MWEKEZAJI MKOANI MARA KUJENGA KIWANDA CHA NYAMA.
Mwekezaji katika sekta ya mifugo mkoani Mara, Mh. Vedastus Matayo, ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Musoma mjini, baada ya kutembelewa na Dawati la sekta binafsi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ameamua kuanzisha kiwanda cha nyama mkoani hapo ili kuboresha soko la mifugo katika mkoa huo na ajira watanzania. Hayo yalibainishwa hivi karibuni na Mbunge huyo wakati alipotembelewa na Dawati la sekta binafsi katika maeneo ya shughuli zake za ufugaji Wilayani Sengereti na Bunda, kwa lengo la kuibua na kushawishi kuwekeza kibiashara kwa Mbunge huyo. Mbunge huyo aliwambia wataalam hao wa Dawati kuwa ana mifugo aina, Ng’ombe zaidi ya 2000 aina ya Borani ambao ndiyo wengi na aina nyingine ya semental ambao ni wachache, mbuzi zaidi ya 2500 na kondoo zaidi ya 1000, mifugo yote hii iko wilaya za Bunda na Sengereti. Aidha aliwaeleza aina ya ufugaji anaofuga wa kugoresha mifugo hiyo ya asili kwa njia ya uhimilishaji kwa kuchukua mbegu bora za mifugo toka NAIC Arus...