DKT. BASHIRU AZIKARIBISHA KAMPUNI KUTOKA ITALIA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa leo Juni 14, 2026 amekutana na ujumbe wa kampuni mbili kutoka nchini Italia ambayo ni ITARE na MULMIX katika Ofisi ndogo za Wizara zilizopo Kambarage Tower jijini Dodoma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuangalia maeneo ya  uwekezaji katika sekta za mifugo na uvuvi.

Kampuni ya ITARE kutoka nchini Italia inajihusisha na ushauri wa kifedha yenye mchanganyiko wa kipekee wa utalaamu na uzoefu katika fedha za miradi na biashara pamoja na uendelezaji wa biashara katika masoko yanayoibukia, ikiwa na mkazo maalum katika Ukanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na Kampuni ya MULMIX imejikita katika usanifu, uzalishaji na usimikaji wa vihenge na mitambo ya kuhifadhia nafaka katika sekta ya kilimo.

Baada ya ujumbe wa kampuni hizo kujitambulisha na kuonyesha utayari wa kuwekeza nchini Mhe. Balozi Dkt. Bashiru amezihakikishia kampuni hizo kuwa serikali ipo tayari kushirikiana na sekta binafsi katika kuwekeza na kufanya biashara kwenye sekta mbalimbali nchini ikiwemo sekta ya mifugo na uvuvi kupitia mfumo wa ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi(PPP).

Aidha, Balozi Dkt. Bashiru ameyataja maeneo muhimu ya kuwekeza kwa sasa katika sekta hiyo kuwa ni uboreshaji wa kosafu za mifugo, uwekezaji katika vyakula vya mifugo na samaki, tasnia ya kuku, miundombinu na teknolojia ya uzalishaji na uchakataji wa maziwa na ukuzaji viumbe maji.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (Kulia), akielezea fursa ya uwekezaji katika sekta ya mifugo na uvuvi wakati wa Kikao na Ujumbe wa Kampuni ya ITARE na MULMIX kutoka Italia katika Ofisi ndogo za Wizara zilizopo Kambarage Tower jijini Dodoma leo  14 Julai 2026.

Mkuu wa Kampuni ya Ushauri wa Kifedha kutoka Italia (ITARE) Bw. Giorgio Traietti (wa kwanza kulia) akieleza jinsi kampuni hiyo inavyotoa ushauri wa kifedha wakati wa kujitambulisha kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi katika Ofisi ndogo za Wizara zilizopo Kambarage Tower jijini Dodoma leo  14 Julai 2026.




Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

UTEKELEZAJI WA UFUGAJI SAMAKI KWA VIZIMBA WAANZA ZIWA TANGANYIKA

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI