Machapisho

VIJANA 3,004 WAOMBA MITAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amesema jumla ya maombi 3,004 kwa ajili ya kuwawezesha mitaji vijana wanaojishughulisha na sekta za mifugo na uvuvi yamepokelewa na Wizara huku uchambuzi wa waombaji waliokidhi vigezo ukiendelea.  Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo leo Mei 26, 2026 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Bunda Mjini Mhe. Ester Amos Bulaya (CCM) aliyehoji ni lini vijana wa Bunda watanufaika na Mradi wa Ufugaji Samaki wa Vizimba kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi? “Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI pamoja na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), ilitangaza Machi 4, 2026 fursa ya mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 23.68 kwa ajili ya vijana wanaojihusisha na sekta za mifugo na uvuvi, hadi sasa jumla ya maombi 3,004 yamepokelewa kutoka maeneo mbalimbali nchini, yakiwemo ya vijana kutoka Bunda, huku uchambuzi ukiendelea ili kupata waombaji wal...

DKT. MADELE AWATAKA WATENDAJI SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU

Picha
◾ Awataka Watendaji hao kuja na Mikakati Mudhubuti ya kudhibiti Uvuvi haramu. ◾ Abainisha Mpango wa Wizara kutenga Hekta 196,324.25 kwa ajili ya Malisho. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Magawa Madele, amewataka Makatibu Tawala Wasaidizi wa Uchumi na Uzalishaji, Madaktari wa Mifugo na Uvuvi wa Mikoa, Maafisa Uvuvi wa Mikoa na Wakuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kufanya kazi kwa weledi, uwajibikaji, uadilifu na uzalendo mkubwa ili kuleta mabadiliko katika Sekta hizo mbili na Taifa kwa ujumla. Akizungumza kwa Niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, leo Mei 25, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao kazi kilichojumuisha Wataalam mbalimbali wa Taasisi za Serikali wa Sekta hizo mbili za Mifugo na Uvuvi, Dkt. Madele amesema lengo la Kikao hicho ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji na usimamizi wa vipaumbele vya Wizara kwa mwaka wa fedha 2026/2027, na kusaidia kutoa mwelekeo na Mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa vipaumbele hivyo. "Ni ma...
Picha
WATAALAM 155 WA WANYAMA WAPATIWA USAJILI  Na. Stanley Brayton, WMUV ◾ Vituo 69 kupewa Usajili katika Utoaji Huduma za Afya ya Wanyama. Baraza la Veterinari Tanzania (VCT) limekamilisha mapitio kwa ajili ya kusajili Wataalam wa Wanyama wenye sifa stahiki, pamoja na Vituo mbalimbali vya kutoa Huduma za Afya ya Wanyama, ikiwa ni moja ya utekelezaji wa Sheria ya Veterinari SURA 319. Akizungumza katika Kikao cha 63 cha Baraza, leo Mei 23 2026 Jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Baraza la Veterinari Tanzania (VCT), ambaye  ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Prof. Lughano Kusiluka amesema Baraza limepitia na kuridhia kuwapa usajili Wataalam wa Wanyama 155 na Vituo vya Utoaji Huduma za Wanyama 69, ikiwa ni moja ya utekelezaji wa majukumu ya Baraza hilo. “usajili huu umefanyika kwa kuzingatia Sheria ya Veterinari SURA 319, pamoja na Kanuni mbalimbali na miongozo ambayo imeangalia uhalali na vigezo mbalimbali stahiki vya Wataalam” amesema Prof. Kusiluka Aidha, Prof. Kusiluka amewa...

TALIRI YAPONGEZWA KWA KUWEKEZA KWENYE UZALISHAJI WA MALISHO YA MIFUGO

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Fabian Madele ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa juhudi zake za kuwekeza katika uzalishaji wa malisho na mbegu bora za malisho ya mifugo, hatua aliyosema ni muhimu katika kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa malisho nchini. Dkt. Madele ametoa pongezi hizo leo Mei 22, 2026 wakati wa ziara yake ya kikazi katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kituo cha West Kilimanjaro kwa lengo la kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo. Akizungumza katika ziara hiyo, Dkt. Madele amesema sekta ya mifugo inaendelea kukabiliwa na changamoto ya upungufu wa malisho kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, hivyo uwekezaji unaofanywa na TALIRI ni hatua muhimu ya kuimarisha ufugaji wenye tija na kuongeza uzalishaji. Aidha, Dkt. Madele amewataka wataalamu wa TALIRI kuendelea kutoa elimu kwa wafugaji kuhusu mbinu bora za ufugaji wa kisasa i...

