TALIRI WEST KILIMANJARO KUWA KITIVO CHA UBORA UZALISHAJI MBUZI, KONDOO.
◾ Ni kufuatia matokeo mazuri ya utekelezaji wa mradi wa ECF Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Daniel Mushi amesema kuwa Wizara yake inakusudia kukifanya kituo cha Utafiti wa Mifugo kanda ya Kaskazini cha West Kilimanjaro kuwa kitivo cha Ubora kwenye uzalishaji wa mbuzi na kondoo walioboreshwa kwa ajili ya kuwapa wafugaji nchini ili waweze kufuga kwa tija. Prof. Mushi amesema hayo leo Machi 05, 2024 baada ya kufika kwenye kituo hicho kilichopo chini ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI) ambapo ameweka wazi nia ya Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuongeza kiwango cha nyama bora inayouzwa nje kupitia kituo hicho. "Kama mnavyotambua nchi yetu kwa sasa imeongeza kasi katika kusafirisha nyama nje ya nchi na zaidi ya asilimia 90 ya nyama tunayopeleka huko ni ya mbuzi na kondoo hivyo tuna kila sababu ya kuongeza uzalishaji wa wanyama hao" Ameongeza Prof. Mushi. Aidha Prof. Mushi amemuelekeza Mkurugenzi wa kituo hicho Dkt. Leonard Marw...