Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2024

WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI ZA MIRADI MBALIMBALI YA UJENZI WAPEWA MIKATABA

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe  (kushoto) akiongea na sehemu ya wakandarasi walioshinda zabuni za miradi mbalimbali ya ujenzi ikiwemo ya minada na  majengo  kwenye  kampasi za LITA  (hawapo pichani) ambapo  amewasisitiza wakandarasi hao kutekeleza miradi  kwa wakati, kuwasiliana kwa haraka pindi inapobidi na ushirikishwaji wa karibu wa viongozi wa kisiasa kwenye maeneo ya miradi, kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa NBC Jijini Dodoma  (24.1.2024) kulia ni Naibu katibu Mkuu (Mifugo) Prof. Daniel Mushi. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (katikati) akisaini mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa soko la upili lililopo kishapu mkoani Shinyanga,  Handeni mkoani Tanga na Nzega mkoani Tabora na mwakilishi wa kampuni ya MACEA Construction Ltd, Bw. Godlove Gandye (kushoto) kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo) Prof. Daniel Mushi (24.01.2024) Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe ...

ULEGA: TANGAZENI VITALU KWA AJILI YA UWEKEZAJI

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewaagiza Naibu Katibu Mkuu, Sekta ya Mifugo, Prof. Daniel Mushi na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera kuhakikisha kuwa maeneo yote yaliyopo katika Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) mkoani Kagera ambayo hayana mgogoro yatangazwe kwa ajili ya uwekezaji. Ulega ametoa maelekezo hayo wakati wa kikao chake na Viongozi mbalimbali wa   Mkoa wa Kagera kilichofanyika leo Januari 22, 2024 chenye lengo la kumaliza migogoro iliyopo baina ya wananchi na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO). Amesema maeneo ambayo yameshapimwa na ambayo hayana mgogoro yatangazwe ili wawekezaji wenye uwezo waweze kupewa kwa ajili ya kufanya ufugaji wenye tija. Sambamba na hayo amewataka Wataalamu kurejea upya kwenye maeneo yote ambayo yameonekana yana migogoro ili kutatua changamoto zilizopo na kuwezesha maeneo hayo yaweze kuendelezwa na wawekezaji wenye uwezo. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega(kulia) akiteta jambo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mh...

WAZIRI ULEGA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA POLAND

Picha
Leo Januari 18, 2024, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amekutana na Wawekezaji kutoka Kampuni ya Uwekezaji ya Contractus ya nchini Poland ambao wameonesha nia ya kufanya uwekezaji kwenye tasnia ya Maziwa hapa nchini. Wawekezaji hao ambao ni Makamu Mwenyekiti wa Kampuni Contractus, Bw. Witold Karczewski na Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara ya Poland ambaye pia ni Meneja Mauzo wa Kampuni, Bw. Adam Borawski wameonesha nia ya kuingia ubia na Serikali ya Tanzania Kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuleta telnolojia ya kisasa ya kupoza maziwa katika vituo mbalimbali vya kukusanyia maziwa nchini. Nia yao kuanzia mwaka 2024/ 2025 kuanza uwekezaji huo ambapo wataanza na vituo 500 nchi nzima vyenye uwezo wa kukusanya kati ya lita 2000 hadi 6000 kwa siku. Uwekezaji huo unatarajiwa   kuongeza ukusanyaji wa lita takribani milioni moja za maziwa kwa siku hapa nchini. Aidha, mpango huo unaotarajiwa kuwa wa miaka 2 unakadiriwa kugharimu TZS. Bilioni 175, na inakus...

DC NGUBIAGAI ASISITIZA MAPAMBANO DHIDI YA UVUVI HARAMU

Picha
◾ Aipa Kongole Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia zoezi la Uhakiki wa Vikundi vya Wavuvi, Wakuzaji viumbe maji. Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai ameiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuziongezea nguvu timu za Doria baharini zilizopo wilayani humo ili ziweze kuendelea kupambana na Uvuvi haramu. Mhe. Ngubiagai amesema hayo baada ya kupokea timu ya wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliyofika Wilayani hapo kwa ajili ya zoezi la uhakiki wa taarifa za vikundi vya Wavuvi na wakuzaji viumbe maji Januari 17, 2023. " Jitihada hizi kubwa za kuwawezesha Wavuvi zitakuwa na maana kubwa zaidi kama tutahakikisha rasilimali za bahari zinapatikana kwa wingi na hili litawezekana kama tuweka mkazo na nguvu kwenye kupambana na uvuvi haramu ukanda huu wa bahari" Amesema Mhe. Ngubiagai. Mhe. Ngubiagai amedokeza kuwa licha ya Wilaya yake kuendelea na doria ya kupambana na changamoto hiyo ikiwa ni pamoja na kukagua nyenzo zinazotumiwa na wavuvi hao bado nguvu waliyona...

PWANI IPO TAYARI KUTEKELEZA BBT-LIFE-MCHATTA

Picha
Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Bw. Rashid Mchatta amekutana na ujumbe kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi upande wa sekta ya Mifugo Januari 15, 2024 na kufanya nao mazungumzo   kuhusu   namna ya kutekeleza mradi wa "Jenga kesho iliyo bora kwa wajasiriamali wanawake na Vijana (BBT-LIFE) kwa Mkoani humo. Akiongoza kikao hicho Bw. Mchatta ameipongeza na kuishukuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kupeleka programu hiyo mkoani kwake ambapo ameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha wakati wote wa utekelezaji wake. "Tunatambua tija kubwa watakayoipata vijana hawa na wanawake watakaofanikiwa kuchaguliwa kuingia kwenye programu hii hivyo niwashukuru sana kwa kuuleta mpango huu hapa Pwani" Amesema Bw. Mchatta. Akizungumza wakati wa kikao hicho  Mkurugenzi msaidizi  wa utafiti na Mafunzo kutoka Wizara ya mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt Hassan Mrutu  amesema kuwa  utekelezaji huo umewalenga vijana na wanawake katika  suala zima la Ufugaji wa kibiashara ambapo jumla ya vija...

MNYETI: “MAAFISA MIFUGO NENDENI KWA WAFUGAJI, ACHENI KUWA WAKUSANYA MAPATO.”

Picha
  Na. Edward Kondela Maafisa mifugo nchini wametakiwa kufanya kazi za udaktari wa mifugo walizosomea na kuwatembelea wafugaji badala ya kuwa wakusanya mapato wa halmashauri. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amebainisha hayo (15.01.2024) mjini Dodoma wakati akizindua Baraza la Veterinari Tanzania awamu ya sita baada ya baraza hilo kupata wajumbe. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa baraza hilo Mhe. Mnyeti amesema baadhi ya maafisa mifugo wamekuwa wakijikita zaidi kwenye kukusanya mapato ya halmashauri minadani badala ya kuwatembelea wafugaji ili kujua matatizo yao. “Maafisa mifugo kwenye halmashauri wanajifanya watumishi wa halmashauri kwa ajili ya kukusanya mapato kwenye minada kukusanya ushuru wa ng’ombe badala ya kufanya kazi za udaktari na kuwatembelea wafugaji.” Amesema Mhe. Mnyeti Aidha, amelitaka Baraza la Veterinari Tanzania kuhakikisha linachukua hatua zaidi kwa maafisa mifugo ambao wamekuwa wakifanya kazi kinyume na maadili pamoja na kuwapati...

MAJONGOO BAHARI, MWANI, KAA NI BIASHARA KUBWA”

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewahimiza wananchi wanaoishi Mtwara na maeneo mengine ya ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi kuchangamkia fursa ya ufugaji   wa Majongoo Bahari, Kaa, Kambakochi pamoja na kufanya kilimo cha Mwani kwa sababu mazao hayo yanahitajika sana katika nchi za Asia hususan China. Waziri Ulega ametoa rai hiyo wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji cha Ruvula kinachojengwa Msimbati, mkoani Mtwara Januari 14, 2024. “Mahitahi ya Majongoo Bahari, Kaa, Mwani, Kambakochi na Mwatiko ni makubwa katika nchi za Asia hasa china, hivyo ni lazima tucheze na fursa tulizonazo ili tuweze kufanikiwa na ndio maana serikali inatoa elimu kuwawezesha wananchi hususan vijana na kinamama kufanya shughuli hizo ili wauze nje ya nchi wajipatie kipato”, alisema Ulega Halikadhalika, aliwahimiza wananchi kujipanga vyema ikiwemo kuunda vikundi ili serikali iweze kuwatambua na kuwapatia mikopo ya vifaa vya kisasa kwa aj...

TANZANIA, RWANDA KUSHIRIKIANA KUKUZA TASNIA YA MAZIWA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega na Waziri wa Kilimo, Maliasili, na Mifugo wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. James Kabarebe wamesaini hati ya makubaliano ya kushirikiana kuendeleza tasnia ya maziwa baina ya nchi hizo mbili. Tukio hilo la utiaji saini limefanyika Visiwani Zanzibar   Januari 12, 2024 sambamba na Sherehe za Kutimiza Miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Akizungumza katika tukio hilo, Waziri Ulega alisema kuwa ushirikiano huo ambao umekusudia kuendeleza viwanda vya usindikaji wa maziwa utasaidia kuongeza uzalishaji wa maziwa wa nchi hizo mbili jambo ambalo litapelekea kupatikana kwa ajira, usalama wa chakula na kukuza uchumi wa kaya na mtu mmoja mmoja kupitia mnyororo wa thamani wa maziwa. Alisema kuwa mpaka sasa bado nchi inaagiza maziwa mengi kutoka nje ya nchi, lakini kupitia ushirikiano huo ana uhakika uzalishaji wa maziwa nchini utaongezeka na kuchechemua biashara baina ya nchi hizo mbili. “Tanzania na Rwanda tumeamua kushirikiana katika mambo...

WAFUGAJI JONGOO BAHARI MTWARA WAASWA KUFUATA TARATIBU

Picha
  Mkurugenzi Msaidizi wa Ukuzaji Viumbe Maji upande wa mazao ya bahari Dkt. Hamis Nikuli amewataka wafugaji jongoo bahari mkoani Mtwara kufuata sheria na taratibu za ufugaji wa zao hilo. Dkt. Nikuli ameyasema hayo wakati wa zoezi la ujazaji wa dodoso linalohusu taarifa za wavuvi na wakuzaji viumbe maji   lililofanyika Januari 12, 2024 kwenye kampasi ya Chuo cha Mafunzo ya Uvuvi (FETA) iliyopo eneo la Mikindani mkoani humo. "Tunahamasisha sana ufugaji wa jongoo bahari kwa sababu wale waliopo kwenye maji ya asili kwa huku Tanzania bara hawaruhusiwi kuvuliwa kwa sasa lakini ni lazima kila mtu au kikundi kifuate taratibu zilizopo kwenye kibali chake na isitokee mmoja wenu akatumia kibali cha mwenzie kuvuna jongoo hao" Amesema Dkt. Nikuli. Dkt. Nikuli ameongeza kuwa ni lazima wafugaji jongoo bahari wote waliopo mkoani humo kuhakikisha wanatoa taarifa sahihi za idadi ya jongoo bahari wanaowafuga na kuwa waaminifu pindi wanapopewa kibali cha kuvuna ili wavune idadi waliyoidh...

UTEKELEZAJI WA UFUGAJI SAMAKI KWA VIZIMBA WAANZA ZIWA TANGANYIKA

Picha
Na, Edward Kondela Serikali imeanza utekelezaji wa ufugaji samaki kwa njia ya vizimba katika Ziwa Tanganyika baada ya mpango huo kuonesha mafanikio makubwa katika Ziwa Victoria. Akizungumza (11.01.2024) katika Mwalo wa Kasanga uliopo Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amesema tayari wizara imeanza kutoa elimu kwa wavuvi wa ukanda wa Ziwa Tanganyika kabla ya kufikisha vizimba hivyo na mbegu bora za samaki. Mhe.Mnyeti ameongeza kuwa kwa sasa serikali imetenga Shilingi Bilioni 20 kwa ajili uwekaji vizimba katika Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa sababu ufugaji wa samaki unakua kwa kasi maeneo mbalimbali duniani kutokana na upungufu wa samaki waliopo kwenye maji ya asili yakiwemo mabonde, maziwa, mito na bahari kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya uharibifu wa mazingira, ongezeko la watu na uharibifu wa mazalia ya samaki. Ameongeza kuwa ili kunusuru upungufu wa samaki katika masoko ya ndani na nje ya nchi serikali imeamua ...

RAS MWANZA AIPONGEZA WIZARA KWA KUWA NA MKAKATI WENYE TIJA KWA KUWAJENGEA VIJANA KUJIAJIRI

Picha
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuweka mkakati wenye tija kwa vijana kwa kuwajengea kuweza kujiajiri kwa kutoa mikopo isiyo na riba ya pembejeo za vizimba, chakula cha samaki na vifaranga vya samaki kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo TADB. Balandya ameyasema hayo ofisini kwake mara baada ya kupokea ugeni   kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ukiongozwa na Afisa Uvuvi Mkuu Bi. Mkomanile Mahundi na kusema ufugaji kwenye vizimba utasaidia sana katika uzalishaji wa samaki. Katika mazungumzo pia alitoa ushauri mpango huo wa ufugaji kwa njia ya vizimba ufanyike kwa awamu kutokana na wingi wa vikundi husika kutoka mikoa ya kanda ya ziwa. "Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Samia imedhamiria kuwainua kundi la vijana kimaendeleo, mpango huu wa ufugaji wa kisasa wa samaki wataalamu kutoka wizarani ukiwawekea mazingira mazuri ya kazi utazidi kuwa na tija kwao kiuchumi", amefafanua Mtendaji huyo wa Mkoa wak...

ZIWA TANGANYIKA KUPUMZISHWA, SERIKALI YAPIGIA CHAPUO UVUVI WA VIZIMBA

Picha
  Na. Edward Kondela Serikali yaazimia kupumzisha shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika kwa kipindi cha miezi mitatu kwa miaka mitatu mfululizo ili kuongeza mazalia ya samaki na kuhamasisha ufugaji samaki kwa njia ya vizimba katika ziwa hilo. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti amebainisha hayo (10.01.2024) kwa nyakati tofauti wakati alipokuwa akiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Katavi na wadau wa uvuvi katika mkoa huo wakiwemo wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi katika Mwalo wa Ikola uliopo katika Wilaya ya Tanganyika. Naibu Waziri Mnyeti amesema serikali imeazimia kupumzisha shughuli za uvuvi katika Ziwa Tanganyika kuanzia tarehe 15 Mei hadi tarehe 15 Agosti Mwaka 2024 ikiwa ni utekelezaji wa Mkataba wa Kikanda wa Usimamizi wa Uvuvi endelevu katika ziwa hilo na bonde lake ambapo nchi wanachama wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika kwa maana ya Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Tanzania   na Zambia zilitia saini mkataba huo Tar...

ZIWA TANGANYIKA KUPUMZISHWA ILI KUWEZESHA SAMAKI KUZALIANA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ametangaza mpango wa Serikali wa kupumzisha  shughuli za uvuvi katika ziwa Tanganyika kwa miezi mitatu ili kuwezesha samaki kuzaliana na kuongeza tija kwa wavuvi wanaofanya shughuli zao ziwani humo. Waziri Ulega  ametoa kauli ya serikali kwa nyakati tofauti ambapo awali alitoa kauli hiyo akizungumza na wadau wa uvuvi kwenye ofisi ya Mkuu wa mkoa Kigoma na baadaye kuzungumza na wananchi na wadau wanaofanya shughuli za uvuvi kwenye Mwalo wa Katonga Manispaa ya Kigoma Januari 9, 2024. Akiwa kwenye kikao cha ndani na wadau wa uvuvi Waziri Ulega alisema kuwa utekelezaji wa mpango huo utaanza rasmi Mei 15 hadi Agosti 15 mwaka huu na hiyo ikiwa ni Utekelezaji wa Mkataba wa Kikanda wa Nchi Wanachama wa Mamlaka ya Ziwa Tanganyika unaoweka hatua na taratibu za usimamizi endelevu wa shughuli za uvuvi katika ziwa hilo. Akieleza sababu ya maamuzi hayo alisema ni kutokana na utafiti kubainisha kuwa kumekuwe...