Nav bar

Jumanne, 1 Machi 2022

IDARA TA DGLF YATEMBELEA KIJIJI CHA OLOLOSOKWANI KUONA ENEO LILILOPENDEKEZWA KWA AJILI YA UJENZI WA JOSHO.

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Dkt. Asimwe Rwiguza (wa kwanza kushoto) akiwa na Wataalam kutoka Sekta ya Mifugo na Uongozi wa Kijiji cha Ololosokwani wakati alipotembelea eneo lililopendekezwa kwa ajili ya ujenzi wa Josho. (15.02.2022)

Baadhi ya wafugaji wa Kijiji katika vijiji vya Ololosokwani na Soitsambu wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha wakisikiliza maelezo ya Wataalam kutoka Sekta ya Mifugo wakati walipotembelea vijiji hivyo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uboreshaji wa Kosaafu za Mifugo, Udhibiti wa magonjwa ya mifugo na Maeneo ya Malisho. (15.02.2022)

Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Mifugo, Dkt. Asimwe Rwiguza akiwasalimu wafugaji wa Kijiji cha Soitsambu wakati Wataalam wa Sekta ya Mifugo walipofika kijijini hapo kwa lengo la kutoa elimu kuhusu uboreshaji wa Kosaafu za Mifugo, Udhibiti wa magonjwa ya mifugo na Maeneo ya Malisho. (15.02.2022)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni