PROF. SHEMDOE AKUTANA NA MWAKILISHI MKAAZI WA SHIRIKA LA JICA

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe amekutana na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi kujadiliana utekelezaji wa makubaliano ya kuendeleza mradi wa Afya Moja unaoangalia magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwenye Mifugo kwenda kwa binadamu  ikiwepo Brucellosis na Kifua Kikuu (TB).

Prof. Shemdoe amekutana na Mwakilishi huyo Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024.

Mradi huo unasimamiwa na Wataalamu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Maprofesa kutoka Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Maprofesa kutoka Chuo cha Mifugo cha Rakuna, kilichopo katika Mji wa Hokaido nchini Japan.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi (kulia) alipokutana nae Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi (kushoto) baada kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (katikati)akiagana na Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Japan (JICA), Bw. Ara Hitoshi (kushoto) muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika Ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma Januari 7, 2024.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO