Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2024

MRADI WA MAZIWA FAIDA KUBORESHA MIUNDOMBINU MBALIMBALI

Picha
  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akishuhudiwa na Balozi Ireland Tanzania Mhe. Mary O’Neill amezindua miundombinu iliyojengwa kupitia mradi wa maziwa faida unaotekelezwa na kituo cha TALIRI Tanga kwa udhamini wa ubalozi wa Ireland chini ya Taasisi ya Teagacs. Akiongea katika uzinduzi huo Shemdoe amesema Mradi wa maziwa faida mbali na kuboresha miundombinu mbalimbali lakini pia umekiwezesha kituo hicho kupata vifaa bora vya maabara kwa ajili ya kufanyia tafiti mbalimbali za mifugo na malisho bora. Shemdoe ameendelea kueleza kuwa lengo la mradi wa maziwa faida ambao umegharimu zaidi ya Bilioni 7 ni kuboresha mnyororo wa thamani wa maziwa kwa wafugaji ambapo kituo cha TALIRI Tanga kimekuwa kikiendelea kutoa mafunzo kwa vitendo juu ya ufugaji wenye tija sambamba na kufanya tafiti mbalimbali za mifugo. Sambamba na hayo, Shemdoe ametoa wito kwa jamii kuendelea kuzalisha na kutumia maziwa kwa wingi kwani tafiti zinaonesha kuwa watanzania tunapaswa kutumia ...

MNADA WA MHUNZE KUFANYIWA UTAFITI WA KINA UWEPO WA TOPE MAJI - PROF. MUSHI

Picha
Na. Stanley Brayton Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza mchakato wa kufanya Utafiti wa kina juu ya chanzo cha tope maji yatokayo katika ardhi ndani ya mnada wa Mhunze Wilayani Kishapu ikiwa ni njia mojawapo ya kujua athari zinazoweza kujitokeza kutokana na uwepo wa hali hiyo katika eneo la ujenzi ambao unaendelea katika Mnada huo ili kuweza kutafuta suluhisho. Hii ni kufuatia hali hii kuleta taharuki kwa wafugaji na wauzaji wa mifugo kwenye mnada huo. Akizungumza, leo Mei 29, 2024 Wilayani Kishapu, mkoani Shinyanga wakati akienda kukagua hali ya eneo la mnada wa Mhunze, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Daniel Mushi amesema Wizara imeamua kufanya Utafiti wa kina ili kujiridhisha kama hali ya mnada wa Mhunze ni salama na kukabiliana na uwepo wa tope kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa watu na mifugo kwenye mnada huo. "Leo tumekuja na wataalam kutoka Taasisi ya madini Tanzania kwa ajili ya kupima kilichotokea na kutupa taarifa, ambapo mpaka sasa wameshafa...

VIJANA WATENGEWA BIL. 10.5 KWA AJILI YA MIRADI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetenga zaidi ya Shilingi Bilioni 10.5 kwa ajili ya mitaji ya miradi ya vijana ili kuwainua kiuchumi. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Patrobas Katambi amebainisha hayo (24.05.2024) jijini Mwanza, wakati wa kuhitimisha mafunzo kwa vitendo ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji awamu ya pili kupitia Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT – LIFE) ambayo imewejenga katika kujiajiri kupitia Sekta ya Uvuvi. Mhe. Katambi amempongeza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) pamoja na viongozi wengine wa wizara kwa kusimamia vyema maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza ajira kwa vijana kupitia sekta za mifugo na uvuvi. Ameongeza kuwa ni wakati sasa kwa vijana kutumia vyema fursa zitokanazo na sekta hizo ili kujipatia ajira na utajiri pamoja na kufuga kisasa na kuuza mazao ya mifugo na uvuvi yakiwa katika ubora unaotakiwa. Kwa upande wake Katibu Mk...

WAVUVI WATAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA KUKABILIANA NA UPOTEVU WA MAZAO YA UVUVI

Picha
Naibu Katibu Mkuu Sekta ya Uvuvi Dkt. Edwin Mhede amewataka wadau wa uvuvi kuhakikisha wanatumia teknolojia za kisasa ambazo ni rahisi zitakazowezesha kukabiliana na changamoto ya upotevu wa mazao ya Uvuvi. Ameyasema hayo Mei 28, 2024 wakati akifungua mkutano wa Uzinduzi wa mradi wa Asia -Africa BlueTech Superhighway ambao utachukua takribani miaka 7 (2024-2030) wenye lengo la kusaidia juhudi za Serikali katika kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi. Mkutano huo ambao umezikutanisha nchi nne Afrika, Dkt. Edwin Mhede amesema wamejielekeza kuhakikisha wanufaika wa mradi huo wanakuwa ni wavuvi wenyewe. Pia amesema eneo ambalo wanalifanyia kazi kwa kushirikiana na Worldfish pamoja na Taasisi za ndani   ni kuhakikisha wanakabiliana na changamoto za upotevu wa mazao ya uvuvi, pamoja na uharibifu mbalimbali unaojitokeza kwenye mnyororo wa thamani wakati watu wakivua, wakisafirisha, wakiuza na kununua samaki. "Katika kutathimini fikra mpya za nini kifanyike zaidi ya hiki, tumejiele...

VIJANA WA BBT – LIFE WAONESHWA VITALU, RAIS SAMIA ATAJWA KWA MCHANGO WAKE MKUBWA KWENYE SEKTA YA MIFUGO

Picha
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka historia ya kutafsiri ndoto halisi ya wingi wa mifugo nchini katika kubadilisha mfumo wa maisha kwa watanzania kupitia sekta hiyo. Akizungumza (21.05.2024) wakati wa hafla fupi ya kuwaonesha vijana wanaohitimu mafunzo ya unenepeshaji mifugo kupitia Programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT – LIFE), inayosimamiwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, vitalu watakavyopatiwa kwa ajili ya ufugaji katika Ranchi za Kagoma na Kitengule zinazosimamaiwa na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Mhe. Julius Laizer amesema Mhe. Rais ameweza kuirasimisha rasmi biashara ya mazao ya mifugo kwa kuwa Sekta ya Mifugo ni muhimu katika maisha ya binadamu. Akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Laizer amesema ni vigumu kutenganisha biashara yoyote inayohusu chakula cha binadamu isifanikiwe, hivyo kuwataka vijana wa BBT – LIFE kusimamia vyema ndoto na maono ya Mhe. Rais kwa kuwa wapo sehemu sahihi katika ku...

WAKAGUZI MIFUGO, MAZAO YAKE WAPIGWA MSASA

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo Mei 22, 2024 imeanza kutoa mafunzo ya siku 3 kwa Wakaguzi wa mifugo na mazao yake waliopo kwenye vituo mbalimbali vya ukaguzi ikiwa ni pamoja na vile vilivyopo kwenye mipaka yote nchini zoezi litakalofanyika mkoani Morogoro. Akifungua Mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo nchini Dkt. Benezeth Lutege amewataka wataalam hao mbali na kutumia vema taaluma zao, wazingatie weledi na watende haki wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao ikiwa ni pamoja na kuomba ushauri pale wanapopata changamoto. “Tunapokuwa kule kwenye vituo vyetu vya ukaguzi tunapaswa kujua sisi ndio sura ya Wizara kwa hiyo tunavyowapokea wageni, tunavyoongea nao na tunavyotoa huduma zetu kuna athari kubwa sana kwa viongozi wetu wanaotusimamia hivyo tunaweza kuwachafua au kuwajengea sifa njema” Ameongeza Dkt. Lutege. Aidha Dkt. Lutege ametoa angalizo kwa vijana hao kuacha kutanguliza mbele maslahi yao wakati wakitekeleza majukumu vituoni ili kuendelea kuj...

TUPAZE SAUTI KUOKOA PUNDA-MNYETI

Picha
  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amewataka wadau wote wanaosimamia ustawi na haki za wanyama kukemea vikali vitendo vitakavyosababisha kutoweka kwa Punda ili wanyama hao waendelee kuwasaidia wananchi katika shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Mhe. Mnyeti ametoa rai hiyo Mei 17, 2024 alipokuwa akifunga Maadhimisho ya siku ya Punda Afrika Mashariki ambayo kitaifa yamefanyika mkoani Dodoma yakitanguliwa na shughuli mbalimbali ikiwemo mijadala iliyolenga kuchukua hatua mbalimbali za kunusuru kutoweka kwa mnyama huyo. “Punda wamekuwa wakifanya kazi kubwa na muhimu sana katika sekta za kiuchumi ambapo   katika shughuli za usafiri hivi sasa wamekuwa wakitumika mpaka kubeba vifaa vya ujenzi na siku za hivi karibuni tumeshuhudia wakibeba madini katika migodi mbalimali nchini” Ameongeza Mhe. Mnyeti. Aidha Mhe. Mnyeti amebainisha kuwa kutokana na umuhimu wa ngozi na viungo vingine vya mnyama huyo ongezeko la uchinjaji wa wanyama hao lilikuwa kubwa h...

warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi,

Picha
  Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia uthibiti wa ubora na masoko ya mazao ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Stephen Lukanga (wa tatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau  wa uvuvi mara baada ya kushiriki warsha ya kujenga uelewa kwa wadau hao kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi (MDS STATEGY) na kupitia mkakati wa masoko wa zao la dagaa, Warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi hoteli ya Flomi mkoani Morogoro Mei16, 2024 Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Upendo Hamidu akichangia hoja wakati wa warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi na kupitia mkakati wa masoko wa zao la dagaa,  Mei 16,2024 mkoani Morogoro. Mratibu wa Mradi unaofadhiliwa na shirika la maendeleo la Norway kupitia Shirika la chakula na kilimo (FAO) Bw. Joseph Lomba akieleza lengo la kufanya utafiti wa kutathmini hali ya upotevu wa rasilimali  ya uvuvi aina ya dagaa wakati wa warsha ya kujenga uele...

shughuli mbalimbali zilizofanyika kwenye Wiki ya Protini iliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge Mkoa wa Dodoma Mei 14, 2024.

Picha
  Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe. Anjelina Mabula (kushoto) akipata maelezo kuhusiana na matumizi mbalimbali ya mazao ya Uvuvi yatokanayo na Samaki aina ya Jodar kutoka Mtaalam wa Utafiti wa mazao hayo wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI) Bi. Siwema Luvanda alipotembelea Mabanda ya maonesho ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika kwenye Wiki ya Protini iliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge Mkoa wa Dodoma Mei 14, 2024. Mbunge wa Isimani Mhe. Wiliam Lukuvi (kulia) akikabidhiwa nyama aina ya Kongwa Beef kutoka kwa Bi. Beatrice Mhina (kushoto) mtaalamu kutoka Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) mara baada ya kuridhishwa na ubora wake alipotembelea Mabanda ya maonesho ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kujionea shughuli mbalimbali zinazofanyika kwenye Wiki ya Protini iliyofanyika kwenye viwanja vya Bunge Mkoa wa Dodoma Mei 14, 2024. Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Halima Mdee (kulia) akipata maelezo kuhusiana na matumizi sahihi ya Chanjo ya Mdondo (Kideli) kwa kuk...

WAZIRI MKUU AZINDUA KITUO CHA UFUGAJI MBUZI, KONGWA

Picha
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Mei 13, 2024 amezindua na kushuhudia makabidhiano ya Kituo Atamizi cha Ufugaji wa Kibiashara kwa Vijana, baina ya Taasisi ya PASS TRUST na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI)kilichopo Kongwa mkoani Dodoma. Akizungumza baada ya makabidhiano ya kituo hicho, ambacho kinathamani ya shilingi bilioni 1.63 ikijumuisha uwekezaji wa vifaa na mindombinu, Mheshimiwa Majaliwa ameagiza uwekezaji utunzwe ili taifa liweze kunufaika kupitia uwezeshwaji wa vijana. Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa lengo la mradi huo ni kuwapatia vijana ujuzi kwa vitendo ikiwemo elimu ya ujenzi wa mabanda, ulishaji, matibabu na usimamizi wa mbuzi lakini pia kutoa mafunzo ya biashara ili vijana waweze kuwa wajasiriamali na kuendeleza biashara ya unenepeshaji mbuzi. Kwa upande wake, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa hadi kufikia Aprili 2024, ongezeko la mauzo ya nyama nje ya nchi limefikia takribani shilingi bilioni 100 ambapo nyama ya mbuzi imeen...

WATUMISHI WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WATAKIWA KUWAJIBIKA NA KUWA WAADILIFU

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amewataka watumishi wa wizara hiyo kuwa na uwajibikaji na uadilifu katika makujumu yao ya kuwatumikia wananchi. Mhe. Mnyeti amebainisha hayo leo (10.05.2024) jijini Dodoma, wakati alipokuwa akihutubia wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kufafanua kuwa ana imani kubwa na watumishi wa wizara hiyo na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuwa na uzalendo. Ameongeza kuwa katika uwajibikaji na uadilifu watumishi wa wizara hiyo wanatakiwa kutojiingiza kwenye matukio ya matumizi mabaya ya ofisi na kuhakikisha wanazidi kuwatumikia wananchi kwa kiwango kikubwa hususan wafugaji na wavuvi ambao wengi wao wanaishi vijijini. Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza hilo, amesema kikao hicho kimetoka na maazimio tisa ambapo pia wajumbe wameridhia Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka 2023/2024 na Mpango wa Bajeti ya Mwaka 2024/2025 k...

UPUMZISHWAJI ZIWA TANGANYIKA WAUNGWA MKONO

Picha
Wananchi wanaojishughulisha na uvuvi katika ukanda wa Ziwa Tanganyika wameunga mkono hatua ya serikali ya kupumzisha shughuli za uvuvi katika ziwa Tanganyika ili kulipa nafasi ziwa kuongeza kiwango chake cha uzalishaji wa samaki. Wananchi hao waliunga mkono hatua hiyo wakati wa hafla ya kukabidhi vizimba vya kufugia samaki, boti za kisasa za uvuvi na doria na pia kupata elimu na uelewa kuhusu upumzishaji wa shughuli za Uvuvi Ziwa Tanganyika iliyofanyika katika Mwalo wa Katonga, mkoani Kigoma Mei 9, 2024. Wakizungumza kwa nyakati tofauti wawakilishi wa wananchi, akiwemo Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Kilumbe Ng’enda alisema kuwa muda ambao umepangwa ziwa kupumzishwa ni muafaka kwa sababu kipindi hicho ni maarufu kwa jina la ‘kilimia’ ambapo ziwa huwa linajifunga lenyewe na kufanya kupungua kwa Mazao ya samaki. Aliongeza kwa kueleza kuwa, kwa muda mrefu sasa wavuvi wamekuwa wakitumia vifaa vyao na mafuta kwenda mbali bila mafanikio yoyote kwa sababu samaki wamepungua sana ziwani, hiv...

ULEGA: TUMEJIPANGA KUIMARISHA BIASHARA YA MAZAO YA MIFUGO

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema wizara yake imejipanga kuyasimamia vyema mazao ya mifugo hususan maziwa, nyama na ngozi ili yazalishwe kwa ubora na kushamirisha biashara kwa lengo la kuyafanya mazao hayo kuwa na mchango mkubwa zaidi kwenye pato la Taifa. Ameyasema hayo wakati akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Nyama na Bodi ya Maziwa kwenye kikao kilichofanyika jijini Dodoma Mei 7, 2024, ambapo alipokea taarifa za utekelezaji wa bodi hizo ambazo kwa sasa zimeunganishwa na kuundwa taasisi moja itakayosimamia mazao hayo ya mifugo. “Tuko katika uundaji wa taasisi nyingine ya usimamizi wa mazao kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, tunakwenda kuunda taasisi nzuri, makini, imara, itakayokwenda kuongeza tija na kushamilisha biashara. Wadau msiwe na wasiwasi, tunatambua juhudi kubwa mnazozifanya, tumejipanga kufanya kazi kwa pamoja kuleta maendeleo ya Tasnia hizi mbili na Sekta ya Mifugo kwa ujumla”, alisema “Niwaahidi kuwa tutajitahidi kwa up...