Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2019

MWEKEZAJI MKOANI MARA KUJENGA KIWANDA CHA NYAMA.

Picha
Mwekezaji katika sekta ya mifugo mkoani Mara, Mh. Vedastus Matayo, ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Musoma mjini, baada ya kutembelewa na Dawati la sekta binafsi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ameamua kuanzisha kiwanda cha nyama mkoani hapo ili kuboresha soko la mifugo katika mkoa huo   na ajira watanzania. Hayo yalibainishwa hivi karibuni na Mbunge huyo wakati alipotembelewa na Dawati la sekta binafsi   katika maeneo ya shughuli zake za ufugaji Wilayani Sengereti na Bunda, kwa lengo la kuibua na kushawishi kuwekeza kibiashara kwa Mbunge   huyo. Mbunge huyo aliwambia wataalam hao wa Dawati kuwa ana mifugo aina, Ng’ombe zaidi ya 2000 aina ya Borani ambao ndiyo wengi na aina nyingine ya semental ambao ni wachache, mbuzi zaidi ya 2500 na kondoo zaidi ya 1000, mifugo yote hii iko wilaya za Bunda na Sengereti. Aidha aliwaeleza aina ya ufugaji anaofuga wa kugoresha mifugo hiyo ya asili kwa njia ya uhimilishaji kwa kuchukua mbegu bora za mifugo toka NAIC Arus...

SERIKALI IMEANDAA SHERIA MPYA YA UKUZAJI VIUMBE MAJI

Picha
Serikali imeandaa sheria mpya ya ukuzaji viumbe maji ili kuboresha sheria ya zamani ya uvuvi ya namba 22 ya mwaka 2003 ikiwa ni hatua itakayosaida kuweka mazingira bora kwa ajili ya wadau wa uvuvi na kuweza kutambua idara ya ukuzaji viumbe maji Haya yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa sekta ya uvuvi Dkt. Rashidi Tamatama   Wakati akifungua mkutano wa kutoa maoni kwa wadau wa uvuvi toka kanda ya   kati Dodoma kwenye ukumbi ya Holly Cross Jijini Dodoma. Katibu Mkuu huyo alisema kuwa sheria hiyo mpya ya ukuzaji viumbe maji itajenga mazingira mazuri kwa wadau wa uvuvi kufanya kazi zao bila vikwazo. Aliendelea kusema kuwa sheria mpya itasaidia kujenga serikali ya awamu 5 ya uchumi wa viwanda vya kati katika sekta ya uvuvi. Katibu Mkuu huyo aliwaambia wadau hao kuwa serikali itawezesha sheria hiyo ya ukuzaji viumbe maji ili kufikia mahitaji sera ya Taifa ya uvuvi ya mwaka 2015 ilivyosema mikakati imeelekezwa kuendeleza rasilim...

ZOEZI LA UOGESHAJI WA MIFUGO KANDA YA KATI

Picha
WIZARA ya mifugo na uvuvi, imeandaa mikakati ya kuboresha sekta ya mifugo hapa nchini, moja ya mkakati huo ni ule wa kudhibiti magonjwa ya mifugo ambapo imewahimiza wafugaji kuzingataia matumizi ya majosho yenye dawa za kuogesha ng’ombe ili kutokomeza magonjwa yatokanayo na kupe. Hayo yalielezwa hivi karibuni na  Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi Mheshimiwa Abdalah Ulega wakati wa zoezi la uhamasishaji wa uogeshaji wa ng’ombe kanda ya kati mkoani Singida, katika kijiji cha Mgori kilichopo halmashauri ya wilaya ya Singida vijijini. Katika uhamasishaji huo waziri Ulega aliwataka wafugaji kufanya zoezi la uogeshaji wa mifugo uliyoanzishwa uwe wenye tija na endelevu, kwa vile hivi sasa hakuna sababu za kushindwa kuogesha mifugo   yao katika majosho yenye dawa ya kudhibiti   kupe yaliyotolewa na serikali bure. Alisema hivi sasa serikali katika zoezi hili, imetoa dawa bure kwa halmashauri zote nchini, na kukarabati majosho yote yaliyokuwa hayafanyi kazi, ili wafugaji...
Picha
MIGOGORO MIKUBWA 14 KATI YA 29 YATATULIWA NA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema wizara kupitia timu yake maalum ya kushughulikia migogoro, hadi sasa imetatua migogoro mikubwa 14 kati ya 29 inayohusisha wakulima na wafugaji pamoja na hifadhi na wawekezaji. Naibu Waziri Ulega amebainisha hayo alipokuwa akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Bw. Lengai Ole Sabaya pamoja na viongozi wengine wa wilaya hiyo, mara baada ya kuarifiwa kuwepo kwa mgogoro wa wakulima na wafugaji katika Wilaya ya Hai na kubainisha kuwa ni hatari kwa jamii inayoishi pamoja kuwa na mgogoro wa aina hiyo. “Nitamsisitiza katibu mkuu mifugo aliangalie kwa karibu sana hili kwa sababu ni hatari sana kwa jamii inayoishi pamoja kutokuwa na maelewano ya kuachiana maeneo kwa ajili ya shughuli zao za kiuchumi.” Alisema Mhe. Ulega Mhe. Ulega ametoa kauli hiyo baada ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Bw. Lengai Ole Sabaya kumuarifu kuwa baadhi ya maeneo yenye...

WANANCHI WAONYWA KUTOTUMIA VIBAYA MATAMKO YA RAIS WA NCHI, KUKWEPA KODI

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka wananchi hususan wafugaji kutotumia matamko ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli vibaya kwa kutafuta mianya ya kutolipa kodi. Prof. Gabriel amebainisha hayo akiwa katika mnada wa upili wa Meserani uliopo wilaya ya Monduli Mkoani Arusha mara baada ya kufanya ziara ya kukagua utendaji kazi wa watumishi waliopo katika mnada huo na kusikiliza kero za wafugaji. Akizungumza na wananchi mara baada ya kufanya ziara hiyo Prof. Gabriel amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika kipindi cha mwezi mmoja itashirikiana na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Monduli kutoa tafsiri sahihi ya mfanyabiashara mdogo anayestahili kukatiwa kitambulisho cha biashara ndogo ndogo (machinga) cha Shilingi Elfu Ishirini kwa mwaka, kilichotolewa na Rais Magufuli kutokana baadhi ya wafugaji kutaka kufahamu endapo wanastahili kupatiwa vitambulisho. “Mheshimiwa rais alikuwa amelenga...

YALIYOJIRI KATIKA MKUTANO WA KUJADILI AFYA YA WANYAMA DUNIANI ULIOFANYIKA MJINI HAMMAMET, TUNISIA.

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Hamis Ulega (MB) amehudhuria Mkutano Mkuu wa 23 wa Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (OIE) Kamisheni ya Afrika, uliofanyika Mjini Hammament nchini Tunisia. Mkutano huo uliojumuisha nchi zaidi ya 25 za bara la Afrika zikiwemo Zambia, Zimbabwe, Misri, Kenya, Uganda, Tunisia na Chad ulikuwa na malengo ya kuangalia afya ya wanyama, haki za wanyama, uzalishaji wa mifugo na usalama wa chakula kitokanacho na mifugo na kutoa mapendekezo kulingana na kanuni za shirika hilo duniani. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Hamis Ulega (MB) akiambatana na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo wa wizara hiyo Dkt. Hezron Nonga amepata fursa ya kufanya kikao cha ana kwa ana na uongozi mkuu wa Shirika hilo la Afya ya Wanyama Duniani (OIE) kwa kuzungumza na rais wa shirika hilo Dkt. Mark Schipp, Mkurugenzi Mkuu Dkt. Monique Eloit na mwakilishi wa shirika hilo kwa Ukanda wa Nchi za Kusini mwa Afrika Dkt. Samuel Wakusama. Katika mazungumzo hay...

MAKUBALIANO KATI YA SERIKALI NA BILL AND MELINDA GATES YATAKIWA KUTEKELEZWA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kufanya ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha mikakati ambayo serikali imekubaliana na Taasisi ya Bill and Melinda Gates katika sekta ya mifugo inatekelezwa kama walivyokubaliana. Naibu Waziri Ulega amesema hayo ofisni kwake jijini Dodoma alipotembelewa na ujumbe kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gates katika ofisi za wizara hiyo na kubainisha kuwa serikali inahakikikisha Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Mifugo Tanzania unatekelezwa na kuishukuru taasisi hiyo kwa kutoa mchango mkubwa katika mpango huo. “Sisi tuko pamoja na nyinyi na tunathamini makubaliano yetu na hatuwezi kuvunja makubaliano yetu ninawahakikishia kuwa nitamuagiza katibu mkuu afanye ufuatiliaji wa karibu sana kuhakikisha kwamba sisi tuna mikakati yetu tunayoifanya  lakini hii mikakati yote inaenda sambamba na kile tulichokubaliana.”  Alisema Mhe. Ulega...

NMB YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA KUKUZA SEKTA YA MAZIWA

Picha
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel ameitaka Benki ya NMB kushirikiana na wizara hiyo katika kukuza sekta ya maziwa nchini kwa kuwa bado kuna mwitikio mdogo wa wananchi kunywa maziwa kutokana na taarifa iliyotolewa na Shirika la Chakula Duniani (WFP) Prof. Gabriel amebainisha hayo Jijini Dodoma, akiwa kwenye kikao na maafisa kutoka idara ya kilimo ya Benki ya NMB, waliofika ofisini kwake kumwelezea mikakati ya Benki ya NMB ambayo imekuwa ikifanya tafiti na wadau wa sekta ya maziwa lengo likiwa ni kutaka kuwekeza katika sekta hiyo. “Kwa takwimu ambazo zimetolewa na Shirika la Chakula Duniani ni kwamba kwa wastani angalau mtu anatakiwa walau atumie lita mia mbili kwa mwaka za maziwa lakini kwa bahati mbaya kwa watanzania wastani ni lita arobaini na saba tu, bado tuna kazi kubwa sana.”  Alisema Prof Gabriel Prof. Gabriel amesema Benki ya NMB inapaswa kuwa na ushirikiano na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Dawati la Sekta ...

WAZIRI MPINA ATEKETEZA NYAVU HARAMU TANGA

Picha
Waziri wa mifugo na uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (Mb) ateketeza vipande vya nyavu haramu 773 zenye chini ya mil 10 ambazo zilikutwa katika maeneo ya Kigombe,Moa na Tanga Jiji Mkoani Tanga. Kufuatia tukio hilo la uteketezaji wa nyavu haramu hizo Mhe Waziri wa Mifugo na Uvuvi amesema, jitihada zinazofanywa na serikali ni kuzuia uvuvi haramu na kulinda rasilimali za Wavuvi.   “Tutahakikisha wavuvi wetu wanapata elimu juu ya uvuvi na kufata sheria, kanuni na taratibu za uvuvi zilizowekwa, alisema mpina. Pia Waziri Mpina alisema kuwa tarehe 1/07/2019 kanuni mpya ya uvuvi zitaanza   kutumika ambapo itakuwa imeondoa changamoto ambazo zinazotukabili. Waziri Mpina alisema pia, jitihada zinazofanywa na serikali ni kuzuia uvuvi haramu na kulinda rasilimali za Wavuvi. “Tunatumia Bil.56 kila mwaka kuagiza Samaki kutoka nje ya Nchi”, alisema Mpina  Waziri Mpina alisistiza kuwa nyavu zote zenye chini ya milimita 10 zikabidhiwe Wizarani na nyavu za kuanzia mili...