Machapisho

DKT. BASHIRU AHIMIZA KUDHIBITI UVAMIZI MASHAMBA YA MIFUGO

Picha
 ◾Awataka Watendaji wa Wizara kuendelea kufanya kazi Kisayansi Na. Stanley Brayton, WMUV Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewahimiza Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo kudhibiti uvamizi wa mashamba ya Mifugo na maeneo ya Uzalishaji wa Mifugo na Uvuvi ili maeneo hayo yaweze kutimiza malengo yaliyokusudiwa ya kuwa maeneo ya kuzalisha mazao ya Mifugo na Uvuvi. Akizungumza leo Mei 9, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo, Dkt. Bashiru amesema kuwa mashamba ya Mifugo yamekuwa na changamoto kubwa kiasi cha maeneo hayo kumegwa na kufanyiwa matumizi mengine bila kufuata utaratibu wa kisheria. "siridhishwi na uvamizi wa mashamba ya Mifugo, na umegaji wa maeneo hayo ambayo yalikuwa yamepangwa kwa ajili ya shughuli za Uzalishaji Mifugo" amesema Dkt. Bashiru  Aidha, Dkt. Bashiru amewataka Watendaji Wakuu wa Wizara kuhakikisha Sekta za Mifugo na Uvuvi zinaendeshwa Kisayansi ili kuweza kuboresha Sekta hizo ambazo ni miongoni ...

SERIKALI YAENDELEA KUSISITIZA ULINZI NA USTAWI WA PUNDA AFRIKA

Picha
Na Chiku Makwai – Geita Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda na kuhifadhi punda kama rasilimali muhimu katika maendeleo ya jamii, hususan kwa wananchi wa maeneo ya vijijini wanaotegemea wanyama hao katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Punda Duniani yaliyofanyika leo Mei 8, 2026 katika eneo la Mgusu mkoani Geita, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo, amesema siku hiyo inalenga kuhamasisha jamii kutambua mchango mkubwa wa punda katika ustawi wa maisha na uchumi wa wananchi. Aidha, Mhe. Komba amesema Serikali inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuzingatia haki za ustawi wa wanyama kama zilivyoainishwa katika Sheria ya Ustawi wa Wanyama Na. 19 ya mwaka 2008, ikiwemo haki ya kupata chakula na maji, kutoteswa, kupatiwa matibabu, kuishi bila hofu pamoja na kuwekwa katika mazingira yanayoruhusu kuonesha tabia zao za asili. Amesisitiza kuwa ...

BI. MEENA AWATAKA WATUMISHI LITA KUENDELEA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA UWELEDI NA UBUNIFU

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amewataka Watumishi wa Taasisi ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uweledi, ubunifu, uchapakazi na uhadilifu mkubwa ili kuweza kuleta matokeo chanya katika Taasisi yao na Sekta ya Mifugo kiujumla.  Akizungumza leo Mei 8, 2026 Jijini Dodoma katika Mkutano wa Kumi na Tatu (13) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi LITA, Bi. Meena amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaitegemea LITA katika kuleta chachu ya mabadiliko ambayo itasaidia kuboresha Sekta ya Mifugo na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa. "Ili kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi ni muhimu kuwa na watumishi ambao wanajituma na kutekeleza wajibu wao kama ambavyo inatakiwa kwa uadilifu na kwa wakati" amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena ameitaka LITA kuwa wabunifu zaidi na kuimarisha ushirikiano na Taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi, katika kuboresha T...

HUDUMA ZA MATIBABU NA ELIMU YA USTAWI WA PUNDA ZAANZA KUTOLEWA GEITA

Picha
Na Chiku Makwai-Geita,  Wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na taasisi zilizo chini yake, kwa kushirikiana na Shirika la INADES-Formation Tanzania na Shirika la ASPA, wameanza  zoezi la kliniki ya matibabu kwa mnyama punda linaloambatana na utoaji wa elimu kuhusu ustawi wa punda katika vituo vya Magogo, Magenge na Mgusu mkoani Geita. Zoezi hilo linalofanyika kwa siku tatu lina lenga kuwapatia wafugaji na watumiaji wa punda elimu kwa vitendo kuhusu matumizi sahihi ya teknolojia bora za vifaa vya kazi, huduma za afya pamoja na utunzaji bora wa punda ili kuongeza ustawi na tija ya mnyama huyo. Aidha, wataalamu hao wametoa huduma mbalimbali za matibabu kwa punda ikiwemo uchunguzi wa afya, tiba na ushauri wa namna bora ya kuwahudumia wanyama hao ili kuepusha magonjwa na mateso yasiyo ya lazima. Zoezi hilo limeanza Mei 6, 2026 na linatarajiwa kuhitimishwa kesho Mei 8, 2026 sambamba na maadhimisho ya Siku ya Punda Kitaifa yatakayofanyika mkoani Geita ambapo Mgeni Rasmi a...

KAMATI YA BAJETI YAIPONGEZA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imeipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kusimamia na kutekeleza vyema ujenzi wa mradi wa kielelezo wa bandari ya uvuvi ya Kilwa Masoko unagharimu shilingi Bilioni 280 ambo kukamilika kwake kunakadiriwa kuzalisha ajira 30,000 katika mnyororo mzima wa thamani wa sekta ya uvuvi nchini. Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Mashimba Ndaki kwa niaba ya wajumbe wa kamati hiyo, wakati wa kikao cha uwasilishwaji wa  taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko na Ununuzi wa Meli za Uvuvi wa Bahari Kuu uliofanywa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi jijini Dodoma Mei 06, 2026. Akizungumza baada ya kupokea taarifa hiyo, Mhe. Ndaki alimpongeza Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa na timu yake ya wataalam kwa kuweza kusimamia vyema maono ya Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Niwapongeze Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuendelea na mradi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko, tusiwe na ...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI IMEFUNGUA MAFUNZO YA UFUATILIAJI WA VYOMBO VYA UVUVI (VESSEL MONITORING SYSTEM – VMS & AIS)

Picha
Na Herry Kilele – Bagamoyo, Pwani Wizara ya Mifugo na Uvuvi imefungua mafunzo ya siku tano kwa wataalamu wa Sekta ya Uvuvi yenye lengo la kujenga uelewa wa matumizi ya mifumo ya ufuatiliaji wa vyombo vya uvuvi (VMS na AIS), hatua inayolenga kuimarisha usimamizi wa rasilimali za uvuvi na kukabiliana na uvuvi haramu nchini. Akizungumza Mei 5, 2026 wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, akimuwakilisha Mkurugenzi wa Uvuvi, Bi. Lilian Ibengwe, Afisa Uvuvi Mwandamizi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, alisema: “Tanzania imebahatika kuwa na rasilimali nyingi za uvuvi, jambo linaloiweka nchi miongoni mwa mataifa 10 yanayoongoza kwa uzalishaji wa samaki kutoka maji ya asili Barani Afrika.” Alibainisha kuwa Sekta ya Uvuvi inachangia asilimia 1.8 ya Pato la Taifa na kutoa ajira kwa zaidi ya Watanzania milioni 6. Aidha, alieleza kuwa pamoja na mchango huo mkubwa, bado kuna changamoto ya kiwango cha chini cha ulaji wa samaki kwa Mtanzania, ambacho ni wastani wa kilo 7.9 kwa mtu kwa mwaka, ikilinganishw...

UHABA WA MALISHO YA MIFUGO UNAVYOMNYIMA USINGIZI DKT. BASHIRU

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb) amesema ili kumaliza changamoto ya uhaba wa malisho ya mifugo, wafugaji lazima wawe na usimamizi mzuri wa mpango wa matumizi bora ya ardhi katika kuzalisha malisho yatakayokidhi mifugo yao. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ameeleza hayo wakati alipotembelea Shamba la kuzalisha Malisho la Langwira Mbarali Mkoani Mbeya Mei 03, 2026 ambapo ameeleza kuwa ukosefu wa malisho  ya mifugo kwa wafugaji hasa kipindi cha kiangazi umekuwa ukimnyima usingizi kutokana na adha wanayopata wafugaji nchini. “Nilikuwa Sijui kama Mawaziri wa Mifugo na Uvuvi huwa hawalali kwa sababu ya wafugaji kukosa malisho,mimi kikianza Kiangazi silali, suluhu ipo katika uzalishaji wa malisho, kwa hiyo ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi lazima tuwe na mpango mzuri wa matumizi bora ya ardhi, tuzalishe kisasa malisho halafu wakati wa kiangazi tuyatumie malisho yaliyohifadhiwa wakati wa  masika” alisema Mhe. Dkt. Bashiru. Pia, Mhe. Balozi Dkt. Bas...