Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2024

TALIRI WEST KILIMANJARO KUWA KITIVO CHA UBORA UZALISHAJI MBUZI, KONDOO.

Picha
◾ Ni kufuatia matokeo mazuri ya utekelezaji wa mradi wa ECF Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Daniel Mushi amesema kuwa Wizara yake inakusudia kukifanya kituo cha Utafiti wa Mifugo kanda ya Kaskazini cha West Kilimanjaro kuwa kitivo cha Ubora kwenye uzalishaji wa mbuzi na kondoo walioboreshwa kwa ajili ya kuwapa wafugaji nchini ili waweze kufuga kwa tija. Prof. Mushi amesema hayo leo Machi 05, 2024 baada ya kufika kwenye kituo hicho kilichopo chini ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) ambapo ameweka wazi nia ya Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuongeza kiwango cha nyama bora inayouzwa nje kupitia kituo hicho. "Kama mnavyotambua nchi yetu kwa sasa imeongeza kasi katika kusafirisha nyama nje ya nchi na zaidi ya asilimia 90 ya nyama tunayopeleka huko ni ya mbuzi na kondoo hivyo tuna kila sababu ya kuongeza uzalishaji wa wanyama hao" Ameongeza Prof. Mushi. Aidha Prof. Mushi amemuelekeza Mkurugenzi wa kituo hicho Dkt. Leonard Marw...

SERIKALI YATOA EKARI 1000 ZA RANCHI KWA WANANCHI MKOANI KILIMANJARO

Picha
 Pia Yawarasimishia ekari 200 walizokuwa wakimiliki awali kinyume na utaratibu. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewapa wananchi wa kijiji cha Kalimaji eneo lenye ukubwa wa ekari 1000 zilizokuwa zinamilikiwa na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) kituo cha West Kilimanjaro kilichopo kanda ya Kaskazini mkoani Kilimanjaro. Akikabidhi eneo hilo kwa kamati ya Usalama ya Mkoa huo leo Machi, 05, 2024 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Daniel Mushi amesema kuwa Wizara yake imeridhia kutoa eneo hilo na kurasimisha ekari 200 za awali zilizokuwa zikitwaliwa na wananchi hao kinyume na utaratibu na kufanya kijiji hicho kuwa na eneo lenye ukubwa wa ekari 1200. "Mhe. Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama sisi kama Wizara tumeridhia kutoa eneo hilo la sehemu ya kituo chetu cha Utafiti cha West Kilimanjaro na tunabariki taratibu zote za kuwamilikisha wananchi wa kijiji hicho ziendelee" Amesisitiza Prof. Mushi. ...

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO

Picha
Na. Edward Kondela Serikali imesema itahakikisha inachukua hatua ya kuwepo kwa taratibu maalum zilizo wazi kwenye biashara ya mabondo ya samaki ili kujiridhisha upatikanaji wake hadi kufika viwandani kwa ajili ya kuchakatwa. Akizungumza (05.03.2024) jijini Mwanza na wamiliki wa viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi katika jiji hilo, wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe, Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amesema serikali itahakikisha inaweka utaratibu ili kujiridhisha namna ya upatikanaji wa mabondo. Prof. Sheikh amebainisha hayo baada ya baadhi ya wamiliki wa viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi kulalamika kuwa baadhi ya wavuvi wamekuwa wakivua samaki ambao wako chini ya viwango vinavyotakiwa viwandani wakiwa na lengo la kuuza mabondo kwenye viwanda vya kuchakata mabondo hayo na kuharibu mazalia ya samaki. Ameongeza kuwa lazima kuwepo utaratibu maalum kujua upatikanaji wa mabondo hadi kufika kwenye viwanda kwa ajili uchaka...

TANZANIA YAKABIDHIWA BOTI KUDHIBITI UVUVI HARAMU

Picha
Na. Edward Kondela Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekabidhiwa boti mbili kutoka Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kufanya doria na kudhibiti uvuvi haramu ndani ya Ziwa Victoria. Akikabidhiwa boti hizo pamoja na injini tatu na redio maalum kwa ajili ya mawasiliano leo (04.03.2024) jijini Mwanza, Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amesema vifaa hivyo vitasaidia katika juhudi za serikali kulinda, kuendeleza na kukuza rasilimali za uvuvi ndani ya Ziwa Victoria na Tanzania kwa ujumla. Amesema anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya kukuza Sekta ya Uvuvi na kukuza mahusiano katika nchi tatu za Tanzania, Kenya na Uganda ambazo zinatumia Ziwa Victoria. Ameongeza kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha inalinda rasilimali za uvuvi huku akitaja hatua ambazo zimechukuliwa ikiwemo ya Rais Mhe. Dkt...

WAFUGAJI MSOMERA WAZURU LITA, TALIRI TANGA

Picha
Wafugaji kutoka kijiji cha Msomera kilichopo Handeni mkoani Tanga leo februari 28, 2024 wametembea taasisi za Wakala ya Mafunzo ya Mifugo nchini (LITA) kampasi ya Buhuri mkoani humo na ile ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) kanda ya Mashariki ambapo wamefurahishwa na elimu ya ufugaji waliyoipata kwenye Taasisi hizo. Akizungumza mara baada ya kukamilisha ziara hiyo ya siku moja, Mwenyekiti wa Kijiji cha Msomera Bw. Martin Paraketi ambaye mbali na kuishukuru Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Taasisi zake kwa kuwawezesha fursa hiyo ya mafunzo amewataka wafugaji wa kijiji chake kuwa mabalozi kwa wafugaji wengine kupitia yale waliyojifunza kutoka kwa wataalam wa taasisi zake. "Tunatambua Serikali imetambua umuhimu wetu kuja kujifunza hapa ili tushirikiane na wataalam wake kutoa elimu ya ufugaji bora kwa wenzetu tuliowaacha huko hivyo nitoe rai kwa wenzangu kila mmoja kutimiza wajibu wa kuelimisha kaya inayomzunguka kule Msomera" Amesema Bw. Paraketi Aidha Bw. P...

WIZARA YAZIDI KUKUTANA NA WADAU WA UVUVI KUTEKELEZA AGIZO LA MHE. RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN

Picha
Na. Edward Kondela Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kuwataka watendaji wa wizara hiyo kuendelea kuwatembelea wadau wa Sekta ya Uvuvi ili kutatua changamoto zao. Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi) Bi. Agness Meena amebainisha hayo leo (28.02.2024) katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam wakati wa kikao cha wadau wa viwanda na biashara ya mazao ya uvuvi ili kusikiliza hoja zao na changamoto zinazowakabili. Bi. Meena amesema wizara inataka kupunguza changamoto zilizopo katika Sekta ya Uvuvi kwa kufanya mikutano na wadau na kufanya maboresho yakiwemo ya kisera na kisheria ili sekta hiyo izidi kutoa mchango mkubwa zaidi katika pato la taifa. Amebainisha kuwa kupitia hotuba aliyotoa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa kugawa boti na vizimba jijini Mwanza, amesema lengo la serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni kutatua changamoto za sekta hiyo kupitia vikao endelevu. Kwa...

VIBALI VYA UVUVI KWA NJIA YA KIELETRONIKI NDANI YA SIKU SABA

Picha
Na. Edward Kondela Serikali imesema katika kipindi kifupi kijacho itahakikisha vibali vinavyohusu masuala ya uvuvi vinatolewa kwa njia ya kieletroniki ndani ya siku saba. Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amesema hayo leo (27.02.2024) katika ofisi ndogo za wizara jijini Dar es Salaam, wakati alipofanya kikao kifupi na baadhi ya wadau wa uvuvi wanaojishughulisha na uuzaji wa nyavu za uvuvi. Prof. Sheikh amesema kuwa mfumo wa kutoa vibali kwa njia ya kieletroniki utawezesha kutolewa vibali ndani ya siku saba ili kurahisisha huduma kwa wadau wa Sekta ya Uvuvi kupata vibali popote walipo. Ameongeza kuwa mikakati ya wizara ni kwamba kabla ya kuisha kwa mwaka wa fedha 2023/24 inatarajia kuanza rasmi utoaji wa vibali hivyo kwa nji ya kieletroniki. Ameongeza kuwa nia ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kupunguza ucheleweshaji wa vibali na kuifanya Sekta ya Uvuvi kuchangia kwa kiasi kikubw...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUTATUA CHANGAMOTO ZA WAVUVI

Picha
  Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga akifungua kikao cha kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili wanufaika wa boti na vizimba na hivyo kuzipati utatuzi, Aidha amewasihi wanufaika kutumia vifaa hivyo kama ilivyokusudiwa na kurejesha mikopo yao kwa uaminifu,  Februari 24,2024 Mkoani Mwanza.   Mkurugenzi wa Ukuzaji Viumbe maji Dkt. Nazaeli Madalla akifafanua baadhi ya hoja zilizoibuliwa  na wanufaika wa mkopo wa vizimba usio na riba  wakati wa kikao kifupi cha kusikiliza changamoto mbalimbali za wanufaika hao kilichofanyika  Buchosa Mkoani Mwanza, Februari 24,2024 Kaimu Mkurugenzi  Msaidizi Ukuzaji Viumbe Maji Baridi, Dkt. Imani Kapinga akujibu baadhi ya maswali yaliyokuwa yakiulizwa  na baadhi ya wanufaika wa mkopo wa  vizimba usio na riba  (hawapo pichani)  wakati wa kikao kifupi cha kusikiliza na kujibu changamoto  zinazowakabili wanufaika hao kilichofanyika Buchosa  Mkoani Mwanza, Februari 24,2023 Mkurug...

SERIKALI YAZINDUA BBT-LIFE (UVUVI) AWAMU YA PILI.

Picha
  Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na wenye ulemavu imezindua awamu ya pili ya program ya Jenga kesho iliyo bora kwa wanawake na vijana kwa upande wa sekta ya Uvuvi maarufu kama “BBT-LIFE” tukio lililofanyika leo februari 23, 2024 kwenye   Wakala ya Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kampasi ya Mbegani Bagamoyo mkoani Pwani. Uzinduzi huo ambao umetanguliwa na mafunzo ya siku 5 ya kubadili fikra kwa vijana na wanawake 300 waliochaguliwa kunufaika na awamu ya pili   program hiyo umefanywa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bi. Agness Meena ambaye amewasisitiza vijana hao kuhakikisha wanatumia vema mafunzo kwa vitendo watakayopewa kwa muda wa miezi 3 kwenye vituo walivypangiwa baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo ya Nadharia. “Baada ya kukamilika kwa mafunzo ya siku 5 ya “mind-set transformation” mnaenda kwenye mafunzo kwa vitendo kwa muda wa miezi 3, nitoe rai kwenu wote mkazingatie yale...

BBT-LIFE (UVUVI) AWAMU YA PILI YANG'OA NANGA

Picha
◾ Wanufaika waanza kupigwa msasa Serikali kupitia wizara ya Mifugo na uvuvi imeanza kutekeleza programu ya "Jenga kesho iliyo bora kwa wajasiriamali wanawake na vijana upande wa sekta ya Uvuvi kupitia mafunzo yanayotolewa kwa vijana na wanawake 300 kutoka pande   mbalimbali za nchi yaliyoanza kutolewa februari 19, 2024 kwenye chuo cha mafunzo ya uvuvi (FETA) kampasi ya Mbegani Bagamoyo mkoani Pwani. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa wizara hiyo Bi. Imelda Adam amewataka washiriki wa programu hiyo kuzingatia yale yote watayoelekezwa wakati wote wa mafunzo hayo ya nadharia yatakayofanyika kwa siku 5 ili waweze kufanya vizuri watakapoenda vituoni kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. "Programu hii inalenga kuwageuza wahitimu wa ngazi mbalimbali kwenye kada ya Uvuvi kuweza kujiajiri badala ya kusubiri kuajiriwa na lengo la Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha vijana na wanawake wengi ...

MHE. ULEGA ARIPOTI SENTRO

Picha
  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (kulia) akifafanua jambo wakati akizungumza na Watangazaji wa Kipindi cha Sentro kinachorushwa na Clouds TV moja kwa moja  kutoka jijini Dodoma Februari 9, 2024. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (wa pili kulia) akizungumza na Watangazaji wa Kipindi cha Sentro kinachorushwa na Clouds TV moja kwa moja kutoka jijini Dodoma  Februari 9, 2024. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Watangazaji wa Kipindi cha Sentro kinachorushwa na Clouds TV muda mfupi baada ya kumaliza kushiriki katika kipindi hicho kutokea jijini Dodoma leo Februari 9, 2024.  

DKT. MPANGO: “WEKENI JICHO LA PEKEE LONGIDO, WANAHITAJI MAJI NA MALISHO.”

Picha
Na. Edward Kondela Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameitaka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutoa jicho la pekee katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha kwa kuongeza mabwawa ya kunyweshea mifugo na kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kulinda malisho. Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mpango amebainisha hayo leo (10.02.2024) Wilayani Longido akiwa kwenye ziara ya kikazi wakati akizindua Kituo cha Afya Ketumbeine na mradi wa kusambaza umeme vijijini awamu ya tatu mzunguko wa kwanza unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Ameongeza kuwa mabwawa yanayoonesha udhaifu yakarabatiwe na hiyo ndiyo itakuwa zawadi kwa wakazi wa Wilaya ya Longido kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Ndugu zangu hawa ni wafugaji, mmeanza kazi vizuri lakini, ninawataka tena kutoa jicho la pekee kwa Wilaya ya Longido, kuongeza mabwawa ya kunyweshea mifugo yao na kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kulinda ma...

PROF. SHEMDOE AKUTANA NA MWAKILISHI MKAAZI WA SHIRIKA LA JICA

Picha
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi kujadiliana utekelezaji wa makubaliano ya kuendeleza mradi wa Afya Moja unaoangalia magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwenye Mifugo kwenda kwa binadamu   ikiwepo Brucellosis na Kifua Kikuu (TB). Prof. Shemdoe amekutana na Mwakilishi huyo Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024. Mradi huo unasimamiwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Maprofesa kutoka Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Maprofesa kutoka Chuo cha Mifugo cha Rakuna, kilichopo katika Mji wa Hokaido nchini Japan. Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi (kulia) alipokutana nae Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024. Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilis...