VIJANA MTWARA KUFAIDIKA NA PROGRAM YA ATAMIZI

Kiongozi wa vijana wanaoendelea na programu maalum ya Atamizi kwa upande Sekta ya Uvuvi waliopo  kwenye kituo cha Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Mikindani, Mtwara. Bw. Charles Songa akiwaongoza wenzake wakati wa mafunzo kwa vitendo kuhusu ufugaji wa matango bahari ikiwa ni sehemu ya Utekelezaji wa Programu hiyo (15.03.2022).

Mkufunzi kutoka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kituo cha Mikindani, Mtwara Bw. Shaban Saleh (kulia) akiwafundisha vijana wanaoendelea na programu maalum ya Atamizi kwa upande wa sekta ya Uvuvi fursa zilizopo kwenye ufugaji wa tango bahari wakati wa Mwendelezo wa Programu hiyo  (15.03.2023).

Mkufunzi kutoka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kituo cha Mikindani, Mtwara Bw. Shaban Saleh (wa pili kutoka kulia) akiielekeza timu ya tathmini kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi inayoongozwa na Bi. Yasinta Magesa (kulia) namna wanavyowawezesha elimu ya Ufugaji wa samaki vijana wanaoshiriki Programu maalum ya Atamizi waliopo kituoni hapo muda mfupi baada ya timu hiyo kuwasili  (15.03 2023)

 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO