RUKWA NAO WAREJESHA UVUVI WA ZIWA TANGANYIKA
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Charles Makongoro Nyerere amewaongoza wananchi wa mkoa huo kwenye hafla ya ufunguzi wa shughuli za Uvuvi wa Ziwa Tanganyika kwa upande wa mkoa huo iliyofanyika kwenye kata ya Kasanga Agosti 17, 2024. Katika hotuba yake ya ufunguzi wa shughuli hizo Mhe. Nyerere ambaye alimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega mbali na kuwashukuru Wavuvi wa mkoa huo kwa uvumilivu wao wakati wote wa ufungaji wa ziwa hilo amewataka kuvua kwa kufuata sheria na taratibu ili kutunza rasilimali iliyopatikana. Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede mbali na kuwaeleza wananchi wa mkoa huo umuhimu wa upumzishwaji wa Ziwa hilo, amewataka wavuvi hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali wakati wote inapokuwa na kampeni inayolenga kulinda rasilimali za Uvuvi. Akitoa Ushuhuda wa mavuno aliyopata baada ya ufunguzi huo, Mmoja wa wavuvi kutoka kijiji cha Kilewani Bw. Adam Pesambili amesema kuwa kwa usiku mmoja tu...