Nav bar

Jumatano, 22 Februari 2023

NZUNDA ATOA MAELEKEZO KWA WATAFITI WA MIFUGO

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda amewataka watafiti wa mifugo kufanya tafiti zinazozingatia maslai ya nchi.

 

Nzunda ameyasema hayo (20.02.2023) wakati akifungua Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa jopo gesi (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro.

 

Watafiti wametakiwa kuzingatia malengo ya nchi katika kuleta mabadiliko kwenye sekta ya mifugo katika tafiti wanazozifanya ili kuongeza tija katika uzalishaji na sio kutumia tafiti hizo kwa matakwa ya wafadhili au maslai yao binafsi.

 

Pia watafiti wametakiwa kuzingatia utaalam, misingi ya maadili, uwajibikaji unaotokana na matendo na matokeo ya tafiti wanazozifanya ukiwemo utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa jopo gesi (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa.

 

Vilevile amewasihi watanzania kuziunga mkono taasisi za utafiti kwa kuwa sayansi huwa haisemi uongo, hivyo kupitia tafiti hizo mabadiliko kwenye sekta ya mifugo.

 

Nzunda amewataka maafisa ugani kuhakikisha wanayafikisha matokeo ya tafiti kwa wafugaji na kuhakikisha yanatumika. Aidha, maafisa ugani wametakiwa kuhakikisha wanawatembelea wafugaji na kutoa ushauri wao pale unapohitajika. Vilevile ameziagiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kuweka utaratibu wa kuwapima maafisa hao ili kuhakikisha wafugaji wanatembelewa.

 

Akiuzungumzia mradi huo, Mratibu wa mradi wa ADGG na Mtafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Duniani (ILRI), Dkt. Eliamoni Lyatuu amesema kuwa taasisi hiyo ya utafiti imekuwa ikifanya tafiti mbalimbali hapa duniani kwa kushirikiana na taasisi za utafiti za nchi husika.

 

Katika mradi huo, wamelenga kufanya utafiti utakaosaidia kuangalia athari za mazingira zinazosababishwa na mifugo, lengo likiwa ni kuhakikisha kuna kuwa na ufugaji wa ng’ombe kwa gharama nafuu na usioathiri mazingira.

 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti Tanzania, Prof. Erick Komba alieleza malengo ya taasisi hiyo katika kuhakikisha wafugaji wananufaika na tafiti mbalimbali zinazofanyika ili waweze kufuga kwa tija. Katika utafiti huo wanaokwenda kuufanya wataangalia pia vyakula vinavyotumika kwenye mifugo kama navyo vinamchango katika kuathiri mazingira.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda akifungua Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa gesi joto (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro ambapo amewasihi watafiti hao kuzingatia malengo ya nchi katika kuleta mabadiliko kwenye sekta ya mifugo katika tafiti wanazozifanya ili kuongeza tija katika uzalishaji. (20.02.2023)


Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Huduma za Ugani, Dkt. Dkt. Angello Mwilawa akizungumza wakati wa Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa gesi joto (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro ambapo alielezea namna wizara inavyoshirikiana na taasisi za utafiti wa mifugo. (20.02.2023)


Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti Tanzania, Prof. Erick Komba akieleza malengo ya taasisi hiyo katika kuhakikisha wafugaji wananufaika na tafiti mbalimbali zinazofanyika ili waweze kufuga kwa tija wakati wa Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa gesi joto (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro. (20.02.2023)


Mratibu wa mradi wa ADGG na Mtafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Duniani, Dkt. Eliamoni Lyatuu akitoa maelezo kwa washiriki kabla ya kufanyika kwa kazi za makundi wakati wa Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa gesi joto (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro. (20.02.2023)


Mratibu wa mradi wa ADGG na Mtafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Duniani, Dkt. Eliamoni Lyatuu akitoa maelezo kwa washiriki kabla ya kufanyika kwa kazi za makundi wakati wa Warsha ya Uzinduzi wa Mradi wa Utafiti wa Mifugo na Mazingira kwa lengo la kuchunguza utoaji wa gesi joto (GHC) na kupunguza gharama za chakula katika mifumo ya wafugaji wadogo wa ng’ombe wa maziwa iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Panama mkoani Kilimanjaro. (20.02.2023)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni