Nav bar

Alhamisi, 16 Machi 2023

KAIMU KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI DKT. CHARLES MHINA AFANYA KIKAO NA MSHAURI ELEKEZI KUTOKA FAO, BI, TERESA AMADOR

Mshauri elekezi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO), Bi. Teresa Amador akiwasilisha taarifa ya majumuisho juu ya Sera na Sheria  za Uvuvi  kwa Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina (kulia) mara baada ya ziara yake Wizarani hapo, Machi 15,2023 Mtumba jijini Dodoma, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Tanzania Bw. Melkizedeck Koddy

Kaimu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina (kulia) akiongea mara baada ya kupokea taarifa ya tathmini ya Sera na Sheria za Uvuvi kutoka kwa Mshauri elekezi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Bi. Teresa Amador  (katika)  kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Tanzania Bw. Melkizedeck Koddy, Machi 15,2023 Mtumba jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Uvuvi Tanzania Bw.  Melkizedeck Koddy, (kulia) akichangia hoja wakati wa kikao cha kupokea taarifa kutoka kwa mshauri elekezi Bi. Teresa Amador kilichofanyika kwenye ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi  mtumba jijini Dodoma,  Machi 14,2023

Kaimu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi , Dkt. Charles Mhina (wa tatu kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mshauri Elekezi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Bi. Teresa Amador (wa tatu kutoka kushoto) na watendaji kutoka Sekta ya Uvuvi mara baada ya kikao kifupi kilichofanyika kwenye ofisi za Wizara hiyo Mtumba Jijini Dodoma, Machi 15,2023

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni