Nav bar

Alhamisi, 16 Machi 2023

VIJANA WAPATIWA MAFUNZO YA UFUGAJI WA SAMAKI KWA NJIA YA VITENDO MKOANI MARA

Mkuu wa Kikosi cha 27KJ Makoko mkoani Mara, Lt. Col. Simon Rugaimukamu (kulia) akiwaeleza wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu namna walivyowapokea vijana ambao wamepelekwa kwa ajili ya kupata mafunzo kwa vitendo kuhusu ufugaji wa samaki kwenye vizimba ambapo ameiomba Wizara kukitumia kituo hicho kama shamba darasa ili vijana na wavuvi waweze kujifunza. (15.03.2023)

Afisa Uvuvi Mwandamizi, Bi. Kresensia Mtweve akizungumza na vijana waliopo kwenye kituo cha 27KJ Makoko mkoani Mara (hawapo pichani) kwa ajili ya kupata mafunzo kwa vitendo kuhusu ufugaji wa samaki kwenye vizimba wakati wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu walipotembelea kituo hicho kuona namna mafunzo hayo yanavyoendeshwa ambapo amewasihi vijana hao kutumia elimu waliyofundishwa ili kuleta tija katika ufugaji. (15.03.2023)

Picha ya pamoja ya wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu na vijana wanaopata mafunzo kwa vitendo kwenye kituo cha 27KJ Makoko mkoani Mara mara baada ya kukagua na kunzungumza na vujana hao. (15.03.2023)

Baadhi ya Vizimba vilivyopo kwenye kikosi cha 27KJ Makoko mkoni Mara vinavyotumika kufugia samaki. (15.03.2023)

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni