MAFUNZO REJEA YA MAAFISA UGANI YAZINDULIWA NCHINI
Na. Fausta Njelekela ◾Wizara kuendelea kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa kununua pikipiki 200. Wizara ya Mifugo na Uvuvi yaanza kutoa Mafunzo rejea kwa Maafisa Ugani wa Mifugo na Uvuvi ambapo mafunzo hayo yenye lengo la kuwafundisha maafisa Ugani masuala mbalimbali ikiwemo kuzingatia ufugaji na uvuvi endelevu, usimamizi endelevu wa rasilimali za mifugo na uvuvi pamoja na sheria na kanuni mbalimbali zinazosimamia sekta za mifugo na uvuvi. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa hafla hiyo iliyofanyika Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma Machi 3, 2026, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Dkt. Fabian Madele amesema mafunzo hayo ni moja ya hatua na mikakati iliyowekwa na wizara ya kuhakikisha inaimarisha huduma za ugani kwa kutoa mafunzo rejea kwa maafisa ugani ili kujenga uelewa wa pamoja katika masuala mbalimbali ya kitaalamu yanayolenga kuongeza tija katika uzalishaji ili kufikia malengo ya kitaifa na kimataifa yanayolenga kuimarisha usalama wa chakula, kuongeza kipato kw...