Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2023

MWELEKEO MPYA

Picha
 

ENEO LA KITARAKA KUTUMIKA KIMKAKATI KUZALISHA MIFUGO KIBIASHARA

Picha
Na Mbaraka Kambona, Singida Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amesema kuwa Serikali imedhamiria kulitumia eneo la kupumzishia mifugo la Kitaraka lililopo wilayani Manyoni, Singida  liweze kutumiwa na vijana watakao hitimu mafunzo katika vituo atamizi kwa ajili ya kufanya shughuli za uzalishaji wa mifugo  kibiashara ili kukuza uchumi wao na Taifa kwa ujumla. Mhe. Ulega alibainisha hayo wakati wa kikao baina yake na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Peter Serukamba (kushoto) alipokutana nae katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, mkoani Singida Januari 30, 2023.  Wakati wa mazungumzo yao, Mhe. Ulega alimueleza Mkuu wa Mkoa huyo kuwa lengo la ziara yake ni kujadiliana nae kuhusu dhamira ya Serikali ya kutaka kulitumia eneo la kitaraka kwa ajili ya kufanya shughuli za uzalishaji wa mifugo ili kuwawezesha vijana  kujipatia ajira lakini pia kuzalisha malighafi ya uhakika kwa ajili ya viwanda vya nyama na kuifanya sekta ya mifugo  kuchangia ipasa...

WAFUGAJI WANAOHAMA BONDE LA MTO KILOMBERO WASIZUIWE-NDAKI

Picha
◼️ Awashangaa watendaji wanaowawekea vikwazo  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amewaagiza viongozi na watendaji wote mkoani Morogoro kutowazuia wafugaji wanaohama kutoka bonde la Mto Kilombero ambapo amesema kuwa kufanya hivyo ni kukwamisha utekelezaji wa agizo la Serikali linalowataka wafugaji na wakulima kuondoka kwenye bonde hilo. Mhe. Ndaki amesema hayo jana (27.01.2023) kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya sekondari Nakaguru iliyopo  Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba mkoani Morogoro ambao ulijumuisha wafugaji na wakulima wanaozungukwa na bonde la Mto Kilombero. “Tangazo la Serikali la kuondoka kwenye  bonde la mto Kilombero ni sahihi na sisi wafugaji tunapaswa kuliheshimu kwa sababu ni lazima tuondoke kwenye bonde hilo kwa sababu ni tuna wajibu wa kulinda maeneo tengefu, oevu na yale yote yaliyotengwa na Serikali kwa ajili ya kufanya shughuli nyingine za maendeleo lakini cha kushangaza naambiwa kuna baadhi ya watendaji wanawazuia...

BILIONI 60 ZAWEKEZWA SEKTA YA UVUVI, NCHI ZA ULAYA ZAHAMASIKA KATIKA UFUGAJI SAMAKI

Picha
Na. Edward Kondela Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewekeza Shilingi Bilioni 60 katika Sekta ya Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2022-2023 ili kuinua kipato cha wananchi kupitia sekta hiyo. Akizungumza jijini Mwanza (26.01.2023) kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayesimamia Sekta ya Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah wakati wa ujio wa mabalozi nane kutoka Umoja wa Nchi za Ulaya kwenye Kampasi ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi Tanzania (FETA), Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Prof. Mohammed Sheikh amesema fedha hizo zimewekezwa kwa ajili ya kuongeza uzalishaji kwa kununua boti na wavuvi wadogo waweze kufika kwenye maji ya kina kirefu kuvua samaki ili kuongeza kipato. Prof. Sheikh amebainisha hayo baada ya ziara ya siku moja ya mabalozi hao katika Kampasi ya FETA iliyopo katika Kata ya Nyegezi, Wilaya ya Nyamagana ili kushuhudia majukumu mbalimbali ya FETA na mradi wa ufugaji samaki wanaoufadhili. Ameongeza kuwa ujio wa mabalozi hao ni wa kawaida ili k...

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SWIOFISH

Picha
  Mkurugenzi Mkuu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei  akiongea wakati wa kikao cha kupokea taarifa za utekelezaji wa mradi wa  SWIOFIC-Nairobi Convention  kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 27,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na Uvuvi Ili kuimarisha usalama wa Chakula kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla. Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bi. Julieth Evance akiwasilisha muhtasari wa kikao kilichopita cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi wa SWIOFIC-Nairobi Convention kwa wajumbe wa kamati hiyo (hawapo pichani) kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 27,2023 Mratibu wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention Bi. Ulrika Gunnartz akiwasilisha mada wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kilichofanyika  Mkoani Tanga Januari 27, 2023 Meneja wa Taasisi ya hifadhi za...

UTEKELEZAJI WA MWELEKEO MPYA WA SEKTA YA MIFUGO NCHINI

Picha
 

HERI YA SIKU YA KUZALIWA

Picha
 

​WAFUGAJI WANAOVAMIA MASHAMBA YA WAKULIMA NI WAHALIFU WASHUGHULIKIWE - NDAKI

Picha
Kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wakulima kwenye mikutano ya hadhara aliyoifanya jana (26.01.2023) kwenye kata za Ulaya na Mbwade Wilayani Kilosa, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki ameagiza wafugaji wote wanaovamia mashamba ya wakulima hao wakamatwe na wachukuliwe hatua za kisheria. Mhe. Ndaki amesema kuwa pamoja na kuwa ufugaji ni shughuli halali kama zilivyo nyingine, inapaswa kufanyika kwa kufuata taratibu na sheria bila kuathiri watumiaji wengine wa ardhi. "Yaani mkulima amelima mazao yake afu kwa makusudi mfugaji anaenda kulisha mifugo yake, huo ni uhalifu na matukio ya aina hii yakithibitishwa kuwa ni kweli basi naomba Mwenyekiti wa Chama cha wafugaji usihangaike hata kunipigia simu kwa sababu na mimi ntasisitiza watu hao wachukuliwe hatua za kisheria" Amesisitiza Mhe. Ndaki. Aidha Mhe. Ndaki ameuagiza uongozi wa Wilaya ya Kilosa kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya Sheria wataalam wote wanaopokea rushwa ili kuchochea migogoro hiyo ya wakulima na w...

SEKTA YA MIFUGO YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MAAGIZO KUHUSU MRADI WA UJENZI WA BWAWA KWA AJILI YA KUNYWESHEA MAJI MIFUGO KATOKA KIJIJI CHA CHAMAKWEZA WILAYANI CHALINZE MKOANI PWANI

Picha
  Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma akitoa maelezo mafupi kabla ya kufunga kikao cha kuwasilisha kwa Kamati taarifa ya Utekelezaji wa Maagizo kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kijiji cha Chamakweza kilichopo Chalinze Mkoani Pwani kilichofanyika jijini Dodoma leo Januari 25, 2023. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki akijibu baadhi ya hoja zilizoibuliwa na Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji wakati wa Kikao cha kuwasilisha kwa Kamati hiyo Taarifa ya Utekelezaji wa Maagizo kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kijiji cha Chamakweza kilichopo Chalinze Mkoani Pwani. Uwasilishaji wa taarifa hiyo umefanyika jijini Dodoma leo Januari 25, 2023. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akieleza jambo wakati wa Kikao cha kuwasilisha kwa Kamati ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji taarifa ya Utekelezaji wa Maagizo kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kijiji cha Chamakweza kilichopo Chalinze Mkoani Pwani kilic...

DKT. TAMATAMAH AKUTANA NA UJUMBE WA UBALOZI WA UINGEREZA KUTOKA SHIRIKA LA FEDHA LA UINGEREZA (UK EF)

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (katikati) akiwa kwenye mazungumzo na ujumbe wa Ubalozi wa Uingereza kutoka Shirika la Fedha la Uingereza (UK EF) katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma juu ya ushirikiano baina ya wizara na shirika hilo kwenye ujenzi wa bandari ya uvuvi katika eneo la Kilwa Masoko, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi. (25.01.2023) Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah akiuonesha ujumbe wa Ubalozi wa Uingereza kutoka Shirika la Fedha la Uingereza (UK EF), (hawapo pichani) mchoro wa bandari ya uvuvi inayojengwa katika eneo la Kilwa Masoko, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi kwa thamani ya Shilingi Bilioni 266 ambapo ujenzi huo unatarajiwa kukamilika Mwezi Septemba Mwaka 2024. Mazungumzo na ujumbe huo juu ya ushirikiano katika ujenzi wa bandari ya uvuvi baina ya wizara na shirika hilo, yamefanyika katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. (25.01.2023) Baadhi ya viongozi kutoka Wizar...

SERIKALI YAPOKEA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UVUVI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) imepokea taarifa ya utekelezaji wa mradi wa usimamizi wa pamoja wa rasilimali za uvuvi na mazingira ya bahari SWIOFIC -Nairobi Convention   unaofadhiliwa na Serikali ya Sweden kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa (SIDA) Akizungumza mara baada ya kupokea ripoti hiyo kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Sekta ya Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Ismael Kimirei, amesema kuwa mradi huo unatekelezwa kwa miaka mitano tangu 2019 na unatarajiwa kumalizika mwezi Disemba 2023 Amesema lengo la mradi kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira, kuimarisha rasilimali za Uvuvi na kuboresha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla "Mradi huu unafanyika kwa majaribio kwa upande wa Tanzania, Madagascar na Msumbiji, baada ya hapo matokeo yatakayotokana na mradi huu yatatumika kama mfano katika nchi nyingine hasa katika nchi za Magharibi mwa Bahari ya Hindi am...

​SERIKALI YATAKA USIMAMIZI MZURI ZAIDI WA SEKTA YA UVUVI, KUFIKIA MALENGO ENDELEVU

Picha
Serikali imedhamiria kuimarisha usimamizi  wa rasilimali za uvuvi nchini ili kuwezesha Sekta ya uvuvi kuendelea kuchangia katika kuleta maendeleo endelevu ikiwa ni miongoni mwa sekta za kiuchumi zinazotoa ajira, kuimarisha usalama wa chakula, maisha ya watu pamoja na  kuongeza mapato ya nje na ndani ya nchi. Hayo yamesemwa Januari 24,2023 mjini Tanga na Mkurugenzi Msaidizi wa  Uendelezaji wa Rasilimali za Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Merisia Mparazo wakati wa ufunguzi wa kikao cha kamati ya wataalam wa  mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention. Alisema kuwa mradi huo unahakikisha kwamba kunakua na ushirikino  katika usimamizi wa  masuala ya Bahari na mazingira yake pamoja na rasilimali za Uvuvi zilizomo nchini. Aidha alibainisha kuwa sekta hiyo imeajiri zaidi ya watu milioni 4.5 wanaojihusisha na shughuli za uvuvi na zile zinazohusiana  na uvuvi wakati takribani 194,804 ni ajira za moja kwa moja kwa wavuvi na watu 31,998 wameajiriwa katika ta...
Picha
  Mkurugenzi wa huduma za Mifugo nchini Prof. Hezron Nonga akifafanua jambo wakati wa kikao cha wadau mbalimbali wa sekta ya Mifugo waliokutana leo (24.01.2023)  kwenye ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi uliopo eneo la Mtumba jijini Dodoma ili kujadili rasimu ya Mwongozo ulioboreshwa wa Utambuzi wa Mifugo. Sehemu ya wadau wa sekta ya Mifugo wakipitia rasimu ya Mwongozo ulioboreshwa wa utambuzi wa Mifugo wakati wa kikao cha kujadili rasimu hiyo kilichofanyika leo (24.01.2023) kwenye Ukumbi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi uliopo eneo la Mtumba jijini Dodoma.

WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO ILIYOGHARAMIWA KWA FEDHA ZA MKOPO KUTOKA SHIRIKA LA FEDHA LA KIMATAIFA (IMF) KUPITIA DIRISHA LA EXTENDED CREDIT FACILITY (ECF) KWA KIPINDI CHA NUSU MWAKA KUANZIA JULAI HADI DISEMBA 2022 KWENYE KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI

Picha
  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti wakati Wizara ilipowasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyogharamiwa kwa fedha za Mkopo kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kupitia dirisha la Extended Credit Facility (ECF) kwa kipindi cha Nusu Mwaka kuanzia Julai hadi Disemba 2022. (23.01.2023) Katibu Mkuu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda (wa pili kutoka kushoto) akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizoulizwa na Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti wakati Wizara ilipowasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo iliyogharamiwa kwa fedha za Mkopo kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kupitia dirisha la Extended Credit Facility (ECF) kwa kipindi cha Nusu Mwaka kuanzia Julai hadi Disemba 2022. (23.01.2023) Katibu Mkuu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (kushoto) akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na Wajumbe wa Kamati ya...