MRADI WA MAZIWA FAIDA KUBORESHA MIUNDOMBINU MBALIMBALI
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akishuhudiwa na Balozi Ireland Tanzania Mhe. Mary O’Neill amezindua miundombinu iliyojengwa kupitia mradi wa maziwa faida unaotekelezwa na kituo cha TALIRI Tanga kwa udhamini wa ubalozi wa Ireland chini ya Taasisi ya Teagacs. Akiongea katika uzinduzi huo Shemdoe amesema Mradi wa maziwa faida mbali na kuboresha miundombinu mbalimbali lakini pia umekiwezesha kituo hicho kupata vifaa bora vya maabara kwa ajili ya kufanyia tafiti mbalimbali za mifugo na malisho bora. Shemdoe ameendelea kueleza kuwa lengo la mradi wa maziwa faida ambao umegharimu zaidi ya Bilioni 7 ni kuboresha mnyororo wa thamani wa maziwa kwa wafugaji ambapo kituo cha TALIRI Tanga kimekuwa kikiendelea kutoa mafunzo kwa vitendo juu ya ufugaji wenye tija sambamba na kufanya tafiti mbalimbali za mifugo. Sambamba na hayo, Shemdoe ametoa wito kwa jamii kuendelea kuzalisha na kutumia maziwa kwa wingi kwani tafiti zinaonesha kuwa watanzania tunapaswa kutumia ...