KAMBAMITI KUPEWA KIPAUMBELE KATIKA KUKUZA SEKTA YA UVUVI - DKT. TAMATAMAH
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah amesema Rasilimali ya samaki aina ya kambamiti ni muhimu katika kutoa ajira, kipato, chakula na lishe, na kuliingizia Taifa fedha za kigeni kama aina nyingine za samaki na hivyo kuchangia katika kupunguza umaskini kwa wananchi. Dkt. Tamatamah aliyasema hayo wakati wa kikao na wakuu wa idara, Taasisi na Vitengo wa sekta hiyo kujadili juu ya rasimu ya mpango wa usimamizi wa zao la kambamiti kilichofanyika jijini Dodoma Mei 23, 2022. Alisema wote tunafahamu kuwa, kabla ya mwaka 2007, uvuvi wa kambamiti ulikuwa ukifanywa na wavuvi wote wakubwa na wadogo, na mwaka 2007 uvuvi huo ulifungwa kwa wavuvi wakubwa kufuatia taarifa za utafiti zilizothibitisha kuendelea kupungua kwa rasilimali hiyo na hivyo kutisha uendelevu wake. Hivyo kufuatia changamoto hiyo mwaka 2012, Serikali iliandaa mpango wa usimamizi wa rasilimali ya kambamiti wa miaka mitano ulioanza kutekelezwa mwaka 2013 na kuisha muda wake mwaka...