Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2023

NZUNDA ATOA MAELEKEZO KWA WATAFITI WA MIFUGO

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda amewataka watafiti wa mifugo kufanya tafiti zinazozingatia maslai ya nchi.   Nzunda ameyasema hayo (20.02.2023) wakati akifungua Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa jopo gesi (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro.   Watafiti wametakiwa kuzingatia malengo ya nchi katika kuleta mabadiliko kwenye sekta ya mifugo katika tafiti wanazozifanya ili kuongeza tija katika uzalishaji na sio kutumia tafiti hizo kwa matakwa ya wafadhili au maslai yao binafsi.   Pia watafiti wametakiwa kuzingatia utaalam, misingi ya maadili, uwajibikaji unaotokana na matendo na matokeo ya tafiti wanazozifanya ukiwemo utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa jopo gesi (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafuga...

KAZI YAZIDI KUENDELEA KUPITIA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Picha
 

BIL 6.2 ZA MABWAWA KUNUFAISHA WAFUGAJI

Picha
Na. Edward Kondela Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha kila sekta nchini ambapo imepanga kujenga mabwawa ya kunyweshea mifugo maji kote nchini. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akizungumza (17.02.2023) wakati alipofanya ziara ya kikazi kukagua maendeleo ya ujenzi wa bwawa la maji la Kwekinkwembe lililopo katika Wilaya ya Kilindi Mkoani Tanga, amesema Rais Dkt. Samia katika bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2022/23 ameridhia kuipatia wizara Shilingi Bilioni 6.2 kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa hayo. Naibu Waziri Ulega amefafanua kuwa kila sekta nchini imeguswa ikiwemo ya mifugo na kwamba hakuna iliyeachwa nyuma hivyo wafugaji watanufaika kwa kupata maji ya uhakika mara baada ya mradi wa ujenzi wa mabwawa ya kunyweshea mifugo maji kukamilika. “Rais Mhe. Dkt. Samia hakuna aliyemuacha pembeni ndiyo maana amegusa wakulima mbegu za ruzuku, amegusa wafugaji mabwawa na majosho, hivyo hakuna aliyeachwa nyuma...

ULEGA: MSOMERA YAZIDI KUNG’ARA MIRADI YA WAFUGAJI YAPAA

Picha
Na. Edward Kondela Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amesema anamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo serikali inahakikisha kila sekta inafikiwa katika maendeleo wakiwemo wafugaji na wavuvi. Naibu Waziri Ulega amebainisha hayo (16.12.2023) wakati alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja katika Kijiji cha Msomera kilichopo Wilaya ya Handeni Mkoani Tanga, kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali inayowahusu wafugaji, yakiwemo mabwawa ya maji, minada ya mifugo, majosho na malambo ili kusogeza huduma karibu kwa wakazi wa kijiji hicho. Amesema mbali na wafugaji ambao serikali imekuwa ikiwafikia kwa kuwapatia huduma mbalimbali za miundombinu kwa ajili ya shughuli za mifugo, wavuvi na wafugaji wa samaki pia wanafikiwa. “Hakuna lililosimama yote yanasonga mbele makandarasi waendelee kushirikisha vyema wenyeji ambao wanajua mazingira ya hapa na wenyeji kushirikiana na makandarasi na wenyewe kuwashiriki...

BI. MWANGISA AFUNGA KIKAO CHA UZINDUZI WA MATAWI YA WANAWAKE WANAOJIHUSISHA NA SHUGHULI ZA UVUVI TANZANIA

Picha
  Mkurugenzi msaidizi wa utawala na rasilimali watu Sekta ya uvuvi, Bi. Marry Mwangisa akitoa neno wakati wa kufunga kikao cha uzinduzi wa matawi ya wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi Tanzania (TAWFA) Kanda ya ziwa Nyasa na maji madogo kwa wanawake hao (hawapo pichani) na kuwahasa kushikamana na kuunda vikundi vitakavyowasaidia kujikwamua kiuchumi Mkoani Iringa Februari 16,2023 Mratibu wa mwongozo wa  Mradi wa kuendeleza Uvuvi mdogo Bi. Lilian Ibengwe akiwapongeza wanawake kwa ushiriki wao (hawapo pichani) na kuwasihi kuzingatia yale yote waliyoelimishwa  wakati wa  kikao cha kufunga  uzinduzi wa matawi ya TAWFA Kanda ya Ziwa Nyasa na maji madogo kilichofanyika kwenye ukumbi wa royal palm Mkoani Iringa, Februari 16,2023 Viongizi wa wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi Tanzania (TAWFA) Kanda ya ziwa Nyasa (picha ya juu) na viongizi wa maji madogo (picha ya chini) wakiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa NTT pamoja na watendaji kutoka Sekta uv...

SERIKALI KUTUMIA BILIONI 1.8 KWA AJILI YA MASHAMBA DARASA YA UFUGAJI SAMAKI

Picha
Serikali  ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt.Rais, Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewezesha Halmashauri kumi na nne (14) kwa kutoa fedha kiasi cha Tsh 1.8 Bilioni kwa ajili ya kujenga miradi ya mashamba darasa ya Ufugaji Samaki. Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe maji, kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Eng.George Kwandu (16.02.2023) alipoenda kukagua moja ya miradi hiyo uliopo Kijiji cha Tubugwe,kata ya Chamkoroma, Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma. Eng. Kwandu amesema mradi huo wa  kijiji cha Tubugwe umegharimu kiasi cha Tsh 128 milioni, kwa lengo la kuwasaidia vijana na wanawake nchini ambapo itaobgeza ajira kwa vijana, kuongeza kipato na kuongeza usalama wa chakula. Aidha, Eng kwandu  amesema mradi huo unatakiwa kutekelezwa katika kipindi cha miezi mitatu, ambapo kutakuwa na Ujenzi wa mabwawa manne ambayo kwa kila moja ina mita za mraba 600, mfeleji wa kupitishia maji, ofisi na jengo la kufundishia ufu...

MAONO YA DKT. SAMIA YAWAVUTIA VIJANA KUJIAJIRI KWENYE UFUGAJI

Picha
Na. Edward Kondela Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeamua kukuza sekta ya mifugo kupitia unenepeshaji wa mifugo ili wananchi waweze kufuga kibiashara na kwa tija zaidi. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amebainisha hayo (15.02.2023) Mkoani Tanga, wakati alipotembelea vijana waliojiunga kwenye vituo atamizi vilivyopo Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) na Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) ili kupata mafunzo ya vitendo ya ufugaji kibiashara na unenepeshaji bora wa mifugo. Mhe. Ulega amefafanua kuwa kupitia dira na maono ya Mhe. Rais Dkt. Samia, serikali imeonelea kuichangamsha Sekta ya Mifugo, kupitia unenepeshaji na ufugaji wenye tija hivyo wizara kuja na programu ya Samia Ufugaji kwa Tija (SAUTI).                                                    “T...

DKT. SAMIA AMWAGA MABILIONI KUINUA FURSA ZA UCHUMI WA BULUU.

Picha
Na. Edward Kondela Serikali imeendelea kutekeleza bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23 katika uwekezaji wa uchumi wa buluu kupitia maji ya Bahari ya Hindi, maziwa na mito ikiwemo kuhamasisha ufugaji wa viumbe maji. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amebainisha hayo (15.02.2023) wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi Mkoani Tanga ambapo katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, kwenye Sekta ya Uvuvi ametembelea vikundi vya ushirika vya ukuzaji viumbe maji vya Jifute kinachonenepesha kaa pamoja na Mondura na Mchukuuni vinavyojishughulisha na ufugaji wa tango bahari ama kwa jina lingine la zamani jongoo bahari pamoja na ukulima wa mwani. Ili kukuza uchumi wa buluu, Naibu Waziri Ulega amesema serikali imeweka Shilingi Bilioni 2.5 kwa ajili ya kuendeleza zao la mwani ambapo tayari Shilingi Milioni 447 zimeshatolewa kwa vikundi mbalimbali, Shilingi Bilioni 11.5 zimetengwa kwa ajili ya kutengeneza boti za kisasa za uvuvi na Shilingi Bilioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa vizimba vya kuf...

KIKOSI KAZI KINACHORATIBU MWONGOZO WA KUENDELEZA UVUVI MDOGO NCHINI KIKIENDELEA NA KIKAO CHA KUZINDUA MATAWI YA WANAWAKE

Picha
  Mwenyekiti wa kikosi kazi cha kitaifa kinachoratibu muongozo wa kuendeleza Uvuvi Mdogo nchini (NTT), Bw. Yahya Mgawe akiwasilisha mada wakati wa kikao cha uzinduzi wa matawi ya wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi Tanzania (TAWFA) Kanda ya ziwa Nyasa na maji madogo   kilichofanyika kwenye ukumbi wa royal palm Mkoani Iringa Februari 15,2023 Afisa Uvuvi Mwandamizi ambaye pia ni mratibu wa dawati la jinsia kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Bi. Upendo hamidu akichangia hoja wakati wa kikao cha uzinduzi wa matawi ya TAWFA Kanda ya ziwa Nyasa na maji madogo kilichofanyika kwenye ukumbi wa royal palm Mkoani Iringa Februari 15,2023 Mteknolojia wa samaki Mkuu, Bi. Flora Ruhanga akichangia hoja kwenye kikao cha uzinduzi wa matawi ya wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi Tanzania (TAWFA) Kanda ya ziwa Nyasa na maji madogo kilichofanyika kwenye ukumbi wa royal palm Mkoani Iringa Februari 15,2023 Mjumbe wa kikosi kazi cha kitaifa kinachoratibu muongozo wa kuen...

SERIKALI, WADAU KUIMARISHA USALAMA WA WAVUVI ZIWA VICTORIA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Dodoma Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Utunzaji wa Rasilimali za Uvuvi (EMEDO) chini ya Ufadhili wa Shirika la Royal National Lifeboat Institution(RNLI) linalojishughulisha na usalama kwenye maji na uokozi wanatekeleza mradi wa kuzuia wavuvi kuzama majini na kuhakikisha wanakuwa salama wakati wote wa shughuli zao katika Ziwa Victoria. Mradi huo wa miaka 3 kuanzia 2022/2025 umelenga kuwaelimisha wavuvi hatua mbambali za kuchukua za kujizuia kuzama majini kabla ya kuingia kazini, lakini pia mradi utajikita katika kutoa mafunzo mbalimbali kwa jamii na wavuvi, BMU na watalamu wengine wa serikali wanaofanya kazi na wavuvi. Pia, Mradi utashirikiana kwa karibu na taasisi za serikali zinazohusika moja kwa moja kwenye suala la usalama kwenye maji . Lengo kuu la mradi huo ni kuhakikisha kuwa wadau wote wa sekta ya uvuvi kwa pamoja wanashirikiana kuchukua hatua mbalimbali za kuzuia matukio ya kuzama kwa wavuvi...

SEKTA YA UVUVI YAZINDUA MATAWI YA TAWFA KANDA YA ZIWA NYASA NA MAJI MADOGO

Picha
  Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Bw. Stephen Lukanga akisoma Hotuba kwa Niaba ya Katibu Mkuu Sekta ya uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah wakati wa uzinduzi wa matawi ya TAWFA Kanda ya ziwa Nyasa na maji madogo kilichofanyika kwenye ukumbi wa royal palm Mkoani Iringa Februari 14,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwaunganisha wanawake wa  Tanzania nzima kupitia vikundi vyao Ili kuwezesha kuwa na sauti ya pamoja, kubadilishana mawazo na uzoefu katika kupata uhakika wa masoko. Mkurugenzi msaidizi wa utawala na rasilimali watu Sekta ya uvuvi, Bi. Marry Mwagisa akitoa neno kwa wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi (hawapo pichani) wakati wa kikao cha uzinduzi wa matawi ya TAWFA Kanda ya ziwa Nyasa na maji madogo kilichofanyika kwenye ukumbi wa royal palm Mkoani Iringa Februari 14,2023 Mwenyekiti wa kikosi kazi cha kitaifa kinachoratibu muongozo wa kuendeleza Uvuvi Mdogo nchini (NTT), Bw. Yahya Mgawe akiongea na wanawake wanaojihusisha na shughuli za uvuvi Tanzania (TAWFA) wakati wa kikao c...

WATAFITI NA WANASAYANSI KUTOKA NCHI 18 DUNIANI WAKUTANA JIJINI ARUSHA

Picha
WATAFITI na wanasayansi kutoka nchini 18 duniani, wamekutana jijini  Arusha kutafuta ufumbuzi wa kutokomeza ugonjwa wa  Ndorobo unaoenezwa na Mbung’o ambao umekuwa tishio kwa wanyama na binadamu kwa nchi za Afrika ikiwemo Tanzania. Akiongea kwenye mkutano huo jana Jijini Arusha Mkurugenzi wa huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Hezron Nonga alisema watafiti hao watakuja na jibu la pamoja la namna ya kutokomeza ugonjwa huo unaotishia soko la Nyama kimataifa. Amesisitiza kuwa uwepo wa ugonjwa wa Ndorobo, Afrika inapata hasara ya takribani dola za kimarekani bilioni 1.2 kutokana na gharama za matibabu na mifugo kukataliwa kuchinjwa . Amesema Tanzania imefanikiwa kudhibiti ugonjwa huo kwa kiasi kikubwa ambapo hadi sasa upo chini ya asilimia 1.5, lakini jitihada zaidi zinahitajika ili kuutokomeza kutokana na mbung’o wengi kuwepo maeneo yaliyo jirani na misitu na hifadhi za wanyama pori na hivyo kusababisha mifugo mingi kukondeana na hatimaye kufa kutokana na vim...

SEKTA YA MIFUGO YAENDELEA KUTOA MBEGU ZA MALISHO KWA WAFUGAJI

Picha
  Wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakishirikiana na mmoja wa wafugaji (katikati) kupima katika mzani kiasi cha mbegu kwa ajili ya kuziandaa ili zipandwe katika shamba la mfugaji lililopo katika Kata ya Itiso, Wilayani Chamwino, Mkoani Dodoma Februari 14, 2023. Sehemu ya Wafugaji na Viongozi wa Kata ya Itiso, Wilayani Chamwino, Mkoani Dodoma wakishiriki katika zoezi la upandaji wa malisho ya mifugo baada ya kupatiwa mafunzo na wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuhusu umuhimu wa kupanda malisho kwa ajili ya mifugo yao. Elimu hiyo ilitolewa Februari 14, 2023. Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali ya Vyakula vya Wanyama, Dkt. Asimwe Rwiguza (kushoto) akiongea na wafugaji wa Kata ya Itiso, Wilayani Chamwino, Mkoani Dodoma Februari 14, 2023 alipowatembelea kwa lengo la kuwahamasisha kuhusu ulimaji wa malisho ili waondokane na utegemezi wa malisho ya asili jambo ambalo limekuwa  likipelekea migogoro kati yao na watumiaji wengine wa Ar...

KIKAO CHA MPANGO WA UNYWAJI MAZIWA SHULENI CHAFANYIKA JIJINI DODOMA

Picha
  Msajili wa Bodi ya Maziwa Nchini, Dkt. George Msalya(aliyesimama) akiongea neno la utangulizi kuhusu mpango wa unywaji maziwa shuleni kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Steve Michael (wakatikati) kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, kilichofanyika Februari 14,2023, Ukumbi wa Royal Village, Dodoma. (Kulia) ni Afisa Tawala Mkuu, John Kusaja. Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw.Steve Michael (wakatikati) akiongea jambo kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, kuhusu namna bora ya kuweka mikakati muhimu ya kusaidia unywaji maziwa mashuleni ili kufikia malengo katika tasnia ya maziwa. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Royal Village, Dodoma 14 Februari 2023, (Kushoto) ni Msajili wa Bodi ya Maziwa Nchini, Dkt. George Msalya na (kulia) ni Afisa Tawala Mkuu,Bw. John Kusaja. Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Steve Michael (...