Nav bar

Jumanne, 31 Januari 2023

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA MRADI WA SWIOFISH

 

Mkurugenzi Mkuu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei  akiongea wakati wa kikao cha kupokea taarifa za utekelezaji wa mradi wa  SWIOFIC-Nairobi Convention  kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 27,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na Uvuvi Ili kuimarisha usalama wa Chakula kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla.

Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bi. Julieth Evance akiwasilisha muhtasari wa kikao kilichopita cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi wa SWIOFIC-Nairobi Convention kwa wajumbe wa kamati hiyo (hawapo pichani) kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 27,2023

Mratibu wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention Bi. Ulrika Gunnartz akiwasilisha mada wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kilichofanyika  Mkoani Tanga Januari 27, 2023

Meneja wa Taasisi ya hifadhi za Bahari na maeneo Tengefu (MPRU) Dkt.Sware Semesi akiuliza maswali wakati  wa kikao cha kupokea taarifa za utekelezaji wa mradi wa SWIOFIC - Nairobi Convention kutoka kwa wataalam wa mradi huo  kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 27, 2023.

Mkurugenzi Msaidizi uendelezaji wa rasilimali za Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Merisia Mparazo akichangia hoja wakati  kikao cha kupokea taarifa za utekelezaji wa mradi wa SWIOFIC-Nairobi Convention  kilichofanyika Mkoani Tanga Januari 27,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na Uvuvi Ili kuimarisha usalama wa Chakula kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla.

Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Bi. Asha Churu (wa pili kutoka kulia) akionyesha eneo la mwalo wa Kwale Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei (wa tatu kutoka kulia)  walipoenda kutembelea  Januari 27,2023.

Mkurugenzi Mkuu kutoka Taasisi ya Utafiti wa  Uvuvi Tanzania (TAFIRI) (wa tatu kutoka kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki wa kamati ya wataalam wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention na baadhi ya wavuvi wa mwalo wa Kwale mara baada ya kutembelea mwalo huo Mkoani Tanga Januari 27, 2023.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni