Nav bar

Alhamisi, 27 Aprili 2023

MKURUGENZI MICHAEL AZUNGUMZA NA WATAALAM KUTOKA SUA KUHUSU UWEZEKANO WA KUPATIWA MAENEO KWA AJILI YA KUANZISHA VITUO ATAMIZI

 

Mkurugenzi, Idara ya Uzalishaji na Maendeleo ya Masoko, Bw. Stephen Michael (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wataalam kutoka Chuo cha Kilimo (SUA) muda mfupi baada ya kufanya nao majadiliano kuhusu uwezekano wa Wataalam hao kupatiwa sehemu katika maeneo ya kupumzishia mifugo ili  waanzishe vituo Atamizi kwa ajili ya kuwafundisha vijana kunenepesha mifugo na kuanzisha Kliniki ya mifugo kwa lengo la  kuwasaidia wafugaji. 


Kulia kwake ni Kiongozi wa msafara wa Wataalam hao kutoka SUA, Prof. Elliot Phiri. Maeneo ambayo wanapendekeza wapatiwe ni pamoja na eneo la kupumzishia mifugo la Kizota lililopo Dodoma na Makuyuni lililopo Monduli, Mkoani Arusha.


Kikao hicho kilifanyika katika Ofisi ndogo za Wizara ya Mifugo na Uvuvi zilizopo katika Jengo la NBC jijini Dodoma Aprili 20, 2023.

Wengine katika picha ni Wataalam kutoka Wizarani na Wataalam wengine kutoka SUA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni