Nav bar

Alhamisi, 4 Aprili 2019

SERIKALI IMEANDAA SHERIA MPYA YA UKUZAJI VIUMBE MAJI




Serikali imeandaa sheria mpya ya ukuzaji viumbe maji ili kuboresha sheria ya zamani ya uvuvi ya namba 22 ya mwaka 2003 ikiwa ni hatua itakayosaida kuweka mazingira bora kwa ajili ya wadau wa uvuvi na kuweza kutambua idara ya ukuzaji viumbe maji

Haya yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa sekta ya uvuvi Dkt. Rashidi Tamatama  Wakati akifungua mkutano wa kutoa maoni kwa wadau wa uvuvi toka kanda ya  kati Dodoma kwenye ukumbi ya Holly Cross Jijini Dodoma.

Katibu Mkuu huyo alisema kuwa sheria hiyo mpya ya ukuzaji viumbe maji itajenga mazingira mazuri kwa wadau wa uvuvi kufanya kazi zao bila vikwazo.

Aliendelea kusema kuwa sheria mpya itasaidia kujenga serikali ya awamu 5 ya uchumi wa viwanda vya kati katika sekta ya uvuvi.

Katibu Mkuu huyo aliwaambia wadau hao kuwa serikali itawezesha sheria hiyo ya ukuzaji viumbe maji ili kufikia mahitaji sera ya Taifa ya uvuvi ya mwaka 2015 ilivyosema mikakati imeelekezwa kuendeleza rasilimali ya mazao ya baharini ikiwemo samaki.

Dkt. Tamatama alisema kuwa sera ya Taifa ya Uvuvi pia inalenga kuendeleza ukuaji viumbe maji ambavyo ni pamoja na kuunda rasilimali ya samaki pamoja na viumbe wengine wa baharini.
Aidha alisema sheria mpya itasaidia nchi kwenda na mabadiliko ya sayansi na teknolojia zinazotumika katika sekta ya uvuvi.

Vilevile Katibu Mkuu Dkt. Tamatama amesema sheria mpya itasaidia kuipatia serikali uhalali wa kufanya kazi ili kuboresha ulinzi wa rasilimali ya uvuvi na mazao yake.

Hivyo Katibu Mkuu huyo alisema sheria hii inakuja kwa wakati muafaka, wakati idadi kubwa ya wanajihusisha na ufugaji wa samaki kama chanzo cha kuongeza kipato cha maisha yao.
Mkutano huo uliwakutanisha wavuvi, wafanyabiashara ya samaki ambao walitoa maoni yao mbalimbali ili kuboresha rasimu ya sheria hiyo mpya kabla ya kwenda bungeni kujadiliwa na kupitishwa.



Katibu Mkuu sekta ya uvuvi Dkt. Rashid  Tamatama  akifungua mkutano wa wadau wa uvuvi wa kutoa maoni ya sheria mpya

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni