Machapisho

UHIMILISHAJI WA MIFUGO KUONGEZA UZALISHAJI WA MAZIWA NCHINI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza Mradi wa Mageuzi ya Tasnia ya Maziwa na Mabadiliko ya Tabianchi (C-SDTP) unaolenga kuongeza uzalishaji wa maziwa na nyama kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya uhimilishaji.  Kauli hiyo imetolewa leo Machi 23, 2026 na Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Stephen Michael, wakati akifungua  mafunzo ya uhimilishaji kwa wataalamu wa mifugo yaliyofanyika  katika Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) mkoani Arusha. kuongeza tija na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi. “Mafunzo haya ni sehemu muhimu ya kuhakikisha wataalamu wanapata ujuzi wa kisasa utakaowawezesha kuwahudumia wafugaji kwa ufanisi zaidi ili kuongeza tija na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi,” amesema  Bw. Michael. Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) Dkt. Dafay Bura amesema lengo kuu la mafunzo hayo ni kuwajengea wataalam wa mifug...

SERIKALI KUANZISHA PROGRAMU YA MAFUNZO YA TEKNOLOJIA YA UZALISHAJI KUKU NCHINI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi, imeanza mchakato wa kuanzisha programu ya mafunzo ya teknolojia ya kuku ili kukidhi mahitaji ya wadau wa sekta hiyo, mchakato ambao umeanza na maandalizi ya mtaala pekee ambapo warsha ya wadau imefanyika ili kupitia na kuboresha Rasimu ya Mtaala wa Teknolojia ya Uzalishaji wa kuku ngazi ya Astashahada na Stashahada yenye lengo la kuanzisha programu hiyo ili kupata wataalamu mahiri watakaochangia kuleta mabadiliko makubwa katika Tasnia. Akizungumza leo Machi 23, 2026 Jijini Dar es Salaam katika Warsha hiyo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, amesema Mafunzo ya ufugaji kuku yamekuwa yakitolewa kwa sehemu ndogo sana ndio maana sasa Serikali imeona ni vyema kuanzisha Mtaala mahususi wa kuzalisha wataalam wabobevu kwenye tasnia hiyo kutokana na uhitaji wa wadau wa sekta binafsi na ukuaji wa sekta yenyewe nchini. "Wizara kupitia Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA) kwa kushirikiana na wadau wa s...

SERIKALI KUJENGA VIWANDA VIWILI VYA KUZALISHA CHAKULA CHA SAMAKI

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza Mkakati wa kujenga Viwanda viwili vya chakula cha Samaki ili kuhakikisha chakula hicho kinapatikana kwa wingi na kwa urahisi zaidi, hatua ambayo itatatua changamoto za upatikanaji wa chakula hicho kwa wavuvi. Akizungumza leo Machi 18, 2026 jijini Mwanza katika Kikao cha kujadili Mwongozo wa hiari wa kusimamia wavuvi wadogo, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Kisaka Meena amesema kwa sasa Serikali ina Mpango wa kujenga Viwanda viwili vya kuzalisha chakula cha Samaki, Viwanda ambavyo vitajengwa Kilwa na Mwanza. "Viwanda hivi vitajengwa kupitia Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO), na Serikali inategemea viwanda hivi vitakuwa msaada kwa wavuvi na wakuzaji Viumbemaji wote nchini" amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena amebainisha kuwa kwa kipindi cha nyuma wavuvi walikuwa wanashida sana na vyakula vya Samaki kiasi cha kupelekea vyakula hivyo kuagizwa kutoka nchi za nje na kuwa vya gharama zaidi,...

QATAR YAFUNGUA SOKO LA NYAMA YA TANZANIA

Picha
Nchi ya Qatar imefungua soko la nyama ya Mbuzi na Kondoo kutoka Tanzania ambalo ililifunga Agosti 25,2025 baada ya kupata taarifa ya uwepo wa ugonjwa wa midomo na miguu (FMD). Akizungumza mapema Machi 18,2026, Mkurugenzi wa huduma za Mifugo nchini Dkt. Benezeth Lutege amesema kuwa taarifa ya kufunguliwa soko hilo imetolewa na nchi hiyo Machi 17,2026 mara baada ya kujiridhisha kuhusu hatua zilizochukuliwa na Tanzania katika kukabiliana na magonjwa ya Mifugo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa karantini ya kisasa na awamu ya kwanza utekelezaji wa kampeni ya chanjo na utambuzi wa Mifugo inayoendelea hivi sasa. “Mara baada ya kufungiwa Serikali ilichukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaandikia nchi ya Qatar kuwaeleza kuwa ugonjwa huo upo sehemu ndogo tu ya nchi yetu na mifugo tunayopeleka huko haitoki kwenye maeneo hayo na bahati nzuri machinjio zetu zote hapa nchini zina sifa ya kuchakata nyama inayokwenda nje hivyo na wao baada ya kujiridhisha ndo wakatufungulia” Ameongeza Dkt. Lutege. ...

BANDARI YA UVUVI BAGAMOYO, TATHMINI YA KIMAZINGIRA YAANZA

Picha
 Na. Edward Kondela Serikali imesema inafanya uwekezaji kwenye miundombinu ya sekta ya uvuvi, hususan kwenye bandari ili kuboresha miundombinu hiyo na kuongeza pato la taifa. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Agnes Meena, amebainisha hayo (17.03.2026) wakati akizindua rasmi zoezi la tathmini ya athari ya mazingira na jamii (ESIA), kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa bandari ya uvuvi katika Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, ambapo amesema uwepo wa bandari hiyo ni muhimu kutokana na kile kitakachokuwa kikifanyika ili kukuza pato la taifa. Bi. Meena akizindua zoezi hilo katika ofisi za Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Kampasi ya Mbegani, amesema bandari hiyo itakayojengwa eneo la Mbegani itakuza sekta ya uvuvi, ambayo bado inahitajika kuchangia zaidi katika pato la taifa na uwepo wa bandari kutachochea zaidi shughuli za uvuvi kuhakikisha mazao yanayotokana na uvuvi hayapotei pamoja na kuongezewa thamani. Aidha, amewataka wataalamu kufanya kazi kwa weledi na kujifunza zaid...

BUNGE LAPONGEZA MAFANIKIO YA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

Picha
◼️Dkt. Bashiru apongeza chama cha wafugaji kwa kufanikisha kampeni hiyo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kamati yake ya kudumu Viwanda, Biashara, Kilimo limepongeza mafanikio yaliyotokana na kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo nchini iliyoanza miezi kadhaa iliyopita. Pongezi hizo zimetolewa Machi 16,2026 na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Deodatus Mwanyika  wakati wa ziara ya kamati yake Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro walikofika kwa ajili ya kukagua utekelezaji wa kampeni hiyo ambapo ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa usimamizi mzuri wa kampeni hiyo kuanzia ngazi ya elimu kwa wafugaji. “Kwa kipindi hiki cha miezi michache ambayo kazi hii imeanza tayari nchi yetu imefungua baadhi ya masoko na imesafisha jina lake kuwa ni moja ya nchi zilizoingia kwenye mpango mkubwa wa chanjo hivyo sisi tunaipongeza sana Serikali ya awamu ya 6 lakini kwa namna ya pekee tunaipongeza sana Wizara ya Mifugo na Uvuvi” Ameongeza Mhe. Mwanyika. Aidha Mhe. Mwanyika am...

BUNGE LAKOSHWA UWEPO WA MELI YA KWANZA YA UVUVI NCHINI

Picha
◼️Nyingine 2 zipo kwenye mchakato wa manunuzi Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzani kupitia Kamati yake ya kudumu ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imefurahishwa na uwepo wa meli ya kwanza ya Uvuvi nchini iliyotia nanga kwenye gati la Shirika la Uvuvi nchini (TAFICO) siku chache zilizopita. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Deodatus Mwanyika mara baada ya kukagua utendaji kazi wa meli hiyo wakati wa ziara ya kamati hiyo iliyofanywa kwenye shirika hilo Machi 13,2026 jijini Dar-es-salaam. “Tumefarijika sana kama kamati kwa sababu jambo hili la meli ni jambo lililoongelewa ndani ya bunge kwa muda mrefu sana tangu 2021 na kwenye usimamizi wetu moja ya mambo tuliyoyaona ni kuona mchango wa sekta ya Uvuvi unaweza kuwa mkubwa zaidi ya hapa ulipofika” Ameongeza Mhe. Mwanyika. Aidha Mhe. Mwanyika amesisitiza kuwa sekta hiyo inagusa watu wa kawaida hivyo endapo watapatikana samaki wa kutosha wanaweza kuuzwa ndani ya mkoa wa Dar-es-salaam na nje ya hapo na hivyo kunufaisha k...