Nav bar

Jumamosi, 4 Machi 2023

KIKAO CHA KUJADILI RAASIMU YA MPANGO WA UNYWAJI MAZIWA SHULENI CHAFANYIKA JIJINI DODOMA

 

Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Stephen Michael akisisitiza baadhi ya maeneo ya kuzingatia wakati wa kupitia Rasimu ya Mpango wa Unywaji Maziwa Shuleni alipokuwa anafungua kikao cha kupitia Rasimu ya mpango huo  Machi 2, 2023 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Royal Village Hotel Dodoma, (Kushoto) ni Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania Dkt. George Msalya na kulia ni Mwakilishi wa Wadau wa Maziwa Nchini Bw. Joakim Balakana.

Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania, Dkt. George Msalya (aliyesimama) akitoa neno la utangulizi kuhusu mpango wa unywaji maziwa shuleni kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo),  Bw. Stephen Michael (katikati) kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni Machi 2, 2023 kwenye Ukumbi wa Royal Village Hotel, Dodoma (Kulia) ni Mwakilishi wa Wadau wa Maziwa Nchini Bw. Joakim Balakana.

Afisa Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko Bw. Edson Kilyenyi akiwasilisha Rasimu ya mpango wa Unywaji maziwa shuleni kwa wajumbe walioshiriki kikao cha kupitia Rasimu hiyo, kilichofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Royal Village, Dodoma, Machi 02,2023

Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Stephen Michael (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe walioshiriki  kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni kilichofanyika kwenye  ukumbi wa Hoteli ya Royal Village Dodoma Machi 2, 2023.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni