Machapisho

SERIKALI KUIMARISHA MINADA YA KIMATAIFA YA MIFUGO NCHINI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha na kuimarisha Minada ya Kimataifa ya Mifugo katika maeneo ya kimkakati nchini, ikiwemo Jimbo la Tarime Vijijini mkoani Mara, kwa lengo la kukuza biashara ya mifugo na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wafugaji na wafanyabiashara. Kauli hiyo imetolewa leo Mei 18, 2026, Bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb) wakati akijibu swali la Mbunge wa Tarime Vijijini, Mhe. Mwita Mwikabe Waitara, ambaye alihoji ni lini Serikali itaanzisha Minada ya Kimataifa ya Mifugo katika jimbo hilo. “Serikali inatambua umuhimu wa kuboresha minada hiyo kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya mifugo katika eneo la Tarime Vijijini pamoja na ukaribu wake na mipaka ya nchi jirani, hali inayotoa fursa kubwa za biashara ya mifugo ndani na nje ya nchi.” Alisema Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, Dkt. Bashiru aliongeza kuwa  Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara ya m...

SERIKALI KUANDAA MWONGOZO WA KURAHISISHA UWEKEZAJI SEKTA YA UVUVI NCHINI

Picha
Serikali imeanza mchakato wa kuandaa Mwongozo ambao utaainisha fursa mbalimbali ili kurahisisha Uwekezaji katika Sekta ya Uvuvi kwa lengo la kuongeza tija katika Sekta hiyo. Akizungumza leo May 16, 2026 Jijini Dodoma kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakati wa Kikao kilichojumuisha Wataalam wa Taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi, ikiwemo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani (DRTE), Bw. Samwel Mdachi amesema kikao kazi hicho ni cha kuandaa Mwongozo wa fursa za Uwekezaji katika Sekta ya Uvuvi nchini. "lengo kuu la kikao hiki ni kuandaa nyenzo itakayosaidia kutangaza na kuelezea kwa kina fursa mbalimbali zilizopo katika Sekta ya Uvuvi na uchumi wa Buluu nchini." amesema Ndg. Mdachi Aidha, Ndg. Mdachi amebainisha kuwa Mwongozo huo unatarajiwa kuwa dira muhimu kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, kwa kuwa utaonesha maeneo yenye fursa, aina za uwekezaji zinazo...

SERIKALI, BENKI YA DUNIA ZAJADILI KUIMARISHA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Bashiru Ally Kakurwa, amekutana na Mkurugenzi wa Kanda wa Benki ya Dunia anayeshughulikia Sekta ya Mazingira kwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini, Bi. Anna Wellenstein, na kufanya mazungumzo yaliyolenga kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo katika kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi nchini. Mazungumzo hayo ni sehemu ya ziara ya ujumbe wa Benki ya Dunia nchini Tanzania iliyoanza leo Mei 11 hadi 13, 2026, ikiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na Benki hiyo katika sekta za maji, kilimo na mazingira. Majadiliano hayo yamejikita katika kutathmini utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Benki ya Dunia, ikiwemo Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Bahari Tanzania (TASFAM), pamoja na kubaini maeneo mapya ya ushirikiano yatakayochangia maendeleo endelevu ya wananchi na ukuaji wa uchumi wa Taifa. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu jijini Dodoma, Bi. Wellens...

SERIKALI YAKABIDHI MITAJI KWA VIJANA 47 WA BBT- UVUVI KAGERA

Picha
Na. Fausta Njelekela  Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Erasto Sima ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, amesema Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia Sekta ya Uvuvi ili kukabiliana na changamoto ya ajira nchini. Mhe. Sima  amesema hayo Mei 9, 2026 katika hafla ya kukabidhi mitaji kwa njia ya mikopo yenye masharti nafuu kwa vijana 47 walionufaika na Programu ya Jenga Kesho Iliyobora (BBT–Uvuvi) iliyofanyika Katika Mwalo wa Bilolo Kemondo Bukoba.  “Programu hii inalenga kutoa mafunzo kwa vitendo pamoja na mitaji ili kuwawezesha vijana kujiajiri na kuwa wawekezaji katika Sekta ya Uvuvi,” amesema Mhe. Sima Aidha, Mhe. Sima amesema kuwa hafla hiyo ni mwendelezo wa ugawaji wa mitaji uliozinduliwa Machi 7, 2026 katika eneo la FETA Nyegezi mkoani Mwanza, ambapo vijana 55 walikabidhiwa pembejeo mbalimbali za ufugaji wa samaki kwa vizimba. Mhe. Sima amewataka wanufaika hao kutumia fursa waliyopewa kwa uwajibikaji, nidhamu na uadilifu ili kuhakikisha miradi...

DKT. BASHIRU AHIMIZA KUDHIBITI UVAMIZI MASHAMBA YA MIFUGO

Picha
 ◾Awataka Watendaji wa Wizara kuendelea kufanya kazi Kisayansi Na. Stanley Brayton, WMUV Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amewahimiza Watendaji Wakuu wa Wizara hiyo kudhibiti uvamizi wa mashamba ya Mifugo na maeneo ya Uzalishaji wa Mifugo na Uvuvi ili maeneo hayo yaweze kutimiza malengo yaliyokusudiwa ya kuwa maeneo ya kuzalisha mazao ya Mifugo na Uvuvi. Akizungumza leo Mei 9, 2026 Jijini Dodoma katika Kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo, Dkt. Bashiru amesema kuwa mashamba ya Mifugo yamekuwa na changamoto kubwa kiasi cha maeneo hayo kumegwa na kufanyiwa matumizi mengine bila kufuata utaratibu wa kisheria. "siridhishwi na uvamizi wa mashamba ya Mifugo, na umegaji wa maeneo hayo ambayo yalikuwa yamepangwa kwa ajili ya shughuli za Uzalishaji Mifugo" amesema Dkt. Bashiru  Aidha, Dkt. Bashiru amewataka Watendaji Wakuu wa Wizara kuhakikisha Sekta za Mifugo na Uvuvi zinaendeshwa Kisayansi ili kuweza kuboresha Sekta hizo ambazo ni miongoni ...

SERIKALI YAENDELEA KUSISITIZA ULINZI NA USTAWI WA PUNDA AFRIKA

Picha
Na Chiku Makwai – Geita Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa kulinda na kuhifadhi punda kama rasilimali muhimu katika maendeleo ya jamii, hususan kwa wananchi wa maeneo ya vijijini wanaotegemea wanyama hao katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii. Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Punda Duniani yaliyofanyika leo Mei 8, 2026 katika eneo la Mgusu mkoani Geita, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye alikuwa mgeni rasmi wa maadhimisho hayo, amesema siku hiyo inalenga kuhamasisha jamii kutambua mchango mkubwa wa punda katika ustawi wa maisha na uchumi wa wananchi. Aidha, Mhe. Komba amesema Serikali inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuzingatia haki za ustawi wa wanyama kama zilivyoainishwa katika Sheria ya Ustawi wa Wanyama Na. 19 ya mwaka 2008, ikiwemo haki ya kupata chakula na maji, kutoteswa, kupatiwa matibabu, kuishi bila hofu pamoja na kuwekwa katika mazingira yanayoruhusu kuonesha tabia zao za asili. Amesisitiza kuwa ...

BI. MEENA AWATAKA WATUMISHI LITA KUENDELEA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KWA UWELEDI NA UBUNIFU

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amewataka Watumishi wa Taasisi ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uweledi, ubunifu, uchapakazi na uhadilifu mkubwa ili kuweza kuleta matokeo chanya katika Taasisi yao na Sekta ya Mifugo kiujumla.  Akizungumza leo Mei 8, 2026 Jijini Dodoma katika Mkutano wa Kumi na Tatu (13) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi LITA, Bi. Meena amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaitegemea LITA katika kuleta chachu ya mabadiliko ambayo itasaidia kuboresha Sekta ya Mifugo na kuchangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa. "Ili kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi ni muhimu kuwa na watumishi ambao wanajituma na kutekeleza wajibu wao kama ambavyo inatakiwa kwa uadilifu na kwa wakati" amesema Bi. Meena Aidha, Bi. Meena ameitaka LITA kuwa wabunifu zaidi na kuimarisha ushirikiano na Taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi, katika kuboresha T...