Nav bar

Jumanne, 24 Mei 2022

WAFUGAJI ACHENI KUTOROSHA MIFUGO KWENDA NCHI JIRANI-NZUNDA

Katibu Mkuu Mifugo Bw.Tixon Nzunda amekemea Vikali tabia ya wafugaji kutorosha Mifugo na kwenda kuuza nchi jirani ya Kenya kwa kukwepa kulipa Ushuru na  tozo halali za serikali.


"Wafugaji wetu wanatorosha Mifugo na kwenda kuuza nchi jirani, kwa kukwepa kulipa tozo na Ushuru halali wa Serikali,wanapitisha Mifugo hiyo katika njia zisizo rasmi,na kibaya zaidi kuna baadhi ya watumishi wa Umma na Polisi wasiokuwa waaminifu wanashiriki utoroshaji huo. Alisema Nzunda"


Hayo ameyasema jana 17 May 2022 alipokuwa Mkoani Tanga akikagua miradi mbalimbali ya  Maendeleo ya Sekta Mifugo.


Nzunda amesema kuwa Tanzania ni nchi ya pili barani Africa kuwa na Mifugo mingi ikitanguliwa na Ethiopia, lakini Sekta hiyo ya Mifugo inachangia asilimia 7.1 tu katika pato la Taifa,amewaasa wafugaji hao na watumishi wa Serikali wasiokuwa waaminifu wanaoshiriki zoezi la utorosha Mifugo nje ya nchi kuacha mara moja.


"Unajua Sekta hii ya Mifugo inaweza kuchangia katika pato la taifa hata kwa asilimia 15 mpaka 20, kama wafugaji wetu wakikubali kubadili fikra zao na kuanza kufuga kisasa wakaacha mtindo wa Sasa wa uswagaji wa Mifugo, kwani Botswana wanamaajabu gani, wanamifugo michache lakini inachangia katika pato la taifa kwa asilimia nyingi kuliko sisi wenye Mifugo Mingi" Alisema Nzunda.


Aidha, Nzunda amesema kuwa kwa muda wa Miezi mitatu tangu ateuliwe kuongoza Sekta ya Mifugo, ametengeneza Mpango Makakati wa kubadilisha Sekta ya Mifugo Nchini ambapo kwa sasa suala la kuogesha,kuchanja na kuzalisha Malisho ya Mifugo kwa wafugaji litakuwa sio jambo la hiari tena,bali ni lazima.


"Wafugaji ni wawekezaji kama wawekezaji wengine,mpango huu mkakati wa kubadilisha Sekta ya Mifugo unawataka wafugaji wachanje ,waogeshe ,walime Malisho na wachimbe malambo na Visima vya maji kwa ajili ya Mifugo yao kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, lengo ikiwa ni kupata Mifugo bora itakayotupatia nyama bora ili tuweze kuuza nyama hiyo nje ya  nchi kwa sababu Masoko yapo" Alisema nzunda.


Vilevile, Nzunda amesema kuwa kwa mwaka fedha 2022/2023 Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) itaanza utekelezaji wa Mkataba wa kazi "performance Contract" hii itasaidia kwa maafisa ugani  kuhakikisha wanakuwa na Registaya wafugaji walio wahudumia kwa wiki, Mwezi na mfugaji huyo atatakiwa kusaini katika regista hiyo kukubali kuwa amepokea huduma hiyo, hii itasaidia watumishi kutokufanya kazi kwa Mazoea. 


Pia, katibu Mkuu huyo wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) amewataka Sekretarieti za Mikoa na Serikali za Mitaa kuhakikisha zinasimamia miradi yote ya Maendeleo inayopelekwa kwenye mamlaka hizo na Wizara za kisekta ili kuhakikisha wanawabana wakandarasi wanaotekeleza Miradi hiyo ili wasifanye kazi chini ya kiwango.


"Miradi yote inayoletwa na Wizara hizi za kisekta au na Serikali kuu, hakikisheni Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri miradi hiyo mnaisimamia vyema maana ni kwa wafaida ya wananchi wa maeneo husika"


Kwa Upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Bi.Pili mnyema alimshukuru Katibu Mkuu Mifugo kwa kutembelea mkoa huo na kufanya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo ya Sekta ya Mifugo na kuahidi kushirikiana na mamlaka za Serikali za Mitaa kuanza kuifuatilia kwa Ukaribu miradi hiyo.


Aidha, Bi Mnyema alikiri uwepo wa changamoto ya wafugaji kutoroshaji Mifugo nje ya nchi katika mkoa huo,na alisema kuwa wao kama mkoa wanajitahidi kufanya doria ili kuzuia utoroshwaji huo wa mifugo lakini shida kubwa ni uhaba wa vitendea kazi kwa ajili ya  utekelezaji wa kazi hiyo ya doria.


Awali Nzunda alitembelea kiwanda cha Maziwa cha Tanga, alikagua mradi wa  mnada wa Mpakani wa Horohoro unaoendelea kutekelezwa na kampuni ya V. J. MISTRY na kumwagiza Mkandalasi huyo kufanya kazi kwa kasi vinginevyo ifikapo 15 june 2022 ataanza kukatwa "liquidation"

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixson Nzunda akiagana na Mkurugenzi Mtendani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Bi.Veronica Zahara (Kushoto) mara baada ya kumaliza ukaguzi wa mnada wa Mpakani wa Horohoro jana tarehe 17/05/2022 Mkoani Tanga.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Bw.Tixon Nzunda (kushoto) akionyeshwa Ramani ya Mnada wa Mpakani wa Horohoro mkoani Tanga na Site Eng.Rweshogora jana tarehe 17/05/2022 baada ya kutembelea Mnada huo.Lengo la ziara hiyo ni kukagua miradi ya maendeleo ya Sekta ya Mifugo.

Mwonekano wa Mnada wa Mpakani wa Horoboro uliopo Mkoani Tanga.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni