SERIKALI NA BROOKE EAST AFRICA KUIMARISHA USTAWI NA ULINZI WA PUNDA NCHINI
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuimarisha mikakati na hatua mbalimbali zinazolenga kuboresha ustawi wa punda nchini, ikiwemo upatikanaji wa lishe bora, maji, huduma za afya, ulinzi pamoja na matumizia salama ya wanyama hao. Akizungumza leo Juni 9, 2026 jijini Dodoma wakati wa kikao na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Brooke East Africa, Dkt. Raphael Kinoti, pamoja na watendaji wa shirika hilo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha ustawi na usalama wa mifugo akiwemo punda unaendelea kuimarika kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa vya ustawi wa wanyama. Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kufanya maboresho ya sera, sheria na kanuni zinazosimamia sekta ya mifugo ili kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo na kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo. “Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha mfumo wa sera na sheria zinazolinda mifugo ili kuendan...