Nav bar

Jumatano, 17 Julai 2019


ZIARA YA KATIBU MKUU UVUVI DKT. RASHID TAMATAMAH MKOANI RUKWA.

Dkt. Rashid Tamatamah amesema mikakati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi hasa kwenye Sekta ya Uvuvi ni kuendeleza ufugaji samaki na kuangalia fursa za kuwekeza katika ufugaji samaki.

Hayo yamebainishwa na katibu Mkuu Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah alipofanya ziara yake leo (15/07/2019) Mkoani rukwa ya kutembelea bwawa la Ilembo, Kiwanda cha kuchakata samaki cha Migebuka Fisheries, soko la Kasanga Pamoja na kuwatembelea Watumishi wa kituo cha Doria cha Kasanga.

FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA UFUGAJI SAMAKI.

Serikali ipo hapa na nia yetu ni kuja na kusikiliza changamoto zinazowakabili katika suala zima la ufugaji samaki.

Serikali ipo hapa na nia yetu ni kuangalia fursa ya kukuza Tasnia ya ukuzaji viumbe maji hasa ufugaji wa samaki na kuwekeza katika malambo ambapo yakitunzwa vizuri yanaweza kutoa samaki wengi kwa wananchi.

Katibu Mkuu Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah amesema hayo leo alipopata fursa ya kutembelea bwawa la Ilembo na kuongea na Wananchi wa Kijiji cha Ilembo, Katika Wilaya ya Sumbawanga.

Lengo la ziara hii ni kuja kuangalia fursa ya maeneo ya kupandikiza samaki kwenye mabwawa,alisema Katibu Mkuu Uvuvi.

Malambo yanayoweka maji mwaka mzima tunataka kuyapandikiza samaki ili wananchi waendelee kupata samaki.

Vilevile kuangalia namna Wizara itakavyotoa mchango kwa Watanzania wanaopata changamoto ya kuingia katika ufugaji samaki.

Pia Dkt. Tamatamah alieleza kuwa, watu wahamasike kufuga samaki kwenye mabwawa na wasitegemee maziwa peke yake ili kujiongezea kipato.

UDHIBITI WA UTOROSHAJI SAMAKI, KULINDA VIWANDA VYA NDANI.

Katibu Mkuu Dkt. Rashid Tamatamah amesema nia ya Mh. Raisi Dkt. John Pombe Magufuli haitafikia ya Serikali ya viwanda kama malighafi yote inakimbizwa nchi za nje.

Alisema hayo leo wakati alipotembelea Kiwanda cha kuchakata samaki cha Migebuka Fisheries kilichopo Kasanga, Wilaya ya Kalambo.

Afisa Mfawidhi kituo cha Rukwa na Katavi Bw. Juma Makongororo amesema, Nguvu kazi ikiongezeka itasaidia kudhibiti uingizaji holela wa mazao ya Uvuvi na dhana haramu za uvuvi.

UIMARISHAJI WA SOKO LA KASANGA

Sisi kama Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kipaumbele chetu ni kuimarisha miundo mbinu ya masoko ya samaki.

Alisema hayo Katibu Mkuu Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah alipotembelea Soko la samaki la Kasanga, Wilaya ya Kalambo Leo na kuongea na uongozi wa eneo hilo la soko.

Kwa niaba ya Wizara napenda kuchukua nafasi hii kushukuru Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kwa juhudi ya kuendelea kuimarisha soko la Kasanga  alisema Katibu Mkuu.

Mara nyingi kuimarisha masoko ya ndani yanaongeza thamani ya samaki na kupata soko la nje na kusaidia kukuza uchumi wa nchi.

KIKAO KAZI KITUO CHA DORIA KASANGA
Katibu Mkuu Dkt. Rashid Tamatamah alipata wasaa wa kuongea na Watumishi wa kituo cha Doria cha Kasanga na kusikiliza changamoto za kazi zinazowakabili katika maeneo yao.



katibu Mkuu Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah afanya ziara yake leo (15/07/2019) Mkoani rukwa ya kutembelea kiwanda cha kuchakata Samaki cha Migebuka Fisheries kilichopo Kasanga
 



 katibu Mkuu Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah leo (15/07/2019) akutana na kuongea na Watumishi wa Kituo cha Doria cha Kasanga, Mkoani Rukwa


Attachments area




katibu Mkuu Uvuvi, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah afanya ziara yake leo (15/07/2019) Mkoani rukwa ya kutembelea bwawa la Ilembo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni