SERIKALI KUIMARISHA MINADA YA KIMATAIFA YA MIFUGO NCHINI
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha na kuimarisha Minada ya Kimataifa ya Mifugo katika maeneo ya kimkakati nchini, ikiwemo Jimbo la Tarime Vijijini mkoani Mara, kwa lengo la kukuza biashara ya mifugo na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wafugaji na wafanyabiashara. Kauli hiyo imetolewa leo Mei 18, 2026, Bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb) wakati akijibu swali la Mbunge wa Tarime Vijijini, Mhe. Mwita Mwikabe Waitara, ambaye alihoji ni lini Serikali itaanzisha Minada ya Kimataifa ya Mifugo katika jimbo hilo. “Serikali inatambua umuhimu wa kuboresha minada hiyo kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya mifugo katika eneo la Tarime Vijijini pamoja na ukaribu wake na mipaka ya nchi jirani, hali inayotoa fursa kubwa za biashara ya mifugo ndani na nje ya nchi.” Alisema Balozi Dkt. Bashiru. Aidha, Dkt. Bashiru aliongeza kuwa Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara ya m...