Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2023

SERIKALI KUKOPESHA WANAWAKE SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Serikali kupitia Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB) inatarajia kutoa mkopo wa Sh1.3 trilioni kusaidia wanawake kuboresha biashara na uwekezaji kwenye mnyororo wa thamani katika sekta za mifugo na uvuvi. Akizungumza kuhusu fursa hiyo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya mifugo na uvuvi Dkt. Daniel Mushi alisema dhumuni la fedha hiyo ni kuwezesha sekta binafsi kuwa kichocheo cha maendeleo, Machi 21, 2023 “Kwa kuanzia walengwa mahsusi ni sekta binafsi hususan kwa biashara zinazoongozwa na wanawake au shughuli zinazoambatana na uchumi wa buluu ikiwemo kilimo cha mwani”alisema Dkt. Mushi. Aidha Dkt. Mushi alisema sio tu kuwainua wanawake katika uwekezaji bali hata kuzalisha fursa za ajira kwenye mnyororo wa thamani wa mazao ya bahari na mifugo kwa ujumla na kupunguza suala la ukosefu wa ajira nchini. “Wajasiriamali watumie fursa hii vizuri ili iwe kioo na baadae tuaminike ili fedha zijazo zipitie moja kwa moja kwenye sekta binafsi na fursa hii itakuja tena ikiwa tutakuwa waaminifu kw...

VIJANA MTWARA KUFAIDIKA NA PROGRAM YA ATAMIZI

Picha
Kiongozi wa vijana wanaoendelea na programu maalum ya Atamizi kwa upande Sekta ya Uvuvi waliopo  kwenye kituo cha Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Mikindani, Mtwara. Bw. Charles Songa akiwaongoza wenzake wakati wa mafunzo kwa vitendo kuhusu ufugaji wa matango bahari ikiwa ni sehemu ya Utekelezaji wa Programu hiyo (15.03.2022). Mkufunzi kutoka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kituo cha Mikindani, Mtwara Bw. Shaban Saleh (kulia) akiwafundisha vijana wanaoendelea na programu maalum ya Atamizi kwa upande wa sekta ya Uvuvi fursa zilizopo kwenye ufugaji wa tango bahari wakati wa Mwendelezo wa Programu hiyo  (15.03.2023). Mkufunzi kutoka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kituo cha Mikindani, Mtwara Bw. Shaban Saleh (wa pili kutoka kulia) akiielekeza timu ya tathmini kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi inayoongozwa na Bi. Yasinta Magesa (kulia) namna wanavyowawezesha elimu ya Ufugaji wa samaki vijana wanaoshiriki Programu maalum ya Atamizi waliopo kituoni hap...

VIJANA WAPATIWA MAFUNZO YA UKUZAJI VIUMBE MAJI KWA VITENDO (ATAMIZI) MAGU MKOANI MWANZA

Picha
Meneja wa Shamba la kufugia Samaki la KONGA AGRIBUSINESS FARM, Bw. Steven Satola akitoa maelezo ya utendaji kazi wa shamba hilo ambalo limepokea vijana wahitimu  waliochaguliwa kupata mafunzo ya vituo atamizi vya uvuvi na ukuzaji Viumbe  maj kwa wataalamu wa Uvuvi waliotoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, walipoenda kutembelea na kuona mafunzo hayo yanavyoendelea kwa vijana hao kwenye shamba hilo lililopo Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza, Machi 15,2023. Wataalamu wa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakiongea na vijana wa mafunzo ya uvuvi na Ukuzaji viumbe maji kwa Vitendo (Atamizi) waliochaguliwa kwenye Shamba la kufugia Samaki la KONGA AGRIBUSINESS FARM, ili kujua wanajifunza nini na changamoto gani wanazioitia wanapokuwa kwenye mafunzo hayo, shamba hilo lipo katika Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza, Machi 15,2023. Vijana waliochaguliwa kwenye mafunzo ya uvuvi na Ukuzaji viumbe maji (Atamizi) wakifanya zoezi la kuhamisha vifanga vya Samaki kwenye bwawa ili waweze kusafisha bwawa h...

VIJANA WAPATIWA MAFUNZO YA UFUGAJI WA SAMAKI KWA NJIA YA VITENDO MKOANI MARA

Picha
Mkuu wa Kikosi cha 27KJ Makoko mkoani Mara, Lt. Col. Simon Rugaimukamu (kulia) akiwaeleza wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu namna walivyowapokea vijana ambao wamepelekwa kwa ajili ya kupata mafunzo kwa vitendo kuhusu ufugaji wa samaki kwenye vizimba ambapo ameiomba Wizara kukitumia kituo hicho kama shamba darasa ili vijana na wavuvi waweze kujifunza. (15.03.2023) Afisa Uvuvi Mwandamizi, Bi. Kresensia Mtweve akizungumza na vijana waliopo kwenye kituo cha 27KJ Makoko mkoani Mara (hawapo pichani) kwa ajili ya kupata mafunzo kwa vitendo kuhusu ufugaji wa samaki kwenye vizimba wakati wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu walipotembelea kituo hicho kuona namna mafunzo hayo yanavyoendeshwa ambapo amewasihi vijana hao kutumia elimu waliyofundishwa ili kuleta tija katika ufugaji. (15.03.2023) Picha ya pamoja ya wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kazi, Ajira na Watu wenye...

KAIMU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI DKT. CHARLES MHINA AFANYA KIKAO NA MSHAURI ELEKEZI KUTOKA FAO, BI, TERESA AMADOR

Picha
Mshauri elekezi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Bi. Teresa Amador akiwasilisha taarifa ya majumuisho juu ya Sera na Sheria  za Uvuvi  kwa Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina (kulia) mara baada ya ziara yake Wizarani hapo, Machi 15,2023 Mtumba jijini Dodoma, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Tanzania Bw. Melkizedeck Koddy Kaimu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina (kulia) akiongea mara baada ya kupokea taarifa ya tathmini ya Sera na Sheria za Uvuvi kutoka kwa Mshauri elekezi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Bi. Teresa Amador  (katika)  kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Tanzania Bw. Melkizedeck Koddy, Machi 15,2023 Mtumba jijini Dodoma. Mkurugenzi Msaidizi wa Uvuvi Tanzania Bw.  Melkizedeck Koddy, (kulia) akichangia hoja wakati wa kikao cha kupokea taarifa kutoka kwa mshauri elekezi Bi. Teresa Amador kilichofanyika kwenye ofisi za Wizara ya Mifu...

WATAALAM KUTOKA SEKTA YA UVUVI WAWATEMBELEA WAFUGAJI WA SAMAKI KWENYE MABWAWA WILAYANI CHAMWINO

Picha
Mfugaji kwenye mabwawa Bw. Manoa Samson (kushoto) akielezea namna walivyoanza ufugaji wa samaki na adi walipofikia kwa sasa pamoja na changamoto na mafanikio waliyoyapata na kuhamasisha wafugaji wengine kutokukata tamaa wakati walipotembelewa na watendaji kutoka wizara ya mifugo na uvuvi, Machi 14, 2023 Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma . Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (uvuvi) Bw. John Mallya (wa pili kutoka kulia) akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wafugaji wa samaki walipowatembelea wafugaji hao kwenye wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Machi 14,2023 Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Mkomanile Mahundi akiwaeleza wafugaji wa samaki kwenye mabwawa aina ya vyakula vya kulisha samaki hao na namna ya kuwalisha wakati walipowatembelea kwenye kijiji cha Handari halmashauri ya wilaya ya chamwino mkoani Dodoma, Machi 14,2023 Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti, mafunzo na Ugani  kutoka wizara ya mifugo na uvuvi (uvuvi) Bw. Anthony Dadu (katikati) akiwa kw...

KIKAO CHA KUIMARISHA USHIRIKIANO BAINA YA SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA NA MKURUGENZI WA MELI ZA ALBACORA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katikati) akiongea na Uongozi wa Kampuni ya Meli ya Albacora alipokutana nao kwa ajili ya kuimarisha ushirikiano baina ya Serikali na Kampuni hiyo hususan kwenye eneo la Uvuvi wa Bahari Kuu. Mhe. Ulega alikutana na Uongozi huo jijini Dar es Salaam Machi 14, 2023. Uongozi wa Kampuni ya Albacora uliongozwa na Mkurugenzi wa Meli, Bw. Imanol Loinaz. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katikati) akimuelekeza jambo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA), Dkt. Emmanuel Sweke (kulia) wakati wa kikao kifupi baina ya Waziri huyo na Mkurugenzi wa Meli za Albacora, Bw. Imanol Loinaz (kushoto) kilichofanyika jijini Dar es Salaam Machi 14, 2023. (kushoto) Mkurugenzi wa Meli za Albacora, Bw. Imanol Loinaz. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katikati) akimuonesha Mkurugenzi wa Meli za Albacora, Bw. Imanol Loinaz maelezo yaliyopo katika Kitabu cha Ilani ya ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 202...

PROF. SHEMDOE AMSHUKURU MHE.DKT.SAMIA KWA KUTOA TSH BILIONI 266.7

Picha
  Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa jumla ya Tsh. Bilioni 266.7   ikiwa ni gharama ya Ujenzi wa mradi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko Mkoani Lindi. "Ninamshukuru sana Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia Tsh. Bilioni 266.7   ikiwa ni gharama ya Mradi ya Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi hapa Kilwa Masoko Mkoani Lindi." Alisema Shemdoe. Aidha, Prof. Shemdoe ameongeza kuwa bandari hiyo ya Uvuvi ikikamilika itakuwa msaada mkubwa sana kwa Watanzania wanaofanya kazi ya uvuvi. Bandari hiyo   itatoa ajira elfu 30 kwa Vijana wa kike na wakiume, itaongeza usafirishaji wa Samaki Nje ya Nchi, itaongeza tija ya Uvuvi Bahari Kuu. Vilevile, Katibu Mkuu ameainisha faida nyingine kuwa bandari hiyo itapunguza upotevu wa Samaki (Post Harvest), itaondoa changamoto ya uvuvi haramu usioratibiwa na kutolewa taarifa, vilevile ...

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

WIZARA YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI KWA KAMATI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo na kuwasilisha taarifa ya muundo na majukumu ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa Bwawa la kuvuna maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo la Matekwe lililopo Nachingwea, Mkoani Lindi, na taarifa ya ujenzi wa bandari ya uvuvi iliyopo Wilayani Kilwa, Mkoani Lindi. Baada ya kupokea taarifa hiyo mapema leo Machi 12, 2023, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. David Kihenzile  alimuhakikishia Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega  kuwa watashirikiana bega kwa bega na Wizara ili kuiwezesha kufikia malengo yake ya kuwahudumia wananchi ili wapate maendeleo  katika shughuli zao za kila siku za ufugaji na uvuvi. Aidha, kamati hiyo inatarajiwa kufanya ziara Mkoani Lindi hivi karibuni kwa ajili ya kutembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akifafanua jambo wakati wa kikao cha ku...

WAZIRI ULEGA AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA TANZANIA NCHINI KOREA

Picha
  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega(kulia) akimueleza jambo  Balozi wa Tanzania nchini Korea, Balozi Togolani Mavura walipokutana ofisini kwake jijini Dodoma mapema leo Machi 8, 2023.  lengo ni kujadiliana kuhusu fursa za ushirikiano baina ya nchi hizo mbili kwenye kukuza na kuimarisha uchumi wa buluu nchini Tanzania. Balozi wa Tanzania nchini Korea, Mhe. Balozi Togolani Mavura (kushoto) akiongea na  Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega walipokutana ofisini kwa Waziri huyo jijini Dodoma Machi 8, 2023. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Korea, Mhe. Balozi Togolani Mavura (kulia kwake) muda mfupi baada ya kumaliza mazungumzo yao mapema leo Machi 8, 2023. Kushoto kwake ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Bi. Agness Meena. Wengine katika picha ni Wataalam kutoka Wizarani.

MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, MACHI 08, 2023

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

SAUTI YETU WIKI HII

Picha
 

SEKTA YA MIFUGO SMT NA SMZ ZAIMARISHA USHIRIKIANO

Picha
Na Saja Kigumbe Serikali ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) zaimarisha ushirikiano Ili kutatua changamoto kwenye Sekta ya Mifugo  ili kufikia uzalishaji wenye tija wa mifugo. Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina wakati akifungua kikao cha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya mapinduzi Zanzibar (SMZ) kilichofanyika jijini Dodoma Machi 3, 2023. ‘’Tumekuwa tukishirikiana pia kwenye maeneo ya masoko kuona ni namna gani tunaweza tukaimarisha masoko ya bidhaa za mifugo kwa pande zote mbili.  Kwa hiyo ushirikiano huu unalenga kuondoa vikwazo ambavyo vinaweza kuifanya biashara ya mifugo isikue kwa haraka ,’’ alisema Dkt. Mhina Dkt. Mhina alisema sehemu zote za Bara na Zanzibar kuna viwanda vya kuzalisha bidhaa za mifugo ikiwemo nyama, ngozi, maziwa na bidhaa nyingine hivyo ushirikiano huo utasaidia kuimarisha sekta hiyo ya mifugo. Aliongez...

KIKAO CHA KUJADILI RAASIMU YA MPANGO WA UNYWAJI MAZIWA SHULENI CHAFANYIKA JIJINI DODOMA

Picha
  Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Stephen Michael akisisitiza baadhi ya maeneo ya kuzingatia wakati wa kupitia Rasimu ya Mpango wa Unywaji Maziwa Shuleni alipokuwa anafungua kikao cha kupitia Rasimu ya mpango huo  Machi 2, 2023 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Royal Village Hotel Dodoma, (Kushoto) ni Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania Dkt. George Msalya na kulia ni Mwakilishi wa Wadau wa Maziwa Nchini Bw. Joakim Balakana. Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania, Dkt. George Msalya (aliyesimama) akitoa neno la utangulizi kuhusu mpango wa unywaji maziwa shuleni kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo),  Bw. Stephen Michael (katikati) kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni Machi 2, 2023 kwenye Ukumbi wa Royal Village Hotel, Dodoma (Kulia) ni Mwakilishi wa Wadau wa Maziwa Nchini Bw. Joakim Balakana. Afisa M...