Nav bar

Alhamisi, 30 Mei 2024

warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi,

 

Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia uthibiti wa ubora na masoko ya mazao ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Stephen Lukanga (wa tatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau  wa uvuvi mara baada ya kushiriki warsha ya kujenga uelewa kwa wadau hao kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi (MDS STATEGY) na kupitia mkakati wa masoko wa zao la dagaa, Warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi hoteli ya Flomi mkoani Morogoro Mei16, 2024

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Upendo Hamidu akichangia hoja wakati wa warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi na kupitia mkakati wa masoko wa zao la dagaa,  Mei 16,2024 mkoani Morogoro.

Mratibu wa Mradi unaofadhiliwa na shirika la maendeleo la Norway kupitia Shirika la chakula na kilimo (FAO) Bw. Joseph Lomba akieleza lengo la kufanya utafiti wa kutathmini hali ya upotevu wa rasilimali  ya uvuvi aina ya dagaa wakati wa warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao hayo, warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Flomi mkoani Morogoro,  Mei 16,2024

4

Mtaalam elekezi wa Mradi wa upunguzaji wa uaribifu wa dagaa nchini Bw. Yahaya Mgawe akiongoza warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi, warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Flomi mkoani Morogoro,  Mei 16,2024

Mkurugenzi Msaidizi anayesimamia uthibiti wa ubora na masoko ya mazao ya uvuvi, Bw. Stephen Lukanga akitoa neno la shukrani mara baada ya ufunguzi wa warsha ya kujenga uelewa kwa wadau kuhusu mkakati wa kupunguza upotevu wa mazao ya uvuvi na kupitia mkakati wa masoko wa zao la dagaa mkoani Morogoro Mei 16,2024.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni