Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2024

RUKWA NAO WAREJESHA UVUVI WA ZIWA TANGANYIKA

Picha
  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Charles Makongoro Nyerere amewaongoza wananchi wa mkoa huo kwenye hafla ya ufunguzi wa shughuli za Uvuvi wa Ziwa Tanganyika kwa upande wa mkoa huo iliyofanyika kwenye kata ya Kasanga Agosti 17, 2024. Katika hotuba yake ya ufunguzi wa shughuli hizo Mhe. Nyerere ambaye alimwakilisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega mbali na kuwashukuru Wavuvi wa mkoa huo kwa uvumilivu wao wakati wote wa ufungaji wa ziwa hilo amewataka kuvua kwa kufuata sheria na taratibu ili kutunza rasilimali iliyopatikana. Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede mbali na kuwaeleza wananchi wa mkoa huo umuhimu wa upumzishwaji wa Ziwa hilo, amewataka wavuvi hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali wakati wote inapokuwa na kampeni inayolenga kulinda rasilimali za Uvuvi. Akitoa Ushuhuda wa mavuno aliyopata baada ya ufunguzi huo, Mmoja wa wavuvi kutoka kijiji cha Kilewani Bw. Adam Pesambili amesema kuwa kwa usiku mmoja tu...

PROF.SHEMDOE AFUNGA MAFUNZO YA WAVUVI KIZIMKAZI- ZANZIBAR

Picha
  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe jana tarehe 16 Agosti 2024 amefunga mafunzo ya wavuvi wadogo wadogo yaliyokuwa yanafanyika Zanzibar, Wilaya ya kusini Unguja katika Kijiji cha Kizimkazi. Akifunga mafunzo hayo Prof.Shemdoe amesema kuwa Mafunzo hayo ni muhimu kwa Wavuvi hao kwasababu lengo lake kubwa ni kuwajengea uwezo Wavuvi katika nyanja mbalimbali ikiwemo ufugaji wa Samaki, Uchakataji wa Dagaa, Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi pamoja na Utunzaji wa mazingira ya bahari ili wazalishe kwa ufanisi na kujiongezea kipato. Aidha, Prof. Shemdoe amesema kuwa anajua wavuvi wanachangamoto mbalimbali na ameahidi changamoto zote walizonazo wavuvi hao zitafanyiwa kazi kwa kuwa Serikali ya Awamu sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni sikivu na inawapenda Wavuvi. Pia Prof.Shemdoe amesema kuwa anamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoendelea kuif...

UHUSISHWAJI WA SEKTA BINAFSI KATIKA UKUZAJI VIUMBE MAJI NI JAMBO LA MSINGI - EMELDA

Picha
Na. Stanley Brayton Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Mafunzo ya Uvuvi, Bi. Emelda Adam ame uhusishwaji wa sekta binafsi katika tasnia nzima ya ukuzaji viumbe maji ni jambo la msingi kwa sababu kwa sababu itaongeza mnyororo wa thamani. Akizungumza, leo Agosti 15, 2024 mkoani Mwanza katika kongamano la Tatu la Afrika Mashariki la Ukuzaji Viumbe Maji lililoudhuliwa na nchi 18 za Afrika, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti na Mafunzo ya Uvuvi, Bi. Emelda amesema ili nchi zinyanyuke kutoka hatua moja kwenda nyingine lazima ishirikishe sekta binafsi . "na itambulike kwa sasa, ukuzaaji viumbe maji unachangia takribani pato la taifa kwa asilimia 50 kwenda 51 ya samaki wengi ambao wanazalishwa duniani." amesema Bi. Emelda Aidha, Bi. Emelda alisema kwa Tanzania kwa sasa katika swala la ukuzaji viumbe maji tupo katika asilimia 10 na bado tuna nafasi ya kusogea mbele zaidi kama tutaendelea kuhusisha sekta binafsi katika swala zima la myororo wa thamani katika ufugaji viumbe maji,...

TANZANIA, CHINA KUIMARISHA BIASHARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amekutana na Waziri wa Forodha kutoka Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Yu Jianhua kujadiliana namna ya kuendelea kuboresha ushirikiano na kutanua fursa za kibiashara baina ya nchi hizo mbili hususan kwenye sekta za mifugo na uvuvi. Waziri Ulega amekutana na waziri Jianhua jijini Dar es Salaam mapema leo Agosti 14, 2024. Akiongea katika mkutano huo, Waziri Ulega amesema kuwa mkutano wao huo ni muendelezo wa mkutano baina ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jiping ambapo walikubaliana masuala kadhaa ya kibiashara baina ya nchi hizo.  “Mkutano wetu wa leo unahusu kufanya majadiliano ya namna ya kuendelea kuboresha ushirikiano na kutanua fursa za kibiashara kwenye sekta za mifugo na uvuvi ikiwa ni muendelezo baada ya mkutano baina ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Ji Ping”, amesema Amesema fursa ya biashara ya mazao ya mifugo na uvu...

MNYETI AWATAKA WADAU WA UVUVI WAZALISHE SAMAKI KWA NJIA YA KISASA

Picha
Na. Stanley Brayton Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amewataka wadau wa uvuvi kuzalisha samaki kwa njia ya kisasa ili kuongeza wingi wa samaki kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watu kwani kwa sasa kuna upungufu wa samaki. Akizungumza, leo Agosti 13, 2024 mkoani Mwanza katika kongamano la Tatu la Afrika Mashariki la Ukuzaji Viumbe Maji lililoudhuliwa na nchi 18 za Afrika, Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mnyeti amesema serikali itaendelea kuhamasisha wadau mbalimbali ili wajitokeze kwa wingi na kufuga kwa teknolojia. "tutaendela kuhamasisha wadau mbalimbali wajitokeze kwa wingi kwani vizimba vipo vingi vinavyohitaji wadau na tunawakaribisha wawekezaji kutoka nchi mbalimbali waje wawekeze kwa sababu maeneo ya kufugia samaki yapo na vizimba vipo." amesema Mhe. Mnyeti Aidha, Mhe. Mnyeti alisema awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeamua kuleta mabadiriko na maboresho makubwa, ...

TEKNOLOJIA YA JUNCAO SULUHISHO MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega  amesema teknolojia ya uzalishaji wa malisho aina ya Juncao ambayo imeanza kutumika hapa nchini ni suluhisho la  kumaliza changamoto za malisho ya mifugo na kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji hapa nchini. Waziri Ulega amesema  hayo wakati alipouongoza ugeni kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) wakiwakilishwa na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja huo,  Earle Courtenay Rattray kutembelea Shamba la Serikali la Mbegu za malisho aina ya Juncao lililopo Vikuge, Kibaha mkoani Pwani leo Agosti 9, 2024. “Katika shamba hili la serikali la Vikuge kuanzia mwaka 2021 hadi mwaka huu wa 2024 tumeshapanda majani ya juncao ekari 21, mbegu zilizozalishwa ni Kilo 178,262, huku zaidi ya  wakulima 957 wakishiriki kulima majani hayo kwa hatua tofautitofauti”, amesema Ulega Aidha, Waziri Ulega ameushukuru Umoja wa Mataifa kwa mchango wao mkubwa katika kuwajengea uwezo wataalam mbalimbali wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuifahamu tek...

NG'OMBE WA KITULO WAMSHANGAZA RIDHIWANI KIKWETE

Picha
◼️ Mnyeti agusia mpango wa Vizimba Ziwa Nyasa  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ameshangazwa na ukubwa wa ng'ombe waliopo kwenye ranchi ya Kitulo mkoani Njombe. Tukio hilo limetokea Agosti 8, 2024 jijini Mbeya kwenye kilele cha Maadhimisho ya Sikukuu ya kimataifa ya wakulima kwa upande wa kanda ya Nyanda za Juu kusini ambapo Mhe. Kikwete alikuwa mgeni rasmi wa tukio hilo akimwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa. "Pale kwetu sisi ni wafugaji tena wafugaji wa kisasa na nilikuwa ninasema nina ng'ombe mkubwa sana lakini leo nimekutana na ng'ombe mwenye uzito wa kilo 900 pale kwenye banda la Shamba la Mifugo la Kitulo, Hongera sana Mkuu wa Mkoa wa Njombe maana shamba hili lipo mkoani kwako" Amesema Mhe. Kikwete. Mhe. Kikwete ametumia jukwaa hilo kutoa rai kwa wafugaji wengine kufuga kisasa ili ufugaji wao uwe na tija na kubadili maisha yao kwa ujumla. "Nimesikia...

RAIS SAMIA ATOA BIL 1.1 KWA VIJANA WA BBT, KUFUGA KWA TIJA

Picha
Na. Edward Kondela Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekabidhi Shilingi Bilioni 1.1 kwa vikundi 25 vya programu ya “Jenga Kesho Iliyo Bora” (BBT) ili viweze kufuga kwa tija. Kabla ya kukabidhi mfano wa hundi hiyo kwa baadhi ya wanufaika wa programu ya BBT, kwenye kilele cha Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi (Nane Nane) ambayo kitaifa yamefanyika kwenye viwanja vya Nzuguni Mkoani Dodoma (08.08.2024), Rais Samia ameonesha kufurahishwa namna vijana wanavyoendelea kunufaika kupitia sekta za mifugo na uvuvi, baada ya kutembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Rais Samia amewataka vijana kutumia vyema fursa zinazojitokeza ili waweze kujiinua kiuchumi na kutoa elimu kwa wenzao ambao bado hawajachangamkia fursa hizo hususan katika sekta za mifugo na uvuvi. Wakati Rais Samia akikabidhi mfano wa hundi hiyo ya Shilingi Bilioni 1.1 kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema fedha hiyo ni ...

MTAKA AKOSHWA NA KAZI ZA WIZARA NANENANE MBEYA

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amepongeza kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi na wadau wake kupitia maonesho ya mwaka huu ya  kimataifa ya Kilimo (NaneNane) kwa upande wa kanda ya Nyanda za Juu kusini yanayoendelea mkoani Mbeya.                        Mhe. Mtaka ametoa pongezi hizo mara baada ya kufika kwenye mabanda ya Wizara hiyo                             ambapo alioneshwa kuvutiwa zaidi na bidhaa ya viatu vinavyotengenezwa kutokana na                                  ngozi inayozalishwa hapa nchini. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) kanda ya nyanda za juu kusini ambaye pia ni Mratibu wa maonesho hayo kwenye kanda hiyo Bw.Edwin Chang'a amemueleza Mhe. Mtaka kuwa Wiz...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI INAENDELEA KUTOA ELIMU YA UBORESHAJI MBARI ZA MBUZI WA KIENYEJI KWA WAFUGAJI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Taasisi ya Utafiti a  Mifugo (TALIRI) inaendelea kutoa elimu ya uboreshaji wa mbari za mbuzi wa kienyeji kwa Wafugaji kupitia maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea kufanyika Kanda ya ziwa Magharibi katika Viwanja vya Nyamhongolo jijini Mwanza. Akitoa elimu hiyo kwa wadau waliotembelea kwenye banda la Wizara hiyo Agosti 06,2024. Afisa Mifugo wa Taasisi hiyo Bw. Amos Kisusi amesema madume ya mbuzi 15 ya Boer kutoka Afrika kusini yametumika kuboresha mbari za mbuzi 450 wa kienyeji waliotolewa na serikali.  Bw. Kisusi amesema uboreshaji wa Mbari za Mbuzi aina ya boer ni moja ya miradi ya wizara ya Mifugo na Uvuvi ambao unayooneshwa kupitia viwanja vya maonesho ya kilimo, mifugo na uvuvi Nane Nane jijini Mwanza, ambapo ulianza mwaka 2021 kwa ujenzi wa mabanda bora ya kuhifadhi Mbuzi aina ya Boer. Aidha, Mbuzi 15 aina ya Boer walipokelewa 2022 kutoka nchini Afrika kusini kwa gharama ya shilingi milioni 42 na wakaanza kupanda majike wa kien...

FETA YATOA ELIMU YA MFUMO WA KUZALISHA SAMAKI NA MAZAO "AQUAPONICS" NANENANE.

Picha
Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi Tanzania (FETA) yatoa elimu ya mfumo wa kuzalisha samaki na Mazao kwa wadau waliotembelea kwenye Maonesho ya Kilimo ya Kimataifa Nanenane yanayoendelea kufanyika Kanda ya Ziwa Magharibi, katika Viwanja vya Nyamhongolo jijini Mwanza. Akitoa elimu hiyo Agosti 04.2024, kwa wadau waliotembelea kwenye banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mkufunzi wa Wakala hiyo kutoka Kampasi ya Nyegezi (Mwanza), Bw. Mukama Ndaro aliwaelezea mfumo huo unavyoleta faida kwa Wafugaji. Bw. Ndaro ameelezea kuwa uchafu unaozalishwa na samaki unakuwa mbolea kwa mazao, na Mazao yanayasafisha maji kwa kuchuja mbolea (mkojo) inayotokana na samaki na kufanya maji hayo yawe masafi kwa matumizi ya ufugaji wa samaki tena.  "Mchakato wa kuchuja mbolea au uchafu unatokana na samaki na chakula hufanywa kwa msaada wa Viorwa aina ya bakteria (Nitrobacter na Nitrosomonas)  Viorwa hao hugeuza Amonia kuwa Nitrite ambazo ni sumu kwa samaki Kisha Nitrite hugeuza kuwa Nitrate ambayo ni mb...

WATAALAMU WAASWA KUPELEKA TEKNOLOJIA YA MIFUGO NA UVUVI VIJIJINI

Picha
Na. Stanley Brayton Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule amewahasa wataalamu wa mifugo na uvuvi kupelekea na kufundisha teknolojia ya mifugo vijijini ili kuwapa wafugaji elimu ya kutosha kuhusu ufugaji wa kisasa kwa lengo la kuleta tija katika sekta hiyo. Akizungumza, leo Agosti 4, 2024 mkoani Dodoma alipotembelea kwenye Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa yanayofanyika Kitaifa mkoani Dodoma katika mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Senyamule amesema wataalamu wahakikishe teknolojia hii inawafikia wadau wote wa mifugo na uvuvi, ususani maeneo ya vijijini. "wataalamu wachukue hatua ya kwenda kwenye makundi ya wafugaji ili kwenda kuwaelimisha kuhusu teknolojia mpya ya ufugaji na kuhakikisha inawafikia" amesema Mhe. Senyamule Aidha, Mhe. Senyamule alisema serikali ya awamu ya sita ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanya mapinduzi makubwa sana katika sekta ya Mifugo na Uvuvi kwani ameshuhudia teknolojia mbalimba...

RC DENDEGO AWAKUMBUSHA WAFUGAJI KUFUGA KWA TIJA NA KIBIASHARA

Picha
Na. Stanley Brayton Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amewakumbusha wafugaji wote hapa nchini Tanzania kufuga kwa tija na kibiashara kwani ufugaji ni utajiri. Akizungumza, leo Agosti 5, 2024 mkoani Dodoma alipotembelea eneo la arena ya mifugo katika maonesho ya nanenane ya Kimataifa yanayofanyika Kitaifa Mkoani Dodoma kushuhudia mifugo mbalimbali ikishindanishwa kwa ubora, Mhe. Dendego amesema wafugaji wanatakiwa kufuga kibiashara ili kuleta tija na kuongeza ajira ili kuondokana na umasikini na kuchangia uchumi wa nchi na wa mfugaji mmoja mmoja. "serikali ya awamu ya sita ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Dkt. Samia Suluhu Hassan inafanya juhudi katika kutekeleza ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020/25 yenye malengo ya kuendeleza Sekta ya Mifugo, Uvuvi na Kilimo" amesema Mhe. Dendego Aidha, Mhe. Dendego alisema shughuli hizi ni pamoja na kuimarisha ushiriki wa sekta binafsi ili kuongeza uzalishaji, tija na thamani ya mazao ya Mifugo, Uvuvi na Kilimo...

PROF. SHEMDOE AHIMIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KWENYE MIFUGO NA UVUVI

Picha
Na. Stanley Brayton Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, amehimiza matumizi ya teknolojia ya Mifugo na Uvuvi kwa wafugaji ili kuweza kuleta tija katika uzalishaji. Akizungumza, leo Agosti 2, 2024 mkoani Dodoma alipotembelea kwenye Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa yanayofanyika Kitaifa mkoani Dodoma, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Shemdoe amesema kuwa katika haya maonyesho kuna teknolojia nzuri sana ya ufugaji na uvuvi kwa hiyo wafugaji na wavuvi wote waje kuchukua teknolojia hii ili kuboresha mifugo yao. "mnakumbuka Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa jana alisema  maana halisi ya haya maonesho ni kwamba wakulima waje kuchukua teknolojia" amesema Prof. Shemdoe Aidha, Prof. Shemdoe alisema haya maonesho ya nanenane ni kwa mara ya kwanza yanaadhimishwa kimataifa hapa mkoani Dodoma na ameweza kutembelea mabanda mbalimbali ya mifugo na uvuvi pamoja na kilimo ikiwa na sehemu ya vipando. Vilevile Prof....

MAJALIWA ARIDHISHWA NA NANENANE DODOMA

Picha
Na. Stanley Brayton Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo na mikoa ya Dodoma na Singida imefanya maajabu ya kipekee katika maonesho ya nanenane ya mwaka 2024 ikiwa tofauti na miaka mingine ya maonesho hayo kwa kuboresha zaidi miundombinu na teknolojia mpya na za kisasa. Akizungumza, leo Agosti 1, 2024 mkoani Dodoma katika Ufunguzi wa Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa Kanda ya Kati - Dodoma, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Kilimo ikishirikiana na menejimenti ya mkoa wa Dodoma na Singida, zimefanya vizuri katika maandalizi ya nanenane kwa mwaka 2024 na ameridhishwa na maandalizi ya maonesho hayo. "mwaka huu Wizara zetu na mikoa ya Dodoma na Singida, zimefanya maajabu makubwa hapa viwanja vya nanenane Nzuguni, hii ni hatua kubwa sana inayohitaji pongezi toka kwenu kwa sababu hii imevunja rekodi ya maonesho yote ya miaka mingine." amesema Mhe. Majaliwa Aidh...