BWAWA LA LITA MILIONI 1.2 LAJENGWA TALIRI KUIMARISHA UZALISHAJI WA MALISHO YA MIFUGO

Picha
Katika jitihada za kuimarisha uzalishaji wa malisho ya mifugo na kuongeza uwezo wa wafugaji kukabiliana na athari za ukame, Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Kanda ya Kaskazini imefanikiwa kujenga bwawa lenye uwezo wa kuhifadhi lita milioni 1.2 za maji kwa ajili ya shughuli za umwagiliaji katika eneo la shamba darasa la uzalishaji wa malisho ya mifugo. Mradi huo unatekelezwa kupitia programu ya kuwajengea uwezo wafugaji na kuimarisha mifumo ya ufugaji kwa familia za kifugaji sambamba na kuchangia uendelevu wa usalama wa chakula nchini. Bwawa hilo lina uwezo wa kuhakikisha upatikanaji wa maji ya uhakika kwa shughuli za umwagiliaji katika shamba darasa lenye ukubwa wa ekari moja kwa kipindi cha hadi miezi mitatu bila kujazwa tena. Hatua inatarajiwa kuongeza ufanisi wa uzalishaji wa malisho hata katika vipindi vya ukame vinavyosababishwa na mabadiliko ya tabia nchi. Akizungumza baada ya kukagua mradi huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta y...

DKT. BASHIRU ATAKA MKAKATI WA TASNIA YA KUKU UZINDULIWE NANE NANE 2026

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa ameiagiza Ofisi ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo pamoja na Watendaji wake kuhakikisha inakamilisha uandaaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Kuendeleza Tasnia ya Kuku nchini na kuuzindua mkakati huo wakati wa Maonesho ya Nane Nane ya Mwaka huu 2026. Balozi Dkt. Bashiru amesema hayo wakati  akifungua rasmi Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Wadau kuhusu Kilimo cha Mikataba, Uwezeshaji wa Fedha kwa Wakulima na Maendeleo ya Vyama vya Wakulima uliofanyika jijini Dodoma leo Mei 22, 2026 ambapo ameeleza kuwa kukamilishwa na kuzinduliwa kwa mkakati huo kutasaidia kuirasimisha tasnia ya kuku ambayo ina mchango mkubwa kwa uchumi na usalama. "Tatizo Kubwa tulilonalo pamoja na sekta hii kuwa kubwa, ni sekta  ambayo haijarasimishwa wala kupewa hadhi inayostahili, ndio maana ndani ya wizara tunaandaa Mkakati wa Kitaifa wa Maendeleo ya sekta ya Kuku, Napenda kuelekeza Ofisi ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wataalam wenzake nahitaji...

DKT. BASHIRU AAGIZA KUFANYIKA TATHMINI MIUNDOMBINU YA KUFUGIA SAMAKI - NANE NANE

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amemwagiza Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kufanya tathmini ya miundombinu ya kufugia samaki kutoka kwa Mwekezaji Hawa Fish Farm ili eneo hilo litumike kwa ajili ya Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT Uvuvi). Balozi Dkt. Bashiru ametoa agizo hilo leo Mei 21, 2026 wakati alipotembelea na kukagua Mabwawa ya Kufugia Samaki ya  Mwekezaji Hawa Fish Farm yaliyopo Viwanja vya Nane Nane vya John Malecela jijini Dodoma, ambapo mwekezaji huyo amesema anaondoka na kwenda kuwekeza sehemu nyingine. "Hatuwezi kuendesha shughuli za kiserikali zinazohusu watu bila kuwa karibu nao na kurahisisha mawasiliano, Nataka maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Viumbe maji kwa nini tumechelewa kumpa majibu mwekezaji huyu kutokana na mapendekezo yake?, Pia ifanyike tathmini ya miundombinu  hii kama inafaa kwa shughuli gani? amesema Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, Balozi Dkt. Bashiru ameongeza kwa kuitaka idara hiyo kuja na wazo mbadala la...