekezo ya Waziri wet...

BILION 7 KUKWAMUA VIJANA KIUCHUMI KUPITIA UFUGAJI SAMAKI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi ,imetenga shilingi bilioni 7 katika mwaka wa fedha 2025/2026 Kwa lengo la kuwezesha vijana kupata mitaji kupitia mikopo yenye masharti nafuu, fedha zitakazo wanufaisha vijana 308 waliopatiwa mafunzo ya ufugaji wa samaki. Hayo yamesemwa   Februari 3, 2026, Bungeni Jijini Dodoma na Naibu  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani  wakati akijibu swali la mbunge wa Bukoba Vijijini Mhe. Dkt. Jasson Samson Rwekiza aliyetaka kufahamu kuhusu mikopo ya vizimba vya samaki ili kukuza uchumi ambapo  amesema katika awamu ya kwanza Serikali ilitoa mikopo ya vizimba 44 yenye thamani ya shilingi milioni 986.80 katika Mkoa wa Kagera ambapo wanufaika 101 walinufaika na mpango huo. Aidha, Mhe. Kamani amesema, Serikali imeanza utekelezaji wa ahadi ya Mhe. Rais ya kutenga shilingi bilioni 200 kwa ajili ya mikopo ya vizimba ndani ya siku 100, hatua itakayoongeza fursa kwa vijana katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Bukoba na Musoma. "Serikali imetoa...

BBT IWEKEZE KATIKA KUZALISHA MALISHO YA MIFUGO – DKT. BASHIRU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amezitaka taasisi zinazotekeleza Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT) kutumia maeneo yao kuzalisha malisho ya mifugo ili kuimarisha ufugaji wa kibiashara. Ametoa kauli hiyo leo Januari 31, 2026 alipokagua Kituo cha BBT cha unenepeshaji wa mbuzi na kondoo Kongwa mkoani Dodoma, akizitaka Kampuni za Ranchi ya Taifa (NARCO), Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) na Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) kuweka kipaumbele katika uzalishaji wa malisho kibiashara, kutokana na kwamba taasisi hizo zina ardhi, utaalam na uzoefu wa kutosha kufanikisha azma hiyo. “Vituo vyetu vyote vyenye ardhi kubwa kama hizi TALIRI, NARCO, LITA kwa sababu tunautaalam na uzoefu  mkubwa nguvu zote zipelekwe kwenye uzalishaji wa malisho, mimi ningefurahi kuona  kuwa hii ni BBT ya malisho” alisema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru.  Aidha, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amehimiza wafugaji kupewa elimu ya uzalishaji wa malisho na kuagiza utekel...