Nav bar

Jumatano, 24 Januari 2024

WAKANDARASI WALIOSHINDA ZABUNI ZA MIRADI MBALIMBALI YA UJENZI WAPEWA MIKATABA

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe  (kushoto) akiongea na sehemu ya wakandarasi walioshinda zabuni za miradi mbalimbali ya ujenzi ikiwemo ya minada na  majengo  kwenye  kampasi za LITA  (hawapo pichani) ambapo  amewasisitiza wakandarasi hao kutekeleza miradi  kwa wakati, kuwasiliana kwa haraka pindi inapobidi na ushirikishwaji wa karibu wa viongozi wa kisiasa kwenye maeneo ya miradi, kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa NBC Jijini Dodoma  (24.1.2024) kulia ni Naibu katibu Mkuu (Mifugo) Prof. Daniel Mushi.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe (katikati) akisaini mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa soko la upili lililopo kishapu mkoani Shinyanga,  Handeni mkoani Tanga na Nzega mkoani Tabora na mwakilishi wa kampuni ya MACEA Construction Ltd, Bw. Godlove Gandye (kushoto) kulia ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo) Prof. Daniel Mushi (24.01.2024)

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akikabidhi mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa soko la upili la Luaguza lililopo Lushoto mkoani Tanga kwa  Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Maruu RPK Group Ltd , Bw. Rhodes Kimambo wakati wa kikao kifupi cha makabidhiano kilichofanyika kwenye ukumbi wa NBC Jijini Dodoma (24.1.2024)

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Mafunzo ya Mifugo (LITA), Dkt. Pius Mwambene (kushoto) akikabidhi mkataba wa makubaliano ya ujenzi wa ukumbi mmoja wa miadhara wenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 100 na ujenzi wa hostel moja yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 150 kwa Arch. Eliah Mpembeni kutoka kampuni ya KADIVA, Mkataba huo umesainiwa kwenye ukumbi wa NBC Jijini Dodoma (24.01.2024)


 Sehemu ya washiriki wa kikao cha makabidhiano ya mkataba wa makubaliano wa   ujenzi miradi ya maendeleo kilichofanyika kwenye ukumbi wa NBC Jijini Dodoma  (24.1.2024)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni