Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2023

HOTUBA YA BAJETI 2023/2024

Picha
 

MTAMBO WA KUZALISHA KIMIMINIKA NAIC WAZINDULIWA.

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe, amemshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuridhia jumla ya fedha Milioni 300 kwa ajili ya kununua mtambo wa Kimiminika (Liquid Nitrogen) kwa ajili ya kuhifadhia mbegu bora za ng'ombe. Prof.Shemdoe ameyasema hayo Jana  28 April, 2023 wakati  akizindua Mtambo huo wa Kuzalisha Kikiminika  (Liquid Nitrogen) kwa ajili ya kutunzia mbegu bora za ng'ombe wa nyama na maziwa katika kituo cha Taifa cha Uhimilishaji (NAIC) Arusha. "Tunamshukuru sana Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kwa kuridhia jumla ya fedha Milioni 300 ili kujazia katika  fedha  iliyotolewa na Bill & Melinda Gates Foundation Tsh milioni 432  kupitia shirika lisilokuwa la kiserikali la Land O'lakes na kufanya jumla ya Tsh 732 milioni zitumike kununua mtambo huo."Alisema Prof. Shemdoe. Prof. Shemdoe amesema kuwa kuwepo kwa mtambo huo sasa katika kituo cha Taifa c...

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO TANZANIA (TALIRI) CHAFANYIKA JIJINI DODOMA

Picha
  Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi) Bi. Agness Meena akisoma hotuba kwa Niaba ya Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe wakati wa ufunguzi wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kilichofanyika kwenye ukumbi wa African dream jijini Dodoma Aprili 28, 2023. Mkurugenzi  Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa MifugoTanzania  (TALIRI), Prof. Erick Komba akiongea na wajumbe wa baraza la wafanyakazi TALIRI  wakati wa kikao kifupi kilichofanyika  jijini Dodoma Aprili 28,2023. Katibu wa Chama cha wafanyakazi wa Taasisi za elimu ya juu, Sayansi, Ufundi stadi, habari na Utafiti (RAAWU), Bw. Bakari Shekimweri akieleza lengo la kuwa na chama cha wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kudumisha ushirikiano miongoni mwao wakati wa kikao kifupi cha wajumbe wa wafanyakazi hao kilichofanyika kwenye ukumbi wa African dream jijini Dodoma Aprili 28,2023. Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara  ya Utafiti, mafunzo na Ugani sehemu ya Hudu...

NDOTO YA RAIS, DKT. SAMIA KUIFUFUA NARCO YAANZA KUTIMIA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan imeiwezesha Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) kiasi cha Shilingi bilioni 4.65 kwa ajili ya kununua vitendea kazi na ng'ombe wazazi ili kuboresha na kuongeza uzalishaji wa kampuni hiyo. Hayo yamefahamika wakati wa ziara ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega aliyoifanya katika Ranchi ya Kongwa iliyopo Wilayani Kongwa, jijini Dodoma Aprili 27, 2023. Wakati akizindua matreka mapya matano (5) na kupokea ngo'mbe elfu moja (1000) kwa ajili ya kuboresha uzalishaji wa kampuni ya NARCO, Mhe. Ulega alimshukuru Mhe. Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha kampuni hiyo ili iweze kujiendesha kibiashara. Alisema lengo la Rais, Dkt. Samia ni kuiimarisha NARCO kwa kuboresha miundombinu na vitendea kazi ili waweze  kunenepesha ng'ombe, kuimarisha biashara ya nyama bora ya Kongwa Beef na kuzalisha malisho ya mifugo kwa wingi na kuyauza ndani n...

MAFUNZO YA UFUGAJI SAMAKI

Picha

MIAKA 59 MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

Picha
 

KIKAO KIFUPI CHA KUPOKEA WASILISHO LA MKAKATI WA UFUATILIAJI WA KIELEKTRONIKI WA ZAO LA PWEZA CHAFANYIKA WILAYANI YA KILWA, MKOA WA LINDI

Picha
  Kaimu Mkurugenzi  Msaidizi wa Udhibiti Ubora na Masoko kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Melkizedeck Koddy akiongea na watendaji kutoka Sekta ya Uvuvi na wawakilishi kutoka kwenye mradi wa Aqua - Farms  wakati wa kikao kifupi cha kupokea  wasilisho la mkakati wa ufuatiliaji wa kielektroniki wa zao la Pweza katika Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Wizara hiyo Mtumba jijini Dodoma. Aprili 25, 2023 Mtafiti kutoka kwenye Mradi wa Aqua-farm , Bw. Cretus Philipo  akiwasilisha mkakati wa ufuatiliaji wa kielektroniki wa zao la Pweza, uliofanyika  Wilayani  Kilwa Mkoani Lindi, wakati wa kikao kifupi kilichofanyika kwenye ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mtumba jijini Dodoma,  Aprili 25,2023. Sehemu ya washiriki wakifuatilia kwa makini  wasilisho la mkakati wa ufuatiliaji wa kielektroniki wa zao la Pweza lililofanyika kwenye Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi wakati wa kikao kifupi   kilichofanyika kwenye ukumbi ...

MIL 1O KWA KILA KIJANA KUFUGA KIBIASHARA

Picha
Na. Edward Kondela Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda amewaasa watanzania hususan vijana wanaopatiwa mafunzo ya unenepeshaji mifugo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo baada ya mafunzo hayo ya mwaka mmoja kila mmoja ataondoka na mtaji usiopungua Shilingi Milioni Kumi kufanya ufugaji kibiashara. Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Pinda ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Baraza la Kumshauri Rais Kuhusu Utekelezaji wa Masuala ya Kilimo na Chakula amebainisha hayo (24.04.2023), wakati alipofanya ziara ya siku moja Mkoani Tanga, kutembelea vituo atamizi vya wizara hiyo vinavyotekelezwa kupitia Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa ajili ya kutoa mafunzo ya vitendo ndani ya mwaka mmoja kwa vijana juu ya unenepeshaji ng’ombe katika kipindi cha miezi mitatu. Akiwa katika vituo hivyo kwa nyakati tofauti amesema ni vyema baada ya mafunzo vijana hao waliopo kwenye vituo atamizi vinane (8) kwenye maeneo mbalimbali nchini kufahamika katik...

MIL 1O KWA KILA KIJANA KUFUGA KIBIASHARA

Picha
Na. Edward Kondela Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda amewaasa watanzania hususan vijana wanaopatiwa mafunzo ya unenepeshaji mifugo na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo baada ya mafunzo hayo ya mwaka mmoja kila mmoja ataondoka na mtaji usiopungua Shilingi Milioni Kumi kufanya ufugaji kibiashara. Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Pinda ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Baraza la Kumshauri Rais Kuhusu Utekelezaji wa Masuala ya Kilimo na Chakula amebainisha hayo (24.04.2023), wakati alipofanya ziara ya siku moja Mkoani Tanga, kutembelea vituo atamizi vya wizara hiyo vinavyotekelezwa kupitia Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kwa ajili ya kutoa mafunzo ya vitendo ndani ya mwaka mmoja kwa vijana juu ya unenepeshaji ng’ombe katika kipindi cha miezi mitatu. Akiwa katika vituo hivyo kwa nyakati tofauti amesema ni vyema baada ya mafunzo vijana hao waliopo kwenye vituo atamizi vinane (8) kwenye maeneo mbalimbali nchini kufahamika katik...

JUKUMU LA KUHAKIKISHA UPATIKANAJI WA MALISHO SI LA SERIKALI PEKEE-DKT. MHINA

Picha
◼️ SUA yaanza utafiti wa nyasi za asili  Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imebainisha kuwa ni wajibu wa kila mdau aliyepo kwenye sekta ya ufugaji kuhakikisha upatikanaji wa malisho na maji ya kutosheleza mahitaji ya mifugo kwa kipindi chote cha mwaka unakuwa ni wa uhakika. Hayo yamesemwa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Charles Mhina wakati akifungua mkutano wa 13 wa wadau wa Nyanda za malisho nchini (RST) uliofanyika mkoani Morogoro Aprili 24,2023. “Katika miaka ya karibuni takwimu zimetuonesha kumekuwa na tatizo la ongezeko la vifo vya mifugo vilivyotokana na ukosefu wa malisho na maji katika baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na athari za mabadiliko ya tabia nchi hivyo kama tusipokabiliana na changamoto hii tutaendelea kupoteza tija kwenye ufugaji wetu” Ameongeza Dkt. Mhina. Dkt. Mhina ametoa rai kwa Mamlaka za Serikali za mitaa kuendelea kubainisha na kutenga maeneo kwenye halmashauri kwa ajili ya malisho ya mifugo huku pia akiwahimiza wafugaji kununua maen...

SHIRIKIANENI NA MAMLAKA HUSIKA ILI MCHANGO WA SEKTA YA UVUVI UONEKANE – MHE. SILINDE

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. David Silinde amezisihi nchi wanachama wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuungana na mamlaka zinazoshughulikia viwanda na biashara na takwimu kuhakikisha mchango wa sekta ya uvuvi unaonekana wazi kwenye pato la Taifa la kila nchi. Mhe. Silinde (Mb.) ametoa wito huo jijini Kampala, Uganda alipozungumza katika Mkutano wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika  Aprili 20,2023 jijini humo. Mhe. Silinde amesema kuwa suala hilo linatokana na ukweli kwamba mazao yanayotokana na uvuvi yanahesabiwa katika sekta za kilimo na uzalishaji na kuacha mazao mengine yakiingizwa katika mnyororo wa thamani wa sekta nyingine na kusababisha mchango wa sekta ya uvuvi katika uchumi wa nchi uonekane mdogo. Akizungumzia ulinzi wa rasilimali za uvuvi katika ziwa hilo Mhe. Silinde amesema uvuvi haramu na uvuvi uliopitiliza u...

TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA NCHI ZA EAC KULINDA RASILIMALI ZA UVUVI ZIWA VICTORIA

Picha
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kushirikiana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhakikisha rasilimali za Ziwa Victoria zinalindwa ili zinufaishe jamii zinazozunguka ziwa hilo na mataifa husika.   Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe aliyeongoza ujumbe kutoka Tanzania katika mkutano huo wa Tano wa Baraza la Mawaziri la Sekya Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Taasisi ya Uvuvi ya Ziwa Victoria (LVFO) ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika ngazi ya Makatibu Wakuu uliofanyika tarehe 19 Aprili, 2023 jijini Kampala, Uganda.   Prof. Shemdoe alisisitiza kuwa Tanzania inaendelea kudhibiti matumizi ya zana haramu za uvuvi, kupiga marufuku uvuvi wa samaki wachanga, kudhibiti utoroshaji wa mazao ya uvuvi na kuhamasisha ufugaji wa samaki kwa vizimba katika Ziwa Victoria bila kuathiri mazingira.   Pia alisema kuwa Tanzania imeimarisha udhibiti wa uingizwaji wa zana haramu za uvuvi na kuendesha ukaguzi w...

MKURUGENZI MICHAEL AZUNGUMZA NA WATAALAM KUTOKA SUA KUHUSU UWEZEKANO WA KUPATIWA MAENEO KWA AJILI YA KUANZISHA VITUO ATAMIZI

Picha
  Mkurugenzi, Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Stephen Michael (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wataalam kutoka Chuo cha Kilimo (SUA) muda mfupi baada ya kufanya nao majadiliano kuhusu uwezekano wa Wataalam hao kupatiwa sehemu katika maeneo ya kupumzishia mifugo ili  waanzishe vituo Atamizi kwa ajili ya kuwafundisha vijana kunenepesha mifugo na kuanzisha Kliniki ya mifugo kwa lengo la  kuwasaidia wafugaji.  Kulia kwake ni Kiongozi wa msafara wa Wataalam hao kutoka SUA, Prof. Elliot Phiri. Maeneo ambayo wanapendekeza wapatiwe ni pamoja na eneo la kupumzishia mifugo la Kizota lililopo Dodoma na Makuyuni lililopo Monduli, Mkoani Arusha. Kikao hicho kilifanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo katika Jengo la NBC jijini Dodoma Aprili 20, 2023. Wengine katika picha ni Wataalam kutoka Wizarani na Wataalam wengine kutoka SUA.

DKT. ASIMWE AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI WA MALISHO YA MIFUGO KATIKA SHAMBA LA VIKUGE. AELEZA MIPANGO YA SERIKALI YA KUTATUA CHANGAMOTO YA CHAKULA CHA MIFUGO NCHINI

Picha
  Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali ya Vyakula vya Wanyama, Dkt. Asimwe Rwiguza (kulia) akikagua maendeleo ya Shamba Darasa  la malisho ya mifugo lililopo katika Kijiji cha Wami Sokoine, Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, Mkoani Morogoro alipotembelea eneo hilo Aprili 19, 2023. kushoto ni  Mjumbe wa kikundi wa shamba darasa hilo, Bw. Jumbe Kamando.  Wizara imeanzisha mashamba darasa 100 katika Halmashauri 44 nchini ili wafugaji waweze kujifunza kwa vitendo namna ya kuandaa, kupanda, kutunza na kuhifadhi malisho ya mifugo. Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali ya Vyakula vya Wanyama, Dkt. Asimwe Rwiguza akiongoza zoezi la kupanda malisho katika shamba la malisho la mifugo la Vikuge lililopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani. Zoezi hilo lilifanyika shambani hapo Aprili 19, 2023.

WADAU WAKUTANA KUJADILI UTAFITI KUONGEZA THAMANI SAMAKI AINA YA DAGAA.

Picha
  Katibu Tawala mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana akisoma hotuba wakati wa ufunguzi wa warsha ya kupokea, kujadili na kupitisha taarifa ya matokeo ya utafiti wa upotevu wa mazao ya uvuvi Nchini, April 19,2023 Mkoani Mwanza Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uvuvi Tanzania Bi. Flora Luhanga akiongea na wadau wa uvuvi  (hawapo pichani) kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwa ufunguzi wa warsha ya kupokea, kujadili na kupitisha taarifa ya matokeo ya utafiti wa upotevu wa mazao ya uvuvi Nchini Aprili 19, 2023 Mkoani Mwanza. Mwenyekiti wa bodi ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) na mshauri mwelekezi wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO), Bw. Yahya Mgawe (katikati) akitoa maelezo ya dagaa waliochakatwa na kufungashwa na wavuvi wadowadogo  kwa Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana (wa pili kutoka kushoto) mara baada ya warsha ya kupokea, kujadili na kupitisha taarifa ya matokeo ya  utafiti wa upotevu wa mazao ya uvuvi Nchini, April 19, 2023 Mkoani ...