UGAWAJI WA MADUME BORA YA NG’OMBE NI UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MABADILIKO WA SEKTA YA MIFUGO - NDAKI
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amesema ugawaji wa madume ya bora ya ng’ombe ni utekelezaji wa mpango wa mabadiliko wa Sekta ya Mifugo. Waziri Ndaki ameyasema hayo leo (24.11.2022) wilayani Chamwino Mkoani Dodoma wakati alipokuwa anagawa madume bora 50 ya ng’ombe aina ya boran ambapo kila mmoja ana uwezo wa kupanda majike 25 kwa mwaka, kwa vikundi vya wafugaji kwa lengo la kwenda kuboresha mifugo yao ambayo mingi ni ya asili. “Mifugo mingi iliyopo hapa nchini ni ya asili na uzalishaji wake wa nyama na maziwa kwa mfugo ni ndogo, hivyo kwa kuanza kuboresha mifugo kwa kutumia madume haya pamoja na njia ya uhimilishaji kutasaidia wafugaji kuwa na mifugo michache ambayo itakuwa na uzalishaji mkubwa wa nyama na maziwa,” Alisema Ng’ombe wa asili huzalisha nyama kilo 80 -120 kwa ng’ombe wakati baada ya kuboreshwa kwa kosaafu mfugaji anaweza kupata kilo 150 – 200 kwa ng’ombe. Lakini pia kwenye upande wa maziwa ng’ombe hawa walioboreshwa kosaafu huwa na uwezo w...