Nav bar

Alhamisi, 16 Machi 2023

VIJANA WAPATIWA MAFUNZO YA UKUZAJI VIUMBE MAJI KWA VITENDO (ATAMIZI) MAGU MKOANI MWANZA

Meneja wa Shamba la kufugia Samaki la KONGA AGRIBUSINESS FARM, Bw. Steven Satola akitoa maelezo ya utendaji kazi wa shamba hilo ambalo limepokea vijana wahitimu  waliochaguliwa kupata mafunzo ya vituo atamizi vya uvuvi na ukuzaji Viumbe  maj kwa wataalamu wa Uvuvi waliotoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, walipoenda kutembelea na kuona mafunzo hayo yanavyoendelea kwa vijana hao kwenye shamba hilo lililopo Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza, Machi 15,2023.

Wataalamu wa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, wakiongea na vijana wa mafunzo ya uvuvi na Ukuzaji viumbe maji kwa Vitendo (Atamizi) waliochaguliwa kwenye Shamba la kufugia Samaki la KONGA AGRIBUSINESS FARM, ili kujua wanajifunza nini na changamoto gani wanazioitia wanapokuwa kwenye mafunzo hayo, shamba hilo lipo katika Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza, Machi 15,2023.

Vijana waliochaguliwa kwenye mafunzo ya uvuvi na Ukuzaji viumbe maji (Atamizi) wakifanya zoezi la kuhamisha vifanga vya Samaki kwenye bwawa ili waweze kusafisha bwawa hilo ambalo wanafanyia mafunzo ya Ufugaji Samaki katika Shamba la KONGA AGRIBUSINESS FARM Lililopo Wilaya ya Magu,Mkoani Mwanza  mbele ya Wataalamu wa uvuvi kutoka  Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Machi 15,2023.

Vijana wa mafunzo ya uvuvi na Ukuzaji viumbe maji kwa Vitendo (Atamizi) waliochaguliwa kwenye Shamba la kufugia Samaki la KONGA AGRIBUSINESS FARM, wakiwaelezea wataalamu wa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (hawapo pichani) namna ya vifaranga vya samaki vinavyozalishwa katika Maabara ya Uzalishaji wa Vifaranga vya samaki (Hatchery), Shamba hilo lipo katika Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza,  Machi 15,2023.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni