Nav bar

Jumatano, 4 Oktoba 2023

WADAU WAKUTANA KUTATHIMINI MRADI WA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA BAHARI

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Kamati tendaji ya mradi wa ushirikiano kati ya Nairobi Convention na Southwest Indian Ocean Commission imekutana jijini Tanga kwa ajili ya kufanya tathmini ya mradi huo unaolenga usimamizi wa mazingira ya bahari na nchi kavu pamoja na usimamizi wa rasilimali za uvuvi

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI ), Dkt. Ismael Kimirei Oktoba 04,2023 ambapo amesema kuwa mradi huo unaotekelezwa katika Wilaya ya Mkinga na Pemba unalenga kutoa majibu ya mahitaji katika uchumi wa buluu

Tumeanzia eneo la Mkinga kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano kati ya Tanzania, Msumbiji na Madagascar na tunategemea kwamba utapanuka kwenda nchi nyingine na ukiangalia upande wa kaskazini mwa bahari ya Hindi kuna nchi ya Kenya ambayo tunatarajia iwe mdau katika mradi huu" amesema Bi. Oliver

Naye Mratibu wa Mradi unaoshughulikia maendeleo ya usimamizi wa rasilimali za bahari kutoka Shirika la Chakula na kilimo (FAO) Bi. Oliver Mkumbo amesema kuwa mradi huo unathamani ya dola za marekani milioni 8 ambazo zimegawanywa katika nchi tatu

"Kubwa ni kuangalia namna gani tuboreshe mazingira lakini wakati huo huo kuangalia rasilimali zilizopo ukanda wa Pwani zimekuwa endelevu na maisha ya watu yameboreshwa kwa shughuli zinazofanyika

Kwa upande wake Afisa uvuvi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga Bw. Ezra Katete amesema kuwa mradi huo umesaidia kwa kiasi kikubwa kutoa elimu kwa wananchi juu ya  kushirikishwa kulinda maeneo yao hususani katika utunzaji wa mazingira na kufanya uvuvi endelevu.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania Dkt. Ismael Kimirei akiongea na wajumbe  wakati wa kufungua kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Mratibu wa Mradi unaoshughulikia maendeleo ya usimamizi wa rasilimali za bahari, Bi. Oliva Mkumbo akichangia hoja wakati wa kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Mkurugenzi Msaidizi wa Uendelezaji wa Rasilimali za uvuvi, Idara ya Uvuvi Bi. Merisia Mparazo akiwasilisha mada kwa wadau wa uvuvi (hawapo pichani) wakati wa kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais Idara ya Mazingira Bi. Magdalena Ngotolainyo akiwasilisha mada kwa wadau wa uvuvi (hawapo pichani) wakati wa kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Meneja wa Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu nchini Dkt. Immaculate Sware Semesi akichangia hoja wakati wa kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Tumaini Chambua  akiwasilisha mada wakati wa kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) , wawakilishi kutoka Nairobi Convention Secretariate na watendaji kutoka Wizara ya mifugo na Uvuvi mara baada ya kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.

Mratibu wa Mradi Kikanda Bi. Ulrika Gunnartz akiwasilisha mada wakati wa kikao cha kamati tendaji cha mradi wa ushirikiano wa SWIOFIC Nairobi Convention kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha VETA Mkoani Tanga, Oktoba 04,2023.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni