Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2026

SERIKALI KUANDAA MWONGOZO WA ULINZI NA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UVUVI NCHINI

Picha
 Na. Stanley Brayton, WMUV Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza kuandaa Mwongozo wa Utendaji Kazi kwa ajili ya Shughuli za Ulinzi na Usimamizi wa Rasilimali za Uvuvi nchini ikiwa na lengo la kuandaa Mwongozo ambao utawezesha utekelezaji wa majukumu ya Usimamizi wa Rasilimali hizo kufanyika kwa ufanisi zaidi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali inayotumika katika Sekta ya Uvuvi. Akizungumza leo Juni 11, 2026 Mkoani Morogoro, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Uvuvi Nchini, katika Kikao kazi cha Kuandaa Mwongozo huo, Mkurugenzi Msaidizi wa Uvuvi Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Christian Nzowa amesema kuwa Wizara imekutana na wadau mbalimbali kutoka Halmashauri zenye Maeneo ya Uvuvi wa mwambao wa Ziwa Victoria, Tanganyika, Nyasa, Maji Madogo na Bahari ya Hindi, pamoja na Maafisa Wandamizi Wastaafu wa Uvuvi na Maafisa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ili kupitia Mwongozo wa kiutendaji ujulikanao kama Standard Operating Procedure SOPs, na ambao utat...

SERIKALI NA BROOKE EAST AFRICA KUIMARISHA USTAWI NA ULINZI WA PUNDA NCHINI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kuimarisha mikakati na hatua mbalimbali zinazolenga kuboresha ustawi wa punda nchini, ikiwemo upatikanaji wa lishe bora, maji, huduma za afya, ulinzi pamoja na matumizia salama ya wanyama hao. Akizungumza leo Juni 9, 2026 jijini Dodoma wakati wa kikao na Mkurugenzi wa Kanda wa Shirika la Brooke East Africa, Dkt. Raphael Kinoti, pamoja na watendaji wa shirika hilo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Serikali imejipanga kuhakikisha ustawi na usalama wa mifugo akiwemo punda unaendelea kuimarika kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa vya ustawi wa wanyama. Ameongeza kuwa Serikali inaendelea kufanya maboresho ya sera, sheria na kanuni zinazosimamia sekta ya mifugo ili kuendana na mahitaji ya sasa ya maendeleo na kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo. “Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha mfumo wa sera na sheria zinazolinda mifugo ili kuendan...

BI. MEENA ATAKA UTAFITI KUWA CHACHU YA MAENDELEO YA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena, amesema kuwa utafiti una nafasi kubwa katika kuleta mageuzi na maendeleo endelevu ya sekta za mifugo, uvuvi na ukuzaji viumbe maji nchini, hivyo ni muhimu kuhakikisha agenda za utafiti zinaendana na mahitaji ya sasa na ya baadaye ya Taifa. Bi. Meena amesema hayo leo Juni 9, 2026, wakati akifungua Warsha ya Wadau ya Kupitia Ajenda za Taifa za Utafiti wa Mifugo pamoja na Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji za mwaka 2026–2030 iliyofanyika katika Ukumbi wa Brand Hotel jijini Dodoma. Amesema uwepo wa wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali, sekta binafsi, vyuo vikuu, taasisi za utafiti, mashirika ya maendeleo, mamlaka za serikali za mitaa na wadau wengine wa sekta hizo unaonesha dhamira ya pamoja ya kutambua mchango wa utafiti katika kukuza uchumi wa Taifa. "Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuimarisha shughuli za utafiti kwa kuanzisha taasisi maalumu za utafiti ambazo ni Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania ...

PROF. SHEIKH AAGIZA MABWAWA YA KITUO CHA UKUZAJI VIUMBEMAJI KINGOLWIRA KUFANYIWA MAJARIBIO YA MWISHO IFIKAPO JUNI 30

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bi. Agnes Meena, ameagiza kufanyika kwa majaribio ya mwisho ya mradi wa mabwawa kumi (10) ya kufugia samaki unaotekelezwa katika Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira mkoani Morogoro ifikapo Juni 30, 2026 ili kuhakikisha miundombinu hiyo inaanza kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa ya kuongeza uzalishaji wa vifaranga bora vya samaki nchini. Prof. Sheikh ametoa maelekezo hayo leo Juni 8, 2026, alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), ikiwemo ukarabati wa kituo cha kutotolesha vifaranga na jengo la mitambo ya umeme pamoja na uchimbaji wa visima na usakinishaji wa pampu za maji. Amesema Serikali ina matarajio makubwa ya kukifanya Kituo cha Kingolwira kuwa kituo kikuu cha kitaifa cha ukuzaji viumbemaji na shamba darasa kwa ajili ya mafunzo, uzalishaji wa vifaranga bora na uhamasishaji wa tek...

DKT. BASHIRU AVUTIWA NA UWEKEZAJI SEKTA YA MIFUGO LEMOTI - MONDULI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa amevutiwa na Mfugaji na Mwekezaji wa mfano Bw. Isaya Ole Mpekure anayemiliki ng'ombe zaidi ya 2,000 mitambo na ghala la kuhifadhia chakula cha mifugo ambapo shamba hilo limekuwa kitovu cha jamii ya wafugaji wa eneo hilo kuboresha mifugo yao na kufuga kwa tija. Amesema serikali itaendelea na mikakati ya kuendeleza sekta ya mifugo ikiwa ni pamoja na utoaji wa huduma za chanjo na utambuzi wa mifugo ili kudhibiti magonjwa,usimamizi na uendelezaji wa ardhi ya malisho na uimarishaji wa mbegu za mifugo na miundombinu ya ufugaji ili kuongeza uzalishaji na kuwakwamua wafugaji nchini. Kauli hiyo ya Waziri Balozi Dkt. Bashiru Juni 7, 2026 akiwa kwenye ziara yake wilayani Monduli Mkoani Arusha ziara  iliyolenga kukagua utekelezaji wa shughuli za mifugo, uwekezaji wa sekta ya mifugo wa Bw. Isaya Ole Mkupure na kushiriki sherehe za kimila za jamii ya wamasai katika kijiji cha Lemote. Katika hatua nyingine Balozi Dkt. Bashiru alisis...

SERIKALI KUONGEZA WIGO TATHMINI YA ATHALI ZA UVAMIZI WA MAJI MONDULI

Picha
Serikali imesema itaongeza wigo kutathmini athari za uvamizi wa maji kutoka Ziwa Manyara kwenye makazi ya wananchi wa Kijiji cha Jangwani Kata ya Mto wa Mbu wilayani Monduli Mkoani Arusha ambapo takriban makazi ya wananchi 600 yameathiriwa. Kauli hiyo imetolewa Juni 06, 2026 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Mb) baada ya kufika katika kijiji hicho na kushuhudia athari za uvamizi wa maji katika makazi hayo ambapo amesema atazungumza na timu ya tathmini ya dharura athari hizo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu  kupanua wigo zaidi wa tathmini. “ Kutokana na athari hizi nimeona jinsi nyumba zilivyovamiwa na maji  nikirudi Dodoma nitazungumza na timu ya tathmini ya athari hizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ili tupanue wigo wa tathmini tusiishie kuangalia kuhusu dharura bali tuangalie kwa kina zaidi pia hata kiuchumi” amesema Dkt. Bashiru Alisema pamoja na mambo mengine tathmini hiyo pia itaangalia namna ya kuwawezesha wananchi kufanya shughuli za kiuchumi ...

NAIBU KATIBU MKUU UVUVI AAGIZA MIUNDOMBINU YOTE YA BANDARI KILWA MASOKO KUFANYIWA MAJARIBIO YA MWISHO MARA MOJA

Picha
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Sheikh, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Agnes Meena, ameagiza kukamilishwa mara moja kwa shughuli za upimaji na uingizaji katika matumizi (Testing and Commissioning) ya miundombinu yote ya mradi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko, ndani ya juma lijalo kutoka sasa, ili kuwezesha kuanza kutumika kwa wakati uliopangwa. Prof. Sheikh ametoa maagizo hayo  wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi huo ambao umefikia asilimia 98.9 ya ukamilishaji, leo 06 Juni 2026, Kilwa mkoani Lindi.  Katika ziara hiyo, Prof. Sheikh alikagua maeneo mbalimbali ya mradi ikiwemo mtambo wa kuzalisha barafu, vyumba vya ubaridi, eneo la kufanyia maandalizi ya samaki, jengo la kupoozea umeme, miundombinu ya kiutawala, karakana ya kutengeneza meli pamoja na gati la kuegeshea meli. Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, Prof. Sheikh alisema ni muhimu kuhakikisha mifumo na vifaa vyote vinafanyiwa upimaji wa kina na ...

SERIKALI YATOA ONYO DHIDI YA UVAMIZI WA ARDHI YA MIFUGO NCHINI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ametoa onyo kwa wananchi wanaovamia ardhi ya Karantini ya Mifugo yenye ukubwa wa ekari 2,176 iliyopo Makuyuni, Halmashauri ya Wilaya ya Monduli mkoani Arusha, akisisitiza kuwa eneo hilo lilitengwa na Serikali kwa ajili ya shughuli za ufugaji wa kisasa. Mhe. Balozi Dkt. Bashiru ametoa onyo hilo leo Juni 6, 2026, baada ya kutembelea na kukagua eneo hilo na kueleza kuwa kati ya eneo hilo, ekari 510 tayari zimetolewa kwa Halmashauri ya Monduli kwa ajili ya upanuzi wa Mji wa Makuyuni pamoja na ujenzi wa machinjio ya kisasa yatakayochochea ukuaji wa uchumi wa halmashauri hiyo. “Tunataka kutumia maeneo yetu kufanya maendeleo ya kisasa ya sekta ya mifugo, wapo baadhi ya watu wanaochochea migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi. Ardhi ya mifugo iliyotengwa inapaswa kutumika kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya mifugo kisasa,” amesema Balozi Dkt. Bashiru. Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mhe. Isaac Joseph...

SERIKALI YAJA NA MIKAKATI YA KUKABILIANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

Picha
Na. Fausta Njelekela  Serikali imeandaa mikakati mbalimbali ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na uharibifu wa mazingira ili kufikia azma ya kuwa na Tanzania ya kijani ifikapo mwaka 2050. Akizungumza leo Juni 5, 2026, wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre (JKCC) jijini Dodoma, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amesema Tanzania inatarajiwa kuwa na watu milioni 118 ifikapo mwaka 2050, jambo litakaloongeza mahitaji ya rasilimali muhimu zinazotegemea mazingira salama na endelevu. “Ongezeko hili la watu litahitaji rasilimali za maji, ardhi yenye rutuba na mazingira bora. Hili linapaswa kutukumbusha wajibu wetu wa kutunza mazingira na kuimarisha usimamizi wake. Natoa maagizo kwa mamlaka zote za serikali za mitaa nchini kuongeza usimamizi wa mazingira kwa kuandaa bustani na kuhakikisha vibali vya ujenzi vinazingatia sharti ...

MASAUNI AITAKA JAMII KUTUNZA MAZINGIRA

Picha
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ameitaka jamii kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Mhe. Masauni ametoa wito huo leo Juni 4, 2026, alipotembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zinazoshiriki Maonesho ya Wiki ya Mazingira yanayofanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma. Akizungumza Katika Maonesho hayo, Mhe. Masauni amesema Tanzania inaendelea kukabiliwa na changamoto za mabadliko ya tabianchi zinazochangiwa kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira, hivyo akasisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi na wananchi katika kuhifadhi mazingira. “Tunajua kuwa kama nchi tuna changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi yanayotokana na uharibifu wa mazingira. Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi zilizopo hapa tunafanya juhudi kubwa kulitatua tatizo hili. Nizipongeze sana taasisi...

MAJOSHO 754 YAJENGWA KUOGESHEA MIFUGO NCHINI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema itaendelea kuratibu ujenzi, ukarabati na uendelezaji wa miundombinu muhimu ya mifugo nchini, ikiwemo majosho katika Wilaya ya Bunda, kwa lengo la kuimarisha huduma za mifugo na kudhibiti magonjwa yanayoathiri mifugo kadri ya upatikanaji wa fedha. Kauli hiyo imetolewa leo June 2,2026 bungeni na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Dkt Bashiru Ally Kakurwa wakati akijibu swali la Mbunge wa Bunda, Boniphace Getere,(CCM)  aliyehoji ni lini Serikali itajenga majosho katika maeneo ya wafugaji ya Mahanga, Tingirime, Nyabuvumbu, Nyabuzume, Kaloreli na Tirig’ati. Akijibu Balozi Dkt. Bashiru alisema Serikali inatambua umuhimu wa majosho katika kudhibiti magonjwa yanayoenezwa na kupe na mbung’o, na kwamba tangu mwaka wa fedha 2021/2022 imeendelea kutekeleza mpango wa ujenzi wa majosho ambapo hadi sasa jumla ya majosho 754 yamejengwa nchini kote. Alisema  kuwa katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilitumia shilingi milio...

MAZIWA NI UCHUMI, TUCHANGAMKIE FURSA - RC JAMES

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Kheri James amewataka Watanzania kuchangamkia fursa za kiuchumi zitokanazo na maziwa. Mhe. James amebainisha hayo Juni 01,2026 kwenye kongamano la wadau wa tasnia hiyo wakati akifunga Maadhimisho ya 29 ya wiki ya maziwa yaliyokuwa yakifanyika mkoani Iringa. “Siku hii ina umuhimu sana kwa sababu kwanza huongeza uelewa kuhusu faida za maziwa kwa watoto, vijana, wazazi na wazee, pili huhamasisha matumizi ya lishe bora kwa jamii, tatu huunga mkono wafugaji na sekta ya mifugo kwa kuongeza matumizi ya maziwa na bidhaa zake na kukuza uchumi kupitia uzalishaji, usindikaji, na ajira zinazotokana na sekta ya maziwa nchini” Amesema Mhe. James. Aidha Mhe. James amewataka wananchi kutoishia kusherehekea pekee bali watumie siku hiyo kujenga utamaduni wa kunywa maziwa yaliyosindikwa angalau kwa wastani wa glasi moja kwa siku kwa ustawi wa afya zao na maendeleo ya uchumi wa Taifa kwa ujumla. Kwa upande wake Msajili wa Bodi ya Maziwa nchini Prof. George Msalya amesema kuwa m...