MKURUGENZI MICHAEL AZUNGUMZA NA WATAALAM KUTOKA SUA KUHUSU UWEZEKANO WA KUPATIWA MAENEO KWA AJILI YA KUANZISHA VITUO ATAMIZI

 

Mkurugenzi, Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Stephen Michael (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wataalam kutoka Chuo cha Kilimo (SUA) muda mfupi baada ya kufanya nao majadiliano kuhusu uwezekano wa Wataalam hao kupatiwa sehemu katika maeneo ya kupumzishia mifugo ili  waanzishe vituo Atamizi kwa ajili ya kuwafundisha vijana kunenepesha mifugo na kuanzisha Kliniki ya mifugo kwa lengo la  kuwasaidia wafugaji. 


Kulia kwake ni Kiongozi wa msafara wa Wataalam hao kutoka SUA, Prof. Elliot Phiri. Maeneo ambayo wanapendekeza wapatiwe ni pamoja na eneo la kupumzishia mifugo la Kizota lililopo Dodoma na Makuyuni lililopo Monduli, Mkoani Arusha.


Kikao hicho kilifanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo katika Jengo la NBC jijini Dodoma Aprili 20, 2023.

Wengine katika picha ni Wataalam kutoka Wizarani na Wataalam wengine kutoka SUA.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO