Nav bar

Jumatano, 25 Januari 2023

​SERIKALI YATAKA USIMAMIZI MZURI ZAIDI WA SEKTA YA UVUVI, KUFIKIA MALENGO ENDELEVU

Serikali imedhamiria kuimarisha usimamizi  wa rasilimali za uvuvi nchini ili kuwezesha Sekta ya uvuvi kuendelea kuchangia katika kuleta maendeleo endelevu ikiwa ni miongoni mwa sekta za kiuchumi zinazotoa ajira, kuimarisha usalama wa chakula, maisha ya watu pamoja na  kuongeza mapato ya nje na ndani ya nchi.


Hayo yamesemwa Januari 24,2023 mjini Tanga na Mkurugenzi Msaidizi wa  Uendelezaji wa Rasilimali za Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bi. Merisia Mparazo wakati wa ufunguzi wa kikao cha kamati ya wataalam wa  mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention.


Alisema kuwa mradi huo unahakikisha kwamba kunakua na ushirikino  katika usimamizi wa  masuala ya Bahari na mazingira yake pamoja na rasilimali za Uvuvi zilizomo nchini.


Aidha alibainisha kuwa sekta hiyo imeajiri zaidi ya watu milioni 4.5 wanaojihusisha na shughuli za uvuvi na zile zinazohusiana  na uvuvi wakati takribani 194,804 ni ajira za moja kwa moja kwa wavuvi na watu 31,998 wameajiriwa katika tasnia  ya ukuzaji  viumbe maji.


Aliongeza kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ina jukumu la kusimamia na kuendeleza rasilimali za uvuvi nchini kwa kuhakikisha ustawi wa jamii ya wavuvi.


Alisema Serikali itaimarisha usimamizi wa rasilimali za Uvuvi na kuboresha maisha ya jamii za wavuvi katika Wilaya ya Nkinga kupitia mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention.


"Lengo la mradi linaendana na sera ya taifa ya uvuvi ya mwaka 2015 inayoeleza kuwa rasilimali za uvuvi zinaendelezwa, zinasimamiwa, zinahifadhiwa na kutumika kwa uendelevu kwa ajili ya ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya binadamu", alisema.


Mkurugenzi Msaidizi uendelezaji wa rasilimali za Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Merisia Mparazo akiongea wakati wa kufungua  kikao cha wataalam wa mradi wa SWIOFIC-Nairobi Convention  kilichofanyika kwenye Wilaya ya Nkinga Mkoani Tanga Januari 24,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na Uvuvi Ili kuimarisha usalama wa Chakula kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla.


Mratibu wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention Bi. Ulrika Gunnartz akiwasiliasha mada wakati wa kikao cha kamati ya wataalam wa mradi huo kilichofanyika kwenye Wilaya ya Nkinga Mkoani Tanga Januari 24, 2023


Mratibu wa Sekta ya Uvuvi kitaifa kutoka Shirika la chakula na kilimo la umoja wa Mataifa (FAO), Bi. Olivia Mkumbo (wa pili kutoka kushoto) akiwasilisha mada wakati wa kikao cha kamati ya wataalam wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention kilichofanyika kwenye Wilaya ya Nkinga Mkoani Tanga Januari 24,2023


Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Bw. Tumaini Chambua akiwasilisha mada wakati wa  kikao cha kamati ya wataalam wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention kilichofanyika kwenye Wilaya ya Nkinga Mkoani Tanga Januari 24,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira na Uvuvi Ili kuimarisha usalama wa Chakula kushughulikia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya jamii za wavuvi kwa ujumla.


Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais ambae pia ni Afisa kiungo wa Nairobi Bi. Magdalena Ngotolainyo akiwasilisha  mada wakati wa kikao cha kamati ya wataalam wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention kilichofanyika kwenye Wilaya ya Nkinga Mkoani Tanga Januari 24,2023 lengo likiwa ni pamoja na kuwezesha ushirikiano katika masuala ya usimamizi wa mazingira Ili kuimarisha usalama wa Chakula, kushughulikia mabadiliko ya tabia nchi na kuimarisha maisha ya  jamii za wavuvi kwa ujumla.


Sehemu ya washiriki wa kikao cha kamati ya wataalam wa mradi wa SWIOFIC -Nairobi Convention wakisikiliza kwa makini mada zilizokuwa zikitolewa na wawezeshaji (hawapo pichani) wa kikao hicho kilichofanyika kwenye Wilaya ya Nkinga Mkoani Tanga Januari 24,2023.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni