Nav bar

Jumatatu, 20 Februari 2023

KIKAO CHA MPANGO WA UNYWAJI MAZIWA SHULENI CHAFANYIKA JIJINI DODOMA

 

Msajili wa Bodi ya Maziwa Nchini, Dkt. George Msalya(aliyesimama) akiongea neno la utangulizi kuhusu mpango wa unywaji maziwa shuleni kabla ya kumkaribisha Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Steve Michael (wakatikati) kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, kilichofanyika Februari 14,2023, Ukumbi wa Royal Village, Dodoma. (Kulia) ni Afisa Tawala Mkuu, John Kusaja.

Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw.Steve Michael (wakatikati) akiongea jambo kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, kuhusu namna bora ya kuweka mikakati muhimu ya kusaidia unywaji maziwa mashuleni ili kufikia malengo katika tasnia ya maziwa. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Royal Village, Dodoma 14 Februari 2023, (Kushoto) ni Msajili wa Bodi ya Maziwa Nchini, Dkt. George Msalya na (kulia) ni Afisa Tawala Mkuu,Bw. John Kusaja.

Mkurugenzi wa Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Steve Michael (waliokaa katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe waliohudhuria kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Royal Village. Dodoma, 14 Februari 2023.

Wajumbe wa kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, wakiwa katika makundi kwa ajili ya kujadiliana na kuboresha Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni na kutoa mawasilisho ya maboresho waliyoyafanya kwa kila kikundi, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Royal Village,Dodoma Februari 14,2023.

Sehemu ya wajumbe waliohudhuria kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni wakiendelea na majadiliano kuhusu wasilisho la  rasimu ya mpango wa unywaji maziwa shuleni, kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Royal Village, Dodoma, Februari 14,2023.


Afisa Mifugo kutoka Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Edson Kilyenyi akiwasilisha mpango wa Unywaji maziwa shuleni kwa wajumbe waliohudhuria kwenye kikao cha kupitia Rasimu ya mpango wa unywaji maziwa mashuleni, katika ukumbi wa Royal Village, Dodoma Februari 14,2023.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni