Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2022

UJENZI WA BANDARI YA UVUVI MBIONI KUANZA

Picha
Na Saja Kigumbe Serikali imeweka wazi kuwa mradi   wa ujenzi wa bandari ya uvuvi   unatarajia kuanza muda wowote kuanzia sasa baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu. Bandari hiyo ambayo inatarajiwa kujengwa Wilayani Kilwa Masoko, Mkoani Lindi inatarajiwa kuwa chachu ya kuimarika kwa uchumi wa buluu nchini. Hayo yalibainishwa Machi 16, 2022 Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti   na Mafunzo ya uvuvi, Dkt. Erastus Mosha wakati wa mkutano wa wadau uliolenga kupitia rasimu ya taarifa ya upembuzi yakinifu wa mradi huo wa kimkakati. Alisema bandari hiyo itaiwezesha nchi kupata mapato kupitia   meli za uvuvi na bidhaa zinazotokana na uvuvi zitauzwa hapa ndani   na nje ya nchi. Dkt. Mosha alisema Serikali tayari imetenga fedha za kufanikisha ujenzi huo ambao unatarajiwa kufanyika katika kipindi cha miaka mitatu kuanzia sasa. “Tanzania hatujawahi kuwa na bandari ya uvuvi na hili limesababisha tumeshindwa kunufaika vya kutosha kupitia ras...

ULINZI WA RASILIMALI ZA UVUVI KUSTAWISHA UCHUMI WA BULUU - ULEGA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewataka wataalam, wavuvi na wafugaji wa viumbe maji kulinda rasilimali za uvuvi ili kustawisha uchumi wa buluu. Naibu Waziri Ulega ametoa kauli hiyo (07.03.2022) wakati alipokuwa akizungumza kwenye uzinduzi wa mwaka wa kimataifa wa uvuvi mdogo na ukuzaji viumbe maji – IYAFA 2022 uliofanyika kwenye uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza. Amesema upo umuhimu wa kuanzisha chombo cha ulinzi wa rasiliamli za uvuvi chenye wataalam wa uvuvi na ulinzi ili kuhakikisha rasilimali hizo zinalindwa. Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan imeweka malengo ya kuhakikisha rasilimali za uvuvi zinalindwa ili kustawisha uchumi wa buluu utakaosaidia kukuza pato la wavuvi, wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi na taifa kwa ujumla. Serikali kwa muda mrefu imekuwa ikisikia changamoto nyingi zinazowakabili wavuvi na rasilimali za uvuvi na kwamba sasa ni wakati muafaka wa kukabiliana na changamoto hizo.Hivyo aliwata...

SERIKALI YADHAMIRIA KUWAINUA WAVUVI WADOGO

Picha
Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Emmanuel Bulayi amesema Serikali imedhamiria   kuboresha Sekta ya Uvuvi   kwa kuwawezesha wavuvi wadogo wakiwemo wanawake ili waweze kunufaika na rasilimali za uvuvi zilizopo nchini. Aliyasema hayo wakati wa hafla ya mashindano ya mbio za kuendesha mitumbwi kwa wavuvi wanawake kutoka mikoa ya Kanda ya ziwa iliyofanyika jijini Mwanza Machi 6, 2022. “ Tumedhamiria kuwainua wavuvi wadogo na ndio maana tumeandaa mwongozo wa hiari na mpango mkakati kwa ajili ya kuendeleza uvuvi, rasilimali na mazao yake hapa nchini,” alisema Bulayi Alisema lengo la Serikali la kuandaa Mwongozo huo kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) ni kukuza mchango wa sekta ya uvuvi mdogo kwa maslahi mapana ya wananchi kiuchumi, kijamii na kimazingira. Aliongeza kwa kusema kuwa mwongozo huo ambao umekubaliwa na Jumuiya ya Kimataifa, unaamsha    misingi ya kusimamia na kuendeleza uvuvi mdo...

RAIS SAMIA KUWAINUA WANANCHI KUPITIA UCHUMI WA BULUU-ULEGA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Lindi Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amejipanga kuwainua wananchi kupitia fursa zinazopatikana katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi ili waweze kukuza kipato chao na kuchangia katika pato la taifa. Ulega alitoa kauli hiyo Machi 1, 2022 alipotembelea vikundi vya ukulima wa mwani, ufugaji samaki na Kambakochi kwa lengo la kuhamasisha wananchi kuchangamkia fursa za ukuzaji viumbe maji zilizopo katika Mkoa wa Lindi. “Nia ya Rais wetu, Mama Samia ni kuhakikisha mnakuwa na kipato kizuri wakati wote, mzunguko wenu wa kipato uimarike kupitia fursa hizi zinazopatikana katika uchumi wa buluu, uchumi wenu ukiimarika umasikini utapungua lakini vilevile mtaweza sasa kuchangia mapato katika Halmashauri zetu na taifa kwa ujumla”,alisema Mhe. Ulega Alisema nia ya serikali ni kutaka kuwawezesha wananchi kujiunga katika vikundi ili waweze kukopesheka kirahisi huku akimue...

WASAIDIENI WANANCHI WANUFAIKE KUPITIA UCHUMI WA BULUU - ULEGA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Lindi Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewataka Wataalam na Watendaji wa Serikali katika Mikoa ya Lindi na Mtwara kuwahamasisha Wananchi kutumia fursa zilizopo katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi hususan ufugaji wa   Majongoo Bahari, Kaa na Ukulima wa Mwani ili waweze kukuza kipato chao. Naibu Waziri Ulega alitoa agizo hilo katika kikao kazi cha mkakati wa Kampeni ya Kuhamasisha Shughuli za Ukuzaji Viumbe Maji Bahari kwa Wataalam wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kilichofanyika Mkoani Lindi Februari 28, 2022. "Uchumi wa buluu ni moja ya vipaumbele vya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake ya Awamu ya Sita, lakini namna gani tumetumia fursa hizo kulingana na uhitaji wa soko ili kuwainua watu katika uchumi wao na Taifa letu ndio kazi yetu sisi wataalam tuliopo hapa", alisema Mhe. Ulega Alisema kuwa wataalam hao kuanzia Maafisa Ardhi, Maafisa Maendeleo na Ushirika, Maafisa Uvuvi na Maafisa Biashara wakishirikiana vyema ...

ULEGA AZIAGIZA HALMASHAURI KUWEZESHA VIKUNDI VYA USHIRIKA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega ameziagiza Halmashauri za  Wilaya hususan zilizopo katika Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi kutoa asilimia 10 zinazotengwa na Serikali kwa ajili ya kuwezesha vijana na kuwapa vikundi vya ushirika vya Wafugaji jongoo bahari, kaa na Wakulima wa Mwani ili waweze kuongeza nguvu na kuendeleza shughuli zao za uzalishaji. Ulega alitoa maelekezo hayo alipokuwa akiongea kwa nyakati tofauti na kikundi cha ufugaji jongoo bahari na kikundi cha wakulima wa mwani alipowatembelea kukagua shughuli wanazofanya Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani Februari 25, 2022. Wakati akiongea na wanavikundi hao, Naibu Waziri Ulega alitumia nafasi hiyo kufikisha ujumbe kwa Wakurugenzi wa Halmashauri kupitia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo, Bw. Shauri Selenda kuwa asilimia 10 zinazotengwa na Serikali kwa ajili ya kuwezesha vijana  wapewe wanavikundi hao wanaofuga jongoo bahari, kaa na kilimo cha Mwani ili waweze kufanya uzalishaji mkubwa ...

ULEGA AHAMASISHA MIKOA YA PWANI KUCHANGAMKIA FURSA UCHUMI WA BULUU

Picha
Na Mbaraka Kambona, Pwani Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amewahimiza Viongozi wa Mikoa iliyopo Pwani ya Bahari ya Hindi hususan Pwani na Dar es Salaam kuhamasisha wananchi wao kujiunga katika vikundi vya ushirika ili wawezeshwe na serikali kunufaika na fursa zinazopatikana katika uchumi wa buluu ikiwemo ufugaji wa kaa, majongoo bahari na kilimo cha mwani. Ulega alitoa rai hiyo katika kikao kazi cha mkakati wa kampeni ya kuhamasisha shughuli za ukuzaji viumbe maji bahari kwa viongozi na wataalam wa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam kilichofanyika Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani Februari 24, 2022. Alisema ili wananchi waweze kunufaika na fursa hizo, suala la kuwa na ushirika ni muhimu sana huku akihimiza kila halmashauri kuhamasisha wananchi kujiunga katika vikundi na kuunda ushirika katika maeneo yao. “Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hotuba yake aliyoitoa Januari 7, 2022 katika kilele cha Matembezi ya Miaka 58 ...

NZUNDA ASISITIZA WATALAAM WA MIFUGO KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw.Tixon Nzunda amesisitiza watalaam wa Mifugo kufanya kazi zao kwa Weledi ili kusaidia Sekta ya Mifugo kusonga mbele. Hayo ameyasema leo 23 feb 2022 alipokuwa akifungua kikao cha Watalaam wa Mifugo na Uvuvi kanda za nyanda za juu kusini na kusini Magharibi, mkoni Katavi. "Watalaam fanyeni kazi zenu kwa Weledi ili wafugaji hawa wafaidike na huduma zenu, kila mtalaam awe na Register, ili mwisho wa siku aulizwe amehudumia wafugaji wangapi katika halmashauri yake, kata au kijiji.Lakini kama hiyo haitoshi kwa mwaka fedha 2023/2024 tutakuwa na mkataba wa utendaji kazi ili kupima utendaji kazi wa watalaam wetu" Alisema Nzunda. Aidha, Nzunda amesema kuwa   Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kuwa na Mifugo mingi, asilimia 1.4 ya ng'ombe wote wako Tanzania na nchi yetu   ni ya pili barani Africa kwa uwingi wa Mifugo ikitanguliwa na Ethiopia, lakini bado tija hiyo ya kuwa na mifugo mingi kiasi hicho haionekani. "Pamoja na ku...

KAIMU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO DKT. CHARLES MHINA AKIKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA JENGO LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Charles Mhina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), (katikati), akitoa maagizo kwa mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa jengo la makao makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na mshauri elekezi wa mradi huo Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), kuhakikisha wanampatia taarifa ya kila wiki juu ya maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Kulia kwa kaimu katibu mkuu ni mbunifu wa majengo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Humphrey Killo anayesimamia mradi huo na kushoto kwa kaimu katibu mkuu ni mbunifu wa majengo kutoka TBA Bw. Weja Ng’olo. (23.02.2022) Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Charles Mhina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), (watatu kutoka kulia), akipatiwa maelezo ya ujenzi wa mradi wa jengo la makao makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoka kwa mmoja wa wasimamizi wa m...

NZUNDA ASISITIZA WAWEKEZAJI KUFUATA TARATIBU NA SHERIA YA MIKATABA YAO.

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw.Tixon Nzunda amesisitiza wawekezaji wa Ranchi ya Taifa ya kalambo kufuata taratibu na sheria ya mikataba waliyoingia na   Ranchi hiyo. Hayo ameyasema   Februari 22, 2022 alipotembelea Ranchi hiyo iliyopo mkoani Rukwa na kupata fursa ya kutembelea baadhi ya Vitalu vya Kalambo Ranchi na kushuhudio ufugaji bora unaofanyika katika Ranchi hiyo.   "Fuateni taratibu mlizokubaliana na Ranchi katika kuendesha shughuli zenu katika vitalu vyenu mlivyopangishwa, kuanzia Vitalu vya muda mrefu mpaka vile vya Muda mfupi, Mikataba yenu inaelekeza mlime malisho kwenye vitalu vyenu,mjenge majosho, mchimbe Visima, nani kati yenu ametekeleza hayo??"Aliuliza Nzunda. Aidha, Katibu Mkuu Mifugo Bw.Tixon Nzunda amekemea vikali wawekezaji ambao hawataki kuchanja mifugo yao, kuogesha au wanachanja mifugo michache na baadhi kuiacha bila kuchanja, amesema kwa kufanya hivyo mifugo hiyo bado itaendelea kuambukizana magonjwa. "Tunataka vitalu ...

Waziri wa mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki watembelea Ofisi za National Service Projects Organization ya Misri na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Misri

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) (wa tatu kutoka kushoto) na ujumbe kutoka Tanzania wakiwa kwenye kikao kifupi na wenyeji wao wa Misri  mara baada ya kuwasili Nchini humo lengo likiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu na kukuza ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi. Februari 21, 2022. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kutoka kushoto) pamoja na ujumbe wake kutoka Tanzania walitembelea Ofisi za National Service Projects Organization ya Misri  na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Misri ukiongozwa na Naibu Waziri wa Ulinzi Jenerali Medhat El  Nahas, lengo likiwa ni pamoja na kueleza fursa za ushirikiano na uwekezaji zilizopo katika Sekta ya Uvuvi Nchini Tanzania. Februari 21,2022 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) (kushoto meza kuu ) akiwa kwenye  picha ya pamoja na  Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Taifa ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji Misri, Jenerali Eslam Attia Rayan, wakiwa na  ujumbe kutoka Tanzania na u...

IDARA TA DGLF YATEMBELEA KIJIJI CHA OLOLOSOKWANI KUONA ENEO LILILOPENDEKEZWA KWA AJILI YA UJENZI WA JOSHO.

Picha
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Dkt. Asimwe Rwiguza (wa kwanza kushoto) akiwa na Wataalam kutoka Sekta ya Mifugo na Uongozi wa Kijiji cha Ololosokwani wakati alipotembelea eneo lililopendekezwa kwa ajili ya ujenzi wa Josho. (15.02.2022) Baadhi ya wafugaji wa Kijiji katika vijiji vya Ololosokwani na Soitsambu wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha wakisikiliza maelezo ya Wataalam kutoka Sekta ya Mifugo wakati walipotembelea vijiji hivyo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uboreshaji wa Kosaafu za Mifugo, Udhibiti wa magonjwa ya mifugo na Maeneo ya Malisho. (15.02.2022) Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Dkt. Asimwe Rwiguza akiwasalimu wafugaji wa Kijiji cha Soitsambu wakati Wataalam wa Sekta ya Mifugo walipofika kijijini hapo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uboreshaji wa Kosaafu za Mifugo, Udhibiti wa magonjwa ya mifugo na Maeneo ya Malisho. (15.02.2022)  

SUMU KUVU TISHIO LA USUGU WA DAWA KWA BINADAMU NA MIFUGO

Picha
  Na. Edward Kondela Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) imesema katika mwaka ujao wa fedha 2022/2023 inatarajia kuongeza wigo wa kufanya vipimo vya ubora wa vyakula vya mifugo ili kubaini aina za sumu kuvu ambazo zinaweza kusababisha madhara ya kiafya kwa binadamu na mifugo. Mtendaji Mkuu wa TVLA Dkt. Stella Bitanyi amebainisha hayo ofisini kwake jijini Dar es Salaam, wakati wa zoezi la kuhakiki ubora wa vyakula vya mifugo vinavyozalishwa hapa nchini lililofanyika mwishoni mwa wiki, zoezi ambalo limefanywa katika wilaya za Temeke na Ubungo na wataalamu kutoka TVLA. Dkt. Bitanyi amesema wakala hiyo inatarajia pia kupima mabaki ya ‘antibiotic’ na dawa nyingine za mifugo ndani ya vyakula vya mifugo ili kuhakikisha ubora wa vyakula vya mifugo kwa kutokuwa na mabaki ya dawa ambazo zinaweza kusababisha usugu wa dawa kwa mifugo pamoja na binadamu atakayetumia mazao yanayotokana na mifugo hiyo. Katika hatua nyingine mtendaji mkuu huyo wa Wakala ya Maabara ya Veterina...