Nav bar

Jumatano, 3 Aprili 2019

WAZIRI MPINA ATEKETEZA NYAVU HARAMU TANGA




Waziri wa mifugo na uvuvi Mhe. Luhaga Mpina (Mb) ateketeza vipande vya nyavu haramu 773 zenye chini ya mil 10 ambazo zilikutwa katika maeneo ya Kigombe,Moa na Tanga Jiji Mkoani Tanga.

Kufuatia tukio hilo la uteketezaji wa nyavu haramu hizo Mhe Waziri wa Mifugo na Uvuvi amesema, jitihada zinazofanywa na serikali ni kuzuia uvuvi haramu na kulinda rasilimali za Wavuvi.  

“Tutahakikisha wavuvi wetu wanapata elimu juu ya uvuvi na kufata sheria, kanuni na taratibu za uvuvi zilizowekwa, alisema mpina.

Pia Waziri Mpina alisema kuwa tarehe 1/07/2019 kanuni mpya ya uvuvi zitaanza  kutumika ambapo itakuwa imeondoa changamoto ambazo zinazotukabili.

Waziri Mpina alisema pia, jitihada zinazofanywa na serikali ni kuzuia uvuvi haramu na kulinda rasilimali za Wavuvi.


“Tunatumia Bil.56 kila mwaka kuagiza Samaki kutoka nje ya Nchi”, alisema Mpina 

Waziri Mpina alisistiza kuwa nyavu zote zenye chini ya milimita 10 zikabidhiwe Wizarani na nyavu za kuanzia milimita 8 hazitaruhusiwa kuvuliwa na zitatakiwa zichomwe moto.

“Nyavu hizi ambazo hazitakiwi zinaua mazalia ya samaki na kuvua samaki wachanga wasioruhusiwa, anaevua kutumia uvuvi haramu katika mnyoro mzima wa shughuli za uvuvi hatapona”. alisema Mpina

Mpina alisema, tutaendelea kupambana na uvuvi haramu Kila mtu afate sheria na taratibu zilizowekwa na tunashirikiana na viongozi wetu kujua mahitaji na kutembelea wavuvi ili tuwasaidie wavuvi wetu. - Mpina

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Bw. Daudi Mayeji Wawekezaji uvuvi alisema, tukizingatia kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizopo ili tuwe na uvuvi wenye tija.

“Natoa elimu kwa wavuvi kuwa,wanavua samaki ambao hawastahili matokeo yake uzalishaji unakuwa mdogo”, alisema Bw. Daudi Mayeji.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh. Luaga Mpina akiteketeza vipande vya nyavu haramu 773 mkoani Tanga


 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni