Nav bar

Jumamosi, 29 Aprili 2023

KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO TANZANIA (TALIRI) CHAFANYIKA JIJINI DODOMA

 

Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi) Bi. Agness Meena akisoma hotuba kwa Niaba ya Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe wakati wa ufunguzi wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kilichofanyika kwenye ukumbi wa African dream jijini Dodoma Aprili 28, 2023.


Mkurugenzi  Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa MifugoTanzania  (TALIRI), Prof. Erick Komba akiongea na wajumbe wa baraza la wafanyakazi TALIRI  wakati wa kikao kifupi kilichofanyika  jijini Dodoma Aprili 28,2023.


Katibu wa Chama cha wafanyakazi wa Taasisi za elimu ya juu, Sayansi, Ufundi stadi, habari na Utafiti (RAAWU), Bw. Bakari Shekimweri akieleza lengo la kuwa na chama cha wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kudumisha ushirikiano miongoni mwao wakati wa kikao kifupi cha wajumbe wa wafanyakazi hao kilichofanyika kwenye ukumbi wa African dream jijini Dodoma Aprili 28,2023.


Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara  ya Utafiti, mafunzo na Ugani sehemu ya Huduma za Ugani, Bw. Samwel Mdachi akitoa neno kwa wajumbe wa baraza la Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) (hawapo pichani) wakati wa kikao kifupi kilichofanyika jijini Dodoma, Aprili 28,2023.


Naibu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bi. Agness Meena (wa tano kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) mara baada ya kikao kifupi kilichofanyika kwenye ukumbi wa African dream jijini Dodoma Aprili 28,2023.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni