MTAKA AKOSHWA NA KAZI ZA WIZARA NANENANE MBEYA

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka amepongeza kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi na wadau wake kupitia maonesho ya mwaka huu ya  kimataifa ya Kilimo (NaneNane) kwa upande wa kanda ya Nyanda za Juu kusini yanayoendelea mkoani Mbeya.

                   Mhe. Mtaka ametoa pongezi hizo mara baada ya kufika kwenye mabanda ya Wizara hiyo                       ambapo alioneshwa kuvutiwa zaidi na bidhaa ya viatu vinavyotengenezwa kutokana na                            ngozi inayozalishwa hapa nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) kanda ya nyanda za juu kusini ambaye pia ni Mratibu wa maonesho hayo kwenye kanda hiyo Bw.Edwin Chang'a amemueleza Mhe. Mtaka kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepeleka teknolojia mbalimbali katika maonesho hayo ikiwa ni pamoja na zile zinazohusu ufugaji bora wa ng'ombe bora wa maziwa na nyama na aina mbalimbali za malisho ya Mifugo.

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

WATAALAMU WATAKIWA KUKUSANYA TAKWIMU SAHIHI ZA KITAFITI

UTEKELEZAJI WA UFUGAJI SAMAKI KWA VIZIMBA WAANZA ZIWA TANGANYIKA

TANZANIA DAIRY BOARD