Nav bar

HOTUBA ZA WAZIRI NA TAARIFA MBALIMBALI

TANZANIA LIVESTOCK MODERNIZATION INITIATIVE
The Tanzania Livestock Modernization Initiative (TLMI) is intended to support the progressive and adaptive development of a vibrant Livestock Sector which is responsive to growing demands and emerging commercial opportunities, and which is economically, socially and environmentally sustainable.
The TLMI aims to harness the potential of meat, diary and poultry sectors for poverty alleviation through improvements across the value chains including improvements in security and access to grazing, access to markets, quality and safely of Livestock products, processing and value addition. It will identify the coordinated intervation needed across sectors to support these improvements and the necessary regulatory environment to ensure safe and healthy Livestock products.
GOALS
The overall goal of the TLMI is to increase food and nutrition security and food safety, create employment opportunities and contribute to the national economy, social and sustainable environment.
PURPOSE
The purpose of TLMI is to improve the Livelihoods of traditional an small holder Livestock farmers and contribution of the sector to the national economy.

HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI MHE. DKT TITUS M KAMANI (MB) ALIYOITOA KWENYE UFUNGUZI WA DUKA LA NYAMA LA RANCHI YA KONGWA KATIKA MAMLAKA YA MJI MDOGO KIBAIGWA TAREHE 22 MEI 2015
Mhe.Prof Peter Msolla (Mb) Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya bunge ya kilimo, Mifugo na Maji;
Mhe. Jb Ndugai (Mb), mbunge wa Kongwa na Naibu Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mhe. Mku wa Wilaya ya Kongwa;
Dkt. Yohaa Budeba, Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi;
Waheshimiwa Madiwani,
Wakurugenzi wa Wizara,
Meneja Mkuu wa NARVCO,
Mameneja wa RANCHI za NARCO,
Wanahabari,
Mabibi na Mabwana. 
Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukusanyika mahali hapa siku hii ya leo tukiwa wazima wenye afya. Aidha, natoa shukrani zangu za dhati kwa kampuni ya NARCO kunialika kuja kutembelea rachi ya kongwa na kufungua duka lenu la nyama katika mamlaka ya mji mdogo wa Kibaigwa ambalolinamilikiwa na ranchi ya kongwa.

Meneja Mkuu, tangu nilipoteuliwa na mheshimiwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete nimekuwa nisisitiza kwa watumishi wa Wizara na Taasisi zake zote kubadili fikra katika kutekelezea majukumu ili kuleta tija katika sekta za Mifugo na Uvuvi. Hii pamoja na kuwa na ubunifu katika uzalishaji na kutafuta rasilimali fedha ikizingatiwa kuwa kiasi kinachotolewa na hazina hakiwezi kutosheleza mahitaji ya taifa zima. Hivyo napenda niwapongeze kwa hatua moja mliyofikia ya kuona umuhimu wa kufungua duka hapa Kibaigwa ili kuwahakikishia wananchi walio karibu na Ranchi yenu ya Kongwa wanafaidika kwa kupata nyama iliyobora.

Meneja Mkuu, pamoja  na kufungua duka katika mji mdogo wa Kibaigwa lakini bado kuhakikisha kuwa wafugaji wanaozunguka wananufaika na elimu ya ufugaji bora na kubadilisha aina ya mifugo waliyonayo ili kuwza kuongeza tija katika uzalishaji na kunufaika kwa kuweza kuuuza mifugo walio wengi huchukua muda mrefu takriban zaidi ya miaka minne hadi kufikia uzito unaokubalisokoni. Jambo hilo linawafanya wawe watumwa wa mifugo yao wenyewe. Wafugaji wanaowazunguka watafaidika zaid kwa kuwa nyie ndio mtakuwa soko kubwa la mifugo ndani na nje nchi hatimaye kuongeza kwa vitendo maelekezo ya ILani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 ambayo pamoja na mambo inaelekeza;

(a) "Kuhimiza wafugaji watekeleze kanuni za ufugaji bora na kuingiakatika ufugaji endelevu wa kisiasa na kibiashara unaozingatia hifadhi ya mazingira" na

(b) "Kuendeleza elimu kwa Wafugaji ili wajue kuwa mifugo waliyonayo ni mali inayoweza  kuvuniwa katika umri na uzito muafaka unaokidhi mahitaji ya soko, ili kuwaondolea umaskini wao badala ya kuridhika na wingi wa mifugo iliyo duni na maisha ya kuhamahama.

Aidha, Ilani ya uchunguzi wa CCM inaelekea kusisitiza kuwa:
"Pamoja na mafanikio mengi tuliyopata na changamoto zilizojitokeza fusra kubwa ya kuendelea kujenga uchumi wa kisasaili kumudu ushindani katika mazingira ya utandawazi na kuongea tija kwa siasa zaidi. Nchi yetu inatambua kuwa changamoto kubwa inayotukabili ni suala la Mapinduzi YA Kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Viwanda.

Meneja mkuu, katika kutekeleza Ilani hii, Wizara yangu ilifanyika mkutano na bodi pamoja na Menejimetiya ya NARCO tarehe 4 Februari, 2014 na kuweka mikakati ambayo itaiwezesha NARCO kuinuka kiuchumi na kufika lengo. Wizara imekuwa ikihimiza umuhimu wa kuendeleza sekta hii ya mifugo katika mnyororo wake wote wa thamani ikianzia na kuendeleza mashamba makubwa, ya kati na madogo ya mifugo yanayoendeshwa kibiashara yaweza kuleta maendeleo ya haraka katika sekta ya ufugaji, kwa kutoa huduma mbali mbali ikiwa ni pamoja na kuzalisha mbegu bora za mifugo na malisho, na kuzisambaza kisasa, viwanda vya nyama na maduka ya kisasa ya kuuza nyama iliyo bora.

Meneja Mkuu,  Ushauri wangu kwenu ni kuwa kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) iendeee kwa kasi na mfumo wa uendeshaji unaolenga kwenye uzalishaji wa kibiashara na unaozingatia matakwa ya soko na hatimaye kuchangia katika juhudi za taifa za kupunguza umaskini (MKUKUTA).

Pia endeleeni na kutoa mafunzo na mbinu za kisiasa za kuendesha sekta hii ya mifugo kibiashara kwa kupitia wataalamu wenu walioko katika Ranchi zenu kwa wafugaji ambao ni majirani zenu. Ni muhimu kutambua kwamba katika mfumo wa soko huhru na utandawazi, anayezalisha kwa ufanisi, ubora na kwa gharama nafuu diye atakayehimili ushindani. Hivyo ni muhimu kubadili mtizamo wa uzalishaji kwa kulenga mahitaji ya soko na NARCO muendelee kueneza dhana hii.

Meneja Mkuu, Ranchi za NARCO nazihimiza ziendelee na jitihada za kuziendeleza kwa kushiikiana na sekta binafsi ili zipate mitaji mikubwa ya uzalishaji, kunenepesha na kuuza idadi kubwa ya ng'ombe bora au mazao yake ila mwaka kwa soko la ndani na nje ya nchi. Hivyo natoa agizo kwa menejimenti ya NARCO kuendelea kuweka mipango madhubuti na iliyo endelevu ya kuvutia sekta binafsi.

Meneja Mkuu, Serikali inajitahidi kuweka mazingira mazuri yakayovutiwa uwekezaji mkubwa katika viwanda vya kusindika nyama. Ninatoa wito kwa mara  nyingine kwa sekta binafsi nchini ijitokeze na itumie fursa hii kuwekeza katika sekta hii ya nyama kwa kujenga machinjio za kisasa na viwanda vya nyama. Pia ranchi hizi za NARCO na ranchi ndogondogo zilizomilikishwa kwa watanzania na zile za watu binafsi nazihimiza zitilie mkazo wa kuzalisha mifugo kwa wingi yenye ubora na yenye tija kwa sababu ya kuwepo na soko la uhakika hapa nchini na nje ya nchi.

Aidha, nitumie nafasi hii kuwahimiza watanzania kuanza sasa kupenda kununua chakula kaa vile nyama itolewayo katika mazingira mazuri na salama ili kulinda afya zao. Hayo niyo maendeleo. Tunaondoana na matumizi ya nyama ambayo haikukaguliwa na kutoka kwenye maeneo machafu eti tu kwa kuwa tumezoea. Hali hiyo ndiyo tufanya tuugue magonjwa bila hata kujua yametoka wapi. Hivyo mahali lilipo duka hili ni eneo la kimkakati kwani licha ya wananchi kibaigwa, lakini pia litahudumia viongozi wengi wanaosafiri kati ya Dodoma na Dar es Salaam.

Meneja Mkuu, ninatoa wito kwa wafanya biashara wa bidhaa za mifugo hapa kibaigwa na sehemu zote nchini, kuanzisha maduka mengine yenye ubora kama hili tuliofungua leo ili kuwezesha wananchi kupata nya ma safi isiyo na magonjwa ili kuboresha afya ya walaji.

Meneja Mkuu, baada ya kusemna haya sasa nitamke kuwa duka lenu la nyamala kisasa limezinduliwa.



MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO ULIOFANYIKA MWANZA KUANZIA TAREHE 5 - 7 SEPT. 2014
                                                             
NAOMBA RADHI KWA WASOMAJI WOTE  TAARIFA YA MAANDISHI YA UFUNGUZI ULIOFANYWA NA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE KAYANZA MIZENGO PETER PINDA HAIPO KWA MAANDISHI ILA IPO KWENYE CLIP ZA VIDEO
 
HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA DKT. TITUS MLENGEYA KAMANI (MB) ALIYOITOA KUMKARIBISHA WAZIRI MKUU – MGENI RASMI KUTOA HOTUBA YAKE KATIKA MKUTANO WA WADAU WA MIFUGO ULIOFAYIKA MWANZA, TAREHE 5 - 7 SEPTEMBA, 2014


Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Waheshimiwa Mawaziri na Manaibu Mawaziri,
Mhe. Injinia Evarist Welle Ndikilo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,
Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya,         
Mhe. Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza,
Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa,
Waheshimiwa Meya wa Majiji, Miji na Manispaa na Wenyeviti wa Halmashauri,
Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri,
Wawakilishi wa Mashirika ya Serikali, yasiyo ya Serikali na Sekta Binafsi,
Wafugaji,
Wageni waalikwa,
Mabibi na Mabwana,
 Asalaam Aleykum, Tumsifu Yesu Kristu, Bwana Asifiwe

1.     Mheshimiwa Waziri Mkuu, awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii, kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutukutanisha leo hapa Mwanza kwenye mkutano huu wa wadau wa mifugo tukiwa na afya njema. Nitumie nafasi hii kukushukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuitisha mkutano huu na kwa kukubali kwako kutufungulia na kisha kuwa Mwenyekiti wa mkutano huu. Aidha, nachukua nafasi hii kuushukuru uongozi wa Mkoa na wananchi wa Mwanza kwa kukubali kuwa wenyeji wetu na kwa mapokezi mazuri waliyotupatia. Nipende pia kuwashukuru washiriki wote kwa kukubali wito wa kuja kwenye mkutano huu muhimu.
2.    Mheshimiwa Waziri Mkuu, Uzalishaji wa mazao ya mifugo nchini bado ni mdogo kwani inakadiriwa kuwa kila Mtanzania anakula wastani wa kilo 11 za nyama, lita 45 za maziwa na mayai 72 kwa mwaka. Ulaji huo, haujafikia viwango vya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa ambavyo ni kilo 50 za nyama, lita 200 za maziwa na mayai 300 kwa mtu kwa mwaka. Inakisiwa kwamba mifugo tuliyonayo nchini inazalisha chakula (nyama, maziwa na mayai) yenye thamani ya zaidi ya shilingi trilioni 20. Kama ingekuwa chakula hicho kinaagizwa kutoka nje ya nchi, kiasi hicho cha fedha kisingepatikana kutoka kwenye bajeti yetu ambayo ni shilingi trilioni 19.
3.    Mheshimiwa Waziri Mkuu, pamoja na uchangiaji huo katika chakula, sekta ya mifugo katika mwaka 2013/2014 ilichangia asilimia 4.4 katika pato la Taifa. Sekta hii ingeweza kuchangia zaidi kama changamoto zinazoikabili zingetatuliwa hivyo ni vyema sekta hii ya mifugo ikasaidiwa kutatua changamoto zilizopo ili iweze kuwa endelevu na kuchangia zaidi katika afya na kipato cha watanzania na uchumi wa nchi kwa ujumla. Ni matumaini yangu kuwa katika mkutano huu tutajadili kwa kina na kutoa mapendekezo kuhusu tufanye nini ili sekta ya mifugo ichangie zaidi katika uchumi wa Taifa.
4.     Mheshimiwa Waziri Mkuu, Mkutano huu unafanyika katika kipindi ambacho sekta ya mifugo na hasa wafugaji wa asili, wakiwa na changamoto nyingi. Ninaamini yale yote yatakayojadiliwa hapa yataleta ufumbuzi wa kudumu wa changamoto mbalimbali zinazokabili sekta hii muhimu katika uchumi wa Taifa. Sekta ya mifugo ina changamoto nyingi zinazohitaji kupatiwa ufumbuzi wa kudumu. Naomba nitaje baadhi ya changamoto zinazoikabili sekta ya mifugo.
Nyanda Duni za malisho
5.     Mheshimiwa Waziri Mkuu, Tatizo la upatikanaji wa malisho hapa nchini linaendelea kuongezeka hasa wakati wa kiangazi ambapo malisho hupungua kwa kiasi kikubwa. Tatizo hilo limesababisha maafa makubwa hasa kwa wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.  Wafugaji wanaohama wamekuwa wakiongezeka kutoka maeneo yenye mifugo mingi na kwenda katika mikoa ya kusini ambako maeneo mengi yanatumika kwa kilimo. Hali hii imesababisha kuwepo kwa migogoro kati ya wafugaji na wakulima. Kwa mfano, migogoro ya wafugaji na wakulima Mkoani Morogoro (Kilosa na Mvomero) na Mkoa wa Pwani (Ikwiriri – Rufiji).
Uhaba wa Maji kwa Mifugo
6.     Mheshimiwa Waziri Mkuu, Sambamba na tatizo la malisho, upatikanaji wa maji kwa ajili ya mifugo limekuwa pia ni tatizo kubwa. Katika kipindi cha kiangazi maji hukauka hata katika baadhi ya mabwawa na malambo na kufanya wafugaji kuhangaika na kuhama ili kunywesha mifugo yao. Pamoja na juhudi za Wizara za kuchimba malambo mapya na kukarabati yaliyopo, bado malambo haya hayatoshi kutokana na wingi wa mifugo. Ujenzi na ukarabati wa malambo nchini unahitaji rasilimali fedha nyingi ili kuipatia mifugo maji ya kutosha.

Magonjwa ya Mifugo
7.     Mheshimiwa Waziri Mkuu, Magonjwa ya mifugo pia ni eneo ambalo linatakiwa kutengenezewa mikakati ya kudumu ili iendelee kuwa na afya na kuzalisha kwa tija. Magonjwa yanayoathiri mifugo kwa kiasi kikubwa (asilimia 70) ni yale yanayoenezwa na kupe. Serikali imejitahidi kujenga na kukarabati majosho na pia kununua dawa za kuogesha mifugo lakini bado magonjwa hayo yanatishia ustawi wa mifugo hapa nchini. Kati ya mwaka 2010/2011 na 2013/2014 Serikali ilitumia shilingi bilioni 4.2 kama ruzuku kununua na kusambaza lita 252,138 za dawa ya kuogesha mifugo.
8.     Wizara imeanza kutenga Maeneo Huru ya Magonjwa ya Mifugo ili kuzuia ueneaji wa magonjwa katika maeneo maalumu kwa lengo la kuimarisha biashara ya mifugo na mazao yatokanayo na mifugo. Katika kuendeleza azma hiyo, Wizara imeimarisha miundombinu ya Kituo cha Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo cha Kanda ya Kusini na kutoa mafunzo kwa wataalamu wake. Hata hivyo, hili ni eneo moja tu na inatakiwa kutenga maeneo ya kutosha nchini ili kuweza kuhudumia mifugo ya kutosha.
Uzalishaji na Usambazaji wa Teknolojia za Mifugo
9.     Mheshimiwa Waziri Mkuu, idadi ya mifugo bora hasa ng’ombe wa maziwa na wa nyama walionenepeshwa ni ndogo sana na hivyo bidhaa za maziwa na nyama hazitoshelezi na kusababisha kuagizwa nje ya nchi ili kutosheleza mahitaji. Idadi ya ng’ombe wa maziwa imeongezeka kutoka 605,000 mwaka 2009 hadi 720,000 mwaka 2013 na kuchangia kiasi cha asilimia 30 cha maziwa yanayozalishwa nchini. Idadi hiyo ni ndogo ikilinganishwa na nchi jirani ya Kenya ambayo ina ng’ombe wa kisasa wa maziwa zaidi ya milioni 4. Aidha, takriban ng’ombe 175,000 walinenepeshwa katika mwaka 2013/2014, kiasi ambacho ni kidogo sana ikilinganishwa na idadi ya ng’ombe ya milioni 22.8.
10.Mheshimiwa Waziri Mkuu, teknolojia ya uhimilishaji inatumika kuzalisha na kupata ng’ombe wa kisasa wanaozalisha maziwa na nyama zaidi. Wizara imeendelea kuimarisha Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC – Usa river Arusha) pamoja na vituo vya kanda vya uhimilishaji 6 vya Kanda ya Ziwa (Mwanza), Mashariki (Kibaha), Kati (Dodoma), Nyanda za Juu Kusini (Mbeya), Kusini (Lindi), Kanda ya Magharibi (Mpanda) na Sao Hill. Hata hivyo, elimu ya kutosha inahitajika kutolewa kwa wafugaji katika suala la uhimilishaji.
Upatikanaji wa Masoko ya Mifugo na Bidhaa zake
·        Mifugo
11.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, masoko ya mifugo na bidhaa zake ndani na nje ya nchi ni suala muhimu kwa maendeleo ya sekta hii ya mifugo. Idadi ya mifugo iliyouzwa minadani imeendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka kutoka ng’ombe 857,208, mbuzi 682,992 na kondoo 122,035  mwaka 2009/2010 hadi ng’ombe 1,215,541, mbuzi 960,199 na kondoo 209,292 mwaka 2013/2014. Ongezeko hilo bado ni dogo ukilinganisha ni idadi yote ya mifugo iliyopo ambayo inatakiwa kuvunwa kwa asilimia 25 kila mwaka. Mauzo ya mifugo minadani yanaendelea kuongezeka kutokana na kuimarisha miundombinu ya minada. Hata hivyo, minada mingi iko katika hali isiyo ya kuridhisha na inahitaji kuimarishwa zaidi ili ifanye kazi kwa ufanisi. Uuzaji wa mifugo nje ya nchi bado ni kidogo sana kwani soko linalotegemewa ni, Comoro na nchi jirani ambazo mahitaji yao yanabadilika mara kwa mara.
·        Zao la Nyama
12.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, mahitaji ya nyama kwa ajili ya soko la nje yameendelea kukua lakini tumeshindwa kuyafikia kutokana na kukosekana kwa machinjio na viwanda vya kuchakata nyama zinazokidhi viwango vya kimataifa. Kwa mfano, katika mwaka 2012 nchi ya Misiri na Zambia zilihitaji tani 50,000 kwa mwaka wakati uwezo wetu ni tani 23,000. Soko la nyama linaweza kuwa la uhakika na kuliingizia Taifa fedha nyingi za kigeni kama tungekuwa na machinjio na viwanda vikubwa vya kusindika nyama. Hivyo, ujenzi wa machinjio ya kisasa ya Ruvu ukikamilika utaongeza mauzo ya nyama bora ndani na nje ya nchi. Aidha, ufugaji wa ngombe wa nyama kisasa ni muhimu ili kuongeza upatikanaji wa nyama bora kwa ajili ya masoko maalumu na kuuza nje ya nchi. Hata hivyo, ufugaji huu unahitaji raslimali kubwa ambazo zimekuwa vigumu kupatikana kutokana na masharti magumu ya kupata mikopo kutoka taasisi za kifedha.
·        Zao la Maziwa
13.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, uzalishaji wa maziwa umeendelea kuongezeka kutokana na kuongezeka kwa wingi wa mifugo. Hata hivyo, ukusanyaji wa maziwa hayo kwa ajili ya masoko ya ndani na usindikaji umekuwa kidogo sana kutokana na miundombinu hafifu ya ukusanyaji na usindikaji. Kwa sasa tunavyo viwanda 74 vyenye uwezo wa kusindika lita 403,000 lakini vinazalisha lita 139,800. Aidha, unywaji wa maziwa nchini bado ni mdogo na hivyo ni muhimu kupanua soko la ndani ili kuongeza uzalishaji, usindikaji wa maziwa na ajira. Programu inayoratibiwa na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ya Unywaji wa Maziwa Shuleni, kupitia Bodi ya Maziwa Tanzania inatakiwa kupanuliwa ili kuongeza wigo wa soko la maziwa la ndani.
·        Zao la Ngozi
14.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, Zao la ngozi ni zao la mifugo muhimu ambalo likiendelezwa lina mchango mkubwa kwa wafugaji na uchumi wa Taifa kwa ujumla. Hata hivyo, zao hili linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na ubora hafifu na makusanyo madogo ya ngozi kutokana na ufugaji usiozingatia kanuni bora za ufugaji ambazo ni aina duni za mifugo, lishe duni kwa mifugo, umri mkubwa wakati wa kuchinjwa, upigaji chapa ovyo katika maeneo muhimu ya ngozi, mikwaruzo itokanayo na miiba au vitu vyenye ncha kali na kupiga viboko. Aidha, elimu duni, mapungufu katika ujuzi wa utendaji kazi kwa wachunaji na wawambaji na kukosekana kwa mbinu za ujasiriamali kwa wafanyabiashara wa ngozi na hali mbaya ya miundo mbinu ya machinjio, makaro ya kuchinjia, mabanda ya kukaushia na maghala ya kuhifadhia ngozi vinachangia pia katika kupunguza ubora  na thamani ya ngozi kwa siku za karibuni tatizo la utoroshwaji wa ngozi nje ya nchi, kupungua kwa uwezo wa viwanda vya kusindika ngozi, bei isiyotabirika ya ngozi zilizosindikwa kwa kiwango cha wet blue na  ushindani usio wa haki wa bidhaa hafifu za ngozi (plastiki na mitumba) zinazoingizwa kutoka nje zimeendelea kudumuza tasnia ya ngozi nchini.
Usimamizi hafifu wa Sheria za Mifugo na Kanuni
15.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, ubora wa mifugo, mazao yatokanayo na mifugo, pembejeo na huduma za mifugo husimamiwa na sheria 10 za mifugo pamoja na kanuni na miongozo mbalimbali.  Usimamizi mzuri wa sheria huongeza ubora wa bidhaa za mifugo na hivyo kuboresha masoko ya ndani na nje ya nchi. Kutozingatiwa kwa sheria na kanuni zake kumesababisha bidhaa na huduma nyingi za mifugo kuwa duni na hivyo kusababisha bidhaa na mazao ya mifugo yanayozalishwa kuwa na ubora hafifu.
16.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, sekta hii pia inasimamiwa na sheria nyingine ambazo usimamizi na utekelezaji wake unawataka wadau kulipa tozo na kodi mbalimbali ambazo zimeendelea kusababisha malalamiko kutoka kwa wadau. Kwa mfano, wadau wa maziwa wanalalamikia matakwa ya sheria zaidi ya kumi (10) ambazo zipo katika mamlaka mbalimbali kisheria na zinasimamia shughuli zinazofanana katika tasnia ya maziwa. Changamoto iliyopo ni jinsi ya kupunguza mzigo wa tozo na kodi zinatozwa na mamlaka mbalimbali kwenye zao lile lile.
17.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, ili kuleta mapinduzi katika sekta ya mifugo, changamoto hizi na zingine ambazo hazikutajwa hapa, zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi. Wizara kwa kushirikiana na wadau wake wanatakiwa kushirikiana kwa karibu ili kupanga mikakati ya pamoja ya kutatua changamoto zilizopo.
18.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, baada ya kueleza changamoto hizo, napenda kukuarifu kuwa kwa sasa sekta ya mifugo inaingia katika mpango wa Matokeo Makubwa Sasa – BRN. Bado tunaendelea na maandalizi stahiki ili kuanza kutekeleza mpango huo. Ni matumaini yangu kuwa katika mpango huo sekta hii itaendelea kwa kasi zaidi ili kuongeza ajira, kuongeza kipato na kupunguza umasikini kwa wananchi wa Tanzania.
19.  Mheshimiwa Waziri Mkuu, mwisho, naomba nitumie nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais na wewe Mhe. Waziri Mkuu kwa kuhimiza maendeleo katika sekta ya mifugo. Hali hiyo ikiendelea sekta hii itakua kwa haraka na kutoa mchango mkubwa katika pato la Taifa na hivyo kuboresha maisha ya Watanzania kwani, Sekta hii imeajiri watanzania wengi.
20.  Baada ya kusema haya Mhe. Waziri Mkuu, kwa heshima sasa naomba utufungulie mkutano na hatimaye uongoze majadiliano.


AHSANTENI SANA KWA KUNISIKILIZA

MADA ILIYOWASILISHWA NA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAKAZI

WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI











MADA KUHUSU USIMAMIZI WA MIGOGORO YA ARDHI HUSUSAN KWA WAKULIMA NA WAFUGAJI ILIYOWASILISHWA KWENYE MKUTANO WA WAKUU WA MIKOA, MAKATIBU TAWALA WA MIKOA NA WAKUU WA WILAYA




Iliyotolewa na Prof. Anna Tibaijuka (MB)
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi











DODOMA
16 NOVEMBA, 2012



TAARIFA TAJWA HAPO  JUU  IPO  KWENYE UKURASA WA MIGOGORO YA WAFUGAJI NA WATUMIAJI WENGINE WA ARDHI

MADA ILIYOWASILISHWA NA PROF KURWIJILA

























































MADA ILIYOWASILISHWA NA PROF. MDOE


































        MADA ILIYOWASILISHWA MKOA WA TABORA 
























MADA YA KITUO CHA UWEKEZAJI TANZANIA WAKATI WA MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO MWANZA









































MADA YA TAASISI YA UTAFITI YA MIFUGO  TANZANIA (TALIRI)


































































MADA YA SEKTA YA MAZIWA TANZANIA ILIYOWASILISHWA KWENYE MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO MWANZA

















ZIARA YA WAZIRI MKOA WA TANGA 

HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI YA MHESHIMIWA DKT.TITUS MLENGEYA KAMANI (MB) KATIKA UFUNGUZI WA MAONYESHO YA KWANZA YA BIASHARA YA MAZIWA MKOA WA TANGA YALIYOFANYIKA KATIKA  VIWANJA VYA TANGA FRESH LTD,KANGE- JIJINI TANGA –TAREHE 15/08/2014

Mheshimiwa mkuu wa mkoa wa Tanga
Katibu tawala wa mkoa wa Tanga
Waheshimiwa wakuu wa wilaya ,
Waheshimiwa madiwani,
Kaimu mwenyekiti wa chama cha wafugaji Tanzania
Katibu wa chama cha wafugaji Tanzania
Mwenyekiti wa jukwaa la wadau  wa maziwa  Tanga
Mwenyekiti wa jukwaa la biashara ya maziwa Tanga
Mwenyekiti wa bodi ya kiwanda cha Tanga fresh ltd,
Mwenyekiti wa bodi ya ushirika  wa maziwa (TDCU)
Wawakilishi wa wadau wa jukwaa la maziwa Tanga ,SNV na AGRI-PROFOCUS,
Wanahabari ,
Wageni waalikwa ,
Mabibi na mabwana,

Awali ya yote napenda tumshukuru mwenyezi mungu  wa rehema kwa kutuwezesha wote kushiriki katika maonyesho haya muhimu siku  hii ya leo .ndugu wanajukwaa ,wafugaji wote , na wageni wetu napenda nianze kwa kuwasalimia kwa salamu ya wanamaziwa.MAZIWA……..
WANAJUKWAA NA WALIKWA WOTE ………..DHAHABU NYEUPE!!!!
Ndugu wanajukwaa,napenda kuwashukuru wanajukwaa la maziwa –tanga  kwa kunichagua  kuwa mgeni rasmi katika maonyesho ya kwanza ya biashara ya maziwa ya Tanga  ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwangu na mhe  Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa jamhuri wa muungano wa  Tanzania  kuiongoza wizara ya maendeleo  ya mifugo na uvuvi. Napenda kusema kuwa haya ni maonyesho ya kwanza ya kipekee yanayohusu maziwa .
Mimi binafsi na serikali kwa ujumla  nawapongezeni sana viongozi wa jukwaa  la wadau wa maziwa  Tanga na uongozi wa mkoa wa tanga kwa umahiri wenu  wa kuratibu shughuli za maziwa.wakati nakagua mabanda ya maonyesho  wiki ya unywaji wa maziwa  kitaifa mjini musoma , niliahidi kuja Tanga ili nijionee hali halisi. kinachonipa moyo zaidi ni kwamba kabla hata sijafika tayari mmebuni kitu kingine kizuri yaani JUKWAA LA BIASHARA  LA WADAU WA MAZIWA, hongereni sana.

Ndugu wanajukwaa faida kubwa  ya maonesho haya ni kukutanisha wadau, kutathimini mafanikio yaliyofikiwa na kutatua kero za wafugaji hususani zile zinazohusu kuongeza uzalishaji wa maziwa. Kutokana na umuhimu huo nachukua fursa hii kuagiza maonesho haya yafanyike kila mwaka  ili kuendeleza kazi hii nzuri mliyoanza. Tanga mmeanza muongozez njia.
Nimebaini kuwa tunaohusika pia na maonesho ya Wiki ya Maziwa na Nane Nane ni walewale, hivyo ninashauri maonesho haya yafanyike mwezi wa Septemba ili wadau wengi waweze kushiriki. Aidha nawapongeza sana kwa kushiriki maadhimisho ya Wiki ya Maziwa na Nanenane na pia kuandaa maonesho haya muhimu katika ngazi ya mkoa yaliyowezesha wadau kujionea , kukutana na kufanya biashara.
Ili kuboresha tasnia ya maziwa sekta ya mifugo kwa ujumla, serikali inabidi ishiriki kikamilifu kupitia wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya zote, Maafisa Mifugo, Kilimo na Ushirika wanapaswa watoe mwongozo kwa wadau wengine wa maendeleo. Hii ni muhimumsana ikizingatiwa kuwa tupo katika mfumo ambao ni shirikishi wa sekta ya umma na sekta binafsi maarufu kama ‘DDP’ katika kutekeleza shughuli za kiuchumi na maendeleo kiujumla.
Ndugu wanajukwaa, napenda pia kumshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tanga na Katibu Tawala wa Mkoa kwa kujitoa kikamilifu kufanikisha pamoja na malezi yao mazuri kwa Jukwaa hili la kihistoria la Wadau wa Maziwa Mkoa wa Tanga ambalo lina mchango mkubwa katika sekta. Katika Maad himisho ya Wiki ya Maziwa Kitaifa Mkoani Mara ni Jukwaa pekee la Tanga lililoweza kuleta washiriki zaidi ya 40. Nawapongeza sana Viongozi wa Jukwaa, Kiwanda cha Maziwa cha Tanga Fresh Ltd, Chama kikuu cha Ushirika cha Maziwa Mkoa wa Tanga (TDCU), Shirika la Maendeleo la Uholanzi –SNV Mtandao wa Kilimo na Biashara wa AGRI-HUB TANZANIA na wafugaji wote wa Mkoa wa Tanga kwa ubunifu wa kuanzisha Jukwaa la Mkoa la Biashara la Maziwa ambalo ni msaada mkubwa katika kutatua kero zao, lakini muhimu zaidi kukutana ili kufanya biashara na kubadilishana ujuzi na elimu.
Ndugu wanajukwaa, nichukue nafasi hii kuwapongeza jukwaa la Tanga kwa jinsi wanavyoratibu masuala yote ya kupunguza kero na kuongeza tija kwa wafugaji na haswa sauti ya mfugaji ngazi ya Mkoa na hivyo kuweka mazingira bora ya ufugaji. Nimepokea kwa furaha kubwa ombi la kuwa Mgeni Rasmi  katika Maonesho haya ya Kwanza ya Biashara ya maziwa kwa kuwa tangu kuteuliwa kwangu kuiongoza Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi haya ni maoneso ya KWANZA  yaliyosimamiwa na JUKWAA la Maziwa ngazi ya Mkoa. Binafsi pamoja na Serikali nawapongeza sana kwa ubunifu na uthubutu wenu .ni kweli ulio wazi kwamba ukitaka kujifunza  shughuli nzuri katika mnyororo wa thamani wa maziwa  njoo Tanga.
Ndugu wanajukwaa,nawakumbusha kuwa maonyesho haya yanalengo la kuunganisha wafugaji na watoa huduma waliopo katika mnyororo  wa thamani wa maziwa na pia yanazingatia changamoto zilizopo kama ambavyo wadau na watafiti  walivyobaini na huku watoa huduma  wataonyesha  wafugaji huduma wanazotoa .ni matarajio yangu kuwa  maonesho yatahamasisha  wafugaji kuwaelewa watakao ingia nao mikataba  katika vituo vya kukusanyia maziwa na hivyo kuleta huduma za uhakika karibu na shughuli zao za ufugaji yaani “DIARY BUSINESS HUBS” ni mategemeo yangu  pia kuwa mtayaendeleza  maonyesho haya muhimu kwa kila mdau wa jukwaa kushiriki kikamilifu kila mwaka ili kuendelea kutatua kero na kuleta tija katika kuongeza uzalishaji wa maziwa na kuboresha ng’ombe waliopo.

Ndugu wanajukwaa,nimefurahi kusikia kuwa jukwaa la wadau  wa maziwa Tanga linaundwa na wadau wa sekta ya maziwa mkoani Tanga na kwamba jukwaa linajitegemea na kufanya kuhudhuria vikao  mara nne kila mwaka . hili ni jambo la kuigwa kwani wngine bila posho hawawezi kukutana . nawapongeza sana na nawaomba mdumishe suala hili ili jukwaa liwe endelevu .
Ni muhimu sana jukwaa likaendelezwa na kujitegemea  bila kutegemea wafadhili kwa asilimia kubwa  na hivyo kuendelea kupata sauti kubwa zaidi , huku dhana ya PPP ikizingatiwa. Kupitia jukwaa matatizo ya kimfumo huonekana na kupata ufumbuzi  kwa wepesi zaidi  kwa wahusika wote .

Ndugu wanajukwaa,licha ya maonyesho lengo la mkusanyiko huu ni pamoja na :
          Kukutanisha wafugaji na watoa huduma bora za kisasa za ufugaji
          Kufungua njia ya wafugaji  kuingia mikataba na watoa huduma ili  wafanye ufugaji endelevu wa ,kisiasa na wakibiashara
          Kujifunza kutoka kwa wataalam na wafugaji waliofanikiwa
          Kuwatambulisha watoa huduma fursa za biashara zilizopo katika mkoa wa Tanga na hivyo wavutiwe kuwekeza kwa wafugaji na wafugaji nao wapate kuendelea zaidi
          Kuwakutanisha wadau na watafiti ,halikadhlika  washarika wa maendeleo na mashirika yasiyo yakiserikali.

Ndugu wanajukwaa, changamoto za wafugaji ni nyingi n azote haziwezi kutatuliwa na serikali peke yake .jukwaa ni sehemu pekee ambayo wadau wote pamoja na serikali wanakutana kujadili changamoto za sekta na kuzitafutia ufumbuzi kwa pamoja . maonyesho haya yamewakutanisha wauzaji wa  dawa za mifugo , wauzaji wa vyakula  vya mifugo, madaktari wa mifugo, watoa huduma za uhamilishaji, watafiti, watoa huduma wa uzalishaji wa ng’ombe, Wafugaji wa mfano, Taasisi mbalimbali za kifedha, Wauzaji wa Mitambo ya Biogesi, Watoa taarifa kama vile vituo vya radio na mitandao ya simu, Wafanyabiashara wa bidhaa za umemejua na wafanyabiashara wa bidhaa nyinginezo.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, ili kufanikiwa katika tasnia ya maziwa nchini , serikali imegawa maeneo ya kipaumbele kwa Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Mashariki, Kaskazini na Kanda ya Ziwa. Aidha, Serikali inaendelea kuhamasisha wafugaji kutumia zaidi teknolojia ya uhimilishaji na huku ikiongeza na kuimarisha vituo vya uhimilishaji nchini. Mathalani, ujenzi wa kituo cha kitaifa cha uhimilishaji kinajengwa Sao Hill-Iringa wakati vituo vya kanda vya Kibaha, Dodoma, Katavi, Mwanza na Mbeya vinazidi kuimarishwa ili kukidhi mahitaji ya mbegu bora yanayotarajiwa kuongezeka.  Serikali vilevile, inakamilisha ujenzi wa kituo kipya cha uhawilishaji viini tete (embryo transfer) kwenye taasisi ya utafiti wa mifugo Mpwapwa. Teknolojia hii inategemewa kuleta suluhisho la haraka katika ubora wa ng’ombe wa maziwa na hivyo tija kwa mfugaji. Napenda kutumia fursa hiikuwahamasisha wafugaji wa Tanzania kuwa muda wa kuanza kutajirika kutokana na mifugo ni sasa, karibisha maarifa mapya na teknolojia, chukua hatua sasa.
Mheshimiwa  Mkuu wa Mkoa, mifugo ni biashara, mifugo ni uchumi. Natamani  kuona wafugaji  wanatambulika kwa utajiri wao  na sio kwa mateso  wanayoyapata kutokana na mifugo yao . kukiwa na uwekezaji mzuri katika mifugo, Taifa litafaidika mikoa na  zitafaidika   na  mfugaji ataneemeka . Hivyo niwaombe mamlaka zote za mkoa , wilaya na vijiji zitenge maeneo mahususi kwa maendeleo ya ufugaji , siyo uchungaji . serikali kwa upande itaendelea  kuangalia maeneo  ya hifadhi  yaliyopoteza sifa , mashamba ya serikali  yasiyotumika vyema zikiwemo baadhi ya ranchi ya Taifa ili zitumike  kwa ufugaji . viwanda  vyetu vyote  74 vya maziwa nchini kikiwemo hiki chenu  cha Tanga  Fresh LTD vinasindika kwa wastani wa asilimia 35 tu ya uwezo wake. Hivyo ni muhimu sana  kuongeza idadi  na ubora wang’ombe  wa maziwa.
Ndugu wanajukwaa, katika kuongeza idadi ya ng’ombe  wa maziwa uzalishaji wa mitamba  hauwezi kuachiwa serikali peke yake ambayo kimsingi inasimamia sera . Hivyo ni vyema mkaongeza ushirikiano na sekta binafsi kama hao MZUAZI HEIFER  BREEDING UNIT-HALE , MANGARA DAIRY BREEDING –PONGWE, LAILA DAIRY AND AGRO CO LTD, na wengineo ili wajiapnue zaidi kuzalisha mitamba bora ya kutosha kukidhi mahitaji ya Mkoa na maeneo mengine ya nchi. Mahitaji ya Mitamba bora nchini inakadiriwa kuwa zaidi ya 60,000 kila mwaka wakati uwezo wa mashamba ya Serikali ni takribani mitamba 1,200 tu kwa mwaka.  Hivyo tunahitaji uwekezaji mkubwa katika eneo hili.
Ni muhimu Jukwaa la Maziwa Tanga likawaalika wenzetu kutoka taasisi za fedha kama vile TIB Development Bank, NMB n.k katika majukwaa na maonesho kama haya ili waweze kuona fursa hizi za uwekezaji na kutoa mikopo nafuu ili wadau waweze kujipanua kiuzalishaji kukidhi mahitaji.
Mheshimiwa  Mkuu wa Mkoa, yapo mabo mengi yamsingi yanayopaswa kuzingatiwa na mfugaji ili kuwa na ufanisi. Upatikanaji wa malisho ya kutosha wakati wa malisho wakati wa kiangazi na maji ni muhimu katika uzalishaji wa maziwa. Aidha, vyakula vya ziada ni vya lazima wakati wote na sio wakati wakati wa kuamua tu. Hivyo wenzetu wa TARILI, LITA Buhuri, Shamba la Mbegu za Malisho la Vikuge, Mruazi, Ofisi ya Mkoa wa Tanga na NAIC Usa river Arusha washirikiane ili mbegu za malisho pamoja na kuwajengea uwezo wafugaji kwa kuwapa mafunzo ya ujasiriamaji na ufugaji wa kisasa ili kuwa na ufugaji endelevu na kiwanda kupata maziwa ya kutosha. Kiwanda chenu kinahitaji kuwekeza karibu bilioni 10 ili kuongeza usindikaji pamoja na aina ya maziwa yanayokaa muda mrefu bila kuharibika (UHT). Hili litakuwa namanufaa tu iwapo iwapo kuna maziwa ya kutosha. Hata hivyo nipende kuwaahidi watu wa Tanga Fresh kuwa Wizara yangu itashirikiana nanyi dhidi ya changamoto zenye nia ovu.
Ndugu wanajukwaa, napenda kuchukua fursa hii kuzungumzia programu ya Unywaji Maziwa Shuleni hapa Tanga. Ipo mikoa ambayo wazazi na wakuu wa shule wanatamani kuwapatia wanafunzi angalau pakiti ya maziwa ya robo lita ya maziwa kila siku lakini wanashindwa kwa kuwa hawana uhakika wa kupata maziwa kila siku. Naomba wananchi wa Tanga mtambue neema ya kuwa na kiwanda ni kubwa nay a kipekee katika nchi yetu. Hivyo boresheni mpango wa Unywaji wa Maziwa Shuleni na kuhakikisha ni wa kudumu.
Ni vyema kufanya mashindano baina ya shule na vyuo ili kutoa hamasa ya unywaji Maziwa Shuleni. Vilevile wakuu wa shule za sekondari na msingi pamoja na vyuo hakikisheni mnatumia mikutano ya baraza na wazazi kuendelea kuwahimiza wazazi kulipa fedha kwa ajili ya watoto wao kupata maziwa kila siku. Uchangiaji wa wazazi wa gharama za kununua maziwa utafanya mpango huu kuwa endelevu,. Ninaamini kila mtu hapa anajua faida za maziwa mwilini na hasa kwa watoto na vijana. Maziwa ni lishe timilifu, ni muhimu sana katika makuzi ya motto.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, ufugaji ndio dawaya hakika na haraka dhidi ya umasikini katika Taifa letu. Hivyo nawaomba viongozi na wadau wote tushirikiane tuweke maono ya pamoja mbele, tukaze nia na mwendo, hakika tutashinda!
Mwisho niwakumbushe kauli mbiu ya maonesho haya isemayo:
‘TUMIA PEMBEJEO NA HUDUMA ZA KISASA KUONGEZA TIJA KATIKA UFUGAJI WA NG’OMBE WA MAZIWA’
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Ndugu Wanajukwaa, kwa kumalizia napenda sasa kutamka rasmi kwamba maonesho ya kwanza ya biashara ya maziwa yamefunguliwa rasmi!
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA.

TAARIFA  FUPI YA SHAMBA LA LAILA AGRO&DAIRY COMPANY LTD  KWA MHESHIMIWA WAZIRI
WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI 15/08/2014

Mheshimiwa mgeni Rasmi, Waziri wa mifugo na uvuvi Dr.Kamani, ninayofuraha kubwa kukukaribisha  kwenye shamba letu la mifugo  lijulikanalo kwa jina la Laila Agro &Dairy company  LTD lililopo kata ya pongwe halimashauri ya jiji la Tanga . 
Mheshimiwa mgeni rasmi, mimi binafsi mkurugenzi  na kwaniaba ya wakurugenzi wenzangu na wafanyakazi wote  tunatoa  shukrani zetu za dhati kwako  wewe binafsi na kwa uongozi mkoa wa Tanga
Na kwa wilaya Tanga kwa kutambua juhudi zetu na kuzithamini na kuziletea ugeni huu mzito shambani kwetu.
Mheshimiwa mgeni rasmi,  nitakua mwizi wa fadhila endapo sitatoa shukrani zangu za dhati kwa ugeni nilioletewa miaka miwili iliyopita ambapo tulitembelewa na muheshimiwa Waziri mkuu  Mizengo Pinda.
Ujio huo ulitupunguzia baadhi ya changamoto  ambazo tulikua nazo tunasema , Ahsanteni sana.

Mheshimiwa mgeni rasmi shamba letu  linaeneo kama ifuatavvyo:- 
v  Hekta 350
v  Ng’ombe 380
v  Tunakamua ng’ombe 80 
v  Tumekausha ng’ombe 45
v  Tunamitambo 80
v  Mitamba ya kati 65
v  Madume 75
v  Ndama 35
v  Tunazalisha lita za maziwa 880 kwa siku 

Aina ya ng’ombe tulio nao:-
v  Friesian,Ashier na Brown swiss 
v  Tunao wafanyakazi 15 wanaume  8na wanawake 7 hesabu ya vibarua hufuatana na hali ya msimu.
v  Kwa upande wa malisho tumepanda majani aina ya sirinkra,sirialisna roddes kwa shamba lote.
Uhusiano na majirani zetu.
Mheshimiwa mgeni rasmi,tunamshukuru mungu sana kwamba tu nauhusiano mzuri na majirani zetu na tunashirikiana nao vizuri.
Mheshimiwa mgeni rasmi, malengo yetu ifikapio mwishoni mwa mwaka 2016 tunakusudia tuwe na uwezo wa kuzakisha lita 5000 za maziwa kwa siku na tuwe na mitambo bora 100 ya kuuza kwa mwaka .
Mheshimiwa mgeni rasmi,  changamoto tulizo nazo hivi kwa sasa ni hizi zifuatazo:- kipindi cha kiangazi kinapokua mda mrefu  utatuzi wake ni umwagiliaji .Miaka miwili iliyopita tulichukua wataalam wa maji ardhini kupima maji  majibu yalionyesha maji yapo mengi na salama .Tulifuatilia kitengo cha umwagiliaji  gharama za michoro na vifaa ilikua kubwa sana , ilikua ni zaidi ya milioni mia mbili na hamsini (250,000,000/=) tulihairisha.
Mheshimiwa mgeni rasmi, ombi, Mheshimiwa Waziri kama kwenye wizara yako au serikali kwa ujumla kuna msaada wowote wa umwagiliaji tukipata malengo yetu  yatakua yamefanikiwa kwa asilimia tisini (90%) 
Mheshimiwa mgeni rasmi ,changamoto nyingine ni upande wa ufugaji ni hizi:-
1.      Maradhi;kulitokea tatizo la ugonjwa ng,ombe 18 walitupa mimba za miezi mitano hadi nane  ambapo ni hasara kubwa sana .
2.      Madawa yasiyo ya viwango yamekua ni kikwazo kikubwa sana kwetu.
3.      Wafugaji kuwa na thamani  duni kwa kupangiwa bei za mazao yao bila kushirikishwa kwa kisingizio cha soko huru.
4.      Upatikanaji wa miji na makazi hautambui uwepo wa wafugaji

HITIMSHO :-
Mheshimiwa mgeni rasmi, ninayasema haya kutokana na kauli yako uluyoitoa bungeni  kuhusu kuchangia mifugo iliyokua inauawa  kabla hujawa waziri ulisema “Mbali na wenye mali kupata hasara hata haki za wanyama hazikuangaliwa “HONGERA SANA .
Mheshimiwa mgeni rasmi ,mwisho kwA maoni yangu  Wizara imepata  JEMBE-CHAPAKAZI.
Mheshimiwa mgeni rasmi kwa pamoja  tutajenga nchi kila mmoja akitimiza wajibu wake. 

Daudi A.Nkya
Mkurugenzi  Mtendaji



TAARIFA YA USHIRIKA WA WAFUGAJI WA NG’OMBE WA MAZIWA (UWAKO)
KWA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI  TAREHE
16-08-2014.

Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya mifugo na Uvuvi,
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga ,
Mheshimiwa katibu tawala wa Mkoa wa Tanga,
Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya,
Waheshimiwa madiwani ,
Mheshimiwa mkurugenzi,
Mheshimiwa Mwenyekiti wa bodi ya TDCU,
Mwenyekiti wa jukwaa la wadau wa maziwa Tanga ,
Waheshimiwa wanaushirika,
Waheshimiwa wageni waalikwa mabibi na mabwana,
Itifaki imezingatiwa, ndugu wanaushirika,wafugaji wote wan g.ombe wa Maziwa na wageni wetu napenda sasa nianze kwa kuwasalimia kwa salamu ya ushirika
USHIRIKA- PAMOJA TUJENGE UCHUMI 

UTANGULIZI
Ushirika wa wafugaji wan g,ombe wa maziwa hapa Korogwe ulianzishwa mwaka 1994 kwa lengo la kuunganisha nguvu na sauti moja ya wafugaji ili waweze kukusanya maziwa na kupata soko la uhakika la mazao ya maziwa na kujikwamua kiuchumi.
Ushirika ulisajiliwa tarehe 18/02/1994 na kupewa namba ya TAR 246 ukiwa na wanachama 68 wanaume 40 wanawake 28. Kwa sasa wanaushirika tupo 77, wanaume 45 na wanawake 32. Ushirika umenunua hisa 19(kumi) kutoka kiwanda cha maziwa Tanga fresh ltd na pia ni mwanachama katika chama kikuu cha ushirika cha Tanga Daires co-operation union ltd (TDCU) ambacho ndicho chama kikuu kinachotokana  na muungano wa vyama vya msingi 12(kumi na mbili)vinavyojishughulisha na ufugaji wa ng’ombe wa maziwa wa mkoani Tanga. 

Ushirika huu ulipata mfadhili kutoka Netherlands(uholanzi)mwaka 1994 ambaye kwa kushirikiana na serikali waliweza kutafuta eneo hili la viwanda na kutujengea kituo hiki cha kutukusanyia maziwa . 

HALI YA CHAMA
Ndugu mgeni rasmi, 
Jumla ya wafugaji wanaoleta maziwa kituoni ni 144 kati ya hao wanachama ni 80 na vijana wanao nunua maziwa vijijini na kuleta kituoni(Bicycle Boys).64.

UKUSANYAJI WA MAZIWA
ushirika unauwezo wa kukusanya maziwa kiasi cha lita 800 kwa siku. Pia kuyahifadhi katika tanki lenye ujazo wa lita 3350.
MTAJI WA CHAMA 
Uwako una mali za aina mbili 
        I.            Mali za kudumu zisizo hamishika
·         Jengo
·         Shamba ekari 82 lipo eneo la mandela

      II.            Mali zinazohamishika
·         Tank lenye ujazo wa lita 3350
·         Jokofu
·         Jenereta na n.k


SHUGHULI ZA CHAMA
kupokea ,kuhifadhi na kupeleka maziwa kiwandani
kuuza maziwa yaliyo sindikwa 
MAFANIKIO 
Mafanikio tuliyo yapata
1)      Uwako imeweza kununua hisa katika banki ya ushirika zenye thamani ya TSHS.milioni tatu (3,000,000/=)
2)      Kujiunga na saccos ya mkoa (TDCU SACCOS)
3)      kununua hisa kwenye kiwanda cha Tanga fresh ltd
4)      Kujiunga na mfuko ya kijamii kama GEPF na NSSF
5)      Ufadhili toka Land “o”lakes

Chama kimepata ufadhili toka land “o” lakes na kupatiwa vifaa vifuatavyo:- 
-computer-1
-vifaa vya kubebea maziwa-75
-pikipiki-1
-mwanachama kupelekwa kusomea uhamasishaji na kupatiwa vifaa vifuatavyo kwa ajili ya chama :-mtungi mkubwa wa lita 35,mtungi mdogo wa lita 3,hewa baridi lita 38 na mbegu 20.
-tumefanikiwa kupandisha ng’ombe 152 mpaka sasa kwa miezi mitano ambao ni wastani wa ng’ombe 25 kwa mwezi. 
-wanachama wamewezeshwa kwa kupatiwa mafunzo mbalimbali ya ;- ufugaji bora ,ujasiliamali, Uwekaji kumbukumbu na ufugaji wa kisasa na kibiashara. 

CHANGAMOTO
Ndugu mgeni rasmi 
1)      Uvamizi wa eneo la chama .
E neo la chama limekua na mgogoro tangu mwaka 2011 na tangu Josiah William ambae alifungua kesi.APPLICATION NO OF 2011 Katika Baraza la Ardhi-korogwe ili atuhamasishe katika eneo hili na kutupa eneo hewa . kwenye kesi hiyo katika baradha la ardhi korogwe tulishindwa na wanachama  kwa kauli moja tuliamua  kukata rufaa kwa mahakama moja kuu ya Tanga ili wapate haki yao.katika rufaa hiyo, ushirika wa wafugaji tulipata haki yetu(tulishinda kesi) ili kinachosumbua ndugu Josiah wiliam akato pingamizi kuwa :-

·         Uwako isiendelee na kesi ya madai
·         Kesi isikilizwe upya 

Mahakama ilikubali kusikiliza pingamizi  basi itasikilizwa tena terehe 15/10/2014. 

2)      Upangaji wa bei
Vyama vya msingi  havihusishwi katika kupanga bei ya maziwa.

3)      Bei ya maziwa
Bei ya maziwa ni ndogo ukilinganisha na gharama za uendeshaji kwa mfugaji. 

Ufuatao ni uchanganuo wa mapato  na matumizi kwa ng’ombe anaetoa lita saba (7) kwa siku.

Mtumishi mkata majani               sh 2000

Kg 2 za pumba                                sh 500

Ununuzi wa maji                             sh  600
Madini                                                  sh 300

Chakula cha mtumishi                         sh 1000             
Ushuru wa chama                               sh  28

Jumla ya gharama za uendeshaji     sh 4628 

Maziwa lita 7@ sh.678=   sh    4746
Garama za uendeshaji     sh     4628
Faida                                   Sh       118 



4)      Magozwa ya mlipuko
      Kwa sasa magonjwa ya mlipuko ni tatizo kubwa katika wilaya yetu, na tunapouliza tunaelezwa na idara husika kuwa serikali imejitoa /haina fedha , lakini kwa upande wa kilimo kuna nguvu kubwa ya kuwasidia wakulima katika pembe jeio. Magonjwa kama homa ya mapafu, FMD,ugonjwa wa ngozi, ni tatizo kubwa na linapunguza nguvu za uzalishaji. hivyo tunaiomba wizara yako iangalie kwa mapana  ili kuweza kumsaidia mfugaji chanjo nyingine. Wafugaji wenyewe wanaweza kumudu/ kugharamia chanjo kama:-E.C.F.

MATARAJIO AU MALENGO YA BAADAE
malengo ya badae ya uwako ni kufanya yafuatayo:-
1.      kujenga kantini kwa ajili ya kuuza mazao ya maziwa yaliyo sindikwa 

2.      kujenga COLD ROOM  kwa ajili ya kuhifadhi mazao ya maziwa

3.      kujenga ghala kwa ajili ya malisho/vya kula vya ziada

4.      kujenga duka la pembe jeo 

MALENGO YA MDA MREFU 
-K upatiwa gari yetu yenye pozeo  kwa ajili ya kubebea maziwa yetu
-kupanda malisho kwenye shamba letu ili kuondoa changamoto wakati wa kiangazi ambapo ni tatizo kwa wafugaji wa ndani.(zero grazing).  

MAPENDEKEZO
Ndugu mgeni rasmi
                                  i.            Tunaomba idara ya Ardhi halmashuri ya mji korogwe itupimie eneo letu na kutumilikisha kwani kesi ya msingi ya ardhi imekwisha na nakala ya hukumu ya kesi tumepewa na kivuli chake tumekipeleka kwenye ofisi ya idara ya Ardhi. 



HITIMISHO 
Ndugu mgeni rasmi,
Tunashukuru kwa kutembelea kwenye ofisi yetu.

Naomba kuwasilisha.

USHIRIKA KWA PAMOJA TUJENGE UCHUMI


TAARIFA YA TAASISI KWA  WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI, MHESHIMIWA  DR.TITUS M. KAMANI (MB) ALIPOTEMBELEA
TVLA-VVBD   TANGA, 15/08/2014

1.UTANGULIZI
Taasisi ilianzishwa mwaka   1971 kama mradi wa utafiti wa kutokomeza ndorobo
(Tsetse research project-TRP)  Kwa kutumia tekinolojia ya kutaasisi ndorobo madume (sterile insect technique-SIT) MWAKA 1981 ilibadilishwa na kuwa taasisi ya utafiti wa ndorobo na malale (Tsetse&Trypanosomiasis Research institute –TTRI) Chini ya shirika la TALIRO . kutokana na kuundwa kwa wakalaza maabara  za mifugo Tanzania (Tanzania veritunary laboratory agency –TVLA) Taasisi ilipewa majukumu mapya na jina jipya  na kuitwa vector & vector –borne diseases Research institute –VVBD) mwaka 2012  .hivi sasa wajibu wetu umeongezeka kutoka kushuhulikia  mbung’o  peke ya ke na kuwa taasisi inayoshughulikia wadudu  na magonjwa waenezayo yanayoathiri  mifugo. 

2.JUKUMU LA TAASISI
          kutafiti, kubuni  na kusambaza mbinu rafiki ,rahisi na nafuu za kudhibiti wadudu na magonjwa yaenezayo kwenye mifugo nchini  kwa kutumia mbinu zinazoweza kutumika kirahisi na jan=mii nchini.
          Kutoa mafunzo yanayohusiana na wadudu  namagonjwa waenezayo kwenye mifugo kwa wanafunzi na wafugaji.
          Kutoa ushauri wa kitaalam kwa watunga sera juu ya wadudu na magonjwa waenezayo

3.UKUBWA WA TAASISI
Wafanyakazi wa taasisi
Taasisi inajumla ya wafanyakazi 42(watafiti12, maafisa ndorobo /mifugo wasaidizi11, watumishi wengine 20.
Eneo la taasisi
          Taasisi inaeneo la hekta 38 zilizomegwa  kwenye eneo kubwa  la kituo cha utafiti wa mifugo (Tanzania livestock Research institute –TALIRI Tanga )
          Taasisi inaeneo lngine lenye ukubwa wa hekta 5,320 lililokuwa  Livestock  Multiplication Unit-LMU mivumoni ilayani pangani.

Shamba hili lilikuwa ni shamba la kuzalisha mitamba (livestock multiplication unit )   kuanzia mwaka 1982 chini ya kurugenzi uzalishaji mifugo .Hata hivyo mpango huo ulipofutwa shamba liliachwa bila msimamizi na uvamizi ukaanza kujitokeza kwa shughuli zenye athari kwa mazingira na miundo mbinu ya shamba kwa kuona uhitaji wa kuwa na shamba la kufanyia utafiti wa magonjwa ya mifugo ,Taasisi ya utafiti wa ndorobo namalale ililiomba shaqmba hilo kutoka kurugenzi  ya uzalishaji wa mifugo mwaka 2003 shamba hilo lilikabidhiwa kwa taasisi hii Tangu wakati huo shamba hili limekua likitumika kama shamba darasa kwa ajili ya wanafunzi wanao somea Tasnia ya mbung,o(astashahada ,stashahada).hadi sasa Taasisi imekua ikipoea wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya mifugovya serikali na vya binafsi .pia linatumika kama shamba la dara sa kwa wakulima na wafugaji kutoka sehemu mbalimbali hasa kutoka mikoa yenye wafugaji asilia ili kujifunza mbinu mbalimbali za kudhibiti mbung’o katika mbuga za malisho.
Malengo makubwa ya sasa ya shamba hilo ni uzalishaji wa mitamba iliyo bora na mbuzi wa kisasa ili kuboresha ufugaji kwa maeneo yanayozunguka shamba na mengineyo ichini.
Majengo ya Taasisi
          Maabara 5

2.Nyumba za  wafanyakazi
Grade A-2, Grade B-1,gRADEc-2,Rest house -1, Nyumba ya mkurugenzi -1(iliyoko mwambani Tanga ).

Shamba la mivumoni Pangani
Ofisi  na majengo mengine 8,Nyumba za wafanyakazi 14, malambo 9, majosho 2, tanki la maji 1(bovu )kisima kimoja kilichochimbwa siku za karibuni .

Magari ya taasisi
          Yanayotembea -3
          Mabovu yanayohitaji matengenezo makubwa -3
          Magari chakavu -3(yanayotakiwa kuondolewa –disposed)
          Trecta moja ,tela na jembe lake

Ushirikiano
Taasisi ina ushirikiano mkubwa na mashirika yafuatayo
          Shirika la kimataifa la nguva la atomiki la Vienna (IAEA-Viena Austria)
          Shirika la afya la duniani (who)
          Bill and Melinda Gates foundation
          Mtandao wa kutokomeza malale Afrika mashariki na kati(EANETT)
          Pan African   Tsetse %Trypanomiasis Eradication  campaign (PATTEC)
          pamoja na vyuo vikuu vya ndani na nje  ya nchi.

TAFITI ZILIZOKWISHA FANYIKA KATIKA TAASISI PAMOJA NA MAFANIKIO
          KUtokomeza mbung’o kwa kutumia tekinolojia ya kutaasisi madume (SIT) 1994-1997,Zanzibar
          Kudhibiti mbung’o (tsetse  control) kwa utumia tekinolojia ya mitego na vitambaa vyenye dawa(targets)(Serengeti,selous,mikumi,sadaani, ngongoro n.k)
          Tafiti za mitego ya mbungo na vivutio vimefanyika kwa ajili ya aina tofauti za mbung’o  kwenye maeneo tofauti nchini mfano Tanga scoop
          Uchunguzi wa madawa ya kuua mbung’o kabla ya kusajiliwa nchini(Dominex,Decatix,ectopor,grenade,ectomin.Amitraz)

          Kushiriki katika kutafiti njia ya haraka na nyepesi ya kutambua vimelea vya malale katika wadudu (xenomonitoring) ili itumike kubaini mlipuko wa ugonjwa wa malale kabla haujalipuka (early warning tool)

KAZI ZINAZOENDELEA
          Matokeo ya utafiti hasa yavitambaa vyenye dawa hivi sasa yanatumika kuondoa mbung,o katika hifadhi zataifa nchini (Serengeti ,Ngorongoro,mikumi katavi,selous,tarangire n.k) na katika baadhi ya almashauri nchini kama vile rufiji ,Handeni ,chunya monduli,kilindi liwale,kilwa,lindi,Kigoma,tabora n.k
          Kutoa mafunzo kwa wakulima na wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi

Ufugaji a ng’ombe ,mbuzi na kondookwenye shamba la mivunoni:mkakati wa kuzalisha ng,ombe aina ya Mpwapwa breed kwa wingi kwa ajili ya wafugaji wa ,maeneo yaliyoko Tanga na mikoa ya jiani inaendelea ,Hivi sasa tuna ng’ombe 201, mbuzi na kondooo 76,mpango wa kuongeza ng’ombe  aina ya mpwap[wa  kwa ajili ya kuzalisha na kusambaza kwa wafugaji uanendelea (tayari jumla ya shilingi milioni 10 zimeshalopwa kwa ajioli ya kuongeza ng.ombe zaidi) pia mpa ngo wa kuzalisha zaidi mbuzi zaidi unaendelea kwaq kutumia madume bora ya aina Tonge nburgn  and saanen.
          Kutoa mafunzo darasa kuhusu ufugaji bora wa mifugo kwa wanafunzi kutoka vyuo vyetu hapa nchini kwa kutumia shamba la mivumoni na kwa wafugaji wanaoplizunguka shamba.
          Uchunguzi wa magonjwa wa mifugo pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam ili kudhibiti magonjwa ya mifugo.
          Uzaji wa jumla na rejareja wa chanzo za kideri /mdondo
          Ulimaji na uvunaji  wa hey kwenye hektari 1000 kwa ajili ya kuwauzia wafugaji.

MATARAJIO YA BAADAE
          Kuanza ufugaji wa ng’ombe wa maziwa oili kutumia fursa iliyopo wa kiwanda cha maziwa Tanga fresh
          Kuongeza uzalishaji wa mitamba bora ( Mpwampwa breed) ambayo imekua ikiulizia Sna na wafugaji.
          Ufugaji wa nyuki wasiouma pembezoni mwa shamba ili kuvuna asali na kuongeza kipato.
          Kuongeza ekari 500 za eneo la kuvuna na kufuga hay ili kufikia ekari 1500
          Uwezekano wa kufuga fruit flies kwa ajili ya kudhibiti wadudu waharibifu na matunda kwa kutumia tekunolojia ya kutaasisi madume.mchakato huo unaendelea.
          Kutokomeza mbung’o wilayani kilosa na Serengeti kwa kutumia SIT
          Kuwa na mtambo wa liquid nitrojen plant kwa ajili ya ukanda wa Pwani mchakato wake unaemdelea .

CHANGAMOTO
          Upungufu mkubwa wa vitendea kazi ili kufanikisha  shughuli za utafiti
          Upungufu wa wawafanyakazi (wanao staafu ni wengi kuliko wanaoajiriwa )no technical succession)
          Uvamizi wa shamba la mivumoni (karibu ekari 1000 zimevamiwa na wakulima )
          Taasisi haina uzio hivyo kuhatarisha usalama wa mali za taasisi.
          Uchakavu wa majengo ya Taasisi

Nawasilisha
Dr. Imma Malale,
KAIMU MENEJA ,
TVLA-VVBD


TAARIFA YA KITUO
KUTOKA:   KITUO CHA UTHIBITI UBORA WA MAZAO YA UVUVI NA MASOKO  KANDA YA      KASKAZINI   TANGA


KWENDA:   WAZIRI WA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI

UTANGULIZI;
Kituo cha uzibiti ubora wa mazao ya Uvuvi na Masoko kanda ya kaskazini kilichopo mkoani Tanga kilianzishwa mnamo ,mwaka 2000 kikiwa na mtumishi mmoja .Baada ya muda wa mwaka mmoja akaongezwa mtumishi wa pili na kufika hadi hivi leo kitengo kina jumla ya watumishi wanne. 
Kanda ya kaskazini inajumla ya mikoa mine ambayo ni Tanga ,Kilimanjaro,Arusha,na Manyara.kitengo kina jukumu la kulinda ,kusimamia na kudhibiti ubora wa mazao ya uvuvi yanayosafirishwa  ndani na nnje ya nchi pamoja na kusimamia ukusanyaji wa maduhuli kwa kushirikiana na kituo cha Doria  uvuvi katika kanda hii ya kaskazini.Kituo kina gari moja (01) aina ya Nissan Quaqui na pikipiki moja (01)DT250.

KAZI ZA KITUO
Lengo kuu la kituo ni kuthibiti ubora na usalama wa mazao ya uvuvi kwa watumiaji /walaji ndani na n je ya nchi na kusimamia masoko ya mazao ya uvuvi kwa kutekeleza sera ya mwaka 1997, sharia ya mwaka 2003 na kanuni ya mwaka 2009 na uvuvi. Ili kufanikisha lengo hili kituo kinafanya malengo mahsusi kwa: 
·         kwa kufanya ukaguzi katika viwanda vya uchakataji /usindikaji wa mazao ya uvuvi,mialo na masoko ya uvuvi.
·         Kisimamia na kufanya kaguzi katika mipaka iliyopo kwenye kanda ya kaskazini .
·         Kutoa vibali vya usafirishaji mazao ya uvuvi ndani na nnje ya nchi.
·         Kutoa elimu kwa wavuvi ,wauzaji wa mazao ya uvuvi na wasindikizaji/wachakataji wa mazao ya uvuvi viwandani .
·         Kusimamia makusanyo ya maduhuli yatokanayo na usafirishaji wa mazao ya uvuvi ndani nan je ya nchi.  

VYANZO VYA MAPATO
Kituo kinakusanya maduhuli kutokana na ukusanyaji wa ushuru wa mazao ya uvuvi yanayosafirishwa nje ya nchi yakitokea hapa jijini Tanga ,faini ya makosa yanayofanywa na wavuvi(compoundment)kama vile kuvua kwa kutumia vyombo visivyosajiliwa,kusafirisha mazao ya uvuvi bila kibali,kuvua bila kuwepo na leseni halali ya uvuvi. 

MAFANIKIO 
Kitengo kimefanikiwa kusimamia ukusanyaji wa maduhuli jumla ya shilingi milioni 28,113,318.15 ambazo ni asilimia 28%

Kituo kimeweza kuwabadili wavuvi hasa wa pweza kuvua pweza wenye uzito wa gram 500 na kuendelea.pia kituo kimeweza kuwapa elimu ya kuhifadhi mazao ya uvuvi kwa ubora na usalama kwa kutumia cool box.
Kilimo kimesaidia kupatikana kwa soko la kudumu kwa wavuvi wadogowadogo kwa kuhamasisha uongozi wa k8iwanda cha kusindika mazao ya uvuvi kununua mazao ya uvuvi ya wavuvi hao.

CHANGAMOTO 
1.Kituo kinakabiliwa na uhaba wa vitendea kazi
2. Kituo kina gari  1 linahitajika lingine
3.Ofisi ya kituo inahitaji matengenezo 

Nawasilisha,                     
Neema I. Respickius
Kny.Kaimu Afisa Mfawidhi,
Kituo cha Uthibiti ubora wa masoko na uvuvi-Tanga



KUTOKA; KITUO CHA UZALISHAJI VIFARANGA NA UKUZAJI  SAMAKI (MACHUI-TANGA)
KWENDA: WAZIRI WA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA MAENDELEO
YA UVUVI

TAARIFA YA KITUO CHA KUTOTOLESHEA VIFARANGA  WA SAMAKI MACHUI- TANGA
UTANGULIZI  
Ujenzi wa kituo cha kituo cha kutotoleshea  vifaranga wa samaki  Machui ni moja kati ya mipango ya muda mrefu wa wizara ya mifugo na maendeleo  ya uvuvi ikitekelezwa na idara ya ufugaji wa viumbe vya majini(Department of Aquaculture) Baada ya idara kugundua kuwa ufugaji wa samaki hauendi sambamba na  mahitaji ya viafranga  vya samaki, wizara iliagiza idara ya ufugaji viumbe kwenye maji ikishirikiana na Halimashauri ya jiji la Tanga kuanzia ujenzi wa kituo mwezi  agost mwaka 2013. Eneo la machui linaukubwa war obo hekta lilinunuliwa katika kijiji cha  Machui kupitia Afisa Mtendaji  kwa kiasi cha 1,500,00/=

HATUA YA UTEKELEZAJI 
Wizara ya maendeleo ya Mifugo na uvuvi inatekeleza kazi ya ujenzi wa kituo  cha kutotolesha vifaranga vya samaki machui-Tanga kulingana na upatikanaji wa fedha za maendeleo.Mpaka  sasa kituo kimejenga matanki sita (6) matanki matatu yalijengwa kwa fedha za maendeleo 2012-2013 na matanki mengine matatu pamoja na kingo za hatchery zilijengwa katika fedha za maendeleo  za mwaka 2013-2014.Matanki matano (5)tu ndio amabyo tayari yamepandwa vifaranga wapatao 698 wa aina ya perege(tilapia) mwatiko  (milk fish) na mkizi. Tanki moja   ado halijawekwa maji kutokana na kupata nyufa . Samaki walipopandwa ndio watakao tumiwa kuzalisha vifaranga wapya  wa samaki(BROODSTOCK)  samaki hao wanakula chakula cha asili kinachozalishwa kwenye bwawa kwa kutumia mwanga wajua (PHOTOSYNTHESIS)  

1.         UJENZI WA MAABARA ,OFISI NA NYUMBA ZA WATUMISHI 
Kazi hii inatarajiwa kutekelezwa katika eneo la Kivindana na ndipo itakapokua ofisi kuu ya kituo.
2.         KUVUTA UMEME
Kazi ya kuuta  umeme inatarajiwa kutekelezwa haraka iwezekanavyo,umeme utavutwa kutoka njia kuu ya umeme baada ya wataalam  wa Tanesko kufanya soroveya kuelekea maeneo  ya ofisi za kituo na matanki ya kuzalisha (kivindani  na machui)
3.         WATUMISHI  
Kituo kinawatumishi wawili(2)  wenye elimu ya shahada na stashahada  ambao wanasimamia na kuendeleza shughuli za kituo .Ikiwa ni pamoja na kutoa ugani kwa wafuga samaki  na wakulima wa mwani.
4.         MIPANGO YA BAADAE 
I.          Kuongeza upatikanaji na uzalishaji wa vifaranga  vinavyo faa kufugwa kwenye maji bahari  kwa ajili ya wafugaji waliopo mkoa wa Tanga . 
II.         Kutafuta maeneo yenye majangwa ya chumvi ili kupanua  mashamba (mabwawa) ya kufugia samaki . 
III.        Kuchukua vifaranga vya oreochromis urolepis kutoka kituo cha utafiti cha pangani (IMS-KIMU) Nakuanza kuwazalisha hapa kituoni  kwa ajili ya wafugajui waliopo mwambao  wa bahari ya Hindi. 
IV.        Kutafuta eneo ili kushirikiana na wazalishaji wa chumvi  kukuza ‘artemia’ 
V.         Kukamilisha makubaliano ya idara  ya ukuzaji viumbe na kijiji  cha kivindani kwa ajili ya kupata eneo kubwa zaidi la kujenga ofisi,hatchery pamoja na mabwawa,hii itasaidia kuweka mazingira yanayofaa kwa ajili  ya samaki wa mapambo na michezo.

5.         CHANGAMOTO 
I.          Mpaka sasa kituo hakina gari wala pikipiki kwa ajili ya watumishi kwenda kituoni  machui na kwenda  kutoa elimu ya ugani kwa wafugaji samaki waliopo mkoa wa Tanga .
II.         Kupitiwa ofisi kwenye jengo la coastal zone pamoja na vifaa vya ofisi .
III.        Vifaa vya kupimia maji (Techinical equipments) 
IV.        Upungufu wa watumishi (mlinzi wa kituo) 
V.         Pump ya kusukuma maji kuingia kwenye matanki.
VI.        Kumalizia ujenzi wa ‘hatchery’ 

HITIMISHO
Wizara ya maendeleo ya mifugo na uvuvvi kwa kushirikiana na halmashauri ya jiji la Tanga inahakikisha mwendelezo wa ujenzi na ufanisi  wa kituo cha machui kwa ustawi wa wananchi wa Tanga na kanda yote yay a kaskazini kwani kuitafungua ajira ,kuongeza kipato na uhakiki wa chakula  bora na salama .
Nawasilisha.
OMARY ALLY MOHAMED
AFISA   MFAWIDHI
KITUO CHA KUTOTOLESHEA VIFARANGA MACHUI
TANGA



KUTOKA; KITUO CHA DORIA UVUVI TANGA
KWENDA; WAZIRI WA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
TAARIFA YA KITUO CHA DORIA UVUVI KANDA YA KASKAZINI-TANGA

UTANGULIZI; 
Kituo cha Doria Uvuvi- kanda ya kaskazini chenye makao yake makuu katika jiji la tanga, kilianzishwa tarehe 14/12/2005,kikiwa na jumla ya wafanyakazi watano(05). Kituo kinafanya kazi katika mikoa ya Tanga Kilimanjaro,Arusha na manyara pamoja na mipaka yote inayopakana nan chi jirani ya Kenya katika suala zima la ulinzi wa rasilimali za uvuvi na ukusanyaji wa maduhuli. Aidha vipo vituo vidogovidogo vya horohoro na namanga vilivyo katika mipaka ya nchi jirani ya Kenya ambayo jukumu lake kubwa ni kukusanya maduhuli yanayotokana na usafirishaji mdogo wa mazao ya dagaa wakavu kwenda nchi jirani ya Kenya pamoja na kuhakiki uhalali wa mazao mengine yote ya uvuvi yanayosafirishwa kwenda nje ya nchi kupitia katika mipaka hiyo na kudhibiti utoroshaji kupitia njia zisizo halali.
Kituo kina gari moja (01) aina ya Toyota land cruiser,pikipiki moja (01)xl250,boti nne mbili zikiwa inboard engine na mbili aina ya outboard engine.
KAZI ZA KITUO
Kituo cha doria uvuvi-kanda ya kaskazini kina jukumu la kulinda na kusimamia rasilimali za uvuvi pamoja na kukusanya maduhuli katika kanda hii ya kaskazini .
Kituo kilipewa lengo la kukusanya maduhuli yasiyopungua  jumla shilingi 100,000,000/= milioni mia moja katika mwaka wa fedha 2013-2014,ikiwa pamoja na kufanya doria 144 za majini nan chi kavu zenye kujumuisha watendaji (mandays)1440. 
VYANZO VYA MAPATO 
kituo kinategemea kukusanya maduhuli kutokana na ukusanyaji wa ushuru wa  mazao tya baharini yanayosafirishwa nje ya nchi yakitokea hapa jijini Tanga ,faini ya makosa yanayofanywa na wavuvi(compoundment) kama vile kuvua kwa kutumia vyombo visinyo sajiliwa, kuvua bila kuwa na leseni halali za uvuvi pamoja na ada ya leseni za uvuvi wa samaki wa mawindo/michezo.

MAFANIKIO
kituo kimeweza kuunganisha wilaya zote za pwani Tanga mjini, Pangani, Mkinga na Muheza) na kufanya doria shirikishi katika maeneo yote ya mwabao mwa Bahari ya Tanga kabla ya hapo kila wilaya ilikua ikifanya doria yake katika eneo lake na kupeleka baadhi ya maeneo ya wilaya husika kutofanya doria kwa mda mrefu.
Kupunguza kwa kiasi kikubwa uvuvi haramu  wa kutumia baruti,makokoro(beach senie)sumu, nyavu za utale(mohofilament)na mikuki.

UKUSANYAJI MADUHULI 
katika mwaka wa fedha 2013-2014 kituo kilipewa lengo la kukusanya jumla ya shilingi milioni mia moja (100,000,000/=) kwa kufanya doria 144 zenye watendaji(mandays)1440.lakini kituo kiliweza kukusanya jumla ya shilingi 28,113,318.15 ambazo ni sawa na asilimia 28% tu ya lengo ya kiasi kilichotakiwa  kukusanywa .kiasi  hicho kilikusanywa kutokana na doria  46 zilizofanywa zikiwa  na nguvu kazi (mandays)460 sawa na asilimia 32%tu ya doria zilizotakiwa kufanyika  na idadi ya watu waliotakiwa kufanikisha Doria zote.  

CHANGAMOTO 
1.         Kituo kinakabiliwa na uhaba wa vitendea kazi, na matengenezo ya boti. 


Nawasilisha,       
Hassan M. Kufuku,
Kny. Afisa Mfawidhi,
Kituo cha Doria Uvuvi-kanda ya kaskazini,
Tanga.


TAARIFA YA KAMPASI YA BUHURI KWA  MHE. DKT.TITUS KAMANI WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI.TAR. 16 AUGUST 2014.
Ndugu,
          Mheshimiwa Waziri
          Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa
          Mheshimiwa Katibu Tawala Mkoa
          Waheshimiwa Viongozi mbalimbali wa Serikali
          Watumishi wa LITA
          Mabibi na Mabwana.
Mheshimiwa Waziri
Napenda kuchukua nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kuwa na afya njema lakini pia kukufikisha salama katika kampasi yetu ya Buhuri na hivyo kupata nafasi ya kuwa pamoja asubuhi hii ya leo.
Mheshimiwa Waziri nichukue nafasi hii kukukaribisha pamoja na viongozi wengine ulioambatana nao katika kampasi yetu ya LITA Buhuri na napenda kusema kuwa tunafarijika sana kwa kuwa pamoja nanyi nasi tutajitahidi mjisikie mko nyumbani.
Mheshimiwa Waziri
Kampasi ya LITA Buhuri ilianzishwa kama Chuo cha Mafunzo ya Mifugo mwaka 1980 kwa ushirikiano kati ya serikali ya Uholanzi na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Madhumuni ya makubaliano yalikuwa ni:
          Kutoa mafunzo na stadi mbalimbali kwa wafugaji vijijini katika fani ya ufugaji bora wa ng’ombe wa maziwa.
          Kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wa mashamba makubwa ya ng’ombe wa maziwa.
          Kutoa mafunzo ya rejea kwa maafisa ugani.
          Kituo cha mfano kwa ajili ya uzalishaji maziwa
          Kituo cha mafunzo kwa vitendo. (Field Practical Attachment) kwa awanafunzi wa vyuo vya kilimo/Mifugo.
Mheshimiwa Waziri
Kumekuwepo mafanikio makubwa kwa ujumla kulingana na madhumuni ya kuanzishwa kwa chuo kwa wakati huo kwani
          Wafugaji 8,335 kati yao 2,881 wakiwa wanawake (34.6%) na wanaume 5,454 (65.4%) walipata mafunzo.
          Maafisa Ugani 537 walipata mafunzo ya rejea.
          Jumla ya wafanyakazi 215 wa mashamba makubwa ya ng’ombe wa maziwa walipata mafunzo.
Mheshimiwa Waziri.
Mwaka 2007, Kampasi ilianza kutoa mafunzo ya muda mrefu na stashahada ya uzalishaji wa wanyama (Diploma in Animal Production), ambapo Juni 2011 jumla ya wahitimu 289 walimaliza mafunzo hayo na wengi wameajiriwa katika sekta mbalimbali za mifugo na wengine kujiajiri.
Mwaka 2012 kampasi ilianza kutoa mafunzo ya Astashahada ya Afya na Uzalishaji Mifugo baada ya Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kuhuisha mitaala katika vyuo vya mafunzo ya mifugo. Ambapo wanachuo 103 (wasichana 31 na wavulana 72) walihitimu mafunzo yao mwezi Juni 2014 na wengine 101 (wasichana 32 na wavulana 69)wapo mwaka wa pili.
Mheshimiwa Waziri
Katika mwaka wa masomo utakaoanza mwezi Septemba 2014 kampasi inatarajia kudahili wanafunzi 135 wa mwaka wa kwanza na hivyo kuwa na jumla ya wanafunzi 236 ongezeko la wanafunzi 32.
Mheshimiwa Waziri
Mwezi Septemba 2011 Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi iliunda wakala wa Vyuo vya Mfunzo ya Mifugo –Livestock Training Agency (LITA) ili kuongeza ufanisi wa kiutendaji ambapo kila kimoja ya vyuo hivyo LITIs imekuwa Kkampasi ya LITA, hadi sasa LITA ina kampasi 6 na vyuo 2.
Mheshimiwa Waziri
Kampasi ya Buhuri ina jumla ya watumishi wa kudumu wa kudumu 42 kati ya hao wakufunzi 15 na watumishi watendaji 27 pamoja na watumishi wengine wa maktaba 31 ambao kwa pamoja tunasaidiana katika shughuli za kiutendaji na utawala.
Mheshimiwa Waziri
Kampasi ina eneo lenye ukubwa wa hekta 885 ambapo ndani yake kuna maeneo ya malisho, majengo ya makazi na ofisi pamoja na vitengo mbalimbali vya uzalishaji. Ambapo idadi ya mifugo ni kama ifuatavyo:
Jedwali 2. Idadi ya Mifugo Kampasi ya Buhuri

Aina ya Mifugo           Idadi
Ng’ombe majike         224
Ng’ombe madume      70
Jumla   294
Mbuzi  57
Kondoo            26
Nguruwe         12

Pia kampasi imekuwa ikizalisha na kusambaza ng’ombe wa maziwa kwa wahitaji mbalimbali. kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali na. 3.

Mheshimiwa Waziri
Malengo ya wakala kuhusiana na kuendeleza kampasi kuwa kituo mahili katika utoaji wa taaluma na uzalishaji ni pamoja na:
Upanuzi wa kampasi ili kuongeza udahili wa wanachuo.
Kwa sasa Kampasi ina wanafunzi 204. Kampasi hii ina mpango wa kuongeza idadi ya wanafunzi wa Astashahada hadi hadi kufikia 300 ifikapo mwaka 2016. Pia tuna mpango wa kuhamisha kozi ya uendeshaji wa nyanda za malisho na uthibiti wa Ndorobo inayoendeshwa katiak Kampasi ya Morogoro baada ya kukosa eneo la kufundishia kutokana na Dakawa Pilot Unit (DPU) iliyotengwa kwa malengo hayo ya serikali kubinafsishwa.
Kuanzisha Ranchi
Kitengo hiki kitakuwa kielelezo cha mafunzo kwa vitendo na kitatumika kwa uzalishaji. Eneo lililotengwa kwa ajili hiyo ni hekari 370 likiwemo eneo linalotumiwa na Holland Diaries Ltd, ambao unatarajiwa kuanza mwaka 2016 na inakadiriwa mradi huu utagharimu Tsh. bilioni 1.3.
 Uzalishaji wa mitamba bora wa ng’ombe wa maziwa 50 kwa mwaka kwa ajili nya kampasi na wafugaji.
Uendelezaji wa nyanda za malisho kila mwaka hekta 45 kwa ajili ya ng’ombe wa maziwa, hifadhi na uvunaji mbegu kwa ajili ya wafugaji. Kazi hii itafanya kwa kushirikiana na wanafunzi wetu, wafanyakazi wa maktabana wafanyakazi wa kudumu.
Kuanzisha kituo kidogo cha usindikaji maziwa (min processing plant) ili kuongeza thamani ya maziwa tutakayozalisha katika kampasi yetu. Makadirio ya thamani ya mradi huu ni shilingi milioni 108.
Upanuzi wa kitengo cha nguruwe kufikia idadi ya nguruwe 120 na ufugaji wa kuku wa mayai kufikia 1,000 utekelezaji wa mradi huu unaanza mwaka huu wa fedha 2014/2015.
Kuongeza uzalishaji wa mifugo na mazao yake mbalimbali kwa ajili ya kuongeza pato ambalo litatumika katika shughuli za uendeshaji mafunzo hivyo kupunguza utegemezi wa chuo kwenye bajeti ya serikali.
Kwa siku za usoni tunafikiria ufugaji wa ngamia na nyati.
Mheshimiwa Waziri
Pamoja na mafanikio tuliyoyapata Kampasi imekuwa na changamoto mbalimbali ambapo kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi pamoja na uongozi wa mkoa na wadau wengine wa maendeleo tunaendelea kuzitafutia ufumbuzi.
          Kampasi ina mgogoro na Holland Dairies Ltd ambao walipeleka shitaka mahakamani kuhusu kuondoka katika eneo la hekari 205 ambalo waliazimwa na Wizara kwa mkataba toka mwaka 2004. Madai ya awali ya kuwa eneo hilo wamilikishwe, yalikwishatolewa hukumu na mahakama kuu tarehe 15/7/2011 ya kwamba eneo hilo ni la kampasi na hivyo wanatakiwa kuondoka.
          Upimaji wa eneo la Kampasi umekamilika hatua inayofuata sasa ni kupata Namba ya eneo (Plot Number) kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ili kuwezesha kutengeneza hati. Vielelezo mbalimbali vilikwishapelekwa wizarani kwa ajili hiyo kwa sasa kinachosubiriwa ni Wizara kutoa anamba ya eneo ili masuala ya hati yaweze kufuatiliwa.
Kuwa na wafanyakazi wengi ambao ni vibarua (mishahara milioni 3.4 kwa mwezi)
Uhaba wa majengo:-
·         Madarasa 2 bwalo la chakula na jiko
·         Maabara na maktaba
·         Mabweni ya wanafunzi
·         Ufinyu wa mtaji wa kuendeleza shamba na kutekeleza miradi iliyopangwa.
·         Vyombo vya usafiri havitoshi (hard top- pikipiki -2 Lorry-1 Mini Bus 1)
·         Uchakavu wa miundombinu kama mashine ya kukamulia, mabomba ya maji na nyumba za wafanyakazi.
Mheshimiwa Waziri
Tunapenda kutoa shukrani kwa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kwa jitihada inazozifanya kutuwezesha kwani imeendelea kulipa mishahara kwa watumishi japokuwa tumekua LITA. Tunaishukuru Wizara kwa kutuwezesha kuanzisha kituo cha Artifical Insemination (AI) kwenye Kampasi yetu hii itakuwa chachu kwetu kuongeza idadi ya ng’ombe waliobora zaidi. Pia naishukuru Serikali kwa kuendelea kuwafadhili wanafunzi wetu katika masomo yao.
Napenda kuchukua nafasi hii kushukuru uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Tanga kwa jinsi tunavyoshirikiana nao katika shughuli mbalimbali za kiutendaji.
Napenda kutoa shukrani zangu kwa LITA makao makuu kwa kushirikiana vyema na uongozi wz Kampasi katika kuhakikisha kuwa tunapata mafanikio tunayotazamia.
Natoa shukrani zangu kwa taasisi za mifugo zilizopo jijini Tanga hususani TARILI na TVLA kwa kutupa ushirikano mkubwa ambao umechangia sana katika mafanikio yetu.
Nawashukuru pia wadau wetu wa cmaendeleo SNV, TDBP, Land O’Lakes na jamii inayotuzunguka katika ushirikiano wao na kampasi yetu.
Ahsanteni
Naomba kuwasilisha
Paul Kidangaking’we Shempemba
KAIMU MKURUGENZI WA KAMPASI.


TAARIFA FUPI YA UVUVI - KATA YA KIGOMBE KWA MHESHIMIWA
WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI.


UTANGULIZI.
Mheshimiwa Waziri, Kata ya Kigombe ina jumla ya wafanyakazi wapatao 5,675 jwa sense ya mwaka 2012.idadi kubwa ya wavuvi inatoka  katika kijiji cha kigombe ambao wanafikia 255,hata hivyo eneo la kigombe  hupata wavuvi wageni kutoka pemba na unguja wapatao150 kwa mwaka. Eneo la uvuvi katika kata ya kigombe ni kilomita 15 kuanzia eneo la gawani hadi dahali (coatal line). 

Mheshimiwa Waziri,Katika kata ya kigombe kuna bandari ya uvuvi na soko la samaki ambalo moja ya shughuli zake ni uthibiti wa mazao ya uvuvi, uwepo wa soko hili hupelekea upatikanajio wa twakimu halisi ya mazao ya uvuvi, kuwepo uwiano wa bei kati ya mvuvi na mlaji na urahisi wa ukusanyaji wa madhuhuli yanayotokana na uvuvi(leseni na ushuru wa samaki). 
Mheshimiwa Waziri,Katika kiasi cha samaki kinachovunwa kwa mwaka ni wastani wa tani 49.72 ambazo thamani yake ni Tsh.159,104,000/= makusanyo ya halimashauri kutokana na leseni pamoja na ushuru ni wastani wa tsh .6,955,200/= kw a mwaka. 
Mheshimiwa Waziri, juhudi za serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2008/2009 halmashauri ilipokea jumla ya shilingi 118,262,037.50(macemp) kwa ajili ya kuwezesha vikundi  vitano vya wavuvi kigombe  na vingine vitano vya wafugaji kuku wa asili, lengo lilikua kuwajengea uwezo wa kiuchumi wavuvi na wananchi wanaoishi mwambao  wa pwani ya bahari ya hindi. 

CHANGAMOTO.
Mheshimiwa waziri,changamoto kubwa iliyopo ni pamoja na :- 
·         Uvuvi haramu wa kutumia baruti na nyavu zenye macho madogo(majuya)
·         Ufinyu wa bajeti kwa ajili ya kuendesha shughuli za doria na elimu kwa wavuvi juu ya uvuvi endelevu. 
·         Uhaba wa wataalamu na vitendea kazi katika sekta ya uvuvi(halmashauri ina mtumishi mmoja) 


Mheshimiwa waziri,pamoja na changamoto zinazo tukabili  wilaya inaendelea na shughuli za kutoa elimu kwa wavuvi ili kuwa na uvuvi endelevu  na kufanya doria za mara kwa mara za udhibiti wa wavuvi haramu kwa kushirikiana na uhifadhi wa bahari(marine park). 

MAPENDEKEZO  .
Mheshimiwa waziri,baadhi ya mapendekezo ambayo tunazani yatasaid8ia kuwa na uvuvi endelevu ni pamoja na:-
·         Kuendelea kutoa elimu ya matumizi endelevu ya rasilimali. 
·         Kuanzisha shughuli mbadala za kiuchumi kwa wananchi wanaoishi pembezoni mwa bahari.
·         Serikali kuu na halmashauri iongeze bajeti kwa ajili ya kusaidia shughuli za uhifadhi za rasilimali za pwani na bahari.
·         Serikali kutoa ruzuku kwa wavuvi kama ilivyo kwa wakulima na wafugaji ili kuwa na uvuvi wenye tija. 

Naomba kuwasilisha.


TAARIFA FUPI YA MAENDELEO YA UTAFITI   WA MIFUGO  KWA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI MH.DKT.TITUS MLENGEYA  KAMANI (MB)  TAREHE 15/8/2014

UTANGULIZI
Mheshimiwa Waziri
Kwanza tunapenda kukukaribisha katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI) –Tanga ikiwa ni mara yako ya kwanza kufika hapa toka kuteuliwa kwako kuwa Waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi.Tunapenda kukupongeza pia kwa kuteuliwa na muheshimiwa Raisi wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania  Dkt.Jakaya Mrisho kikwete kuwa waziri wa Maendeleo ya Mifugo na uvuvi . Tunaamini na tunamatumaini kuwa utasimamia vema sekta hii ya mifugo  kwani uanataaluma ya uendelezaji mifugo  hasa katika masuala ya kuzuia na kutibu magonjwa yasumbuayo upatikanaji wa tija katika sekta ya mifugo. 

Mheshimiwa Waziri,
Taasisi ya utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) ilianzishwa chini ya sheria NO.4 YA 2012 na taasisi yetu ni miongoni mwa Taasisi (7)zinazounda TALIRI.Tunapenda kuipongeza serikali yetu kwa kupitisha sheria ya uundwaji wa Taasisi  hii ambayo itasimamia kikamilifu  utafiti wa mifugo Tanzania ili kuongeza uzalishaji na kipato kwa wananchi na uchumi wa Taifa kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Waziri,
Dira ya TALIRI ni kuwa Taasisi ya mifugo ya mfano inayochangia kuboresha hali ya maisha ya wafugaji na wadau wengine (To be model livestock Research Insititute that contributes  towards improved livelihood of famers and other stake holder) na dhimaya TALIRI  ni kutengeneza , kusambaza na kuhamasisisha matumizi ya tekinolojia sahihi kwa wadau wote wa mifugo ili kuboresha uzalishaji endelevu wa mifugo (To develop ,disseminate and promote use of appropriate techinologies to stake holders inorder to improve live stock productivity sustainably). 
Mheshimiwa Waziri ,
Jukumu kubwa la Taasisi hii ni kufanya utafiti wa uendelezaji Mifugo hasa katika kanda ya Mashariki yenye mikoa ya Tanga,Dar-es-salaam,Pwani na Morogoro.utafiti umeelezwa kwenye kutathimini aina za mifugo na vyakula ,malisho, na huduma kwa mifugo ambazo zinaleta uzalishaji bora na wenye tija katika kanda hii. Mkazo mkubwa unawekwa katika kuzalisha ng’ombe chotara kwa ajili ya maziwa ,kuku,mbuzi,na ng’ombe wa asili wanaotunzwa kwenye nyanda za majani na mbuga.pia taasisi imeteuliwa kuwa mojawapo ya Taasisi mahiri katika utafiti wa uzalishaji maziwa (Diary centre of exelllence) chini ya mradi wa EAAPP (Eastern Africa A gricultural productivity projeck).
Mheshimiwa Waziri
Historia fupi ya taasisi utafiti wa mifugo-Tanga
Kihistoria eneo la Taasisi lilikua linamilikiwa na wakazi /wenyeji mpaka kipindi cha vita kuu ya pili ya dunia (1939) wanajeshi wa anga walipofanya kambi yao.Baada ya vita (1946),eneo likawa ni la shamba la ng’ombe wa maziwa.mwaka 1950,shamba likabadilishwaq na kuwa kituo cha uchunguzi wa mifugo likiwa na lengo la kuzaliha nyama walioendelezwa na kuwagawanya  kwa wafugaji. Mpango wa uzalishaji ulianzishwa ,uliousisha chotara  wa ng’ombe aina ya Boran na Friesian,Guarnsey na jersey.mpango huu ulikatishwa mwaka 1965 nakazi nyingi za utafiti ziliendelezwa kwenye kutatua matatizo ya matunzo ya wanyama .mnamo mwaka 1969 kituo kilitambulika kama Taasisi ya utafiti na mafunzo.
Mpango wa uboreshaji ng’ombe ulianzishwa ambapo ng’ombe aina ya Boran wenye damu 100% na wale wenye damu pungufu ya 25%ya ng’ombe wa kisasa walipandishwa na ng’ombe aina ya sahiwal. Lengo hasa lilikua ni kuzalisha na kusambaza majike ya sahiwal yenye damu kati ya 82.5-100%katika kipindi hiki kulianzishwa pia ufugwaji wa nguruwe uliohusisha majike 17 aina ya large White na dume 1 aina ya land race.
Kuanzia mwaka 1973 jina la kituo likabadilishwa na kuwa kituo cha utafiti wa Mifugo na kupewa jukumu la kufanya kazi za utafiti juu ya uzazi, lishe,na matunzo ya ng’ombe wa maziwa katika ukanda wa mashariki.jukumu hili liliendelea pamoja na kutokea kwa mabadiliko katika mfumo wa utawala mwaka 1081-1989 ambapo kituo kiliwekwa chini ya shirika la utafiti wa Mifugo Tanzania(Tanzania Livestock Research Organization-TALIRO).Mwaka 1989 kituo kilirudishwa chini ya wizara ya kilimo na maendeleo ya mifugo . kwa sasa kituo kimekua mojawapo ya Taasisi za utafiti kwenye Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa mifugo (TALIRI) chini yaWizara ya Maendeleo ya mifugo na Uvuvi.

Mheshimiwa Waziri,
Rasilimali na muundo wa taasisi ni kama ifuatavyo
1.      Rasilimali watu
Mheshimiwa  Waziri taasisi inawafanyakazi 40 ambapo 11 kati yao ni watafiti na 11 watafiti wasaidizi wa wafanyakazi  wa kada nyingine 18.vilevile taasisi inawafanyakazi wa muda 29 wakati wote kwa shughuli za shamba.

2.      Rasilimali Ardhi
Mheshimiwa Waziri,shamba kuu la Taasisi lilikua na ukubwa wa hektari 800 mwaka 1973,lakini eneo hilo limezidi  kupungua kufikia hektari 386 kufuatia kukua kwa jiji la Tanga.Taasisi ina shamba linguine lenye ukubwa wa hekta 753 lililopo eneo la Buhuri wa kilometa sita kutoka kituoni.

3.      Muundo mbinu ya Taasisi
Mheshimiwa Waziri,Taasisi inamajengo ya ofisi 2 jengo la maabara moja na jingo la kantini ,pia inamajengo mawili (2) ya karakana na stoo eneo la ofisi ,majengo haya ni ya muda mrefu ambayo yanahitaji ukarabati .kwa eneo la makazi ,kuna nyumba za watumishi  zipatazo 31 ambazo pamoja na majengo mengine yanahitaji ukarabati mkubwa .pia kunajengo kubwa kwa shyghuli za ukamuaji,stoo ya vyakula vya ziada,banda la utunzaji ndama na chumba cha kuhifadhi baridi(cold room)ambavyo vilifanyiwa ukarabati katika mwaka wa fedha 2011/2012. 

4.      Mifugo
Mheshimiwa Waziri,shamba lina ng’ombe 254 na mbuzi 47. Ng.ombe waliopo kituoni ni chotara wanaotokana na ng,ombe wa kisasa aina ya Friesian na jersey na ng’ombe wa kiasili  aina ya Boran za zebu.pia wapo ng’ombe 19 aina ya maasai kwa ajili ya mradi wa kuboresha vinasaba vya ng’ombe wa asili unaofadhiliwa COSTECH.

5.      Muundo wa taasisi.
Mheshiiwa Waziri,Taasisi ina idara ya utafiti 5 na idara saidizi 4 hizi ni:Utafiti wa malisho(pasture and forages Research), Utafiti wa ng’ombe wa maziwa (diary cattle Research) utafiti wa wanyama wadogowadogo wanaocheua (small ruminants Research),utafiti wa wanyama wadogowadogo wanaocheua (Non-ruminants Research) na utafiti wa sayansi jamii(socio-economics)idara saidizi ni idara ya shamba (farm)Afya ya mifugo(Animal health)utawala (administration)na uhasibu(financial,accounts and procurement).idara hizi zitabadilika kufuatia kutokubalika kwa muundo wa Taliri.Taasisi pia inakamati mbalimbali:menejiment,utafiti na taaluma ,ukarabati,zabuni na tathmini(quality assuarance) na wakuu wa idara (hods) pia kuna chama cha wafanyakazi(RAAWU).
MIRADI YA UTAFITI 
 Mheshimiwa waziri, taasisi inatafiti mbalimbali zinazosimamia ikishirikiana pia na Taasisi mbalimbali za kitaifa na kimataifa ILRI,CIAT,IRISH,AID,IFAD,ASARECA,COSTECH,SNV,SUA,EGERTON UNIVERSITY,KARI na EIAR.
mheshimiwa waziri,kwa ushirikiano huu taasisi imeweza kufanya yafuatayo,
·         Kutengeneza b”FEAST Tool”. Inayoweza kubainisha matatizo ya upatikanaji wa malisho katika mwaka
·         Kutengeneza “Techfit tool”inayoweza kuweka vipao mbele nanamna yakutatua matatizo yaliyo inishwa na FEAST Tool.Hii imejaribiwa nchini India na Ethiopia  na sasa uipo kwenye hatua za mwisho za majaribio nchini Tanzania na Kenya kwa kupitia wanafunzi wa ngazi za uzamili na uzamivu.
·          Kupitia mradi wa EAAPP, Taasisi yetu tumeshiriki kwenye kusimamia maboresho ya sera za maziwa na mazao yake kwenye nchi za afrika mashariki na kati (Reginal Dairy policies harmonization) ambapo Tanzania inaratibu taratibu za uingizaji  na usafirishaji  wa vyakula vya ziada  na malisho (import and export procedures for compounded feeds and forages) Kenya inaratibu utoaji wa mitamba na uwekaji kumbukumbu(movement of heifers and diary records) Uganda na Ethiopia inaratibu usindikaji wa maziwa (processing)
·         Mheshimiwa Waziri, kwa kupitia mradi huu pia , Taasisi imeshiriki kwenye mchakato wa upatikanaji wa mbegu za malisho katika soko (pasture and release) kwa ushirikiana  na taasisi ya kuidhinisha utoaji wa mbegu Tanzania (TOSCI) pamoja na wadau wengine.lengo ni kuhakikisha mbegu za malisho zinaidhinishwa kisheria na kuweza kupatikana katiaka masoko  ili kuwafikia wafugaji na wadau wengine.            
Usambazaji wa tekinolojia (Technolojia dissemination)
Mheshimiwa Waziri,Taasisi yetu inashiriki sana katika usambazaji wa tekinolojia zilizotokana na tafiti mbalimbali  zilizofanyika hapa nchini na na nje ya nchi .mbinu mbalimbali zilizotumika kufikisha tekinolojia hizo kwa wadau mbalimbali ni pamoja na :

·         Kutoa mafunzo na ziara za mafunzo
·         Vipeperushi na vijarida
·         Vitini
·         Mikutano ya kimataifa ,kitaifa na maonyesho ya kilimo ya kila mwaka
·         Kuunda vikundi vya wafugaji na majukumu bunifu
·         Kutumia mashamba darasa

   Mheshi miwa Waziri,
 Miradi inayoendeshwa ndani ya Taasisi (on station projecks)ni hii ifuatayo
        I.            Breeding for optimum Diary in the humid coastal belt of Tanzania (Uzalishaji wa ng’ombe chotara anayeweza kutoa maziwa ya kutosha  kutokana na mazingira ya ukanda  wa mashariki wa Tanzania)
Mradi huu unalenga kuwa na nucleus herd kwa ng,ombe chotara ambao walifanyiwa utafiti  nakuonekana kwamba wanaweza kufanya vizuri  katika ukanda wa pwani (coastal humid belt). Kwa mwaka huu madume 40 na majike 10 waliuzwa kwa wafugaji katika wilaya ya Tanga ,Muheza na Mkinga.

      II.            Improvement of local Goats and milk production by cross breeding with dual purpose bucks in small holder farming systems of North-Eastern Tanzania.
Mradi huu unawanufaisha wafugaji ambao hawana uwezo wa kufuga ng’ombe wa kisasa wa maziwa lakini wanapenda kupata maziwa .lengo ni kuongeza utoaji wa maziwa kwa mbuzi wa kwa mbuzi wa asili kupitia chotara ambao hupatikana kwa kupandisha jike  la asili kwa dume la mbuzi wa kisasa . kwa mwaka huu jumla ya mbuzi 14(madume9,majike 5,)yaliuzwa kwa wafugaji katika mkoa ya Tanga (10) na pwani(4)

    III.            Identification and improving existing indigenous lines of chickern in traditional production systems in north-eastern Tanzania .
Mradi huu unapata pesa toka serikalini .utafiti wa awali kuhusu kuku wa asili ulionyesha kuwa miongoni mwa kuku wa asili wenye umbo dogo wanataga mayai mengi wakati wale wenye umbo kubwa wanataga mayai kidogo .mradi unalenga kupata kuku  wa asili mwenye umbi kubwa na anayetaga mayai mengi  kwa kuwachanganya wenye umbo kubwa na dogo (blending)aina zilizopo kwenye taasisi kwa sasa ni kishingo,kinyavu,bukini,kuchi,multicolor feathered,black australop(ex-malawi)na bovine brown.

    IV.            Pasture and forage germplasm evaluation for improvement of ruminant feeding in the eastern zone of Tanzania.
Mradi huu hupata fedha serikalini lakini kwa kiasi Fulani EAAPP na MILKIT  kwa lengo la kuwa na benki ya aina mbalimbali ya malisho ikiwemo miti malisho ,nyasi, mikunde,na mikunde miti,hii husaidia kuwapatia mbegu wafugaji pale ambapo huitaji kuendeleza mashamba ya malisho au nyanda za malisho.

      V.            Establishment of cenchrus for hay and seed production to meet demands of animal feeds for sustainable livestock productivity.
Malisho aina ya cenchrus ciliaris ndiyo yanayofanya vizuri kwenye ukanda  wa pwani hivyo mradii huu unalenga kuzalisha aina hiyo kwa wingi ili wafugaji waweze kupata mbegu kwa kuendeleza mashamba yao na nyanda za malisho. Taasisi imeweza kuanzisha ekari 160 kwa shamba la buhari na ekari 30 kwa shamba kuu ,aidha tani 40 zilisambazwa kwa wafugaji na mikate 2500ilivunwa.

Mheshimiwa Waziri,
Miradi inayoendeshwqa mashambani (on farm project) nii hii ifuatayo
        i.            The use of FI cross bred bulls on zebu cows for production of cross bred with quarter exotic blood for production at farmers level.
  Mradi huu unapata fedha kutoka serikalini lengo likiwa ni kuwa na midume chotara ambayo yanastahimili ukanda wa pwani kwa ajili ya  kuboresha ng’ombe wa asili na kuwezesha kupata maziwa mengi kwa wafugaji ambao hawawezi kupata ng’ombe  wa kisasa . kwa mwaka jana madume chotara 36 yalipelekwa kwa wafugaji wa wilaya ya tanga muheza na mkinga .

Mheshimiwa Waziri,
Mirdi inayofadhiliwa na taasisi /mashirika mbalimbali ni kama ifuatavyo

MIRADI INAYOFADHILIWA  NA EAAPP
Taasisi inashiriki katika miradi mitatu kati ya miradi mitano chini ya uhifadhi wa EAAPP
a)      Improving value addition and marketing of milk for small holders (VAMMS) in EAAPP and ASARECA countries.
Mradi huu unafanyika katika nchi ta Tanzania ,Kenya na Ethiopia. Lengo kuu ni kusaidia wafugaji wadogowadogo na ngombe wa maziwa kuongeza thamani Ya maziwa.kwa Tanzania mradi unafanyika kanda ya mashariki  katika wilaya ya Bagamoyo na muheza .Watafiti kwa Tanzania ni Taliri-Tanga na Sua. 
b)      Enhancing adoption of appropriate policies and safety standards of feeds and milk for improved livelihood in the ECA Countries.
Mradi huu unafanyika katika nchi ya Tanzania ,Kenya na Ethiopia . lengo kuu ni kubaini sera na “standards”za vyakula na mazao yatokanayo na maziwa ili kuleta ushindikani katika soko la ndani nan je ya nchi za Afrika Mashariki .TALIRI-Tanga na SUA ndio wasimamizi wakuu.

c)      Improving indigenous cattle for diary production through targeted selection and cross breeding in the EAC contries
Mradi  huu unafanyika katika nchi ya Kenya na Tanzania .lengo ni kutumia ng’ombe wetu wa asili kupata chotara watakaotoa maziwa mengi na wanaoweza kuhimili mazingira ya kitropiki.mpaka sasa madume 32ya ng’ombe yamesambazwa kwenye vijiji 7 vya kanda ya mashariki na nyanda za juu za kusini.

d)      MIRADI INAYOHIFADHIWA  NA NFAST-COASTECH
1.      Enhancing availability and productivity of dairy cattle through genetic stabilizationin in Tanzania .
Mradi huu unalenga kuongeza maziwa kwa chotara wa ng’ombe wretu wa asili(majike)na wale wakigeni. Mradi unatekelezwa nyanda za juu kusini(majike aina ya iringa red) na wale wa kigeni. Mradi unatekelezwa nyanda za juu kusini (majike aina ya iringa red)na kanda ya mashariki (majike aina ya maasai) .TALIRI-uyole ndio wasimamizi wakuu.  

2.Developing and promoting a stratified model ta transform traditional beef cattle production into commercial oriented beef cattle industry in Tanzania
Mradi huu unalenga kumwezesha mfugaji wan g,ombe wa nyama kupata soko la ndani nan je kwa kuwaweka wafugaji katika makundi ya wazalishaji,wakuzaji na wanaofanya feed lot.mradi unafanyika kanda ya mashariki ,kanda ya kati na kanda ya ziwa lengo likiwa pia kutumia vizuri machinjio zetu za kisasa zilizokwu=isha jengwa na ambazo zinzkaribia kumalizika usoni . TALIRI-Tanga ,TALIRI-M PWAPWA  na TALIRI –mabuki ndio wasimamizi wakuu.

3.ILRI-LED COLLABORATIVE PROJECTS
1.Milk project
Enhancing dairy-based live hoods in Indian and  Tanzania through feed innovation and valie chain development approaches
Mradi huu unatumia majukwaa bunifu(innovation platform) na mnyororo wa thamani (value chain) ili kuweza kupata chakula cha ziada na malisho na malisho kwa kipindi cha mwaka mzima . mradi unafadhiliwa na  I FAD na unatekelezwa India  na Tanzania . kwa Tanzania mradi unafanyika  katika mkoa wa Tanga (lushoto na handeni) na mkoa wa morogoro (kilosa na mvomero).wasimamizi wa kuu ni ILRI, CIAT,TALIRI-Tanga na Sua .

2.more milk in Tanzania 
A dapting dairy market hubs for pro-poor small holder value chains in Tanzania.
Mradi huu unatumia njia ya “market hubs” ili kuboresha uzalishaji wa maziwa kwa wingi na uwezekano  wa kupata pembe jeo na masoko kwa urahisi .madi unatekelezwa moa wa Tanga na morogoro kwenye vijiji 30(Tanga 14 na morogoro 16) wahusika wakuu ni ILRI,CIAT,Heifer,TALIRI-Tanga na SUA.

IV. MIRADI INAYOFADHILIWA NA ASARECA
1.Intergrated productivity enhancing technology packages in small holder dairy helds in the ECA  sub –region
mradi unatekelezwa katika nchi za AS ARECA na kwa Tanzania TALIRI –Tanga na SUA ndio wasimamizi wakuu wa mradi ambapo morogoro (wilaya ya mvomero) na T anga (wilaya ya Tanga na Muheza) ndipo mradi unapofanyika . lengo ni kumsaidia mkulima ambaye pia ni mfugaji kutumia fursa zilizopo kuongeza tija  katika uzalishaji wa mazao na maziwa. 

V.MIRADI INAYOFADHILIWA NA USAID
1.Sustainable intensification in the sub-humid maize based cropping systems of Babati .
Mradi huu upo chini ya Africa rising(Africa –Research in sustainable intensification for next Generation) na unalenga kutumia malisho yaliyo endelezwa kwenye mfumo wa kilimo cha mahindi ili kuongeza upatikanaji wa lishe endelevu kwa mifugo na kuongeza matumizi bora ya ardhi . mradi unatekelezwa katika mkoa ya Manyara (wilaya ya Babati).

Mheshimiwa Waziri ,
Changamoto za kiutumishi na nyinginezo ni kama zifuatazo
§  Utumishi
Mheshimiwa Waziri, tunapenda kuipongeza serikali kwa kutambua umuhimu wa utafiti wa mara kwa mara kuajiri watumishi wa ngzi mbalimbali kulingana na uwezo wake .Hata hivyo Muheshimiwa Waziri ,Taasisi bado imekua na upungufu wa wafanyakazi katika ngazi zote yaani watafiti, watafitiwasaidizi,sapporting staff hasa walinzi, wachungaji na wakauaji ambao ni vibarua .baada ya serikali kuondoa ajira  za watumishi wa kada mbalimbali Taasisi imelazimika kuajiri vibarua wapatao 29 ili kufanikisha kazi za kuchunga ,kukamua na uklinzi.Hali hiyo imefanya Taasisi kutumia fedha nyingi  kuwalipa kila mwezi. Tunaomba serikali kupitia bodi Ya  TALIRI  NA wizara ya maendeleo ya mifugo na uvuvi  iwaajiri watumishi wa kada hizi ambazo ni muhimu sana katika shughuli za kila siku za Taasisi.

Idara ya wafanyakazi TALIRI Tanga 

Aina

Elimu

Aina ya
Ya kudumu

Ajira
Ya muda mfupi
Idadi waliopo kazini
Idadi waliopo masomoni
Gap

Researchers
Phd
Msc
Bsc
1
6
10
0
0
0
1
6
8
0
1
2
7
9
18

Field officers
Diploma
certificate
4
1
0
0
4
1
0
0
20
10

others
Field
Auxiliary
Watchman
supporting

7
3
8

16
9
4

23
12
12

0
0
0

15
6
8
total


40

29

67

3

92


§  Usafiri
Mheshimiwa waziri, tunaishukuru pia serikali kwa kuendelea kutatua matatizo ya uhaba wa vyombo vya usafiri kwenye idara na taasisi zake ili kufanikisha shughuli mbalimbali zikiwemi za utafiti. Pamoja na jitihada hizo hapa kwetu bado tuna uhaba wa wa vyombo hivyo , tunalogari moja ambalo ndilo zima mengine yote ni mabovu na ugharimi pesa nyingi kwa matengenezo ya mara kwa mara na pia kukwamisha shughuli za utafiti.

§  Fedha za kufanyia utafiti
  Mheshimiwa waziri ,serikali imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya shughuli za kawaida za maendeleo ya  na zautafiti kila mara ingawa wakati mwingine fedha zinazotolewa zimekua hazitoshelezi hivyo kurudisha nyuma shughuli za utafiti na maendeleo ili kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu ya taasisi.
§  Uchakavu wa majengo
Uchakavu wa majengo na nyumba za wafanyakazi ikiwa ni pamoja na mabanda  ya kufanyia utafiti  limeendelea kuwa tatizo kwa ufanisi na wafanyakazi kwenye taasisi
§  Maabara
Uhaba wa maabara ya utafiti wa lishe ya mifugo ,kuongeza thamani ya maziwa na uzalishaji mifugo.

Mheshimiwa waziri,
Mtazamo wa baadae wa Taasisi (future plans )ni kama ifuatavyo
§  Kuongeza idadi ya mifugo (ng’ombe wa mazaiwa na nyama )ndani ya taasisi na kwa wafugaji kwa kutumia MOET(Multiple ovaluation embryo transfer)kwa kuwa na maabara (in vitro laboratory) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali (INDICUS,SCF,na COSTECH,KARI).
§  kufanya utafiti za kuongeza ubora wa maziwa na maziwa yatokanayo maziwa (milk handling,processing and value addition) kwa kuwa na maabara (milk processing laboratory)innovation platforms na hub business model.
§  Kuendelea kushirikiana na wadau m,balimbali zikiwemo taasisi za kitaifa na kimataifa kufanya tafiti mbalimbali kwa maendeleo ya mifugo.

 Mheshimiwa waziri,
Hitimisho
Utafiti ni sehemu muhimu sana katika kuzidi kuinua sekta hii ya mifugo.  Kupitia kwako muheshimiwa Waziri tunaomba serikali ishughulikie changamoto tulizo nazo ili kuongeza ufanisi na kufikia malengo ya taasisi.
Mheshimiwa Waziri,Tunapenda kukukaribisha tena  kwenye Taasisi yetu mara upatapo nafasi.

Nawasilisha


RISALA YA WANANCHI WA KIJIJI CHA MSOMERA HANDENI KWA MHESHIMIWA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI DRT. TITUS MLENGEYA KAMANI (MB) TAREHE 18/08/2014.
Mheshimiwa waziri wa mifugo na uvuvi kwanza sisi wananchi wa kijiji cha Msomera, tunatoa shukrani zetu kwa Mwenyezi Mungu aliyekuongoza wewe pamoja na wote ulioambatana nao katika msafara wako kutembelea kijiji chetu.
Mheshimiwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi kijiji cha Msomera kilianishwa rasmi mwaka 1922 baada ya viongozi wa tarafa ya Sindeni ambayo ndipo kilipo na tarafa ya Mswaki ambayo sasa ipo Wilaya ya Kilindi walipofanya kikao cha pamoja na kuona haja ya kuanzishwa kwa vijiji viwili vya wafugaji ambavyo ni Msomera tarafa ya Sindeni na Lengusero tarafa ya Mswaki ambacho kwa sasa kipo Wilaya ya Kilindi baada ya mgawanyo wa Wilaya hizi.  Kijiji kimefanya jitihada kubwa ya kupata haki yake na cheti chake na ulipofika tarehe 2 januari mwaka huu, kijiji kilikabidhiwa cheti chake na Mkuu wa Wilaya ya Handeni Muhingo Rweyemamu. Tunashukuru kwa wote walioweka jitihada zao katika kufanikisha hili.
Kijiji hiki nkina jumla ya watu 4900, wanaume  2150 na wanawake 2750. Kuna jumla ya mifugo 59,362 ikiwa ni pamoja na ng’ombe 23,500, mbuzi 16,000, kondoo 19,500na punda 362. Kijiji kina josho ambalo kwa sasa huduma imesimama kutokana na uhaba wa maji. Aidha hali ya maji itakapotengemaa huduma itaendelea kama kawaida.
Hapo awali kulikuwa na mabwawa mawili ambayo ni Msomera na Mlunduzi lakini kwa bahati mbaya mabwawa yote yamebomolewa kwa mvua na hivyo kufanya maisha ya wakazi wa kijiji hiki kuwa ya adha kubwa kwa binadamu na mifugo. Na kwaajili ya adha hiyo ndiyo sababu maifugo mingi haipo kijijini hapa na imetawanyika sehemu mbalimbali ndani nan je ya Wilaya ya Handeni.
Mnamo tarehe 23.3.2014 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ngugu Jakaya Mrisho Kikwete alitembelea kijiji chetu na kutoa ahadi ya kutujengea mabwawa mawili, visima virefu vitatu, kuboresha mifugo yetu kwa kuhalimisha majike zaidi ya 200  kutupa zawadi ya ng’ombe toka ranchi yake na madume 2, kuwapeleka wafugaji watano wa kijiji hiki kwenye mafunzo  Afrika Kusini, uanzishwaji wa Ranchio ndogondogo za wananchi kupitia Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na mwisho kina mama wawili kwenda kumkabidhi Mama Salma Kikwete vazi la kimasai. Kwa ajili hiyo  Mheshimiwa Waziri tunakuomba kwa heshima kubwa umkumbushe Mhe. Rais hadi alizotoa ili ikiwezekana zitekelezwe ili kuwaondolea wananchi wa kijiji hiki matatizo yaliyopo.
Mheshimiwa waziri, kijiji hiki kimepimwa kisheria na kina ukubwa wa hekta za mraba 50,971. Kwa sasa kijiji kipo kwenye mchakato wa kutengeneza mpango bora wa ardhi ambao utabainisha mipaka ya kijiji hiki na vijiji vya jirani kwa kutengeneza barabara za kuonyesha mipaka. Na mipaka ya ndani itakayotenganisha maeneo ya makazi, malisho, kilimo, vyanzo vya maji na hifadhi kwa lengo la kuboresha utunzaji wa mazingira na kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji.
Vilevile kijiji kitakosa fadhila endapo hakitamshukuru Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Handeni ndugu Muhingo Rweyemamu ambaye juhudi zake kubwa zimeweza kufanikisha mambo mbalimbali ya maendeleo ya kijiji hiki.
Mwisho Mhe. Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi tunakutakia safari njema wewe na msafara wako na Mwenyezi Mungu akubariki sana.
Naomba kuwasilisha
Imeandaliwa na Wananchi wa kijiji cha Msomera.
Ahsante.
.

KUTOKA : KITUO CHA UDHIBITI UBORA WA MAZAO YA UVUVI NA MASOKO KANDA YA KASKAZINI –TANGA
KWENDA: WAZIRI WA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
UTANGULIZI
Kituo cha uthibiti ubora wa mazao ya Uvuvi na masoko kanda ya kaskazini kilichopo mkoani Tanga kilianzishwa mnamo mwaka 2000 kikiwa na mtumishi mmoja .baada ya mda wa mwaka mmoja akaongezwa mtumishi wa pili na kufikia hadi hivi sasa kitengo kina idadi ya watumishi wane.
Kanda ya kaskazini ina jumla ya mikoa mine ambayo ni Tanga ,Kilimanjaro ,Arusha na Manyara,kitengo kinamajukumu ya kulinda ,kusimamia na kidhibiti ubora wa mazao ya uvuvi yanayosafirishwa ndani na nnje ya nchi pamoja na kusimamia ukusanyaji wa maduhuli  kwa kushirikiana na kituo cha Doria Uvuvi katika kanda hii ya kaskazini , kituo kina gari moja aina ya Nissan quaqui na pikipiki moja DT 250

KAZI ZA KITUO
Lengo kuu la kituo ni kudhibiti ubora na usalama wa mazao ya Uvuvi kwa watumiaji/walaji ndani na nnje ya nchi na kusimamia masoko ya mazaop ya Uvuvi kwa kutekeleza sera za mwaka 1997,sheria ya mwaka 2003 na kanuni ya mwaka 2009 za Uvuvi.ili kufanikisha lengo hili kituo kinafanya malengo mahususi kwa

          Kufanya kaguzi katika viwanda vya uchakataji /usindikaji wa mazao ya uvuvimialo na masoko ya Uvuvi.
          Kusimamia na kufanya kaguzi katika mipaka iliyopo kwenye kanda ya kaskazini
          Kutoa vibali vya usafirishaji mazao ya Uvuvi ndani na nnje ya nchi
          Kutoa elimu kwa wavuvi ,wauzaji wa mazao ya Uvuvi na wasindikaji /wachakataji wa mazao ya Uvuvi viwandani
          Kusimamia makusanyo ya maduhuli yatokanayo na usafirishaji wa mazao ya Uvuvi ndani na nnje ya nchi’

VYANZO VYA MAPATO
Kituo kinakusanya maduhuli kutokana na ukusanyaji wa ushuru wa mazao ya Uvuvi yanayosafirishwa nje ya nchi yakitokea hapa jijini Tanga ,faini ya makosa yanayofanywa na wavuvi (compoundment) kama vile  kuvua kwa kutumia vyombo visivyo sajilia ,kusafirisha mazao ya Uvuvi bila kibali,kuvua bila kuwa na leseni halali ya Uvuvi.

MAFANIKIO
Kituo kimefanikiwa kusimamia  ukusanyaji wa maduhuli   jumla ya shilingi milioni 28,113’318.15 ambazo ni asilimia 28%
Kituo kimeweza kuwabadili wavuvi hasa wa pweza kuvua pweza wenye uzito wa gram 500 na kuendelea ‘pia kituo kimeweza kuwapa elimu ya kuhifadhi mazao ya uvuvikwa ubora na usalama kwa kutumia cool box
Kituo kimesaidia kupatikana  kwa soko la kudumu kwa wavuvi wadogowadogo  kwa kuhamasisha ongozi wa kiwanda kwa kusindika mazao ya Uvuvi kununua mazao ya Uvuvi kwa wavuvi hao.


Nawasilisha.


KAMPUNI YA RACHI ZA TAIFA LTD
RANCHI YA MZERI HILL
TAARIFA FUPI YA RANCHI YA MZERI HILI KWA WAZIRI WA MAENDELEO
MIFUGO NA UVUVI DKT .TITUS KAM ANI   (  MB)
TAREHE 18 AUGUST 2014

MH. WAZIRI
Tunayo furaha ya pekee  kukukaribisha kwenye Ranchi hii ya mzeri
Hii haswa kwa kuwa ziara hii ni yakwanza kutembelea kutoka
Mheshimia .Rais  Jakaya Mrisho kikwete akuteua kwenye wadhifa
Wako huu.A idha kwa niaba ya wafanyakazi wote wa mzeri hii ni Ranchi
Naomba kuchukua nafasi hii kutoa taarifa fupi ya Ranchi.

1.1 HISTORIA YA RANCHI YA MZERIHILL                                                                         
Ranchi ya mzeri hill ilianzishwa mwaka 1968 chini ya awamu ya kwanza ya program   Ya Taifa ya kuendeleza  Mifugo (NATIONAL   LIVE STOCK   DEVELOPMENT PROGRAMME -  Phase 1  1968 -1971)  Mradi huo ulikua unahifadhiwa na Benki ya  Dunia  kwa mkopo ambapo serikali serikali ya Tanzania ilitoa asilimia 30 ya gharama zote. Aidha , awamu ya pili ya mpango  (1978- 1982) kulikua na uwekezaji na  uimarishaji wa Ranchi .   

           1.2   Ranchi hii iko km.35  kaskazini mwa mji wa Handeni km. 47  kusini mwa mji wa 
                    Mombo na km 45  kusini magharibi wa mji wa korogwe , Ranchi ipo mkoa wa Tanga
            Wilaya ya Handeni  na Korogwe. Ina msambao wa mchanganyiko wa nyasi ,kundekunde
Udongo mweusi na wakichanga sehemu ndogo na inapata mvua kiasi cha mm 760 -800 kwa mwaka.kutokana na kuwa na udongo na mvua  kiasi cha kutosha shughuli za ufugaji zimefanyika kwa ufanisi mkubwa. Joto la hapa ni 18c-32c. na mvua ni za misimu miwili ya kiasi ya milimita 760-800.   
1.3       Mandhari ya Ranchi hii ni mazuri kwa ufugaji  na nyasi zake zenye virutubisho vya     
            Kutosha kwa uboreshaji wa mifugo.Ranchi inaukubwa wa hekta 41,246.11, lakini kufuatia
            Uamuzi wa serikali wa kugawa RANCHI ndogondogo ambazo zimemilikishwa kwa
           Wawekezaji wa kitanzania ,sasa Ranchi mama (Core Ranch) imebaki na eneo la 
           Ha 21,236 ambayo inauwezo wa kuweka ng’ombe 7,000. Kwa sasa Ranch ina ng’ombe
           2367,kondoo 206 mbuzi 62 na farasi 2. 
2      LENGO LA KUANZISHWA  
        Ranchi ya mzeri hill imepewa majukumu makubwa kama ifuatavyo:-
                     I.            Kuzalisha na kusambaza ng’ombe bora kwa wafugaji.
                   II.            Kuzalisha na kunenepesha ng’ombe wa nyama kwa soko la ndani kwa sasa.
                 III.            Kuwaelekeza wafugaji kuhusu muelekeo wa ufugaji bora bna matumizi ya ng’ombe katika kilimo cha kutumia maksai ambayo na teknolojia rahisi ns sahihi na uyinzaji wa mazingira .

3    IDADI YA WAFANYAKAZI  
      Ranch inajumla ya wafanyakazi 40 (wakudumu 8,mikataba 22.idadi hii huongezeka na kupungua kutokana na idadi ya mifugo iliyopo. 

4. MIFUGO
4.1.Ranch ina ng’ombe wanakua wa nyama aina ya boran wenye asili ya kaskazini mwa Kenya,
(Ambao nao walitoka Ethiopia na Sudan) ng’ombe wa boran wanaumbile kubwa wanakua haraka na wanamudu mazingira yetu vizuri  kuliko aina nyingine za kigeni.Aidha nyama yake inaladha nzuri kwa kula na kuweka mafuta ndani ya nyama badala ya juu ya nyama.  
Kutokana na borani ,Ranchi pia huzalisha mtambo wa maziwa kwa njia ya uhimilishaji  kwa kupandisha na mbegu za Friesians chotara wanao zalishwa na kuuzwa kwa wafugaji wadogo wadogo kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa.  

4.2 kondoo
      Ranchi inakondoo wa nyama aina ya Black headed Persian( BHP) wenye asili ya afrika kusini
      Uzito wake hufika kilo 150. Pia chotara kati ya BHD na Doppers hutoa machotara yenye uzito 
Kilo 80 mpaka 120. Aina hii ya kondoo inanyaama nzuri ambayo haitoi shombo wakati wa kupika na kwa wakaji pia. 

4.3 Mbuzi  
      Ranch pia inafuga mbuzi kwa ajili ya nyama ambao  majike ya kienyeji wamezalishwa na aina
      Anglonubian na kupata mbuzi chotara wakubwa na wenye nyama nzuri ambao hutoa kilo 
60 mpaka 80.

4.4 Farasi
 
     Ranch hufuga farasi kwa ajili ya doria  na hivyo kurahisisha shughuli za ufuatiliaji za ufuatiliaji wakiwa malishoni. 

5. UZALISHAJI 
5.1 katika msimu huu wa mwaka  2013/2014 Ranchi ya mzeri imezalisha ndama 660 idadi ambayo ni sawa na asilimia 73 ya lengo la uzalishaji. 
Aidha uzalishaji kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia 2008/2009 hadi 2013/2014
Unaonyeshwa kwenye jedwali lililo ambatanishwa.


Uzalishaji wa kipindi cha miaka 5 kuanzia 2008/2009 -2013/2014 

2008
2009
2009
2010
2010
2011
2011
2012
2012
2013
2013
2014













Wastani majike
1200

1302

1300

1378

950

900

Idadi ya ndama
960
80%
1041
80%
1105
85%
797
70%
686
72%
660
73%
Vifo vya ndama
20
2%
20
1.9%
20
1.8%
13
1%
20
1.7%
12
0.1%
Vifo wakubwa
173
1.7%
57
1.3%
39
1.1%
106
3%
106
4%
48
2%
Jumla vifo
193
1.7%
77
1.4%
59
1.3%
116
3.5%
126
3%
60
1.4


6. MIUNDO MBINU
 Hali ya miundo mbinu ni nzuri kiasi na baadhi inafanya kazi na nyingine mbovu.
   Miundo mbinu inayo fanya kazi ni kama ifuatayo:-
·         Mitambo ya kunyunyizia dawa  -2 (spray race)
·         Matanki ya maji makubwa -5
·         Matanki ya maji madogo -6
·         Kisima kirefu lita 10000 kwa saa 1
·         Vibanio -2
·         Feedlot-1
·         Mabwawa-5
·         Malambo-8
·         Mabanda ya mbuzi /kondoo 2
·         Band la hei 1
·         Gereji/kapenta1
·         Banda la magari 1banda la ngozi 1
·         Duka la kuuza /kuchinja nyama 1
·         Gari Toyota Hilux su 36877  1
·         Lori fuso su 37223 1
·         Pikipiki tairi 3 su 35951   1
·         Trecta new Holland su 35939 1
·         Treila la Hei su 37128  1
·         Bailar ya kufunga hei 1 Mbovu
·         Mower ya kukata majani 1
·         Jembe la plau 1
·         Mizani ya mifugo 2
·         Kompyuta 3
·         Over head projecta 1
·         Laminaton/Binding/cutter 3
·         Photocopy/fax 1
·         Printer 2
·         Generator KVA 15  1
·         GeneratorKVA 7.5 1
·         Mashine za maji/ pump 2/2
·         Sola  nyumba 8

7.0       MAFANIKIO
           Baadhi ya mafanikio ni pamoja na ;
                        I.            Ranchi inajiendesha yenyewe kwa sasa kwa kutumia rasilimali zilizopo japo hazitoshi.
                      II.            Ranchi imekua ikiuza ng’ombe kwa ajili ya kuchinja kwa wafanya biashara wa nyama  na kwa sasa Ranchi inachinja kiasi kikubwa kwa ajili ya duka lake lililopo korogwe
                    III.            Ranchi inanunua ng’ombe wa kunenepesha kutoka kwa wafugaji wadogowadogo wa asili  (zebu) .Mpango huu unawapatia wafugaji wadogowadogo soko la uhakika kwa ajili ya mifugo yao (mwaka 2010 hadi 1792 walinunuliwa)
                    IV.            Ranchi inafunga wastani wa robota15,000 za hei kwa mwakla kutoka shamba la majani lenye thamani ya tsh milioni 60 na hivyo kuongezea shamba mapato.
                      V.            Ranchi imefungua duka la kisasa mjini korogwe ambalo huuza ng’ombe wawili kwa siku na wateja ni korogwe ,Lushoto, na Mombo.     
8.0    CHANGAMOTO 
                                I.            Kama ilivyo kwa Ranchi nyingine za NARCO , zipo changamoto mbalimbali tunazokabiliana nazo katika uendeshaji. miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na; 

         8.1      kukosa mtaji kumesababisha yafuatayo; 
                              II.            Kasi ndogo ya ununuzi wa mifugo ya kunenepesha kutoka kwa wafugaji wadogowadogo
                            III.            Mifugo michache kulinganisha na ukubwa wa eneo hvyo kuongeza gharama za uzalishaji.
                            IV.            Kasi ya kupunguza vichaka imekua ndogo hivyo kupunguza uzalishaji wa malisho  na kuongeza kazi ya upotevu wa mifugo mara kwa mara.
                              V.            Ranchi imekua ikiuza mashamba kila mwaka kwa muda mrefu ili kugharamia shughuli za uzalishaji nah ii imechangia kwa majike wazazi .


      8.2      Matatizo mengine. 
                                I.            Uharibifu wa mazingira unatokana na uchomaji miti ovyo ukataji wa miti kwa ajili ya mbao na uchomaji mkaa.
                              II.            Kupanda kwa gharama za uendeshaji hasa bei za madawa , vipuli na mafuta
                            III.            Milipuko ya magonjwa mara kwa mara CBPP,FMD. 



9     MIPANGO YA BAADAE :

                                                        I.            Kuongeza idadi ya mifugo kwa kuongeza uzalishaji na ununuzi wa ng’ombe wa kunenepesha kutoka kwa wafugaji wa ng’ombe wa asili  kutokana na fedha za mikopo  kutoka kwenye taasisi za fedha 
                                                      II.            Kuendelea kuzalisha mitambo chotara F1 wa maziwa kwa uhamilishaji kulingana na mahitaji
                                                    III.            Kuendeleza nyanda za malisho  kwaz kupandsa majani na mikundekunde yenye ubora ili kupambana ya ukame ya dhamira ya kupunguza madhara ya vifo hasa wakati wa kiangazi 
                                                    IV.            Upunguzaji wa vichaka kwa njia mbalimbali ili kuboresha  malisho ya mifugo kwa kuzingatia utaalam utokanao na matokeo ya mradi  uliofadhiliwa na tume ya sayansi9 COSTECH)
                                                      V.            kuendelea kutoa elimu kwa  Ranchi ndogondogo, wafugaji wadogowadogo ili kuwepo ufugaji endelevu na wenye tija na wafanyakazi ili kuwepo  ufugaji endelevu na wenye tija
                                                    VI.            kuongeza maduka mawili ya nyama katika eneo la Tanga mjini,Mombo, ili kupanua wigo wa masoko  

                      10.              VITALU RANCHI NDOGONDOGO.        
Ranchi inajumla ya vitalu     kumi ikiwemo Ranchi mama. Vitalu hivyo
                                       Ha,2127.22 hadi Ha, 4164.64. ifuatayo ni taarifa ya vitalu hivyo kwa kuzi
                                      Ngatia miundo mbinu , mifugo pamoja na ukubwa wake kama ifuatavyo:-

                                               I.            STAGE FARM LTD 645/1-AREA 2231.74 HA
Mifugo 
Ng’ombe 400,mbuzi na kondoo 250 
Miundo mbinu:-  
Mazizi 2,nyumba 2 za tofali,spray race
Wafanyakazi- 7
Maji mto –pangani
Usafiri pikipiki 1 .


                                             II.            KLUB AFRIKO 645/2-AREA 2127.22  HA 
Mifugo:-Ng’ombe 81, kondoo na mbuzi 227
Miundo mbinu:-
Mazizi 2, Mabanda ya mbuzi 2
Nyumba za tofali 2 Maji mto pangani
Usafiri –pick up moja na trekta
wafanyakazi 5

                                           III.            SADO FARM  645/4 –AREA 3733.12 HA
Mifugo :- ng’ombe 90, mbuzi 210 na kondoo 340
Miundo mbinu :-
Nyumba 2 za tofali
Zizi moja
Mabanda ya mbuzi 2
Spray race 1
Wafanyakazi 6

                                          IV.            OLOSIPA RANCH 645/5- AREA 3676.177 HA
Mifugo ng’ombe:- 1300, mbuzi 210 na kondoo 400
Miundo mbinu:-
Nyumba 3 za tofali, nyumba za kawaida 6 za mabati
Feedlot 1
Mabwawa 2  usafiri pickup 1, trecta 2 na pikipiki 2
Wafanyakazi 21
Umeme – solar + generator

                                            V.            MAJOR ONE 645/6 AREA 4164.64 HA
Mifugo:- ng’ombe 150 , kondoo 350 na mbuzi 120
Miundo mbinu :-
Nyumba 3 za tofali  na nyingine 3 zinaendelea kujengwa
Usafiri pick up 1 na pikipiki 2 
Bwawa 1
Wafanyakazi 5 

                                          VI.            SHALOM  FARMING AND PLANTATION 645/7 –AREA 3231. 00 HA
MIFUGO :- ngombe 520,
Miundo mbinu:-
Mabwawa 2
Borehole 1 Lambo 1
Nyumba za bati 2
Mazizi 2
Usafiri – gari 1 pick –up
                                        VII.            GOOD CHANCE 645/8-AREA 3012.12 HA
Mifugo:- ng’ombe 60
Kondoo na mbuzi 25
Miundo mbinu :-
Nyumba 2 za tofali
Wafanyakazi 7
Usafiri pick up 1, trekta 1 na pikipiki  2
Maji mto pangani


                                      VIII.            LEIMBA RANCHI 645/9- AREA 3144.14 HA
Mifugo :- Ng’ombe 800
Miundo mbinu:-
                                           IX.            Nyumba 2 za bati
Maji mto pangani 
Usafiri pikipiki 2

                                             X.            KWEISEWA VILLAGE 654/10  AREA  3065.78 HA
Eneo hili wamepewa wanakijiji waendelee kwa shughuli za kilimo na ufugaji.


               10.1           CHANGAMOTO ZA VITALU 
Changamoto za vitalu zimo katika maeneo haya makuu yafuatayo:-

a.      Kasi ya uendelezaji ni ndogo ambao wameendeleza vizuri ni vitalu vine. 
b.      Ukosefu wa maji .


10.2                          MAFANIKIO 
      Wenye vitalu wanauhusiano mzuri na Ranch ya mzeri hill  imekua shamba darasa  na wamekua wakifuatilia kwa karibu matokeo ya mradi  unao fadhiliwa na COSTECH hapa shambani na wamehaidi kutekeleza matokeo haya kwa vitendo. 

            11.      MRADI UNAO FADHILIWA NA TUME YA SAYANSI(COSTECH)
                        Mwaka 2012 ya sayansi kampuni ilibuni mradi na kupata ufadhili wa tume
ya    sayansi  ( COSTECH)  NARCO I;lishirikiana na chuo kikuu cha SOKOINE
na huu mradi ni wa miaka 3. 
                  Mradi huu ulilenga kufanya  tafiti mbalimbali hasa katika maeneo                       makubwa matatu ambayo ni  :-  

                                     I.            Uboreshaji wa malisho na nyanda za malisho  ambayo majibu ya mwisho yameonyesha kuwepo kwa mafanikio mazuri na yenye tija  kwa kutumia gharama nafuu , lakini pia teknolojia iliyotumika ni rahisi na hvyo kumuwezesha kila mfugaji kumudu kuboresha kila eneo  lake la malisho , kwa mfano  uzalishaji umeongezeka kutoka tani 2.5 mpaka tani 9 kwa hekta. 

                                   II.            Uboreshaji wa kosafu kwa kutumia njia ya uhamilishaji ambapo mbegu bora ya borani  ilitumika kupandisha majike borani wanapopatikana ndanim ya Ranch hii . katika zoezi hili jumla ya ng’ombe 547 walihimilishwa na ng’ombe 364 walipata mimba ambao ni sawa na asilimia 66.5%  na kufaulu kuzalisha jumla ya ndama 359. Ndama hao wamezaliwa wakiwa  na uzito kati ya kilo 35 hadi 40  ukilinganisha na ndama waliozaliwa  kutokana na upandishaji wa asili (madume ) wenye uzito kati ya kilo 25 hadi  30 

                                 III.            Unenepeshaji ulilenga na kuzingatia aina ya mifugo inayonenepeshwa, wakati wa kunenepesha na kiwango wa uzalishaji wa chakula ili kuangalia uwiano wa ongezeko  la uzito baina ya makundi hayo  yanayonenepeshwa na kwa wakati gani . 

   Katika zoezi hili imeonekana  kuwa ng’ombe wa kienyeji akinenepeshwa huongezeka gram 500 kwa siku tofauti na ng’ombe wa nyama wa kisasa (borani) waliongezeka gramu 1000-1500 kwa siku , hata hvyo imegundulika wakati mzuri  wa kunenepesha mifugo kwa gharama nafuu ni kipindi cha mvua na chenye malisho yakytosha. 

       12          SHUKRANI.
      12.1      Nashukuru uongozi wa wilwya za Handeni na Korogwe na Mkoa wa Tanga  kwa
                    Namna ambavyo wamekua wakishirikiana nasi kwa shughuli mbalimbali kwa nia ya
                  Kuendeleza Ranchi hii na wananchi.

     12.2       Tunashukuru wizara yetu ya maendeleo ya mifugo na uvuvi na bodi ya narco na
uongozi mzima wa kampuni kwa juhudi zinazoendelea za kuiboresha kampuni. 

  12.3       TUnaipongeza serikali  kwa kuona umuhimu wa kuimilikisha baadhi  ya maeneo kwa
                  Wawekezaji wa kitanzania pamoja na kufungua milango  ya kukaribisha wawekezaji
wakubwa kwa ranchi za mfano  .Tunaomba serikali iendelee na juhudi za kuitafutia
kampuni mtaji wa kutosha , kama mkaguzi na mzibiti mkuu wa fedha serikali  alivyo
pendekeza katika ripoti zake za miaka mitatu iliyopita. 


 13.          HITIMISHO 
Mh: Waziri,
                Tunaomba kuihakilisha serikali kwamba uwezo wa kufanya kazi tunao , Utaalam tunao
                Nia ya kujifunza zaidi tunayo Juhudi na maarifa tunayo na nia ya kuendeleza Ranchi tu 
               Nayo hivyo tunaomba tupate MTAJI na  tuongezewe mifugo ili tuendeshe Ranchi kwa u
Fanisi zaidi kuliko ilivyo hivi sasa.

NAWASILISHA
EUZEBIUS  RWIZA  MUTAYABARWA
MENEJA WA RANCHI


ZIARA YA WAZIRI MKOA WA MTWARA


HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI MHE. DKT . TITUS MLENGEYA KAMANI (MB) WAKATI WA UZINDUZI WA JENGO LA OFISI YA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO TANZANIA (TALIRI) NALIENDELE, MTWARA TAREHE 2 AGOSTI, 2014.
Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara;
Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Lindi;
Makaibu Wakuu wa Wizara ;
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu COSTECH;
Wakurugenzi wa Taasisi za Utafiti wa Mifugo na Uvuvi;
Wataalamu wa mifugo na Uvuvi;
Viongozi na Wananchi wa Nalindele.
Waandishi wa Habari.
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana
Napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema na kuweza kukutana leo katika hafla hii fupi na muhimu ya kufanya uzinduzi wa jingo la Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Mifugo Kituo cha Naliendele hapa Mtwara. Aidha, nachukua fursa hii kuwashukuru ninyi nyote mliotenga muda wenu wa kuja kujumuika nasi hapa leo.
Ndugu Mkuu wa Mkoa ,Wageni waalikwa na Wananchi; Sekta za Mifugo na Uvuvi ni muhimu  kutokana na mchango wake katiak kuwapatia wananchi lishe bora, ajira na hivyo kuchangia kuondoa au kupunguza umasikini pamoja na kukuza uchumi wa Taifa. Kwa mwaka 2013/2014Sekta ya Mifugo ilikua kwa asilimia 3.8 na kuchangia katika  pato la Taifa kwa asilimia 4.4. Tanzania inakadiriwa  kuwa na ng’ombe milioni 22.8, mbuzi milioni 15.6 na kondoo milioni 7.0. vilevile wapo kuku wa asili 35.5, kuku wa kisasa milioni 24.5 na nguruwe milioni 2.01. ulaji wa mazao ya mifugo kulingana na viwango vya mataifa (FAO, 2011) ni kilo 50 za nyama, lita 200 za maziwa na mayai 300 kwa mtu kwa mwaka. Kwa upande wa nchio yetu viwango vya ulaji wa mazao hayo kwa sasa nui wastani wa kilo 12 za nyama, lita 45 za maziwa na mayai 75 kwa mtu kwa mwaka. Viwango hivi ni vidogo sana ukilinganishwa na mapendekezo ya FAO. Jitihada za makusudi zinatakiwa kuwekwa katika kuhakikisha kuwa wananchi wanahamasishwa kutumia mazao ya mifugo kwa lengo la kuboresha afya zao ili hatimaye tuweze kukaribia viwango vinavyopendekezwa kimataifa.
Ndugu Mkuu wa Mkoa ; Serikali inajizatiti katika kufikia Azimio la Maputo la kutenga karibu asilimia 10 ya GDP yake kwa utafiti ambapo tathimini ya mwaka 2012/2013  inaonesha tunafikia karibu asilimia 8 ukichanganya fedha zote zinazotolewa na Serikali na Wadau wa Maendeleo.

Katika kuimairisha na kuendeleza utafiti Serikali imeweka na inaendelea kuweka mazingira mazuri ya kuendeleza utafiti ikiwemo kuwepo kwa Sera, sharia , kanuni na miundo ya Asasi zinazosimamia na kuendesha utafiti kote nchini kupitia chombo kikuu kinachoratibu cha COSTECH kwa kushirikiana na Wizara husika. TALIRI ambayo imeanzishwa chini ya sharia namba 4 ya mwaka 2012 kuanziaq mwaka huu 2014/2015 itakuwa ianjiendesha chini ya usimamizi na ushauri wa bodi yake ambayo nimeiteua hivi karibuni. Hivyo naiagiza bodi ya TALIRI kuanza kazi mara moja kusimamia na kuelekeza Taasisi hii itekeleze majukumu yaliyokusudiwa na kuweza kujiendesha kisasa na kuleta tija. Mnatakiwa kuhakikisha kuwa mnatumia fursa zote zilizopo na kuacha kufanya kazi kwa mazoea.
Ndugu wananchi; napenda pia kusisitiza na kuelekeaza vityuo vyote vya utafiti chini ya mwavuli wa TALIRI ambavyo vimetamkwa kwa majina katika sharia na vinginevyo vitakavyoanzishwa kutokana na sharia hii vifanye kazi kwa ubunifu wa gharama nafuu lakini wenye matokeo ya haraka ili kufanya secta ya mifugo iwe kiongozi wa uchumi hapa nchini katika muda mfupi ujao. Bodi inayosimamia TALIRI  lazima kuhakikisha inaimarika, inakua haraka na kutoa matokeo mazuri ya kiutafiti katika viwango vya kiamtaifa. Mikakati ya kuboresha miundombinu ya kusomesha wataalamu waliobobea  wenye shahada za juu za PHD waongezeke na miundo mbinu na maabara kuwa za kisasa hadi zifikie viwango  vya kushiriki katika mafunzo ya postgraduate MSc  na PhD zikiwa kama Deemed universities ‘’
Ndugu mkuu wa mkoa ,Wageni waalikwa na wananchi ;  Kazi ya ujenzi wa ofisi ya TALIRI Naliendele ambayo leo nina lizindua ni katika mwendelezo wa utekelezaji wa Ilani ya uchunguzi wa CCM ya 2010-2015 kama ilivyoainishwa  katika ibara ya 38 katika vifungu (e) na(h) vya ilani hiyo kama ifuatavyo:
1.       Kuendeleza elimu kwa wafugaji ili wajue kuwa mifugo waliyonayo ni mali ambayo inaweza kuvunwa katika umri na uzito muafaka unaokidhi mahitaji ya soko , ili kuwaondolea umaskini wao  badala ya kuridhika na wingi wa mifugo iliyo duni na maisha ya kuhamahama .
2.       Kuimarisha utafiti wa mifugo kwa kuboresha na kuhifadhi kosaafu za mifugo ya mifugo ili kuongeza uzalishaji na tija
Serikali imeendelea kudhihirisha utashi wa kisiasa (political will) kwa vitendo kwa kuimarisha utafiti wa mifugo na tafiti nyingine .Kupitia mpango huu serikali imegharimia ujenzi wa jingo hili la TALIRI Naliendelee ambapo limegharimu shilingi 470,821,600/=. Aidha serikali inaendelea naku gharamia ukarabati wa maabara ya Uhawilishaji wa viini tete (embryos) kutumia teknolojia za “embyo transfer” zinazojumuisha (MOET/OPIVF-Multiple ovulation and Embryo Transfer; Ovum Pick-up InVitro fertilization) katika vituo vyake kuanzia na TALIRI Mpwapwa. Nichukue fursa hii kuwapongeza TALIRI kwa kubuni na kuanza kutekeleza ujenzi wa miundombinu ya kutumia teknolojia hii ambayo imeanza kuenea na kutumika duniani kama njia za kusambaza”genomes” zenye sifa kwa wingi na haraka. Matumizi ya teknolojia hizipamoja na nyingine kama “Clonining” zinaweza kupunguza urefu wa muda wa kuzaliana kwa mifugo- “Generation Interval” ambayo ni kubwa kuliko ilivyo ka mazao ya kilimo ya muda mfupi. TALIRI lazima mjipange kujenga uwezo wa wataalamu wenu kuweza kufanya utafiti na kutumia teknolojia hizi na kuwafundisha ndani nan je ya nchi na kuzieneza kwa wafugaji nchini badala ya kuendelea kuzisikia tu kila siku kwenye taarifa na matarajio yenu.
Ndugu Mkuu wa Mkoa; nimetaarifiwa kuwa taliri mnaendelea na ujenzi wa mtambo wa kuchakata maziwa katika kituo cha TALIRI  Uyole na inaendelea kukamilisha ujenzi wa maabara ya utafiti wa nyama ya ng’ombe katika kituo cha TALIRI Mabuki. Napenda kuwapongeza kwa juhudi hizo na kuwaagiza mzikamilishe mapema ili ziweze kutumika na kutoa matunda yaliyokusudiwa. Tafutebni fedha kutoka vituo vingine nje ya vituo vya kawaida kwa kuandika na kuwasilisha maandiko ya miradi maeneo mbalimbali hususani katika mifuko ya kimataifa inayotoa fedha kwa tafiti mbalimbali. Kwa upande wa serikali Wizara yangu itaendelea kuwaombea na kusisitiza Serikali iendelee kugharamia mafunzo ya watafiti wa mifugo katika ngazi mbalimbali kwa lengo la kupata wataalamu mahiri katika sekt6a pana ya utafiti, uzalishaji na afya ya mifugo na samaki.
Ndugu Mkuu wa Mkoa; kwa muda mrefu kumekuwa na changamoto ya kuwepo uunganisho mdogo baina ya utafiti, mafunzo na ugani. Napenda kuchukua fursa hii kuiagiza TALIRI kuanzisha na kuendesha kitengo imara cha usamabazaji teknlojia (technology transfer) katika vituo vyenu kwa kuwa na “Communication and Documentation Center”  mbele tu  za ofisi zenu ambazo zimekuwa chanzo cha kupata taarifa zote za teknolojia zilizokuwa zimekwisha  iva na tayari kwenda kwa watumiaji. Nchini India chini ya mwavuli wa India  Agriculture Research Institute (ICAR) KILA Taasisi ya Utafiti ina kitengo imara cha Mawasiliano na Elimu kwa Umma (Communication and Technology Transfer) mbali na taratibu mlizozizoea za siku ya Wakulima/Wafugaji katika vituo vyenu na tafiti za nje nza kushirikisha wadau.
Kwa upande wa wananchi wa Mkoa Mtwara na Mikoa yote  nchini natoa wito wajenge taratibu na tabia za kufika au kuwasiliana mara kwa mara na vituo vya Taasisi ya Utafiti  wa Mifugo na Uvuvi nchini ili waweze kujifunzza, kuona na kuchukua teknolojia bora zinazoweza kuboresha ufugaji na uvuvi/ ufugaji viumbe kwenye maji ili waweze kuongeza tija na kipato kinachotokana na matumizi ya teknolojia zinazozalishwa kwenye vituo vyetu vya utafiti.  Elimu hutafutwa,  hivyo nawaomba wananci nao waongeze udadisi ili ufugaji wao uwe na tija.
Ndugu Mkuu wa Mkoa; pamoja na mafanikio ya utafiti na jitihada za Serikali kuumarisha utafiti wa mifugo bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali. Mojawapo ya cha changamoto hizi ni pamoja na wananchi wanaozunguka mashamba na vituo vya utafiti kuvamia ardhi iliyotengwa kwa ajili ya shughuli za utafiti. Wananchi katika maeneo yanayozunguka vituo kama vile TALIRI Kongwa , Mpwapwa, Mabuki, Tanga na kituo kidogo cha Mnima Wilayani Newala wamekuwa na tabia ya kuingia kinyume na utaratibu kwenye mashamba haya kwa nia ya kutaka kulima, kuchunga na hata kujenga na hivyo kusababisha uharibifu wa miundombinu na mazingira. Napenda kuchukua fursa hii kuagiza wananchi wote waliopo jirani na vituo vyetu vya utafiti kuheshimu sharia na taratibu zilizowekwa wanapotaka kutumia maeneo  yaliyotengwa na Serikali kwa ajili ya shughuli za utafiti.
Ndugu Mkuu wa Mkoa ; napenda kuhutimisha hotuba yangu kwa kutoa shukrani  zangu za dhati na za Wizara yangu kwa ushirikiano uliopo na unaoendelea na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)  ambayo Serikali iltoa fedha kupitia kwao na yenyewe kutoa fedha kugharamia uimarishaji wa miundombinu ya uatafiti, ujenzi wa miundombinu mipya ya utafiti pamoja na kusomesha watyafiti kwa lengo la kuimarisha na kuboresha utafiti nchini. Pamoja na Taasisis hizo wizara yangu inashauri na kuomba COSTECH kujumuisha Wakala zetu za mafunzo FETA na LITA kuimarisha uwezo na miundombinu ya utafiti ili nazo ziweze kufanya utafiti kutumia wataalamu waliobobea ambao wanazidi kuongezeka kadri Serikali inavyozidi kusomesha.
Nimalize kwa kuwasihi tena wananchi wa Mikoa hii ya Mtwara la Lindi waendelee kushirikiana kna vituo vya utafiti vilivyopo katika ukanda huu wa Kusini ikiwemo TALIRI  Naliendele ili wajipatie maarifa na ujuzi unaotokana na jitihada zinazofanywa na wataalamu wetu. Ninawathibitishia tena kwa Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kuimariosha shughuli za utafiti kwa lengo kuhakikisha kuwa ufugaji na uvuvi unakuwa wa tija na unamkomboa mfugaji na mvuvi kutoka katiak lindi la umasikini.
Maada ya maelezo haya napenda kutamka kuwa “jingo la ofisi ya TALIRI Naliendele limezinduliwa rasmi”
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA.



HOTUBA ILIYOTOLEWA NA KAIMU MKURUGENZI MKUU WA TALIRI DKT. RASHID MSANGI, TAREHE 02/08/2014 WAKATI WA UFUNGUZI WA JENGO LA UTAFITI WA MIFUGO MTWARA NALIENDELE
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Jengo hili la ofisi ya taasisi ya utafiti wa mifugo Naliendele unalozindua leolimegharimu jumla ya shillingi 470,500,000 kati hizo Tume ya   Sayasi na teknolojia (COSTECH) ilichangia jumula ya shilingi 370,500,000 na Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ilichangia jumla ya shilingi 100 milioni.Tunapenda kuishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia COSTECH kwa kutoa fedha hizi ambazo zimewezesha ujenzi wa jengo hili. Jengohili ambalo unalizindua leo litaongeza na kuimarisha kazi za utafiti katika kituo hiki.
Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Mpaka sasa serikali kupitia COSTECH inaendelea kufadhili miradi mitano  ya  utafiti ikiwemo utafiti wa kuku,malisho, nguruwe na ng’ombe wa nyama iliyopo TALIRI  Mpwampwa , Kongwa na Uyole. Aidha COSTECH inaendelea kugharamia ukarabati wa miundombinu ya utafit ikiwemo ukarbati wa maabara ya baiteknolojia (biotecknology) nalishe ya mifugo, Kwa upande mwingine maabara za lishe ya mifugo (animal nutrition laboratory) na baitecknolojia zilizokarabatiwa bado zinahitaji vifaa kuziwezwsha kufanya kazi zilizokusudiwa. Vilevile COSTECH inagharamia mafunzo ya watafiti walioajiriwa na TALIRI waliopo masomoni katikachuo kikuucha Sokoine cha kilimo (SUA) .Tunaishukuru serikali na Tume ya Taifa ya Sayansi na Tecknolojia kwa uwezehaji huo. Aidha tunaomba COSTECH iwezeshe kupata vifaa vya maabara illi ziweze kufanya kazi zilizokusudiwa.
 Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
 Taasisi inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufuwa vitendea kazi na rasilimali watu na fedha. Watafiti wamekuwa wanaandika miradi mbalimbali kwa wadau wa maendeleo ya ndani na nje ili kuweza kuongeza fedha za utafiti na ununuzi wa vitendea kazi. Aidha  Taasisi inakubaliwa na uhaba wa nyumba za watumishi ,lakini pia hata ambazo zipo ni chakavu na zinahitaji kukarabatiwa ,taasisi imekuwa ikitenga fedha zamaendeleo kwa ajili ya ukarabati wa nyumba zake, ingawa fedha hazitoshi.
Moja ya changamoto kubwa zinazoikabili Taasisi ya utafiti wa MifugoTanzania kwa ujumla wake ni uvamizi wa maeneo ya aridhi ambapo wananchi wanaoishi karibu na mashamba ya Taasisi wanakwenda kinyume cha sharia kwa ajili ya kulima, kuchunga, hata kujenga. Hali hii, inasababisha watafiti kushidwa kutekeeza majukumu yao ya kitaaluma ikiwemo kusimamia mipango ya udhabiti wa magonjwa ya mifugo na tafiti za uendelezaji wa malisho bora. Aidha, usalama wa watumishi wa taasisi unahatarishwa zaidi pale ambapo migogoro imepelekea ugomvi. Naomba wananchi walio karibu na mashamba ya taasisi kuwa ni vema kutii sheria na utaratibu zinazohusu matumizi ya rasilimali za umma yakiwemo mashamba ya TALIRI, kwani faida zinazipatikana ni Kwa ajili ya manufaa ya watanzania wote. Aidha, taasisi inawaomb waheshimiwa wabunge na madiwani, kuendelea kuwaelimisha wananchi juu ya kuheshimu mipaka halali ya mashamba ya serikali na taasisi zake.

Mheshimiwa Mgeni Rasmi,
Baada yakusema hayo machache, napenda kukushukuru tena Kwa kukubali kufika Kwa ajili ya shughuli hii.nawatakia wageni wetu wote hafla njema
Ahsanteni sana.



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI





Telegram:Mji Mtwara
Simu: 0732333118
Fax : 0732333118
Barua pepe: vicmtwara@gmail.com
           





                                               
In reply please quart:



 


Kituo cha huduma za mifugo
Kanda ya kusini,
s.l.p 186,
Mtwara



 


                  




                                                                                                    02/08/2014
Kumb. Na.
ADM.20/ZVC/MT/VOL.lll/450

TAARIFA FUPI YA KITUO CHA HUDUMA ZA MIFUGO CHA KANDA YA KUSINI (ZVC MTWARA): KWA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI, MH. DR. TITUS MLENGEYA KAMANI (MB)

Salaam
Mh. Waziri,

Naomba kwa niaba ya idara ya huduma za mifugo na watumishi wote wa kituo cha huduma za mifugo kanda ya kusini; ninakushukuru kwa kuweza kufika katika kituo na kuahirisha majukumu mengine uliyonayo kitaifa.

Utangulizi

 Kituo cha huduma za mifugo cha kanda ya kusini (ZVC Mtwara) kimeanzishwa mwaka 2012 kutokana kugawanywa kwa kituo cha uchunguzi wa magonjwa ya mifugo cha kanda ya kusini (VIC Mtwara) kufuatia kuundwa kwa wakala wa maabara ya mifugo Tanzania (TVLA). Hivyo kituo hiki kwa sasa kinafanya kazi zote zilizokuwa zikifanya na VIC Mtawra isipokuwa utambuzi wa magonjwa ya wanyama ambayo kwa sasa inafanywa na wakala.

Mh. Waziri, kihistoria VIC Mtwara ilizinduliwa mwaka 1982 na Hayati Baba wa Taifa, Mwl, Julius Kambarge Nyerere ikiwa ni mpango wa serikali wa kuingiza na uendelezaji wa mifugo kanda ya kusini. Kituo hiki kilikuwa kikihudumia mikoa mitatu yaani Lindi, Mtwara na Ruvuma. Baadhi ya kazi za iliyokuwa VIC Mtwara ni:
1.     Uchunguzi na ufuatiliaji wa magonjwa mbalimbali ya mifugo kwa ajili ya kubaini kimaabara
2.     Kiusimamia uzuiaji wa magonjwa ya mifugo kwa kushirikiana na halmashauri zote za wilaya, miji, wafugaji binafsi, wafanyabiashara za mifugo na wadau wote wa sekta ya mifugo kwa ujumla.
3.     Kufanya utafiti wa magonjwa ya mifugo.
4.     Upimaji wa kimaabara wa samuli za wanyama.
5.     Udhibiti wa usalama wa biashara za mifugo, wanyama porina mazao yanayotokana na wanyama.
6.     Kuchunguza na kufuatilia magonjwa ya mifugo yanayoathiri pia binadamu kama vile Kimeta, Mafua ya ndege na Kifua Kikuu, Kichaa cha Mbwa na Ugonjwa wa Kuharibu Mimba.
7.     Kusambaza chanjo za mifugo, kufuatilia na kusimamia ufanisi wa chanjozote za magonjwa muhimu kiuchumi na kijamii katika kanda ya kusini.
8.     Kutoa ushauri wa mafunzo ya muda mfupiya uzuiaji na udhibiti wa magonjwa ya wanyama kwa wadau mbalimbali wa sekta ya mifugo kwa kushirikiana na wizara na wadau mbalimbali wa sekta ya mifugo.
9.     Upimaji wa ubora wa dawa za kuogeshea mifugo.
10. Ukusanyaji wa ushuru wa biashara ya mifugo katika masoko ya upili (hayajaanzishwa katiak kanda yetu.).

Mh. Waziri, baada ya kuanzishwa kituo cha huduma za mifugo cha kanda (ZVC Mtwara) kimeendelea na majukumu yote ya iliyokuwa VIC isipokuwa upimaji wa sampuli za maabara na ubora wa dawa za kuogesha mifugo ambazo zipo TVLA au taasisi zingine za serikali.

Kwa sasa kituo chetu mbali ya kufanya kazi hizo juu, chini ya idara ya huduma za mifugo ya wizara yako, ZVC ina majukumu mengine kama vile
       I.            Kusimamia kituo cha uhimilishaji wa ng’ombe kilichopo Lindi Manispaa.
    II.            Kushirikiana na taasisi za kitafiti kama vile TALIRI, SUA, NIMRI, TVLA, TFDA, TANAPA, TAWIRI na nyingine nyingi.
 III.            Kusimamia miradi iliyowekwa na wizara katika kanda.
IV.            Kusimamia ustawi wa wanyama kwa kushirikiana na halmashauri za wilaya na wadau wote mifugo.

Mafanikio
Mh. Waziri kituo kimeendelea kuwa ni tegemeo na kimbilio la matatizo mengi ya wafugaji na jamii. Kwa mfano:
       I.            Tumeweza kubaini na kuweza kuudhibiti ugonjwa wa Sotoka ya mdbuzi na kondoo kwa kuubaini kimaabara na kufuatilia uchanjaji wa mifugo katika maeneo ambayo yalikuwa hayajaathirika.
    II.            Pia ugonjwa wa mdondo/kideri kwa kuku wa asili umeweza kupungua kwa kiwango kikubwa kutokana na uelewa wa wafugaji juu ya matumizi ya chanjo dhidi ya mdondo ikiwa ni pamoja na I2
 III.            Kupitia mradi wa wizara wa kutokomeza kichaa cha mbwa tumefanikiwa kuzuia vifo vya wanyama na binadamu katika halmashauri zinazopitiwa na mradi.
IV.            Tumeweza kufuatilia vifo vya ng’ombe katika jeshi la magereza mkoani Lindi na kudhibiti.
   V.            Pia tumeweza kudhibiti ugonjwa hatari wa kuku katika banda la utafiti wa kuku TALIRI Naliendele.
VI.            Tumefanikiwa kutoa ushauri wa kiutaalamu katiak jeshi la polisi na mahakama juu ya wafugaji au mfugaji aliposhitaki wezi wa mifugo .
VII.            Tumeweza kufuatilia, kuchukua sampuli na kuwasilisha maabara kwa utambuzi wa milipuko ya magonjwa ya homa ya mapafu ya ng’ombe na ugonjwa wa kuoza miguu au midomo.
VIII.            Baadhi ya watumishi wameweza kujiendeleza kitaaluma na kupitia mmiradi ya wizara.
IX.            Vilevile kituo kina baadhi ya watumishi ambao wameweza kutoa machapisho ya kisayansi katika majarida ya kisayansi ya kimataifa.
   X.            Pamoja na kugawanyika VIC,ZVC Mtwara na TVLA katika kituo  hiki tumeendelea kufanya kazi kwa pamoja na bila ya kuelezwa hakuna anayeweza kuuona mgawanyiko katika shughuli zetu.

Pamoja na mafanikio haya juu kituo kinakumbana na changamoto nyingi kama ifuatavyo:
       I.            Uhaba wa watumishi. Kwa sasa kituo kina jumla ya watumishi watano tu  VO-2, LFO-2 na dereva mmoja. Kituo kinahitaji kuongezwa watumishi kama ifuatavyo VO-1, LFO-2, Mhasibu 1, Mnunuzi 1, PS -1 na dereva 1.
    II.            Kituo kinahitaji kuwa na ofisi nje ya maabara na miundombinu ya kuhifadhi chanjo lakini bado hakijafanikiwa kupata fedha za ujenzi wa ofisi ijapokuwa katika bajeti iliyopita tumeweza kuweka katiak bajeti ya maendeleo.
 III.            Gari tunalo moja la mradi wa kichaa cha mbwa ambalo limekuwa likitumika katika ofisi zetu mbili (TVLA na ZVC Mtwara). Hivyo likienda safari kituo kinabaki bila usafiri.
IV.            Ucheleweshwaji wa malipo ya fedha za matumiziya ofisi unaotokana na mfumo mpya wa malipo katika hazina. Hili husababisha kituo kushindwa kutumia fedha katika shughuli zake. Mfano OC ya mwezi Mei haijalipwa kutokana na matatizo ya mfumo TISS ijapokuwa hazina ndogo ilikuwa imeshaziingiza kwa malipo.

Mh. Waziri ili kupunguza changamoto za kituo, na hususani bajeti finyu inayotolewa ya OC kati ya milioni 16 na milioni 26 kwa mwaka; baadhi yetu watumishi tumekuwa tukiandika miradi na kufanikisha fedha kiasi cha shilingi milioni mia moja ishini na moja (mil. 121) katiak miaka miwili iliyopita. Pamoja na hilobado kituo kinaomba utusaidie tuweze kufanikisha yafuatayo:
       I.            Ujenzi wa ofisi kama utakavyozindua leo hapa taliri tunakadiria shilingi milioni mia tatu sabini zinaweza kufanikisha hilo.
    II.            Kupata gari moja au mawili zaidi aina ya landcuiser station wagon kwa kuwa shughuli zetu zinahitaji kusafiri mara kwa mara.
 III.            Wizara iendelee kuajiri watumishi wa sekta mifugo hapa kituoni na hata katika halmashauri.

Mwisho japo si kwa umuhimu tunaomba upokee taarifa hii na tunakukaribisha sana uzidi kufanya ziara kama hii mara kwa mara wakati mwingine.

Wako katika ujenzi wa Taifa letu na ninayoheshima kuwasilisha.

Dr. Albano Oscar Mbyuzi
Afisa Mfawidhi
Kituo cha huduma za mifugo kanda ya kusini
ZVC Mtwara.






HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA DK. TITUS MLENGEYA KAMANI (MB) KWENYE UZINDUZI WA MFUMO WA KITAIFA WA UTAMBUZI NA UFUATILIAJI MIFUGO ULIOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA SHULE YA MSINGI MTONGANI, MLANDIZI WILAYA YA KIBAHA, JULAI 22, 2014.

Mheshimiwa Mwamtumu Mahiza, Mkuu wa Mkoa wa Pwani;
Mheshimiwa Diana Templelman, Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa Chakula na Kilimo (FAO);
Mhreshimiwa Minoru Homma, Mwenyekiti wa Development Partners - Agricultural Working Group;
Mheshimiwa Halima Kihemba , Mkuu wa Wilaya ya Kibaha;
Mheshimiwa Abuu Juma, Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini;
Mheshimiwa Mansuli Ally Kisebengo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha;
Mheshimiwa Kasongo Kirendu, Makamu Mwenyekiti wa Hlmashauri ya Wilaya ya Kibaha;
Mheshimiwa Fatma Shari, Diwani wa Kilangalanga;
Wakurugenzi wa Wizara na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya mliohudhuria;
Dr. Helmut Karb, Mkandarasi wa ADT-UBK toka Ujerumani;
Wenyeviti wa Vyama vya Wafugaji, Asasi na Wadau wengine wa Mifugo.
Waandishi wa Habari;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana.

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kufika siku ya leo tukiwa na afya tele. Aidha, napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru waandaaji wa hafla hiikunialika kuwa Mgeni Rasmi kwenye Uzinduzi wa Mfumo wa Kitaifa wa Utambuzi na Ufuatiliaji Mifugo.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) kupitia Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Wilaya ya Kibaha kupitia Mkuu wa Wilaya na Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha pamoja na wadau wengine waliochangia kwa namna moja au nyingine katika kuandaaa na kufanikisha shughuli hii muhimu kwa mustakabali wa uchumi wan chi yetukupitia biashara ya mifugo.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa, Tanzania imejaliwa kuwa na rasilimali kubwa ya mifugo. Kulingana na takwimu zilizopo, idadi bya mifugo nchini inakadiriwa kuwa na ng’ombe milioni 22.8, mbuzi milioni 15.6 na kondoo milioni 7.0. vilevile wapo kuku wa asili 35.5, kuku wa kisasa milioni 24.5 na nguruwe milioni 2.01. rasilimali ya mifugo hii tuliyonayo inatosheleza soko la ndani ya nchi na tunaweza kuuza ziada nje ya nchi. Tanzania tunauza wastani wa tani 353 za nyama ya mbuzi na kondoo kwa mwaka yenye thamani ya US$ 1,343,960 katika soko la Mashariki ya kati tu na hatujaingia la Asia ya mbali na Ulaya ambako moja ya masharti ni kuwa na mfumo wa utambuzi wa mifugo unaofanya kazi. Uchumi wa mifugo unategemea sana upatikanaji wa soko la uhakika kwa mifugo na mazao yako. Nchi nyingi duniani ambamo mifugo inachangia katika uchumi ni kutokana na masoko makubwa ya mifugo. Soko zuri la  
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Ndugu Wafugaji, mfumo wa Utambuzi na Ufuatiliaji Mifugo ni nyenzo muhimu na yalazima katika ufugaji kwa sasa dunianikote ili kuwezesha kukubalika katika masoko ya kimataifa. Pamoja na hayo ni nyenzo inayosaidia kukabilian na magonjwa ya mifugo, wizi wa mifugo, uhamishaji au usafirishaji holela wa mifugo na hivyo kuepusha migogororo baina ya wafugaji na wakulima pamoja na watumiaji wengine wa ardhi.
Mfumo wa utambuzi na ufuatiliaji mifugo kwa tafsiri rahisi ni utaratibu unaotuwezesha kuwa na alama katika mifugo katika mifugo na kuweka kumbukumbu za matukio muhimu katika maisha ya mifugo yetu. Utaratibu wa kuweka kumbukumbu ndio usajili wa mifugo, wafugaji na matukio muhimu ya mifugo yetu. Mfano kuzaliwa, vifo, kupotea, kuhama au kusafirisha, chanjo au matibabu mengine ili kuhifadhi kumbukumbu zote hizi nilizotaja na nyingine nyingi unahitajika mfumo wa kompyuta uliojengwa mahsusi kwa ajili ya shughuli hiyo. Kwa bahati nzuri Tanzania tumepata msaada wa Dola za Kimarekani 475,000 sawa na Tsh. 781,375,000/= kutoka kwa wnzetu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) ambao walitusaidia kuujenga Mfumo kupitia wazabuni wa Kampuni za Kijerumani zilizoitwa UBK na ADT. Nimearifiwa kwamba mfumo huu wa kompyuta umekamilika na sasa umeanza kufanya kazi katika Wilaya za mfano za Kibaha, Bagamoyo na Mheza ambapo jumla ya ng’ombe 5,845 wametambuliwa.
Ndugu wafugaji, Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania lilitunga Sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuattiliaji Mifugo Na 12 ya mwaka 2010 (Sura 184) na pia Waziri waMaendeleo ya Mifugo na Uvuvi chini ya Sheria hii alitoa kanuni zza kuwezesha utekelezaji wa sheria hii kupitia Tangazo la Serikali namba 362 (G.N. 362)
Sharia hii na kanuni zake zinatumika  kwa pamoja na sheria nyingine chini ya Wizara yangu ambazo nazo zinalenga kuboresha uzalishaji wa mifugo na soko lake. Sheria hizi  ni pamoja na Sheria ya Magonjwa ya Mifugo (Animal Diseases Act  2003), Sheria ya Tasnia ya Nyama (Meat Industry Act, 2006), Sheria ya Nyanda za malisho na Rasilimali ya Vyakula vya Mifugo Na. 13 ya mwaka 2010 na Sheria ya Ngozi (Sheria Na.18,2008).
Ndugu wafugaji, utekelezaji wa Mfumo huu baada ya kuuzindua leo hautakuwa jambo la hiyari au utashiau utashi wa mfugaji bali ni lazima kwa mujibu wa Sheria na Kanuni. Hivyo, napenda kuchhukua fursa hii kuwashauri na kuwaelekeza wafugaji wote katika maeneo ambayo Waziri nitatangaza kuwa ya Utambuzi wa Mifugo(Compusory Livestock Identification Areas) washiriki katika kutambua na kusajili mifugo yaona wawe tayari kuchangia katika ununuzi wa vifaa vya utambuzi wa mifugo hiyo. Serikali kupitia Wizara yangu pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa itasimamia na kuratibu utekeleza wa Mfumo kwa faida ya wafugaji na maendeleo ya sekta kwa ujumla.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Ndugu Wafugaji, Ili usimamizi na utekelezaji wa mfumo huu uwe endelevu katika ngazi za Mamlaka za Serikali za Mitaa, Wizara yangu inazishauri mamlaka hizi kufufua na kutumia mifuko ya Maendeleo  ya Mifugo (Livestock Development Fund LDF). Mfuko huo utawezesha kuwa na fedha za mzunguko za kununulia vifaa vya utambuzi na kuchangia gharama za nyingine za  uendeshaji. Napenda nichukue nafsi hii kuwapongeza  Halmashauri za Wilaya za Karagwe na Ngara Mkoani Kagera kwa tafsiri sahihi ya kifungu cha 24Kifungu Kidogo cha 2 cha Sheria ya Utambuzi na Ufuatiliaji Mifugo ambacho kimetamka kwamba wanufaika na mfumo huu wachangie gharama ambapo walitaka wafugaji wao kuchangia. Hivyo  Mamlaka za Serikali mza Mitaa  nyingine nchini hazina budi kuiga mfano huu.
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Wananchi, Ili ufuatiliaji wa mifugo na mazao yake katika mnyororo wa thamani wa mifugo nuwezekane kupitia huu. Hapana budi wadau wanaohusika kuanza ufugaji, wasafirishaji, waendesha minada, waendesha machinjio na Maafisa Ugani pamoja na wasimamizi wa Kanzidata ya Mfumo (TANLITS Database) watimize majukumu yao kama yale ya kutambua mifugo, kutoa taarifa ya mifugo inapozaliwa, kufa, kuchinjwa au kusafirishwa.
Ndugu wafugaji na wananchi, mwisho napenda nitoe shukrani zangu za dhati kwa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Kimataifa (FAO), kwa msaada wa kugharamia ujenzi wa mfumo huu. Aidha, shukrani hizi ziwaendee Washirika wetu wa Maendeleo (Development Partners) waliokuwa wakichangia katika  Mfuko wa ASPP Busket Fund (Irish Aid, IFAD, JAICA na Benki ya Dunia), Mradi wa EAAPP (Benki ya Dunia) na Serikali kwa kugharamia unu nuzi wa wa vifaa vya utambuzi na usajili wakati wa ujenzi wa mfumo huu.
Vilevile napenda nishukuru Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Watendaji wa Wizara yangu, Wafugaji na Wananchi wa Mlandizi kwa kuandaa hafla hii.
Napenda kutambua nafasi na ushiriki wa taasisis mbalimbali kwenye ujenzi wa Kanzidata ya Mfumo wa Utambuzi na Ufuatiliaji Mifugozikiwemo;  Ofisi ya Taifa ya Takwimu ambao wametuwezesha kupata takwimu mbalimbali za maeneo na ramani, Mamlaka ya Vitambulisho ya Taifa na Wakala wa Serikali Mtandao kwa ushauri na Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kwa mawasiliano ya mtandao. Aidha nalipongeza Shirika la Utafiti wa Maendeleo ya Viwanda (TIRDO)LILILOSHIRIKI Katika hatua za awali za uanzishwaji wa mfumo kwa kuwezesha mijadala ambayo hatimaye ilizaa mfumo huu. Pia Benki ya Rasilimali (TIB) ambayo imeonesha nia ya kushiriki kwa kuhamasisha wale wanaotaka kuwekeza katika ufugaji kuzingatia matakwa ya kuwa na mfumo huu.
Ndugu wananchi, natoa wito kwa Taasisi nyingine za Kitaifa na Kimataif kuendelea kushirikiana na Wizara yangu kuimarisha na kuboresha zaidi  mfumo huu ili uweze kukidhi mahitaji ya Nchi nzima naviwango vya Kimataifa.
Pamoja nanyi narejea tena kusisitiza kauli mbiu ya uzinduzi wa mfumo huu; “SAJILI MIFUGO YAKO KWA UHAKIKA WA SOKO NA UDHIBITI WA WIZI WA MIFUGO NA MIGOGORO”
Baada ya kusema hayo napenda kutangaza kuwa Mfumo wa Kitaifa wa Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji Mifugo Mifugo Umezinduliwa Rasmi.
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA.


UTEUZI












VIKAO VYA WAKUU WA IDARA/VITENGO NA WATENDAJI WAKUU WA WIZARA

Kila wiki siku ya  Jumatatu ni siku ya kufanya Kikao cha Wakuu wa Idara na Vitengo wa wizara kuanzia saa nne kamili asubuhi. Kama unahitaji kumuona katibu Mkuu Naibu Katibu Mkuu, Mkuu wa Idara au Kitengo, hakikisha unamuona kabla ya saa za kikao .  


BARAZA LA WAFANYAKAZI 

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi ilifanya Kikao cha Baraza hilo katika ukumbi wa ST Gaspar pale Dodoma mapema mwezi juni 2011 tarehe 16 na 17 /06 na kutoa Maazimio ambayo sasa yanatekelezwa . Watumishi wote walishiriki katika uchaguzi wa uongozi mpya wa TUGHE hapa Wizarani na RAAWU kwa upande wa Utafiti kule Mpwapwa ambapo ndipo ilipo Taasisi ya Taifa ya Utafiti ya Mifugo Mpwapwa. Wakuu wa Idara na Vitengo wamepewa dokezo la kukumbushwa utekelezaji wa maazimio yaliyopitishwa pale Dodoma dokezo la tarehe 11/10/2011 na Katibu wa Baraza .

HOTUBA YA BAJETI  2011/12

Hotuba ya bajeti ya wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi imechapishwa kwenye gazeti la Uhuru na Habari leo tarehe 28/07/2011, pia inapatikana kwenye mtandao wa wizara http://www.mifugo.co.go.tz/  


MAANDALIZI YA MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA KWA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI  YATAFANYIKA VIWANJA VYA SABASABA BARABARA YA KILWA -  DAR-ES-SALAAM KUANZIA TAREHE 1 - 12/12/2011

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi inapenda kuwajulisha Wadau na Wananchi kuwa itashiriki kwenye maonyesho tajwa hapo juu, yatakayofanyika kuanzia tarehe 1 - 12 /12/2011. Wadau wote wanakaribishwa, ambapo baadhi ya wadau watakuwa ni sehemu ya maadhimisho hayo, kwa wale ambao hawatashiriki moja kwa moja waje waone wenzao hatua waliyopiga mbinu ,utaratibu na utendaji wao wa kazi. (KUONA NI KUAMINI) Hakuna lisilo wezekana Vilevile mtapata fursa ya kuelezewa na Wizara ni huduma gani ambazo ikiwa ni Idara au Vitengo vya Mifugo na Uvuvi hufanya katika kuendeleza Sekta hizo muhimu katika maisha ya Mtanzania,  nini jukumu la Wizara katika kutekeleza Sera Mipango na Mikakati mbalimbali ambayo imeandaliwa  na Wizara. Aidha Wadau watakuwepo kuonyesha matokeo ya Sera, Mipango Mikakati mbalimbali ambapo wataeleza na kuonyesha wamenufaika vipi na usimamizi na ufuatiliaji huo wa Wizara katika kutekeleza azma ya Serikali ya kuendeleza sekta hizo mbili kwa ujumla. 

Wote Mnakaribishwa

WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI.

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, imegawanyika kwenyeSekta kuu mbili  yaani Sekta ya
  •  Mifugo 
  • Uvuvi 
  • zile za Mtanbuka
Sekta ya Mifugo ina Idara zifuatazo:
  1. Huduma za Mifugo.,
  2. Uzalishaji, Masoko na Matumizi ya ardhi kwa mifugo,
  3. Utafiti Mafunzo,Ugani Utanmbuzi na ufuatailiaji wa Mifugo.
  4. Maabara Kuu ya Mifugo
  5. Baraza ka Vetenary
  6. Taasisi ya Taifa ya Utafiti Mpwapwa
Sekta ya Uvuvi ina Idara zifuatazo
  1. Maendeleo ya Uvuvi
  2. Uzalishaji Viumbe kwenye Maji.
Idara za Mtambuka
  1. Sera na Mipango
  2. Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu.
Viengo Mtambuka
  1. Fedha
  2. Sheria
  3. Ukaguzi wa Ndani
  4. Manunuzi
  5. Mawasiliano Serikalini.
Kila Idara au Kitengo kina Mkuu wa Idara/Kitengo Je unahitaji kuwasiliana na Mkuuwa Idara au Kitengo tuma barua yako ya maombi kwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi tuma maswali yako kabla ili yamfikie mhusika ayajibu kwa uhakika nawe utakabidhiwa.

"TUSHIRIKIANE KATIKA KUENDELEZA WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI"