Nav bar

Ijumaa, 27 Oktoba 2023

WADAU WAKUTANA KUWEKA MIKAKATI KUENDELEZA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI


Wataalam na wadau wa  sekta ya Mifugo Nchini, wamekutana jijini  Arusha kwa lengo la kujadili namna ya kuongeza uzalishaji katika sekta hizo ambayo italeta tija  kwa wananchi.

Hayo yamesemwa na  Mwenyekiti wa chama cha wataalamu wazalishaji mifugo na Uvuvi ,Dkt. Jonas  Kizima katika ziara ya kutembelea mbuga ya  Tarangire, ikiwa ni sehemu ya kongamano la siku tatu la kisayansi liloanza Oktoba  26 jijini  Arusha

Alisema kuwa  lengo kubwa ni  kupitia machapisho ya kisayansi yaliyoletwa na wadau  ili angalau waweze kutoa matokeo ya tafiti, na kutatua changamoto  katika sekta ya Mifugo na Uvuvi

"Katika hizi siku tatu, tumetenga siku moja ya kuja kutembelea mbuga za wanyama nchini, na mwaka huu tumechagua  Tarangire   ili kupata muda wa kufurahi na kujifunza zaidi, Pia tunaunga juhudi za Rais katika kuongeza watalii nchini kupitia Royal  tour na kuongeza pato kupitia utali,"alisema Dkt. Kizima

Naye Dkt Zablon Nziku, alisema  kuwa katika  kongamano hilo pia wameweza kujadili kwa kina Teknolojia   bora zilizotumika au zinazotumika katika kuwasaidia wadau wetu kuongeza uzalishaji.

"Pamoja na kujifunza mambo mbalimbali ya kisayansi katika uendelezaji wa Mifugo na Uvuvi nchini, bado tunaona ipo haja  ya kufanya ziara kwenye vivutio vyetu vya utalii ili kuwaonyesha  wageni kutoka nje, nasi tunaweza kufanya utalii, hii itasaidia ongezeko la watali wa ndani,"alisema

Aidha baadhi ya washiriki    akiwemo Bi. Neema Urassa alisema  kufanyika kwa ziara hiyo kutawasaidia watumishi na wadau wa sekta hiyo kutambua vivutio vya hapa nchini.

"Pia itamjengea mtumishi anaporudi katika eneo lake la kazi kufanya kazi kwa jitihada na inaongeza ufanisi wa kazi, kwa kufanya hivi kwa sekta zote kutaongeza utalii wa ndani na kuongeza pato la nchi,"alisema Bi. Neema


Sehemu ya wataalam wazalishaji mifugo na Uvuvi wakiwa kwenye picha za pamoja  katika ziara ya kutembelea mbuga ya  Tarangire, ikiwa ni sehemu ya kongamano la siku tatu la kisayansi liloanza Oktoba  26 jijini  Arusha

Sehemu ya wataalam wazalishaji mifugo na Uvuvi wakiwa kwenye picha za pamoja  katika ziara ya kutembelea mbuga ya  Tarangire, ikiwa ni sehemu ya kongamano la siku tatu la kisayansi liloanza Oktoba  26 jijini  Arusha

Sehemu ya wanyama wanaopatikana kwenye mbuga ya Tarangire.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni