Nav bar

Jumanne, 6 Agosti 2024

WATAALAMU WAASWA KUPELEKA TEKNOLOJIA YA MIFUGO NA UVUVI VIJIJINI

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule amewahasa wataalamu wa mifugo na uvuvi kupelekea na kufundisha teknolojia ya mifugo vijijini ili kuwapa wafugaji elimu ya kutosha kuhusu ufugaji wa kisasa kwa lengo la kuleta tija katika sekta hiyo.

Akizungumza, leo Agosti 4, 2024 mkoani Dodoma alipotembelea kwenye Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa yanayofanyika Kitaifa mkoani Dodoma katika mabanda ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Senyamule amesema wataalamu wahakikishe teknolojia hii inawafikia wadau wote wa mifugo na uvuvi, ususani maeneo ya vijijini.

"wataalamu wachukue hatua ya kwenda kwenye makundi ya wafugaji ili kwenda kuwaelimisha kuhusu teknolojia mpya ya ufugaji na kuhakikisha inawafikia" amesema Mhe. Senyamule

Aidha, Mhe. Senyamule alisema serikali ya awamu ya sita ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanya mapinduzi makubwa sana katika sekta ya Mifugo na Uvuvi kwani ameshuhudia teknolojia mbalimbali na nzuri katika mabanda ya Mifugo na Uvuvi.

Mhe. Senyamule alisema ata sekta binafsi pia wamepokea mabadiriko hayo ya kiteknolojia, ususani upande wa vijana wa Jenga Kesho iliyo Bora (BBT) ambao wanatumia teknolojia hizi kama ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba.

Vilevile Mhe. Senyamule ametoa wito kwa wadau wote wa Mifugo na Uvuvi  kutumia fursa hii ya maonesho haya ya nanenane ili kuweza kujifunza na kupata ufahamua juu ya teknolojia hii ya mifugo na uvuvi.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni