Nav bar

Jumanne, 23 Januari 2024

ULEGA: TANGAZENI VITALU KWA AJILI YA UWEKEZAJI


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewaagiza Naibu Katibu Mkuu, Sekta ya Mifugo, Prof. Daniel Mushi na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera kuhakikisha kuwa maeneo yote yaliyopo katika Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) mkoani Kagera ambayo hayana mgogoro yatangazwe kwa ajili ya uwekezaji.

Ulega ametoa maelekezo hayo wakati wa kikao chake na Viongozi mbalimbali wa  Mkoa wa Kagera kilichofanyika leo Januari 22, 2024 chenye lengo la kumaliza migogoro iliyopo baina ya wananchi na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO).

Amesema maeneo ambayo yameshapimwa na ambayo hayana mgogoro yatangazwe ili wawekezaji wenye uwezo waweze kupewa kwa ajili ya kufanya ufugaji wenye tija.

Sambamba na hayo amewataka Wataalamu kurejea upya kwenye maeneo yote ambayo yameonekana yana migogoro ili kutatua changamoto zilizopo na kuwezesha maeneo hayo yaweze kuendelezwa na wawekezaji wenye uwezo.



Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega(kulia) akiteta jambo na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe. Erasto Sima wakati wa kikao chake na Viongozi mbalimbali wa  Mkoa wa Kagera kilichofanyika leo Januari 22, 2024 chenye lengo la kumaliza migogoro iliyopo baina ya wananchi na Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO).


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni