Nav bar

Alhamisi, 16 Machi 2023

WATAALAM KUTOKA SEKTA YA UVUVI WAWATEMBELEA WAFUGAJI WA SAMAKI KWENYE MABWAWA WILAYANI CHAMWINO

Mfugaji kwenye mabwawa Bw. Manoa Samson (kushoto) akielezea namna walivyoanza ufugaji wa samaki na adi walipofikia kwa sasa pamoja na changamoto na mafanikio waliyoyapata na kuhamasisha wafugaji wengine kutokukata tamaa wakati walipotembelewa na watendaji kutoka wizara ya mifugo na uvuvi, Machi 14, 2023 Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma .

Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (uvuvi) Bw. John Mallya (wa pili kutoka kulia) akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na wafugaji wa samaki walipowatembelea wafugaji hao kwenye wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Machi 14,2023

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Mkomanile Mahundi akiwaeleza wafugaji wa samaki kwenye mabwawa aina ya vyakula vya kulisha samaki hao na namna ya kuwalisha wakati walipowatembelea kwenye kijiji cha Handari halmashauri ya wilaya ya chamwino mkoani Dodoma, Machi 14,2023

Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti, mafunzo na Ugani  kutoka wizara ya mifugo na uvuvi (uvuvi) Bw. Anthony Dadu (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wafugaji wa samaki kwenye mabwawa  na wataalam kutoka sekta ya uvuvi mara baada ya kuwatembelea wafugaji hao na kuona namna wanafanya ufugaji wao na changamoto zinazowakabili kwenye wilaya ya chamwino mkoani Dodoma, Machi 14,2023

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni