BANDARI ALIYOAHIDI MHE. DKT. SAMIA SASA IPO TAYARI – MHE. TELACK
Na Kilwa, Lindi Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, amesema Bandari ya Uvuvi ya Kilwa Masoko, ambayo iliahidiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ipo tayari kuanza kutoa huduma baada ya kufikia hatua za mwisho za ukamilishaji wake. Akizungumza leo Juni 25, 2026, wilayani Kilwa mkoani Lindi wakati wa zoezi la kihistoria la majaribio ya mitambo na miundombinu mbalimbali ya bandari hiyo, Mhe. Telack amesema kiwango cha ukamilishaji wa mradi huo kimefikia asilimia 99.99, huku hatua iliyobaki ikiwa ni kuwasha na kuthibitisha utendaji wa mitambo mbalimbali. Amesema miongoni mwa majaribio yaliyofanyika leo ni pamoja na kuwasha mitambo ya kuzalisha barafu, ambayo inauwezo wa kuzalisha barafu tani 100 kwa siku mitambo hiyo inauwezo wa kugandisha barafu kwa nyuzi joto 3 sentigredi. “Hii ni ishara kuwa Bandari yetu sasa iko tayari kuanza kazi, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameandika historia kwa kujenga Bandari ya kwanza ya kisasa ya uvuv...