Machapisho

WANANCHI WAJITOKEZA KUJIFUNZA UFUGAJI BORA KATIKA BANDA LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Wananchi mbalimbali wanaendelea kutembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Mifugo na Mnada wa Kimataifa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mbogo Ranchi, Ubena Zomozi, wilayani Chalinze mkoani Pwani, kwa lengo la kujifunza teknolojia na mbinu bora za ufugaji zinazolenga kuongeza tija na kukuza uchumi wa mifugo. Wakiwa katika banda hilo, wananchi wanapata elimu kuhusu uzalishaji na uhifadhi wa malisho ya mifugo, umuhimu wa kupima ubora wa maziwa, teknolojia ya uhimilishaji, huduma za chanjo na udhibiti wa magonjwa ya mifugo, pamoja na fursa mbalimbali za kiuchumi zinazopatikana katika sekta ya mifugo. Aidha, wataalamu kutoka taasisi mbalimbali zilizo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi wanaendelea kutoa ushauri wa kitaalamu na kujibu maswali ya wananchi ili kuwawezesha kufanya ufugaji wenye tija, unaozingatia matumizi ya teknolojia na mbinu bora za kisasa. Katika maonesho hayo yaliyoandaliwa na Mbogo Ranchi, taasisi mbalimbali za sekta ya mifugo zinashiriki k...

WAFUGAJI WATAJWA KUWA KINARA UTEKELEZAJI DIRA YA MAENDELEO 2050

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema wizara hiyo imeanza mchakato wa kufanya mapitio ya sera ya mifugo ya mwaka 2006 na kuandaa mkakati mahususi utakaofanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo Chalinze Mkoani Pwani kwenye Maonesho na Mnada wa Mifugo yanayofanyika katika Ranchi ya Mbogo Farm kuanzia Juni 19 hadi 22  na kueleza kuwa mikakati hiyo itasaidia kuwa na uwiano wa vipaumbele vya wizara na Dira ya Maendeleo 2050. “Kwa mujibu wa Dira, sekta binafsi inatarajiwa kuchangia katika uchumi wa nchi kwa asilimia 70 ifikapo 2050 na wafugaji ndio sekta binafsi tangu kuzaliwa kwa ufugaji, kwahiyo wao ndio watakuwa wa kwanza kuifikia hiyo asilimia 70” amesema Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, ameleza kuwa Serikali imeendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kuimarisha na kuendeleza sekta ya mifugo nchini akitolea mfano Mbogo Ranchi ambayo imekuwa ikishirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika uzalishaji ...

MATUNDA YA BBT-UVUVI AWAMU YA PILI YAANZA KUONEKANA

Picha
◼️Wanufaika wengine 26 wawezeshwa mitaji  Mwanza Utekelezaji wa awamu ya pili ya programu ya Jenga Kesho iliyo Bora (BBT) kwa upande wa sekta ya Uvuvi umeanza kuonesha matunda baada ya samaki waliopandikizwa takribani miezi 3 iliyopita kuanza kukua hadi kufikia gramu 250 Akizungumza mmoja wa wanufaika hao Bw. Erasto Deo mbali na kuishukuru Serikali kwa kuwawezesha mikopo ya masharti nafuu isiyo na riba amesema kuwa hatua hiyo imewaonesha mwanga wa mafanikio wanayotarajia pindi watakapovuna samaki hao kuanzia mwezi Novemba mwaka huu. “Mikopo hii ina manufaa makubwa sana kwa sababu kwa mfano sisi tulipandikiza vifaranga 11,000 ambavyo kama vitaendelea kukua vizuri hadi kufikia gramu 500 tuna uhakika wa kupata tani tano na nusu ambapo kwa bei ya sasa ya kilo ya samaki hapa Mwanza bei ya huku uwandani ni shilingi 8500 hivyo hata tukipata tani 4 tuna uhakika wa kupata milioni 32 ambayo kiuhalisia mtu akikopa hela hiyo atarudisha milioni 60 kwa miaka 5” Ameongeza Bw. Deo. Kwa upande wake...

DKT. MWIGULU ATAKA KILIMO CHA MALISHO KUWA MWAROBAINI WA MIGOGORO YA WAFUGAJI

Picha
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amewataka wafugaji kulima malisho ya mifugo ili kupunguza changamoto ya migogoro ya ardhi na ukosefu wa malisho ya mifugo. Mhe. Dkt. Mwigulu ametoa kauli hiyo leo Juni 19, 2026 Wilayani Chalinze Mkoani Pwani wakati akifungua Maonesho na Mnada wa Mifugo, yaliyofanyika katika Ranchi ya Mbogo na kueleza kuwa changamoto  ya uhaba wa malisho imekuwa kikwazo  kwa wafugaji nchini, hivyo amewahimiza wafugaji na wadau wote wa sekta ya mifugo kutumia maonesho hayo kujifunza juu ya kilimo cha malisho, uboreshaji wa mbegu za mifugo ili kuleta tija na kuchangia pato la taifa. “Nitumie fursa hii kuwahimiza wadau wote wa mifugo nchini kutumia fursa ya maonesho haya kujifunza kuhusu matumizi ya teknolojia za kisasa za ufugaji na kilimo cha malisho ya mifugo ili kuongeza uzalishaji, kuuza na kununua mifugo bora kwenye minada inayoambatana na maonesho haya." amesema Mhe. Dkt. Mwigulu  Aidha, Mhe. Dkt. Mwigulu...

DKT. BASHIRU ARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA MAONESHO YA MIFUGO

Picha
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ameridhishwa na maandalizi kuelekea Maonesho na Mdana wa Mifugo 2026 yanayozikutanisha nchi tatu ambazo ni Tanzania, Kenya na Namibia yatakayofanyika Ubena Zomozi, ambapo Maonesho hayo yanatarajiwa kuzinduliwa kesho tarehe 19 Juni, 2026 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba. Akizungumza leo Juni 18, 2026 Wilayani Chalinze Mkoani Pwani, wakati akikagua Maendeleo ya Maandalizi hayo, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amesema mpangilio wa Maonesho ya Mifugo umekaa vizuri, na amewapongeza wadau mbalimbali walioshiriki kuandaa Maonesho hayo ambayo yatafungua fursa kwa wafugaji nchini. "Maonesho haya ni fursa kwa wafugaji kwani wataweza kujifunza jinsi ya kufuga kisasa na kwa tija, na kupata elimu mbalimbali kuhusu Malisho ya Mifugo" amesema Mhe. Balozi Dkt. Bashiru  Aidha, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameipongeza Menejimenti ya Wizara kwa Maandalizi mazuri ya Kilimo cha Malisho, amba...

RIDHIWANI AVUTIWA NA HUDUMA ZINAZOTOLEWA BANDA LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Na. Chiku Makwai- Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete ameonesha kuvutiwa na huduma na elimu mbalimbali zinazotolewa katika banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi alipotembelea banda hilo kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma. Akiwa katika banda hilo, Waziri huyo alipata maelezo kutoka kwa wataalamu wa Wizara na taasisi zake kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa kwa wananchi, ikiwemo ushauri wa kitaalamu katika sekta za mifugo na uvuvi, fursa za uwekezaji, pamoja na mikakati inayotekelezwa na Serikali katika kuendeleza sekta hizo kwa manufaa ya wananchi na uchumi wa Taifa. Waziri Ridhiwani alieleza kuridhishwa na namna wataalamu wanavyotoa huduma kwa wananchi kwa ukaribu na ufanisi, huku akisisitiza umuhimu wa taasisi za umma kutumia maadhimisho hayo kama jukwaa la kuwafikia wananchi moja kwa moja na kusikiliza changamoto zao ili kuboresha ut...

DKT. MHINA AHIMIZA USHIRIKI WA SEKTA BINAFSI KATIKA KUIMARISHA MATUMIZI YA CHANJO ZA MIFUGO

Picha
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Dkt. Charles Mhina, amesema kuwa matumizi sahihi ya chanjo ni moja ya nyenzo muhimu katika kudhibiti magonjwa ya mifugo, kuongeza uzalishaji na kuimarisha ushindani wa sekta ya mifugo nchini.  Dkt. Mhina ameyasema hayo leo Juni 16, 2026 jijini Arusha wakati akifungua Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Mifugo kuhusu Chanjo na Uchanjaji wa Mifugo ulioandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, GALVmed, FAO Tanzania na TAHO. Akizungumza katika mkutano huo, Dkt. Mhina amesema sekta ya mifugo ina mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania kupitia usalama wa chakula na lishe, ajira, kipato cha kaya pamoja na mauzo ya bidhaa za mifugo ndani na nje ya nchi.  Hata hivyo, amesema maendeleo ya sekta hiyo bado yanakabiliwa na changamoto za magonjwa mbalimbali ya mifugo yakiwemo Sotoka ya Mbuzi na Kondoo (PPR), Ugonjwa wa Midomo na Miguu (FMD), Brucellosis na...