Nav bar

Jumatano, 2 Machi 2022

KAIMU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO DKT. CHARLES MHINA AKIKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA JENGO LA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Charles Mhina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), (katikati), akitoa maagizo kwa mkandarasi wa ujenzi wa mradi wa jengo la makao makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na mshauri elekezi wa mradi huo Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), kuhakikisha wanampatia taarifa ya kila wiki juu ya maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma. Kulia kwa kaimu katibu mkuu ni mbunifu wa majengo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Humphrey Killo anayesimamia mradi huo na kushoto kwa kaimu katibu mkuu ni mbunifu wa majengo kutoka TBA Bw. Weja Ng’olo. (23.02.2022)

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Charles Mhina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), (watatu kutoka kulia), akipatiwa maelezo ya ujenzi wa mradi wa jengo la makao makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoka kwa mmoja wa wasimamizi wa mradi huo unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma ambapo kaimu katibu mkuu huyo ameeleza kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo. (23.02.2022)

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Charles Mhina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), (katikati), akiwa ameambatana na baadhi ya watendaji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA) na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakati akikagua ujenzi wa mradi wa jengo la makao makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma baada ya kutoridhishwa na kasi ya ujenzi huo na kuagiza kuchukuliwa kwa hatua za haraka, ikiwemo ya muda wa kazi kuongezwa ili kukamilisha mradi huo katika muda wa miezi 24 kama ilivyoainishwa kwenye mkataba. (23.02.2022)

Muonekanao wa maendeleo ya ujenzi wa mradi wa jengo la makao makuu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, unaotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) pamoja na mshauri elekezi wa mradi huo Wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), ambapo Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Charles Mhina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), ametembelea na kukagua mradi huo na kukataa ombi la NHC la kuongezewa muda wa zaidi ya miezi 24 nje ya mkataba ili kutekeleza mradi na kuagiza kuongezwa kwa muda wa saa za kazi, uwepo wa wafanyakazi zaidi pamoja na vifaa vya kutosha kwa ajili ya ujenzi. (23.02.2022)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni