Nav bar

Ijumaa, 27 Januari 2023

DKT. TAMATAMAH AKUTANA NA UJUMBE WA UBALOZI WA UINGEREZA KUTOKA SHIRIKA LA FEDHA LA UINGEREZA (UK EF)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (katikati) akiwa kwenye mazungumzo na ujumbe wa Ubalozi wa Uingereza kutoka Shirika la Fedha la Uingereza (UK EF) katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma juu ya ushirikiano baina ya wizara na shirika hilo kwenye ujenzi wa bandari ya uvuvi katika eneo la Kilwa Masoko, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi. (25.01.2023)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah akiuonesha ujumbe wa Ubalozi wa Uingereza kutoka Shirika la Fedha la Uingereza (UK EF), (hawapo pichani) mchoro wa bandari ya uvuvi inayojengwa katika eneo la Kilwa Masoko, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi kwa thamani ya Shilingi Bilioni 266 ambapo ujenzi huo unatarajiwa kukamilika Mwezi Septemba Mwaka 2024. Mazungumzo na ujumbe huo juu ya ushirikiano katika ujenzi wa bandari ya uvuvi baina ya wizara na shirika hilo, yamefanyika katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. (25.01.2023)


Baadhi ya viongozi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) wakiwa kwenye kikao cha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah wakati wa mazungumzo na ujumbe wa Ubalozi wa Uingereza kutoka Shirika la Fedha la Uingereza (UK EF) katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma juu ya ushirikiano baina ya wizara na shirika hilo kwenye ujenzi wa bandari ya uvuvi katika eneo la Kilwa Masoko, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi. (25.01.2023)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Rashid Tamatamah (wanne kutoka kushoto mstari wa mbele) akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe wa Ubalozi wa Uingereza kutoka Shirika la Fedha la Uingereza (UK EF) na baadhi ya viongozi wa wizara Sekta ya Uvuvi, baada ya mazungumzo juu ya ushirikiano baina ya wizara na shirika hilo katika ujenzi wa bandari ya uvuvi inayojengwa katika eneo la Kilwa Masoko katika Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi. Mazungumzo na ujumbe huo juu ya ushirikiano katika ujenzi wa bandari ya uvuvi baina ya wizara na UK EF, yamefanyika katika ofisi za wizara hiyo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. (25.01.2023)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni