Machapisho

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI MBIONI KUANZISHA KITUO CHA HUDUMA KWA WATEJA

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi ipo katika hatua za mwisho za kuanzisha Kituo cha Huduma kwa Wateja kitakacholenga kupokea, kusikiliza na kushughulikia changamoto za wadau wa sekta ya mifugo na uvuvi, sambamba na kutoa taarifa na ufafanuzi kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi kuhusu utoaji wa huduma bora kwa wateja yaliyofanyika leo, Julai 8, 2026, jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina, amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za wizara kuboresha utoaji wa huduma kwa wafugaji, wavuvi na wadau wengine wa sekta hizo. Dkt. Mhina amesema mafunzo hayo yanawahusisha wataalamu walioteuliwa kutoka idara na vitengo mbalimbali vya wizara, kwa lengo la kuwajengea uwezo na ujuzi katika utoaji wa huduma bora kwa wateja, ambao utakuwa msingi wa ufanisi wa Kituo cha Huduma kwa Wateja...

NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AIPONGEZA TALIRI KWA UTOAJI ELIMU YA UFUGAJI SABASABA

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Prof. Mohamed Sheikh, ameipongeza Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa namna ilivyojipanga kutoa elimu ya ufugaji na kuonesha teknolojia mbalimbali za kisasa katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, jijini Dar es Salaam. Prof. Sheikh ametoa pongezi hizo leo, Julai 4, 2026, alipotembelea banda la TALIRI na kujionea shughuli mbalimbali za uhamasishaji na utoaji elimu kwa wananchi pamoja na wadau wa sekta ya mifugo. Amesema jitihada zinazofanywa na Taasisi hiyo zinachangia kwa kiasi kikubwa kuwafikishia wafugaji teknolojia na maarifa yatakayosaidia kuongeza tija, uzalishaji na maendeleo ya sekta ya mifugo nchini. Akizungumza katika banda la TALIRI, Meneja wa Sehemu ya Uhaulishaji wa Teknolojia, Bw. Gilbert Msuta, amesema Taasisi imejipanga kuhakikisha wananchi na wadau wanaotembelea banda hilo wanapata elimu kuhus...

NAIBU KATIBU MKUU ARIDHISHWA NA HUDUMA ZA TVLA SABASABA

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh, leo Julai 4, 2026, ametembelea banda la Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea mabanda ya taasisi zilizo chini ya Wizara. Lengo la ziara hiyo lilikuwa kujionea maandalizi yaliyofanyika katika mabanda ya taasisi mbalimbali pamoja na kujiridhisha na ubora wa huduma na elimu inayotolewa kwa wafugaji, wavuvi na wananchi wanaotembelea maonesho hayo. Akiwa katika banda la TVLA, Prof. Sheikh alipokea maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na Wakala kutoka kwa Dkt. Julius Mwanandota, Daktari Mtafiti wa Mifugo. Huduma hizo ni pamoja na uchunguzi na utambuzi wa magonjwa ya mifugo, uzalishaji na matumizi sahihi ya chanjo za mifugo, uchunguzi wa ubora na usalama wa vyakula vya mifugo, usajili na uhakiki wa viuatilif...

IDARA YA UVUVI YAKUSANYA SHILINGI BILIONI 39.6 ZA MADUHULI KWA MWAKA WA FEDHA 2025/2026

Picha
Idara ya Uvuvi iliyo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekusanya Shilingi bilioni 39.6 za maduhuli katika mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni ongezeko kutoka Shilingi bilioni 32 zilizokusanywa katika mwaka uliopita, na mafanikio hayo yametokana na zoezi maalum la ufuatiliaji wa ukusanyaji wa maduhuli lililolenga kuimarisha ulipaji wa tozo stahiki, kuzuia utoroshaji wa mazao ya uvuvi na kuhakikisha utekelezaji wa sheria, kanuni na taratibu za uvuvi nchini. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kikao kazi cha utoaji wa taarifa ya ufuatiliaji na ukusanyaji wa maduhuli kilichofanyika Julai 4, 2026, jijini Dar es Salaam, Naibu Katibu wa Wizara hiyo (Uvuvi), Prof. Mohamed Sheikh, alisema kiasi kilichokusanywa kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 ni Shilingi bilioni 39.6, ambapo mwaka jana kiasi kilichokusanywa kilikuwa bilioni 32 tu. Alisema zoezi hilo lilitekelezwa katika kanda mbalimbali za uvuvi nchini, zikiwemo Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Kati, Kanda ya ...

BARAZA LA KISEKTA LA MAWAZIRI AFRIKA MASHARIKI LA KILIMO NA USALAMA WA CHAKULA LAKUTANA

Picha
Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Kilimo na Usalama wa Chakula la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) limekutana jijini Dar es Salaam kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kuleta mageuzi katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kwa lengo la kuongeza uzalishaji, kuimarisha usalama wa chakula na kuboresha lishe katika ukanda wa Afrika Mashariki. Akizungumza wakati wa Mkutano wa 19 wa Baraza hilo uliofanyika Julai 2, 2026, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, amesema wajumbe walijadili taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya mikutano iliyopita, hali ya usalama wa chakula na lishe katika ukanda wa Afrika Mashariki, utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Mifugo na Uvuvi, pamoja na maendeleo ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Kilimo katika Bara la Afrika (CAADP). Prof. Sheikh amesema Baraza hilo pia lilijadili mikakati mbalimbali ya kuimarisha maendeleo ya sekta hizo, ikiwemo Mkakati wa Kuendeleza Zao la...

BIMA YA KIDIGITALI YA MIFUGO YAZINDULIWA

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amezindua Bima ya Kidigital ambayo imewezeshwa kwa ushirikiano baina ya Kampuni ya Bima ya CRDB pamoja na Kampuni ya ACRE Africa ambayo itatumia teknolojia ya kisasa kulinda mali za wafugaji nchini. Akizungumza leo Juni 29, 2026, katika Uzinduzi wa Bima ya Kidigitali ya Mifugo ijulikanayo kama Smart Mifugo, katika Hoteli ya Serena iliyopo Jijini Dar es Salaam, Bi. Meena amesema katika kukabiliana na changamoto za wafugaji, Kampuni ya Bima ya CRDB pamoja na Kampuni ya ACRE Africa, zimeleta suluhisho la ubunifu ambalo linatumia teknolojia ya kisasa kulinda mali za wafugaji wetu kupitia Smart Mifugo, na wafugaji kwa sasa wanaweza kupata bima kwa urahisi zaidi kwa njia ya kidijitali, salama na yenye uwazi. "Nimejulishwa kuwa kutakuwa na mfumo wa DigiBima App unaorahisisha usajili, malipo ya bima, na uwasilishaji wa madai, ambayo ni hatua muhimu katika kupeleka huduma karibu zaidi na wananchi, hususan wafugaji walioko vi...

BI. MEENA AMTAKA MKANDARASI KUKAMILISHA SOKO LA SAMAKI KIPUMBWI KWA WAKATI

Picha
◾Mradi wafikia asilimia 60 za utekelezaji. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya World Class Engineering Contractors Limited kuongeza kasi ya ujenzi wa Soko la Samaki la Kipumbwi, lililopo Wilaya ya Pangani, mkoani Tanga, ili mradi huo ukamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa Wavuvi na wadau wa Sekta. Akizungumza leo Juni 27, 2026, wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Masoko ya Samaki Mkoani Tanga, Bi. Meena amesema Soko la Samaki la Kipumbwi ni miundombinu muhimu kwa maendeleo ya Sekta ya Uvuvi, kwani litawawezesha wavuvi na wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi kuongeza thamani ya bidhaa zao, kukuza biashara na kuinua vipato vyao, hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla. Amesema pamoja na umuhimu wa mradi huo, utekelezaji wake umefikia asilimia 60 pekee, huku ukitarajiwa kukamilika ifikapo Juni 30, 2026. "Fedha zote za mradi zipo tayari, hivyo ni wajibu wa mkanda...