KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUIMARISHA USALAMA WA CHAKULA NCHINI
Baraza la Kumshauri Rais Masuala ya Kilimo na Chakula limekutana na Wizara ya Kilimo pamoja na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa lengo la kujadiliana namna ya kuongeza uzalishaji katika sekta hizo ili kuimarisha usalama wa chakula nchini. Mwenyekiti wa Baraza hilo na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda ameongoza kikao hicho leo Machi 24, 2026 katika Ukumbi wa Kilimo Four Jijini Dodoma ambapo amesema kuwa baraza hilo limekuwa likiimarisha ushirikiano wa wadau na sekta binafsi katika kuongeza uzalishaji na kuzihimiza Wizara za Kilimo, Mifugo na Uvuvi kufanya kazi kwa umoja ili kuyafikia malengo ya kuongeza uzalishaji ifikapo Mwaka 2030. “Malengo haya yanatupeleka 2030 leo hii 2026 unaona kabisa muda sio rafiki kwa hiyo nguvu kubwa sana inahitajika lakini tukiwa wamoja hatutashindwa kuyafikia” amesema Mhe. Pinda. Akisoma taarifa ya Mpango wa Kuongeza Uzalishaji wa Chakula Nchini Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dkt. Florence Turuka amesema dhamira ya serikali katika se...