Nav bar

Jumanne, 1 Machi 2022

Waziri wa mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki watembelea Ofisi za National Service Projects Organization ya Misri na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Misri

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) (wa tatu kutoka kushoto) na ujumbe kutoka Tanzania wakiwa kwenye kikao kifupi na wenyeji wao wa Misri  mara baada ya kuwasili Nchini humo lengo likiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu na kukuza ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi. Februari 21, 2022.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kutoka kushoto) pamoja na ujumbe wake kutoka Tanzania walitembelea Ofisi za National Service Projects Organization ya Misri  na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka Misri ukiongozwa na Naibu Waziri wa Ulinzi Jenerali Medhat El  Nahas, lengo likiwa ni pamoja na kueleza fursa za ushirikiano na uwekezaji zilizopo katika Sekta ya Uvuvi Nchini Tanzania. Februari 21,2022

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) (kushoto meza kuu ) akiwa kwenye  picha ya pamoja na  Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Taifa ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji Misri, Jenerali Eslam Attia Rayan, wakiwa na  ujumbe kutoka Tanzania na ujumbe kutoka Misri wakati wa ziara rasmi nchini  humo, lengo likiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu na kukuza ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi. Februari 21, 2022.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto waliokaa) na Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Taifa ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji Misri  Jenerali Eslam Attia Rayan wakitia saini kwenye  hati ya makubaliano ya ushirikiano Kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) na Kampuni ya Taifa ya NCFA. Februari 21, 2022 nchini Misri, lengo likiwa ni kukuza ushirikiano na uwekezaji katika minyororo ya thamani ya uvuvi na ukuzaji viumbe maji pamoja na kukuza utaalam katika Sekta ya Uvuvi.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni