Nav bar

Ijumaa, 27 Januari 2023

SERIKALI YAPOKEA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA UVUVI


Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) imepokea taarifa ya utekelezaji wa mradi wa usimamizi wa pamoja wa rasilimali za uvuvi na mazingira ya bahari SWIOFIC -Nairobi Convention  unaofadhiliwa na Serikali ya Sweden kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa (SIDA)

Akizungumza mara baada ya kupokea ripoti hiyo kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Sekta ya Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), Dkt. Ismael Kimirei, amesema kuwa mradi huo unatekelezwa kwa miaka mitano tangu 2019 na unatarajiwa kumalizika mwezi Disemba 2023

Amesema lengo la mradi kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira, kuimarisha rasilimali za Uvuvi na kuboresha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla

"Mradi huu unafanyika kwa majaribio kwa upande wa Tanzania, Madagascar na Msumbiji, baada ya hapo matokeo yatakayotokana na mradi huu yatatumika kama mfano katika nchi nyingine hasa katika nchi za Magharibi mwa Bahari ya Hindi ambako utatekelezwa mradi mkubwa zaidi" amesema

Ameeleza kuwa Serikali ya awamu ya sita inaendelea na jitihada za kuboresha mazingira ya uvuvi hasa Ukanda wa Pwani ikiwemo kuanzisha miradi mikubwa ya kuendeleza miradi ambayo imekwisha muda wake

"Nia ni kuona uzalishaji katika dhana pana ya uchumi wa bluu inafanya kazi na wananchi wetu wanapata maboresho kwa maana ya kupata kipato na lishe bora kwa kuzingatia usalama wa chakula ili kuinua uchumi wao binafsi na uchumu wa taifa kwa ujumla

Aidha amebainisha kuwa pamoja na mambo mengine Serikali imeendelea na jitihada za kuboresha sekta ya uvuvi ikiwemo kuanzisha ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa Masoko na Zanzibar

Amewataka wananchi na wavuvi kuwa tayari kupokea fursa zote zinazoletwa kupitia miradi mbalimbali ili kuungana na Serikali ya awamu ya sita ambayo imejikita pia katika kuendeleza kutekeleza miradi hiyo pindi inapomalizika.


Mkurugenzi Mkuu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei akiongea wakati wa kufungua  kikao cha kupokea taarifa za utekelezaji wa mradi wa  SWIOFIC- Nairobi Convention  kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 26,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na Uvuvi Ili kuimarisha usalama wa Chakula kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla.

Mkurugenzi Mkuu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa kamati ya wataalam wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention mara baada ya kikao cha kupokea taarifa za utekelezaji wa mradi huo kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 26, 2023.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni