BILION 7 KUKWAMUA VIJANA KIUCHUMI KUPITIA UFUGAJI SAMAKI
Wizara ya Mifugo na Uvuvi ,imetenga shilingi bilioni 7 katika mwaka wa fedha 2025/2026 Kwa lengo la kuwezesha vijana kupata mitaji kupitia mikopo yenye masharti nafuu, fedha zitakazo wanufaisha vijana 308 waliopatiwa mafunzo ya ufugaji wa samaki. Hayo yamesemwa Februari 3, 2026, Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Ng’wasi Kamani wakati akijibu swali la mbunge wa Bukoba Vijijini Mhe. Dkt. Jasson Samson Rwekiza aliyetaka kufahamu kuhusu mikopo ya vizimba vya samaki ili kukuza uchumi ambapo amesema katika awamu ya kwanza Serikali ilitoa mikopo ya vizimba 44 yenye thamani ya shilingi milioni 986.80 katika Mkoa wa Kagera ambapo wanufaika 101 walinufaika na mpango huo. Aidha, Mhe. Kamani amesema, Serikali imeanza utekelezaji wa ahadi ya Mhe. Rais ya kutenga shilingi bilioni 200 kwa ajili ya mikopo ya vizimba ndani ya siku 100, hatua itakayoongeza fursa kwa vijana katika maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Bukoba na Musoma. "Serikali imetoa...