Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2019

WAFUGAJI WA TANZANIA KUPITIA MRADI WA SAHIWAL WAZURU NCHINI KENYA

Picha
WAFUGAJI wa Tanzania kupitia Mradi wa Utafiti wa uboreshaji na utunzaji wa Mbari za ng’ombe aina ya Sahiwal wako nchini Kenya kwa ziara ya mafunzo yaliyoratibiwa na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa ufadhili wa Shirika la Kimataifa la AU-IBAR. Wafugaji hao kutoka Umoja wa Wafugaji wa Sahiwal Longido (UWASALO) wamekutana na wafugaji wa Transmara nchini Kenya wanaonufaika na ufugaji kwa kutumia teknolojia ya uhimilishaji na kuhifadhi na uendeleza nyanda za malisho ya mifugo. Akizungumza mara baada ya kutembelea wafugaji wa ng’ombe aina ya Sahiwal katika eneo la Kilgoris - Transmara, nchini Kenya, Mratibu wa Mradi huo wa Sahiwal kutoka Tanzania, Dk. Zebron Nziku amesema ziara hiyo imekuwa na tija kubwa kwa wafugaji wa Tanzania hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali inafanya mageuzi makubwa katika uboreshaji Koosafu za Mifugo. Dk. Nziku amesema mradi huo tayari umeendesha mafunzo yaliyohusisha wataalam na wafugaji kutoka Halmashauri ya Longido nchini Tan...

SHIRIKA LA KIMATAIFA LA AU-IBAR LAFADHILI MAFUNZO YA WAFUGAJI WA TANZANIA NA KENYA.

Picha
SHIRIKA la Kimataifa la AU-IBAR linalofadhili Mradi wa Utafiti wa uboreshaji na utunzaji wa Mbari za ng’ombe aina ya Sahiwal limefanikiwa kuwapeleka wafugaji wa Tanzania nchini Kenya kujifunza mbinu bora za uboreshaji mifugo. Mradi huo unaotelekezwa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) umewezesha kunufaisha wafugaji wengi wa jamii ya Kimasai katika Wilaya ya Longido Mkoa wa Arusha kuanza uboreshaji mifugo yao kupitia njia ya uhimilishaji. Akizungumza na wafugaji katika eneo la Kiligoris na Naivasha nchini wakati wa ziara ya mafunzo kwa wafugaji wa Tanzania, Mratibu Mwenza wa mradi huo kutoka TALIRI Makao Makuu Dodoma, Neema Urassa alisema mradi huo umeleta tija wafugaji wengi hasa katika Wilaya ya Longido. Urassa alisema katika utekelezaji wa mradi huo wafugaji mia moja kutoka wilayani Longido mkoani Arusha wamenufaika kwa kujengewa uwezo kupitia mafunzo ya utunzaji bora wa ng’ombe na ufugaji wa kibiashara wenye tija utakao...

DENI LA TSHS BIL. 7 LAWAWEKA PABAYA WADAIWA SUGU WA NARCO

Picha
Serikali imesema wadaiwa wote waliowekeza katika ranchi za taifa zinazomilikiwa na Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) walipe madeni yao kabla haijachukua hatua ya kuwanyang’anya maeneo na kuwafikisha mahakamani. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amesema hayo jijini Dodoma katika ofisi za makao makuu ya NARCO wakati akizungumza na wawekezaji waliopatiwa vitalu 111 katika ranchi za taifa zilizopo maeneo mbalimbali nchini kwa ajili ya kulisha mifugo yao ambapo hadi sasa wanadaiwa Tshs Bilioni Saba. “Lipeni bila shuruti, ahadi yangu kwenu mkifanya majukumu yenu ofisi yangu itawapatia ushirikiano wa kutosha, kama mheshimiwa rais akiendelea kuniacha hapa katika wizara hii wale ambao hawalipi watakuwa wamepoteza sifa za kuwa wawekezaji na siyo kwamba itaishia hapo tutachukua hatua za kisheria na watalipa deni ili kusudi watanzania wengine wawekeze ambao wanaweza kulipa hela ya serikali, hulipi nitakuondoa tena nitakufunga.” ...
Picha
ZIARA YA KATIBU MKUU UVUVI DKT. RASHID TAMATAMAH MKOANI RUKWA. Dkt. Rashid Tamatamah amesema mikakati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi hasa kwenye Sekta ya Uvuvi ni kuendeleza ufugaji samaki na kuangalia fursa za kuwekeza katika ufugaji samaki. Hayo yamebainishwa na katibu Mkuu Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah alipofanya ziara yake leo (15/07/2019) Mkoani rukwa ya kutembelea bwawa la Ilembo, Kiwanda cha kuchakata samaki cha Migebuka Fisheries, soko la Kasanga Pamoja na kuwatembelea Watumishi wa kituo cha Doria cha Kasanga. ▶ FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA UFUGAJI SAMAKI. Serikali ipo hapa na nia yetu ni kuja na kusikiliza changamoto zinazowakabili katika suala zima la ufugaji samaki. Serikali ipo hapa na nia yetu ni kuangalia fursa ya kukuza Tasnia ya ukuzaji viumbe maji hasa ufugaji wa samaki na kuwekeza katika malambo ambapo yakitunzwa vizuri yanaweza kutoa samaki wengi kwa wananchi. Katibu Mkuu Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah amesema hayo leo alip...

ZIARA YA JPM NAMIBIA, YAWAIBUA WAWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA MIFUGO NCHINI

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amemshukuru Rais Dkt. John Magufuli kufuatia ziara yake ya kikazi ya siku mbili aliyofanya nchini Namibia kuanzia Mei 27 hadi 28 Mwaka 2019, kuanza kuonesha mafanikio baada ya kupokea ugeni kutoka Kampuni ya Burmeister and Partners (PTY) Ltd inayomikili kiwanda cha kuchakata nyama nchini Namibia iliyoonesha nia ya kuwekeza hapa nchini. Akizungumza (09.07.2019) ofisini kwake katika mji wa serikali eneo la Mtumba Jijini Dodoma na mmoja wa wakurugenzi katika kampuni hiyo Bw. Hendrick Boshoff, Prof. Gabriel amesema lengo la ziara yake ni kupata taarifa za awali, kutoka kwa wataalam wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ili waweze kuwa na njia sahihi ya uwekezaji ambao utakuwa na tija kwa watanzania kupitia Sekta ya Mifugo. “Mheshimiwa rais alifanya ziara ya kikazi ya siku mbili nchini Namibia akiambatana na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina na viongozi wengine, nichukue fursa hii kwa nia...

NARCO WATAKIWA KUJIENDESHA KWA FAIDA NA KUTOA GAWIO SERIKALINI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeitaka Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) kubadilika na kufanya shughuli zake kwa tija ili iweze kunufaika na rasilimali ardhi na mifugo inayomiliki. Akizungumza wakati akitembelea na kujionea shughuli zinazofanywa katika ranchi za Ruvu iliyopo Mkoani Pwani na Mkata iliyopo Mkoani Morogoro jana (01.07.2019), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amezitaka ranchi hizo zilizo chini ya NARCO kuhakikisha zinatumia vitu ardhi inazomiliki ili kufuga mifugo itakayoongeza tija kwa taifa. Prof. Gariel akiwa katika Ranchi ya Ruvu amemuelekeza meneja wa ranchi hiyo Bw. Elisa Binamungu kuhakikisha ranchi hiyo inafuatilia pia madeni yote inayodai ili iweze kupata fedha na kujiendesha kwa kutumia fursa zilizopo za kuuza kwa tija mazao ya mifugo ikiwemo nyama na maziwa. “Lengo la ziara yangu ni kuhakikisha mnatekeleza agizo alilolitoa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina June 15 mwaka huu, alipokut...

KATIBU MKUU UVUVI AFUNGA MAFUNZO YA UFUATILIAJI UBORA NA UNADHIFU WA MAJI

Picha
Katibu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah amewataka washiriki wa mafunzo ya siku sita ya uelewa wa ufuatiliaji wa ubora na unadhifu wa maji na mazingira kuzingatia mafunzo hayo ili yawe na tija katika ukanda wa Bahari ya Hindi. Akizungumza jijini Dar es Salaam (30.06.2019) wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyokuwa yakifanyika katika Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) Dkt. Tamatamah amesema mafunzo hayo yaliyofadhiliwa na Serikali ya Watu wa China kupitia Sino-Africa Joint Research Centre (SAJOREC) na East African Great Lakes Urban Ecology (EAGLU) kwa kushirikiana na TAFIRI yanalenga kuboresha sekta ya uvuvi nchini pamoja na nchi zinazonufaika na Bahari ya Hindi pamoja na maziwa yaliyopo nchini. Kuhusu mafunzo hayo katibu mkuu huyo Dkt. Tamatamah amesema washiriki walipata mafunzo kupitia mihadhara iliyotolewa na wakufunzi wabobezi kutoka China na Tanzania pamoja na kukusanya takwimu kutoka mito iliyopo Mkoani Dar es Salaam na kuchakata ta...

HABARI PICHA

Picha
Kaimu  Mkurugenzi  Msaidizi  wa  Mazao  ya  Mifugo, Usalama  wa  Chakula  na  Lishe  Bw. Gabriel  Bura  mwenye  shati  la  mistari  (kulia),  Bw. John  Chobo  kushoto  pamoja  na picha  ya  pamoja  na  Afisa  Mfawidhi  kituo  cha  Uchunguzi  wa  Magonjwa  ya  Mifugo Mwanza  Bi. Subira  Samwel,  na  wafanyakazi  wa  kiwanda  cha  nyama  cha  Chobo  walipoenda  kutembelea  kiwanda  hicho  kilichopo  katika  Wilaya ya  Misungwi  jijini Mwanza Bw. Gabriel  Bura Kaimu  Mkurugenzi  Msaidizi  wa  Mazao  ya Mifugo  na  Usalama wa  Chakula  na  Lishe  akishuhudia  hatua  za  uchinjaji  wa  mbuzi  kuanzia mwanzo hadi kufikia hatua ya ku...

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAPONGEZWA KWA NIA YA KUANZISHA USHIRIKA WA WAFUGAJI WA ASILI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepongezwa kwa jitihada zake za kuboresha mazingira ya wafugaji nchini, baada ya kuanzisha mchakato wa uanzishwaji wa chama cha ushirika wa wafugaji wa ng’ombe wa asili. Akifungua semina iliyowahusisha wafugaji wa ng’ombe wa asili waliopo Wilayani Tunduru, Mkoani Ruvuma katibu tawala wa wilaya hiyo Bw. Ghaibu Lingo amesema ushirika huo utakapoanzishwa itakuwa rahisi kwa uongozi wa wilaya hiyo kutatua na kuwabaini wafugaji waliopo ili waweze kusaidiwa namna ya kukua kiuchumi na kuboreshewa mazingira ya maeneo ya ufugaji. Bw. Lingo amesema kupitia ushirikia huo pia itakuwa rahisi kwa serikali ya wilaya kufahamu idadi halisi ya ng’ombe wa asili waliopo wilayani hapo na mahitaji yanayotakiwa yakiwemo ya majosho na madawa kwa ajili ya kuwahudumia mifugo. Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Ugani kutoka Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Dkt. Pius Mwambene amesema kuanzishwa kwa chama cha ushirika wa wafugaji wa ng’ombe wa asili ni kati ya male...

SERIKALI YADHAMIRIA KUPUNGUZA UMASKINI KUPITIA ZAO LA NGOZI

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imedhamiria kupunguza umasikini kwa kuboresha kipato cha wafanyabiashara na kuongeza ajira kwa wananchi kupitia zao la ngozi hususan ngozi itokanayo na wanyama wafugwao hapa nchini. Hayo yamesemwa   na Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko, Dkt.Felix Nandonde wakati akifungua mafunzo ya wachunaji wa ngozi wa machinjio ya Manispaa ya Morogoro mjini humo. Dkt.Nandonde amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha kuwa washiriki wanaongeza utaalamu katika uchinjaji, uchunaji, ukaushaji, uhifadhi,usafirishaji na usindikaji ili kuzalisha ngozi bora itayokuwa na thamani zaidi. Akiongelea mchango wa zao la ngozi kwenye pato la Taifa na la mtu mmoja, mmoja, Dkt.Nandonde alisema kuwa hadi mwezi Machi mwaka 2018/19 jumla ya sh.bil.5.2 zilikusanywa kutokana na usafirishaji ngozi na bidhaa zake nje ya nchi. Akifafanua kuhusu sheria Na.18 ya Mwaka 2008, inayosimamia biashara ya ngozi nchini, Dkt.Nandonde alisema kuwa sheria hiy...

UTAYARI WA MATAIFA YETU KATIKA KUPAMBANA NA MAGONJWA YA MIFUGO.

Picha
Kwa sasa nchi ya Tanzania inauwezo wa kutengeneza dawa ya kudhibiti baadhi ya magonjwa ya mlipuko katika taasisi ya TVLA iliyopo Kibaha jijini Dar es salam, ikiwemo dawa ya ugonjwa Wa kimeta ambayo imeonekana kuwa tishio kwa Mifugo ,wanyamapori na binadamu. Alisema hayo Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kwenye ufunguzi wa zoezi la majaribio ya udhibiti Wa magonjwa ya milipuko katika eneo la mpaka Wa Namanga unaoinganisha nchi ya Tanzania na Kenya ,utakao endeshwa kwa siku nne na wanachama Wa jumuiya iliyofanyika Mpakani Namanga. Alieleza kuwa ,Wizara yake imejipanga vizuri dhidi ya magonjwa ya mlipuko kwa mifugo, na zoezi hili linaloendelea lipo chini ya umoja Wa afrika mashariki lakini wanashirikiana kwa pamoja katika kuhakikisha utayari Wa nchi wanachama unatekelezeka,hata sasa wamefanikiwa kudhibiti ugonjwa wa Kimeta ambao una athari kwa Mifugo,wanyamapori na binadamu Alifafanua kuwa,kuna wataalamu wakutosha wanaoshughulikia magonjwa haya pindi ya...