DKT. LUTEGE: MAFUNZO YA MADAKTARI WA MIFUGO YATAIMARISHA FURSA ZA MASOKO YA NJE
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuimarisha uwezo wa wataalamu wa mifugo nchini kwa kuwapatia mafunzo yanayolenga kukidhi viwango vya kimataifa katika sekta ya mifugo, hatua itakayochangia kuongeza fursa za masoko ya mifugo na mazao yake ndani na nje ya nchi. Akizungumza katika hafla ya kuhitimu mafunzo kwa Madaktari wa Mifugo iliyofanyika leo Juni 25, 2026 katika Ukumbi wa Royal Hotel jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo nchini, Dkt. Benezeth Lutege, amesema mafunzo hayo yamekuja kufuatia tathmini iliyofanywa na Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (WOAH) ili kubaini kama wataalamu wa mifugo nchini wanaendana na viwango vya kimataifa vinavyohitajika katika biashara ya mifugo na mazao ya mifugo. "Kupitia ushirikiano kati ya Shirika la Afya ya Wanyama Duniani na Chuo Kikuu cha Minesota, Tanzania imepata fursa ya kushiriki katika mafunzo hayo ambapo wataalamu tisa (9)wamehitimu, huku wataalamu wengine 26 wakitarajiwa kuanza mafunzo kwa njia ya mtandao." Amesema Dkt. ...